Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 117404

NEWZ ALERT:MABASI YA ABOOD NA HAPPY NATION YAPATA AJALI NA KUJERUHI 12 MLIMA KITONGA YALIKUWA YAKITOKEA MBEYA KUELEKEA DAR

$
0
0


Globu ya Jamii inatoa taarifa kwa Wenye ndugu waliosafiri kwenye Basi la Abood na Happy Nation kutoka Mbeya kwenda jijini Dar es salaam,yamepata ajali mlima Kitonga hivi punde,ambapo taarifa kutoka kwa mashuhuda waliokuwa eneo la tukio wameeleza kuwa katika ajali hiyo wamejeruhiwa abiria 12.

Mmoja wa Mashuhuda wa tukio hilo alieleza kuwa ajali hiyo imetokea baada ya basi la Abood kukosa breki na kuligonga roli la FM ambalo halikuanguka ila liligonga Fuso iliyokuwa imebeba ndizi na kutumbukia korongoni baadae likaigongana na basi la Happy Nation na mabasi yote kutumbukia korongoni .
 
Taarifa rasmi kutoka kwa Mkuu wa Kikosi cha Zimamoto Mkoa wa Iringa Kamanda Kenedy Komba akiwa eneo la tukio ametihibitisha kutokea kwa ajali hiyo huku akielezea kuwa  taarifa za awali majeruhi ni 12 na kati ya hao majeruhi watatu wamekimbizwa hospitali ya Rufaa mkoa wa Iringa kwa matibabu zaidi, hakuna vifo vilivyotokea katika ajali hiyo.
 
Moja ya Lori lililogongwa na kumbukia korongoni

Viewing all articles
Browse latest Browse all 117404

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>