Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110182 articles
Browse latest View live

MAMA SAMIA KATIKA UBORA WAKE KATIKA MAJIMBO YA MONDULI NA LONGIDO MKOANI ARUSHA

$
0
0
 Wananchi wakiwa wamejawa hamasa kwa nyimbo na nderemo wakati Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassam, alipowasili kwenye Uwanja wa mkutano wa kampeni za CCM leo, katika jimbo la Monduli mkoani Arusha.
  Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassa, akihutubia wananchi wa kwenye uwanja wa mkutano wa kampeni, eneo Namanga, Longido mkoani Arusha, leo
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu, akiwasikiliza kina mama waiokuwa wakichota maji katika eneo la mtaa wa madukani, Longido mkoani Arusha.
 Kijana akishangilia wakati mgombea mwenza wa urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan alipowasili eneo la Madukani, Longido mkoani Arusha leo kuhutubia mkutano wa kampeni.
 "MWAKA HUU MTAISOMA NAMBA" Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassani akimwambia Mgombea Udiwani wa Chadema, Anna Oloiwa, aliyefika kwenye mkutano wa kampeni wa mgombea mwenza huyo, uliofanyika eneo la Madukani, Longido mkoani Arusha leo.

PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO


NEC YAKABIDHI POLISI MAJINA YA WATU 52,078 WALIOJIANDIKISHA ZAIDI YA MARA MOJA KATIKA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

$
0
0
 Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Kailima Ramadhan (kushoto), akimkabidhi Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Benedict Wakulyamba orodha ya majina 52,078 ya watu waliojiandika katika daftari la kudumu la wapiga kura kwa mfumo wa BVR zaidi ya mara mbili Dar es Salaam leo, kwa ajili ya uchunguzi na baadae hatua za kisheria zichukuliwe kwa wahusika.
 Masanduku ya BVR yakiwa yamehifadhiwa Bohari ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
 Mtaalamu wa mfumo wa ulinzi wa NEC, Adolf Kinyelo akitoa maelekezo ya jinsi ya mfumo huo unavyofanya kazi.
Picha hii ni baadhi ya watu waliojiandikisha zaidi ya mara mbili katika daftari hilo.

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imelikabidhi jeshi la polisi orodha ya majina ya watu zaidi ya 52,000 ambao wamebainika kujiandikisha zaidi ya mara moja kwenye daftari la kupigia kura kwa mfumo wa Biometric Voters Registration (BVR), akiwemo Diwani wa Kata ya Kimara, Pascal Manota (Chadema).

Idadi hiyo ilibainishwa Dar es Salaam jana na Mkurugenzi wa NEC, Ramadhan Kailima wakati wa ziara na waandishi wa habari katika bohari ya utayarishaji wa vitambulisho vya kupigia kura kwa mfumo wa BVR.

KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

TABORA WANUFAIKA NA MAFUNZO YA ULINGO – TANZANIA WOMEN CROSSPARTY PLATFORM (TWCP)

$
0
0
Mwenyekiti wa Kikundi cha Maigizo cha Kirumba Sanaa Group kilichopo Jijini Mwanza Katumba Khalid Maduwa akiwa na Kitambulisho chake cha Kupigia Kura.

Maduwa ambae pia ni Mshereheshaji (Mc Katumba) na Mtangazaji wa 99.4 Radio Metro Fm, ameungana na Binagi Media Group katika Kampeni yake ya Kuwahamasisha Watanzania waliojiandikisha katika daftari la wapiga kura kujitokeza kwa wingi katika kuwachagua viongozi bora wa kuwatumikia na si bora viongozi ambao wakati mwingine huchaguliwa kutokana na kutoa rushwa. Kampeni hiyo inaitwa "PIGA KURA, EPUKA KULA".

"Napenda kuwaasa Watanzania wenzangu kuwa tunahitaji uchaguzi wa Amani na Haki bila uvunjifu wa Amani. Tupige kura ili tuwachague viongozi sahihi kwa ajili ya Maendeleo ya Taifa letu". Anasema Maduwa.
Bonyeza HAPA Kufahamu Zaidi.

2015-07-24 22:07 GMT+03:00 Mkala Fundikira :
ULINGO WA WANAWAKE WANASIASA – Tanzania Women Crossparty Platform (TWCP) ni shirika lisilo la kiserikali lililoendesha mafunzo ya kuwajengea uwezo watia nia wanawake, vijana, na watu wenye ulemavu katika nyadhifa mbalimbali za uongozi wa nchi ikiwa ni kuchangia kutoa elimu inayolenga kuleta usawa kama haki msingi ya Mtanzania. 
Mafunzo hayo yamedhaminiwa na UNWomen.

Mafunzo hayo yamewanufaisha walengwa husika kwa kujipatia elimu hiyo huku wawezeshaji wakiwa ni Hilda Stuart Dadu na Emmiliana Msaguka waliohakikisha wanawafikia watiania katika mkoa wa Tabora na kuendesha mafunzo hayo pale Student Center.

BALOZI WA MISRI AMUAGA RAIS KIKWETE IKULU

$
0
0

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na kuagana na Balozi wa Misri anayemaliza muda wake Mhe.Hossam Moharram Ikulu jijini Dar es Salaam leo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete wakiagana  na Balozi wa Misri  anayemaliza muda wake Mhe.Hossam Moharram Ikulu jijini Dar es Salaam leo.
(picha na Freddy Maro)

HESLB YAWATAKA WAOMBAJI MIKOPO KUREKEBISHA TAARIFA ZAO

$
0
0
Na Mwandishi Wetu

BODI ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetangaza orodha ya waombaji wa mikopo kwa mwaka wa masomo 2015/2016 ambao fomu za maombi zimegundulika kuwa na upungufu na kuwataka kufanya marekebisho kabla au ifikapo tarehe 11 Septemba mwaka huu (2015).


Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Bodi hiyo leo (Ijumaa, Agosti 28, 2015), jumla ya fomu za waombaji wa mikopo 7,788 kati ya 68,445 zilizopokelewa na kuhakikiwa zimegundulika kuwa fomu zina upungufu na kuwataka waombaji kusoma majina yao katika tovuti ya Bodi (www.heslb.go.tz).


Kwa mujibu wa taarifa hiyo iliyotolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Bw. George Nyatega, (Pichani) waombaji ambao fomu zao zimegundulika kuwa na upungufu wanatakiwa kurekebisha kabla au ifikapo tarehe 11 Septemba mwaka huu (2015).


“Baada ya kusitisha uombaji wa mikopo kwa njia ya mtandao kwa mwaka wa masomo 2015/2016, Bodi ilianza kufanya uchambuzi wa maombi yote yaliyopokelewa na kugundua kuwa maombi 7,788 ya mikopo yanakosa taarifa muhimu,” inasomeka taarifa hiyo.

  

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, taarifa muhimu zinazokosekana ni pamoja na sahihi za waombaji, nakala za vyeti vya kuzaliwa vya waombaji, sahihi na picha za wadhamini na baadhi ya fomu za maombi kutosainiwa na wanasheria na maafisa wa serikali za mitaa kama maelekezo yanavyotaka.


WADAU WA MAENDELEO YA VIWANDA WATANGAZA VYEMA FURSA ZA UWEKEZAJI NCHINI

$
0
0
 Naibu katibu mtendaji kutoka Ofisi ya Rais Tume ya Mipango anayesimamia klasta ya Miundombinu na huduma, mhandisi Happiness Mgalula akitoa hotuba katika mkutano uliowahusisha ujumbe wa wadau wa maendeleo ya viwanda kutoka Tanzania  na ujumbe wa  wawekezaji kutoka nchini China.

 Picha ya pamoja kati ya wadau wa maendeleo ya viwanda kutoka Tanzania na ujumbe wa wawekezaji kutoka nchini China.
 Wajumbe wa mkutano wakisikiliza kwa makini hotuba kutoka kwa Naibu katibu mtendaji Ofisi ya Rais Tume ya Mipango, Mhandisi Happiness Mgalula wakati wa mkutano.
Wajumbe wa mkutano wakiwa wanasoma kwa makini baadhi ya nyaraka katika mkutano huo.

EU KUTUMA WAANGALIZI 128 KWAAJILI YA UICHAGUZI MKUU

$
0
0
Katibu Mkuu  wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula, na Balozi wa Umoja wa Ulaya Nchini Tanzania, Mhe. Filiberto Sebregondi, wakibadilishana Hati ya Makubaliano ya kuruhusu waangalizi wa uchaguzi kutoka Umoja wa Ulaya (EU) kuingia nchini kufuatilia Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 mwaka huu.
Hati hiyo ya makubaliano imesainiwa leo, 28-08-2015, katika ukumbi wa mikutano wa Wizara hiyo.
 Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga,(kulia) akizungumza katika hafla hiyo ya kusaini hati ya Makubaliano ya kuruhusu waangalizi wa uchaguzi kutoka Umoja wa Ulaya (EU) kuingia nchini kufuatilia Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 mwaka huu.
Bi. Mindi Kasiga akiwatambulisha waandishi wa Habari, waliohudhuria hafla hiyo (hawapo pichani).

KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

NSSF YASHIRIKI KWENYE MKUTANO WA MWAKA WA WADAU WA KOROSHO MKOANI LINDI LEO

$
0
0
SHIRIKA la Taifa la Hifadhi ya Jamii NSSF limeshiriki kwenye mkutano wa Wadau wa Korosho unaofanyika kwenye Hoteli ya Peace Beach Mkoani Lindi,mkutano huo utakaofanyika kwa Siku mbili mfululizo utahusisha wadau wa Korosho kutoka Tanzania nzima.

Katika Mkutano huo ambao NSSF imepata nafasi ya kutoa  mada imewahimiza wadau hao waweze kujiunga na NSSF ili waweze kupata mafao bora yatolewayo na mfuko huo, Mafao hayo yakiwemo Matibabu bure, Kuumia Kazi, Uzazi kwa Kina mama , Mikopo kwa wanachama na Mengineyo.



Akiongea katika Mkutano huo Meneja wa NSSF Mkoa wa Mtwara , Stanley Milanzi amewaambia wadau huo kupitia Mpango wa NSSF Wakulima Scheme wakulima wa Mkoa wa Mtwara wamepata karibia Shilingi bilioni mbili kama mikopo kutoka NSSF.
 Meneja Kiongozi wa Masoko na Uhusiano  wa NSSF, Eunice Chiume(wa tatu Kushoto)  akiwa na Kaimu Meneja Mkoa wa Lindi, Jumbe Dona (wa pili Kushoto), Afisa  Matekelezo Kuruthum Yusufu ( Wa kwanza Kushoto), Afisa Mwandamizi wa Uhusiano Salim Kimaro (wa tatu Kulia), Afisa Uendeshaji Muandamizi Abasi Cothema (wa pili Kulia) na Afisa Mafao wa Mkoa wa Lindi Paschal Mushi (Wa kwanza Kulia) kwenye mkutano wa Wadau wa Korosho unaofanyika leo katika hoteli ya Peace Beach Mkoani Lindi.
Maofisa wa NSSF wakiwasaidia wadau wa Korosho kujaza fomu za uanachama ili waweze kujiadikisha kujiunga na NSSF.
Meneja wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya jamii (NSSF), Mkoa wa Mtwara, Stanley Milanzi akitoa mada kwa wadau wa zao la Korosho kwenye mkutano wa mwaka wa wakulima wa korosho uliofanyika leo mkoani Lindi.

Meneja Wa NSSF Mkoa wa Mtwara, Stanley Milanzi  akiwaelekeza wadau wa Korosho jinsi ya kujaza fomu za NSSF ili waweze kujiandikisha na NSSF.
 Meneja wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya jamii (NSSF), Mkoa wa Mtwara, Stanley Milanzi akitoa mada kwa wadau wa zao la Korosho kwenye mkutano wa mwaka wa wakulima wa korosho uliofanyika leo mkoani Lindi.

MAADHIMISHO WIKI YA NENDA KWA USALAMA BARABARANI YAFANYIKA MKOA WA KIPOLISI TEMEKE

$
0
0
Mkuu wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Temeke, Endrew Satta akiwakabidhi vyeti baadhi ya madereva wa bodaboda waliofuzu mafuzo ya Pikipiki katika wiki ya nenda kwa Barabarani iliyofanyika katika viwanja vya Mwembe yanga Temeke jijini Dar es Salaam leo.
 Mkuu wa Jeshi la Polisi Mkowa wa Temeke, Endrew Satta akitembelea mabanda ya maonyesho ya wiki ya nenda kwa usalama Barabarani iliyofanyika katika viwanja vya Mwembe yanga Temeke jijini Dar es Salaam leo.
Umoja wa waendesha  Pikipiki  Temeke (UWAPITE) wakiwa kwenye picha ya pamoja katika vianja vya Mwembeyanga katika maazimisho ya wiki ya nenda kwa usalama Barabarani.(Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii)

TWIGA KUFUNGUA DIMBA NA IVORY COAST

$
0
0
TIMU ya Taifa ya Wanawake (Twiga Stars) inayotarajiwa kuondoka nchini mwishoni mwa mwezi Agosti kuelekea nchini Congo-Brazzavile kwenye Fainali za Michezo ya Afrika (All Africa Games) imepangwa kufungua dimba na timu ya Wanawake ya Ivory Coast Septemba 6, 2105.
Twiga Stars iliyoweka kambi kisiwani Zanzibar kwa takribani mwezi mmoja sasa, itacheza mchezo wake pili Septemba 9, dhidi ya Nigeria kabla ya kumalizia mchezo wake wa mwisho hatua ya makundi dhidi ya wenyeji Congo-Brazzavile Septemba 12, 2105.
Jumla ya timu nane za Wanawake kutoka Barania Afrika zinashirki fainali hizo ambazo ni Nchi za Afrika Kusini, Cameroon, Ghana, Misri (wamejitoa) kundi B, na wenyeji Congo-Brazzavile, Ivory Coast, Nigeria na Tanzania kutoka kundi A.
Timu mbili za juu kutoka kila kundi zitafuzu kwa hatua ya nusu fainali.

WHO YATOA MSAADA WA DAWA ZA KUTAKASA MAJI JIJINI DAR ES SALAAM LEO

$
0
0
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Usitawi wa Jamii Dk Donan Mmbando  akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani kwa kulishukuru shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) kwa kutoa msaada wa Dawa za kutakasa maji (Water Guard ) leo jiji Dar es Salaam kulia ni Mwakilishi wa shirika la Afya Ulimwenguni hapa Nchini Dk Rufaro Chatora.
 Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza kwa makini Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Usitawi wa Jamii Dk Donan Mmbando leo jiji Dar es Salaam
 Mwakilishi wa shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) hapa Nchini Dk Rufaro Chatora akimkabidhi msaada huo Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dk Donan Mmbando  leo jiji Dar es Salaam
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dk Donan Mmbando  akimkabidhi Mgaga Mkuu wa Serikali, Dk.Grace Magembe  msada huo ulio tolewa na shirika la Afya Ulimwenguni leo jijini Dar es Salaam
( Picha na Emmanuel Massaka)

MAGUFULI AHIDI KUANZISHA MAHAKAMA YA MAFISADI NA WALA RUSHWA IWAPO ATACHAGULIWA KUWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA.

$
0
0
 Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi,Dkt John Pombe Magufuli akihutubia maelfu ya wananchi katika viwanja vya Nzovwe mjini Mbeya jioni ya leo,kwenye mkutano wa kampeni ya kuwaomba ridhaa Watanzania ya kuwaongoza katika awamu ya tano.


Dkt Magufuli amesema kuwa serikali atakayoingoza atakapopata ridhaa ya kuingia Ikulu,itazifanya huduma za Afya kuwa bora na kuwabana wahudumu wa afya wenye tabia ya kuchukua dawa na kuziuza kwa watu binafsi.



Magufuli ambaye yupo katika mikoa ya Nyanda za juu kusini katika kampeni ya kusaka nafasi ya kuwa raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania,amesema suala la afya litakuwa moja ya ajenda zake muhimu atakapoingia madarakani.


Katika hatua nyingine Dkt Magufuli amewaleza wananchi kuwa iwapo watampa ridhaa ya kuiongoza Tanzania,atahakikisha anaanzisha mahakama maalumu ya Mafisadi na Wala rushwa.
 Mbunge wa zamani wa jimbo la Kyela Mzee John Mwakipesile akimpigia debe Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dkt  John Pombe Magufuli wakati mgombea huyo alipofika jimboni humo kuomba kura za wananchi ili wamchague kuwa rais.Mzee Mwakipesile amesema kuwa anamuunga mkono Dkt Magufuli na atahakikisha anashiriki kikamilifu kuhakikisha mgombea huyo anaibuka na ushindi kwa kishindo.
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kyela Dkt Harrison Mwakyembe akimpigia debe Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dr. John Pombe Magufuli wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya Nzovwe mjini Mbeya jionu ya leo.
  Naibu Waziri wa Fedha Mh Mwigulu Nchemba akihutubia katika  mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika viwanja vya Nzovwe mjini Mbeya,ambapo Mwigulu aliwaomba wananchi hao waliojitokeza kwa wingi kumpigia kura za ndio Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli na hatimae aweze kuiongoza Tanzania katika awamu ya tano kwa sababu ana sifa zoto za kuongoza nchi.
 Maelfu ya Wananchi waliojitokeza kwa wingi katika viwanja vya Nzovwe Mbeya jioni ya leo,ambapo Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli aliwahutubia wananchi hao.
 Naibu Waziri wa Fedha Mh Mwigulu Nchemba akihutubia katika  mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika viwanja vya Nzovwe mjini Mbeya,ambapo Mwigulu aliwaomba wananchi hao waliojitokeza kwa wingi kumpigia kura za ndio Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli na hatimae aweze kuiongoza Tanzania katika awamu ya tano kwa sababu ana sifa zoto za kuongoza nchi.
 Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi,Dkt John Pombe Magufuli akihutubia maelfu ya wananchi katika viwanja vya Nzovwe mjini Mbeya jioni ya leo,kwenye mkutano wa kampeni ya kuwaomba ridhaa Watanzania ya kuwaongoza katika awamu ya tano,Magufuli amewaambia wananchi hao kuwa atahakikisha  huduma za afya zinaimarishwa ipasavyo,katika suala la Elimu Magufu aliwaeleza Wananchi kuwa iwapo watamchagua katika nafasi hiyo ya Urais atahakikisha elimu kuanzia darasa la kwanza mpaka kidato cha nne itatolewa bure,aidha pia amewataka Watanzania kuwa wamoja katika kuhakikisha wanailinda na kuitunza amani iliyopo nchini. 
 Wananchi wakimsikiliza Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akiwahutubia katika mkutano wa kampeni katika viwanja vya Nzovwe mjini Mbeya. 
 Wafuasi na wapenzi wa chma cha CCM wakishangilia 
Maelfu ya Wananchi waliokusanyika katika viwanja vya Nzovwe mjini Mbeya wakimsikiliza Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika jioni ya leo.
 Jicho la samaki katika ubora wake kwenye mkutano wa kampeni za CCM katika viwanja vya Nzonvwe mjini Mbeya.

RAIS KIKWETE ATOA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA FAMILIA ZA WALIOPATWA NA AJALI YA MOTO

$
0
0
THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS





TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia Salamu za Rambirambi Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mheshimiwa Said Meck Sadik kufuatia vifo vya watu tisa wa familia moja ya Bwana Masoud Matal vilivyotokea alfajiri ya tarehe 27 Agosti, 2015 kwa ajali ya moto.


Wanafamilia hao wakiwemo watoto watano walipoteza maisha baada ya nyumba yao iliyoko katika Mtaa wa Gulam, eneo la Buguruni Malapa katika Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam kuungua na kuteketea kabisa kwa moto.  Baba wa familia, Bwana Masoud Matal alisalimika kwa vile hakuwamo katika nyumba hiyo wakati ikiungua.


“Nimepokea kwa mshtuko mkubwa na nimesikitishwa mno kutokana na taarifa za kupoteza maisha kwa watu tisa wa familia moja ya Bwana Masoud Matal baada ya nyumba yao kuunguzwa na kuteketezwa kabisa na moto alfajiri ya tarehe 27 Agosti, 2015”, amesema kwa huzuni Rais Kikwete akiomboleza vifo vya wanafamilia hao.


“Kwa hakika hili ni pigo kubwa kwa Bwana Masoud Matal, lakini namuomba awe mvumilivu kwa machungu yote ya kupotelewa ghafla na familia nzima, lakini  yote amwachie Mwenyezi Mungu muweza wa yote”, ameongeza kusema Rais Kikwete.


Katika salamu zake hizo, Rais Kikwete amemwomba Mheshimiwa Sadik kumfikishia Salamu zake za rambirambi na pole nyingi kwa Bwana Masoud Matal kutokana na msiba huo mkubwa uliompata, na amesema anamuomba Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema azipokee na kuzilaza Mahala Pema Peponi Roho za Marehemu wote, Amina.


Imetolewa na;

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

Ikulu – Dar es Salaam.

28 Agosti,2015



BBC DIRA YA DUNIA IJUMAA 28.08.2015

VOA Kiswahili: Zulia Jekundu S1 Ep 38: Star Wars, Katy Perry, Elvis Presley


Taarifa Ya Kukanusha Uwepo Wa Mvua Kubwa Na Upepo Mkali

Kenyan Fraudster Suspect in Dar Court

$
0
0
A fraudster suspect, Philiph Mbithi Mutiso (28), Kenyan National (pictured with his lawyer),  resident of Namanga in Kenya appeared at the Kisutu Resident Magistrate’s Court in Dar Es Salaam on 28th August 2015 faced with three charges under the Economic and Organised Crime Control Act of 2002, including fraudulently operating of a communication network and illegally receiving and terminating  International Telecommunications Traffic, using unlicensed equipment thus causing a loss amounting to Tshs 757,200,000/- to the Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA) and the United Republic of Tanzania.  
The suspect who unlawfully operated the international gate-way in Arusha Region and Namanga  appeared before the Principal Resident Magistrate Huruma Shahidi was remanded till 10th September 2015 when the case comes up for another mention. Several fraudster suspects have been intercepted and booked interfering with the national communication network system, since the establishment of the Telecommunications Traffic Monitoring System (TTMS).  (Photo by  Semu Mwakyanjala,  TCRA)  

MAADHIMISHO YA WIKI YA NENDA KWA USALAMA MKOA WA KIPOLISI TEMEKE

$
0
0
 Kaimu Mwenyekiti wa kamati ya Usalama Barabarani,Thabeet Massa akimkaribisha mgeni rasimi katika mazimosho ya wiki ya nenda kwa Barabarani jiji Dar es Salaam
 Mkuu wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Temeke,Endrew Satta akihutubia wananchi juu ya kuedesha  kwa    salama okoa maisha katika harakati za  wiki ya nenda kwa Barabarani jiji Dar es Salaam
 Mkuu wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Temeke,Endrew Satta akiwakabidhi vyeti madereva bodaboda waliofuzu mafuzo ya Pikipki katika wiki ya nenda kwa Barabarani jiji Dar es Salaam 
 Mkuu wa Jeshi la Polisi Mkowa wa Temeke,Endrew Satta akitembelea mabanda ya maonyesho ya wiki ya nenda kwa usalama Barabarani jijini  Dar es Salaam
Umoja wa waendesha  Pikipiki  Temeke (UWAPITE) wakiwa kwenye picha ya pamoja katika maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama Barabarani jijini  Dar es Salaam. Picha na Emmanuel Masaka wa Globu ya Jamii

MAGUFULI AMJULIA HALI NA KUMPA POLE MEYA WA JIJI LA MBEYA MH ATHANAS KAPINGA BAADA YA KUPATA AJALI

$
0
0
 
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi (CCM),Ndugu John Pombe Magufuli akimjulia hali na kumpa pole aliyekuwa Meya wa jiji la Mbeya Mh.Athanas Kapunga aliyepata ajali wilayani Momba mkoani Mbeya wakati wa mbio za maandalizi ya Kampeni hivi karibuni,Mh Kapunga amelazwa kwenye chumba maalum cha wagonjwa  mahututi (ICU) katika hospitali ya Rufaa mjini humo.
 Mmoja wa Wauguzi walioko kwenye chumba maalum cha wagonjwa  mahututi (ICU),akimpa maelezo mafupi Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi (CCM),Ndugu John Pombe Magufuli alipokwenda kumjulia hali n kumpa pole aliyekuwa Meya wa jiji la Mbeya Mh.Athanas Kapunga aliyepata ajali wilayani Momba mkoani Mbeya wakati wa mbio za maandalizi ya Kampeni hivi karibuni.
 Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi (CCM),Ndugu John Pombe Magufuli akisalimiana na baadhi ya Wauguzi walioko katika chumba maalum cha wagonjwa mahututi (ICU) katika hospitali ya Rufaa Mbeya,mara baada ya kumjulia hali na kumpa pole aliyekuwa Meya wa jiji la Mbeya Mh.Athanas Kapunga aliyepata ajali wilayani Momba mkoani Mbeya wakati wa mbio za maandalizi ya Kampeni hivi karibuni.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi (CCM),Ndugu John Pombe Magufuli akisalimiana na Mke wa Meya Mama Kapinga mara baada ya kutoka kumjulia hali na kumpa pole aliyekuwa Meya wa jiji la Mbeya Mh.Athanas Kapunga aliyepata ajali wilayani Momba mkoani Mbeya wakati wa mbio za maandalizi ya Kampeni hivi karibuni.

 PICHA NA MICHUZI JR-MBEYA

MAGUFULI ALIVYOTIKISA JIJI LA MBEYA

Viewing all 110182 articles
Browse latest View live




Latest Images