Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 117380

Serikali na familia zavutana juu ya mazishi ya Kiongozi wa Upinzani nchini DR Congo

$
0
0
Mwili wa kiongozi wa upinzani nchini DR Congo, Etienne Tshisekedi hautarudishwa nyumbani wiki hii kama ilivyopangwa hapo awali.

Familia ya Tshisekedi aliyefariki mwezi uliopita nchini Ubelgiji akiwa na umri wa miaka 84, ilikuwa imepanga kufanya mazishi ya ndugu yao nchini DR Congo Jumamosi inayokuja.

Mdogo  wa Marehemu Tshisekedi, Gerard Mulumba aliuambia mtandao wa BBC kwamba familia haijakukubaliana na serikali kuhusiana na eneo atakalozikwa ndugu yao mjini Kinshasa.
Familia ya Tshisekedi wanataka mwili uzikwe katika makao makuu ya chama cha UPDS alichokianzisha.

Lakini serikali inataka kumzika katika maziko ya Gombe yaliyopo katikati ya mji, na mpaka sasa hakuna  jibu rasmi kuhusiana na tangazo hilo.

Kifo cha Tshisekedi kimeliweka taifa hilo katika hali tete kwa kuwa kilijiri wakati ambapo kulikuwa na majadiliano kati ya serikali na upinzani kumaliza mgogoro wa kisiasa ambao umesababishwa na hatua ya rais Kabila kukataa kujizulu baada ya kukamilika kwa muhula wake wa kuongoza mnamo mwezi Disemba.

Uchaguzi unakaribia kabla ya mwisho wa mwaka na mwana wa Tshisekedi Felix amechaguliwa kuongoza upinzani katika mazungumzo hayo.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 117380

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>