Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye (wa pili kushoto) akiwa pamoja na uongozi wa kituo cha redio 93.7 Efm wakati alipotembelea kituo hicho asubuhi hii ikiwa ni sehemu ya ziara yake aliyoianza ya kutembelea vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini. kushoto kwake ni Mmiliki wa kituo cha Radio ya EFM, Francis Ciza (Dj Majay) na kulia ni Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Redio EFM, Dennis Ssebo.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye akizungumza jambo wakati akifanyiwa mahojiano katika moja ya vipindi vya redio hiyo.