Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 117380

Amri mpya ya Trump yapokelewa kwa mashaka

$
0
0
Rais wa Marekani Donald Trump amesaini amri mpya inayozuia watu kutoka mataifa 6 yenye Waislamu wengi kuingia nchini Marekani, ikiwa ni marekebisho ya amri ya kwanza ambayo ilikwamishwa na maamuzi ya mahakama.

Amri hiyo mpya ya Rais iliyosainiwa na Donald Trump ambayo itaanza kutekelezwa tarehe 16 mwezi huu wa Machi, inashikilia marufuku ya siku 90 kwa wasafiri wanaotoka katika mataifa sita yenye waislamu wengi kuingia nchini Marekani. Nchi hizo ni Iran, Libya, Syria, Somalia, Sudan na Yemen. Inawahusu wale tu watakaotaka kupata visa kwa wakati huu, ikiwa na maana kuwa haiwaathiri watu 60,000 ambao tayari wamezipata visa, kama ilivyokuwa kwa amri ya awali.

Iraq ambayo ilikuwa kwenye orodha ya amri ya mwanzo imeondolewa, na kwa mujibu wa waziri wa mambo ya nchi za nje wa Marekani Rex Tillerson, hatua hiyo imetokana na ushirikiano uliopo baina ya nchi hizo mbili.

''Iraq ni mshirika muhimu katika vita dhidi ya kundi la IS. Mikakati ya uhakiki iliyofanywa mnamo mwezi mmoja uliopita, imeonyesha hatua mbali mbali za kiusalama, ambazo zitaziwezesha serikali ya Iraq na wizara ya mambo ya nje ya Marekani, kutimiza lengo la pamoja, la kuzuia watu wenye malengo ya kigaidi kufika nchini Marekani''. Amesema Tillerson.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 117380

Trending Articles