Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 117139

KANUSHO

$
0
0
Tunapenda kutaarifu Umma kuwa kuna mtu aliyefungua ukurasa katika mtandao wa kijamii wa ‘Twitter’ kwa kutumia jina la Mhe. Charles Mwijage(MB), Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji na kuweka taarifa kuwa “Kilichotokea kwa Clouds Media ni kitendo cha kinyama na wala si uungwana kabisa tunajenga nchi ya viwanda na si ya kutishana”
Wizara inakanusha taarifa hiyo ya kizushi iliyosambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii yenye lengo la kuleta chuki na kuchafua jina la Waziri pamoja na Wizara yetu kwa ujumla.
Wizara inachukua hatua za kisheria kuwatambua wale wote waliohusika na kutengeneza ukurasa huo bandia.
Tunatoa wito kwa wahusika wote kuacha mara moja kusambaza taarifa hii potofu.

IMETOLEWA NA
KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI,
WIZARA YA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
 22 March, 2017

Viewing all articles
Browse latest Browse all 117139

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>