TOLEO Na. 8 LA JARIDA LA WIZARA YA ARDHI , NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imetoa jarida lake la mwaka (Toleo Na. 8). Jarida hili haliuzwi. Kuna nakala chache ambazo zinapatikana Wizarani katika Kitengo cha huduma kwa mteja. Aidha, kutakuwa na nakala nyingine chache ambazo zitasambazwa katika maeneo mbalimbali kama; Wizarani na katika Ofisi za Halmashauri nchini.
Jarida hili litapatikana pia hivi karibuni kwenye tovuti ya Wizara (www.ardhi.go.tz).
Mwananchi pata nakala yako upate kuhabarika kuhusu shughuli na matukio mbalimbali ya Wizara.
Na. Kitengo cha Mawasiliano Serikalini – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.