
Wizara inakanusha taarifa hiyo ya kizushi iliyosambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii yenye lengo la kuleta chuki na kuchafua jina la Waziri pamoja na Wizara yetu kwa ujumla.
Wizara inachukua hatua za kisheria kuwatambua wale wote waliohusika na kutengeneza ukurasa huo bandia.
Tunatoa wito kwa wahusika wote kuacha mara moja kusambaza taarifa hii potofu.
IMETOLEWA NA
KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI,
WIZARA YA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
22 March, 2017