ANDREA NGOBOLE, PMT
Kampuni ya Tanzanite One, imetoa msaada wa Sh 20 milioni kwa chama cha Madalali wanawake,wanaouza madini ya Tanzanite mkoani Arusha .
Wakurugenzi wa kampuni hiyo, inayomilikiwa kwa pamoja na kampuni ya Sky Associate Ltd na shirika la madini la taifa(STAMICO), Faisal Shabhai na Hussein Gonga walitangaza uamuzi huo wakati wakizungumza na madalali , katika ukumbi wa polisi jijini hapa.
Faisal alisema kampuni yao ambayo inachimba Tanzanite, imetoa msaada wa sh 20 milioni,ili kuendelea kutekeleza mahusiano mema na wadau wa Tanzanite na jamii ya wanawake ambao wanajihusisha na biashara ya kuuza madini hayo.
Alisema msaada huo, umetokana na maombi ya wanawake hao, kusaidiwa waliyotoa katika mkutano wa mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo na viongozi wa Tanzanite One.
Katika hatua nyingine kampuni hiyo imetenga kiasi cha sh 200 milioni kwa ajili ya mradi wa ujenzi wa hospitali ya kisasa Mererani.![]()
Madini ya Tanzanite ambayo yanapatikana eneo la mererani pekee duniani yakiwa tayari yamekatwa na kusanifiwa sasa yatauzwa kimataifa katika kituo kitakachonjengwa Arusha![]()
Mtaalamu wa kukata madini Adam Idd Lacha akiwa anakata na kusanifu madini ya Tanzanite ya kampuni ya Tanzanite one ambayo ndio inatoa mafunzo hayo.![]()
Waziri wa nchi ofisi ya Rais (TAMISEMI) George Simbachawene akiwa anapewa maelezo juu ya madini ya Tanzanite , na wakurugenzi wa Tanzanite One, Faisal Juma na Hussein Gonga. Alipokuwa katika kituo cha kuuza madini cha kampuni hiyo.
Kampuni ya Tanzanite One, imetoa msaada wa Sh 20 milioni kwa chama cha Madalali wanawake,wanaouza madini ya Tanzanite mkoani Arusha .
Wakurugenzi wa kampuni hiyo, inayomilikiwa kwa pamoja na kampuni ya Sky Associate Ltd na shirika la madini la taifa(STAMICO), Faisal Shabhai na Hussein Gonga walitangaza uamuzi huo wakati wakizungumza na madalali , katika ukumbi wa polisi jijini hapa.
Faisal alisema kampuni yao ambayo inachimba Tanzanite, imetoa msaada wa sh 20 milioni,ili kuendelea kutekeleza mahusiano mema na wadau wa Tanzanite na jamii ya wanawake ambao wanajihusisha na biashara ya kuuza madini hayo.
Alisema msaada huo, umetokana na maombi ya wanawake hao, kusaidiwa waliyotoa katika mkutano wa mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo na viongozi wa Tanzanite One.
Katika hatua nyingine kampuni hiyo imetenga kiasi cha sh 200 milioni kwa ajili ya mradi wa ujenzi wa hospitali ya kisasa Mererani.

Madini ya Tanzanite ambayo yanapatikana eneo la mererani pekee duniani yakiwa tayari yamekatwa na kusanifiwa sasa yatauzwa kimataifa katika kituo kitakachonjengwa Arusha

Mtaalamu wa kukata madini Adam Idd Lacha akiwa anakata na kusanifu madini ya Tanzanite ya kampuni ya Tanzanite one ambayo ndio inatoa mafunzo hayo.

Waziri wa nchi ofisi ya Rais (TAMISEMI) George Simbachawene akiwa anapewa maelezo juu ya madini ya Tanzanite , na wakurugenzi wa Tanzanite One, Faisal Juma na Hussein Gonga. Alipokuwa katika kituo cha kuuza madini cha kampuni hiyo.