Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110186 articles
Browse latest View live

VOA: Zulia Jekundu S1 Ep 34: Justin Bieber, Johnny Depp, Taraji Henson & Emmy 2015


SATURDAY, JULY 25, 2015 MCHUNGAJI NATSE AWAAGA JIMBO LA KARATU ,QAMBALA KUPEPERUSHA BENDERA YA CHADEMA

$
0
0
Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki,Joshua Nassari akizungumza kwenye mkutano huo uliofanyika katika viwanja vya hosteli ya KKKT Karatu na kumpongeza mch.Natse kwa kuamua kuachia nafasi wanachama wengine.

Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki,Joshua Nassari akizungumza kwenye mkutano huo uliofanyika katika viwanja vya hosteli ya KKKT Karatu na kumpongeza mch.Natse kwa kuamua kuachia nafasi wanachama wengine.
Mshindi wa kura za maoni za Ubunge Jimbo la Karatu,Willy Qamballa akiwashukuru wajumbe baada ya kujizolea kura 217 na mpinzani wake wa karibu Lazaro alipata kura 84.

Mshindi wa kura za maoni za Ubunge Jimbo la Karatu,Willy Qamballa akifurahia na wafuasi wake baada ya kutangazwa mshindi. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

KOMBE LA KAGAME: YANGA YAIFUNGA KMKM 2-0

$
0
0
 Mshambuliaji wa Yanga, Donald Ngoma akimtoka beki wa KMKM, Khamis Ali Khamis wakati wa mchezo wa Kombe la Kagame uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Yanga imeshinda 2-0.
 Deus Kaseke akiwatoka wachezaji wa KMKM.
 Golikipa wa timu ya KMKM ya Zanzibar, Nassor Abdulla Nassor akiokoa moja ya hatari langoni mwake wakati timu yake ilipopambana na Yanga katika mchezo wa Kombe la Kagame.
Donald Ngoma (kulia) akiwania na beki wa KMKM, Khamis Ali Khamis.
Mashabiki wa Yanga wakishangilia timu yao.

Dr Shashi Tharoor MP - Britain Does Owe Reparations

KIOTA KIPYA CHA MARAHA CHA JOZI LOUNGE CHAZINDULIWA MSASANI VILLAGE JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
Kiota Kipya Cha Maraha kimezinduliwa Kimezinduliwa Jijini Dar es Salaam jana Jiioni. Kiota hicho Jozi Lounge, inapatikana Pande za Msasani Village, jirani kabisa na Shule ya Msingi Msasani.
 Mmiliki wa Jozi Lounge, Dismass Massawe (kushoto)  akifungua   Champaign wakati wa uzinduzi wa kiota hicho.  Hafla hiyo ilihudhuriwa na wadau mbalimbali ambao walikunywa na kucheza mpaka majogoo.Hiyo ndiyo habari ya Mujini.
Mmiliki wa Jozi Lounge, Dismass Massawe (kushoto)huku meneja wake ni Nick Rawlings(Mzungu anayefungua Champaign).
 Sehemu ya Counta ya kiota hicho cha Jozi.
Wadau wakipiga picha kabla ya kuzama ndani kwenye kiota cha maraha.
 DJ mkali anaeporomosha muzic wa hatari

 Wadau kutoka Kampuni ya Executive Solution ya jijini Dar es salaam ambao ndio walikuwa waratibu wakuu wa uzinduzi huo wakishow love.
 Ilikuwa ni hatari kuyarudi magoma mwanzo mwisho. Hakuna kulala wala kuchoka ndani ya Jozi Lounge

KUAHIRISHWA SAFARI YA TRENI YA ABIRIA KWENDA BARA HADI LEO JIONI JULAI 25, 2015

$
0
0

Uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania –TRL unasikitika  kuwataarifu wananchi na abiria waliokuwa wasafiri na treni ya leo Ijumaa Julai 24, 2015 kutoka Dar es Salaam kwenda bara kuwa safari hiyo imeahirishwa hadi kesho saa 11 jioni. 
Kwa mujibu wa taarifa hiyo sababu za kuahirishwa safari hiyo ni ajali ya treni ya mizigo iliyotokea leo Ijumaa Julai 24, 2015  saa 8:15 alasiri maeneo  ya  Stesheni  za Mazimbu –Mkata mkoani  Morogoro ambapo ilihusisha mabehewa matano ya  treni ya  mizigo iliyokuwa inasafiri kwenda Bara, manne  yaliacha njia na moja kuanguka kabisa.

Tayari Wahandisi wa TRL wako eneo  la ajali kufanya tathmini na kuanza zoezi la uokoaji,  ikiwemo kazi ya kuyanyanyua mabehewa yaliyopata ajali na kisha kukarabati njia ili iwezwe kupitika mapema hapo kesho.

            Uongozi wa TRL inawaomba radhi wananchi na wateja wake wote nchini  kwa usumbufu             utakaojitokeza.

            -Tamati-

            Imetolewa na Afisi ya Uhusiano ya TRL kwa Niaba ya

            Kaimu  Mkurugenzi Mtendaji ,

            Mhandisi  Elias Mshana

            Dar es Salaam,


            Julai 24,  2015.

TAARIFA KWA UMMA JUU YA MAKALA ILIYOTOLEWA NA GAZETI LA MWANANCHI

MSAADA TUTANI

$
0
0
MKAZI wa Heka wilayani Manyoni Mkoani Singida Joha Athumani(pichani), anaomba wasamaria wema kumsaidia msaada wa matibabu kwaajili ya mtoto wake Halima Mohamed mwenye umri wa mwaka mmoja na nusu anayesumbuliwa na tatizo la kutoona.

Akizungumza na ripota wa Globu ya Jamii Kanda ya Kati, Joha alisema kutokana na uchunguzi uliofanyika katika Hospitali ya wilaya ya Manyoni zinahitajika fedha zaidi ya shilingi laki tano (500,000/=) kwaajili kufanyiwa upasuaji mtoto huyo.

Alisema kwasasa hana uwezo wa kumtibia mtoto huyo kutokana kupewa rufaa ya kwenda Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ili mtoto huyo aweze kufanyiwa upasuaji.

Hata hivyo alisema kwa sasa hana msaada wowote kutokana na mumewe kumkimbia baada ya kuzaa mtoto mwenye tatizo hilo.

Mkazi huyo wa Heka alisema mwanaye alianza kusumbuliwa na tatizo la kutoona akiwa na umri wa miezi mitatu mpaka sasa, ambapo amezunguka huku na huku lakini hajafanikiwa kupata matibabu ya mtoto wake.

Ameomba wasamaria wema watakaoguswa kumsaidia, wawasiliane na mwandishi wa gazeti hili kupitia namba 0712 561279.
Barua ya rufaa aliyoandikiwa Joha Athumani ya kwenda hospitali ya Taifa Muhimbili kwaajili ya matibabu ya mwanaye Halima Mohamed.

TTCL yaunganisha Ofisi na Kanda za MSD kwenye Mkongo

$
0
0
Ofisa Mkuu wa Masoko na Mauzo wa kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Peter Ngota akimkabidhi Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Cosmas Mwaifwani (kushoto) hati ya makubaliano ya mradi wa huduma za mkongo kwa ofisi za Bohari ya Dawa Tanzania. Hafla hiyo ya makabidhiano ya mradi wa huduma za mkongo kwa ofisi za Bohari ya Dawa Tanzania imefanyika leo Makao Makuu ya Ofisi za MSD Dar es Salaam. Ofisa Mkuu wa Masoko na Mauzo wa kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Peter Ngota akimkabidhi Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Cosmas Mwaifwani (kushoto) hati ya makubaliano ya mradi wa huduma za mkongo kwa ofisi za Bohari ya Dawa Tanzania. Hafla hiyo ya makabidhiano ya mradi wa huduma za mkongo kwa ofisi za Bohari ya Dawa Tanzania imefanyika leo Makao Makuu ya Ofisi za MSD Dar es Salaam. Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Cosmas Mwaifwani akizungumza katika hafla ya makabidhiano ya mradi wa huduma za mkongo kwa ofisi za Bohari ya Dawa Tanzania inayotolewa na kampuni ya TTCL. Ofisi za Kanda za MSD zimeunganishwa na Makao Makuu na huduma za mkongo wa mawasiliano ili kufanya kazi zake kwa haraka na ufanisi zaidi.  Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Cosmas Mwaifwani akizungumza katika hafla ya makabidhiano ya mradi wa huduma za mkongo kwa ofisi za Bohari ya Dawa Tanzania inayotolewa na kampuni ya TTCL. Ofisi za Kanda za MSD zimeunganishwa na Makao Makuu na huduma za mkongo wa mawasiliano ili kufanya kazi zake kwa haraka na ufanisi zaidi.Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Cosmas Mwaifwani (kushoto) akisaini hati ya makabidhiano ya mradi wa huduma za mkongo kwa ofisi za Bohari ya Dawa Tanzania (MSD) leo Makao Makuu ya Ofisi za MSD Dar es Salaam, kulia ni Ofisa Mkuu wa Masoko na Mauzo wa kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Peter Ngota akishuhudia. Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Cosmas Mwaifwani (kushoto) akisaini hati ya makabidhiano ya mradi wa huduma za mkongo kwa ofisi za Bohari ya Dawa Tanzania (MSD) leo Makao Makuu ya Ofisi za MSD Dar es Salaam, kulia ni Ofisa Mkuu wa Masoko na Mauzo wa kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Peter Ngota akishuhudia.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Kadama Malunde Mwenyekiti Mpya wa Wanahabari Shinyanga

$
0
0
Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga aliyemaliza muda wake, Shija Felician akimpongeza Mwenyekiti mpya wa Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga, Kadama Malunde (mwenye suti) baada ya kutangazwa mshindi katika uchaguzi wa Klabu hiyo. Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga aliyemaliza muda wake, Shija Felician akimpongeza Mwenyekiti mpya wa Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga, Kadama Malunde (mwenye suti) baada ya kutangazwa mshindi katika uchaguzi wa Klabu hiyo. Viongozi wa Klabu ya waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga waliomaliza muda wao wakijiuzuru nyadhifa zao kabla ya uchaguzi mkuu kupata viongozi wapya wa klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club- SPC)Msimamizi wa uchaguzi mkuu wa waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga David Nkulila akizungumza jambo wakati wa uchaguzi mjini Shinyanga 

Rais Kikwete aagana na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia

$
0
0
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha ikulu na kufanya mazungumzo na mwakilishi mkazi wa Benki ya Dunia hapa nchini Bwana Philipe Dongier anayemaliza muda wake.Bwana Dongier alikwenda kumuaga Rais Kikwete ikulu jijini Dar es Salaam jana jioni.(picha na Freddy Maro)

SIMU TV: HABARI TOKA VITUO VYA TELEVISHENI

UZINDUZI WA KAMPENI YA WAZAZI NIPENDENI AWAMU YA PILI WAFANYIKA VIWANJA VYA MWEMBE YANGA TEMEKE JIJINI DAR

$
0
0
 Mkurugenzi wa Huduma za Kinga Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dk.Neema Rusibamayila kwa niaba ya Waziri wa wizara hiyo Dk. Seif Rashid  (wa pili kushoto), akikata utepe kuashiria uzinduzi wa  kampeni ya Wazazi Nipendeni awamu ya pili  katika viwanja vya Mwembe Yanga Temeke Dar es Salaam leo mchana. Wa kwanza kushoto ni Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID), Anna Bodipo Memba na wa pili kulia ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Grace Magema. 
 Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID), Anna Bodipo Memba (kulia), akitoa hutuba yake kwenye uzinduzi huo.
 Mshauri wa masuala ya Afya ya Jamii kutoka Taasisi ya HBC, Mdadike Thabit (kulia), akimuelekeza jambo mgeni rasmi katika uzinduzi huo Mkurugenzi wa Huduma za Kinga Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dk.Neema Rusibamayila wakati alipokuwa akitembelea mabanda ya watoa huduma kabla ya kufanyika uzinduzi huo.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Kipindi cha Nyumbani Na Diaspora na David Kyungu

J&M VIRGO WASHUSHA MALI MPYA

$
0
0
 DUKA LAKO PENDWA LA J&M VIRGO LIMESHUKA MALI MPYA NA ZA UHAKIKA KABISA KWAKO WEWE MTANZANIA ILI UWEZE KUNG'AA

J&M VIRGO WENYE UHODARI WA KUUZA VIWALO VYA NGUVU NA VYA KISASA JIJI LA DAR ES SALAAM ,WANAPATIKANA PALE MIKOCHENI KWA WARIOBA,JENGO LA C&G PLAZA GHOROFA YA KWANZA.FIKA ILI UWEZE KUJIPATIA VITUZZ NA VIWALO VYA KIJANJA,POCHI BABKUBWA,MOKA MATATA NA MICHUCHUMIO YA HAJA KWA KINA DADA.

KWA KUONA MALI ZAIDI TEMBELEA LIBENEKE LAO


KANALI MSTAAFU ISAAC MWISONGO AMUUNGA MKONO DKT MAGUFULI

DR.MARY MWANJELWA USHINDI WA KISHINDO UBUNGE VITI MAALUM MKOWA WA MBEYA

$
0
0
Mgombea ubunge viti maalum mkoa wa mbeya Dr.Mary Mwanjelwa aibuka mshindi katika kura za maoni kutoka kwa wajumbe wa ccm mkoa wa mbeya na kupata ridhaa ya kulejea tena katika kiti  cha ubunge viti maalum mkoa wa Mbeya kwa ushindi wa kishindo wa asilimia 97 na kuwashinda wagombea kumi (10) kati ya kumi na moja (11) walio kuwa wakigombea na kutaka kuteuliwa na wajumbe wa ccm mkoa wa mbeya...Picha zote Na Fadhiri Atick, Mbeya.
Mshindi wa ubunge viti maalum kupitia chama cha mapinduzi mkoa wa mbeya Dr.Mary Mwanjelwa akiwashukuru wajumbe wa ccm mkowa wa mbeya mara baada ya ushindi katika uchaguzi wa kumpata mbunge viti maalum mkoa wa mbeya ulio fanyika tar:24-07-2015, katika ukumbi wa nyerere Musti jijini mbeya.

BASATA YAWATAKA WASANII WAFUATE TARATIBU WANAPOENDA NJE YA NCHI

$
0
0
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) ambalo ni msimamizi wa sekta ya Sanaa nchini linawakumbusha wasanii wote nchini kuhakikisha wanafuata sheria, kanuni na taratibu zilizopo wanapokwenda nje ya nchi kufanya maonesho au kushiriki shughuli yoyote ya Sanaa ili kuepuka matatizo na mikanganyiko mbalimbali inayoweza kujitokeza.

Kwa mujibu wa taratibu zilizopo, msanii yeyote anapokwenda nje ya nchi anapaswa kujaza fomu maalumu inayotolewa na BASATA na baadaye kupewa kibali bure (bila gharama yoyote) ambacho mbali na kueleza wapi msanii anaelekea kinaeleza kwa kina tarehe ya kuondoka kwa msanii na ile ya kurudi nchini.

Kutokana na kukua kwa sekta ya Sanaa nchini hususan muziki na filamu wasanii wengi wamekuwa wakipata fursa ya kwenda nje ya nchi kufanya maonesho na shughuli zingine za Sanaa hivyo suala la kufuata sheria, kanuni na taratizu za kupata vibali vya kwenda nje ya nchi ni muhimu sana ili kuhakikisha kwanza; safari zao zinakuwa na baraka ya moja kwa moja kutoka Serikalini, pili kusaidia upatikanaji wa takwimu sahihi za wasaniii wanaokwenda nje ya nchi, tatu usalama wa wasanii wetu na mwisho, kuwakabidhi bendera ya taifa kama ishara ya uwakilishi na ubalozi wa nchi yetu katika mataifa wanayoyatembelea.

DKT MAGUFULI AREJEA JIJINI DAR BAADA YA KUJITAMBULISHA MIKOA KADHAA,APOKELEWA KWA KISHINDO

$
0
0
 Mgombea Urais alieteuliwa na Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia wananchi wa Mji wa Bagamoyo (hawapo pichani) alipokuwa akirejea jijini Dar jana jioni akitokea mkoani Dodoma.Dkt Magufuli amejitambulisha vyema kila alikopita na kupokelewa kwa kishindo katika mikoa na vitongoji vyake aliyopita ikiwemo jijini Mwanza,Geita,dodoma,Morogoro,Pwani na jiji la Dar kwa ujumla.
 Wakazzi wa Bagamoyo wakimsikiliza Dkt Magufuli wakati alipokuwa akijitambulisha kwao na kuwashukuru kwa kujitokeza kwa wingi kumpokea,alipokuwa akitoka mkoani Dodoma kurejea jijini Dar jana jioni.
 Baadhi ya Wakazi wa Mji wa Chalinze wakimsikiliza Mteule wa Chama cha Mapinduzi CCM kwa nafasi ya Urais ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. John Pombe Magufuli aliposimama mjini hapo kuwashukuru na kujitambulisha kwa Wananchi wa Chalinze alipokuwa akirejea jijini Dar jana jioni akitokea mkoani Dodoma.
 Aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Chalinze,ambaye anawania tena nafasi ya Ubunge katika jimbo hilo Mh.Ridhiwani Kikwete akiwasalimia Wananchi wa Chalinze na kumkaribisha Mgombea Urais alieteuliwa na Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. John Pombe Magufuli aliposimama mjini hapo kuwashukuru Wananchi wa Chalinze (hawapo pichani) pamoja na kujitambulisha kwao alipokuwa akirejea jijini Dar jana jioni akitokea mkoani Dodoma.
  Baadhi ya Wakazi wa Mji wa Chalinze wakimshangilia kwa mayowe Mteule wa Chama cha Mapinduzi CCM kwa nafasi ya Urais ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. John Pombe Magufuli aliposimama mjini hapo kuwashukuru na kujitambulisha kwa Wananchi wa Chalinze alipokuwa akirejea jijini Dar jana jioni akitokea mkoani Dodoma.
   Aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Chalinze,ambaye anawania tena nafasi ya Ubunge katika jimbo hilo Mh.Ridhiwani Kikwete pamoja na  Mgombea Urais alieteuliwa na Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. John Pombe Magufuli wakifurahia jambo mjini Bagamoyo,aliposimama mjini hapo kujitambulisha na kuwashukuru kwa kujitokeza kwao kwa wingi kumpokea,alipokuwa akirejea jijini Dar jana jioni akitokea mkoani Dodoma.
 Mkazi wa Bagamoyo akifurahia jambo
 Wananchi wakimshangilia Dkt Magufuli (hayupo pichani) alipokuwa akijitambulisha kwao hapo jana mjini Bagamoyo.




KAMPUNI YA MAFUTA YA ENGEN HAPA NCHINI YAPATA MKURUNGENZI MPYA

$
0
0
 Mkurungenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mafuta ya Engen Tanzania, Mubita Akapelwa  akiwashukuru baadhi ya wafanyakazi wa kampunikwa ushirikiano walio uonesha wakati wa utendaji wake kazi katika hafla ya  kumuaga na kumkaribisha Mkurugenzi Mtendaji  Mpya wa Kampuni hiyo Paul Mhato iliyofanyika katika ukumbi wa Sea criff jijini Dar es Salaam. 
 Kutoka kushoto ni Mkurugenzi MtendajiMpya wa Kampuni ya Mafuta ya Engen Tanzania, Paul Mhato akifurahia  jambo  katika hafra  ya kumkaribisha Mkurugenzi mpya wa kampuni hiyo na kumuaga Mkurungenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mafuta Engen hapa nchini, Mubita Akapelwa   aliee maliza muda wakekatikati kulia ni Meneja Utawala Kampuni ya Mafuta Engin  Tanzania Shannel Sihuimba.
 Kushoto ni Mkurungenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mafuta ya Engen Tanzania, Mubita Akapelwa   aliemaliza muda wakeakipeana mkono wa shukurani na  Meneja Masoko wa Kampuni ya Mafuta EnginTanzania Shabaani Kajungilo.
 Mkurungenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mafuta ya Engen Tanzania, Mubita Akapelwa   aliemaliza muda wake  wa kufanya kazi katika kampuni hiyo (kushoto)akipokea zawadi kutoka kwa  Msaidizi wa Mkurungenzi wa  Kampuni ya Mafuta ya Tanzania ya Engen  Donathi Mbarara.
Mkurungenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mafuta ya EngenTanzania, Mubita Akapelwa   aliemaliza muda wake  akiwa katika picha ya pamoja na Baadhi  ya wafanyakazi wa Kampuni hiyo.
  Picha na Emmanuel Massaka.
Viewing all 110186 articles
Browse latest View live




Latest Images