Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 116984

Ngoma Africa band watua kwa Wayahudi kutumbuiza sherehe za uhuru wa israel

$
0
0
Habari nyeti zimevuja sasa hivi kuwa Ngoma Africa band aka FFU UGHAIBUNI  bendi maarufu ya muziki wa dansi barani Ulaya yenye makao kule nchini Ujerumani inatua nchini Israel kutumbuiza katika onyesho maalum la siku ya uhuru wa nchi hiyo ijulikanayo kama  Yom Haatzmaut siku ya tarehe 1 mpaka 2 Mei 2017 mjini Tel Aviv.
Mmoja ya wanaitifaki wa maonyesho hayo Bi.Shimone amesema bendi hiyo ndio ya kwanza ya Kiafrika kupata mwaliko wa kutumbuiza katika maonyesho hayo lakini hakutaka kuelezea zaidi.
Habari zaidi za uhakika zimevuja kuwa bendi hiyo imesafiri kimya kimya kutoka Ujerumani kuelekeahuko Uyahudini kwa ajili ya onyesho  hilo. Kiongozi wa bendi hiyo Kamanda Ras Ebrahim Makunja amethibitisha mwaliko huo wa kihistoria na kuiambia Globu ya Jamii kwamba wao hivi sasa wako Tel Aviv wakingoja kumwaga lazi.
 Kiongozi wa The Ngoma Africa Band wana FFU UGHAIBUNI akiongoza gwaride kujiandaa na libeneke la Israel
 Nyomi ya The Ngoma Africa Band wana FFU UGHAIBUNI katika moja ya maonesho yao
Kikosi kazi cha The Ngoma Africa Band wana FFU UGHAIBUNI

Viewing all articles
Browse latest Browse all 116984

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>