Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 117045

KIGOMA YANUFAIKA NA TAASISI YA MKAPA

$
0
0
Mkoa wa Kigoma umenufaika na nyumba mpya 30 za watumishi wa Afya pamoja na vitendea kazi (baiskeli 200, mabegi 225, mabuti 25 na makoti ya mvua 25) kwa ajili ya wahudumu wa Afya ngazi ya jamii vikiwa na ujumla wa thamani ya Shs 1,806,985,822 billioni kutoka kwa Taasisi ya Benjamin W. Mkapa. 

Akizungumza wakati wa ukabidhiwaji wa nyumba na vitendea kazi hivyo Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Brigedia Jenerali (Mstaafu) Emmanuel Maganga, alisema ya kuwa mkoa wa Kigoma unakabiliwa na upungufu wa watumishi wa afya kwa asilimia 65 ya mahitaji kamili na moja wapo ya sababu zinazopelekea upungufu huo ni ukosefu wa mahali pazuri pa kuishi. 

Hivyo nyumba hizi zilizojengwa na Serikali kwa usimamizi wa Taasisi ya Mkapa zitasaidia kupunguza makali ya uhaba wa watumishi kwa mkoa wa Kigoma na nchi nzima kwa ujumla. 

Mkuu wa mkoa aliwasisitizia Wananchi pamoja na watumishi wa afya wanaotumia nyumba hizo kuzitunza na kuzithamini kwani zimejengwa kwa faida yao. Hivyo hivyo kwa upande wa vitendea kazi aliwasisi wahudumu wa afya ngazi ya jamii kuvitumia kwa lengo lililokusudiwa ambalo ni kuwafikia wana jamii ndani ya jamii zao na kuweza kuwapa huduma bora za afya. 

“Napenda kutoa wito kwa mashirika yanayojenga nyumba kama vile shirika la nyumba la Taifa, Mifuko ya hifadhi ya jamii, watumishi ujenzi n.k wafirikie zaidi kujenga kwenye vituo vyetu vya Afya na Zahanati ambapo Serikali inaweza kuwapangishiwa watumishi wake” alisisitiza, Mh. Maganga



Mfano wa moja kati ya nyumba mpya 30 zilizojengwa na kukabidhiwa kwa mkoa wa kigoma na Taasisi ya Mkapa.
Dkt. Ellen Mkondya-Senkoro, Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Mkapa akitoa ufafanuzi wa jiwe la ufunguzi kwa Mhe. Brigedia Jenerali (Mstaafu) Emmanuel Maganga, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma wakati wa halfa ya ukabidhishwaji wa nyumba mpya 30 za watumishi wa Afya iliyofanyika katika zahanati ya Kalinzi mkoani kigoma. 

Kikundi cha kina mama wa mkoa wa kigoma wakiimba kwa furaha mbele ya Mkuu wa Mkoa, Mhe. Brigedia Jenerali (Mstaafu) Emmanuel Maganga wakati wa hafla ya kukabidhiwa nyumba mpya 30 za watumishi wa afya zilizojengwa na Taasisi ya Mkapa mkoani Kigoma. 
Watu waliohudhiria hafla ya ukabidhiwaji wa vitendea kazi vitendea kazi (baiskeli 200, mabegi 225, mabuti 25 na makoti ya mvua 25) kwa wahudumu wa afya ngazi ya jamii 


Viewing all articles
Browse latest Browse all 117045

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>