Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 119811 articles
Browse latest View live

Huwezi amini Diamond Platnumz sasa anatumia itel A37

$
0
0
TAKRIBANI wiki mbili baada ya itel kumtangaza balozi wake ambaye ni Diamond platnumz, sasa imebainishwa sababu za Diamond platnumz kuipenda simu hiyo ambayo ni tolea jipya la itel A37 ambayo imezinduliwa rasmi mwishoni mwa wiki iliyopita jijini Dar es Salaam.

Miongoni mwa sababu zilizoelezwa na Diamond kuhusu itel A37 ni pamoja na ubora na ukubwa wa skrini ya A37 ambayo ina 5.7” HD+ Waterdrop ikiwa ni full skrini.

Kabla ya uzinduzi huo Diamond aliwaambia wafanyabiashara ambao ni wadau wa

“itel A37 ni lazima niwe nayo kila siku ina skirini kubwa inatoa mwonekano bomba wa chochote ninachokitazama kwenye skrini ndio sababu naipenda sana na kizuri zaidi simu hii ina face unlock” amenukuliwa Diamond.
Kulingana na maelezo ya kampuni ya itel, face unlock ni mbadala wa fingerprint na hufanya kazi kwa ufanisi na ni salama na rahisi, ili kufungua itel A37 mtumiaji atatakiwa kutazama kwenye skrini ya A37 na simu itajifungua yenyewe.


Mbali na hilo itel A37 imeundwa kwa namna ambayo kama mtumiaji anataka kujipiga picha maarufu sefie na asingependa kubofya kwa kidole basi anaweza kutabasamu tu mbele ya kamera ya itel A37 na hapo atakuwa tayari ameshajipiga picha.

Kikubwa zaidi itel A37 imedizainiwa ikiwa na ukanda maalum mzuri wa kuvutia (ribbon), hii inakumweka mtumiaji kwenye ulimwengu wa fasheni mahali popote anapokuwepo.

Zaidi ya hayo, simu ya itel A37 imewekewa ulinzi wa macho kwa mtumiaji, hii inajulikana kama eye care ambapo mtumiaji atatumia simu hiyo kusoma vitabu ama kutazama chochote kwa mwanga laini usio na mionzi inayoumiza macho.

Simu hiyo iliyozinduliwa ina rangi tatu ambazo ni, Dark Blue, Light Purple, Gradient Green.
Rangi za itel A37 Dark Blue, Light Purple, Gradient Green.


RAIS WA ZANZIBAR ALHAJ DK.HUSSEIN ALI MWINYI AKISOMA RISALA YA KUUKARIBISHA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHANI

$
0
0

 SERIKALI imeahidi kuchukua hatua kali kwa mfanyabiashara yoyote atakaebainika kupandisha bei za bidhaa au huduma kwa utashi ama tamaa bila ya kuwepo sababu ya msingi kwani tayari imeshatoa bei elekezi za bidhaa muhimu za chakula.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema hayo leo katika risala yake aliyoitoa kwa wananchi kupitia vyombo vya habari ya kuukaribisha mwezi Mtukufu wa Ramadhan mwaka huu 2021 Miladia sawa na mwaka 1442 Hijria.

Katika risala yake hiyo, Alhaj Dk. Mwinyi alisema kwamba kwa pamoja ni vyema wananchi wenye kipato cha chini wakafikiriwa hasa katika kipindi cha mwezi Mtukufu wa Ramadhani ambapo mahitaji ya familia yanaongezeka.

Alisisitiza kwamba kwa msingi huo huo, wafanyabiashara wa bidhaa zote zikiwemo za nguo ni vyema wakazingatia uwezo wa wananchi kwani kuwakatia nguo watoto katika kipindi hichi kwa ajili ya Sikukuu ni sehemu ya utamaduni wa wananchi wote wa Zanzibar.

Aliongeza kuwa inafurahisha kuona kwamba licha ya kuwepo kwa changamoto za usafirishaji na upatikanaji wa biadhaa mbali mbali, shughuli za biashara na upatikanaji wa chakula hapa nchini zinaenda vizuri ambapo bidhaa zote muhimu zinapatikana wakati huu  mwezi wa Ramadhani ukikaribishwa.

Alhaj Dk. Mwinyi alisema kuwa taarifa za Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo inatoa matumaini ya kuwepo kwa chakula cha kutosha yakiwemo mazao ya muhogo na ndizi ambayo hutumiwa na wananchi wengi kwa futari katika mwezi wa Ramadhani.

Aidha, Alhaj Dk. Mwinyi alisema kuwa mnamo Machi 04 2021 alikutana na wafanyabiashara wakubwa wanaoingiza chakula na kuwataka washirikiane na Serikali kufanya maandalizi mazuri katika kuhakikisha kwamba bidhaa zote hasa za chakula kwa wananchi wa Zanzibar ziweze kupatikana katika  kipindi chote cha mwezi wa Ramadhani na baada ya hapo.

Alhaj Dk. Mwinyi alieleza kwamba kwa hakika ibada ya Saumu  ina mchango mkubwa katika kuimarisha uchamungu, jambo ambalo ni jema na linaleta manufaa hapa Duniani na kesho Akhera.

“Kwa hivyo, tuukaribishe Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kwa furaha na matumaini na tujiandae kunufaika kutokana na neema na fadhila mbali mbali zilizo katika kipindi chote cha Mwezi huu tunaoukaribisha”, alisema Alhaj Dk. Mwinyi.

Pamoja na hayo, Alhaj Dk. Mwinyi aliwaomba Waumini wa Dini ya Kiislamu kuhimizana kutekeleza ibada za Faradhi sambamba na kukithirisha ibada za Sunna ili kupata radhi za Mola ambapo miongoni mwa ibada iliyosisitizwa zaidi kufanywa kwa wingi katika mwezi wa Ramadhani ni kusoma Qur-an tukufu.

Alieleza kwamba katika kutafuta fadhila za Mwezi Mtukufu wa Ramadhani imehimizwa kujitahidi sana kutekeleza ibada ya sala zote za Faradhi na sala za Sunna, kuomba dua, kusoma nyiradi mbali mbali, kufanya itikafu, na kutekeleza Sunna nyengine zinazoambatana na Mwezi wa Ramadhani.

Aliongeza kwamba jambo jengine linalohimizwa kutekeleza zaidi ndani ya Mwezi wa Ramadhani ni kutoa sadaka hasa kwa watu wenye mahitaji, Mayatima, Wazee, Masikini na Mafakiri ibada ambayo inaongeza baraka na mahusiano mema katika jamii.

Alhaj Dk. Mwinyi pia, alitumia fursa  hiyo kuwahimiza wananchi pamoja na viongozi na Watumishi wa Manispaa zote nchini juu ya umuhimu wa kuzingatia usafi katika miji hasa katika masoko na maeneo yanayohusika na uuzaji wa vyakula ili kujiepusha na maradhi ya mripuko.

Kadhalika, aliwahimiza viongozi wa Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA) kuhakikisha huduma za maji zinawafikia wananchi hasa katika maeneo ambayo huduma hiyo haipatikani kwa uhakika.

Aliwataka Masheha wa Shehia ambazo zina matatizo ya maji wawasiliane na (ZAWA) ili kuhakikisha hatua zinachukuliwa zikiwemo kuwapelekea wananchi magari ya maji kwa lengo la kuondokana na usumbufu wa kupata huduma hiyo.

Sambamba na hayo, Alhaj Dk. Mwinyi aliwahimiza viongozi wa Mamlaka ya Usafiri na Usalama Barabarani pamoja na Jeshi la Polisi kuhakikisha wanasimamia ipasavyo sheria za usalama barabarani wakati wote na kuongeza nguvu hasa katika kipindi hiki ambacho mahitaji ya usafiri huongezeka.

Aliwataka kuwachukulia hatua kali za kisheria madereva watakaojaribu kuvunja sheria  za usalama barabarani kwa kwenda mwendo wa kasi pamoja na wale wenye tabia ya kuwasumbua wananchi kwa kuwashusha bila ya kuwafikisha mwisho wa vituo vilivyopangwa na Serikali.

Hata hivyo, Alhaj Dk. Mwinyi aliwakumbusha wananchi wenye dharura maalum na wale wasiokuwa Waislamu waendeleze utamaduni wa kujizuia kula hadharani, kutovaa nguo zisizoendana na maadili ya Kizanzibari sambamba na kuepuka matendo yatakayowakwaza Waislamu wenye kutekeleza ibada ya funga.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi akisoma risala kwa Wananchi kuukaribisha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kwa mwaka 2021,sawa na Mwaka 1442 Hijria, kupitia vyombo vya habari katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu)

 

MFANYABIASHARA AKANA KUTENDA KOSA, ARUDISHWA LUMANDE

$
0
0
MFANYABIASHARA, John Kyenkungu 65, anayeishi Eneo Mikocheni Mkoani Dar es Salaam, amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu tuhuma za kughushi hati ya nyumba ili kuchukulia mkopo.

Akisoma hati ya mashtaka wakili wa Serikali, Adolph Lema amedai mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Augustina Mmbando kuwa katika tarehe isiyojulikana mwaka 2014, mshtakiwa Kyenkungu alitenda kosa la kughushi hati hiyo.

Imedaiwa, siku hiyo mshtakiwa kwa nia ya kudanganya alighushi hati ya mkopo ya mwaka 2014 na kusaini kwamba Said Nassoro amekubali kutumia hati ya nyumba yake yenye namba 25480 kiwanja namba 516 kitalu B, iliyopo Mikocheni kama dhamana ya kupata mkopo kutoka benki ya Equity huku akijua kuwa siyo kweli.

Imeendelea kudaiwa kuwa, Agosti 23, 2014 jijiji Dar es Salaam mshtakiwa alighushi barua ya 23/8/2014 kwamba Said Nassoro amekubali kutumia hati ya nyumba yake yenye namba 25480 kiwanja namba 516 kitalu B, iliyopo Mikocheni kama dhamana ya kupata mkopo kutoka benki ya Equity huku akijua kuwa siyo kweli.

Hata hivyo mshtakiwa amekana kutenda kosa hilo na amerudishwa rumande baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamama yaliyomtaka kuwa na wadhamini wawili ambao watasaini bondi ya Sh. Milioni 100 kila mmoja huku mshtakiwa akitakiwa kuweka fedha taslimu sh. Milioni 75 au hati ya mali isiyohamishika ya kiasi hicho cha pesa.

Kwa mujibu wa upande wa mashtaka upelelezi katika kesi hiyo bado haujakamilika na imeahirishwa hadi Aprili 21, 2021.

NJIKU AWATAKA WANAFUNZI KUWA WAZALENDO

$
0
0

Afisa Tarafa Kata ya Ikungi mkoani Singida,  Yahaya Njiku , akihutubia kwa niaba ya mkuu wa wilaya hiyo Edward Mpogolo wakati akizungumza na Vijana Wanafunzi wa Katoliki Tanzania (TYCS) wahitimu wa Kidato cha Sita wa Shule ya Sekondari Ikungi mkoani Singida  katika sherehe ya kuagana na wanafunzi wenzao wa kidato cha 

5-1 iliyofanyika juzi wilayani humo.

Vijana Wanafunzi wa Katoliki Tanzania (TYCS)  wahitimu wa Kidato cha Sita wa Shule ya Sekondari Ikungi wakiwa wamejipanga tayari kuingia ukumbini katika sherehe ya kuagana na wanafunzi wenzao wa kidato cha 5-1 iliyofanyika juzi wilayani humo.
Walimu wakiwa kwenye sherehe hiyo.
Wazazi wakiwa kwenye sherehe hiyo.
Vijana Wanafunzi wa Katoliki Tanzania (TYCS)  wahitimu wa Kidato cha Sita wa Shule ya Sekondari Ikungi wakiwa kwenye sherehe hiyo.
Afisa Elimu Kata ya Ikungi, Mghenyi Nkuwi, akizungumza katika hafla hiyo.
Vyeti vikitolewa.
Vyeti vikitolewa.
Wazazi wakiwa kwenye sherehe hiyo.
Picha ya pamoja na mgeni rasmi.
Mgeni rasmi akikabidhiwa keki..
Mshereheshaji wa sherehe hiyo (MC) akiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi na walimu.



Na Dotto Mwaibale, Singida.


AFISA Tarafa Kata ya Ikungi mkoani hapa Yahaya Njiku amewataka vijana wanafunzi wa Katoliki Tanzania (TYCS) waliohitimu kidato cha sita katika Shule ya Sekondari ya Ikungi kuwa wazalendo wa nchi yetu.

Njiku ambaye alikuwa mgeni rasmi kwa niaba ya mkuu wa wilaya hiyo Edward Mpogolo aliyasema hayo wakati akizungumza na wanafunzi hao katika sherehe ya kuagana na wanafunzi wenzao wa kidato cha 5-1 iliyofanyika juzi wilayani humo.

"Mnapaswa kuwa wazalendo na uzalendo unatafusiri nyingi kwanza unapaswa kuipenda nchi yetu kuifahamu  kuithamini na kuitunza." alisema Njiku.

Alisema wakiwa kama vijana wanaohitimu kidato cha sita na wale ambao wanaendelea na masomo ni lazima kwanza wawe wazalendo.

Alisema sisi tupo katika Taifa la Tanzania hatuna lingine zaidi ya Tanzania hivyo tunapaswa kulitunza na kulitetea popote pale duniani.  

Njiku aliwaambia vijana hao kuwa uzalendo unatakiwa kuuanza wakiwa na umri mdogo na kuwa hawawezi kuwa wazalendo pasipo kulielewa taifa lao kuanzia historia yake, misingi na jinsi lilivyopatikana.

"Niwaombe ninyi wahitimu na nyie mnaoendelea na masomo ni lazima mfahamu historia ya taifa letu kwani leo hii mpo hapa mna furaha kwa kucheza muziki, michezo mbalimbali na kubadilishana mawazo kuna watu waliteseka kuliangaikia taifa letu akiwepo Baba wa Taifa Hayati Julius Kambarage Nyerere na wenzake.

Alisema ni muhimu kwa vijana hao kusoma masomo ya uraia ili waweze kulielewa taifa lao kwani wakilielewa wataweza kulitetea.

Katika hatua nyingine Njiku aliwataka vijana hao kuwa mabalozi wa kuhamasisha amani hapa nchini na kuwaombea viongozi wetu hasa Rais Samia Suluhu Hassan ambaye aliapishwa hivi karibuni kuongoza nchi baada ya aliyekuwa Rais wetu Dkt.John Magufuli kufariki.

Aliwataka wahitimu hao kuendelea kumuomba Mungu ili waweze kuendelea na masomo yao ya  elimu ya juu kwani kumaliza kidato cha 5-6 sio mwisho wa kusoma.

"Nyinyi wanafunzi mnakila sababu ya kuendelea na masomo kwani Serikali  kupitia Rais wetu Mama Samia Suluhu imeweka mazingira bora ya kusoma kwa kutoa elimu bure." alisema Njiku. 

Aidha Njiku aliwaambia wahitimu hao kuwa nidhamu na uwajibikaji ni jambo jema litakaloweza kuwafanya waishi vizuri wakiwa shuleni, nyumbani na jamii na bila kuacha kumuomba Mungu ambaye siku zote hawezi kumuacha mtu amuombaye.

Njiku aliwataka vijana hao kuto jiingiza katika vitendo visivyo na maadili badala yake watumie muda wao kwa kujisomea na kuendeleza vipaji vyao vya michezo walivyonavyo na kuwapa heshima wazazi wao wanao wasomesha kwa kufanya vizuri mitihani yao.

Wahitimu hao 19 katika risala yao kwa mgeni rasmi walitaja baadhi ya mafanikio waliyopata wakiwa shuleni ni kushiriki katika kuchangia ujenzi wa parokia ya mtakatifu Rita wa Kashia wilayani humo.

MGOMBEA AANZA KAMPENI AKIWA NDANI YA JENEZA

$
0
0




Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

MWANASIASA Maarufu nchini Mexico  Carlos Mayorga ameingia katika mijadala mbalimbali baada ya kuzindua kampeni zake za Ubunge akiwa ndani ya jeneza France24 imeripoti.

Carlos Mayorga alitumia njia hiyo kuonesha hali halisi ya taifa hilo ambalo mamia ya watu wanakufa kutokana na virusi vya Corona pamoja na vurugu zinazohusiana na biashara.

Akiwa mgombea kutoka chama cha Encuentro Salidario kusini mwa jimbo la Chihuahua Mayorga alisema, alifikia uamuzi huo kwa malengo ya kufikisha ujumbe kwa wanasiasa ambao wanasababisha watu kupoteza maisha kutokana na kutojali kwao.

Mwanasiasa huyo aliwasili katika kampeni zake katika daraja linalotengenesha mji wa wa Ciudad Juarezy na El Paso Texas akiwa ndani ya jeneza la rangi ya fedha.

 Carlos Mayorga aliambatana na wasaidizi waliovaa mavazi na vifaa vya kujilinda wakiwa na mashada ya maua kama ishara ya kupaza sauti juu ya janga hilo ambapo hadi sasa watu 200,000 wamefariki nchini humo kutokana na Covid-19.

Vyombo vya habari vilimnukuu mwanasiasa huyo akisema;

"Wanasiasa wameendelea kukaa kimya wakati matukio ya uhalifu yakiendelea, na wameendelea kukaa kimya kuhusu hali mbaya ya Covid-19." Alinukuliwa.

Zaidi ya watu 300,000 wameuawa nchini Mexico tangu Serikali itoe nguvu kwa jeshi katika kupambana na vita dhidi ya dawa za kulevya 2006 kwa mujibu kwa taarifa rasmi.

#VIDEO: RAIS SAMIA SULUHU HASSAN ALIPOKUTANA NA RAIS MSTAAFU WA AWAMU YA PILI MZEE MWINYI JIJINI DAR

#VIDEO: UTAMU​ WA TIKITI NA BEI YAKE.

Taliss yatwaa ubingwa wa kuogelea Tanzania

$
0
0



waogeleaji wakishindana katika mashindano ya taifa ya kuogelea

***************************

Na Mwandishi Wetu-Dar es Salaam.

Klabu ya Taliss –IST imenyakuwa ubingwa wa Taifa wa mashindano ya kuogelea baada ya kukusanya pointi nyingi zaidi ya klabu nyingine tano zilizoshiriki katika mashindano hayo.

Klabu hiyo imepata jumla ya pointi 1, 826 ambapo pointi 586 zilikusanywa kwa upande wa wanawake na pointi 1, 160 zilikusanywa kwa upande wa wanaume.

Huu ni ubingwa wa tatu mfululizo kwa klabu hiyo tokea mwaka 2018. Mwaka 2019 pia ilitwaa ubingwa huo na mwaka jana mashindano hayo hayakufanyika kutokana na ugonjwa wa virusi vya corona.

Meneja wa klabu hiyo Hadija Shebe alisema kuwa moyo wa kujituma, mafunzo mazuri na ushirikiano baina ya shule, klabu na wazazi ndiyo nguzo pekee ya kupata mafanikio katika mashindano hayo yaliyoshirikisha waogeleaji zaidi ya 90.

“Waogeleaji wetu wamefanya vizuri sana na wanahitaji pongezi, tunajivunia kwa mafanikio haya, ni makubwa kwa upande wa klabu hasa baada ya kuunganika na shule,” alisema Hadija.

Klabu ya Bluefins ya jijini ilishika nafasi ya pili kwa kupata pointi 1,748 baada ya kupata pointi 818 kwa upande wa wavulana na pointi 862 kwa wasichana.

Muasisi na kocha wa klabu hiyo, Rahim Alidina, aliwapongeza waogeleaji wote, makocha na wazazi kwa ushirikiano na kuifanya klabu yao kumaliza katika nafasi ya pili.

Nafasi ya tatu ilichukuliwa na Klabu ya Dar es Salaam (DSC) ambayo ilipata pointi 1,486 ambapo kwa upande wa wanaume walipata pointi 888 na pointi 538 zilikuwa kwa wanawake huku nafasi ya nne ikienda kwa Mwanza kwa kupata pointi 904 na kufuatiwa na FK Blue Marlins katika nafasi ya tano kwa kupata pointi 578 na Mis Piranhas wakishika nafasi ya sita kwa kupata pointi 410.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Kuogelea Tanzania (TSA), Inviolata Itatiro alisema mashindano hayo yamefanikiwa na waogeleaji kuleta ushindani mkubwa.


MATUKIO MBALIMBALI WAKATI BUNGE LIKIPITISHA MPANGO WA TAIFA WA MAENDELEO YA MIAKA MITANO, BUNGENI DODOMA

$
0
0


Na. Farida Ramadhani na Peter Haule, WFM, Dodoma


Bunge la Jamhuri ya Mungano wa Tanzania leo Jumatatu tarehe 12 Aprili, 2021 limepitisha Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/22 hadi 2025/26.

Mpango huo utakaogharimu zaidi ya shilingi trilioni 114.8 umepangwa kutekeleza maeneo makuu matano ya kipaumbele, ikiwemo kuchochea uchumi shindani na shirikishi, kuimarisha uwezo wa uzalishaji viwandani na utoaji huduma.

Vipaumbele vingine ni kukuza uwekezaji na biashara, kuchochea maendeleo ya watu na kuendeleza rasilimali watu.

" Tutahakikisha kwamba miradi yote ya kimkakati iliyoainishwa kwenye Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano itatekelezwa kama ilivyopangwa", alisema Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) wakati akihitimisha mjadala kuhusu Mpango huo Bungeni jijini Dodoma.

Shabaha ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/22 hadi 2025/26 ni pamoja na kupandisha kiwango cha ukuaji wa uchumi kutoka asilimia 6.0 ya mwaka 2021 hadi kufikia wastani wa asilimia 8.0 itakapofika mwaka 2026.

Aidha mfumuko wa bei umebashiriwa kuendelea kubaki katika wigo wa tarakimu moja kwa wastani wa asilimia kati ya 3.0 hadi 5.0 katika kipindi cha muda wa kati na akiba za kigeni kukidhi mahitaji ya uagizaji wa huduma na bidhaa kutoka nje kwa kipindi kisichopungua miezi minne.

Malengo mengine ni kuhakikisha kuwa mapato ya ndani ikijumuisha mapato ya Halmashauri yanaongezeka kutoka asilimia 15.9 ya pato la Taifa mwaka 2021/22 hadi asilimia 16.8 itakapofika mwaka 2026 na sekta binafsi inatarajiwa kuzalisha ajira mpya zipatazo milioni nane kati ya Julai 2021 na Juni 2026.

Miongoni mwa viongozi wa Wizara ya Fedha na Mipango, waliohudhuria uhitimishaji wa mjadala huo wakiongozwa na Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) ni Naibu wake Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni (Mb) pamoja na Manaibu Katibu Mkuu Bi. Amina Khamis Shaaban na Bw. Adolf Ndunguru na baadhi ya Wakuu wa Idara na Vitengo.

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akihitimisha hoja za Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/22 – 2025/26, bungeni jijini Dodoma.

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akihitimisha hoja za Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/22 – 2025/26, bungeni jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe.  Mhandisi Hamad Yussuf Masauni (Mb), akifafanua hoja mbalimbali zilizowasilishwa na wabunge wakati wa kuchangia kuhusu Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/22 – 2025/26, bungeni jijini Dodoma.


Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) na Naibu wake, Mhe.  Mhandisi Hamad Yussuf Masauni (Mb) wakifuatilia michango mbalimbali iliyotolewa na wabunge kuhusu Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/22 – 2025/26, bungeni jijini Dodoma.

Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa akiteta jambo na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba(Mb) muda mfupi baada ya kuhitimisha hoja ya Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/22 – 2025/26, bungeni jijini Dodoma.

Wabunge wakishangilia wakati wa kuhitimisha hoja kuhusu Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/22 – 2025/26, uliowasilishwa juma lililopita na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), bungeni jijini Dodoma.

Manaibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Amina Khamis Shaaban (kushoto) na Bw. Adolf Ndunguru (kulia) wakiwa na baadhi ya wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara hiyo wakifuatilia michango mbalimbali iliyokuwa ikitolewa na wabunge kuhusu Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/22 – 2025/26, bungeni jijini Dodoma.

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb)(kushoto) na Naibu wake, Mhe.  Mhandisi Hamad Yussuf Masauni (Mb)(kilia) wakitoka katika ukumbi wa Bunge baada ya kuhitimisha hoja ya Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/22 – 2025/26, bungeni jijini Dodoma.

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) na Naibu wake, Mhe.  Mhandisi Hamad Yussuf Masauni (Mb) wakiteta jambo na baadhi ya viongozi wa wizara hiyo baada ya Bunge kupitisha Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/22 – 2025/26, wakiwa nje ya viwanja vya Bunge jijini Dodoma.

 

 

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini WFM)

 

VODACOM YASHIRIKIANA NA BRITAM TANZANIA KUZINDUA VODABIMA KUPITIA M-PESA

$
0
0

 

Mkurugenzi wa M-Pesa, Epimack Mbeteni (katikati), Afisa Mtendaji Mkuu wa Britam Tanzania, Raymond Komanga (kushoto) na Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti wa TIRA, Zakaria Muyengi (kulia) wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya uzinduzi wa huduma mpya ya VodaBima  (Bimika Kidijitali) itakayowezesha mteja kulipia bima  kwa simu ya mkononi kupitia M-Pesa. Uzinduzi huu umefanyika leo jijini Dar Es Salaam.

Mkurugenzi wa M-Pesa, Epimack Mbeteni akizungumza kwenye  uzinduzi wa huduma mpya ya VodaBima  (Bimika Kidijitali) itakayowezesha mteja kulipia bima  kwa simu ya mkononi kupitia M-Pesa. Uzinduzi huo umefanyika leo jijini Dar Es Salaam.

Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti wa TIRA, Zakaria Muyengi akizungumza kwenye  uzinduzi wa huduma mpya ya VodaBima  (Bimika Kidijitali) itakayowezesha mteja kulipia bima  kwa simu ya mkononi kupitia M-Pesa. Uzinduzi huo umefanyika leo jijini Dar Es Salaam.

Afisa Mtendaji  Mkuu wa Britam Tanzania, Raymond Komanga ( kushoto )  akizungumza kwenye  uzinduzi wa huduma mpya ya VodaBima  (Bimika Kidijitali) itakayowezesha mteja kulipia bima  kwa simu ya mkononi kupitia M-Pesa. Uzinduzi huo umefanyika leo jijini Dar Es Salaam.

……………………………………………………………………………

Jukwaa la kidijitali linalowezesha upatikanaji wa huduma za bima kwa urahisi zaidi na za bei nafuu kwa kushirikiana na kampuni ya Britam Tanzania.

  • Zaidi ya wateja milioni 13 wa M-PESA kupata Bima ya Magari kupitia simu zao
  • Aina zingine za huduma za Bima kuongezwa katika orodha ya huduma.

Tarehe 12 Aprili 2021. Dar es Salaam. Kampuni inayoongoza ya Teknolojia na Mawasiliano nchini, Vodacom Tanzania leo imetangaza kuzindua ‘VodaBima’ – huduma ya kidijitali itakayowapa wateja huduma ya bima kupitia M-Pesa na hivyo kuchochea matumizi ya huduma za bima kwa Watanzania kwa kutumia huduma hiyo kwa njia ya kidijitali.

Kulingana na ripoti ya Finscope 2013, matumizi  ya Bima nchini ilikuwa asilimia 13.0 ikiwa imeongezeka kutoka kutoka asilimia 6.8 2009. Pamoja na ukuaji huu, bima bado ni moja ya huduma za kifedha ambazo hazitumiki sana nchini. Sababu tofauti zinatajwa ikiwa ni pamoja na mwamko mdogo, kutokuaminika kwa huduma na vikwazo vya kupata huduma. Kama kampuni ya teknolojia iliyo na maono ya kuibadilisha Tanzania na kubadilisha maisha kupitia teknolojia, Vodacom inapenda kuziba pengo hili kwa kutoa suluhisho la kidijitali ambalo litarahisisha upatikanaji wa bidhaa za Bima.

Akizungumza Jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi wa M-Pesa, Epimack Mbeteni alisema kuwa VodaBima ni nyongeza mpya kwa jalada la M-Pesa la bidhaa na huduma zote zinalenga kufanya ujumuishaji wa kidijitali nchini Tanzania uwe wa kweli.

“Kwa miaka 13 sasa, Vodacom M-Pesa imekuwa kichocheo muhimu katika ukuaji wa ujumuishaji wa kifedha nchini na kila wakati tunatafuta njia mpya za kushinikiza uchumi jumuishi wa kidijitali. Vodacom inakusudia kuziba pengo la upatikanaji wa huduma za bima kwa kutoa suluhisho la kidijitali ambalo litapunguza gharama na kuongeza upatikanaji wa bidhaa za Bima. 

VodaBima huwapa wateja fursa ya kujiwekea akiba ya Bima bila malipo katika mkoba wao wa VodaBima kwa mwaka mzima. Jukwaa la VodaBima litatuma taarifa za kumbukumbu kupitia SMS wakati Bima ya gari yako inakaribia kuisha.

Bwana Mbeteni ameongeza kuwa bidhaa hiyo mpya italeta huduma za bima karibu na wateja na kuongeza urahisi na upatikanaji wa huduma hiyo. Aliongeza kuwa huduma hiyo itakuza sekta ya bima nchini kwa ujumla. VODABIMA inatumia miundombinu bora ya teknolojia ya M-Pesa na mtandao mpana wa Vodacom ambayo inapatikana katika maduka Vodacom  nchini kote kuhakikisha usalama, urahisi wa upatikanaji wa huduma za bima.

“VodaBima ni huduma ya kwanza ya aina yake sokoni, huduma hii inarahisisha upatikanaji wa huduma za bima pamoja na mfumo wa kufanya madai. Kwa sasa tunatoa bima ya gari lakini tunapanga kuleta bidhaa zingine ili kukidhi mahitaji ya wateja na kwenda sambamba na mabadiliko ya soko,” alisema Mbeteni.

Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Bima Tanzania – TIRA, Zacharia Muyengi alisema kuwa kuongezeka kwa upatikanaji wa huduma za bima kupitia simu za mkononi kutawanufaisha wateja zaidi kwani sasa watafahamu kwa kina huduma mbalimbali za bima zinazotolewa sokoni.

“Tunafanya kazi kukuza na kudumisha soko la bima linalojumuisha, lenye ufanisi, la haki na salama kwa faida na ulinzi wa wamiliki wa sera. Tunakaribisha matumizi ya teknolojia ya mawasiliano pamoja na ubunifu wa bidhaa  ili kuleta huduma hizi karibu na watu. Uzinduzi wa VodaBima ni hatua inayoelekea kuboresha huduma  ya bima nchini,” alifafanua Muyengi.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Britam Tanzania Raymond Komanga ambao wanashirikiana na Vodacom kusambaza huduma ya bima kupitia teknolojia ya kidijitali alisema kuwa matumizi ya teknolojia ya mawasiliano ya simu katika kupata bima ni hatua itakayofanya huduma hiyo ipatikane kwa watu wengi zaidi. Aliongeza kwamba huduma hiyo itasaidia kuhamasisha watu wengi zaidi kutumia huduma ya  bima na kukuza sekta hiyo kwa ujumla.

“Huduma ya VodaBima ni ya kimapinduzi kwa sababu italeta urahisi kwa wateja kupata huduma za bima kutoka kwa watoa huduma. Wateja hawatalazimika kutembelea kampuni za bima kwani wanaweza kupata huduma hiyo  kupitia simu zao za mkononi,” alisema Komanga huku akiongeza kwamba jamii itaelimika zaidi juu ya bidhaa na manufaa ya utumiaji wa huduma za bima.

Uzinduzi wa VodaBima ni sehemu ya mpango wa ujumuishaji kupitia teknolojia ya kidijitali ya kampuni ya Vodacom na hatua nyingine zaidi katika kuleta huduma karibu na wateja kupitia ubunifu  na teknolojia ya mawasiliano kupitia simu za mkononi.

“Tunataka wateja wetu wapate huduma ya bima iliyoimarishwa pande zote. VodaBima ni bidhaa ya ziada ambayo inaweza kupatikana kupitia zana (App) mpya ya M-Pesa ambapo wateja wanaweza kupata bidhaa zingine kama huduma za mikopo na akiba kama Songesha na M-Pawa,” alihitimisha Mbeteni.

Uzinduzi wa VodaBima ni sehemu ya mpango wa ujumuishaji  kupitia teknolojia ya kidijitali ya kampuni ya Vodacom katika kuleta huduma karibu na wateja kupitia ubunifu  na teknolojia ya mawasiliano kupitia simu za mkononi. 

WAZIRI MKUU BUNGENI LEO JIJINI DODOMA

$
0
0

 

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na wageni kutoka Moshono Arusha ambao  walitembelea Bunge  jijini Dodoma kwa mwaliko wa Mbunge wa Arusha, Mrisho Gambo ( kushoto),  Aprili 12, 2021

MAADHIMISHO YA KUMBUKIZI YA SOKOINE KUFANYIKA SUA MOROGORO

$
0
0

Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine Cha Kilimo (SUA)  Prof. Maulid Mwatawala (wa kwanza kulia) akizungumza na Waandishi wa habari kuhusu maadhimisho hayo yatakayofanyika Chuoni hapo mwezi huu mwishoni kulia kwake ni Prof. Samweli Kaboto Mwenyekiti wa kamati ya mandalizi ya maadhimisho hayo.

Mwenyekiti wa kamati ya maadhimisho hayo Prof. Samweli Kabote ( Wa kwanza kushoto)   akizungumzia maandalizi hayo kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kuzungumza na waandishi wa habari. Katikati ni Prof. Maulid Mwatawala Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo na Mariam Mwayela.Wa kwanza kulia ni Afisa Mahusiano na Masoko wa SUA.


Afisa Mahusiano na Masoko wa SUA, Mariam Mwayela ( kulia) akitoa neno la ukaribisho kwa washiriki wa mkutano huo wa waandishi wa habari,
Washiriki wa mkutano huo na Wandishi wa habari wakifuatilia taarifa inayotolewa kuhusu maadhimisho hayo ya Kumbukizi ya Hayati Edward Moringe Sokoine yatakayofanyika mwishoni mwa mwezi ujao
Mkutano ukiendelea.
Washiriki wa mkutano huo na Wandishi wa habari wakifuatilia taarifa inayotolewa kuhusu maadhimisho hayo ya Kumbukizi ya Hayati Edward Moringe Sokoine yatakayofanyika mwishoni mwa mwezi ujao.


Washiriki wa mkutano huo na Wandishi wa habari wakifuatilia taarifa inayotolewa kuhusu Maadhimisho hayo ya Kumbukizi ya Hayati Edward Moringe Sokoine yatakayofanyika mwishoni mwa mwezi ujao.
Mkutano ukiendelea.
 


Na Calvin Gwabara, Morogoro.


CHUO Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA kimeahidi kunedelea kuenzi mchango wa AliyekuwaWaziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine kutokana na ushupavu wake kama kiongozi katika kusimamia uchapakazi, Kilimo vijijini, Uzalendo na kuchukia rushwa.

Hayo yamebainishwa na Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo ambaye ni Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Upande wa Taaluma Prof. Maulid Mwatawala wakati akizungumza na waandishi wa habari chuoni hapo juu ya maadhimisho ya kumbukumbu ya Hayati Edward Moringe Sokoine kwa mwaka 2021.

“Chuo kiliamua kutekeleza maamuzi ya kuadhimisha siku hii kuanzia mwaka 1992 kwa kuwa kiongozi huyu alikuwa mchapa kazi na alipigania ,masuala ya kilimo hasa katika mapinduzi vijijini na utoshelevu wa chakula kwa watanzania” Alisisitiza Prof. Mwatawala.

Prof.Mwatawala aliongeza kuwa katika kipindi cha uongozi wake Hayati Sokoine alipiga vita suala la rushwa na kuimarisha uadilifu katika utumishi wa umma ambapo serikali iliyopomadarakani inayazingatia na kuyaenzi kwa ajili ya maendeleo yaTaifa.

Kaimu Makamu huyo wa Mkuu wa Chuo alibainisha kuwa maadhimisho hayo kwa  mwaka huu yatafanyika kuanzia tarehe 24-27 Mei, 2021 chuoni hapo baada ya kuhairishwa hapo awali kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Tanzania Hayati Dkt. John PombeMagufuli.

Aidha alisema mambo yatakayofanyika katika wiki hiyo ya maonesho yateknolojia na ubunifu katika Kilimo, Ufugaji naUvuvi, kufanya mkutano  wakisayansi kwa wanataaluma, watafiti, wanafunzi na wadau mbalimbalii, mdahalo wa kitaifa wa kumbukizi  yaSokoineutakaofanyika siku ya tarehe 27 Mei 2021, kutoa huduma za afya kwa binadamu hususani magonjwa yasiyo ambukiza, kutoa huduma za tiba ya  mifugo 

kupitia  hospitali ya rufaa ya wanyama bure kwa jamii, kuchangia damu salama na kufanya michezo mbalimbali ambayo itaambatana na zawadi kwawashindi..

Hayati Edward Moringe Sokoine alifariki dunia kwa ajali ya gari Aprili 12, 1984 akiwa na umri wa miaka 46 katikaMkoa wa Morogoro akitokea Dodoma katika kikao cha Bunge na katika kipindi chake cha uongozi alihudumu kwa vipindi viwili.

“Kwa mwaka huu 2021 itakuwa ni maadhimisho ya 17 kumuenzi Hayati Edward Moringe Sokoine toka kumbukizi ya kwanza mnamo mwaka 1992  ya maadhimisho hayo  ambayo hufanyika kila mwaka Chuoni ” alisema prof. Mwatawala.

Awali akimkaribisha mgeni rasmi mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya kumbukizi ya hayati Edward Sokoine Moringe Prof. Samweli Kabote kutoka SUA alisema kuwa huwezi kuongea historiaya Chuo cha Sokoine cha Kilimo SUA bila kumtaja Hayati Sokoine kwasababu Chuo kimebeba jina lake.

 Wiki ya Kumbukizi ya Hayati Edward Moringe Sokoine mwaka huu yamebeba kaulimbiu isemayo, Teknolojia za kilimo, kuzalisha kwa tija na ushindani katika Soko, Kuelekea Nchi ya Uchumi wa juu wa Kati.   

RC Njombe aagiza bodi ya Parole ikasaidie kupunguza msongamano wa wafungwa

$
0
0

Na Amiri Kilagalila, Njombe

Msongamano wa wafungwa kwenye gereza kuu la mkoa wa Njombe (mpechi) umekuwa kikwazo kikubwa katika utendaji kazi za kila siku katika gereza hilo.

Hayo yameelezwa leo na mkuu wa gereza hilo mkoa wa Njombe, Emmanuel Lwinga katika uzinduzi wa bodi ya Parole ya mkoa huo uliofanyika mkoani hapa.

Amesema gereza hilo lilipaswa kuwa na wafungwa wasiozidi 100 lakini kwasasa kuna wafungwa 300 hali inayosababisha gereza hilo kuwa na msongamano mkubwa.

Amesema  kutokana na wilaya ya Wanging'ombe kutokuwa na gereza hivyo wafungwa wote wa wilaya wanapelekwa katika gereza la mkoa na kusababisha wafungwa kujaa katika gereza hilo.

Amesema kupitia sheria ya Parole itasaidia kupunguza msongamano gerezani kwasababu sheria hiyo inaruhusu wale wenye vigezo ambao wamefungwa zaidi ya miaka minne kunufaika na sheria hiyo.

Amesema  mchako wake unaanzia gerezani kwa kupendekeza jina la mfungwa kisha kwenda katika kijiji anachotoka mfungwa huyo kwa ajili ya kuchunguza.

"Yule aliyefanyiwa kosa anahojiwa kama wanaweza kumpokea na akikubali mapendekezo yanapelekwa bodi ya mkoa na bodi hiyo inapeleka ngazi ya taifa na baadae kwa waziri," amesema   Lwinga.

Amesema wanufaika wa sheria hiyo ni wale wenye makosa madogo isipokuwa ya yanayohusiana na ubakaji na uhalifu wa kutumia silaha, hawahusiki na msamaha huo.

Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhandisi Marwa Rubirya ambaye alikuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo uliofanyika gerezani hapo amesema  malengo ya kuanzishwa bodi ya Parole ni kupunguza changamoto kubwa ya msongamano wa wafungwa katika magereza.

Amesema bodi hiyo itasaidia kupitia orodha ya baadhi ya majalada ili kuona uwezekano wa kupunguza msongamano kwa baadhi yao kuachiwa chini ya sheria hiyo.

"Lengo la pili ni kushirikisha jamii katika suala zima la urekebishaji wa tabia kwa wale wanaokutwa na hatia" amesema  Rubirya.

Baadhi ya wajumbe wa bodi hiyo akiwemo Sheikh wa Mkoa wa Njombe, Rajabu Msigwa na Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) dayosisi ya Kusini, George Fihavango wamesema jamii inapaswa kujifunza kusamehe kwakuwa kila mmoja ni mkosaji mbele ya mungu.

"Katika mazingira ya kidini hata sisi huwa tunamkosea muumba wetu na yeye huwa anatusamehe, anasema nipo tayari kuwasamehe waja wangu pindi wanaponiomba msamaha," amesema  Rajabu.

 

Mwanafunzi wa darasa la tatu afariki baada ya kujaribu kujinyonga

$
0
0

 Na Amiri Kilagalila, Njombe


Mwanafunzi wa darasa la tatu shule ya msingi Ikelu iliyopo Makambako mkoani Njombe, Claud Florence (9) amefariki dunia baada ya kujinyonga akiwa anacheza na wenzake.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Njombe, Hamisi Issah amesema mwanafunzi huyo alikwenda shambani na wazazi wake na wadogo zake watatu akiwa huko alianza kucheza na wadogo zake na baadae kuchukua kikoi na kuanza kujaribisha namna mtu anavyojinyonga.

Amesema baada kufanya kitendo hicho katika mti pori uliopo hapo shambani matokeo yake alijikuta amening'inia kwenye mti huo huku wazazi wakiwa hawana taarifa yoyote wakiwa wanaendelea na kulima.

Amesema wazazi walipofika walifungua hicho kikoi na kumkuta mtoto wao akiwa taabani na kuchukua uamuzi wa kumpeleka hospitali na baadae kufariki dunia.

Amewataka wazazi kuwa makini na malezi ya watoto wao kwani malezi ya watoto ni pamoja na kuangalia aina ya michezo wanayocheza katika mazingira yanayofaa.

"Watoto hawa wamecheza michezo ya kupitiliza mpaka wamejaribisha kujinyonga na mwenzao mmoja kajiua kabisa" amesema Issah.

 

CRDB WAZINDUA RASMI AKAUNTI YA JUNIOR JUMBO AKAUNTI MKOANI ARUSHA

$
0
0

 mkuu wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro katikati akiwa  pamoja na wafanyakazi wa benki ya CRDB mara baada ya kuzindua  rasmi akaunti ya mtoto ijulikanayo kama Junior Jumbo Account
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru  Jelly Murro   akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa benki ya CRDB ,wazazi na watoto juzi  mara baada ya kuzindua rasmi   account ya mtoto ijulikanayo kama [Junior Jumbo account] kutoka CRDB



Na Woinde Shizza , Michuzi TV-ARUSHA

 

Malezi bora katika familia ndiyo msingi wa malezi kwa watoto katika jamii yetu hivyo wazazi wametakiwa kuzingatia kutoa malezi bora kwa watoto wao ndani ya familia na jamii kwa jumla ili kuwa na taifa lenye uchu wa kujiletea maendeleo.

 

Hayo yamesemwa na mkuu wa wilaya ya Arumeru  Jelly Murro  wakati akizindua account ya mtoto ijulikanayo kama [Junior Jumbo account] kutoka CRDB  ambapo alisema  wazazi wanawajibu wa kuwalea watoto katika malezi bora na wawe na utaratibu wa kuwawekea akiba ya pesa kwa ajili ya maisha yao  ya badae ili iweze kuwasaidia katika masomo yao na itawajengea  maadili mazuri ili kujenga taifa bora lenye watoto wanaojitambua, kujithamini.

 

Muro alisema wazazi wana wajibu wa kuwalea watoto katika malezi bora ili kujenga utu, uzalendo na upendo kwa watoto na jamii kwani malezi katika familia ni msingi katika ujenzi wa taifa linalozingatia uzalendo, maadili mema, utu na uwajibikaji katika maendeleo yao na taifa.

 

“unapo muwekea mtoto akiba yake katika benki kwanza inakusaidia wewe mzazi kuwa na uhakikia wa kulipa ada kwa muda wowote pia ,mnajua kabisa wazazi mtoto unaporudishwa rudishwa ada unamuathiri kisaikolojia kwani atapata mawazo mengi ambayo yatampelekea hata kushidwa kufanya vizuri darasani”alisema Muro

  

Kwa upande wake Neema  Njau ambae ni mzazi alisema kuwawekea watoto na vijana akiba ni utaratibu mzuri wa kuweza kuwasadia katika kujiendeleza kielimu na kujenga taifa lenye maadili na upendo.

 

 

 Kwa upande wake meneja biashara wa kanda David Peter  alisema kuwa wanatambua wateja wao wana malengo ambayo wamejiwekea katika maisha yao, na wao kama Benki ya kizalendo wana jukumu la kuhakikisha wateja  wanafikia malengo yao kupitia huduma na bidhaa bunifu zinazotolewa na benki  ikiwemo huduma ya kuweka akiba kupitia akaunti mbalimbali kama vile akaunti hii ya Junior Jumbo account.

 

 

Alisema wanaendelea kuboresha huduma na miundombinu yake ya kutoa huduma hususani ile ya kidijitali, ambapo aliwataka wateja kuwafungulia watoto wao akaunti hii  kwani ni mkombozi mkubwa sana kwa mtoto   na nimsaada mkubwa pia kwa mzazi.


Njombe:Maelfu wajitokeza uwanja wa ndege kupokea mwili wa hayati askofu Alfred Maluma

$
0
0

Gari iliyobeba mwili wa hayati askofu wa jimbo la Njombe ukitoka uwanja wa ndege mara baada ya kuupokea mwili huo uliowasili leo mchana kutokea jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya mapadre mkoani Njombe wakiupokea mwili wa hayati askofu wa jimbo la Njombe kutoka kwenye ndege ulipowasili ukitokea Dar es Salaam.
Mwili wa askofu Maluma ukiwa kwenye jeneza mara baada ya kushushwa uwanja wa ndege ukiombewa tayari kwa kupelekwa kanisani.
Baadhi ya wananchi wakiwa barabarani kushuhudia maandamano mara baada ya kupokea mwili wa askofu Maluma wa jimbo la Njombe.
Kati kati aliyevaa miwani myeupe ni mzee Philip Mangula makamu mwenyekiti wa chama cha mapinduzi CCM Tanzania bara na wakwanza kulia ni mkuu wa mkoa wa Njombe Mhandisi Marwa Lubirya wakiwa kanisani wakati wa kuaga mwili wa askofu Maluma katika kanisa katoliki jimbo la Njombe
Kati kati aliyevaa barakoa ni mbunge wa jimbo la Njombe mjini Deodatus Mwanyika wakiwa kanisani wakati wa kuaga mwili wa askofu Maluma.
 

IMEKULETEA VICHWA VYA HABARI MAGAZETI YA LEO APRIL 13,2021

NJIKU AWATAKA WANAFUNZI KUWA WAZALENDO

$
0
0

Afisa Tarafa Kata ya Ikungi mkoani Singida,  Yahaya Njiku , akihutubia kwa niaba ya mkuu wa wilaya hiyo Edward Mpogolo wakati akizungumza na Vijana Wanafunzi wa Katoliki Tanzania (TYCS) wahitimu wa Kidato cha Sita wa Shule ya Sekondari Ikungi mkoani Singida  katika sherehe ya kuagana na wanafunzi wenzao wa kidato cha 

5-1 iliyofanyika juzi wilayani humo.


Vijana Wanafunzi wa Katoliki Tanzania (TYCS)  wahitimu wa Kidato cha Sita wa Shule ya Sekondari Ikungi wakiwa wamejipanga tayari kuingia ukumbini katika sherehe ya kuagana na wanafunzi wenzao wa kidato cha 5-1 iliyofanyika juzi wilayani humo.
Walimu wakiwa kwenye sherehe hiyo.
Wazazi wakiwa kwenye sherehe hiyo.
Vijana Wanafunzi wa Katoliki Tanzania (TYCS)  wahitimu wa Kidato cha Sita wa Shule ya Sekondari Ikungi wakiwa kwenye sherehe hiyo.
Afisa Elimu Kata ya Ikungi, Mghenyi Nkuwi, akizungumza katika hafla hiyo.
Vyeti vikitolewa.
Vyeti vikitolewa.
Wazazi wakiwa kwenye sherehe hiyo.
Picha ya pamoja na mgeni rasmi.
Mgeni rasmi akikabidhiwa keki..
Mshereheshaji wa sherehe hiyo (MC) akiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi na walimu.



Na Dotto Mwaibale, Singida.


AFISA Tarafa Kata ya Ikungi mkoani hapa Yahaya Njiku amewataka vijana wanafunzi wa Katoliki Tanzania (TYCS) waliohitimu kidato cha sita katika Shule ya Sekondari ya Ikungi kuwa wazalendo wa nchi yetu.

Njiku ambaye alikuwa mgeni rasmi kwa niaba ya mkuu wa wilaya hiyo Edward Mpogolo aliyasema hayo wakati akizungumza na wanafunzi hao katika sherehe ya kuagana na wanafunzi wenzao wa kidato cha 5-1 iliyofanyika juzi wilayani humo.

"Mnapaswa kuwa wazalendo na uzalendo unatafusiri nyingi kwanza unapaswa kuipenda nchi yetu kuifahamu  kuithamini na kuitunza." alisema Njiku.

Alisema wakiwa kama vijana wanaohitimu kidato cha sita na wale ambao wanaendelea na masomo ni lazima kwanza wawe wazalendo.

Alisema sisi tupo katika Taifa la Tanzania hatuna lingine zaidi ya Tanzania hivyo tunapaswa kulitunza na kulitetea popote pale duniani.  

Njiku aliwaambia vijana hao kuwa uzalendo unatakiwa kuuanza wakiwa na umri mdogo na kuwa hawawezi kuwa wazalendo pasipo kulielewa taifa lao kuanzia historia yake, misingi na jinsi lilivyopatikana.

"Niwaombe ninyi wahitimu na nyie mnaoendelea na masomo ni lazima mfahamu historia ya taifa letu kwani leo hii mpo hapa mna furaha kwa kucheza muziki, michezo mbalimbali na kubadilishana mawazo kuna watu waliteseka kuliangaikia taifa letu akiwepo Baba wa Taifa Hayati Julius Kambarage Nyerere na wenzake.

Alisema ni muhimu kwa vijana hao kusoma masomo ya uraia ili waweze kulielewa taifa lao kwani wakilielewa wataweza kulitetea.

Katika hatua nyingine Njiku aliwataka vijana hao kuwa mabalozi wa kuhamasisha amani hapa nchini na kuwaombea viongozi wetu hasa Rais Samia Suluhu Hassan ambaye aliapishwa hivi karibuni kuongoza nchi baada ya aliyekuwa Rais wetu Dkt.John Magufuli kufariki.

Aliwataka wahitimu hao kuendelea kumuomba Mungu ili waweze kuendelea na masomo yao ya  elimu ya juu kwani kumaliza kidato cha 5-6 sio mwisho wa kusoma.

"Nyinyi wanafunzi mnakila sababu ya kuendelea na masomo kwani Serikali  kupitia Rais wetu Mama Samia Suluhu imeweka mazingira bora ya kusoma kwa kutoa elimu bure." alisema Njiku. 

Aidha Njiku aliwaambia wahitimu hao kuwa nidhamu na uwajibikaji ni jambo jema litakaloweza kuwafanya waishi vizuri wakiwa shuleni, nyumbani na jamii na bila kuacha kumuomba Mungu ambaye siku zote hawezi kumuacha mtu amuombaye.

Njiku aliwataka vijana hao kuto jiingiza katika vitendo visivyo na maadili badala yake watumie muda wao kwa kujisomea na kuendeleza vipaji vyao vya michezo walivyonavyo na kuwapa heshima wazazi wao wanao wasomesha kwa kufanya vizuri mitihani yao.

Wahitimu hao 19 katika risala yao kwa mgeni rasmi walitaja baadhi ya mafanikio waliyopata wakiwa shuleni ni kushiriki katika kuchangia ujenzi wa parokia ya mtakatifu Rita wa Kashia wilayani humo.

NAIBU WAZIRI WA MAJI AKAGUA MIRADI YA MABILIONI MBINGA

$
0
0



Naibu Waziri wa maji Maryprisca Mahundi kulia akifungua koki katika mradi wa maji wa Kipapa na Mhilo uliotekelezwa na wakala wa maji vijijini Ruwasa mkoa wa Ruvuma ambao umewezesha wakazi wa kijiji ch Kipapa katika halmashauri ya wilaya ya Mbinga kuondokana na kero ya maji safi na salama iliyokuwepo kwa muda mrefu.


Naibu Waziri wa Maji MaryPrisca Mahundi amefanya ziara ya kikazi Wilayani Mbinga mkoani Ruvuma kwa kukagua miradi ya maji ya mabilioni ya fedha.

Katika ziara hiyo Mahundi amekagua mradi wa maji wa Kipapa na Mhilo ambao umetekelezwa kwenye Kata za Kipapa na Langiro, Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga wenye thamani ya shilingi Milioni 647.4

Mradi huo umekamilika na umeanza kuhudumia wananchi kwa kutoa maji safi na salama.

Naibu Waziri wa Maji pia ametembelea na kukagua miradi mingine miwili ya maji ambayo ni mradi katika Kijiji cha Lifakara unaokadiriwa kugharimu Shilingi Milioni 651 na mradi unaojengwa Kata ya Bethlehemu ambao unatarajia kugharimu sh.Bilioni 1.4 hadi kukamilika kwake.

Katika ziara hiyo Naibu Waziri wa maji pia amekagua miradi ya maji inayotekelezwa kwenye vijiji vya Amani Makolo, Mabuni, Luhagara na Litumbandyosi wilayani Mbinga.

Akizungumza baada ya kukagua miradi hiyo Naibu Waziri wa Maji ametoa mwezi mmoja kwa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Mkoa wa Ruvuma(RUWASA) kuongeza vituo vya kuchotea maji kwenye kitongoji cha Kiosi, Kijiji cha Kipapa.

“RUWASA hakikisheni mnaanza utekelezaji wa mradi wa kusambaza maji kwenye Kijiji cha Langiro Asili, Kata ya Langiro ndani ya kipindi cha miezi mitatu ijayo’’,alisisitiza Mahundi.

Kwa upande wake Meneja wa RUWASA Mkoa wa Ruvuma Mhandisi Rebman Ganshongwa ametoa rai kwa wananchi kutunza vyanzo vya maji sanjari na miundominu ya maji iliyopo kwenye maeneo yao ili miradi hiyo iweze kudumu kwa muda mrefu na kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.

MZUNGUKO WA PILI WA ROBO FAINALI YA UEFA NA EUROPA KUENDELEA WIKI HII

$
0
0

*Bashiri na Meridianbet na Uwe Miongoni Mwa Mabingwa!


HII ni wiki ambayo tutazijua mbivu na mbichi za baadhi ya timu kunako Mashindano ya UEFA na Ligi ya Europa. Dakika 90 zitaamua.


Jumanne hii, Chelsea watawakaribisha FC Porto pale Stamford Bridge. Chelsea anafaida ya magoli 2 aliyopata kwenye mchezo wa kwanza, vipi ataendelea kuwa mbabe au Porto atapindua meza? Meridianbet tumekuwekea Odds ya 1.50 kwa Chelsea.


PSG kuwaalika Bayern Munich katika jiji la Paris. Matokeo ya 3-2 yanawapa matumaini PSG lakini lolote linaweza kutokea kwa mabingwa watetezi – Bayern Munich. Meridianbet tumekusogezea Odds ya 2.30 kwa Bayern Munich.


Jumatano tutatua pale Signal Iduna Park, Borussia Dortmund kuwaalika Manchester City, hapatoshi. Matokeo ya 2-1 pale Etihad ni faida kwa City lakini Dortmund wananafasi ya kupindua matokeo wakiwa kwenye ubora wao. Hii itakuwaje? Unaweza kuifuata Odds ya 1.75 kwa City kupitia Meridianbet.


Liverpool kuwaalika Real Madrid pale Anfield. Licha ya kuwaumiza Aston Villa wikiendi iliyopita, wanakwenda kukutana na Madrid iliyotoka kumfunga Barcelona kwenye El Classico. Faida ya magoli 3, ni motisha kwa Madrid. Meridianbet tumekuwekea Odds ya 2.00 kwa Liverpool.


Alhamisi hii tunasafiri mpaka nchini Italia, AS Roma watawaalika Ajax. Faida ya magoli 2 kwenye mchezo wa kwanza, inawapa nguvu Roma. Ajax watapindua matokeo? Meridianbet tumekupatia Odds ya 2.45 kwa Ajax.


Tutamaliza kwa mchezo wa Slavia Prague vs Arsenal. Timu zote zilitoka sare ya 1-1 pale Emirate Stadium, lakini hali itakuaje Alhamisi hii? Odds ya 1.95 kwa Arsenal inaweza kukutoa kimasomaso baada ya dakika 90 za mchezo huu.


Meridianbet, Nyumba yenye Odds Bora na Bonasi Kubwa!

Viewing all 119811 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>