Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 117140

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE IMEITAKA SERIKALI KUHAKIKISHA INATOA FEDHA ZA MRADI WA UJENZI WA JENGO LA ABIRIA NAMBA TATU

$
0
0
KAMATI ya Kudumu ya Bunge imeitaka serikali kuhakikisha inatoa fedha za mradi wa ujenzi wa jengo la abiria namba tatu (terminal III) kwa wakati ili mradi huo uweze kukamilika kama ilivyopangwa. 

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Profesa Norman Sigalla aliyasema hayo wakati wa kufanya majumuisho baada ya kutembelea mradi huo leo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA). 

Alisema kukamilika kwa jengo hilo kwa wakati uliopangwa utawapa heshima Watanzania lakini pia kupunguza msongamano katika jengo la sasa la Terminal II. 

“Nchi inapoenda kwa sasa ni kuzuri, lakini ili kukamilika ujenzi huu kwa wakati tunaomba serikali itoe fedha ili kufanikisha hilo, baada ya kukamilika kila ndege itatua hapa nchini na hivyo kuongeza pato la Taifa,” alisema Profesa Sigalla. 
01.Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Miundombinu Mhe.Prof Norman Sigalla akizungumza na wana kamati wakati wa ziara ya mradi wa ujenzi wa jengo la tatu la abria (terminal) katika kiwanja cha ndege cha kimataifa Julius Nyerere leo jijjini Dar es Salaam. 
02.Katibu Mkuu wa Uchukuzi Dkt Leonard Chamriho akizungumza wana kamati wakati wa ziara ya mradi wa ujenzi wa jengo la tatu la abria (terminal) katika kiwanja cha ndege cha kimataifa Julius Nyerere leo jijjini Dar es Salaam. 
Wana kamati wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Miundombinu wakimsikiliza Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Miundombinu Mhe.Prof Norman Sigalla
.Wana kamati wa kamati ya kudumu ya Bunge wakitembelea mradi wa ujenzi wa jengo la tatu la abria (terminal) katika kiwanja cha ndege cha kimataifa Julius Nyerere leo jijjini Dar es Salaam. 
Ujenzi ukiendelea wa jengo la abiria namba tatu (Terminal. ).Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 117140

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>