Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 118921 articles
Browse latest View live

BRELA YAGAWA VIFAA VYA MICHEZO TIMU YA TAIFA QUEENS

$
0
0



Na.Khadija Seif,Michuziblog

TAASISI na Makampuni yameaswa kusaidia wanamichezo ili waweze kufanya vizuri mashindano ya kimataifa na kuliwakilisha vyema taifa la Tanzania kidunia.

Hayo yamesemwa Leo Novemba 21,2023 na Kaimu Afisa Mtendaji mkuu Taasisi ya Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Loy Mhando wakati akikabidhi vifa ya kimichezo timu ya Taifa ya mpira wa netiboll ( TAIFA QUEENS) ,amesema brela ni mdau mkubwa wa michezo na inatambua mchango mkubwa kupitia kwenye tasnia ya michezo kwani ni sehemu ya biashara na ajira kwa vijana wengi.

Aidha mhando ameeleza kuwa Taasisi hiyo imekua ikishirikiana kwa karibu na michezo mbalimbali ikiwemo michezo inayoandaliwa na Shirikisho la michezo ya wizara na idara za Serikali na mikoa (SHIMIWI).

Mhando amekabidhi vifaa vya michezo ikiwemo trucksuits jozi 25 pamoja na mipira mitano ya netiboli yenye thamani ya shilingi milioni tatu za kitanzania kama sehemu ya kuwapa moyo wa kufanya vizuri wachezaji wa timu ya taifa ya netiboli ( TAIFA QUEENS).

"Ufadhili huu unatokana na maombi ya Chama cha mpira wa netiboli (CHANETA) kuomba sehemu ya ufadhili wa vifaa vya kimichezo kwa timu ya taifa queens ili waweze kujiandaa na mashindano mbalimbali ya kitaifa hivi karibu."

Pia amewaomba makampuni na taasisi zingine kutoa mchango wao katika michezo kwani bado timu nyingi zina uhitaji wa hali na mali kuhakikisha timu zao zinakuwa imara na zinailetea sifa taifa kwa ujumla.

Kwa upande wake Katibu mkuu wa Chama cha Netiboli nchini (CHANETA) Rose Mkisi ametoa pongezi kwa taasisi ya brela kwa kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Rais Dkt.Samia Suluhu kuhamasisha na kutoa misaada mbalimbali kwa timu za michezo hapa nchini.


"Vifaa hivi vilivotolewa vitaenda kuamsha ari,hamasa zaidi na morali kwa wachezaji wetu kuhakikisha wanafanya vizuri katika mchezo wa mpira wa netiboli kimataifa."

Mkisi amefafanua zaidi kuwa vifaa hivyo vinaenda kuongeza chachu ya kufanya vizuri kuelekea michuano mbalimbali.

 

Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Loy Mhando Leo Novemba 21,2023 Jijini Dar es Salaam akikabidhi trucksuits pamoja na mpira kwa Katibu Mkuu wa Chama cha mpira wa netiboli (CHANETA) Rose Mkisi kama sehemu ya kuwasilisha ugawaji wa vifaa vya kimichezo kwa timu ya taifa ya mchezo wa netiboli (TAIFA QUEENS)
A

fisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya  Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Loy Mhando katikati,kushoto kwake Katibu Mtendaji mkuu Chama cha mpira wa Netiboli (CHANETA) Rose Mkisi huku kulia kwake Katibu kamati ya michezo Taasisi ya  Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Robert Mashika mara baada ya kukabidhi vifaa vya michezo Jozi 25 pamoja na mipira miatano kwa Chama cha mpira wa netiboli (CHANETA) Jijini Dar es Salaam


PROF. BISANDA: SERIKALI YATOA UFADHILI WA MASOMO YA SAYANSI KWA WASICHANA

$
0
0
Kuendeleza wasichana kielimu katika fani za sayansi ni jambo muhimu ambalo litaongeza ushiriki wa wanawake katika maendeleo ya viwanda nchini Tanzania.

Prof. Elifas Bisanda, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, ametanabaisha hayo katika kikao cha kamati cha masuala ya jinsia ya Chuo iliyoketi Novemba 13, 2023 makao makuu ya chuo Kinondoni jijini Dar es Salaam.

“Tunaipongeza sana serikali yetu chini ya uongozi mahiri wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kutoa ufadhili wa masomo ya Sayansi kwa wasichana wapatao elfu moja (1000). Tayari wasichana 141 waliopatikana awamu ya kwanza wameshaanza masomo kupitia ufadhili huo. Ni mafanikio makubwa nchini kwani tunakwenda kuongeza ushiriki wa wanawake katika maendeleo kupitia sayansi, hesabu, uhandisi, kilimo na teknolojia. Hivyo, tunawahimiza wenye sifa stahiki kutuma maombi yao kwa ajili ya awamu ya pili ili wadahiliwe na kuanza masomo yao na kunufaika na ufadhili wa asilimia 100.” Amesema Prof. Bisanda.

Aidha, ametoa rai kwa viongozi wa wilaya, watendaji wa kata na mitaa kushiriki katika kuipasha jamii habari hizi njema ili kuibua matumaini ya wasichana walioanza kukata tamaa ya kuendelea kielimu katika maeneo yao.

Ufadhili huo unahusisha wasichana waliokatisha masomo yao kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kupata ujauzito, ukatili wa kijinsia, umasikini, kuondokewa na wazazi na walezi na sababu nyingine zozote.

Ufadhili unatolewa kwa Watanzania wote kutoka bara na visiwani ikihusisha kulipiwa ada yote, kupewa vishikwambi, kupata malazi wakati wa mafunzo ya ana kwa ana, nauli na bima ya afya.

Aidha, sifa za kitaaluma ambazo mwanafunzi husika anatakiwa kuwa nazo ni:

(a) Awe mhitimu wa kidato cha sita mwenye ufaulu wa angalau pointi 1.5 kwenye masomo mawili ya tahasusi za Sayansi, hesabu, uhandisi, kilimo na teknolojia.

(b) Mhitimu wa Stashahada katika fani za sayansi, hesabu, uhandisi, kilimo na teknolojia mwenye ufaulu wa GPA ya 2.9-2.0

(c) Mhitimu mwenye NTA level 5/Professional Technician level II Certificate

Waombaji wenye sifa tajwa wafike kwenye vituo vya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania ambavyo vipo katika mikoa yote ya Tanzania bara pia Tanzania Visiwani (Unguja na Pemba) kujaza fomu za maombi.

Pia, maombi yanaweza kufanywa kwa muombaji kupakua fomu ya maombi kupitia www.out.ac.tz na kuijaza fomu hiyo kisha kuituma kupitia barua pepe ofpheet@out.ac.tz

Mwisho wa kupokea maombi ya awamu ya pili ni tarehe Novemba 30, 2023.

KATIBU MKUU OFISI YA MAKAMU WA RAIS ATETA NA MENEJA USIMAMIZI MIRADI WA SHIRIKA LA MAZINGIRA LA UMOJA WA MATAIFA

$
0
0
Na Mwandishi Wetu,

DODOMA.

22.11.2023

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi. Mary Maganga amekutana na kufanya mazungumzo na Meneja Usimamizi wa Miradi inayofadhiliwa na Mfuko wa Mazingira wa Dunia kutoka Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP) Dkt. Daniel Pouakouyou.

Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika Mji wa Serikali, Mtumba Jijini Dodoma leo Jumatano Novemba 22, 2023 viongozi hao wamejadili utekelezaji wa Mradi wa Urejeshaji wa Uoto wa Asili na Uhifadhi wa Bioanuai (SLR) na kufanya mapitio ya vipaumbele vya miradi mipya ya mazingira inayoandaliwa na Tanzania kwa kushirikiana na UNEP.

Dkt. Pouakouyou amesema UNEP itaendelea kuwa mshirika wa Tanzania katika ufadhili wa miradi ya mazingira ukiwemo mradi wa SLR unaotekelezwa katika Mikoa 5 nchini iliyopo katika Mabonde ya Mto Ruaha na Bonde la Ziwa Rukwa ikijumuisha wilaya za Iringa, Wanging’ombe, Mbarali, Mbeya, Sumbawanga, Tanganyika na Mpibwe.

Ameongeza kuwa lengo la ziara hiyo ni kuangalia vipaumbele vya miradi mipya ya mazingira inayofadhiliwa na UNEP na kuona maeneo mahsusi yanayohitaji ushirikiano wa karibu baina ya shirika hilo na Serikali ikiwemo upatikanaji wa fedha za utekelezaji wa miradi hiyo.

Tunashukuru ushirikiano tunaendelea kuupata kutoka kwa Serikali. UNEP itaendelea kufadhili miradi mipya ya mazingira ikiwemo mradi wa uhifadhi wa maeneo ya ardhi oevu katika mfumo ikolojia ya bonde la Mto Wami-Ruvu ambalo ni moja ya vyanzo vikuu cha maji kwa Mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Morogoro na maeneo ya jirani” amesema Dkt. Poukouyou.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi. Mary Maganga amemueleza Dkt. Poukouyou dhamira na juhudi zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali katika kukabiliana na athari za uharibifu wa mazingira na mabadiliko wa mazingira ikiwemo urejeshaji wa uoto wa asili katika maeneo mbalimbali ya nchi.

“Tunaishukuru UNEP kwa kuendelea kufadhili miradi ya mazingira hapa nchini. Tumeandaa Mpango Kabambe wa Mazingira wa mwaka 2022-2032 ambapo moja ya maeneo kipaumbele ni pamoja na urejeshaji wa uoto wa asili, bioanuai na kuboresha hali ya mifumo-ikolojia na kujenga uwezo wa jamii kuwa na shughuli endelevu za uzalishaji” amesema Bi. Maganga.

Kikao hicho pia kimehudhuriwa na Wataalamu mbalimbali kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Ofisi akiwemo Mkurugenzi Msaidizi wa Mazingira Dkt. Paul Deogratius na Mratibu wa Kitaifa wa Mradi wa SLR, Dkt. Damas Mapunda na Afisa Mazingira Mwandamizi, Bw. Thomas Chali.

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi. Mary Maganga akiongoza kikao baina ya Watendaji Waandamizi wa Ofisi hiyo na Meneja Usimamizi Miradi inayofadhiliwa na Mfuko wa Mazingira wa Dunia kutoka Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP), Dkt. Daniel Pouakouyou. Kikao hicho kililenga katika kujadili utekelezaji wa Mradi wa urejeshaji wa uoto wa asili na kuhifadhi bioanuai (SLR) na vipaumbele vipya vya miradi ya mazingira nchini. Kikao hicho kimefanyika leo Jumatano Novemba 22, 2023.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi. Mary Maganga akizungumza jambo na Meneja Usimamizi wa Miradi inayofadhiliwa na Mfuko wa Mazingira wa Dunia kutoka Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP), Dkt. Daniel Pouakouyou wakati wa kikao baina yao kilichofanyika katika Mji wa Serikali, Mtumba Jijini Dodoma leo Jumatano Novemba 22, 2023. Kikao hicho kililenga katika kujadili utekelezaji wa Mradi wa urejeshaji wa uoto wa asili na kuhifadhi bioanuai (SLR) na vipaumbele vipya vya miradi ya mazingira nchini
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi. Mary Maganga akibadilishana mawazo na Meneja Usimamizi wa Miradi inayofadhiliwa na Mfuko wa Mazingira wa Dunia kutoka Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP), Dkt. Daniel Pouakouyou pamoja na Mkurugenzi Msaidizi wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Paul Deogratius muda mfupi baada ya kumalizika kwa kikao baina yao katika Ofisi za Mji wa Serikali, Mtumba Jijini Dodoma leo Jumatano Novemba 22, 2023. Kikao hicho kililenga katika kujadili utekelezaji wa Mradi wa urejeshaji wa uoto wa asili na kuhifadhi bioanuai (SLR) na vipaumbele vipya vya miradi ya mazingira nchini
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi. Mary Maganga akibadilishana mawazo na Meneja Usimamizi wa Miradi inayofadhiliwa na Mfuko wa Mazingira wa Dunia kutoka Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP), Dkt. Daniel Pouakouyou pamoja na Mkurugenzi Msaidizi wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rail Dkt. Paul Deogratius muda mfupi baada ya kumalizika kwa kikao baina yao kilichofanyika katika Ofisi za Mji wa Serikali, Mtumba Jijini Dodoma leo Jumatano Novemba 22, 2023.

Meneja Usimamizi wa Miradi inayofadhiliwa na Mfuko wa Mazingira wa Dunia kutoka Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP), Dkt. Daniel Pouakouyou akizungumza jambo na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi. Mary Maganga na Watendaji waandamizi wa Ofisi hiyo muda mfupi baada ya kumalizika kwa kikao baina yao kilichofanyika katika Mji wa Serikali, Mtumba Jijini Dodoma. Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Paul Deogratius na kushoto ni Mratibu wa Kitaifa wa Mradi wa Urejeshaji wa Uoto wa Asili na Uhifadhi wa Bioanuai (SLR) kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Damas Mapunda.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi. Mary Maganga akiwa katika picha ya pamoja na Meneja Usimamizi wa Miradi inayofadhiliwa na Mfuko wa Mazingira wa Dunia kutoka Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP), Dkt. Daniel Pouakouyou muda mfupi baada ya kumalizika kwa kikao baina yao kilichofanyika katika Mji wa Serikali, Mtumba Jijini Dodoma leo Jumatano Novemba 22, 2023. Kikao hicho kililenga katika kujadili utekelezaji wa Mradi wa urejeshaji wa uoto wa asili na kuhifadhi bioanuai (SLR) na vipaumbele vipya vya miradi ya mazingira nchini.

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi. Mary Maganga akiagana na Meneja Usimamizi wa Miradi inayofadhiliwa na Mfuko wa Mazingira wa Dunia kutoka Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP), Dkt. Daniel Pouakouyoumuda mara baada ya kumalizika kwa kikao baina yao kilichofanyika katika Ofisi za Mji wa Serikali, Mtumba Jijini Dodoma leo Jumatano Novemba 22, 2023. Kikao hicho kililenga katika kujadili utekelezaji wa Mradi wa urejeshaji wa uoto wa asili na kuhifadhi bioanuai (SLR) na vipaumbele vipya vya miradi ya mazingira nchini.

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi. Mary Maganga akiagana na Meneja Usimamizi wa Miradi inayofadhiliwa na Mfuko wa Mazingira wa Dunia kutoka Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP), Dkt. Daniel Pouakouyou muda mara baada ya kumalizika kwa kikao baina yao kilichofanyika katika Ofisi za Mji wa Serikali, Mtumba Jijini Dodoma leo Jumatano Novemba 22, 2023. Wengine pichani ni Watendaji Waandamizi wa Ofisi ya Makamu wa Rais akiwemo Mkurugenzi Msaidizi wa Mazingira Dkt. Paul Deogratius (kulia) na kushoto ni Mratibu wa Kitaifa wa Mradi wa Urejeshaji wa Uoto wa Asili na Uhifadhi wa Bioanuai (SLR) kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Damas Mapunda. Kikao hicho kililenga katika kujadili utekelezaji wa Mradi wa urejeshaji wa uoto wa asili na kuhifadhi bioanuai (SLR) na vipaumbele vipya vya miradi ya mazingira nchini.


(NA MPIGAPICHA WETU)

ROF NOMBO AWATAKA WATAFITI KUTATUA CHANGAMOTO ZA JAMII

$
0
0
Katibu Mkuu, Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo amewataka watafiti na wanavyuo nchini kutambua kuwa wanawajibu wa kutatua changamoto zilizopo kwenye jamii.

Katibu Mkuu amesema hayo wakati akifungua zoezi la utoaji wa zawadi kwa Wanachuo, Watafiti na Viongozi wa Chuo waliofanya vizuri kwenye masomo yao kupitia Ndaki mbalimbali za Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) iliyofanyika chuoni hapo.

Prof. Nombo amesema Chuo ni sawa na Kiwanda kama Hayati Mwalimu Julius Nyerere alivyesema, Chuo ni kama Kiwanda kwa sababu kinazalisha wataalamu wanaopaswa kutumia utaalamu wao kwa manufaa ya jamii na kiwanda hicho kinapaswa kuzalisha wataalamu na wahitimu watakaokuwa na manufaa kwenye jamii na kuonesha umaana wa elimu na bila kutatua changamoto hakutakuwa na umaana wa elimu mtu aliyosomea.

“Ukisoma tu kama hutatua tatizo kwenye jamii umaana wa elimu yako unakuwa haupo, huo ni wito kwa watafiti na wahitimu wote waliopo kwenye vyuo watambue kuwa wanawajibu wa kutatua changamoto mbalimbali kwenye jamii” alisema Prof Nombo.

Alisema majukumu ya Vyuo Vikuu ni kufundisha, kutoa mafunzo, kufanya tafiti na kuzifikia jamii na kwamba kwa kupitia matokeo ya tafiti ndipo jamii itafikiwa na kuchukua suluhisho la changamoto za kijamii zilizopo.

Naye mmoja wa watafiti aliyepata tuzo ya mtafiti bora wa mwaka kutoka Ndaki ya Tiba ya Wanyama na Sayansi za Afya, Profesa Robinson Mdegela amesema amefanikiwa kupata tuzo hiyo baada ya kufanya tafiti yenye kugusa maisha ya Watanzania ikiwemo kupambana na ongezeko la usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa tatizo linalokaribia kuua watu karibu 12500 kwa mwaka kiwango ambacho ni karibu mara 10 ya idadi inayosababishwa na malaria au UKIMWI.

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) Prof. Raphael Chibunda amesema kwa mwaka huu 2023 wamefanikiwa kutoa zawadi 248 ambazo hutolewa kila mwaka ili kuonesha ushindani na kuleta mabadiliko makubwa.
Prof. Chibunda amesema mabinti wanaonekana kuwa mstari wa mbele katika kupata zawadi na kuongezeka kila mwaka jambo ambalo linaashiria wanazidi kuongeza juhudi ya kusoma na kuweka changamoto kubwa kwa wanafunzi wa jinsia ya kiume.

Naye mwanafunzi aliyepata tuzo tatu ikiwemo ya mwanafunzi bora wa kike na pia mwanafunzi bora mwaka wa tatu kwa Shahada ya Usimamizi wa Nyuki na Rasilimali Zake SUA Vaileth Chiwango alisema alipata tuzo hizo ambazo atazitumia kubadilisha jamii hasa inayofanya ufugaji wa nyuki kizamani kwa kutumia mizinga ya kisasa na kusimama kimaendeleo.


TUFANYE TAFITI ZENYE TIJA KWA TAIFA-PROF. KASHAIGILI

$
0
0
Utekelezaji wa Miradi ya Utafiti inayohitaji utaalam ni muhimu ikaandikwa kwa ushirikiano baina ya watafiti mbalimbali wakiwemo wa ndani na nje ya nchi ili kuongeza Tija na uwezekano wa kupata ufadhili zaidi ya hayo ni kufanya Tafiti zitakazo zalisha matokeo bora.

Hayo yameelezwa na Prof. Japhet Kashaigili ambae ni Mratibu wa Utafiti na Machapisho kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) na Mshindi wa zawadi ya Mtafiti bora wa Chuo kwa mwaka 2022/2023 wakati akizungumza na wanahabari kwenye Mkutano wa Majalisi SUA ambao uliambatana na utoaji wa Tuzo kwa wanafunzi waliofanya vizuri kwenye masomo yao na watafiti katika Tafiti na kukiletea tija Chuo hicho.

Prof. Kashaigili amesema Mradi ambao ameuleta chuoni hapo unahusu maswala ya Mabadiliko ya Tabianchi na Ustahimilivu katika Nyanda Kavu za Kitropiki kuboresha upatikanaji wa maji Jijini Dodoma hivyo ni mkubwa kwakuwa umegharimu zaidi ya shilingi bilioni 2.4 ukilinganisha na mingine ambayo ipo.

Aidha Prof. Kashaigili amesema Mradi huo umeweza kuwepo na kuonekana kuleta Tija kutokana na ukubwa wake yote hiyo ni kwasababu ya ushirikiano uliopo katika utekelezaji wa Mradi huo ambao umeshirikisha Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) na Taasisi mbalimbali za Uingereza, India na Afrika Magharibi ambapo kwa ujumla zipo Taasisi nane kwaajili ya utekelezaji wa Mradi huo.

“Upataji wa zawadi nikiwa kama Mtafiti bora wa Chuo ambae nimefanya Tafiti au Miradi ambayo imeonekana kukiletea heshima Chuo lakini pia kukiongezea kipato kwangu limekuwa ni jambo la fahari sana kwasababu kuna watafiti wengi hapa chuoni lakini nimeonekana mimi” alisema Prof. Kadhaigili

Kwa upande wake Prof. Robinson Mdegela ambaye pia alipata tuzo ya Mtafiti bora wa mwaka 2023 kutoka Ndaki ya Tiba ya Wanyama na Sayansi Shirikishi SUA amesema amefanikiwa kupata tuzo hiyo baada ya kufanya tafiti yenye kugusa maisha ya watanzania ikiwemo kupambana na ongezeko la usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa tatizo linalokaribia kuua watu karibu 12500 kwa mwaka kiwango ambacho ni karibu mara 10 ya idadi inayosababishwa na malaria au UKIMWI.

Amesema tangu ameanza kufanya tafiti SUA amefanikiwa kupata miradi zaidi ya 35 na kupeleka chuoni karibu shilingi Bilioni 23 kati ya hizo ameweza kutoa ufadhili kwa wanafunzi katika ngazi ya Uzamivu 57 na Umahiri 79 sambamba na kuchapisha majarida 2500.

“Kwa mwaka jana nilipata zawadi ya kuwa mtafiti bora niliechangia kupata fedha nyingi chuoni ambazo mwaka huu nimezitumia katika kufanya tafiti na kusaidia wanafunzi kupata ufadhili wa kufanya masomo yao katika ngazi mbalimbali za elimu zao.



Fwd: HALMASHAURI KUU YA CCM PWANI YAMPA MAUA YAKE, RC KUNENGE KWA USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

$
0
0
Na Mwamvua Mwinyi,Pwani
Nov 22

HALMASHAURI Kuu ya CCM Mkoa wa Pwani, imeridhishwa na usimamizi wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo unaofanywa na Serikali mkoa ambao umetekelezwa kwa asilimia 98 :";pamoja na kumshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kupeleka trilioni 1.19 kwa ajili ya kutekeleza miradi hiyo.


Aidha imetoa rai kwa Serikali mkoa , kuhakikisha inaendelea kutekeleza kwa kasi miradi ya maendeleo ambayo bado haijakamilika ili ifikapo Disemba 2024 iwe imekamilika.


Hayo yalijiri wakati Kamisaa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, alhaj Abubakari Kunenge alipowasilisha taarifa ya utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) March 2021-Juni 2023, katika kikao Maalum Cha Halmashauri Kuu ya CCM Mkoani humo.


Kunenge alijinasibu kuwa wanatekeleza ilani kwa vitendo ,na kuahidi kuendelea kusimamia miradi ya maendeleo ambayo ipo mbioni kukamilika .


Akielezea utekelezaji upande wa miundombinu alieleza ,ujenzi wa barabara kutoka Kibaha- Chalinze- Morogoro km 220 kuwa njia nne (Express way) mradi huu unatekelezwa kwa mfumo wa EPC +F Engineering, Procurement, Construction and Financing ,ujenzi unatekelezwa na Mwekezaji.


"Usanifu wa awali wa mradi huu kuanzia Kibaha hadi Morogoro umeshafanyika , kwasasa Mwekezaji anatafutwa ili ujenzi uanze"


"Barabara hii itapunguza changamoto ya msongamano wa magari na kupunguza ajali ambazo huwa ukijitokeza "alieleza Kunenge.


Hata hivyo Kamisaa huyo alieleza, miradi mingine inaendelea kwa kiwango cha lami katika barabara kuu na barabara za mkoa ikiwemo Kibaha - Mapinga km 23.


SEKTA YA VIWANDA


Idadi ya viwanda imeongezeka kutoka viwanda 1,472 mwaka 2022/2023 viwanda 120 ni vikubwa , 120 vya kati, 271 vidogo na 1,014 vidogo sana.


Kunenge alieleza, kunaongezeko la viwanda 53 ambavyo viwanda 30 ni vikubwa ,ujenzi wa viwanda vipya 15 vinaendelea.


UTALII


Utalii mkoa una vivutio 87 vinavyojumuisha mambokale, misitu ya Hifadhi ya mazingira asilia ,mapori ya akiba ya selous na Wamimbiki ,hifadhi za Taifa za Nyerere na Saadan na fukwe nzuri za bahari.


Ongezeko la watalii limepelekea mapato kuongezeka kutoka sh Bil 9,439,529,840 hadi sh.Bil 14,888,903,208.


Kunenge alieleza ,Mafia imejifungua na kujitangaza kwa utaliii wa Uchumi wa Bluu na Samaki papapotwe samaki anaevutia na kuwa kivutio kikubwa , na aliongeza wanaendelea kuutangaza mkoa kwa utalii uliopo.


NISHATI


Ujenzi wa bwawa la Mwalimu Nyerere JNHPP 2115 MV, utekelezaji umefikia asilimia 93 na unatarajia kukamilika Juni 2024.


Alieleza, njia ya kusafirisha Umeme ya 400 KV kutoka JNHPP hadi Chalinze 160 KV na usf 51 m,sh 39 Bilioni sawa na Jumla ya Bilioni 158 utekelezaji asilimia 99 ,utakamilika disemba 2023.


Kituo cha kupoozea umeme Chalinze Bilioni 128 utekelezaji umefikia asilimia 85.5 utakamilika disemba 2023.


MAJI


Mkoa una vijiji 417 ,mitaa 73 hadi sasa vijiji 331 vimepata maji yenye kujitosheleza, vijiji 57 vina huduma ya wastani sawa na asilimia 79.3 ya wakazi wote wa Mkoa ikiwa asilimia 77 ya wakazi wa Mkoa ikiwa asilimia 77 ya wakazi waishio Vijijini na asilimia 85 ya wananchi Vijijini.


AFYA


Kunenge alieleza, kuna ongezeko la upatikanaji wa dawa, vifaa tiba ,vitendanishi kutoka asilimia 92 kwa kipindi cha februari- machi 2021 hadi asilimia 93.2 kipindi cha april- mei 2023.


Tunaangalia bajeti inayoletwa kutatua changamoto,tunatekeleza , kuna miradi iliyokamilika ,na ipo ambayo haijakamilika,tunajinasibu tunatekeleza kwa vitendo na anayetaka kuyaona na kujifunza aje mkoa wa Pwani ajionee" alieleza Kunenge.


Nae Mwenyekiti wa CCM Mkoani Pwani, Mwinshehe Mlao alieleza , miradi imetekelezwa na amepongeza usimamizi mzuri unaofanywa kwenye miradi ya maendeleo.


Alitaka mkoa kuongeza kasi ya usimamizi wa miradi ambayo inaendelea kutekelezwa .


Mlao alisema Chama na Serikali ni kitu kimoja ,hivyo alihimiza ushirikiano baina ya Chama na Serikali ili kuinua maendeleo na uchumi kwa wananchi.


Kwa upande wake ,Katibu wa CCM Mkoani Pwani, Bernard Gatty alieleza, kamati ya siasa ya mkoa ilifanya ziara katika wilaya zote kuangalia utekelezaji wa ilani ya Chama na kusema utekelezaji umefikia asilimia 98.


Alieleza kwa utekelezaji huo ,wanaimani na ushindi kwa uchaguzi ujao wa Serikali ya mitaa 2024 na uchaguzi mkuu 2025.


"Rais Samia Suluhu Hassan ametutendea haki kutuletea fedha nyingi, watalaam wamefanya kazi yao na Serikali kusimamia kikamilifu, hatuna shaka kujibu hoja kwa wapiga kura wetu,"alisisitiza Gatty.



MHE. RIDHIWANI KIKWETE AFURAHISHWA NA MIRADI YA TASAF IRINGA

$
0
0

Na. Lusungu Helela- Iringa

Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe Ridhiwani Kikwete ameupongeza uongozi wa Mkoa wa Iringa kwa usimamizi mzuri katika utekelezaji wa miradi inayotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii -TASAF.

Amesema kupitia usimamizi mzuri wa utelekezaji wa miradi hiyo, TASAF imeweza kutatua changamoto mbalimbali za kiuchumi na kijamii katika kaya za walengwa pamoja na wananchi katika maeneo ya utekelezaji.

Mhe Ridhiwani amesema hayo mkoani Iringa wakati akizungumza na Walengwa wa Tasaf wa Kata ya Ruaha iliyopo katika Manispaa ya Iringa mara baada ya kukagua daraja lilojengwa katika eneo la Kingemgosi ikiwa ni utekelezaji wa shughuli za Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini unaotekelezwa na TASAF.

Kwa mujibu wa taarifa ya TASAF mkoa wa Iringa inaonesha kuwa jumla ya miradi 474 ikiwemo uchimbaji wa visima vya asili, utengenezaji wa barabara, uzibaji wa makorongo na kuanzishwa kwa mashamba ya korosho ilitekelezwa kati ya Julai 2022 na Juni 2023.

Pia, mkoa ulipokea jumla ya shilingi bilioni 10.3, kati ya hizo shilingi bilioni 8.9 zilitolewa kwa Walengwa 30,988 kutoka vijiji 585 wakati shilingi bilioni 21.6 zilikuwa ni kwa ajili ya usimamizi ngazi ya mkoa na halmashauri.

“Nimefarijika sana kwa namna shughuli za TASAF zinavofanyika hapa katika mkoa wa Iringa likiwemo daraja lililojengwa katika eneo la Kigenamgosi, haya ni matokeo ya ushirikiano thabiti kati ya uongozi wa mkoa na watendaji wote wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii,” amesema.

Kwa upande wake, Mwakilishi Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Oscar Maduhu amewahakikishia na walengwa wa TASAF kuwa waendelea kubuni miradi ya kimaendeleo kwani serikali imetanga jumla ya Sh. 51 bilioni kwa ajili ya Walengwa hao.

“TASAF inaendelea kuhakikisha walengwa wote wanahudumiwa ipasavyo ili kuwaondoa katika hali ya umasikini uliokithiri kupitia ruzuku,miradi ya ajira za muda pamoja na kuwapa elimu ya kuweka na kukopa katika vikundi mbalimbali,” alisema Maduhu.

Awali, Mkuu wa wilaya ya Iringa Mjini, Mhe. Veronika Kessy amesema mpango wa TASAF umesaidia kuinua hali za uchumi kwa walengwa pamoja na kuchechemua biashara mbalimbali kwa wananchi wenye kipato cha chini.

Amesema, utoaji fedha za Mpango umewezesha kaya za walengwa kuboresha makazi na kujenga nyumba za matofali ya kuchoma na kuezeka kwa bati badala ya nyasi.

“Hadi kufikia mwezi Juni 2023, jumla ya walengwa 918 wa TASAF katika mkoa wa Iringa waliweza kuboresha makazi yao,” amesema.


 

Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na wanufaika wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii  (TASAF) mara baada ya kukagua daraja lilijengwa na wanufaika hao kataika eneo la Kinegamgosi, Kata ya Ruaha mkoani Iringa
.

Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akiwa ameambatana na baadhi ya viongozi wa mkoa wa Iringa wakikagua daraja lilijengwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii  (TASAF)  wanufaika hao katika eneo la Kinegamgosi, Kata ya Ruaha mkoani Iringa
Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF, Oscar Maduhu akizungumza  wanufaika wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii  (TASAF)     mara baada ya Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Ridhiwani Kikwete  kuzungumza nao.
Sehemu ya wanufaika wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii  (TASAF) wakifurahia jambo wakati Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete alipokuwa akizungumza nao katika kata ya Ruaha iliyopo katika Manispaa ya Iringa

Dkt Jafo ashiriki Mkutano wa Mawaziri wa Afrika Mashariki Arusha

$
0
0

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo akisalimiana na Katibu wa Mkuu Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) Dkt. Peter Mathuki wakati wa Mkutano wa Kawaida wa 44 wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki unaoendelea katika ukumbi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) jijini Arusha leo Novemba 22, 2023. Pembeni yao ni Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Angellah Kariuki.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo akijumuika na mawaziri wengine wa Serikali ya Tanzania kushiriki Mkutano wa Kawaida wa 44 wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki unaoendelea katika ukumbi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) jijini Arusha leo Novemba 22, 2023.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo akijumuika na mawaziri wengine wa Serikali ya Tanzania kuimba wimbo wa Afrika Mashariki wakati wa Mkutano wa Kawaida wa 44 wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki unaoendelea katika ukumbi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) jijini Arusha leo Novemba 22, 2023.

MAKAMU MWENYEKITI WA CCM ZANZIBAR RAIS DKT. MWINYI MWINYI AONGOZA KIKAO CHA KAMATI MAALUM YA HALMASHAURI KUU YA CCM ZANZIBAR

$
0
0

 

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar ambae pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa katika ukumbi wa mkutano Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Zanzibar, kwa ajili ya Kuongoza Kikao cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Zanzibar kilichofanyika leo 22-11-2023, na  (kulia kwa Rais) Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa  ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Hemed Suleiman Abdullah.(Picha na Ikulu)
 

NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dkt. Mohammed Said Dimwa akisoma ajenda za Kikao cha Kamati Maluum ya Halmashauri Kuu ya CCM Zanzibar, kabla ya kufungulia kwa Kikao hicho na Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar ambae pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia kwake) na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Mhe. Hemed Suleiman Abdullah, kilichofanyika leo 22-11-2023 katika ukumbi wa Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Wilaya Mjini Unguja Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu)
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar ambae pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiongoza Kikao cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Zanzibar, kilichofanyika leo 22-11-2023, katika ukumbi wa Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Wilaya ya Mjini Unguja Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu)
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar ambae pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiongoza Kikao cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Zanzibar, kilichofanyika leo 22-11-2023, katika ukumbi wa Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Wilaya ya Mjini Unguja Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu)

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar ambae pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akongozana na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dkt. Mohammed Said Dimwa, baada ya kumalizika kwa Kikao cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Zanzibar, kilichofanyika leo 22-11-2023 katika ukumbi wa Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Jijini Zanzibar Wilaya ya Mjini Unguja..(Picha na Ikulu)  

WAJUMBE wa Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Zanzibar wakiwa katika ukumbi wa mkutano Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Zanzibar, kabla ya kuaza kwa Kikao cha Kamati Maalumu ya Halmashauri Kuu ya CCM Zanzibar, kilichoongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar  ambae pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, kilichofanyika leo 22-11-2023 katika ukumbi wa Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Wilaya ya Mjini Unguja Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu)

WAANDISHI HABARI ZA MTANDAONI WATAKIWA KUJIUNGA NA TOMA

$
0
0

* Maadili, kanuni na teknolojia vyatajwa kufikia mafanikio

WAANDISHI wa habari za mtandaoni nchini wametakiwa kujiunga kupitia mwavuli wa taasisi ya Tanzania Online Media Alliance (TOMA,) ambao ni mtandao wa waandishi wa habari za mtandaoni ili kujijenga kitaaluma, na kuwa na sekta moja ya waandishi wa habari za mtandaoni yenye sauti moja ya kutetea maslahi yao.

Akizungumza wakati akifungua mpango mkakati huo Mkurugenzi wa Klabu za waandishi wa habari Tanzania (UTPC,) Kenneth Simbaya amesema kuwa katika kuyafikia malengo ni muhimu waandishi wa habari kufanya kazi kwa manufaa ya Umma pamoja na kuzingatia sheria na kanuni hususani katika wakati huu ambao Sayansi na Teknolojia inakua kwa kasi.

Amesema, Uzinduzi wa mpango mkakati huo wa mtandao wa waandishi wa habari za mtandaoni umelenga kuwaunganisha wanahabari hao pamoja na kuwajengea uwezo wa kuandika habari zinazoendana na wakati na kuzingatia ubora wa matumizi kwa Umma wa watanzania.

"Sayansi na Teknolojia inakua kwa kasi, lazima tuzingatie nidhamu katika kufikisha ujumbe kwa jamii pamoja na kuzingatia weledi na sheria za habari...nazipongeza klabu za waandishi wa habari za mikoa yote kwa jitihada mnazochukua katika kuimarisha zaidi tasnia hii ya habari hususani klabu ya waandishi wa habari Mkoa wa Arusha ambako imetoka taasisi hii ya TOMA." Amesema.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa taasisi ya Freedom House ambao ni wadhamini wa mradi huo Daniel Lema amesema kuwa, lengo na kuzindua mpango mkakati huo ni kutoa mwelekeo wa namna ya utekelezaji wa shughuli za taasisi ya TOMA kwa miaka mitano ijayo.

"Mtandao huu kwa waandishi wa habari za mtandaoni umelenga kuwaunganisha wanahabari hao na kuwa na sauti moja na kutetea maslahi yao kote nchini kama sekta moja ya waandishi wa habari za mtandaoni." Amesema.

Aidha ameeleza kuwa TOMA imelenga kuboresha habari zinazotolewa na waandishi wa habari za mtandaoni kwa kuhakikisha zinahusisha sauti za pembezoni ambazo hazisikiki katika uga huo ikijumuisha makundi mbalimbali ikiwemo asasi za kiraia na watu waliopo pembezoni ambako sauti zao hazisikiki na kuhakikisha zinaletwa katika uga wa habari za mtandaoni.

Pia ametoa mwito kwa waandishi wa habari za mtandaoni kujiunga na chombo hicho ambacho kimeundwa kwa ajili yao na kuwataka wajiunge kwa manufaa ya kujijenga kitaaluma, kutoa na kujibu changamoto zinazowakabili.

Mmoja ya wanachama wa TOMA na Mkurugenzi wa Kijukuu Blog kutoka Kahama William Bundala amesema, uzinduzi huo wa mpango mkakati wa miaka mitano ijayo ni fursa kwa wanahabari za mtandaoni kwa kuwa inawaleta pamoja na kubadilishana uzoefu.

"Waandishi wa habari habari za mtandaoni tupo wengi, na kupitia TOMA tunaamini wanahabari wengi zaidi watajiunga katika idadi ya wanachama 260 tuliyopo ili kujenga zaidi tasnia hii ya habari za mtandaoni kwa kuzingatia sheria na kanuni za habari." Amesema.

 

Mkurugenzi wa Klabu za waandishi wa habari Tanzania (UTPC,) Kenneth Simbaya akizungumza wakati akizindua mpango mkakati wa taasisi ya Tanzania Online Media Alliance (TOMA,) na kuwataka waandishi wa habari za mtandaoni kuzingatia weledi, kanuni na maadili katika kuwasilisha taarifa kwa jamii. Leo jijini Dar es Salaam.
 

Mkurugenzi mkaazi wa taasisi ya Freedom House Daniel Lema akizungumza wakati uzinduzi wa mpango mkakati huo na kueleza kuwa TOMA imelenga kuwaunganisha waandishi wa habari za mtandaoni na kuwa na sauti moja ya kutetea maslahi yao nchini kama sekta moja ya waandishi wa habari za mtandaoni. Leo jijini Dar es Salaam.
 

Mwanachama wa TOMA na Mkurugenzi wa Kijukuu Blog William Bundala akizungumza mara baada ya kuzinduliwa kwa mpango mkakati huo na kutoa mwito kwa waandishi wa habari kujiunga na mtandao huo ili kujijenga zaidi kitaaluma na kubadilishana uzoefu. Leo jijini Dar es Salaam.

 

Matukio mbalimbali wakati wa uzinduzi wa mpango mkakati wa taasisi ya Tanzania Online Media Alliance (TOMA.) Leo jijini Dar es Salaam.

KAMPUNI YA DMG YAAHIDI UKARABATI MELI WA VIWANGO ZIWA VICTORIA, TANGANYIKA

$
0
0
Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya kizalendo ya Dar es Salaam Merchant Group (DMG) imeahidi ukarabati wa viwango na kukamilika kwa wakati baada kupewa kazi ya kukarabati meli kongwe ya abiria na mizigo MV. Liemba iliyopo mkoani Kigoma (Ziwa Tanganyika), MV. Ukerewe pamoja na meli ya MT. Nyangumi zinazofanya kazi Ziwa Victoria.

Akizungumza jijini Mwanza mara baada ya kusaini mikataba hiyo mitatu ya ukarabati wa meli hizo na Kampuni ya Huduma za Meli Nchini (MSCL) yenye thamani ya zaidi bilini 48, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Dar es Salaam Merchant Group (DMG), Rayton Kwembe amesema:

“Tunaaidi ukarabati uliotukuka na wenye viwango ambapo kwenye utekelezaji huu tunafanya kwa ushirikiano na Kampuni ya M/S Brodosplit JSC ya Nchini Croatia kwa garama ya Zaidi ya shilingi bilioni 48.”

Mkurugenzi huyo alisema kuwa ukarabati wa meli kongwe ya abiria na mizigo MV. Liemba utatumia gharama ya shilingi bilioni 32 wakati ukarabati wa MV. Ukerewe utafanywa kwa shilingi bilioni 6 wakati ukarabati wa meli ya MT. Nyangumi utafakinishwa kwa gharama ya shilingi bilioni 8.

Kwembe aliongeza: “Kampuni yetu ya DMG inaishukuru sana serikali yetu ya awamu ya Sita chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutuamini na tunaiahidi Serikali kuwa kamwe hatutawaangusha katika utekelezaji wa miradi hii.”

Alisisitiza kwa kusema, “Tutajitaidi kwa hali na mali kuhakikisha kuwa miradi hii ya ukarabati tunaifanya kwa muda muafaka ili meli hizi ziweze kuendelea kufungua fursa nyingi za ajira binafsi na kupunguza gharama za usafirishaji sambamba na kuongeza tija katika shughuli za biashara hivyo kuwafanya wananchi wengi kunufaika.”

Mkuruenzi huyo wa DMG alidokeza kuwa kampuni yao ina uzoefu wa muda mrefu na utaalam wa kushiriki katika miradi mikubwa inayohusisha matengenezo ya meli na uundaji kwa ujumla kutoka hatua ya awali mpaka kukamilika.

Alibainisha: “Lakini pia Kampuni yetu ya DMG ipo katika mahusiano mazuri na taasisi za fedha ambapo mahusiano haya yanatusaidia kupata fedha stahiki kwa wakati pale zinapoitajika ili kusaidia miradi yetu kwenda na muda ulipangwa."

Alisisitiza: "Ili kutekeleza vyema miradi ya ujenzi wa meli na matengenezo yake, DMG ilianzisha Idara ya kushughulikia mambo hayo mwanzoni mwaka 2017 kwa nia ya kutatua changamoto zinazoikabili Sekta hii iliyo katika uchumi wa bluu kwa kuleta maendeleo.

Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Huduma za Meli (Mscl), Eric Hamissi amesema Serikali imeamua kuwekeza katika ukarabati wa meli hizo kutokana na uimara wake na kuokoa gharama ya kujenga au kutengeneza meli mpya.

"Kuna watu walikuwa wananiuliza kwanini Serikali inafanya ukarabati wa meli hii sasa ni wajibu kwamba mbali na meli hizi kuwa na miaka mingi lakini gharama za kutengeneza meli mpya kama hizi moja ni zaidi ya Sh120 bilioni lakini pia baada ya wataalamu kuchunguza meli zilizopo tulibaini bado vyuma vyake vina ubora mkubwa na havina uchakavu ndio maana Serikali ikaamua kuwekeza," amesema Hamissi.

Akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini wa mikataba mitatu ya ukarabati wa meli uliofanyika katika Bandari ya Kusini jijini Mwanza, Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi, David Kihenzile ametaka ukarabati huo kuzingatia muda wa mkataba.

"Nitumie fursa hii kuwaomba wananchi jiandaeni kutumia fursa hii ya miradi ambayo inatekelezwa na Serikali na popote pale tunapofanya miradi naomba wananchi wenyeji wapewe kipaumbele cha kupewa ajira na nitoe rai kwa kwa viongozi wa mikoa kusimamia vyema na kuhakikisha mnalinda na mnapinga uhujumu uchumi katika miradi hii," amesema Kihenzile.
Mkuu wa Kitengo ca Ukarabati wa Meli wa Kampuni ya Dar es Salaam Merchant Group (DMG), Mhandisi Michael Masambwa (kushoto) pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Huduma za Meli (Mscl), Eric Hamissi (kulia) wakitia saini mikataba ya ukarabati wa meli za MV Liemba, MT Ukerewe na MT Nyangumi hafla iliyofanyika bandari ya kusini jijini Mwanza.
Mkuu wa Kitengo ca Ukarabati wa Meli wa Kampuni ya Dar es Salaam Merchant Group (DMG), Mhandisi Michael Masambwa (kushoto) wakishikana mikono na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Huduma za Meli (Mscl), Eric Hamissi (kulia) ili kubadilishana mikataba mara baada ya kusaini mikataba hiyo ya ukarabati wa meli za MV Liemba, MT Ukerewe na MT Nyangumi hafla iliyofanyika bandari ya kusini jijini Mwanza.
Mkuu wa Kitengo ca Ukarabati wa Meli wa Kampuni ya Dar es Salaam Merchant Group (DMG), Mhandisi Michael Masambwa (kushoto) pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Huduma za Meli (Mscl), Eric Hamissi (kulia) wakionyesha mikataba mara baada ya kusaini  mikataba hiyo ya ukarabati wa meli za MV Liemba, MT Ukerewe na MT Nyangumi hafla iliyofanyika bandari ya kusini jijini Mwanza.

“TUWAUNGE MKONO WATU WENYE ULEMAVU NCHINI” NAIBU WAZIRI NDERIANANGA

$
0
0

NA. MWANDISHI WETU

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Ummy Nderiananga aemtoa wito kwa wadau kuendelea kuunga mkono watu wenye ulemavu nchini katika nyanja mbalimbali ikiwemo kuwapatia vifaa saidizi ili kurahisisha upatikanaji wa huduma na kujiletea maendeleo yao.

Ameyasema hayo Novemba 22, 2023 wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa saidizi kwa watu wenye ulemavu katika Mkoa wa Mtwara vilivyotolewa na Kampuni ya Sigara ya TCC ikiwemo fimbo nyeupe, vyereani, baiskeli na viti mwendo kwa lengo la kuwasaidia katika na kuyafikia mahitaji waliyonayo.

Naibu Waziri Ummy alisema kuwa kundi la wenye ulemavu ni vyema lisiachwe nyuma kwa kuzingatia mchango wao katika jamii hususan katika shughuli mbalimbali ikiwemo za kiuchumi.

“Watu wenye ulemavu tunamahitaji mengi, hiki kilichofanywa leo na kampuni ya Sigara kimenifurahisha sana na mmeonesha namna gani mnajali na mmiunga Serikali mkono kwa vitendo, na mmegusa kundi hili Muhimu, niwaombe na wadau wengine kufanya kwa kuzingatia mahitaji yao,” alisema Mhe Nderiananga.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Kanali Ahmed Abbas Ahmed aliupongeza uongozi wa Kampuni ya Sigara kwa kuendelea kuwakumbuka watu wenye ulemavu huku akitoa wito kwa wadau mbalimbali kuendelea kuunga mkono jitihada za Serikali katika kuhakikisha hakuna kundi linaliloachwa nyuma kwa lengo la kuendelea kuchangia katika shughuli za kujiletea maendeleo yao na Taifa kwa ujumla.

“Ninawashukuru wadau wetu Kampuni ya Sigara kwa kuona umuhimu wa kuwakumbuka watu wenye ulemavu, sisi Mkoa tumefarijika sana kwa mchango wenu endeleeni kufanya hivyo kwa makundi yenye mahitaji,” alieleza Kanali Abbas

Naye Mwenyekiti wa Jukwaa la Watu wenye ulemavu Mtwara akitoa shukrani kwa niaba ya viongozi wa SHIVYAWATA mkoa Bi. Zamda Said alipongeza Kampuni ya Sigara kwa kuwasaidia vifaa hivyo huku akitumia nafasi hiyo kuwaasa watu wenye ulemavu kuvitunza vifaa hivyo na kuvitumia kwa malengo yaliyokusudiwa.

“Msiuze vifaa hivi, tuvitumie kwa manufaa yetu na wengine, ili inapotokea wadau wanajitokeza kutusaidia wasikatishwe tamaa kwa kutokutunza vifaa husika,” alisema Bi. Zamda.

 

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga akiongea wakati wa halfa ya kukabidhi vifaa saidizi vilivyotolewa na Kampuni ya Sigara nchini kwa watu wenye ulemavu mkoani Mtwara tarehe 22 Novemba, 2023.


 

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga akikabidhi vifaa saidizi kwa watu wenye ulemavu mkoa wa Mtwara vilivyotolewa na Kampuni ya Sigara nchini (TCC) tarehe 22 Novemba, 2023 katika Ofisi ya Mkuu wa mkoa huo.

 

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga akikabidhi baiskeli kwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Watu wenye Ulemavu Mtwara Bi. Zamda Said ikiwa ni sehemu ya vifaa vilivyotolewa na Kampuni ya Sigara nchini kwa lengo la kusaidia watu wenye ulemavu mkoani Mtwara. 

(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)

TRA YARUDISHA SHUKRANI KWA WALIPA KODI SHULE YA MSINGI KISARAWE 11

$
0
0
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA), imetumia Sh. milioni 50 kujenga madarasa na kununua madawati, ikiwa ni shukrani ya mamlaka hiyo kwa walipakodi.

Akizungumza leo Novemba 22, 2023 alipokuwa akikabidhi madarasa na madawati hayo katika Shule ya Msingi Kisarawe II iliyopo Manispaa ya Kigamboni jijini Dar es Salaam, Naibu Kamishna Mkuu wa Idara ya walipakodi wakubwa, Eunice Luheluka, amesema TRA imejenga madarasa mawili pamoja na madawati 100.

Amesema lengo ni kushiriki kwa namna ya pekee kugusa huduma za kijamii kwa wananchi kwa kuunga mkono juhudi za serikali kuwahudumia wananchi.

Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Wilaya ya Kigamboni, Upendo Mahalu, ameishukuru TRA kwa ufadhili huo na kuyaomba mashirika na makampuni mengine kujitokeza kusaidia ujenzi wa miundombinu ya shule.

"Kama mnavyofahamu Wilaya yetu bado ni changa ina mahitaji mengi. Tuna upungufu wa madarasa na madawati japokuwa tumepata fedha kupitia mradi wa Boost, bado mahitaji ni makubwa," amesema.

Mkuu wa Shule ya Msingi Kisarawe II, Joseph Kavishe, amesema baada ya ufadhili wa TRA, shule inaupungufu wa madarasa 18 na madawati 192.

"Mradi huo utatusaidia kupunguza mrundikano darasani na utawawezesha wanafunzi 300 waliokuwa wanakaa chini kupata madawati. Tumeamua madarasa haya mapya yatumiwe na wanafunzi wa darasa la kwanza ili kuwapa utulivu wawapo shuleni," amesema.



JAMII YAASWA KUWASAIDIA WATOTO KUKABILIANA NA ATHARI ZA MABADILIKO YATABIA NCHI

$
0
0

Baadhi ya wanafunzi kutoka shuke mbalimbali Jijini Arusha wakiwa katika kuadhimisha siku ya mtoto duniani ambayo kwa Tanzania imefangila leo JinininArudha katika hotel ya Mount Meru kutokana na muingiliano wa majukumu , kwani hadhimishwa kila novemba 20 kila mwaka Baadhi ya wanafunzi kutoka shuke mbalimbali Jijini Arusha wakiwa katika kuadhimisha siku ya mtoto duniani ambayo kwa Tanzania imefangila leo JinininArudha katika hotel ya Mount Meru kutokana na muingiliano wa majukumu , kwani hadhimishwa kila novemba 20 kila mwaka

Baadhi ya wanafunzi kutoka shule mbalimbali Jijini Arusha na wanafunzi kutoka Zanzibar wakiwa na Idara ya mtoto Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Sebastiani Kitiku ,pamoja na baadhi ya viomngozi mbalimbali wenye dhamana ya kuwaaangalia watoto wakiwa katika picha ya pamoja katika kuadhimisha siku ya mtoto duniani ambayo kwa Tanzania imefangila leo JinininArudha katika hotel ya Mount Meru kutokana na muingiliano wa majukumu , kwani hadhimishwa kila novemba 20 kila mwaka



Vero Ignatus Arusha


Maadhimisho Siku ya Mtoto duniani yaliyotokana na mkataba wa kimataifa wa Haki za mtoto ya mwaka 1989,ambapo nchi ya Tanzania iliridhia kulindwa kwa za haki watoto sambamba na kuwasaidia namna ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi

Hayo yamesemwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo amewataka washauri elekezi wa mazingira kujikita kwenye Kumjengea mtoto uwezo wa kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi kwani chakula kinapokosekana watoto ndiyo wanaoathirika zaidi

Ametoa wito huo leo Jijini Arusha katika siku ya mtoto duniani na huku akisema Jabo la kuwalimda watoto na kutunza mazingira ni suala ambalo halina majadala Lazima tulipe kipaumbele

Akizungumza katika siku hiyo ya Mtoto duniani Mkuu wa Idara ya mtoto Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Sebastiani Kitiku alisema siku hiyo wanajadili juu ya
Mabadiliko ya tabia nchi na watoto na namna ya kulinda mtoto sambamba na
Kujaribu kukumbushana umuhimu wa hali za watoto

Kitiku ameainisha haki tano za watoto ikiwa ni pamoja na kutunza haki za watoto didhi ya ukatili,haki ya Kuishi kuendelezwa ,kulindwa ,kushiriki nakushirikishwa katika masuala yanayowahusu pamoja na kuhakikisha hawabaguliwi kwa haki yeyote ile.

Akitoa salam za mkoa kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Arusha , mkuu wa wilaya ya Arumeru Emmanuela Kaganda amesema watoto ni 50% ya watanzania wote hivyo ameishikuru Wizara ya Maendeleo ya Jamii na UNICEF kuchagua mkoa huo kwaajili ya kufanyika maadhimisho hayo na amewahakikishia kuwa mkoa upo shwari salama na timamu

Kwa upande wake muwakilishi Mkazi Unicef Tanzania Bi Elk Wisch amesema kuwa kizazi hiki watoto chipukizi jamii inahitajika kuwaweka katika shughuli wanazozifanya ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi


Wisch amesisitiza kuwa lazima Watoto,vijana balehe wafundishwe kupanda miti ili kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa pamoja na kuepuka kuwapoteza wanyama waliopo hatarini kupotea, hiyo itajenga maana halisi ya Kauli mbiu ya siku ya mtoto Duniani.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia wanawake na amesema kuwa Maadhimisho hayo kwa nchi ya Tanzania yamefanyika leo tarehe 22/11badala ya novemba 20 kutokana na mwingiliano wa majukumu huku akiendelea kusisitiza kulindwa kwa haki za watoto nanamna ya kuwafunza kukabikiana na mabadiliko ya tabianchi.

Aidha Mpanju amesisitiza kuwa kaulimbiu hiyo ni dhahiri imekuja kwa wakati muafaka kwaajili ya kuwasaidia watoto wetu kutambua na kuwapatia elimu ya kutosha ili waweze mabalozi wazuri wa kukabiliana na mabadiliko hayo kwani serikali inaratibu na kusimamia haki zote za watoto ikiwemo haki ya kuishi na kumlinda didhi ya vitendo vyote vya ukatili.

Tawi la NMB Dumila lazinduliwa rasmi

$
0
0


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe, Adam Malima (wa tatu kulia), akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Tawi jipya la Benki ya NMB Dumila lililopo mkoani Morogoro, wengine katika picha ni Mkuu wa Wilaya ya Kilosa, Shaka Hamdu Shaka (wa tatu kushoto), Afisa Mkuu Wateja Binafsi na Biashara wa Benki ya NMB, Filbert Mponzi (wa pili kulia), Mkuu wa Idara ya Masoko na Mawasiliano wa Benki ya NMB, Rahma Mwapachu (kulia), Meneja Uendeshaji Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Dodoma, Lilian Silaa (kushoto) na wa pili kushoto ni Meneja wa NMB Kanda ya Kati, Janeth Shango.


Meneja Tawi la NMB Dumila, Innocent Kato alimwelezea Mhe, Adam Malima kuhusu huduma zilolewazo na Tawi la NMB Dumila baada ya uzinduzi rasmi.

Sehemu ya wageni waalikwa Waliohudhuria uzinduzi wa Tawi la NMB Dumila.



 


PROF. MKENDA AVITAKA VYUO VIKUU KUWEKEZA KWENYE TAFITI

$
0
0

 

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amevitaka vyuo vikuu nchini kutenga Fedha kwa ajili ya tafiti zitakazo saidia kutatua changamoto za jamii ya Tanzania.

Ameyasema hayo leo Novemba 22, 2023 Morogoro wakati akizungumza kwenye Mkutano Mkuu wa Baraza la 23 la wahitimu wa Chuo Kikuu Mzumbe.Amesema Serikali tayari imeandaa mazingira wezeshi ya kuongeza nguvu katika matumizi ya Tehama , ili kuendana na kasi ya utandawazi
Aidha Prof. Mkenda amesema  kwa mwaka wa fedha 2022/23 Serikali imetenga kiasi cha sh milioni 500 kwa Chuo Kikuu Mzumbe ili kuboresha miundombinu ya Chuo hicho.

Kwa upande wake Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Prof. Williamu Mwegoha
amesema  mafanikio mbalimbali ya Chuo hicho ikiwemo kukamilisha ujenzi wa hostel ambazo zitabeba zaidi ya wanafunzi 1026, kuongezeka kwa udahiri wa wanafunzi na kufikia asilimia 17.3%.
Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Prof. Elisante Ole Gabriel, akizungumza wakati wa Mkutano Mkuu wa Baraza la 23 la wahitimu wa Chuo Kikuu Mzumbe.
Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu Mzumbe, Prof. Saida Yahya Othman akizungumza.
Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu Mzumbe, Prof. Saida Yahya Othman (kulia) akiteta jambo na Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Prof. William Mwegoha.Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam  Malima akisoma hotuba yake wakati wa Mkutano Mkuu wa Baraza la 23 la wahitimu wa Chuo Kikuu Mzumbe. (PICHA ZOTE NA EMMANUEL MASSAKA,MICHUIZI TV)


Sehemu ya watumishi wa chuo hicho.
Sehemu ya watumishi wa chuo hicho.


Sehemu ya watumishi wa chuo hicho. (PICHA ZOTE NA EMMANUEL MASSAKA,MICHUIZI TV)























WAZIRI BASHUNGWA AWATAKA TANROAD KUWASIMAMIA KWA UMAKINI WAKANDARASI WANAOTEKELEZA MIRADI NCHINI

$
0
0



WAZIRI wa Ujenzi Inocent Bashungwa kushoto akikagua barabara inayotoka Kwamsisi kuelekea Pangani mkoa ni Tanga wakati wa ziara yake kulia ni Mkuu wa wilaya ya Handeni Albart Msando



Waziri wa Ujenzi Inocent Bashungwa akizungumza mara baada ya kuikagua barabara hiyo kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Handeni Albarto Msando

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Handeni Saitoti Zelothe akizungumza wakati wa ziara hiyo kulia ni Waziri wa Ujenzi Inocent Bashungwa








Na Oscar Assenga,HANDENI


WAZIRI wa Ujenzi Inocent Bashungwa ameiagiza Wakala wa Barabara nchini (TANROAD) kuhakikisha wanawasimamia kwa umakini wakandarasi wanaotekeleza miradi ya barabara nchini kutokana na kusuasua na serikali kutoridhishwa na kasi ya ujenzi.

Sanjari na agizo hilo pia amesema iwapo miradi hiyo ya barabara itaendelea kusuasua atalazimika kumshauri Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ambadilishe Mtendaji Mkuu wa Tanroad nchini Mohamed Besta kama ataendelea kucheka na wakandarasi hao bila ya kuwachukulia hatua.

Bashungwa aliyasema hayo leo wakati wa ziara yake ya siku moja wilayani Handeni na Pangani ambapo alikagua barabara ya kutoka Tanga-Pangani hadi Bagamoyo ambayo inatekelezwa na mkandarasi wa kampuni ya Kichina ya Railway 15, hakuridhishwa na kasi ya ujenzi wake.

Alisema kwamba kuna miradi mingi imekuwa ikisuasa suasua lakini bado wanaendelea kuiangalia bila kuchukua hatua jambo ambalo linakwamisha juhudi kubwa za Serikali kuifungua nchi kupitia miradi ya barabara ya kimkakati.

“Barabara hii nikuambie Mkurugenzi Mkuu wa Tanroad, kama hatutachukua hatua kwa muda unaotakiwa miradi kama hii inayoendelea kusuasua nitamshauri rais akubdilishe hatuwezi kuendelea namna hii”Alisema Waziri Bashungwa.

“Lakini pia Kaimu Mkurugenzi wa Miradi Tanroad tumemuamini tumekukaimisha ili usimamie hayo tumekuwa na wewe uone, Boniface Mkumbo yule aliyekuwa kabla yako nilipokuja kumtoa ilikuwa mbinde kwa sababu ya kulindana sasa Mkurugenzi Mtendaji baada ya wao utakuwa wewe kama usipobadilika”Alisema

Waziri huyo alisema haiwezekani anapokwenda kila kipande cha barabara nchini niwaamshe nyie hapana lazima mbadilike kama sijawaamsha na ile mipango mlioniambia naenda kukagua barabara lakini sitaki wakandarasi wa aina hii kule yule CR 7 hawa ni CR 15 wanaweza kukuta mtu na binadamu yake.

“Lakini yule CR 7 ni shida kwani miradi kama sita imesimama kwa sababu ya kurundikiwa miradi na nyie mnajiita CR 15 nyie mnauhusiana na C7 hii ni tatizo kila mradi mnaoufanya hii barabara wananchi mmesikia mipango ya Serikali ninakwenda kuikagua”Alisema.

Aliwaambie wananchi tayari Serikali imeshaleta fedha lakini mkandarasi anawachelewesha wameona ni kwanini wanawachelewesha Mkurugenzi wa barabara hautakiwa kuwa ofisini unapaswa uzungumze maeneo mbalimbali nchini ili uweze kuona changamoto

Awali akizungumza wakati wa ziara hiyo Mtendaji Mkuu wa Tanroad alimueleza Waziri Bashungwa kwamba hatua ambazo wamechukua ni kumuelekeza mkandarasi aongeze vifaa na awe na mpango kazi ambao unaendana na wakati.

Alisema kwa sababu kwa sasa yupo nyuma ya asilimia 19 ya mpango wake ya kazi na Novemba 14 waliwaita makao makuu na kukaa kikao nao na baadae Novemba 28 wamewaita tena ili kuona kama yale maelekezo yametekelezwa.

Naye kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Handeni Albert Msando alisema kwamba wananchi wa eneo la Kwamsisi wameandika Historia kwa kuwa Waziri wa kwanza kufikia na kuzungumza nao na kutembelea barabara hii na wananchi walikuwa wamekata tamaa.

Alisema kwamba wanawaomba wanapokwenda kwa maofisi ya wakuu wa wilaya wasije na kuondoka na waache kujifungia ofisini wabadilike watumie ofisi zilizopo katika maeneo wanayotekeleza miradi.

“Mh Waziri sisi hapa leo tunapoteza tuna mazao mengi tunalima unaweza kukaa wiki nzima hautaja toa mazao na hivyo kupoteza mapato mengi ambayo serikali yangepatikana kwamsisi jana na juzi wamekusanya 0 hakuna gari zinaingia shambani kwa sababu ya ubovu wa barabara”Alisema

Alisema kwa sababu wao ni wazalishaji wengi ya muhogo barabara hii itakuwa mkombozi na wananchi hao watakukuyumbisha hivyo Tanroad lazima waangalie mahitaji ya wananchi na fedha imetengwa haenda hatua moja mbele.

WATAALAM ANDAENI MAANDIKO UBORESHAJI WA BIASHARA YA UTALII ILIYOPO DUNIANI KWA SASA

$
0
0


Baadi ya wanafunzi wa Chuo cha Utalii Kampasi ya Arusha (NCT)kama wanavyoonekana katika picha

Wanafunzi wa Chuo cha Utalii Kampasi ya Arusha (NCT)wakimsikiliza Naibu Waziri wa maliasili na Utalii Dunstan Kitandula alipotembelea chuoni hapo kama wanavyoonekana katika picha



Na,Vero Ignatus,Arusha

Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imeutaka Uongozi na watumishi wa Chuo cha Utalii Kampasi ya Arusha (NCT)kimetakiwa kuwa na wabunifu katika kuandika maandiko yanayoendana na hali halisi ya biashara ya utalii Duniani, kwani kutakapokuwa na maandiko ya kisasa yanayoshawishi uboreshaji wa biashara ya utalii ndivyo tutakavyo kuza biashara ya utalii na kuongeza mchango wa pato la taifa kutoka katika Chuo cha Utalii Tanzania

Ameyasema hayo Naibu Waziri wa maliasili na Utalii Dunstan Kitandula wakati alipokuwa akiongea na watumishi wa chuo hicho kilichopo maeneo ya Sakina Jijini Arusha ambapo aliutaka uongozi wa chuo hicho kujipima au kujitathimini kwa kina namna ambavyo wataweza kubeba mzigo mkubwa kutokana na mikakati ambayo imejiwekea na makubaliano waliyowekeana na taasisi mbalimbali ambazo chuo cha Utalii kitandaa wataalamu wa ukarimu wa taasisi hizo

Aidha Kitandula aliongeza kuwa ili chuo hicho kiwe hai na kuonekana lazima kuwepo na maandiko ya kibiashara yanayoshawishi wafadhili au serikali kutoa fedha kwa ajili ya maendeleo ya chuo,vilevile amepongeza chuo hicho kwa jitihada na hatua mbalimbali wanazochukua katika kuhakikisha chuo kinatoa wahitimu walio bora na waliopata mafunzo kwa vitendo katika uhalisia wa biashara ya utalii inayoendela Duniani.

“Nawapongeza kwa ujenzi unaondelea katika eneo hili kwani kwa kufanya hivyo mtaongeza udahili wa wanafunzi katika fani mbalimbali zinazoendeshwa hapa chuoni” Alisema Mhe. Kitandula

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo cha Utalii Tanzania, Dkt. Florian Mtei akizungumza kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii kuzungumza, ameushukuru uongozi wa wizara unaoongozwa Mhe. Angellah Kairuki Waziri wa Maliasili na Utalii kwa kuwa umekuwa karibu na Chuo katika kusaidia mambo mbalimbali kwa ajili ya ajili ya Maendeleo ya Chuo cha Utalii Tanzania

SOMBI ATOA VIFAA VYA TEHAMA KWA SENATE

$
0
0

 

Aahidi UVCCM itaendelea kuwashika mkono vijana

Na MWANDISHI WETU

MAKAMU Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Rehema Sombi, amesema umoja huo utaendelea kuwaunga mkono vijana wote wanauokiunga mkono Chama katika utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2020-2025.

Ahadi hiyo ameitoa leo Novemba 21, 2023 alipokabidhi vifaa mbalimbali vya kiofisi kwa Senate ya Vyuo na Vyuo Vikuu hatua iliyotokana na ombi la kufanya hivyo alipozitembelea Senate mbalimbali kwa lengo la kuimarisha utendaji wao.

Rehema amewataka vijana waliopata fursa ya kupata elimu katika ngazi na taasisi mbalimbali kuhakikisha wanasoma kwa bidii na maarifa makubwa.

“Leo imekuwa faraja kubwa kwangu kuwa mahali hapa na kutekeleza ahadi hii ya kuwaletea vifaa ya TEHAMA pamoja na ‘stationaries’.

“Kama mnavyojua kuwa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) ni chombo kinachowaunganisha vijana wote wa Tanzania wanaounga mkono sera, siasa na itikadi ya Chama Cha Mapinduzi. 

“Shabaha ya Chama kuunda Umoja wa Vijana wa CCM ni kuwa shule ya kuandaa wanachama safi, viongozi bora wa CCM imara. Kwa mnasaba huo, UVCCM inaendelea kuandaa vijana kuwa raia wema kwa taifa letu na kwamba chombo hiki ni sawa na tanuri la kuoka makada wazuri wa Chama chetu,” amesema.

Amesema kuwa umoja huo una wajibu wa kuongoza shughuli zinazohusu maendeleo na maslahi ya vijana nchini.

Kwa mujibu wa Rehema, kutokana na msingi huo ndio maana zilianzishwa senate za vyuo vikuu za UVCCM ikiwa njia mojawapo ya kuwatambua vijana wenye vipawa na kuwaandaa kulitumikia taifa “vijana ambao watakuwa na imani ya Chama chetu na watakubali kuishi katika misingi ya taifa letu.”

“Binafsi kwa niaba ya umoja wa vijana nilipata wasaa wa kutembelea senate za vyuo kadhaa ambapo pamoja na mambo mengine mlinieleza ukosefu wa vifaa vya TEHAMA na stationaries.

“Nimeendelea kufanya juhudi kuhakikisha nawaona wadau wa maendeleo. Naushukuru Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) kupitia kwa Mkurugenzi Mkuu wake, Bi. Justina Mashiba kwa kuonesha nia na kutoa mchango katika kugusa wanafunzi na elimu ya juu na kutupatia vifaa hivi ambavyo leo naviwasilisha kwenu,” amesema.

Amesisitiza kuwa UVCCM itaendelea kuwa kamisaa wa kuhakikisha inatambua mchango wa vijana wanaounga mkono juhudi za Chama walioko vyuo vikuu kupitia senate na kuwa daraja la kuwaunganisha na wanachi katika ujenzi wa maendeleo ya taifa.









WANATAALUMA CHUO CHA UTALII ARUSHA WATAKIWA KUANDAA MAANDIKO YA UBORESHAJI UTALII YANAYOENDANA NA DUNIA YA SASA

$
0
0



Na Jane Edward,Arusha

Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imeutaka Uongozi na watumishi wa Chuo cha Utalii Kampasi ya Arusha (NCT)  kuwa wabunifu katika kuandika maandiko yanayoendana na hali halisi ya biashara ya utalii Duniani, kwani kutakapokuwa na maandiko ya kisasa yanayoshawishi uboreshaji wa biashara ya utalii ndivyo tutakavyo kuza biashara ya utalii na kuongeza mchango wa pato la taifa kutoka katika Chuo cha Utalii Tanzania

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa maliasili na Utalii, Mhe. Dunstan Kitandula(Mb) alipokuwa akiongea na watumishi wa chuo hicho kilichopo maeneo ya Sakina Jijini Arusha.

Mhe. Kitandula aliongeza kuwa ili chuo hicho kiwe hai na kuonekana lazima kuwepo na maandiko ya kibiashara yanayoshawishi wafadhili au serikali kutoa fedha kwa ajili ya maendeleo ya chuo.

Aidha, Mhe. Kitandula  aliutaka uongozi wa chuo hicho kujipima au kujitathimini kwa kina namna ambavyo chuo hicho kitaweza kubeba mzigo mkubwa kutokana na mikakati ambayo imejiwekea na makubaliano waliyowekeana na taasisi mbalimbali ambazo chuo cha Utalii kitandaa wataalamu wa ukarimu wa taasisi hizo.

Sanjari na hayo, Mhe. kitandula amepongeza chuo hicho kwa jitihada na hatua mbalimbali wanazochukua katika kuhakikisha chuo kinatoa wahitimu walio bora na waliopata mafunzo kwa vitendo katika uhalisia wa biashara ya utalii  inayoendela Duniani.

“Nawapongeza kwa ujenzi unaondelea katika eneo hili kwani kwa kufanya hivyo mtaongeza udahili wa wanafunzi katika fani mbalimbali zinazoendeshwa hapa chuoni” Alisema Mhe. Kitandula

Awali akizungumza kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii kuzungumza,  Mkuu wa Chuo cha Utalii Tanzania, Dkt. Florian Mtei ameushukuru uongozi wa wizara unaoongozwa Mhe. Angellah Kairuki Waziri wa Maliasili na Utalii kwa kuwa umekuwa karibu na Chuo katika kusaidia mambo mbalimbali kwa ajili ya ajili ya Maendeleo ya Chuo cha Utalii Tanzania.



 

Viewing all 118921 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>