Na. Frank Geofray-Jeshi la Polisi.
Wakuu wa Upelelezi wa makosa ya jinai kusini mwa Afrika wametakiwa kuongeza ushirikiano katika kubadilishana taarifa za wahalifu na uhalifu unaovuka mipaka ili kuufanya ukanda wa kusini mwa Afrika kuwa salama.
Wito huo umetolewa na Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi, Abdulrahman Kaniki mjini Bagamoyo alipokuwa akifungua mkutano wa siku mbili wa Wakuu wa Upelelezi wa Polisi kutoka Shirikisho la Wakuu wa Polisi kwa nchi za kusini mwa Afrika (SARPCCO) unaofanyika sambamba na kamati za ufundi za SARPCCO kwa lengo la kupanga mikakati ya kupambana na uhalifu na wahalifu.
Kaniki alisema ili kuwabaini wahalifu kwa urahisi ni vyema ushirikiano wa kubadilishana taarifa ukafanyika kwa haraka hasa kwa kuimarisha teknolojia ya habari na mawasiliano na mafunzo kwa maafisa wa Polisi ili kuwajengea uwezo wa kubaini mapema viashiria vya uhalifu katika maeneo yao.

Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi, Abdulrahmani Kaniki akisaluti kwa wimbo wa taifa kabla ya kutoa hotuba ya ufunguzi wa mkutano wa kamati ndogo za kiufundi za shirikisho la wakuu wa Polisi wan chi za kusini mwa afrika SAPRCCO. Mkutano huo wa siku mbili unafanyika Bagamoyo mkoani Pwani kujadili mikakati ya kukabili uhalifu unaovuka mipaka. Kushoto ni Mkurugenzi wa upelelezi wa makosa ya Jinai DCI, Robert Boaz. Picha Na Hassan Mndeme-Jeshi la Polisi.

Naibu Inspekta Jenerali wa Jeshi la Polisi, Abdulrahmani Kaniki akitoa hotuba ya ufunguzi wa mkutano wa kamati ndogo za kiufundi za shirikisho la wakuu wa Polisi wan chi za kusini mwa afrika SAPRCCO. Mkutano huo wa siku mbili unafanyika Bagamoyo mkoani Pwani kujadili mikakati ya kukabiliana uhalifu unaovuka mipaka. Picha Na Hassan Mndeme-Jeshi la Polisi.

Naibu Inspekta Jenerali wa Jeshi la Polisi, Abdulrahmani Kaniki akionyesha zawadi kutoka kwa Mkuu wa Interpol kanda ya kusini (kulia) baada ya kutoa hotuba ya ufunguzi wa mkutano wa kamati ndogo za kiufundi za shirikisho la wakuu wa Polisi wan chi za kusini mwa afrika SAPRCCO. Mkutano huo wa siku mbili unafanyika Bagamoyo mkoani Pwani kujadili mikakati ya kukabiliana uhalifu unaovuka mipaka. Picha Na Hassan Mndeme-Jeshi la Polisi.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA