Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (wa pili kushoto), akishiriki kupalilia katika shamba la dengu la mwanakijiji cha Manawa, Kata ya Misasi, Luhoyo Mwilima (Wa tano kulia), akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM na Uhai wa Chama katika jimbo la Misungwi mkoani Mwanza, leo.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana,Leo aliendelea na ziara yake katika jimbo la Misungwi linaloongozwa na Mh. Charles Kitwanga ambaye pia ni naibu Waziri wa Nishati na Madini akitembelea maeneo mbalimbali na kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010-2015, inayotekelezwa na serikali ikiwa ni pamoja na kusikiliza kero mbalimbali zinazowakabili wananchi ili kuzipatia ufumbuzi.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akikatiza katika kijiji cha Mahando,mara baada ya kuweka jiwe la msingi katika Ofisi ya CCM tawi la Kijiji cha Mahando, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM na uhai wa Chama katika jimbo la Misungwi mkoani Mwanza leo.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akimueleza jambo Mbunge wa Jimbo la Misungwi Dkt.Charles Kitwanga,walipokwenda kuwasalimia Mama Lishe na kuzisikiliza changamoto zao na namna ya kuwasaidia kwa namna moja ama nyingine.
Wananchi wa kijiji cha Nyang'homango wakimshangilia Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana alipowahutubia katika kijiji hicho ,wilayani Misungwi mkoani Mwanza.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezo Nape Nnauye akiwahutubia na kuwasalimia wakazi wa kijiji cha Nyang'homango waliokusanyika kwa wingi ,ikiwemo pia kumsilikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana
Mbunge wa jimbo la Misungwi Dkt.Charles Kitwanga akiwasalimia wananchi katika kijiji cha Nyang'homango,wilayani humo.
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana (wapili kulia) akisindikizwa kwa ngoma ya Sungusungu, alipokuwa akienda kuzindua Ofisi ya CCM na kuzungumza na wananchi katika Kijiji cha Mahando, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya CCm na Uhai wa Chama katika jimbo la Misungwi mkoani Mwanza leo.
PICHA NA MICHUZI JR-MISUNGWI,MWANZA