Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 117024

DKT NCHIMBI: MWAJIRI NA MWAJIRIWA SI MTU NA ADUI YAKE

$
0
0
Waajiri wote Mkoani Singida hususani wakurugenzi wa halmashauri ambao ndio wenye watumishi wengi wameelekezwa kujenga mahusiano mazuri baina yao ili kuboresha utumishi wao.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi ametoa maelekezo hayo wakati wa maadhimisho ya siku ya wafanyakazi mkoani hapa yaliyofanyika katika uwanja wa Peolpe’s mjini Singida.

Dkt. Nchimbi amesema mwajiri na mtumishi sio maadui bali wanapaswa kujenga mahusiani mazuri hasa kwa mwajiri kujenga mazoea ya kufahamu sifa za watumishi wake, shida na matatizo yao.

Ameongeza kuwa waajiri wamekuwa wakisubiria watumishi wakosee ndio wawape adhabu lakini haipaswi kuwa hivyo kwani mwajiri anatakiwa ahakikishe anaweka mazingira mazuri na kumuelimisha mtumishi asifanye makosa.

“Ukiona mtumishi anafanya mambo yanayokinzana na sheria, kanuni na utaratibu, usimkaripie wala kumtega, mtafutie afisa ustawi wa jamii. Kwa vyo vyote afisa ustawi wa jamii atamrejesha kwenye mstari stahiki na mambo yatakwenda vizuri”.
 Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akimkabidhi afisa wa usalama kutoka shirika la TANESCO Mkoa wa Singida Juma Mauba zawadi ya cheti na  TV flat screen baada ya kuchaguliwa kuwa mfanyakazi bora mwaka 2017.
 Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akiwa ameshikama na Mwenyekiti wa Shirikisho la vyama vya wafanyakazi TUCTA Mkoa wa Singida Aaran Jumbe (kulia kwake) na Mkuu wa Wilaya ya Singida Elias Tarimo (kushoto kwake) wakiimba wimbo maalumu wa wafanyakazi wa Mshikamano daima pamoja na wimbo wa taifa.
 Watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi wakati akihutubia kwenye maadhimisho ya siku ya wafanyakazi kwa Mkoa wa Singida.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Viewing all articles
Browse latest Browse all 117024

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>