Wizara ya Nishati na Madini kupitia Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) imeendesha mafunzo kuhusu mfumo mpya wa uhifadhi data na utoaji taarifa kwa ajili ya nishati jadidifu ujulikanao kama Tanzania Renewable Energy Information Management System (TREIMS) kwa wadau wa nishati jadidifu wenye lengo la kutangaza fursa za uwekezaji katika nishati jadidifu nchini, mjini Njombe

Msimamizi wa Mradi wa Kuwajengea Uwezo Wataalam wa Nishati na Tasnia ya Uziduaji (CADESE), Paul Kiwele akisoma hotuba ya ufunguzi kwa ajili ya mafunzo kuhusu TREIMS kwa wadau wa nishati jadidifu kwa niaba ya Kamishna Msaidizi- Nishati Jadidifu kutoka Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi, Styden Rwebangila

Sehemu ya wadau wa nishati jadidifu wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zinawasilishwa katika mafunzo hayo.

Msimamizi wa Mradi wa Kuwajengea Uwezo Wataalam wa Nishati na Tasnia ya Uziduaji (CADESE), Paul Kiwele (kushoto) akielimisha moja ya wadau katika mafunzo hayo