
Jumuiya ya waTanzania Rome- Italia
Picha kwa hisani ya Tanzania Community Rome- Italy
Na Vijimambo Blog
Natumaini wote hamjambo na mnaendelea vizuri na majukumu ya kila siku ya maisha yanayotukabili kila siku ya uhai wetu. Baada ya salamu ningependa kuanza moja kwa moja na swala ya jumuiya za waTanzania nje ya nchi tuipendayo Tanzania, kumekuwepo na migogoro mingi kwenye hizi jumuiya na mishikamano inayoleta umoja kupungua siku hadi siku mpaka inasikitisha na kutia huruma.
Jumuiya za waTanzania ughaibuni zilikua imara sana wakati zilipoanzishwa miaka ya nyuma hasa mwanzoni mwa miaka ya 80 na jumuiya zilikua imara sana wakati huo ikiwemo wanajumuiya wanachama kuwa hai kwa kuchangia michango yao ya kila mwezi hadi mwaka.
Sababu moja wapo kubwa ya jumuiya hizi kuwa hai ni idadi ndogo ya waTanzania iliyokuwepo ughaibuni iliyofanya urahisi wa mawasialino kwa kujuana na kutembelea kama ndugu waliotoka nchi moja tofauti na sasa waTanzania wamekua wengi mpaka wengine imekua vigumu kujuana.