Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 117112

RAS TANGA ATAKA WAANDISHI WA HABARI KUPEWA USHIRIKIANO

$
0
0
KATIBU Tawala Mkoa Tanga Mhandisi Zena Said ameziagiza taasisi za Serikali na mashirika ya umma kutoa ushirikiano kwa waandishi wa habari pindi wanapohitaji taarifa kutoka kwenye taasisi hizo kwa ajili ya kuhabarisha umma.

Ameyazungumza hayo leo wakati wa kuadhimisha siku ya uhuru wa vyombo vya habari Duniani ambapo Mkoa Tanga maazimisho hayo yalifanyika katika ukumbi wa klabu ya waandishi wa habari na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka taasisi za serikali na zisizo za kiserikali.

Hatua hiyo imekuja mara baada ya waandishi wa habari kutoa malalamiko yao mbele ya Katibu Tawala huyo wa Mkoa ambae alikua mgeni rasmi katika maazimisho hayo ya kuwa zipo baadhi ya taasisi za Serikali kushindwa kutoa ushirikiano kwa waandishi wa habari pindi wanapohitaji kutekeleza majuku yao ya kazi.

Burhan Yakubu ambae ni mjumbe na mwaandishi wa habari alisema kumekuwepo na utaratibu usioendana na maadili ya kiuwandishi katika Hospitali kuu ya Rufaa ya Bombo kwa kutengeneza urasimu wa kupatikana kibali kutoka kwa katibu tawala Mkoa wakati mwandishi anapohitaji kupatiwa tariifa zozote kutoka katika Hospitali hiyo
Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Zena Saidi akifungua maadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari Duniani kimkoa yaliyofanyika kwenye ukumbi wa klabu ya waandishi wa habari mkoani Tanga (Tanga Press Club) leo kulia ni Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoani Tanga,Hassan Hashim kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoani Tanga,Lulu George 
Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoani Tanga,Hassan Hashim akizungumza katika maadhimisho hayo leo 
Makamu Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoani Tanga,Lulu George akizungumza katika maadhimisho hayo kushoto ni Katibu Msaidizi Alex Abraham .


Viewing all articles
Browse latest Browse all 117112

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>