Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110170 articles
Browse latest View live

MARY NAGU UZINDUA KAMPENI ZA CCM ARUSHA

$
0
0


SAM_5821Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Sera Mahusiano na Uratibu Dkt.Mary Nagu akimnadi mgombea Ubunge pamoja na madiwa katika uzinduzi wa kampeni jimbo la Arusha mjini tarehe 5/9/2015 katika uwanja wa soko kuu jijini Arusha(Picha zote na Pamela Mollel wa jamiiblog Arusha)
SAM_5835Umati wa watu uliojitokeza katika uzinduzi wa kampeni za ccm jimbo la Arusha mjini katika ene la soko kuu jijini Arusha,ambapo rasmi walizindua kampeni za ubunge na udiwani
SAM_5823Mgombea ubunge jimbo la Arusha mjini kupitia chama cha mapinduzi ccm Philemon Mollel maarufu kwa jina naMonaban akimwaga sera zake katika uzinduzi huo ambapo alikiri kuleta mabadiliko makubwa ya kimaendeleo endapo ataibuka mshindi katika uchaguzi mkuu.
 

JK NA DKT. JOHN POMBE MAGUFULI WAUTEKA MJI WA MOROGORO KWA MKUTANO WA KIHISTORIA WA KAMPENI

$
0
0

 Sehemu ya gharika la wananchi  katika Uwanja wa Jamhuri Mjini Morogoro Jumapili kwa mkutano wa kampeni wa mgombea Urais kwa tiketi ya chama hicho tawala
 Sehemu ya gharika la wananchi  katika Uwanja wa Jamhuri Mjini Morogoro Jumapili kwa mkutano wa kampeni wa mgombea Urais kwa tiketi ya chama hicho tawala
 Sehemu ya gharika la wananchi  katika Uwanja wa Jamhuri Mjini Morogoro Jumapili kwa mkutano wa kampeni wa mgombea Urais kwa tiketi ya chama hicho tawala
 Sehemu ya gharika la wananchi likimpokea mgombea wa Urais kwa Tiketi ya CCM Dkt. John Pombe Magufuli  katika Uwanja wa Jamhuri Mjini Morogoro Jumapili kwa mkutano wa kampeni

 Rais Kikwete akimnadi mgombea wa Urais kwa Tiketi ya CCM Dkt. John Pombe Magufuli  katika Uwanja wa Jamhuri Mjini Morogoro Jumapili

 Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Dkt. Jakaya Kikwete na Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakiwapungia mikono wananchi huku wakiwa wameshika kofia zao. 
Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

FLAVIANA MATATA ATEULIWA KUWA BALOZI WA UTALII NEW YORK CITY NCHINI MAREKANI

$
0
0
 Katibu mkuu wizara ya maliasili na utalii Adelhelm Meru akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusiana na kumtambulisha Flaviana Matata  kuwa balozi wa utalii jimbo la New York City nchini Marekani.Kutoka kulia ni Flavianao Matata na kushoto Kaimu Mkurugenzi mwendeshaji Bodi ya Utalii TTB Devota Mdachi.
Katibu mkuu wizara ya maliasili na utalii Adelhelm Meru akimkabidhi cheti   cha kumtambua kuwa balozi wa utalii jimbo la New York City nchini Marekani Flaviana Matata  katikati ni Kaimu Mkurugenzi mwendeshaji Bodi ya Utalii TTB Devota Mdachi.

WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA AKUTANA NA BALOZI WA BURUNDI NA QATAR

$
0
0
 Waziri Mkuu Mizengo Pinda akisalimiana na Balozi wa Burundi hapa Nchini  Bwana Issa Ntambuka ambaye alifika ofisini kwa Waziri Mkuu leo jijini Dar es salaam kwa mazungumzo ya kikazi.
 Waziri mkuu Mizengo Pinda akimsikiliza kwa makini Balozi wa Burundi hapa nchini Bwana Issa Ntambuka ambaye alifaka ofisini kwa Waziri Mkuu leo Jijini Dar es salaam kwamazungumzo ya kikazi.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akutana na Balozi wa Qatar hapa Nchini Bwana Abdullah Jassim Al Maadadi ambaye alifika ofisini kwa Waziri Mkuu leo Jijini Dar es salaa kwa mazungumzo ya kikaza
Picha na Chris Mfinanga.

WAWEZESHAJI WA KITAIFA WA STADI ZA MAISHA KANDA YA ZIWA WAPIGWA MSASA

$
0
0
 Afisa Vijana Kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni, na Michezo Bw. Godfrey Massawe akizungumza na vijana (hawapo pichani) wakati wa Mafunzo ya Wawezeshaji wa Kitaifa wa Stadi za Maisha  kwa vijana wa Mikoa ya Kanda ya Ziwa leo Jijini Mwanza. Mafunzo haya yamehusisha vijana kutoka Mkoa wa Simiyu, Mara, Kagera, Shinyanga na Mwanza.
 Wawezeshaji wa Kitaifa wa masuala ya Stadi za Maisha kutoka Mikoa ya Kanda ya Ziwa wakisikiliza kwa makini mada iliyokua ikiendelea wakati wa Mafunzo ya Wawezeshaji wa Kitaifa leo Jijini Mwanza. Kulia ni Mtaalamu wa masuala ya Vijana Bw. Robert Semkiwa.
 Wawezeshaji wa Kitaifa wa masuala ya Stadi za Maisha kutoka Mikoa ya Kanda ya Ziwa wakijadiliana wakati wa mafunzo kwa vijana hao leo Jijini Mwanza.
Picha naGenofeva Matemu – Maelezo, Mwanza

HAKUNA CHAMA CHA SIASA KINACHOITWA TPP - MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA

SHERIA MPYA YA MTANDAO MWISHO CHUMBE..?

$
0
0
Logo ya Zanzibar Diaspora Association (ZADIA)
Na Mwandishi wetu swahilivilla Blog

Wanadiaspora wameelezea wasiwasi wao kuwa sheria mpya ya Makosa Ya Mtandao iliyoanza kufanya kazi tarehe mosi mwezi huu nchini Tanzania, huenda ikaishia kisiwa cha Chumbe kilichopo katikati ya Dar es salaam na Zanzibar,  imefahamika.

Hayo yamekuja kwenye kongamano maalum lililoandaliwa na Jumuiya Ya Wazanzibari Waishio nchini Marekani (ZADIA) kujadili Sheria Mpya ya Makosa Ya Mtandao na Athari zake Kisiasa.

Wageni rasmi katika kongamano hilo lililofanyika kwa njia ya simu walikua ni Mwandishi khabari Bi Salma Said, na Mwanadiplomasia mstaafu Bw. Muhammed Yussuf Mshamba. 

NEC YATOA ONYO KALI DHIDI YA UKIUKWAJI WA MAADILI KIPINDI HIKI CHA KAMPENI

$
0
0
 (i)           Kutozingatia muda wa kumaliza Mikutano ya Kampeni
Kuna baadhi ya Vyama ambavyo katika mikutano yao vimekiuka Kipengele hiki kwa kufanya mikutano zaidi ya saa 12.00 jioni.  Kuendelea kufanya Mkutano wa Kampeni zaidi ya muda huo ni ukiukwaji wa Kipengele cha 2.1 (c) cha Maadili ya Uchaguzi  wa Rais, Wabunge na Madiwani ya mwaka 2015 kinafafanua kuwa Mikutano yote ya Kampeni itafanyika kuanzia saa 2.00 asubuhi hadi saa 12.00 jioni.
(ii)        Kubandika mabango ya Kampeni, matangazo au Mchoro wowote kwenye maeneo yasiyoruhusiwa au bila idhini ya wahusika
Baadhi ya Vyama vimeanza kubandika mabango, michoro na picha za Wagombea wao katika majengo au vyombo vya usafiri vya watu binafsi au Taasisi mbalimbali bila idhini ya wamiliki husika.
Napenda kuwakumbusha kuwa, kwa mujibu wa Kipengele cha 2.2. (g) cha Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya mwaka 2015, hairuhusiwi kufanya hayo bila idhini ya wamiliki husika.
(iii)      Kuchafua, kubandua au kuharibu matangazo au picha za Kampeni za Vyama vingine
Tume imeanza kupokea malalamiko kutoka baadhi ya Vyama kuwa, mabango au picha za Kampeni za Vyama vyao yanabanduliwa au kuchafuliwa na wafuasi wa Vyama vingine.

JOTO LA ASUBUHI LA 93.7 EFM JUMANNE SEPTEMBER 08 - 2015

MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA KINONDONI WA CHAMA CHA ACT WAZALENDO, KARAMA MASUDI "KALAPINA" AZINDUA KAMPENI ZAKE

$
0
0
 Mgombea wa ubunge wa jimbo la Kinondoni kwa tiketi ya chama cha ACT Wazalendo Kalapina akikabidhi sera na ilani ya chama cha ACT Wazalendo kwa kiongozi wa chama hicho katika soko la Tandale.
Mgombea wa ubunge wa jimbo la Kinondoni kwa tiketi ya Chama cha ACT Wazalendo Kalapina akizungumza na wakazi wa tandale wakati wa kufungua Kampeni za chama chicho jijini Dar es Salaam.
Mgombea ubunge jimbo la kawe kupitia chama hicho, Janet Joel Akizungumza na wakazi wa tandale alipopata nafasi ya kuwasalimia wananchi wa mtaa huo.
Baadhi ya vijana wakimshangilia Kalapina baada ya kumaliza kuzungumza na kumwaga sera zake kwa wakazi wa tandale.

Na:Elisa Shunda,Dar
MGOMBEA ubunge jimbo la Kinondoni kupitia chama cha ACT wazalendo,  Karama Masudi “Kalapina” azindua kampeni zake katika eneo soko la Tandale baada ya kushinda kesi ya kuwekewa pingamizi na mgombea ubunge wa jimbo hilo kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Iddi Azzan.

Akizungumza na wakazi wa eneo hilo  mgombea huyo alisema kuwa baada ya kuwekewa pingamizi lisilokuwa na mantiki yoyote na mgombea mwenzake  hatimaye baada ya kushinda leo wameamua kufungua kampeni zao na watazunguka jimbo zima kueleza sera za chama chake  na mambo muhimu ambayo atayasimamia endapo wananchi wa jimbo la Kinondoni wakimpa ridhaa ya kuwaongoza.

Ndugu wananchi baada ya kushinda pingamizi lililowekwa na mgombea mwenzangu hatimeye nimeshinda, nipende kusema kuwa mkini kuchagua mbunge wenu nitahakikisha suala la madawa ya kulevya linaisha katika wilaya yetu kwani matumizi ya madawa ya kulevya yanaondoa nguvu kazi ya taifa kama nilivyoanzisha kipindi cha televisheni katika kuelimisha vijana wenzangu kuachana na matumizi ya madawa ya kulevya ndivyo nitakapoenda kuwasemea kule bungeni juu ya uingizwaji wa madawa ya kulevya nchini uwe mwisho ili kuwakomboa vijana wenzangu na dimbwi hili hatari” alisema Masudi.

Aidha mgombea huyo alizitaja sera zake muhimu atakazosimamia pindi akichaguliwa kuwa mwakilishi wao kuwa ni elimu bora, afya nzuri kwa wananchi wote na kuhakikisha katika jimbo la Kinondoni linakua na miundombinu mizuri ya kupitisha majitaka.

Endapo mkini chagua kuwa mbunge wenu nitahakikisha nasimamia jimbo letu katika suala la elimu mahitaji yote muhimu kama vitabu, madawati na kuwepo kwa maabara kwenye shule hizo, upande wa afya nitahakikisha dawa zinapatikana kwa wingi katika zahanati zetu pamoja na hospitali ya Mwananyamala na kuhakikisha wakinamama wajawazito hawalali wawili wawili kwenye kitanda kimoja au kulala chini na mwisho nitahakikisha miundombinu ya jimbo la Kinondoni inakuwa katika hali nzuri ili kujiepusha na magonjwa nyemelezi kama kipindupindu nitahakikisha  mifereji itakuwa katika hali nzuri na jimbo letu litabadilika liwe la mfano kama mji wa Manhattan” Alisema Masudi.

Aidha mgombea huyo alimaliza kwa kusema ni wakati wa mabadiliko kwa wakazi wa jimbo la Kinondoni kumchagua mwakilishi atakayeenda kuwasemea matatizo yao na siyo kupeleka watu wenye maslahi yao binafsi ambao wanaenda bungeni kwa ajili ya kuhakikisha biashara zao haramu zinapita kwa urahisi kutokana na wao kuitwa waheshimiwa, pamoja na mgombea huyo alisindikizwa kwenye mkutano huo na mgombea ubunge jimbo la Kawe,Janet Joel, mgombea ubunge jimbo la Tarime,Deo Meck pamoja na kuwaombea kura na kuwanadi wagombea udiwani kata ya Tandale, Makumbusho na Mwananyamala.

WANANCHI KUWENI MAKINI NA WANAOCHOCHEA CHUKI-BALOZI SEIF IDDI

$
0
0
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif AliIddi akisalimiana na Wananchi wa Kijiji cha Kwale Wilaya ya Micheweniwakati alipowasilikuzungumza nao.
 Balozi Seif akizungumza na Wananchi na Wana
CCM wa Kijiji cha Kwale Wilaya ya Micheweni akitekeleza ahadi aliyotoa
kwa Wazee Waasisi wa Kijiji hicho ya kufika kusalimiana nao.
 Baadhi ya Wananchi na wanaCCM wa Kijiji cha Kwale
wakifuatilia Hotuba ya Balozi Seif hayupo pichani alipofika Kjijini
hapo kusalimiana nao.

MAKAMU wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi
amewatahadharisha Wananchi kuwa makini na Watu wanaochochea chuki
miongoni mwa Jamii jambo ambalo  Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
kamwe haitakubali kuona amani ya Nchi inachezewa kizembe.

Alisema wapo watu waliochoka na amani iliyopo nchini kwa kuanza
kushabikia cheche za kujiandaa kuwashawishi Vijana wawe tayari kufanya
fujo mara tuu baada  ya zoezi la kupiga kura kwenya uchaguzi Mkuu wa
Mwezi Oktoba mwaka huu.

Balozi Seif Ali Iddi ametoa tahadhari hiyo wakati akizungumza na
Wananchi amoja na Wana  CCM wa Kijiji cha Kwale Wilaya ya Micheweni
Mkoa wa Kaskazini Pemba akitekeleza ahadi aliyowapa wazee wa Kijiji
hicho hivi karibuni ya kuwatembelea na kusalimiana nao.

MSAFARA WA JAMES MBATIA WAISIMAISHA VUNJO

$
0
0
Msululu wa magari ukimsindikiza mgombea huyo.
Msafara wa Pikipiki ukimsindikiza mgombea Ubunge katika jimbo la Vunjo kupitia chama cha NCCR-Mageuzi na UKAWA ,James Mbatia wakati wa kwenda kufanya uzinduzi wa Kampeni katika jimbo hilo.
Mgombea Ubunge katika jimbo la Vunjo James mbatia kaiwa ameongozana na mkewe ,Catherine Mbatia na motto wao Chelsea wakiingia katika uwanja wa michezo wa chuo cha Ualimu Mrangu kwa ajili ya mkutano wa ufunguzi rasmi wa kampeni.
Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

NITASIMAMIA SHERIA KWA KUWAWAJIBISHA WATAKAO PINDISHA SHERIA KWA MANUFAA YAO-DKT MAGUFULI

$
0
0
 Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Pombe Magufuli(katikati) akiwanadi Mbunge wa Handeni Mjini Dk. Abdallah Kigoda (kulia) na Mgombea wa Ubunge Jimbo la Handeni Vijijini Ndugu Mboni Mhita kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika katika uwanja wa Kigoda mjini Handeni.

Wakati kampeni za kuwania Urais,Ubunge na Udiwani zikidizi kushika kasi nchini,Mgombea urais kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi CCM Dkt John Pombe Magufuli,amesema atasimamia utawala wa sheria kwa kuwawajibisha wale wote wanaopindisha sheria kwa faida yao.

Magufuli aliyepewa jukumu la kuipeperusha bendera ya chama cha Mapinduzi,katika ngazi ya urais,amesema utawala wake hautakuwa na simile na wanaopoka haki za wanyonge,amesema kuwa ni jambo lisilokubalika kuona haki za wanyonge zikipokwa na matajiri wachache na kuelezea kuwa atawashughulikia kwa mujibu  sheria zilizopo.

Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Pombe Magufuli akisoma bango la vijana wafanya biashara ndogo ndogo wa eneo la Dumila maarufu kama Feri wakati akielekea mkoani Tanga ikiwa muendelezo wa mikutano ya kampeni za CCM .

Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akiwahutubia wananchi wa wasili katika kijiji cha Muheza-Masagala akielekea wilayani Handeni kuwahutubia wananchi katika mkutano wa kampeni
Baadhi wananchi wa kijiji cha Vyadigwa wakimsikiliza Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli (hayupo pichani) alipowahutubia wakazi wa kijiji hicho wilayani Kilindi
Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akiwasili katika kijiji cha Muheza-Masagala akielekea wilayani Handeni kuwahutubia wananchi katika mkutano wa kampeni

Team Magufuli ya Handeni nayo ilikuwepo kuwahamasisha wananchi wampigie kura ya ushindi Dkt Magufuli,kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Kigoda.
Wakifuatilia mkutano wa kampeni ndani ya Mvomero .

Wananchi wa Handeni wakimsikiliza Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli kwenye mkutano wa Kampeni za CCM uliofanyika kwenye uwanja wa Kigoda mjini Handeni.
 Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Pombe Magufuli akihutubia wakazi wa Turiani mkoani Morogoro na kuwaambia atahakikisha migogoro ya ardhi inamalizika na kuileta jamii kuishi kwa amani na upendo.

PICHA NA MICHUZI JR-HANDENI

PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

NGOMA AFRICA BAND (AKA FFU-UGHAIBUNI)WAFUNGA KAZI VECHELDE FESTIVAL,UJERUMANI

$
0
0
Kikosi Kazi Ngoma Africa Band aka FFU-Ughaibuni chenye maskani nchini ujerumani juzi siku ya Jumamosi ya 5 September 2015 kilifanikiwa kufunika katikaonyesho Vechelde Festival nchini Ujerumani. Bendi hiyo maarufu barani ulaya kwa kuwadatisha washabiki wa muziki wa kiafrika kule ughaibuni imejijenga umaarufu katika kila kona na kuwekwa kileleni katika nafasi ya juu na washabiki wake wa
kimataifa.  Inaongozwa na kamanda Ras Makunja na kuwa na utajiri wa wanamuziki vijana wenye wingi wa vipaji .
wasikilize at www.reverbnation.com/ngomaafricaband
jiunge nao pia at https://www.facebook.com/NgomaAfricaBand




























MKUBWA FELLA AANZISHA BAND NYINGINE YA VIJANA KUTOKA MKUBWA NA WANAWE

$
0
0
Mkurugenzi wa kituo cha Mkubwa na Wanawe, Mkubwa Fella ameweza kutoa zao la vijana wengine kutoka Mkubwa na Wanawe ambao wanafanya muziki wa Taarab na kuwabariki jina la Moyo Band, band hii imechanganya wanawake na wanaume na kwa mala ya kwanza itatambulishwa siku ya Ijumaa ya tarehe 11 pale Dar Live wakati Yamoto Band wakizindua Chupa lao jipya ambalo limefanyika SA Cheza kwa Madoido. Zaidi msikilize Saidi Fella Akielezea......

PROFESA MBARAWA MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA MKOANI PEMBA KWA TIKETI YA CCM AKIZINDUA KAMPENI

$
0
0
Profesa Mbarawa mgombea ubunge jimbo la mkoani Pemba kwa tiketi ya CCM akizungumza na wananchi wa Mkoani Pemba wakati wa kuzindua kampeni za chama cha CCM mkoani humo jana.

KWA VIGEZO HIVI WE SI KIBARUA NI MUAJIRIWA KISHERIA

$
0
0
   Na  Bashir  Yakub
MAKALA  haya  yataeleza   tofauti  kati  ya  kibarua  na  ajira  ili  isiwe  unaitwa  kibarua  kumbe  kisheria  umeajiriwa  na  unastahili  stahiki  zote  za  kiajira. 

Wako  watu  wengi  wanafanya kazi  lakini  hawajui  wanafanya  kazi  katika  mwavuli  upiyawezekana  mtu  akawa  amefanya  kazi  miaka  mingi  lakini  bado  kazi  anayofanya  haitambuliki  anaifanya  kama  nani.   

Na  mara  nyingi  hii  hujitokeza  katika  kazi  zile   ambazo  si  za  kitaaluma,Kazi  zisizo    za  kitaaluma   ni  kama   kufanya  kazi  za  ndani, kusaidia  mashambani,  kusaidia  katika ujenzi  na  nyingine  zinazofanana  na  hizo. 

  Lakini  pia  siku  hizi  kutokana  na ongezeko  la  ukosefu  wa ajira  hata kazi  ambazo  ni  za  kitaaluma  nazo  zimekumbwa  na janga  hili.
 Kwa sasa katika  ofisi  nyingi    wapo  watu  wanafanya  kazi  za  kitaaluma  lakini  haijulikani  kama  wameajiriwa  au  ni  vibarua. 

Wapo  watu  wamekaa  maofisini  hata  miaka  mingi   wakiitwa   wafanya  mazoezi ( intern) Wapo  wahasibu, madaktari, walimu, wachumi,  na  wengine  wengi.   

Waajiri  hupenda  sana  hali  hii  kwakuwa   huwapatia  faida  kubwa,  Kwanza  huwalipa  kiduchu  watu  hawa     lakini  pili hukwepa  kulipa  stahiki zao  nyingine  za  kiajira  kama  malipo  ya  muda  wa  ziada,matibabu, likizo, kuumia  kazini  na  stahiki  nyinginezo.

1.NINI  MAANA  YA  AJIRA.
Ajira    ni  mahusiano  ya  kikazi  kati  ya  mwenye  kazi  na  mfanyakazi  ambapo  mwenyekazi  huwa  na  mamlaka   ya kutawala,  kudhibiti, na  kuelekeza  namna ,  jinsi, na  wakati  gani  kazi  husika  ifanyike. 

 Wako  watu  wanafikiria  na  kujua  kuwa  ili  kazi  iitwe  ajira  ni  lazima  yawepo  maandishi  ya  kimkataba, hapana  hili  si  lazima, muhimu  ni  kama  inavyoelekezwa  katika tafsiri  hapo  juu. 

 Hii  ina  maana  ili  kazi  iitwe ajira  vipo  vigezo  vinavyozingatiwa na  hasa hivyo  nilivyotaja  kwenye  tafsiri, kimsingi  yapo  mambo  matano  ambayo   yakitokea  kazi  yoyote  unayofanya  itaitwa  ajira  na  utastahili  kupata  haki  zote  za  kiajira  kama  muajiriwa, tutaona mambo  hayo  hapa  chini.
2.   JE  WE  NI  KIBARUA  AU  MUAJIRIWA.
Yapo  mambo  matano   yatakayokujulisha kuwa we  si  kibarua  bali ni  muajiriwa.
( a ) Kwanza  ikiwa  una  mkataba  maalum   unaoeleza   aina  kazi  unayofanya,  sehemu  ya  kazi,   pesa  unazolipwa, , muda  wa  kazi, likizo  na mengine  usiambiwe  wewe  ni  kibarua. 

Makubaliano  ya  kimaandishi  ya  namna  hii   yanakupa  hadhi  ya   muajiriwa  na  unastahiki  haki  zote  za  muajiriwa  kwakuwa  we utakuwa  ni  muajiriwa  na  si  kubarua.
( b ) Pili  ikiwa  vitendea  kazi  unavyotumia   vinamilikiwa  na  mwenye  kazi,  mfano  we  ni  dereva  na  gari  si  la  kwako  ni  la  tajiri, unafanya  usafi  lakini  vifaa  vyote  vya  usafi  ni  vya  tajiri,  unafanya  kazi  za  ndani na  kila  kitu  ndani  ni  cha  tajiri. Basi  ikiwa  hilo  liko  hivyo  ni  kigezo  kuwa  hiyo  ni  ajira  na  si  kibarua.
( c ) Tatu  ikiwa  mamlaka  ya  kuamua  kazi  ifanyike  vipi,  kwa  namna  gani   na  kwa wakati  gani  anayo  yule  aliyekupa  kazi  basi  nacho  ni  kipimo  kuwa  hiyo  ni  ajira.  Kwa  mfano  bosi  na  sekretari  wake.  Kwakuwa  bosi  ndiye  huagiza  kazi  ifanyike  vipi, kwa  namna  gani n.k  bosi  huyo  hawezi  kusema  kuwa  hajamuajiri  huyo  sekretari.  Hii  ni  tofauti  na  pale  unapomleta  fundi  ujenzi  nyumbani.  Utamuonesha  kazi  lakini   hutakuwa  na  uwezo  wa  kumuelekeza  afanyeje  kazi  kwakuwa   yeye ndiye  fundi na  anajua namna ya  kufanya  kazi  yake.
( d ) Nne  suala  la  nani  anawajibika  na  hasara  inapotokea  nalo ni  kipimo  iwapo  umeajiriwa  au  ni  kibarua.  Kwa  mfano  ukimkodisha  dereva  hata  kwa  miaka  miwili  ikiwa  kila    gari  linapoharibika  au  kupata ajali  hutengeneza  yeye  hawezi  kusema  umemuajiri,  lakini  ikiwa   utatengeneza  wewe  unayemkodi  dereva  basi  itakuwa  ni kipimo  kuwa  yupo  katika  ajira.

( e ) Tano   ni  faida.  Nani  hunufaika  na  faida  nacho  ni kipimo  ikiwa  umeajiriwa   au  ni  kibarua.
Haya  ndiyo  mambo  makuu  yatakayokuashiria  ikiwa  umeajiriwa  au  unafanya  kibarua  na  si  mengineyo.

MWANDISHI   WA   MAKALA  HAYA   NI   MWANASHERIA  NA  MSHAURI   WA  SHERIA  KUPITIA  GAZETI  LA  SERIKALI   LA   HABARI   LEO  KILA  JUMANNE  , GAZETI  JAMHURI   KILA  JUMANNE  NA  GAZETI  NIPASHE  KILA  JUMATANO.    0784482959,        0714047241              bashiryakub@ymail.com

MATEMBEZI MOSHI – DAR YA KUSAFISHA MAZINGIRA

$
0
0
Kiongozi wa msafara wa wanamazingira waliotembea kwa miguu wakiokota taka za plastiki pembezoni mwa barabara kutoka Moshi mkoani Kilimanjaro na kuja jijini Dar es Salaam, Felix Garbe (kushoto) akimkabidhi ufagio Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Ubungo Kibo Dar es Salaam, Sophia Yusuf ikiwa ni ishara ya kuhamasisha wakazi wa Dar es salaam kuchukua jukumu la kutunza mazingira. Tukio hilo lilifanyika baada ya wanamazingira hao kuwasili jijini Dar es Salaam baada ya safari iliyowachukua muda wa wiki tano kumalizika.
 (Picha: Hisani ya Nipe Fagio)

Amour Genius ft Kadjanito-Wanimaliza

$
0
0
Combination sounds presentation produced by 
Man Water directed by Adam Juma Nextlevel production

BBC DIRA YA DUNIA JUMATATU 07/09/2015

Viewing all 110170 articles
Browse latest View live




Latest Images