Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 117164

TFF YAGONGA MWAMBA TRA, OFISI ZAENDELEA KUFUNGWA

$
0
0
TFF YAGONGA MWAMBA TRA, OFISI ZAENDELEA KUFUNGWA


Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini TFF limeendelea kuwa katika sintofahamu baada ya ofisi zake kufungwa na Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA) baada ya kuwa na malimbikizo ya mda mrefu.

Maofisa hao kutoka kampuni ya YONO Auction Mart walipewa mamlaka na TRA ya kufungia ofisi hizo za TFF huku wakiwambia hawaruhusiwi kuendelea na kazi mpaka pale watakapomalizana na TRA.

Kwa mujibu wa deni hilo, TFF wanadaiwa deni la nyuma ambalo lilikuwa chini ya uongozi wa Leodigar Tenga ikiwemo kodi ya aliyekuwa kocha wa timu ya taifa Marcio Maximo na kodi ya mechi ya Taifa Stars na Brazil.

Katika sakata hilo ambapo timu ya Serengeti Boys ipo kambini ndani ya Shirikisho hilo, wameendelea kusalia lakini wamepewa masharti ya kutokutumia uwanja huo kwa mazoezi mpaka pale watakapomalizana na TRA.

Baadhi ya viongozi wa TFF walijaribu kwenda ofisi za TRA mkoa wa Ilala kujua ni jinsi gani wanalimaliza sakata hilo liligonga mwamba na kushindwa namna ya kujikwamua kwenye adha hiyo.
 Maofisa wa Yono Auction wakiwa pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa TFF wakiwapa maelezo ya kutokuendelea kuwepo ndani ya viunga vya ofisi hizo
 Ofisi za TFF zikiwa zimefungwa.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 117164

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>