More Channels
Showcase
Articles on this Page
(showing articles 19821 to 19840 of 65691)
- 09/28/15--06:31: _WAFANYAKAZI KISSA P...
- 09/28/15--06:43: _Rais Kikwete kuzind...
- 09/28/15--12:37: _HABARI KUTOKA VITUO...
- 09/28/15--12:41: _BBC DIRA YA DUNIA J...
- 09/28/15--12:48: _President Kikwete m...
- 09/28/15--13:07: _CHOPA YA CCM YATUA ...
- 09/28/15--13:17: _Tanzania yatangaza ...
- 09/28/15--13:26: _MAALIM SEIF ATEMBEL...
- 09/28/15--13:30: _WASANII WA BONGO MO...
- 09/28/15--13:38: _Sheria ya Kuratibu ...
- 09/28/15--17:00: _SIKU YA MOYO DUNIAN...
- 09/28/15--20:42: _UTARATIBU WA KISHE...
- 09/28/15--20:53: _TAARIFA ZAIDI KUHUS...
- 09/28/15--21:01: _VIJANA WAANZISHA CL...
- 09/28/15--21:09: _ MUZIKI MNENE KIBAHA
- 09/28/15--21:20: _FAHAMU UGONJWA WA B...
- 09/28/15--21:25: _USIKU WA ESTER DIAN...
- 09/28/15--23:10: _JIFUNZE LUGHA YA ALAMA
- 09/29/15--00:53: _Kipindi cha JUKWAA ...
- 09/29/15--01:07: _MECHI ZA UEFA USIKU HU
(showing articles 19821 to 19840 of 65691)
Channel Description:
Most read Swahili blog on earth
0 |
|
0 |
|
Wafanyakazi Kissa Pharmacy wakisikiliza kwa makini maelezo ya mmoja wa watoa huduma katika mapango hayo Ndugu Allan Yohana kabla ya kuanza rasmi shughuli ya kutembelea mapango hayo.(JAMIIMOJABLOG) |
The Amboni Caves are the most extensive limestone caves in East Africa. They are located 8 km north of Tanga City in Tanzania off the Tanga-Mombasa road. The caves were formed about 150 million years ago during the Jurassic age. It covers an area of 234 km². According to researchers the area was under water some 20 million years ago. There are altogether ten caves but only one is used for guided tours.
Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) Devotha Mdachi (kulia) akizungumza jana Dar es Salaam kuhusu maandalizi ya onesho la Swahili International Expo linalotarajiwa kufanyika kwa siku tatu kuanzia Oktoba Mosi hadi 3, mwaka huu katika ukumbi wa mlimani City Dar es Salaam.Kushoto ni Meneja wa kampuni ya fastjet Jimmy Kibati kama mmoja wa wadhamini.
Mratibu wa onesho la Swahili International Expo Philip Chitaunga (kulia) akizungumza Dar es Salaam jana kuhusu onesho hilo linalotarajiwa kufanyika kwa siku tatu kuanzia Oktoba Mosi hadi 3, mwaka huu katika ukumbi wa mlimani City Dar es Salaam.Wenginekutoka kushoto ni Meneja wa kampuni ya fastjet kama mmoja wa wadhamini, Kaimu Mkurugenzi TTB Devotha Mdachi na Milat Mekennon kutoka shirika la ndege la Ethiopia.
ONESHO la Swahili International Expo linatarajiwa kufanyika wiki hii, kuanzia tarehe 1-3 Oktoba,2015 katika ukumbi wa Mlimani City ambapo Rais Jakaya Kikwete anatarajiwa kuwa mgeni rasmi.
Hii ni mara ya pili kwa Onesho hili kufanyika,Mwaka jana ilikuwa mara ya kwanza October 1- -4,2014
Onesho la mwaka jana liliweza kuwavutia Waoneshaji 40,Mawakala wa Utalii walioalikwa kutoka nje ya nchi 19 (hosted Buyers),Waaandishi wa Habari kutoka nje ya nchi 4 (media),Wageni waliotembelea onesho hilo 1,200,Wadhamini 40 na Mdhamini mkuu alikuwa Ethiopian Airlines
Mwaka huu Waoneshaji ni 100,Mawakala wa utalii na waandishi wa habari walioalikwa 43, Wageni wanaotegemewa kutembelea onesho 2,000,Wadhamini 41 na Wadhamini wakuu wamegawanyika katika makundi.
Kuna Platinum Category ambao ni Ethiopian Airlines – Mdhamini Mkuu (usafiri kwa ajili ya mawakala wa nje walioalikwa)
Pia kuna Gold Categoryambao ni Fast Jet Airline Limited, An’gata camps Ltd, FB cars Ltd, Gibbs Farm,Ramada Resort Dar es ssalaam, SAA North America, Seacliff Hotel, Sopa Lodges and Spicenet Tanzania .
Kwa upande mwingine kuna Silver category ambao ni Hifadhi za Taifa, Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, Antelope Tours and Safaris, Azam Marine, Congema Tours and safaris Ltd, Fernandes Tours & safaris, Melau Tours & Safaris Ltd, Precision Air Services, Shirika la ndege la Qatar, Rwandair, Shirika la ndege la Afrika Kusini , Shidolya Tours & Safaris Ltd, Sun Tours &travel Lts and Shirika la ndege la Uturuki.
Wengine ni BougainvillaSafari Lodge, Ledgar Plaza Hotel, Cenizaro Hotels & Resorts, Emerald Collection Zanzibar, Essque zalu Zanzibar, Holiday Inn Dar es salaam, Kudu Lodge, Kunduchi bBeach Hotel, Manyara Wildlife safari Camp, Maru Maru Hotel, Mberesero Lodges & Tented Camps, Melia Zanzibar, Neptunes Hotels, New Africa Hotel, Ocean Paradise Resort & Spa, PlanHotel Hospitality Group, Protea Hotel Courtyard, Seacliff Court Hotel & Luxury Apartments, Seacliff Resort & Spa Zanzibar, Serena Hotel, Southern Sun Dar es salaam, White Sands Hotel.
Black tomato, Boogle Woogle, Cultural Art Center,Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira.
Kwa upande mwingine kutakuwa na kitengo cha Hosted Buyers Programme ambapo Programme Maalum ya kuwatembeza mawakala wa Utalii katika maeneo Wageni hao watatembelea Zanzibar , Lake Manyara na Ngorogoro.Lengo ni kuona, kujifunza kuhusu utalii wa Tanzania, na kuonja (kuexperience ) ukarimu wetu.
Pia kutakuwa na kitengo cha Cultural Village ambalo ni Eneo lililotengwa kwa ajili ya maonesho ambapo wajasirimali wadogo wataweza kuonesha bidhaa na huduma zao.
Baadhi ya bidhaa hizo ni kama Tinga Tinga, Wachongaji vinyago, watengenezaji wa Sanaa mbalimbali, wanamitindo, vikundi vya burudani muziki wa bendi na burudani (Utalii Band) na Kikundi cha utamaduni kutoka Chuo cha Tumaini , Arusha .Pia kutakuwa na Nyama Choma (wageni wataweza kupata vyakula vya kitanzania )
Kwa ujumla TTB inawataka watanzania watembelee onesho hilo kutokana na ukweli kwamba onesho la S!TE ni fursa ya kuhamasisha utalii wa ndani,Watoa huduma mbalimbali za kitalii watakuwepo, wataweza kutumia fursa hiyo kutoa maelezo kuhusu huduma zao na kuwahamasisha watanzania kutembelea maeneo ya kitalii (vikundi mbalimbali vitawea kuhamasika –wanafunzi, wafanyakazi nk)
Dk. Magufuli asema iwapo atapata ridhaa yakuiongoza nchi atahakikisha anatoa mikopo kwa wasomi wanao maliza elimu ya juu nchini. https://youtu.be/bjV9jNZsh9Q
Tanzania yapata mkopo wa zaidi ya shilingi bilioni 240 kutoka serikali ya Poland kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda cha matrekta. https://youtu.be/W70x_FxENZo
Kampuni ya bima ya insuarance TANRI yasema huduma za bima ni muhimu kwa mtanzania sababu zinatoa kinga dhidi ya majanga mbalimbali. https://youtu.be/NAm0yAbsdJE
Timu ya Azam Fc yasema swala la kuzalilishwa kwa mshambuliaji wa John Bocco na mlinzi wa Mbeya city Juma Nyoso wanaliacha mikononi mwa TFF. https://youtu.be/JsHwxJOMS3M
Taasisi ya taifa ya utafiti wa magonjwa ya binadamu yatoa tahadhari kuhusu uwezekano mkubwa wa kutokea mlipuko wa homa ya bonde la ufa. https://youtu.be/3JxqAVSOb5o
Mwili wa marehemu mama Celine Kombani waagwa leo huku makamu wa rais akiongoza maombolezo hayo katika viwanja vya karimjee. https://youtu.be/zHGeLbZA6Jo
Mkutano wa mgombea urais Edward Lowassa wavunjika mkoani Tanga baada ya umati mkubwa wa watu kujitokeza na kuzimia kwa wingi. https://youtu.be/7tdAhq_BxY0
Dk John Pombe Magufuli ahaidi mfumo wa utoaji huduma za afya kwa watanzania ikiwemo kuboresha upatikanaji wa dawa. https://youtu.be/IhsjD9GeFHE
Bodi ya utalii Tanzania yatangaza kua maonesho ya kimataifa ya sekta ya utalii yatafanyika kuanzia oktoba 1-3 mlimani city. https://youtu.be/r0i-XZgYY5w
Jumla ya wachezaji 24 wanaounda kikosi cha timu ya taifa stars kitakachocheza dhidi ya Malawi chatangazwa rasmi.https://youtu.be/ryM00jNJhZA
Kundi la mashabiki wanaosadikiwa kua klabu ya Nice ya ligi kuu Ufaransa walishambulia gari la rais wa PSG kwa mawe.https://youtu.be/D3I_lBsseaA
Mgombea uraisi wa CCM Dr.Magufuli amtaka mwekezaji wa mashine za kusagia mahindi Iringa kuhakikisha zinafanya kazi la sivyo atazirudisha. https://youtu.be/33w2SRw5_NA
Ugonjwa wa Kipindu pindu waendelea kutishia maisha katika maeneo mbali mbali hapa nchini baada wakazi 11 kulazwa mkoani Singida. https://youtu.be/EEla58ZIofQ
Uhalifu dhidi ya makanisa mkoani Kagera waendelea kushika kasi baada ya makanisa matatu kuvunjwa na thamani zake kuchomwa moto. https://youtu.be/9sKnCWfDYJs
Umoja wa katiba ya wananchi mkoani Tabora walitaka jeshi la polisi nchini kutofungamana na chama chochote ili kutunza amani kuelekea uchaguzi mkuu. https://youtu.be/i2MyvoicC_w
Mlipuko wa Kipindu pindu wazua tharuki na kutishia maisha ya wakazi wa musoma baada ya mtu mmoja kufariki huku wengine 60 wakilazwa. https://youtu.be/wktGWSoJ1Tk
President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete meets the United Nations Secretary General’s Special Advocate for Inclusive Finance for Development (or as it's more simply known, UNSGSA) Netherlands Queen Maxima at the UN Headquarters in New York this afternoon (photo by Freddy Maro)




0 |
|
0 |
|
THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: ikulucommpress@googlemail.com
Website : www.ikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425 |
|
PRESIDENT’S OFFICE,
STATE HOUSE,
1 BARACK OBAMA ROAD,
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
|
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Tanzania yatangaza hatua tano za kuendeleza haki za wanawake na usawa wa kijinsia
· Yaahidi kufanya mabadiliko makubwa ya kisera na kisheria
· Miongoni mwa Sheria zitakazohusika ni Sheria ya Ndoa na Sheria ya Urithi
· Ni katika utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu - SDG’s
Tanzania imeahidi kuchukua hatua tano muhimu za kutetetea na kuendelea haki za wanawake kati ya sasa na mwaka 2030, ikiwa ni pamoja na kufanya mabadiliko makubwa ya kufuta sheria zinazokandamiza wanawake na kutunga sheria za kuleta usawa wa kijinsia, yote katika utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG) mapya kwa manufaa ya wanawake wa Tanzania.
Miongoni mwa hatua hizo itakuwa ni pamoja na kufuta ama kufanya mabadiliko ambayo yanaendeleza vitendo vya kiutamaduni ambavyo kwavyo vinaendeleza ubaguzi wa wanawake kama vile Sheria ya Ndoa, Sheria ya Urithi na kutunga Sheria ya Kukomesha Ukatili dhidi ya wanawake.
Msimamo huo wa Tanzania umeelezwa Jumapili, Septemba 27, 2015 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete alipozungumza katika Mkutano wa Usawa wa Jinsia na Uwezeshaji wa Akinamama: Dhamira ya Kuchukua Hatua uliohudhuriwa na wakuu wa nchi mbali mbali duniani kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa (UN) mjini New York, Marekani.
Rais Kikwete ameuambia mkutano huo ulioitishwa kwa pamoja na Jamhuri ya Watu wa China, Denmark, Mexico na Kenya kuwa hatua ya pili ambayo Tanzania inakusudia kuchukua ni kuridhia makubaliano yote ya kimataifa kuhusu haki za akinamama hasa Makubaliano ya Kimataifa Juu ya Kukomesha Aina Zote za Ubaguzi Dhidi ya Wanawake – Convention on the Elimination of All Forms of Discrimination Against Women (CEDAW).
Hatua nyingine ambazo Rais Kikwete amesema kuwa Tanzania itachukua katika miaka 15 ijayo ili kuhakikisha usawa wa kijinsia nchini ni zifuatazo:
· Kuendeleza na kuunga mkono upatikanaji wa raslimali fedha zinazolenga kuongeza usawa wa kijinsia kwa mujibu wa Ajenda ya Kugharimia Maendeleo ya Addis Ababa, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha zinatolewa pesa za kutekeleza mipango ya kitaifa na ya Serikali za mitaa za kukomesha ukatili dhidi ya wanawake.
· Kuhakikisha utekelezaji wa uwakilishi wa uongozi wa asilimia 50-50 kati ya wanawake na wanaume katika nafasi zote za maamuzi kwenye ngazi zote.
· Kupatikana na kutumiwa kwa data na habari za ukweli katika utunzi wa sera na utoaji maamuzi ya kukomesha ubaguzi wa kijinsia.
· Kutunga na utekelezaji mfumo wa uwajibikaji na ufuatiliaji wa haki za kijinsia na haki za akinamama zilizokubaliwa kitaifa na kwenye ngazi ya Serikali za mitaa.
Rais Kikwete pia amewaambia wajumbe wa mkutano huo kuhusu hatua za kisera na kisheria ambazo zimechukuliwa na Tanzania katika miaka ya karibuni kujenga usawa wa kijinsia, ikiwa ni pamoja na Sheria ya Ardhi ya mwaka 1999 na marekebisho yake ya mwaka 2004 ambayo yanawapa akinamama nafasi na haki ya kupata, kushikilia, kutumia na kumiliki ardhi.
Hatua nyingine ni kuwapa wanawake nafasi za maamuzi na uongozi katika nyanja za kisiasa na maisha ya umma. Katika kutekeleza hilo, idadi ya wabunge wanawake imeongezeka kutoka asilimia 21.5 ya wabunge wote mwaka 2005 hadi kufikia asilimia 34.5 mwaka huu, mawaziri wanawake wameongezeka kutoka sita mwaka 2005 hadi kufikia 26 mwaka huu na idadi ya majaji wanawake imeongezeka kutoka wanane mwaka 2005 hadi kufikia 41 mwaka huu.
Rais Kikwete amesema kuwa hatua nyingine zilizochukuliwa na Serikali ni kupunguza vifo vya wanawake wakati uzazi, kutunga Sheria dhidi ya ukatili wa kijinsia na ukatili dhidi ya wanawake na watoto; kuanzishwa kwa uandaaji wa Bajeti inayotilia maanani mahitaji ya wanawake na kuongeza uwezekaji wa kiuchumi wa akinamama kupitia kuanzishwa kwa Benki ya Wanawake Tanzania (TWB) yenye kulenga kutoa mikopo ya masharti nafuu kwa akinamama wafanyao biashara ndogo ndogo na za kati.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
28 Septemba, 2015
0 |
|
0 |
|
Na: Hassan Hamad, OMKR
Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama Cha Wananchi CUF Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, ametembelea kisima kinachosadikiwa kuwa na mafuta katika eneo la Tundauwa, na kusema kuwa mafuta ya Zanzibar yatachimbwa katika kipindi kifupi kijacho.
Amesema kwa miaka mingi Zanzibar imeshindwa kuchimba mafuta yake kutokana na kutokuwepo mikakati imara, na kuahidi kuwa iwapo atachaguliwa kuwa Rais wa Zanzibar atahakikisha kuwa suala hilo linawekewa mikakati imara ya uchimbaji, ili wananchi waweze kunufaika na rasilimali hiyo muhimu kwa maendeleo ya taifa.
Kwa mujibu wa kumbukumbu zilizopatikana katika eneo hilo, kisima hicho chenye urefu wa zaidi ya futi 12 elfu na mia saba, kilijengwa miaka 53 iliyopita na kuonesha dalili za kuwepo mafuta.
Wakati huo huo Maalim Seif ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, ametembelea Jumuiya ya maendeleo ya wanawake Tundauwa, na kutoa wito kwa wananchi wa kijiji hicho kujiunga na jumuiya hiyo ili kupata mafanikio zaidi.
Amesema jumuiya hiyo inayojihusisha na masuala mbali mbali yakiwemo uhifadhi wa mazingira na kilimo, imekuwa mfano mzuri wa kuigwa kutokana na mafanikio inayoyapata tokea kuanzishwa kwake.
“Jumuiya hii inafanya kazi nzuri ya kupigiwa mfano, hivyo natoa wito kwa wananchi wa vijiji hivi kujiunga kwa wingi ili kuleta mafanikio zaidi” amesema Maalim Seif.
Mapema akisoma risala ya Jumuiya hiyo, bibi Raya Abdallah Rashid amesema lengo la kuanzishwa kwa jumuiya hiyo ni kupambana na umaskini, maradhi pamoja na uhifadhi wa mazingira.
Amesema Jumuiya hiyo pia imekuwa ikiielimisha jamii juu ya athari za mabadiliko ya tabia nchi na dawa za kulevya.
Amesema Jumuiya hiyo iliyoanzishwa mwaka 2007 imepata mafanikio makubwa yakiwemo kutambuliwa kama jumuiya rasmi, kupanda mikoko ekari mbili kwa ajili ya uhifadhi wa mazingira, ufugaji wa nyuki na kilimo cha mboga mboga.
Hata hivyo bi Raya amesema bado wanakabiliwa na changamoto ikiwa ni pamoja na ukosefu wa jengo la ofisi, na kulazimika kuanzisha ujenzi ambapo zaidi ya shilingi milioni saba na nusu tayari zimetumika kwa ajili ya ujenzi huo, na kuomba kupatiwa misaada zaidi ili wamewe ukamilisha ujenzi wao.
Katika hatua nyengine Maalim Seif ambaye ni Katibu Mkuu wa CUF, amefungua tawi jipya la CUF Tandani shehiya ya Kilindi lililokuwa chini ya Chama cha ADC.
Amesema Tawi hilo limebadilishwa kutoka ADC na kuwa tawi la CUF baada ya wanachama 25 wa ADC kuamua kujiunga na CUF na kuongeza idadi ya wanachama wa tawi hilo kufikia 103.
Tawi jengine la ADC la eneo la meli tisa Wingwi, pia lilibadilishwa kuwa tawi la CUF baada ya wanachama wake kukihama chama hicho.
Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CUF Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akipandisha bendera katika tawi la CUF Tandani shehiya ya Kilindi lililokuwa chini ya Chama cha ADC, kuashiria ufunguzi rasmi wa tawi hilo.
Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CUF Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akizungumza na wanachama wa wanachama wa Jumuiya ya maendeleo ya wanawake Tundauwa. (Hawapo pichani).
Picha na Salmin Said, OMKR
0 |
|
0 |
|
Baadhi ya Wasanii nyota wa Filamu hapa nchini wakiongozwa na Jacob Steven a.k.a JB wakiwa wamenyanyua juu mikono yao kwa pamoja ni Ushindi sambamba na Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli (wa tatu kushoto),kuonesha kuwa wasanii hao wanamuunga mkono Dkt Magufuli katika mbio zake za kuusaka Urais kwa kutembea nchi nzima kutumia Bajaji zao tano,ambapo Bajaj mojawapo itakuwa na kazi ya kukusanya kadi za wale wanaomua kurudi/kujiunga na chama cha CCM.
Magufulika staili kama kawa,hata baadhi ya wasanii nyota wa Bongo Movie hapa nchini wakiongozwa na Nnape Nnauye (pili shoto) walikumbwa na zoezi hilo jioni ya leo mbele ya wakazi wa Iringa na vitongoji vyake waliokuwa wamefurika kwenye mkutano wa kampeni ndani ya uwanja wa Samora,zoezi hilo kwa sasa limeanza kujizolea umaarufu mkubwa hapa nchini,la kupiga push up kama ionekanavyo pichani.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi (CCM),Dkt John Pombe Magufuli akihutubia umati wa wananchi wa Iringa na vitongoji vyake kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni uliofanyika jioni ya leo septemba 28 ndani ya uwanja wa Samora mkoani Iringa.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi (CCM),Dkt John Pombe Magufuli akihutubia umati wa wananchi wa Iringa na vitongoji vyake kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni uliofanyika jioni ya leo septemba 28 ndani ya uwanja wa Samora mkoani Iringa.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye akiwaeleza wananchi sababu zilizosababisha CCM kutomteua Lowasa kuwa mgombea urais kupitia CCM hasa kutokana na hasa kile kilichoelezwa kuwa na kadhia ya ufisadi ya rushwa,mbapo pia Nape amewaomba Wananchi kumuombea afya Mgombea huyo wa Urais kupitia Chadema, ili aje ashuhudie CCM ikishinda nafasi ya Urais.
Wananchi wa Iringa na vitongoji vyake wakishangilia wakati Dkt Magufuli alipokuwa akiwaomba wampigie kura ya ndio itakapofika Oktoba 25,mwaka huu (ambapo uchaguzi mkuu unatarajiwa kufanyika )ili aweze kuibuka mshindi na kuchaguliwa kuwa Rais wa awamu ya tano
Dkt Magufuli akimkabidhi Ilani ya Uchaguzi ya CCM Mgombea ubunge Jimbo la Iringa mjini, Ndugu Frederick Mwakalebela wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika katika uwanja samora mjini Iringa.
Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli akimnadi mgombea Ubunge wa jimbo la Kilolo Ndugu Venance Mwamoto,kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika Ilula,mkoani Iringa.
Baadhi ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali wakiwa kazini kwenye mkutano wa Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli,jioni ya leo kwenye uwanja wa Samora mkoani Iringa.
PICHA NA MICHUZI JR-IRINGA
PICHA ZAIDI INGIA HAPA
PICHA NA MICHUZI JR-IRINGA
PICHA ZAIDI INGIA HAPA
0 |
|
0 |
|
1. Mwezi Machi, 2015, Bunge la 10 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Lilipitisha Sheria ya Kuratibu Ajira za Wageni Nchini Na.1 ya Mwaka 2015 (The Non - Citizens (Employment Regulation) Act). Sheria hii ilisainiwa na Mheshimiwa Rais mwezi Mei, 2015 na imetangazwa kuanza kutumika rasmi tangu tarehe 15/09/2015 kupitia Gazeti la Serikali Na. 406 la mwaka 2015.
2. Sheria hii inaanzisha Mamlaka moja ya utoaji wa vibali vya ajira kwa wageni
na Mamlaka hiyo ni Kamishna wa Kazi.
3. Kwa kuzingatia matakwa ya Sheria hii, Wawekezaji au Waajiri wanaokusudia kuajiri wageni nchini wanapaswa kuwasilisha maombi kwa Kamishna wa Kazi na hati maalum ya kibali cha Ajira itatolewa kwa mgeni husika.
4. Mgeni atakayepatiwa kibali cha ajira atatakiwa kuwa na kibali cha Ukaazi ambacho kinatolewa na Idara ya Uhamiaji.
5. Ada ya Vibali vya Ajira italipwa kwa kuzingati aina ya daraja la kibali husika kama ifuatavyo;
i. Daraja A kwa Wawekezaji na waliojiajiri wenyewe-USD 1,000
ii. Daraja B kwa Taaluma maalum zilizoainishwa chini ya Sheria-USD 500
iii. Daraja C kwa Taaluma nyinginezo-USD 1,000
iv. Daraja D kwa walioajiriwa na Mashirika ya Dini na ya hisani-USD 500
v. Daraja E kwa ajili ya Wakimbizi- Bure.
Malipo au Ada ya huduma hii italipwa kupitia Akaunti inayotajwa hapa chini;
Name: Permanent Secretary, Ministry of Labour and Employment
A/C No: 0250211745400
Bank: CRDB
Aidha ,Mfumo huu mpya wa utoaji wa vibali vya Ajira kwa wageni utaanza rasmi tarehe 1/10/2015 na maombi yawasilishwe Ofisi ya Kamishna wa Kazi,makao Makuu ya Wizara ya Kazi na Ajira,jengo la NSSF-Mwl.Nyerere Tower,Na 42,iliyopo Barabara ya Bibi Titi Dar-es-salaam.
6. Wizara inapenda kutoa Rai kwa wadau wote kutoa ushirikiano ili kutekeleza matakwa ya Sheria kwa ufanisi wa maendeleo ya nchi yetu.
Imetolewa
Ridhiwani M. wema
Msemaji.
Wizara ya Kazi na Ajira.
28/09/2015
SIKU YA MOYO, WANANCHI KUPIMWA SHINIKIZO LA DAMU BURE.
KATIKA kuazimisha siku ya afya ya Moyo Duniani Hospitali ya Taifa Muhimbili-MNH- leo itatoa huduma ya upimaji wa shinikizo la damu bure pamoja na kuwashauri wale watakaopatikana na tatizo hilo.
Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu siku ya afya ya moyo Duniani ambayo huazimishwa Septemba 29 kila mwaka , Daktari Bingwa wa magonjwa ya Moyo Tulizo Shemu kutoka Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kitwete amesema magonjwa ya moyo yanachangia asilimia 31 ya vifo vyote vinavyosababisha takribani watu MIlioni 17. 3 kufa kila mwaka .
Inasadikika itakapofika mwaka 2030 zaidi ya watu Milioni 25 watakuwa wanapoteza maisha kutokana na maradhi hayo hasa katika nchi zilizo na uchumi wa chini na kati.
Siku ya afya ya moyo Duniani hutoa fursa kwa watu wote Duniani kuazimisha kwa vitendo katika kujilinda na janga la magonjwa ya moyo na mishipa ya damu ambayo yanachangia vifo vingi .
Dokta Shem ametaja baadhi ya visababishi vinavyochangia magonjwa ya moyo kuwa ni matumizi ya tumbaku, chumvi , pombe, vyakula vyenye mafuta, kutofanya mazoezi , unene uliokithiri , kutotibu ugonjwa wa kisukari na kuwa na mafuta mengi kwenye damu.
Kauli mbiu ya mwaka huu ni kuweka mazingira mazuri ya afya bora ya moyo katika sehemu zetu tunazofanyia kazi kwa kuhakikisha kila mtu anatoa mchango katika kujenga afya bora ya moyo ili kupunguza visababishi vinavyochochea magonjwa hayo.
Daktari Bingwa wa magonwa ya moyo, Dk Tulizo Shemu (kulia) wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) akizungumza na waandishi wa habari katika taasisi hiyo kuhusu siku ya afya ya moyo duniani ambayo inafanyika Septemba 29, kila mwaka.
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo nchini, Dk Tatizo Wane (kulia) wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) akizungumza na waandishi wa habari katika taasisi hiyo kuhusu siku ya afya ya moyo duniani ambayo inafanyika Septemba 29, kila mwaka. Kesho watu watapimwa bure shinikizo la damu na watakaopatikana na tatizo hilo watapewa ushauri wa bure. Pia siku ya kesho (Septemba 29, 2015) Taasisi hiyo itagawa vepeperushi, majarida na CD zinazozungumzia magonjwa ya moyo.
Baadhi ya waandishi wa habari.
KUSOMA ZAIDI links goes to sheriayakub.blogspot.com
Na Bashir Yakub.
Tulipoandika namna bora na taratibu maalum za kufuata unapotaka kununua ardhi tulisema pia kuwa taratibu za ununuzi wa ardhi huwa zinatofautiana kutegemea na mazingira ya kila ardhi.
Tukasema unaponunua ardhi kwa msimamizi wa mirathi ni tofauti na unaponunua kwa mmiliki mwenyewe. Unaponunua ardhi ya familia ni tofauti na unaponunua isiyo ya familia.
Vilevile unaponunua ardhi ya kijiji ni tofauti na unaponunua ardhi isiyo ya kijiji. Taratibu hutofautiana na hasa tofauti ipo katika nyaraka ambazo zinatakiwa kuambatanishwa ikiwa kama ithibati ya ununuzi. Hata uandishi wa mkataba wa manunuzi pia nao huwa na tofauti katika hili.
1.ARDHI YA KIJIJI KWA UWEKEZAJI.
Wako watu wamekuwa wakinunua ardhi hasa huko vijijini lakini baadae wamekuwa wakijikuta katika migogoro mikubwa na wenyeji. Mwamko wa kununua maeneo kama bagamoyo, kisarawe, huko chanika dondwe na maeneo mengine umekuwa mkubwa sana.
Hata hivyo mwamko unavyoongezeka ndivyo na migogoro inavyoongezeka. Kubwa katika migogoro hii ni hatua ya wanunuzi kutokufuata utaratibu wa ununuzi aidha kwa kujua, kutokujua au kupotoshwa.
Wakati mwingine ni uelewa mdogo miongoni mwa wenyeji lakini zaidi ni hili la kutofuata utaratibu. Mara zote huwa tunasema ni bora zaidi mgogoro unapotokea halafu ukukute ulifuata taratibu wakati wa manunuzi. Bila shaka hautakuwa na athari kubwa kwako lakini ni mbaya zaidi ukitokea halafu ukukute kuna taratibu hukufuata kwa bahati mbaya au bila kujua. Unakuwa katika hatari ya kupoteza. Unapokwenda kununua ardhi ya kijiji kwasababu yoyote ile hasa uwekezaji upo utaratibu maalum wa kufuata nitakaoeleza.
2. ARDHI YA KIJIJI NI NINI.
Ardhi ya kijiji ni ile ardhi iliyopo katika mipaka ya kijiji fulani ilyoainishwa na mamlaka za wilaya husika huku ikiwa na hati ya usajili wa kijiji. Ardhi hii hulindwa kwa taratibu za kimila za eneo husika ikiwa ni pamoja na sheria namba 4 ya 1999.
3. UTARATIBU WA KUNUNUA ARDHI YA KIJIJI KISHERIA.
( 1 ) Maombi maalum huandaliwa na kuwasilishwa kwa mtendaji wa kijiji ambaye hupatikana katika kila kijiji.
( 2 ) Maombi huandaliwa katika fomu maalum ambazo hupatikana katika kila ofisi za kijiji. Si maombi ambayo huandaliwa kama barua za kawaida za maombi.
( 3 ) Ikiwa mwombaji ni mtu mmoja basi atasaini sehemu maalum na ikiwa ni maombi kwa niaba ya famliia basi watu wawili kutoka ile familia watasaini na ikiwa ni ardhi kwa ajili ya kikundi pia wawakilishi wasiopungua wawili kutoka kile kikundi watasaini kwa niaba ya wengine.
( 4 ) Kama mwombaji ni chama cha ushirika au kampuni basi inatakiwa kuwepo wadhamini wawili kwa ajili ya shirika au kampuni hiyo. Wanaweza kuwa zaidi ya wawili lakini wasipungue.
( 5 ) Kama anayeomba ardhi si mwenyeji wa eneo husika basi atatakiwa kuwa na wadhamini wasiopungua watano ambao ni wenyeji wa eneo hilo. Sharti ni kuwa kati ya hao wadhamini wasiwepo ndugu wa mwombaji.
( 6 ) Mwombaji atatakiwa kuambatanisha katika maombi yake tamko linaloonesha ardhi nyingine anayoimiliki Tanzania nje na hiyo anayoomba.
( 7 ) Ikiwa ardhi inaombwa kwa ajili ya makazi basi mwombaji atatakiwa kuambatanisha tamko linaloonesha kuwa ataanza ujenzi wa makazi hayo ndani ya miezi mitatu tangu siku ya kuidhinishiwa ardhi.
( 8 ) Ikiwa mauzo ni heka 50 au kuendelea ni lazima yaidhinishwe na mkutano mkuu wa kijiji.
( 9 ) Baada ya kukamilisha taratibu hizo halmashauri ya kijiji itakaa vikao na ndani ya siku tisini itatakiwa kutoa majibu.
Kamwe usikubali kuuziwa ardhi ya kijiji na viongozi wa kijiji bila kufuata utaratibu huu. Hii hasa ni kwa wawekezaji wanaochukua maeneo makubwa kwa shughuli za kiuchumi.
MWANDISHI WA MAKALA HAYA NI MWANASHERIA NA MSHAURI WA SHERIA KUPITIA GAZETI LA SERIKALI LA HABARI LEO KILA JUMANNE , GAZETI JAMHURI KILA JUMANNE NA GAZETI NIPASHE KILA JUMATANO. 0784482959, 0714047241 bashiryakub@ymail.com
0 |
|
0 |
|
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Taarifa zaidi kuhusu Mahujaji kutoka Tanzania waliofariki na kujeruhiwa huko Saudi Arabia.
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kupitia Ubalozi wake mjini Riyadh, Saudi Arabia imepokea taarifa kuwa hadi kufikia tarehe 27 Septemba, 2015 watu waliopoteza maisha kufuatia tukio la mkanyagano (stampede) wa Mahujaji waliokuwa wakielekea Jamarat kutupa vijiwe huko Mina nje kidogo ya mji wa Makkah, lililotokea siku ya Alhamisi tarehe 24 Septemba, 2015 wameongezeka na kufikia 769 na majeruhi 934.
Aidha, Wizara kupitia Ubalozi huo inaendelea kufuatilia hatma ya Mahujaji wa Tanzania waliopotea katika tukio hilo la ajali ambapo hadi sasa Mahujaji wa Tanzania wapatao 50 bado hawajaonekana. Vikundi wanavyotoka Mahujaji hao na idadi yao ni kama ifuatavyo:-
1. Ahlu Daawa-Mahujaji 30;
2. Khidma Islamiya-Mahujaji 16; na
3. TCDO-Mahujaji 4
Vile vile juhudi za Ubalozi kwa kushirikiana na Tanzania Hajj Mission na viongozi wa vikundi vilivyopoteza Mahujaji wao zimefanikiwa kuutambua mwili wa hujaji mmoja aliyefariki dunia anayejulikana kwa jina la Shafi Khamis Ali kutoka kikundi cha Ahlu Daawa. Kutambuliwa kwa mwili wa hujaji huyo kunafanya idadi ya Mahujaji wa Tanzania waliofariki dunia katika ajali hiyo kufikia watano (5).
Pia, Wizara kupitia Ubalozi wake imepokea taarifa ya kupatikana kwa hujaji mwingine anayeitwa Nasra Abdullah akiwa hai naye kutoka kikundi hicho cha Ahlu Daawa.
Kuhusu majeruhi, taarifa kutoka Ubalozini zinaeleza kuwa, hujaji mmoja aliyejulikana kwa jina la Mahjabin Taslim Khan alipata majeraha yaliyopelekea kukatwa mguu na kwa sasa anaendelea kupata matibabu huku hali yake ikiendelea vizuri.
Ubalozi unaendelea na juhudi za kuwatafuta Mahujaji wengine wa Tanzania ambao bado hawajaonekana kwa ajili ya kubaini wale waliofariki au majeruhi wanaoendelea kupatiwa matibabu.
Mahujaji wengine wa Tanzania wapo salama ambapo tarehe 26 Septemba, 2015 walimaliza ibada ya hija na tarehe 28 Septemba, 2015 wameanza safari ya kurejea nyumbani.
Wizara inaendelea kuwaomba Wananchi kuwa watulivu katika kipindi hiki kigumu wakati Serikali ikiendelea kufuatilia.
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali kwa Umma,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,
Dar es Salaam
28 Septemba, 2015
Mratibu wa Kampeni upande wa Vijana CCM kwa Mkoa wa Dar es Salaam na Vyuo Vikuu Bw. Daniel Zenda akizungumza na Zaidi ya Vijana 500 kutoka Jimbo la Mbagala wakati wa uzinduzi wa MAGUFULI Club jijini Dar es Salaam jana. MAGUFULI Club imeanzishwa kama jukwaa la kuwakutanisha vijana nchini kote wanaomuunga mkono mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi Dkt. John Pombe Magufuli.
Mratibu wa MAGUFULI Club wilaya ya Temeke Bw. Peter Dafi akizungumza na vijana kutoka Jimbo la Mbagala wakati wa uzinduzi wa MAGUFULI Club jijini Dar es Salaam jana. MAGUFULI Club imeanzishwa kama jukwaa la kuwakutanisha vijana nchini kote wanaomuunga mkono mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi Dkt. John Pombe Magufuli.
Baadhi wa vijana wakifuatilia uzinduzi wa MAGUFULI Club katika Jimbo la Mbagala jana jijinI Dar es Salaam.
Wanachama wa MAGUFULI Club wakifurahia wakati uzinduzi wa Club hiyo katika Jimbo la Mbagala jana jijini Dar es Salaam.
Picha na: Frank Shija
93.7 EFM yajinyakulia ushindi baada ya kuwafunga kibaha veterans mabao mawili kwa moja, katika mchezo uliochezwa mwishoni mwa wiki katika uwanja wa Tamco kibaha, Mechi hiyo ni baadhi ya mechi zinazoendelea baina ya EFM na timu mbalimbali za wasikilizaji wake, Kupitia kampeni ya Muziki mnene bar kwa bar .
Burudani haikuishia hapo, baada ya mechi hiyo shangwe ziliendelea ndani ya kibaha kontena. Ilikuwa ni bandika bandua ya ngoma kali kutoka kwa Rdj’s wa 93.7 EFM na shamra shamra kutoka kwa timu nzima ya EFM na wakazi wa kibaha.
0 |
|
0 |
|
NA JAMIIMOJABLOG)
WATU wengi wanasumbuliwa na tatizo hili ambalo huwafanya kuwa na uoga na aibu wa kuelezea na kushindwa hata kwenda hospital kupata tiba
JE, UNAJUA BAWASIRI/HEMORRHOIDS NI NINI????!!
~Ni ugonjwa unaotokana na kuathirika kwa mishipa ya damu ya ndani na Inje ya sehemu ya haja kubwa na wakati mwingine mishipa hiyo huweza kupasuka/kuteleza na kuvuja damu kwenye njia ya haja kubwa na kasababisha kutoka kinyama au uvimbe.
~ugonjwa huu wa bawasiri kwa lugha ya kitaalamu tunauita HEMORRHOIDS ilhali kwa lugha ya kingereza unafahamika kama piles
~tatizo hili huwaathiri watu wote ila zaidi huwaathiri watu wazima kuliko watoto na inakadiriwa kuwa karibu 50%ya watu wote wako katika hatari ya kupata tatizo hili katika umri wa miaka 30_50
AINA ZA BAWASIRI
~Kuna Aina mbili za bawasiri
(A) BAWASIRI YA NDANI
~Aina hii ya bawasiri hutokea ndani ya mfereji wa haja kubwa huwa haiambatani na maumivu na wengi huwa hawajitambui kuwa Wana tatizo hili
~Aina hii hutokana na kuvimba na kuharibika kwa mshipa wa artery za ndani ya mfereji wa haja kubwa
~Aina hii imegawanyika katika madaraja manne
(1)DARAJA LA KWANZA ~Hii ni bawasiri ambayo haitoki mahali pale panapohusika
(2)DARAJA LA PILI ~hii hutokea wakati wa haja na kurudi yenyewe ndani baada ya kujisaidia.
(3)DARAJA LA TATU :hii hutokea wakati wa haja kubwa na mtu kuweza kurudisha ndani yeye mwenywe.
(4)DARAJA LA NNE :hii ni bawasiri inayotoka na huwa ngumu kurudi
(B)BAWASIRI YA NNJE
~Aina hii ya bawasiri hutokea katika eneo la mwisho kabisa la mfereji wa haja kubwa na huambatana na maumivu makali na kuwashwa kwa ngozi katika eneo la tundu Hilo pia husababisha mishipa ya damu (vena) kupasuka na damu kuganda na kasababisha Aina ya bawasiri iitwayo THROMBOSED HEMORRHOIDS
CHANZO CHA TATIZO
~chanzo halisi cha ugonjwa huu hakijapatikana ila Kuna vitu ambavyo huwa chanzo cha kupata ugonjwa wa bawasiri ambayo ni ÷
👉KUFANYA MAPENZI KINYUME NA MAUMBILE
👉KUHARISHA KWA MUDA MREFU
👉TATIZO LA KUTOPATA CHOO
👉MATATIZO YA UMRI
👉KUKAA KITAKO KWA MUDA MREFU
👉UZITO KUPITA KIASI
👉MATUMIZI YA VYOO VYA KUKAA KWA MUDA MREFU
DALILI ZA BAWASIRI
👉Ngozi kuwasha katika eneo la tundu la haja kubwa
👉kupata maumivu makali wakati wa kujisaidia
👉kutokea uvimbe katika eneo la tundu la haja kubwa
👉kujitokeza kwa kinyama katika eneo la tundu Hilo
👉kinyesi kuwa na damu na kunuka harufu mbaya sana
MATIBABU NA JINSI YA KUEPUKA TATIZO LA BAWASIRI
~matibabu ya bawasiri hutegemea na Aina ya bawasiri pia tiba iliyozoeleka ni kukatwa kinyama na kuendelea na lishe ya chakula hata hvyo tiba hii si nzuri kwasababu huwa haitibu chanzo cha tatizo hivyo huwa rahisi kujirudia hivyo tiba nzuri ni kutumia dawa na anion chip kubandika mahali penye tatizo na kuondoa tatizo Hilo
~Pamoja na hayo bawasiri ni ugonjwa unaoweza kuepukika kwa kuzingatia
👉KULA MBOGAMBOGA ZA MAJANI, MATUNDA, NA NAFAKA ZISIZOKOBOLEWA
👉KUNYWA MAJI MENGI ANGALAU GRASS 6/12 Kwa siku
👉EPUKA KUKAA CHOONI KWA MUDA MREFU
MADHARA YA TATIZO LA BAWASIRI
👉kupata upungufu wa damu (anemia)
👉Kupata tatizo la kutokuweza kuhimil choo
👉hupunguza nguvu za kiume na kuondoa hamu ya tendo la ndoa kwa wanawake
👉kuathirika kisaikolojia
👉kukosa moral ya kufanya Kazi kutokana na maumivu makali
WASILIANA KWA 0717035770 AU 0753692612.
Bi Harusi mtarajiwa Ester Diana Nana (kushoto) akigonisha glasi na msimamizi wake, Hellen, wakati wa sherehe ya kuagwa (Send off) iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki.
Bi harusi mtarajiwa akiwa na mumewe mtarajiwa wakielekea kupata chakula cha usiku ukumbini hapo. Watarajiwa hao wanatarajia kufunga ndoa jumamosi ya wiki hii.
Wakati wa mlo wa usiku
Kipindi hiki hukujia kila JUMATATU, kujadili mambo mbalimbali na zaidi kuhusu UCHAGUZI MKUU WA TANZANIA 2015
Hiki ni kipindi kilichosikika Septemba 28, 2015
Kutoka Tanzania tuliungana na Liberatus Mwang'ombe. Mgombea ubunge jimbo la Mbarali kwa tiketi ya CHADEMA
Studioni alikuwepo Dj Luke Joe, na kwa njia ya simu tukaungana na wasikilizaji wengi ndani na nje ya Marekani
KARIBU


Hii ni ratiba ya mechi za Jumatano ya September 30