Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 118616 articles
Browse latest View live

KAWAMBWA AKABIDHI PIKIPIKI KWA MADEREVA BODA NA KUWAASA WAJASIRIAMALI KUUNDA VIKUNDI

$
0
0




*****************************
NA MWAMVUA MWINYI,BAGAMOYO
Mbunge wa jimbo la Bagamoyo, Dkt. Shukuru Kawambwa amekabidhi pikipiki tatu kwa kikundi cha waendesha bodaboda kilichopo kitongoji cha Benki kata ya Dunda ,Huku akiwaasa wajasiriamali kutopuuzia kujiunga vikundi kwani vinasaidia kupata fursa mbalimbali kirahisi.
Pikipiki hizo ambazo zimenunuliwa kutokana na mkopo uliotolewa na halmashauri ya Bagamoyo kwa vijana, zimekabidhiwa kwa kikundi hicho kinachojulikana kwa jina la Umoja wa Madereva wa Bodaboda Stendi Geti namba 4, (UMABOS G4).
Akizungumza wakati wa kukabidhi pikipiki hizo, Mbunge huyo wa jimbo la Bagamoyo Dkt. Shukuru Kawambwa aliwapongeza vijana hao kwa kuchangamkia fursa na kwamba wao ni mfano wa kuigwa.
Alisema Serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi wake Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Magufuli inawajali wananchi wa hali ya chini ndiomana kila halmashauri kuna mfuko kwaajili ya vijana, kinamama na walemavu ambapo makundi hayo hukopeshwa na kurejesha bila ya riba.
Alisema serikali haiwezi kumpa fedha mtu mmoja mmoja lakini inatoa kwa vikundi ili iwe rahisi kuwahudumia watu wengi wenye uhitaji kwa wakati mmoja. 

Kwa upande wake, Diwani wa kata ya Dunda, Dickson Makamba aliwapongeza vijana hao na kusema kuwa hao ni vijana wa mfano katika kata yake. 

Alisema kikundi hicho hakina muda mrefu toka kuanzishwa kwake lakini mafanikio yake ni makubwa katika kipindi kifupi ukilinganisha na vikundi vingine ambavyo vina muda mrefu. 

Awali akisoma taarifa ya kikundi Katibu wa kikundi hicho Abdalla Shabani Jongo alisema malengo yao ni kupata pikipiki tano na kwamba mpaka sasa wamefanikiwa kupata pikipiki tatu .

Mzeewa miaka 75 auawa na kufungwa kamba kuonesha alijinyonga

$
0
0

Na Amiri kilagalila,Njombe
Mzee Arusha Nziku (75) mkazi wa wilaya ya Wanging’ombe mkaoni Njombe,amekutwa amefariki nyumbani kwake huku akiwa amefungwa kamba ndani ya nyumba yake kuonyesha emejinyonga.
Kamanda wa polisi mkoa wa Njombe Hamisi Issa amesema waliotekeleza mauaji hayo walitumia kamba kumfunga na kuonyesha kama amejinyonga.
“Ni mzee ambaye amekufa akiwa nyumbani kwake na hawa wauaji walichokifanya ni kwamba baada ya kumuua wakamfanya kama amejinyonga,ile kamba wameifunga lakini kwa ufupi wa lile jingo na urefu wa ile kamba inaonyesha kifo ni cha mashaka”alisema Hamis Issa
Aidha amesema mpaka sasa jeshi la polisi limeingia kazini kuhakikisha ni kitu gani kilicho sababisha kifo cha mzee huyo.
 

WENYE MAGONJWA SUGU HUATHIRIKA ZAIDI NA COVID -19

$
0
0

Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

NAIBU Waziri wa Afya, Dkt. Faustine Ndugulile amewashauri watu wenye magonjwa sugu kuchukua tahadhari zaidi hasa kwa kupima afya na kufuata ushauri wa wataalamu katika kukabiliana na ugonjwa unaosababishwa na virusi vya  Corona (Covid -19.) ambao hadi sasa maambukizi yake nchini yamefika watu 32 na vifo vitatu.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter Ndugulile amechapisha taarifa iliyoeleza kuwa mtu mwenye magonjwa sugu ikiwemo kisukari, shinikizo la damu, pumu, ugonjwa wa moyo na unene uliopitiliza huathirika zaidi na Covid-19.

Aidha Dkt. Ndugulile ameongeza kuwa mtu mwenye magonjwa hayo yupo kwenye hatari zaidi na wanaweza kupoteza maisha na
amewashauri watu kuchukua tahadhari zaidi kwa kupima afya na kuzingatia ushauri wa kitaalamu juu ya magonjwa hayo ili kupunguza madhara zaidi katika kipindi hiki ambacho dunia inapambana katika kukabiliana na janga hilo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Wizara ya Afya, leo Aprili 10, 2020 jumla ya watu walioambukizwa ugonjwa wa corona imefika 32, na waliofariki dunia kutokana na ugonjwa huo imefikia watatu.

VOA SWAHILI: Zulia Jekundu Episode 276

HOTUBA YA RAIS DKT. MAGUFULI KANISANI CHATO - IBADA YA IJUMAA KUU YA PASAKA APRILI 10, 2020

Covid 19: Meet the 13 Female Health Ministers in Africa Leading the Fight Against Covid-19 Pandemic

$
0
0
Across the world, the Coronavirus has not only become another disaster to wipe us all out of the earth but has also put the spotlight on the level of competence of our political leaders.
In Africa, the case is not different as governments are putting in draconian measures to halt the spread just like their counterparts in Europe and Asia.

With the eminent role health ministers are playing in fighting this global pandemic, I delved into a special finding to uncover the female faces leading the battle and definitely deserve commendation for the works, they have put in so far albeit sorrowful to know that, their works are faced with several challenges because of the under-resourced facilities they manage and how they will be risking their lives in the battle against the virus.

Beyond their competence, they have proven to stand tall in the delivery of their duties as their role in this pandemic go beyond providing counsel to the presidents but an opportunity to manage the global crisis, as they provide all kinds of support to doctors, nurses, and other health workers in their countries while also collaborating with their counterparts to make sure patients receive treatment and citizens are well informed about the situation in their countries.

In my research on 51 African countries, Africa has only 13 female ministers in charge of health across the continent. Out of the 13, 9 are medical doctors and the others were appointed based on their political leadership track records.

The countries that deserve applaud for such laudable appointments of women are Angola, Burkina Faso Congo Republic, Egypt, Eritrea, Ethiopia, Guinea Bissau, Liberia, Mozambique, Somalia, Tanzania and Uganda.

Prince Akpah, Managing Director of leading African PR & Rating Firm, Avance Media, presents the list of 12 Female Health Ministers in Africa leading countries to help fight the Covid-19 disease.

1.       Amna Nurhusein, Minister of Health, Eritrea
She was appointed in 2009 as minister of health in Eritrea. She previously held positions such as Minister of Tourism and is a leading member of the People's Front for Democracy and Justice in Eritrea.

2.       Dr Fawziya Abikar, Minister of Health, Somalia
Dr Fawziya Abikar is the health minister of Somalia

3.       Dr Hala Zayed, Minister of Health and Population, Egypt               
Dr. Zayed served as President of the 57357 Academy of Health Sciences, Chairwoman of the Supreme Committee for Combating Corruption at the Ministry of Health and Advisor to the Minister of Health and Population

She also held other positions including; Director General of the General Department of Hospitals in the Medical Therapy Sector of the Ministry, the Head of the Central Administration for Monitoring and Follow-up and the Head of the Department of Grants and Loans at the Ministry

Dr. Zayed holds a Master’s degree in Obstetrics and Gynecology, and a doctorate and Master's degree in Business Administration

Dr. Zayed supervised a series of national projects in the health sector, in which the World Bank, the World Health Organization and many international donors contributed

4.       Dr. Jacqueline Lydia Mikolo, Minister of Health and Population, Congo Republic       
Jacqueline Lydia Mikolo is Congo Republic’s Minister of Health and Population since May 6, 2016. She was previously Public Procurement and Regulatory Coordinator at the Department of Major Works 

At the 69th World Health Assembly, held May 23–28 in Geneva, she presented the Congolese Health Program, entitled "The march towards development", which sets itself as a primary goal to facilitate access to health for the population with inexpensive and quality care over the period 2016-2021. This goes through several achievements such as the establishment of universal health insurance, the construction of general hospitals in all departments, the strengthening of the management of certain diseases or the maintenance of free access to care for certain segments of the population

       5.      Dr. Léonie Claudine Sorgho/Lougue, Minister of Health, Burkina Faso
Dr. Léonie Claudine Sorgho / Lougue is a radiologist doctor, university Professor of radiology, medical imaging and radio diagnostics. She was Director of the Research and Training Unit in Health Science, Ouaga I Joseph KI-ZERBO University in Burkina Faso from 2015 to 2019 and member of the jury of the 18th and 19th Human Medicine, Pharmacy, Odontology, Veterinary Medicine and Animal Production aggregation competitions at CAMES.

Dr Sorgho / Lougue teaches Radiology, Medical Imaging and Radiodiagnostics at Ouaga University I Professor Joseph Ki-Zerbo and supervises medical and specialization students. She is also Director of the UNESCO Chair "Gender, Women, Science, Society and Sustainable Development" of universities, institutes and research centers, Head of Radiology and Medical Imaging Department and Director in charge of University Hospital Planning and cooperation at the Center Hospitalier Universitaires Pédiatrique (CHUP) Charles De Gaulle.

Dr Sorgho / Lougue is also a member of several university and learned societies: evaluation group of the International Conference of Deans of Faculties of Medicine of French Expression (CIDMEF) and member of the board and the Board of Directors of said Conference, Conference African of the Deans of Faculties of Medicine of French Expression (CADMEF) of which she is the General Treasurer, Burkinabe Society of Radiology and Medical Imaging (SOBURAD) as a founding member and Treasurer

6.       Dr. Lia Tadesse Gebremedhin, Minister of Health, Ethiopia          

Dr Lia Tadesse Gebremedhin is Ethiopia's minister of health. She was previously the executive director of the Center for International Reproductive Health Training at the University of Michigan. She previously served as project director for the Maternal and Child Survival Program at Jhpiego Ethiopia. Lia also led research in Reproductive Health, Public Health and OB-Gyn. 

She earned her doctor of medicine and master of health care administration at Jimma University, and specialized in obstetrics and gynaecology at Addis Ababa University.

7.       Lizzie NKOSI, Minister of Health, Eswatini 
Senator Lizzie Nkosi is Eswantini’s health minister.
                                                                                                       

8.       Maria Inácia Có Sanhá, Minister of Public Health, Family and Social Cohesion, Guinea Bissau
Maria Inácia Có Sanhá, is Guinea Bissau’s Minister of Public Health, Family and Social Cohesion. She graduated in Potuguse at the Escola Normal Superior Tchico Té in Bissau.

She was President of the Instituto de Mulher e Criança, Director General of Social Solidarity and Family, Head of the Department of Information and Professional Guidance, Employment Technician of the General Directorate of Labour, Employment and Professional Training (DGTEFP) - Ministry of Public Service and Labour. 

She twice occupied the portfolio of the Secretary of Hospital Management in the current government before she was promoted to take up the role of Minister of Public Health, Family and Social Cohesion.

9.       Dr. Nazira Abdula, Minister of Health, Mozambique 
A paediatrician by profession, Nazira Abdula graduated from Maputo Central Hospital with complementary stages in the Hospital São João do Porto in Portugal. Abula earned a Master’s degree in Nutrition and Dietitian from the University of Flinders, Australia, in 2006. She worked as a general practitioner at Medical Mavalane General Hospital from 1993 to 1997 and was involved in the program to combat malaria in the Mavalane area. During the cholera epidemic of 1997, she led the cholera infirmary of Maputo Central Hospital. She has taught at the Catholic University of Mozambique, and in the Health Sciences Institute of Maputo and Beira. Having been Deputy Minister of Health from 2010 to 2014 in the previous administration, Abdula was appointed Minister of Health in January 2015.

10.       Dr. Ruth Jane Aceng, Minister of Health, Uganda     
Jane Ruth Aceng is a paediatrician and the Minister of Health in the Cabinet of Uganda. 
She previously served as the Director General of Medical Services in the Ugandan Ministry of Health.
Her service began when she was a medical officer in the health ministry. Before her appointment as the Director General of Medical Services, she was serving as executive director of Lira Regional Referral Hospital.
Dr. Aceng has vast experience both as a manager and a practicing medical personnel, which she accumulated while serving in various capacities as: Medical Officer, Senior Medical Officer, Medical Officer Special Grade, Medical Superintendent, Consultant Paediatrician, Senior Consultant Paediatrician, Hospital Director, and the Director General of Health Services for the Ministry of Health, Uganda.


11.   Dr Silvia Lutucuta, Minister of Health, Angola
Sílvia Paula Valentim Lutucuta, is a Physician, Cardiologist and University Professor, Head of the Postgraduate and Scientific Research Department at the Faculty of Medicine, with experience in Research - Molecular Biology and Genetics of Cardiovascular Diseases.
She entered the Faculty of Medicine Universidade Agostinho Neto-Huambo at just 16 years old, completed her degree in the 6 years established in 1990, as she was the youngest and best student, at just 21 years old, she was offered a scholarship. Immediate Postgraduate study and inspired by her maternal grandmother, a great nationalist Angolan woman who always defended the importance of advanced training in women, her emancipation and economic independence who suffered from severe Heart Disease, she specialized in Cardiology at Hospital Santa Maria in Lisbon - Portugal- Head of Service Celeste Vagueiro and integrating the team of Prof. Doctor Fausto Pinto.
She started his teaching career at just 19 years old, as a Monitor in the Department of Medicine at the Faculty of Medicine in Huambo in the Department of Morphology Chair of Histology.
With the growing need to reinforce the teaching staff of the FMUAN Department of Medicine, she was then transferred to Luanda during the internship and became a supervisor of this department and after completing her degree she moved to the Assistant category, an activity that was interrupted during her training abroad.

12.   Ummy Ally Mwalimu, Minister of Health, Community Development, Gender, Seniors and Children, Tanzania     
Ummy Ally Mwalimu is the Minister of Health, Community Development, Gender, Seniors and Children in the Cabinet of Tanzania since 2015. She is a two-term Member of Parliament, appointed to a seat reserved for women.
She completed her schooling from the Korogwe Girls Secondary School in 1993. In 1998, she received a Bachelor of Laws from the University of Dar es Salaam. She received her Master of Laws degree from the University of Pretoria in 2001. Between 2000 and 2010, she worked in various governmental and NGO agencies in legal, research and governance roles
In President Jakaya Kikwete's administration, she served in a succession of ministerial roles as Deputy Minister in the Ministry of Community Development, Gender and Children and Deputy Minister in the Vice President's Office and the Ministry of Justice and Constitutional Affairs.

13.   Dr. Wilhemina Jallah, Minister of Health, Liberia        
Dr. Wilhelmina Jallah is Liberia’s minister of health but was previously the head of obstetrics and gynaecology at the John F. Kennedy Medical Center in Monrovia, Liberia, 
She helped provide medical services to young survivors of rape, many of whom require fistula repair surgery and has practised medicine in Liberia for a very long time.


Author, Prince Akpah

TEKNOLOJIA MURUA, IFAHAMU INFINIX S5pro YENYE SELFIE YA JUU

$
0
0
TEKNOLOJIA  inaendelea kukua kwa kasi katika uzalishaji wa simu janja na Infinix Imethibitisha hili kupitia toleo jipya la Infinix S5pro iliingia sokoni mapema mwezi huu. Infinix S5pro ni simu ya kwanza kwa kampuni ya Infinix kuwa na teknlojia ya pop up camera.

 Fahamu mengi zaidi ya Infinix S5pro;
Simu hizi zina RAM zenye ukubwa tofauti wa 4GB na 6GB hivyo itakuwezesha kufungua programu au kufanya mambo mbalimbali kwa wakati mmoja bila kukwama kwama, na uwezo wake wa kuhifadhi taarifa (video, picha, miziki, faili) ni 64GB na 128GB. 

Aidha, ina sehemu ya kuweka memory card kwa ajili ya kuiongezea uwezo wa kuhifadhi taarifa.
Kwa wale wanaopenda simu zenye kioo kikubwa na chenye ubora simu hii yenye uzito wa gramu 195 ni kwa ajili yao kwani kioo chake (IPS LCD) kina ukubwa wa inchi 6.53" chenye ubora wa 1080p. 

Kamera yake ya mbele (selfie camera) yenye 40MP ni ya kipekee zaidi ambapo hutokezea juu ya simu pale unapotaka kupiga picha na ukimaliza inarudi kujificha ndani ya simu, (mechanical pop-up piece) hii inakuwezesha kupata picha zenye ubora zaidi.

Wale wapiga picha, simu hii ina kamera 3 za nyuma ambapo kamera ya kwanza ina 48MP (f/1.8 lens), kamera nyingine ina 2MP ambayo hii ni sensor kwa ajili ya picha za karibu (potraits) ambazo huonesha hadi sehemu ya mabega. Kamera ya mwisho (QVGA) ni maalum kwa ajili ya kuweka sawa mwanga wakati wa upigaji picha. Pia inauwezo wa kurekodi video zenye ubora na muonekano ang'avu wa hadi 1080p. Yote haya ni kuhakikisha wewe mtumiaji unapata kilicho bora zaidi.

Uwezo wa betri ya simu hii ni 4,000 mAh ambayo inaweza kukaa zaidi ya siku moja bila kuichaji. Simu hii ina mfumo endeshi (OS) Android 10, na utaweza kuuboresha kadiri maboresho yatakavyotoka. 

Katika kuhakikisha kuwa unapata habari mahali popote ulipo, ndani ya simu kuna programu ya redio (FM Radio). Jingine ni kwamba tumeimarisha usalama wa taarifa zako kwani utaweza kuifunga simu yako kwa kutumia alama za kidole.

Wajanja wanatumia vyenye ubora wa kipekee, tembelea sasa duka letu la Infinix lililopo karibu nawe uwe wa kwanza kujipatia simu hii. Ukikosa utaambia nini watu?

Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) yatoa Zawadi kwa watoto

$
0
0

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akimkabidhi mtoto mwenye matatizo ya moyo aliyelazwa katika Taasisi hiyo Elizabeth Omari zawadi ya Pasaka wakati wa ugawaji wa zawadi hizo kwa watoto leo Jijini Dar es Salaam


Maafisa Uuguzi wa wodi ya watoto wenye magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiongozwa na Mkurugenzi wa Kurugenzi ya huduma ya Uuguzi Robert Mallya kumkabidhi zawadi ya pasaka mama wa mtoto Wilson Willium wakati wa ugawaji wa zawadi hizo kwa watoto leo Jijini Dar es Salaam

 Maafisa Uuguzi wa wodi ya watoto wenye magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiongozwa na Mkurugenzi wa Kurugenzi ya huduma ya Uuguzi Robert Mallya kumkabidhi zawadi ya pasaka mama wa mtoto Silvanus Brayton  wakati wa ugawaji wa zawadi hizo kwa watoto leo Jijini Dar es Salaam
Maafisa Uuguzi wa wodi ya watoto wenye magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Teresia Marombe na Rehema Bakari wakimkabidhi mtoto mwenye matatizo ya moyo aliyelazwa katika Taasisi hiyo Ikram Samari zawadi ya pasaka wakati wa ugawaji wa zawadi hizo kwa watoto leo Jijini Dar es Salaam
Picha na: Genofeva Matemu - JKCI

TEKNOLOJIA MURUA, IFAHAMU INFINIX S5pro YENYE SELFIE YA JUU

$
0
0
TEKNOLOJIA  inaendelea kukua kwa kasi katika uzalishaji wa simu janja na Infinix Imethibitisha hili kupitia toleo jipya la Infinix S5pro iliingia sokoni mapema mwezi huu. Infinix S5pro ni simu ya kwanza kwa kampuni ya Infinix kuwa na teknlojia ya pop up camera.

 Fahamu mengi zaidi ya Infinix S5pro;
Simu hizi zina RAM zenye ukubwa tofauti wa 4GB na 6GB hivyo itakuwezesha kufungua programu au kufanya mambo mbalimbali kwa wakati mmoja bila kukwama kwama, na uwezo wake wa kuhifadhi taarifa (video, picha, miziki, faili) ni 64GB na 128GB. 

Aidha, ina sehemu ya kuweka memory card kwa ajili ya kuiongezea uwezo wa kuhifadhi taarifa.
Kwa wale wanaopenda simu zenye kioo kikubwa na chenye ubora simu hii yenye uzito wa gramu 195 ni kwa ajili yao kwani kioo chake (IPS LCD) kina ukubwa wa inchi 6.53" chenye ubora wa 1080p. 

Kamera yake ya mbele (selfie camera) yenye 40MP ni ya kipekee zaidi ambapo hutokezea juu ya simu pale unapotaka kupiga picha na ukimaliza inarudi kujificha ndani ya simu, (mechanical pop-up piece) hii inakuwezesha kupata picha zenye ubora zaidi.

Wale wapiga picha, simu hii ina kamera 3 za nyuma ambapo kamera ya kwanza ina 48MP (f/1.8 lens), kamera nyingine ina 2MP ambayo hii ni sensor kwa ajili ya picha za karibu (potraits) ambazo huonesha hadi sehemu ya mabega. Kamera ya mwisho (QVGA) ni maalum kwa ajili ya kuweka sawa mwanga wakati wa upigaji picha. Pia inauwezo wa kurekodi video zenye ubora na muonekano ang'avu wa hadi 1080p. Yote haya ni kuhakikisha wewe mtumiaji unapata kilicho bora zaidi.

Uwezo wa betri ya simu hii ni 4,000 mAh ambayo inaweza kukaa zaidi ya siku moja bila kuichaji. Simu hii ina mfumo endeshi (OS) Android 10, na utaweza kuuboresha kadiri maboresho yatakavyotoka. 

Katika kuhakikisha kuwa unapata habari mahali popote ulipo, ndani ya simu kuna programu ya redio (FM Radio). Jingine ni kwamba tumeimarisha usalama wa taarifa zako kwani utaweza kuifunga simu yako kwa kutumia alama za kidole.

Wajanja wanatumia vyenye ubora wa kipekee, tembelea sasa duka letu la Infinix lililopo karibu nawe uwe wa kwanza kujipatia simu hii. Ukikosa utaambia nini watu?

SERIKALI YASEMA LICHA YA MIPAKA YA NCHI KUJIFUNGA WAGENI WACHACHE WANAOINGIA NCHINI WANAHUDUMIWA KWA HADHI SAWA NA MATAIFA MENGINE DUNIANI.

$
0
0

Serikali imesema licha ya mipaka ya nchi kujifunga kutokana na janga la ugonjwa wa COVID 19,wageni wachache wanaoingia nchini wanapokelewa kwa mujibu na taratibu za kuingia nchini na kuhudumiwa kwa hadhi inayoendana na mahitaji ya Kimataifa kama ilivyo katika nchi nyingine yeyote duniani huku tahadhari ya kujikinga na ugonjwa huo ikipewa kipaumbele.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Kanali Wilbert Augustine Ibuge ameyasema hayo alipofanya ziara katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kukagua na kujionea namna wageni kutoka mataifa mbalimbali wanavyopokelewa na hatua wanazopaswa kuzifuata kabla ya kuruhusiwa kuingia nchini.

Balozi Kanali Ibuge amesema licha ya ukweli kwamba kwa sasa wageni wanaoingia nchini ni wachache sana kutokana na mipaka kujifunga ni muhimu serikali kuhakikisha kuwa wale wachache wanaoingia wanafuata taratibu za nchi na kupewa utaratibu wa namna ya kujikinga na ugnjwa wa COVID 19 bila ya uwepo wa malalamiko kutoka kwa wageni hao.

Ameongeza kuwa ameridhishwa na hali ilivyo katika uwanja huo wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kwa kuwa hadhi wanayopewa wageni hao haina tofauti na hatua zinazochukuliwa katika mataifa mengine duniani na kwamba ni muhimu kufanya hivyo ili kuhakikisha usalama wa Taifa na raia wake kwa ujumla.

Amewataa watumishi wanaoendelea kutoa huduma katika uwanja huo kuchukua tahadhari ya kujikinga na COVID 19 huku wakitumia kauli nzuri wakati wa kutoa huduma.

Katika ziara hiyo Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Kanali Wilbert Ibuge amekagua jengo la kwanza la uwanja huo na jengo jipya la tatu akiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka ya viwanja vya ndege TAA Mhandisi Julius Ndyamukama.

WAZAZI NA WALEZI WASHAURIWA KUWALINDA WATOTO WAO DHIDI YA UGONJWA WA CORONA (COVID-19).

$
0
0
NA PATRICIA KIMELEMETA

WAZAZi na walezi wameshauriwa kuwalinda watoto wao ili wasiweze kupata maambukizi ya ugonjwa wa covid -19 ambao unaweza kuhatarisha maisha yao.

Rais wa Chama Cha Madaktari Tanzania (MAT), Dr Elisha Osati amesema kuwa, mzazi au mlezi ana jukumu la kumlinda mtoto wake ili asiweze kupata maambukizo hayo hasa katika kipindi hiki ambacho Dunia imekumbwa na ugonjwa huo.

"Watoto walio chini ya miaka 8, bado wadogo, wanahitaji msaada wa ulinzi na usalama kutoka kwa wazazi au walezi wao, hivyo basi katika kipindi hiki ambacho Dunia imekumbwa na maambukizi ya ugonjwa wa covid-19, wanapaswa kuwa makini na kuhakikisha kiwa,watoto wao hawapati maambukizi haya na wanaendelea kuwa salama," amesema Osati.

Akitolea mfano wa mtoto mwenye umri wa chini ya mwaka mmoja ambaye hawezi kufanya chochote bila msaada wa mzazi au mlezi wake,jukumu kubwa la kumlinda ili asiweze kupata maambukizi hayo linabaki kwa mzazi au mlezi.

Ameongeza kuwa, kwa sababu bado anahitaji malezi na makuzi yaliyo salama kutokana na umri wao kuwa mdogo na kwamba hawawezi kujitetea kwa jambo lolote ambalo litaweza kuhatarisha maisha yake.

Amesema kuwa, kutokana na hali hiyo, wazazi au walezi wanapaswa kusikiliza taarifa zinazotolewa na serikali  kuhusiana na ugonjwa huo na kuchukua tahadhari kwao na kwa watoto wao ili wasiweze kupata maambukizi au kuwaambukiza.

"Serikali inatoa taarifa za Mara kwa mara kuhusiana na ugonjwa wa Covid -19, hivyo basi ni muhimu kwa wazazi au walezi kuzifuatilia na kuchukua tahadhari ili kuepuka matatizo yanayoweza kujitokeza," amesema.
Rais wa Chama Cha Madaktari Tanzania (MAT), Dr Elisha Osati

KIWANDA CHA AFRICAB KINAVYOSISITIZA UBORA KATIKA UZALISHAJI BIDHAA ZA PVC

$
0
0
Na Said Mwishehe, Michuzi TV

UWEPO wa biashara ya mabomba ya plastiki (PVC) yasiyo na ubora katika soko nchini kwa kiasi kikubwa kumetajwa kuchangiwa na baadhi ya wenye viwanda vinavyozalisha bidhaa hiyo kutozingatia sheria sambamba na waagizaji wasio wa nje ya nchi wasio waaminifu.

Hatua hiyo pamoja na mambo mengine imebainishwa kuwa moja ya sababu kuu ya wananchi kupata hasara mbalimbali hususani pale linapotokea bomba hilo kupasuka na kusababisha athari katika njia za umeme na wakati mwingine hata kusababisha kuungua kwa nyumba na miundombinu mingine ya umeme.

Kimsingi mabomba hayo(PVC), huzalishwa maalumu kwa ajili ya matumizi ya usafirishaji wa nyaya za umeme katika ujenzi wa nyumba na majengo mengine lakini pia miundombinu inayotekelezwa katika miradi mbalimbali ikiwemo ya majengo na umeme nchini.

Akizungumza hivi karibuni kuhusu shughuli zinazofanyika kiwandani hapo, Mkurugenzi Mkuu wa Kiwanda cha utengenezaji wa vifaa vya umeme cha Kilimanjaro Cables (AFRICAB) kinachozalisha mabomba ya PVC maalumu kwa ajili ya usambazaji wa umeme Mansoor Moiz, ameeleza kwa kina kuhusu ubora wa bidhaa zinazozalishwa kiwandani hapo.

Kwa mujibu wa Mansoor, Tanzania inapiga hatua kubwa katika uzalishaji wa mabomba hayo, isipokuwa kumekuwepo na changamoto ya baadhi ya wenye viwanda hivyo kuzalisha bidhaa zisizo na ubora.

Alisema uzalishwaji huo wa mabomba yasiyo na ubora unaotakiwa kulingana na viwango vya TBS, kimsingi umekuwa ukisababisha athari katika soko na kwamba imekuwa ngumu kuwabaini wahusika wa bidhaa hizo kwa kuwa hawajitambulishi katika bidhaa hizo kama watengenezaji.

“Kujenga jina ya kampuni inachukua maisha lakini kwa mara moja unaweza kuanguka, tunapaswa kuzingatia ubora wa bidhaa zetu kulingana na matakwa ya Shirika la Viwango Tanzania(TBS),ni wajibu wetu kuwa waminifu kwa Serikali yetu, kama wazalishaji wote tujifanya hivyo wazi kuwa tutaepusha athari kwa watanzania wenzetu ikiwemo kuokoa nyumba zao kuungua, fedha na hata maisha yao kwa ujumla,” amesema Mansoor

Ameongeza kimsingi kazi ya usambazaji wa nyaya ‘cables’ maeneo tofauti ikiwemo chini ya ardhi inahitaji mabomba yenye viwango vya kutosha na teknolojia ya hali ya juu, tofauti na hivyo mabomba hayo yanaweza kupasuka na kusababisha madhara yasiyo tarajiwa huku akiwataka wenye viwanda vinavyozalisha bidhaa hiyo nchini kote kuifanya kazi hiyo kwa ushirikiano wa pamoja na weledi .

“Ni muhimu tushirikiane kwa pamoja katika suala hili, tujivunie nchi yetu na viwanda vyetu huku tukijua kuwa kuzalisha bidhaa zisizo na ubora ni kuwaumiza wananchi wenzetu na kulikosea heshima taifa letu ambalo katika uongozi huu chini ya Rais John Magufuli limetupa fursa kubwa ya kuwekeza katika viwanda,” amesisitiza Mansoor

Hivi karibuni Rais John Magufuli alitoa rai kwa wenye viwanda hao kuhakikisha wanazalisha bidhaa zenye ubora pamoja na kuangalia uwezekano wa kuwa na bei ya chini ya bidhaa hizo ili kulinda soko la ndani sambamba na kumwezesha mwananchi kumudu.

Amesema ni ajabu kwa bidhaa zinazozalishwa hapa nchini kuwa na bei ya ghali zaidi ya zile zinazoingizwa kutoka nje ya nchi na kuhoji nini sababu ya viwanda hivyo kuwa na bei ya juu katika bidhaa hizo wakati hazilazikiki kusafirishwa kutoka nje ya nchi.

UGONJWA WA MATUNDU KWENYE MOYO NI MIONGONI MWA MAGONJWA HATARISHI KWA WATOTO WACHANGA

$
0
0

NA PATRICIA KIMELEMETA

UGONJWA wa matundu kwenye moyo kwa watoto wachanga ni miongoni mwa magonjwa hatarishi ambayo yanaweza kusababisha udumavu au wakati mwingine kifo Kwa mtoto.

Ugonjwa huo ambao unaathiri kuta za ventrikali za moyo au kwa kitaalamu ujulikana kama (Ventricular Septal Defect) (VSD) unashambulia moyo wa mtoto jambo ambalo linaweza kumuongezea maradhi mengine.

Mtoto mwenye matatizo hayo,anaweza kubainika mara baada ya kufanyiwa vipimo ambapo kwa sasa hali inaonyesha kuwa, watoto wawili hadi 6 kati ya 1,000 wanaweza kuzaliwa na tatizo hilo.

Rais wa Chama Cha Madaktari Tanzania(MAT),Dk. Elisha Osati amesema kuwa, kutokana na hali hiyo, wazazi na walezi wana jukumu la kuwalinda watoto wenye natatizo hayo ili wasiweze kupata maradhi mengine ambayo yataweza kuhatarisha maisha yao.

"Taasisi ya Jakaya Kikwete imekua mstari wa mbele kuwasaidia na kuwafanyia operesheni watoto wanaozaliwa na matatizo ya moyo, lengo ni kuhakikisha wanapona kabisa ili waweze kukua vizuri," amesema Dk Osato.

Ameongeza kuwa, hivyo basi wazazi na walezi wana jukumu la kuhakikisha kuwa, wanawapeleka watoto wao hospitali mapema ili waweze kupatiwa matibabu pamoja na kuwalinda ili wasiweze kupata maradhi mengine ambayo yatahatarisha maisha yao.

Amesema kuwa, jukumu la ulinzi na usalama wa mtoto mwenye matatizo hayo linaanzia kwa mzazi au mlezi, hivyo basi wanapaswa kutimiza wajibu wao ili kuepuka changamoto za makuzi ya mtoto zinazoweza kujitokeza.

Amesema kuwa, serikali itaendelea kutoa elimu ya malezi na makuzi kwa wazazi ili watoto waweze kukua vizuri ili wasiweze kupata matatizo mengine ambayo yatasababisha kudumaza ubongo wao na kushindwa kukua ipasavyo.
 

Bora useme usaidiwe kuliko kufa na tai shingoni

$
0
0
Na Paul R.K Mashauri

Mara nyingi unapopitia tatizo kubwa katika maisha mfano kupoteza mtu au watu unaowapenda iwe ni mtoto, mume au mke sio jambo ambalo utasahau ndani ya mwaka mmoja. Kuna ambao walipoteza familia zao wakati wa mauaji ya wayahudi yaliyofanywa na Adolf Hitler kule Ujerumani zaidi ya miaka 80 iliyopita lakini mpaka leo vizazi na vizazi havijasahau. 
Kuna waliopoteza familia zao wakati wa mauaji ya halaiki ya Rwanda "Rwanda Genocide" zaidi ya miaka 20 iliyopita lakini mpaka leo hawajasahau. Kuna ambao wamepoteza familia zao wakati huu wa COVID-19 na hatujui wanapitia nini. 
Kule Italia kwa mfano unakuta mtu amebaki yeye tu. Kapoteza mke, watoto, mashangazi, wajomba nk. Ukivaa viatu vyao utajua ninachozungumza. Hii huleta kitu kinaitwa "Post-traumatic stress disorder (PTSD)"

Dalili za "Post-traumatic stress disorder (PTSD") ni pamoja na "kupoteza-focus mara kwa mara", kukosa usingizi mpaka utumie dawa za usingizi "insomnia", msongo wa mawazo mpaka utumie "depressants" nk. Kuona mauzauza yaani unaona vitu ambavyo havipo mpaka watu wanafikiri "umerogwa" kumbe ni "Post-traumatic stress disorder (PTSD"). Ni mbaya sana usiombe upitie hiyo kitu. Ukipata hili tatizo mtafute "therapist" kwa ajili ya kitu kinaitwa "Cognitive Restructuring" au "Neuro-Linguistic Programming". Usiache iendelee ndani ya ubongo wako. Madhara yake ni kupata ajali, kushindwa kufanya kazi vizuri, kufukuzwa kazi pia mawazo ya kujinyonga "suicidal thoughts"

Nilipewa wimbo huu uitwao "you can Forgive" nilipokumbuka ziara yangu kule Kibondo na Kasulu katika kambi za wakimbizi wa Burundi na Rwanda. Kule nilikutana na kijana ambaye alipoteza familia yake yote, mali zake zote na biashara zake zote. Baadaye nikasoma kitabu kinaitwa LEFT TO TELL cha dada mmoja Mnyarwanda anaitwa Immaculee Ilibagiza ambaye naye alipoteza familia yake wakati wa mauaji ya halaiki nchini Rwanda. Wote hawa walipitia "Post-traumatic stress disorder (PTSD)". Immaculee Ilibagiza alipona haraka "recovery" kwa sababu ya imani yake kwa Mungu. Alipoona wimbo huu alilia.

Kupata "Post-traumatic stress disorder (PTSD)" sio lazima uwe umepitia mauaji ya haraiki "genocide" au uwe mkimbizi. Wapo wanaopoteza watoto wao au ndugu zao pia wakapata hili tatizo. Kila siku unawaza pengine kuna mahala ulikosea ndio maana mtoto wako akaondoka. Ukiona watoto wa wengine unaumia roho nk. Nina kesi ya namna hiyo ambayo mama mmoja "banker" alishindwa kabisa kufanya kazi ikabidi anitafute na mimi kwa sababu sio eneo langu nikampeleka kwa "counsellor" Dr. Chris Mauki.

Inawezekana leo ukawa huna "Post-traumatic stress disorder (PTSD)" lakini huwezi kujua kesho au keshpokutwa. "Nobody knows tomorrow except God". Nimepitia huko ndio maana ninaona ni vyema kuongea na wewe. Nilipopitia "Post-traumatic stress disorder (PTSD)" miaka michache iliyopita nilipata ajali mbaya 3 na sikuwezi kufanya kazi kwa miaka 3 mfululizo. "It was terrible". Nilipopata ajali, sikuwa nimelewa pombe na wala sikuwa najifunza gari lakini sikuwa na uwezo wa ku"concentrate" au kuwa na "focus" nikiwa barabarani. Ilinichukua muda sana ku "recover" kwa sababu wakati huo sikuwa naelewa kuwa napitia "Post-traumatic stress disorder (PTSD)".

Wewe unabahati unasoma mambo haya kwa mtu aliyepitia. Ina maana siku ukipitia tulichopitia sisi utajua kinachotokea na utajua nini ufanye. Mfano, wengine wanapitia "Post-traumatic stress disorder (PTSD)" wakipata kesi mfano kesi za mauaji, kesi za uhujumu uchumi nk. Unaweza ukasikia mtu amefariki ghafla kwa sababu ya presha lakini ukweli ni kwamba presha alikuwa nayo siku zote isipokuwa tatizo analokabiliana nalo linampa sana msongo wa mawazo kiasi kwamba amepata "depression" na matokeo yake ni "Post-traumatic stress disorder (PTSD)".

Mwingine inaweza ikawa ni ugonjwa alionao ambao hana uhakika wa kupona mfano "cancer". Kwa kujua kuwa ugonjwa wake ni mbaya, huyu mtu anaingia katika hatua ya "Post-traumatic stress disorder (PTSD)". Hata kama alikuwa aishi miaka 20 mingine, kwa sababu ya mawazo mengi yanayozunguka kichwani kwake anajikuta akiondoka mapema zaidi kuliko ambavyo ilistahili. Anaanza kuona vitu ambavyo wewe huviona. Unaweza ukasema ni "spiritual" lakini kumbe sio "spiritual" ni tatizo la "Post-traumatic stress disorder (PTSD)". Hii ni kuonyesha tu kuwa tatizo hili linaweza likampata mtu yoyote.

Kuna namna nyingi za kugundua kuwa unaelekea katika "Post-traumatic stress disorder (PTSD)". Ni zipi hizo? Kwanza kabisa unapopata tatizo lolote linalokutia hofu, mashaka au kukushtua na kukupa msongo wa mawazo "stress" unapitia hatua kubwa 4 ambazo ni 1. kukataa "denial" 2. hasira "grief" 3. "depression" 4. "bargaining" 5. "acceptance". Wewe hujawahi kuambiwa fulani amefariki ukakataa mpaka siku ya kuaga ndio ukakubali? Au unaambiwa mke wako kafumaniwa unakataa! Unasema "mama Athumani? Haiwezekani wamekosea jina!

Kwahiyo ukipata tatizo lolote iwe ni ugonjwa, kesi, ndoa jaribu sana kuchunguza uko katika hatua gani. Je ni hatua ya 1. kukataa "denial" 2. hasira "grief" 3. "depression" 4. "bargaining" au hatua ya 5. "acceptance". Hii ni muhimu ili uwe na uwezo wa kujua hapa nahitaji msaada na kweli utafute msaada kabla mambo hayajaharibika. Kwa sababu ukiingia katika "depression" tayari ni tatizo. Ni muhimu sana ukawahi ukiwa katika hatua ya kwanza kabla hujaingia hatua ya pili.

Kwanini nasema ni bora utafute msaada ukiwa katika hatua ya kwanza. Ni kwa sababu ukishaingia katika hatua ya majuto "grief" mara nyingi kuna uwezekano pia wa kupata hasira. Hata ukisikia mtu amemkata viungo vya siri mke wake au mume wake ujue alikuwa katika hatua hii ya pili. Ukipata hasira unaweza ukafanya jambo lolote baya. Na pia ukivuka hatua ya "grief" ukaingia hatua ya "drepression" maana yake ni kwamba uwezo wako wa kufikiria umeathiriwa na msongo wa mawazo. Kwa mantiki hiyo unaweza ukafanya maamuzi au kuapata matatizo ambayo wewe mwenyewe huoni wala huna utambuzi wake. Ndio maana ukifikia hatua hii, wengi hufikiria kukupelea "rehab"-Kigamboni au Bagamoyo.

Swali ni kwanini wengi wanashindwa kuvuka hatua ya kwanza? Ni kwa sababu ya kutokuwa na utamaduni wa kuzungumza "changamoto zetu". Tofauti na jamii za kimagharibu mfano wazungu, Afrika hatuna utamaduni wa kusema yanayotusibu "sharing". Mara nyingi tunaona aibu kusema "nina tatizo". Unawaza watu watanifikiriaje? Na hii ni kwa sababu pia ya kupenda umbeya. Jamii zetu zinapenda sana maneno maneno hasa matatizo ya watu "small talk". Kwahiyo hofu tuliyonayo ni kwamba tukisema basi maneno yatasambaa mji mzima. Ambayo ni kweli. Unamwambia jambo lako mtu kesho unalikuta "group la WhatsApp kama siyo Instagram.

Hii ni tofauti na nchi za kimagharibi ambapo kuna makundi maalum "support groups" kwa watu wanaopitia matatizo. Hakuna wa kumcheka mwenzake wala kumshangaa. Ukipoteza kazi kuna wenzako ambao pia wamefukuzwa kazi wanakutana katika "support group". Umechumbiwa ghafla mume mtarajiwa haonekana kuna wenzako wenye tatizo kama lako nao wanakutana "support group". Kwetu ukitolewa mahari halafu mume akakimbia hakuna wa kukutana nawewe zaidi ya kukutana na maneno mtaana kuwa "unagundu". Ndio maana watu wanakufa na tai shingoni. Kwa sababu mazingira yetu ni ya kupenda kuona watu wana matatizo, wanashindwa, wanadhalilika, wanashitakiwa, wanatumbuliwa, wanasambaratika.

Sasa ufanye nini? Kutokana na hali yetu ni vyema unapogundua kuwa una tatizo ukatafuta mtu unayemuamini sana wa kuzungumza naye. Ukishindwa kabisa basi nenda kwa mtaalam "counsellor" ambaye yeye kwa taaluma yake ni marufuku kutoa siri na akitoa siri yako una uwezo wa kumshitaki kisheria. Anatakiwa awe na usiri "confidentiality". lakini usisahau kuwa yeye pia ni mwanadamu. Kwahiyo unatakiwa uwe na imani kwa Mungu wako. Kumbuka hata mshauri "counsellor" naye anapitia changamoto kama za kwako. Usifikiri kwa sababu mtu ni "counsellor" basi mambo yake shwari. Dunia iache kama ilivyo!

Kwa hiyo kimbilio la pekee ni kwa Mungu wako. Soma Biblia ina mifano mingi sana ya watu waliopitia katika matatizo kama yako lakini mwisho wake waliyashinda na kuishi pasipo "Post-traumatic stress disorder (PTSD)". Kuna Ayubu ambaye alipoteza mali zake zote na magonjwa juu yake. Mke wake akamshangaa, marafiki zake wakamsema na mengine mengi. Lakini Mungu akampa uponyaji na mali maradufu. 
Kuna Yusufu ambaye yeye aliuzwa na ndugu zake. Kisha akasingiziwa ametaka kumbaka mke wa Potifa na kuwekwa jela. Lakini Mungu akamtoa na kumpa uwaziri mkuu nchini Misri. Hizi sio hadithi, ni historia ya kweli katika historia ya dunia na ushahidi upo. 
Ninachokisema ni kwamba kuna namna nyingi za kuepuka "Post-traumatic stress disorder (PTSD)".Kuna kuongea na watu unaowaamini, Kuna kumuona "counsellor". Lakini kiboko ya yoye, muombe Mungu na soma Biblia. Unapotafakari yote haya sikiliza maneno ya faraja katika wimbo huu wa Paul Mashauri-Faraja@2019

All rights reserved. No part of this article may be reproduced, distributed, or transmitted in any form or by any means including photocopying, recording or other electronic or mechanical methods, without the prior written permission of the author. You can contact the author through ceo@masterclassworldwide.co.tz or Tel: +255 714 508508-Paul R.K Mashauri.

MBUNGE KINGU AUNGA MKONO AGIZO LA RAIS KUCHAPA KAZI KIPINDI HIKI CHA CORONA

$
0
0

 Katibu wa Mbunge wa Singida Magharibi, Abubakari Muna (katikati), akikagua ujenzi wa nyumba ya mama na mtoto inayojengwa Kata ya Muhintiri wilayani Ikungi.
 Ujenzi ukiendelea.
 Hapa wakipeana maelekezo ya ujenzi huo.
Ujenzi wa choo cha Zahanati ya Kata ya Muhintiri ukiendelea.



Na Dotto Mwaibale, Singida.

MBUNGE wa Singida Magharibi, Elibariki Kingu ameendelea kuunga mkono agizo la Rais Dkt. John Magufuli la kuwataka wananchi kote nchini kuendelea kuchapa kazi katika kipindi hiki ambacho tunakabiliwa na ugonjwa wa corona.

Kingu licha ya kuwa Bungeni amekuwa akiendelea kutekeleza miradi yake ya maendeleo jimboni kwake kwa usimamizi wa Katibu wake Abubakari Muna jambo ambalo limewatia moyo wananchi na kujitojeza kushiriki huku wakichukua tahadhari ya kujikinga na maambukizi ya Virusi vya corona.

Akizungumzia na waandishi wa habari  juzi, Kingu alisema kazi za maendeleo zinaendelea kama kawaida kama Rais John Magufuli alivyoelekeza.

"Nipo bungeni lakini kazi za maendeleo jimboni zinaendelea na zinasimamiwa na Katibu wangu Muna na wananchi wanajitokeza kwa wingi kushiriki" alisema Kingu.

Alisema miradi inayoendelea kujengwa ni ujenzi wa nyumba ya mama na mtoto na choo cha Zahanati ya Kata ya Muhintiri.

Kingu alisema mradi mwingine ni ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Mpetu na Kinyampembee ambao ujenzi wake umefikia ngazi ya linta.

Rais Dkt.Johnn Magufuli alipokuwa akihutubia taifa kuhusu ugonjwa wa corona aliwataka wananchi kuendelea kufanya kazi huku wakichukua tahadhari ya kujikinga na ugonjwa huo.

Alisena hakuna nradi utakaosimama kwa sababu ya kuhofia ugonjwa huo na kuwataka wananchi kila mmoja kufanya kazi ili kuinua uchumi wa nchi yetu.

UN chief Special Appeal to Religious Leaders

MAHOJIANO NA MWANAMUZIKI MKONGWE ALAIN DEKULA KAHANGA 'VUMBI' SEHEMU YA KWANZA

MAHOJIANO NA ALAIN DEKULA KAHANGA 'VUMBI' SEHEMU YA PILI

MIAKA 36 YATIMIA TOKA KIFO CHA CAMARADA EDWARD MORINGE SOKOINE!!!

$
0
0
1. USULI:

Jumapili mujarab ya leo, tarehe 12.4.2020, Taifa letu linatimiza miaka 36 toka kipenzi cha Watanzania, Mh. EDWARD MORINGE SOKOINE afariki kwa ajali ya gari siku ya Alhamis, tarehe 12.4.1984 eneo la Dakawa, wilayani Mvomero, mkoani Morogoro.

ATIKALI hii inamuelezea Kiongozi huyu shupavu toka alipozaliwa hadi alipofariki. Hii itawasaidia wengi, hasa The Dot.Com Generation, kuelewa kwanini Taifa linamuenzi Kiongozi huyu ambaye alikuwa ni Zawadi ya Mungu kwa Watanzania.

2. SOKOINE Azaliwa

Jumatatu ya tarehe 1.8.1938, katika kitongoji cha Kilasho, kijiji cha Emairete, Monduli Juu, Arusha, huku mvua kubwa na radi vikirindima,  alizaliwa mtoto wa kiume buheri wa afya, aliyeitwa EDWARD MORINGE SOKOINE. Baba yake aliitwa SOKOINE OLE SEVERE na mama yake aliitwa NAPELEL SINYATI NOOMAYAKI.


3. SOKOINE Apelekwa Shule

Mwaka 1949, akiwa na miaka 11, wazazi wa wake walimpeleka shule ya msingi Monduli.  Mwaka 1953, alifanya mtihani wa kitaifa "STD Four Territorial Examinations" na baada ya kufaulu akajiunga na "Monduli Middle School " hadi mwaka 1956 na baadaye akajiunga na shule ya sekondari Umbwe.

4. SOKOINE Ajiunga TANU

Tarehe 1.1.1961, SOKOINE alijiunga na chama cha Tanganyika African National Union (TANU) kilichokuwa kikipigania uhuru wa Tanganyika.

5. SOKOINE Agombea Ubunge 1965

Tarehe 25.10.1965, SOKOINE, akiwa kijana mdogo tu wa miaka 27, lakini mwenye akili na ubunifu mwingi, aligombea na kushinda ubunge kwa kishindo jimbo la Monduli.

6. Mh. SOKOINE Aukwaa Uwaziri Mdogo

Mwaka 1967, SOKOINE akiwa na miaka 29 tu, aliteuliwa na Rais NYERERE kuwa Naibu Waziri, Wizara ya Mawasiliano, Uchukuzi na Kazi.

7. Mh. SOKOINE Ashinda Ubunge 1970

Katika uchaguzi mguu, tarehe 25.10.1970,   Mh. SOKOINE aligombea tena ubunge jimbo la Manduli na kushinda kwa kishindo.

8. Mh. SOKOINE Aukwaa Uwaziri Kamili

Mwaka 1970, baada ya Uchaguzi Mkuu, Rais NYERERE alimteua Mh. SOKOINE kuwa Waziri wa Nchi. Aidha, mwaka 1972, baada ya kuvutiwa na uchapakazi wake usio wa kawaida, Rais NYERERE alimteua SOKOINE kuwa Waziri katika Wizara nyeti ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.

9. Mh. SOKOINE Awa Mjumbe wa CC

Baada ya TANU na  ASP kuungana tarehe 5.2.1977 huko Zanzibar, Mh. SOKOINE akawa Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM (CC).

10. Mh. SOKOINE Ateuliwa Waziri Mkuu

Kutokana na uchapakazi wake mujarab usio na mawaa yoyote, tarehe 13.2.1977, Rais NYERERE, baada ya kulifumua Baraza la Mawaziri, akamteua Mh. SOKOINE kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa TZ.

11. Mh. SOKOINE Ajiuzulu Uwaziri Mkuu 1980

Tarehe 7.11.1980, Mh. SOKOINE alijiuzulu Uwaziri Mkuu na kwenda masomoni Yugoslavia. Rais NYERERE akamteua Mh. CLEOPA  DAVID MSUYA kuwa Waziri Mkuu.

12. Mh. SOKOINE Arejea 1983, Ateuliwa Waziri Mkuu

Mh. SOKOINE alirejea nchini mwaka 1983. Kutokana na imani kubwa aliyokuwa Rais NYERERE kwa Mh  SOKOINE, mara moja akamteua tena kushika wadhiwa wake wa Waziri Mkuu, tarehe 24.2.1983.

13. Mh. SOKOINE Atinga Bungeni Machi 1984

Mh. SOKOINE aliwasili bungeni Dodoma mwezi Machi 1984 na kama Kiongozi wa Serikali bungeni, aliliongoza Bunge kwa umahiri na weledi wa hali ya juu.

14. Mh. SOKOINE Ajumuika na Wabunge

Jumatatu ya tarehe 9.4.1984, Mh. SOKOINE alijumuika na wabunge waliokwenda kusali asubuhi kanisa la Mt. Paul.

Usiku wa Jumanne, tarehe 10.4.1984, Mh. SOKOINE aliandaa karamu kabambe "Cocktail party" na kuwaalika Mawaziri na Wakuu wa Mikoa. Katika dhifa hiyo, Mh. SOKOINE alizunguka na kuongea na kila mmoja wao.

Kesho yake jioni, siku ya Jumatano, tarehe 11.4.1984, Mh. SOKOINE, aliyekuwa mtu mwema na mwenye utu, aliandaa karamu kwaajili ya wabunge wa mkoa wa Arusha ambapo aliwasisitizia kuhakikisha wanafanya kila wawezalo ili kuwasaidia Wamasai kuondokana na ufukara mkubwa walionao.

15. Mh. SOKOINE Alivunja Bunge

Siku ya Jumatano, tarehe 11.4.1984, Mh. SOKOINE alilivunja bunge na kuliaga ambapo alitiririka:

"Ndugu Spika, ningependa kumalizia kwa kukubaliana na wabunge kuwa lazma tutafute njia ya kuikomesha tabia hii ya kutumia fedha bila ya idhini ya Bunge........ Mungu akipenda tutakutana katika kikao kijacho. Mimi nitasafiri kwa njia ya barabara ili nijionee hali ya mazao ya wakulima wetu.....".

16. Mh. SOKOINE Apata Ajali, Afariki

Alhamis, tarehe 12.4.1984, Mh. SOKOINE aliondoka Dodoma na msafara wake akiwa ndani ya Mercedes Benz yake huku msafara huo ukiongozwa na gari la polisi. Magari yote yaliyokuwa yakikutana na msafara huo, yalikuwa yakipaki pembeni kuupisha, baada ya kuamriwa na gari la mbele la polisi. 

Baada ya msafara huo kufika Dakawa, kilometa 30 toka Morogoro, ghafla kilisikika kishindo kikubwa sana!. Mercedes Benz ya Mh. SOKOINE iligongana uso kwa uso na gari aina ya Toyota Landcruiser lililokuwa likiendeshwa na DUMISAN DUBE(23), mpigania uhuru wa ANC aliyekuwa akiishi Mazimbu, Morogoro. DUBE, aliyekuwa kwenye mwendo kasi kama MICHAEL SCHUMACHER, hakuweza kusimama aliposimamishwa na polisi. DUBE alikuwa na abiria wawili ambao ni BOYCE MOYE na GEORGE PERCY.

Mh. SOKOINE, aliyekuwa amekaa kiti cha nyuma huku akiwa hajafunga mkanda, alirushwa na kugonga kioo cha mbele ambapo aliumia sana shingoni na kifuani na kufariki akiwa njiani kupelekwa hospitali ya serikali Morogoro ambako alipofikishwa madaktari walieleza kuwa amekwishafariki!.

Bw. YUSTO CHUMA, aliyekuwa mlinzi wake ambaye alikaa kiti cha mbele kushoto, aliumia vibaya na Bw. ALLY ABDALLAH, aliyekuwa dreva wake, alivunjika mguu.

17. Rais NYERERE Alitangazia Taifa Kifo

Alasiri ya siku hiyo ya Alhamis, Radio Tanzania Dsm ilisitisha ghafla vipindi vyake na kupiga wimbo wa Taifa. Rais NYERERE, mara tu baada ya wimbo wa Taifa, kwa uchungu mkubwa lakini kwa ujasiri wa hali ya juu, akalitangazia Taifa kuhusu kifo hicho cha kipekee, ambapo alisema-:

"Ndugu wananchi, leo mnamo saa saba mchana, ndugu yetu na kijana wetu, Edward Sokoine, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, alipokuwa akirudi Dar Es Salaam kutoka Dodoma, gari lake lilipata ajali na amefariki dunia. Naomba muamini Edward amefariki kwa ajali na si kitu kingine".

18. Nchi Nzima Yakumbwa na Vilio, Simanzi

Baada tu ya taarifa hiyo,  nchi nzima, toka Kalumbulo Kyela hadi Kahororo Kagera, vilio vilitamalaki na wananchi walikumbwa na simanzi kubwa kwa kuondokewa  na kipenzi chao na kupelekea kazi na shughuli zote kusimama. Kikao cha UWT kilichokuwa kikifanyika ofisi ya CCM Lumumba kilisambaratika mara tu baada ya Mwenyekiti wa UWT, Mh. Mama SOPHIA KAWAWA alipowatangazia wajumbe habari hizo za kusikitisha zilizoleta jakamoyo na jitimai kubwa!.

 Aidha, watanzania waliokuwa nje ya nchi nao walimlilia sana SOKOINE.

19. Serikali Yatangaza Maombolezo

Kufuatia kifo hicho cha Jemedali SOKOINE, serikali ilitangaza maombolezo ya wiki mbili na bendera kupeperushwa nusu mlingoti nchi nzima.

20. Mwili wa SOKOINE wafikishwa Ikulu

Mwili wa marehemu SOKOINE ulifikishwa Ikulu, saa 11 jioni ya siku hiyo hiyo ukiwa umefunikwa kwa bendera ya Taifa.

21. Rais NYERERE Ashindwa Kuvumilia, Aangua Kilio:

Mwili wa marehemu SOKOINE uliwekwa sehemu maalum Ikulu. Rais NYERERE, akiambatana na mama MARIA, alijongea kwenye mwili huo na kuifunua bendera ya Taifa. Kisha akaweka mikono yake miwili kwenye paji la uso wa SOKOINE. 

Rais NYERERE na mama MARIA, aliyekuwa ameshika kitambaa cheupe, walishindwa kuvumilia na wakalia kwa uchungu mno hadi walinzi wao walipowaondoa. Rais NYERERE alikuwa na huzuni kubwa na ilikuwa ni mara ya kwanza kwa watu kumuona akilia hadharani!.

Kwa hakika ilikuwa ni huzuni kubwa kwavile marehemu SOKOINE ndiye aliyekuwa akitarajiwa kwa 99% kuwa ndiye angekujakuwa Rais wa TZ mwaka 1985.

22. Mh. JOSEPH NYERERE Azua Timbwili na Kimuhemuhe Ikulu

Mh. JOSEPH NYERERE, mdogo wa Rais NYERERE, ambaye alijulikana kwa kutomung'unya maneno, ghafla bin vuu, alitinga ulipo mwili wa SOKOINE huku akilia kwa uchungu. Akiwa na uchungu na hasira kwa pamoja, Mh. JOSEPH akazomoka maneno mengi mf-:
"Mwalimu, huna ulinzi. Waziri Mkuu anakufa barabarani?!!.

Kufuatia kimuhemuhe na taharuki hiyo, walinzi wa Ikulu walimuondoa haraka maeneo ya Ikulu.

Jioni hiyo ya Alhamis, mwili wa SOKOINE ukapelekwa hospitali ya Lugalo kuhifadhiwa.

23. Jeneza Latengenezwa Usiku wa Manaani!

Bw. GEORGE CHRISTOS alipewa jukumu la kutengeneza jeneza la marehemu SOKOINE. Baba yake bwana huyu alikuwa Mgiriki na mama yake alikuwa Msukuma aliyeitwa MARIA, mmoja wa mabinti wa Chifu KIDAHA.

Bw. CHRISTOS ndiye aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Bohari Kuu, TZ.

Bw. CHRISTOS na mkewe, Bi. ELIZABETH WALKER, walitinga hospitalini na kuchukua vipimo vya marehemu SOKOINE aliyekuwa mtu wa miraba minne.

Bw. CHRISTOS, Bi. WALKER na Mh. PAUL MKANGA, aliyekuwa Katibu Mkuu, Ujenzi walienda kwenye kiwanda cha Hem-Singh, Chang'ombe ambapo walimkuta mwenyewe akiwa katika harakati za kufunga. Kutokana na unyeti wake, ikabidi aendelee na kazi na akamaliza kulitengeneza jeneza hilo usiku wa maanani na Bi WALKER akalipamba kwa umahiri mkubwa kisha likapelekwa hospitalini. 

24. Marehemu SOKOINE Aagwa Dsm

Ijumaa, tarehe 13.4.1984, wakazi wa jiji la Dsm, ZNZ na mikoa ya jirani walifurika kumuaga kipenzi chao. Kwa hakika, ulikuwa ni umati mkubwa ambao ulikuwa haujawahi kuonekana toka tupate uhuru. Rekodi ya umati huo ilikuja kuvunjwa na umati uliojitokeza kumuguaga Baba wa Taifa, Octoba 1999. 

25. DALADALA Zawapeleka Watu Bure "Airport'!

Jumamosi, tarehe 14.4.1984, ilikuwa ni siku ya wananchi kuelekea "Airport" kuusindikiza mwili wa SOKOINE kuelekea Arusha.

Daladala zote Dsm ziliwachukua wananchi na kuwapeleka bure "Airport" , ukiwa ni mchango wao kuntu kwa kipenzi chao, marehemu SOKOINE.

Mh. SOKOINE, mwaka 1983, baada ya kuona UDA "inambwelambwela", ndipo alipoanzisha utaratibu wa "DALADALA". Jina hilo lilitokana na neno "Dollar" ambapo "Exchange  rate" kwa wakati huo ilikuwa ni shilingi TANO ambayo ndio ilikuwa nauli ya Daladala.

Mwili wa SOKOINE, hatimaye, ukafika salama Arusha.

26. Mh. SOKOINE Apumzishwa Nyumba yake ya Milele

Jenerali JOHN BUTLER WARDEN "Black Mamba", Mtanzania chotara, akisaidiwa na Vijana wa TPDF alijenga kaburi la aina yake. Hii ilipelekea Jenerali WARDEN aje kupewa kandarasi ya kujenga kaburi la marehemu Rais SAMORA MOSES MACHEL wa Nchumbiji aliyefariki baada ya ndege yake aina ya Tupulov Tu 134, kuanguka tarehe 19.10.1986.

Mazishi ya marehemu SOKOINE, huko Monduli, yalipewa heshima zote za kitaifa na yalihudhuriwa na maelfu ya watu wakiongozwa na Rais NYERERE na yalihudhuriwa pia na viongozi toka nje ya nchi.

Miongoni mwao ni Mh OLIVER TAMBO aliyekuwa Rais wa ANC na Mh. ALFRED NZO aliyekuwa Katibu Mkuu, ambao walieleza masikitiko yao kwa kifo hicho kusababishwa na raia mwenzao wa Afrika Kusini, DUMISAN DUBE.

27. Mh. SOKOINE Aacha Wake 2, Watoto 11

Mh. SOKOINE alipofariki aliacha wake wawili (NAPONO na NAKITETO) na watoto 11, wakiwemo wawili ambao walikuwa kuwa viongozi ie Balozi JOSEPH na mbunge NAMELOK.

28. DUBE Afikishwa kwa "PILATO", "Apigwa Mvua 3!"

Tarehe 12.6.1984, DUMISAN DUBE alifikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi, Morogoro, mbele ya Mh. Mh. SIMON KAJI (PRM). Upande  wa Mashtaka uliongozwa na JOHNSON MWANYIKA (SSA) ambaye alikuwa na mashahidi 21, aliwemo mkulima aliyeshuhudia ajali hiyo.

DUBE aliposomewa mashtaka 7, alikiri hivyo Mh. KAJI akampa kifungo cha miaka 3.

29. Mambo yaliyofanya Mh. SOKOINE Kuwa Kipenzi cha Rais NYERERE na Watanzania:

29.1 Mh. SOKOINE alichukia Rushwa, hakupenda Utajiri

Msibani Monduli, Rais NYERERE alieleza- "Marehemu Edward alichukia na kupambana na rushwa kwa dhati kabisa. Hakuwa na mali yoyote ukiachilia ng'ombe wa urithi. Alikuwa na suti 3 na viatu pea 2 tu".

29.2 SOKOINE Alipenda Usawa

Mh. SOKOINE alieleza, tarehe 1.2.1977- "Katika nchi inayojali haki na usawa, majeshi lazma yawe kwa faida ya wote".

29.3 SOKOINE Alisisitiza Maendeleo

Mh. SOKOINE alieleza, tarehe 11.12.1982:- "Naskia huko mikoani baadhi ya viongozi wanagombea nyumba na magari. Hayo sio mambo muhimu. Viongozi wanapaswa kugombania maendeleo ya wananchi wetu. Huu ni ugomvi mtakatifu".

29.4  Mh. SOKOINE Alikuwa Mbunifu

Mh. SOKOINE alianzisha Mfuko Maalum "The Presidential Trust Fund" Ikulu, ambapo kila mwezi alikuwa akiweka sehemu ya mshahara wake ili kuwasaidia akina mama kukopa!. Wakinamama wengi wamenufaika kwa mfuko huu.

29.5 Mh. SOKOINE Alikuwa Mchamungu

Mh. SOKOINE alikuwa mchamungu sana. Alikuwa Mkristu Mkatoliki na Mwanachama wa  Utawa wa Tatu wa Mt. Francisca.

29.6 Mh. SOKOINE alikuwa Mchapakazi Hodari

Mh. SOKOINE alifanya kazi hadi mara nyingine usiku wa maanani. Aliwachagua vijana 2 hodari MARTENS LUMBANGA na PHILLEMON LUHANJO waliokuwa chini ya Katibu Mkuu,  HORRACE KOLIMBA. Hawa watatu walibatizwa jina "Wafuasi wa SOKOINE" kwani nao walikuwa waadilifu na wachapakazi makini na waliongozana nae kila alikokwenda.

29.7 SOKOINE alichukia sana Viongozi Wazembe

Mh. SOKOINE hakuwa na simile na Viongozi wazembe, kama alivyoeleza tarehe 26.3.1983- "Ole wake Kiongozi mzembe nitakayemkuta. Viongozi wazembe na wabadhilifu wahesabu siku zao".

29.8 SOKOINE alichukia Upuuzi

Mwezi Machi 1983, Mh. SOKOINE alifanya ziara mkoani Singida. Mmoja wa viongozi mkoani humo akamfuata Bw. ACCADOGA CHILEDI aliyekuwa "Press Secretary" wa SOKOINE  na kumwambia- "Mzee tumeishamtayarishia blanketi chapa ya mtu, atafurahi sana kwani huku Singida ni wazuri mno". Bw. CHILEDI akamjibu- "Hivi we mheshimiwa, je, SOKOINE unaumjua au unamsikiaga tu? Ebu ondoka na huo upuuzi wako maana nikimwambia Mh. SOKOINE, ujue utapoteza kazi yako hapahapa!".

Mbio alizotimua Kiongozi huyo baada ya kuelezwa hivyo na Bw. CHILEDI, hata kishada USAIN BOLT angesubiri!.

30. Dr. JPM alimkubali Sana SOKOINE

Dr. JPM, tarehe 12.4.2018, alieleza kinagaubaga kuwa alimpenda sana SOKOINE-

"Tarehe 12.4.1984, Mh. Edward Sokoine alipofariki kwa ajali ilikuwa huzuni kubwa sana nchini. Mimi nilikuwa JKT Mpwapwa "OPERESHENI YA NGUVUKAZI". Mimi nilimpenda sana marehemu Sokoine kwani alipiga vita rushwa, wizi na unyonyaji. Marehemu Sokoine alikuwa Mzalendo kwelikweli na kamwe hatasahaulika Tanzania. Ni wito wangu tumuige marehemu Sokoine".

31. MWISHO:

Marehemu EDWARD MORINGE SOKOINE alikuwa ni Zawadi ya Mungu kwa Watanzania.

32. TAFAKURI JADIDI:

Je, wewe Kiongozi au Mwananchi wa kawaida, unamuishi vipi marehemu SOKOINE kama Rais wetu Dr. JPM alivyotuasa?.

Imeandikwa na MZEE WA ATIKALI 

Aprili 12, 2020

KENYA's CMG ARGWINGS KHODEK-: A DOYEN OF LEGAL PROFESSION & EAST AFRICA'S FIRST BLACK LAWYER

$
0
0

By MZEE WA ATIKALI  ✍️✍️✍️


1. Introduction

The late CLEMENT MICHAEL GEORGE ARGWINGS  KHODEK , popularly known as "CMG", made history in 1949 when he became the First Black Lawyer in East Africa. CMG, who died in a mysterious road accident on 29.1.1969, was a Kenyan citizen.

2. Birth Date & Place

CMG was born in 1923 in Nyanza, Kenya.

3. Education

CMG was sent to a local mission school and later to St Mary's school, Yala and St. Mary's College, Uganda where he sat his Cambridge School Certificate in 1936.

In 1937, CMG enrolled at the prestigious Makerere University College where he was awarded a  teaching diploma in 1940.

CMG would then spend some years teaching in then Nyanza & Rift Valley Provinces, Kenya.

4. CMG Pursues a Law Degree

In 1947, CMG was awarded a Govt scholarship to study social sciences at Cardiff university, Wales.

By then, the colonial Government was not allowing Africans to study Law-opting to give scholarships for other degrees especially education degrees.

Thus, when CMG applied  to the Colonial Government to be allowed to study Law,  the request was turned down pronto!.

But upon arrival in Wales, a determined CMG enrolled for a Law degree alongside his sanctioned Bachelor of Arts and obtained the former in 1949 and another in Social Sciences.

CMG was interested in the Western education as his motto was - "Learn the education of the whiteman, know his tricks and wisdom, then use his tools to chase him away from your land".

5. CMG Marries an Irish Woman

While in Wales, CMG married Ms MAVIN TATE, an Irish woman.

6. CMG Becomes a Member of the Bar

CMG became a member of the Bar at Lincoln's Inn, London-one of the four prestigious professional bodies in England & Wales.

7. CMG Returns Home

CMG could have stayed in London as a well paid lawyer but he surprised his colleagues when he, in 1952, sailed back to Kenya.

8. Weird Segregation Laws in Kenya

CMG & his wife met a quagmire over their living conditions.

In colonial Kenya, a black man having sexual relationship with a white woman would be punished by death and a whiteman having sexual relations with a black woman was not punished.

Furthermore, Nairobi was segregated; Westlands was designated-White only and Eastlands was black-only. This proved to be a problem for the couple as they were not allowed onto each other's  race's areas.

Moreover, CMG couldn't legally kiss, walk hand-in- hand in public with his Irish wife. so, in a test case on Segregation laws, he went to court and won.

9. CMG Seeks Employment at AG's Chambers

Upon his arrival, CMG sought employment at the AGC but was given a salary which was a third of what Europeans in the same grade were getting.

10. CMG Becomes the Only Kenyan With a Law Firm

CMG protested but his pleas fell on deaf ears. So, he left to start his own law firm at Church House and he was the only African in Kenya with a law firm.

11. CMG Becomes the Sole Criminal Lawyer

By September 1952, the courts had jailed more than 500 Mau-Mau supporters.

Singlehandedly, CMG took on the formidable challenge of defending these fellow Kenyans and did it with gusto. He successfully appealed on a legal technicality.The west media hated him and dubbed him "The Mau-Mau Lawyer".

12. CMG's Irish Wife Dies

CMG's Irish wife, Ms MAVIN TATA, died. Their marriage had been blessed with two issues namely Ms CAROLE & SHIRLEY.

13. CMG Becomes a Member of LEGCO

CMG became active in politics and became a member of LEGCO representing what is now Nairobi  Eastlands constituency.

14. CMB Meets Ms JOAN

Ms JOAN OMONDI narrates how the two met:
"One day I visited my cousin Mrs YUNEAH OUKO in Kisumu. Coincidentally, CMG was also visiting Dr. WILLIAM OUKO, with whom he had studied in the UK. Though I was in another room with YUNEAH, I could hear them discussing about me. One thing led to another. CMG,then, helped me to go to study in the UK".

15. CMG Proposes to JOAN

In 1961, CMG, who was attending the Lancaster Conference that was discussing Keny's imminent independence, proposed to Ms JOAN, in London, who consented.

16. CMG Marries Ms JOAN

CMG married Ms JOAN,  first traditionally in 1962 and later at a glamorous wedding in Nairobi.

17. CMG Becomes an MP

In 1963, CMG became an MP for Gem constituency in independent Kenya.

18. CMB Appointed Assistant Minister

When Kenya became independent  on 12.12.1963, H.E President JOMO KENYATTA appointed CMG Assistant Minister for Defence.

19. CMG Becomes a Cabinet Minister

In 1966, H.E President KENYATTA appointed CMG as Minister for Natural Resources and in 1967 as Minister for Foreign Affairs.

20. CMG Dies in a Mysterious road accident

On 29.1.1969, CMG and Ms JOAN parted earlier that day from a reception. She drove home ahead of him to attend the children. He didn't return home. At 11.30 Pm, police went to her house and informed her that CMB had been involved in an accident. She went to hospital. CMG was alive. He could speak but was in great pain. He passed on at 5.30 AM.

CMG was survived by his wife, JOAN OMONDI and their children CAROLE,  SHIRLEY, GEM, CAESAR, SHARON & EUGENE who are all graduates.

CAROLE & SHIRLEY were CMG's daughters with his Irish wife, MAVIN. They were taken in and raised by JOAN & CMG following their mother's death.

21. Conclusion

The late CLEMENT MICHAEL GEORGE ARGWINGS KHODEK made waves, in 1949, when he became the First Black Lawyer in East Africa.

For just two decades at the courtroom and in politics, CMG had no match. CMG used his education to push for independence, providing the intellectual expertise and articulation of issues against the colonial authorities. Thereafter, he served as a minister in three dockets.

CMG will always be remembered as a trailblazing lawyer and a seasoned politician who shaped independent Kenya.

By MZEE WA ATIKALI  ✍️✍️✍️


April 11, 2020
Viewing all 118616 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>