Na Rhoda Ezekiel Kigoma,
MKUU wa Wilaya ya Kakonko, Kanali Hosea Ndagala ameahidi kuwachukulia hatua wasimamizi wa miradi ya ujenzi wa vyumba vya madarasa, endapo watashindwa kukamilisha miradi hiyo na kuhakikisha inakamilika kwa muda muafaka kutokana na changamoto iliyopo ya upungufu wa vyumba vya madarasa kutatuliwa.
Maagizo hayo aliyatoa jana wakati akikagua ujenzi wa madarasa manne na ofisi mbili katika Shule ya Msingi Kakonko Wilayani humo, ambapo alibaini kuwepo kwa tatizo la ucheleweshwaji wa vifaa vya ujenzi kwa mafundi hali inayo pelekea kusua sua kwa ujenzi huo.
Mkuu huyo alisema mradi huo ulitakiwa kuwa umekabidhiwa, lakini mpaka sasa bado haujakamilika kutokana na uzembe wa baadhi ya wasimamizi Wa mradi huo kushindwa kuwasimamia mafundi ipasavyo waweze kukamilisha ujenzi huo, na ifikapo mwezi wa tatu Mwishoni ujenzi huo uwe umekamilika na wanafunzi wapate madarasa yao waendelee kuyatumia.
" niwatake Wahandisi wa halmashauri kwa kushirikiana na Watendaji wa kijiji kuwasimamia mafundi kwa karibu ilikuhakikisha mradi huu unakamilika kwa wakati endapo mtashindwa kusimamia ipasavyo tutawajibishana, Wananchi wamejitahidi kuchangia na Serikali imetoa fedha kwa wakati ni lazima muhakikishe mnakamilisha suala hili ilikuwatia moyo wananchi kuendelea kuchangia jitihada za Serikali",alisema Kanali Ndagala.
Maagizo hayo aliyatoa jana wakati akikagua ujenzi wa madarasa manne na ofisi mbili katika Shule ya Msingi Kakonko Wilayani humo, ambapo alibaini kuwepo kwa tatizo la ucheleweshwaji wa vifaa vya ujenzi kwa mafundi hali inayo pelekea kusua sua kwa ujenzi huo.
Mkuu huyo alisema mradi huo ulitakiwa kuwa umekabidhiwa, lakini mpaka sasa bado haujakamilika kutokana na uzembe wa baadhi ya wasimamizi Wa mradi huo kushindwa kuwasimamia mafundi ipasavyo waweze kukamilisha ujenzi huo, na ifikapo mwezi wa tatu Mwishoni ujenzi huo uwe umekamilika na wanafunzi wapate madarasa yao waendelee kuyatumia.
" niwatake Wahandisi wa halmashauri kwa kushirikiana na Watendaji wa kijiji kuwasimamia mafundi kwa karibu ilikuhakikisha mradi huu unakamilika kwa wakati endapo mtashindwa kusimamia ipasavyo tutawajibishana, Wananchi wamejitahidi kuchangia na Serikali imetoa fedha kwa wakati ni lazima muhakikishe mnakamilisha suala hili ilikuwatia moyo wananchi kuendelea kuchangia jitihada za Serikali",alisema Kanali Ndagala.
Sehemu ya Madarasa hayo ambayo bado hayajakamilika
MKUU wa Wilaya ya Kakonko, Kanali Hosea Ndagala akizungumza na baadhi ya Wanafunzi wa shule ya msingi Kakonko,alipofana ziara ya kukagua madarasa manne na ofisi mbili zilizoko katika ujenzi katika shule hiyo.
MKUU wa Wilaya ya Kakonko, Kanali Hosea Ndagala akikagua ujenzi wa madarasa manne na ofisi mbili katika Shule ya Msingi Kakonko Wilayani humo, ambapo alibaini kuwepo kwa tatizo la ucheleweshwaji wa vifaa vya ujenzi kwa mafundi hali iliyo pelekea kusua sua kukamilika kwa ujenzi huo.