Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110170 articles
Browse latest View live

Exciting New Telenovela Channel Eva Launches Only on DStv in Africa

$
0
0
MultiChoice Africa is excited to announce the launch of Eva, a brand new telenovela channel made for Africa by AMC Networks International – Zone (AMCNI Zone). The channel is set to go live across Africa on Monday, 23rd of March on DStv channel 141.

Eva will bring the sizzle to DStv Premium, Compact Plus and Compact subscribers’ television screens with their line up of hot Latin American telenovelas fully dubbed in English. Viewers who enjoy their life with added spice will be treated to a potent mix of love, jealousy and betrayal in the shape of high quality serial dramas. The new addition to DStv will launch with a host of high production value programmes including Prisoner of Love (Amor Cautivo), a saga about three families, the Santacruz, Bustamante and Del Valle who are united by a terrible secret, that premieres on Monday, 23rd March at 18:00 CAT, then every weekday at 12:00 CAT.

The channel also offers three first run episodes of telenovelas every weekday with omnibus episodes at weekends. These include: The Perfect Woman (La Mujer Perfecta) - a story of six women who do everything in their might to become “perfect,” on air from Monday, 23rd March at 23:00 CAT, and will continue weekdays at 17:00 CAT. The others are bold and romantic programmes bursting with passion - The Swindler (El Encantador) and Timeles Love (Vivir Destiempo).

“We’re delighted with the addition of this new channel Eva that was developed with the African viewer in mind. This move forms part of our ongoing commitment to adding unparalleled, quality world-class entertainment to the DStv platform,” says Nico Meyer, CEO of MultiChoice Africa. “We trust this channel will bring more excitement to our viewers’ television experience with its lineup of star-studded telenovela content.”

Louise Cottrell, Vice President, Affiliate Sales for AMCNI Zone adds: “We have worked with DStv for many years and have several channel brands carried on the DStv platform, and we have always known that romance and telenovelas would be a perfect fit for the marketplace too. So it is incredibly exciting to be able to introduce Eva to Africa, a fresh and up to date television channel dedicated to romance and all its associated drama – in English and Portuguese languages.”

Eva will be available to DStv Premium, Compact Plus, Compact subscribers from 23 March 2015 at 17:30 CAT on DStv Channel 141.

For more information on Eva, visit www.dstv.com.

JARIDA LA WIKI NISHATI NA MADINI TOLEO LA 58

JUMUIYA YA VIJANA WA CHAMA CHA MAPINDUZI (UVCCM) MKOA WA KILIMANJARO WAKUTANA JIMBO LA VUNJO

$
0
0
Kamanda Msaidizi wa Jumuiya ya Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) wilaya ya Moshi Vijijini ,Innocent Mellecky akizungumza katika kikao hicho kilicho shirikisha wenyeviti wote wa jumuiya hiyo mkoa wa Kilimanjaro.
Baadhi ya wajumbe wa Jumuiya hiyo.
Mwenyekiti mstaafu wa Jumuiya ya Vijana wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Kilimanjaro,Godliving Mushi akizungumza katika kikao hicho.
Kaimu katibu wa Jumuiya ya Vijana wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Kilimanjaro Joel Makwaia akizungumza jambo katika kikao hicho.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Vijana (UVCCM) mkoa wa Kilimanjaro Fredrick Mushi akizungumza katika kikao hicho. Picha zaidi BOFYA HAPA

USIKOSE KUFATILIA MICHEZO YA LIGI KUU YA UINGEREZA KUPITIA SUPERSPORT NDANI YA DSTV PEKEE

MSIPOKEE MAHARI ZA WATOTO WENU WAKIWA WANAFUNZI - MAMA SALMA KIKWETE

$
0
0
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiongea na wananchi wa Kijiji cha Bweni katika Kata ya Kanga waliofika shuleni hapo kwa ajili ya kusalimiana naye.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiongea na wananchi wa Kijiji cha Bweni katika Kata ya Kanga waliofika shuleni hapo kwa ajili ya kusalimiana naye.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiongea na wananchi wa Kijiji cha Bweni katika Kata ya Kanga waliofika shuleni hapo kwa ajili ya kusalimiana naye.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akifurahia zawadi alizopewa na akina mama wajasiriamali wa Kata ya Kanga huko Mafia mara baada ya kumaliza kuzungumza na wanafunzi na wananchi wa eneo hilo.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akifurahia zawadi alizopewa na akina mama wajasiriamali wa Kata ya Kanga huko Mafia mara baada ya kumaliza kuzungumza na wanafunzi na wananchi wa eneo hilo.

MH. PINDA AHUTUBIA MKUTANO WA MAAFA JAPAN

$
0
0
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akihutubia katika mkutano wa tatu wa dunia kuhusu upunguzaji wa hatari ya majanga duniani uliofanyika katika mji wa Sendai nchini Japan ambako alimwakilisha Rais Jakaya Kikwete Machi 14, 2015.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiwa katika mkutano wa tatu wa dunia kuhusu upunguzaji wa hatari ya majanga duniani uliofanyika katika mji wa Sendai nchini Japan ambako alimwakilisha Rais Jakaya Kikwete Machi 14, 2015. Kulia ni Naibu Waziri wa mambo ya Nje na ushirikiano wa Kimataifa, Mahadh Maalim na watatu kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mohamed Abood Mohamed. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

KUMBUKUMBU YA Marehemu ULLY HARUN KIWANGA

$
0
0
Bi. Pilly Mpenda na Familia ya watoto wa  marehemu Harun Kiwanga wanapenda kuwakaribisha katika Dua ya kumrehemu mpendwa wao ,Marehemu ULLY HARUN KIWANGA ambaye anatimiza mwaka mmoja toka kufariki kwake,hapo kesho siku ya Jumapili tarehe 15.3.2015 kuanzia saa 5 asubuhi nyumbani kwao Kinondoni Block 41. Karibuni sana

MREMA AENDELEA KUANDAMWA VUNJO,WANANCHI WACHANGA PESA KUMCHUKULIA FOMU INNOCENT MELLECKY WA CCM

$
0
0

Inocent Melleck akizungumza na baadhi ya wananchi waliojitokeza kumchangia fedha kwa ajili ya kuchukulia fomu za kuwania Ubunge katika jimbo la Vunjo.

Innocent Melleck akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wananchi hao waliojitokeza kumchangi fedha kwa ajili ya kugombea Ubunge katika jimbo la Vunjo.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

MBUNGE wa jimbo la Vunjo,Agustino Mrema(TLP) ameendelea kupata upinzani katika Jimbo lake baada ya baadhi ya wananchi kujitokeza hadharani na kumchangia pesa,Innocent Melleck Shirima kwa lengo la kumchukulia fomu wakati wa kugombea nafasi ya Ubunge kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi.

Tayari joto la uchaguzi mkuu wa mwezi Oktoba mwaka huu limeanza kushika kasi katika jimbo hilo baada ya Mwenyekiti wa Chama cha NCCR –Mageuzi,James Mbatia kuombwa na wananchi wa jimbo hilo kugombea nafasi ya Ubunge.


MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AIWAKILISHA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA KIUCHUMI NA MAENDELEO WA MISRI (EGYPT THE FUTURE).

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia katika mkutano wa Kiuchumi na maendeleo wa Misri, uliofunguliwa jana Machi 13, 2015 na Rais wa Misri, Abdel-Fattah El- Sisi, mjini Sharm El-Sheikh, Misri.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Wawekezaji wa Misri wanaotaka kuwekeza katika Sekta ya Viwanja Wilayani Mkuranga, wakati alipokutana nao kwa mazungumzo leo, Machi 14, 2015 mjini Sharm El- Sheikh, Misri,alikohudhuria mkutano wa Kiuchumi na maendeleo wa Misri, uliofunguliwa jana Machi 13, 2015 na Rais wa Misri, Abdel-Fattah El- Sisi, mjini Sharm El-Sheikh, Misri.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Rais wa Misri, Rais wa Misri, Abdel-Fattah El- Sisi, wakati walipokutana kwa mazungumzo baada ya mkutano huo, uliofanyika jana Machi 13, 2015 mjini Sharm El-Sheikh, Misri.

NHIF KUPIMA AFYA NA KUKUSANYA DAMU KWA USHIRIKIANO WA MPANGO WA TAIFA WA DAMU SALAMA KATIKA MIKOA SITA

$
0
0
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Michael Mhando akizungumza na Waandishi wa habari Dar es Salaam jana kuhusiana na zoezi la upimaji afya na kukusanya damu salama kwa ushirikiano na Mpango wa damu salama katika mikoa sita nchini. Kushoto ni Afisa Uhusiano wa Mpango wa taifa wa Damu Salama, Rajab Mwenda.
Baadhi ya maofisa wa NHIF walioshiriki mkutano huo na waandishi wa habari wakifuatilia kwa makini. 
**********

PAZI REUNION HOUSTON, TEXAS LEO KUWAKA MOTO WACHEZAJI WENGI NDANI YA NYUMBA

$
0
0
 Timu ya Pazi wanaume wakipata picha ya pamoja na mashabiki wao walipokua nyumbani kwa madikodiko ambaye pia ni mmoja wa waratimu wa tamasha hili la kumbukumbu ya timu hiyo iliyowika miaka mingi katika ukanda wa Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla. Tamasha hili lililobeba jina la Pazi Reunion litafikia tamati leo Jumamosi March 14, 2015 kwa mechi kadhaa na kuakumbuka na kuaenzi viongozi na wachezaji wa timu hiyo waliotangulia mbele ya haki.
 Pazi Queens wakiwa katika picha ya pamoja leo patakua hapatoshi.
Patrick Mwigula kutoka South Carolina na Atiki Matata kutoka Uingereza wachezaji wa Pazi waliowika miaka ya nyuma wakijadili mchezo wa leo kama walivyokutwa na kamera ya Vijimambo.

BOFYA HAPA KUONA PICHA ZAIDI

LOWASSA- NAWAPONGEZA KATIBU MKUU WA CCM,NDUGU KINANA NA NAPE KWA KAZI KUBWA WANAYOIFANYA YA KUKIIMARISHA CHAMA

$
0
0
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akilakiwa kwa furaha na Mbunge wa Jimbo la Monduli, Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa wakati wa mapokezi  yaliyofanyika Makuyuni, tayari kuanza ziara mkoani Arusha leo.ikiwa ni mwendelezo wa ziara ya kuimarisha uhai wa chama, kukagua miradi inayotekelezwa kwa kufuata Ilani ya Uchaguzi ya CCM, pamoja na kusikiliza kero za Wananchi na kuzitafutia ufumbuzi
Mhe. Lowassa amewafagilia Kinana na Nape kwa kazi nzuri wanaoifanya ya kuzunguka mikoa mbalimbali kwa ajili ya kuimarisha uhai wa chama ambapo alimshauri Ndugu Kinana kupunguza kasi wanayokwenda nayo kwani ni kubwa. Pia alisema hakuna katibu wa chama aliyefanya kazi kubwa ya kukiimarisha chama kama Kinana.
 Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye akisalimiana na Mbunge wa Jimbo la Monduli, Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa wakati wa mapokezi yaliyofanyika Makuyuni, tayari kuanza ziara mkoani Arusha leo.ikiwa ni mwendelezo wa ziara ya kuimarisha uhai wa chama, kukagua miradi inayotekelezwa kwa  kufuata Ilani ya Uchaguzi ya CCM, pamoja na kusikiliza  kero za Wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.
  Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akijadiliana jambo na Mbunge wa Jimbo la Monduli, Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa wakati wa mapokezi  yaliyofanyika Makuyuni, tayari kuanza ziara mkoani Arusha leo.ikiwa ni mwendelezo wa ziara ya kuimarisha uhai wa chama, kukagua miradi inayotekelezwa kwa kufuata Ilani ya Uchaguzi ya CCM, pamoja na kusikiliza kero za Wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.
  Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akizinduw mradi wa umeme vijini (REA) katika kijiji cha Lolkisale,Wilayani Monduli mkoani Arusha.
Pichani kulia,Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Mbunge wa jimbo la Monduli,Edward Lowassa (kushoto) wakishiriki kupaka rangi jengo la hospitali ya wilaya,jengo hilo hadi kukamilika linatarajia kutumia kiasi cha fedha shilingi bilioni tisa
 Pichani kulia,Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Mbunge wa jimbo la Monduli,Edward Lowassa (kushoto) wakishiriki kuweka vitofali katika jengo la hospitali ya wilaya,jengo hilo hadi kukamilika linatarajia kutumia kiasi cha fedha shilingi bilioni tisa.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na baadhi ya wakulima wa mpunga wakishiriki kwa pamoja upaliliaji wa shamba la Mpunga,Mto wa Mbu,wilaya Monduli mkoani Arusha.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (kushoto) akiwa sambamba na Mbunge wa jimbo la Monduli,Edward Lowassa wakitoka kushiriki kupalilia shamba la Mpunga,Mto wa Mbu wilayani Monduli mkoani Arusha.

PICHA NA MICHUZI JR-MONDULI

PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

Serengeti Global Services LTD a.k.a wazee wa kazi Presents....

MSAADA WA MATIBABU UNAHITAJIKA KWA KIJANA BARAKA RAMADHANI

JK AFANIKISHA HARAMBEE YA KUCHANGIA UJENZI WA CHUO KIKUU CHA TUMAINI, 1.6bn/- zapatikana usiku huu diamond jubilee hall dar es salaam

$
0
0
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Waziri wa Elimu na Ufundi Mhe. Anne Kilango Malecela, Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dr Alex Gehaz Malasusa, Mwenyekiti wa Harambee hiyo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Bw. Nehemia Mchechu na wachangiaji wakubwa katika harambee hiyo iliyofanyika usiku huu katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salaam ambapo jumla ya shilingi bilioni 1.6 kati ya shilingi bilioni 2 zinazohitajika zilipatikana. Michango hiyo ni ya kufanikisha upanuzi wa chuo hicho katika awamu ya pili.
 Rais Kikwete katika picha ya pamoja na wakuu wa majimbo ya KKKT, Wachungaji, Wainjilisti na wafanyakazi wa Parish na viongozi wengine
 Rais Kikwete katika picha ya pamoja na wakuu wa majimbo ya KKKT, Wachungaji, Wainjilisti na wafanyakazi wa Parish na viongozi wengine
 Rais Kikwete akipongezwa kwa kufanikisha harambee hiyo
Rais Kikwete katika picha ya pamoja na kamati ya maandalizi ya harambee hiyo iliyoongozwa na mwenyekiti wake Mzee Arnold Kilewo ( wa kwanza kulia mbele) baada ya harambee hiyo iliyofanyika usiku huu katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salaam ambapo jumla ya shilingi bilioni 1.6 kati ya shilingi bilioni 2 zinazohitajika zilipatikana. Michango hiyo ni ya kufanikisha upanuzi wa chuo hicho katika awamu ya pili.

ngoma azipendazo ankal - kindly sponsored by isumba lounge...live in action every friday & saturday nite with dj jd and fast eddie at the controls!

Serikali yaipongeza Vodacom kwa kuanzisha huduma ya Kilimo Klub

$
0
0
Naibu waziri wa Kilimo,Chakula na Ushirika Mheshimiwa Godfrey Zambi amezitaka taasisi na mashirika binafsi nchini kubuni mbinu za kuleta mapinduzi katika sekta ya kilimo nchini hususani kuwaendeleza wakulima wadogo ambao idadi yao kubwa wanaishi maeneo ya vijijini. 
 Mheshimiwa Zambi ametoa wito huo jana wakati akifungua kongamano la simu moja la Kilimo Klub lililoandaliwa na kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania na alisema kuwa kuna idadi kubwa ya wakulima wanaishi katika umaskini mkubwa na wanafikia hatua ya kuzalisha chakula cha kutosheleza mahitaji yao na familia zao. 
 “Tunataka kuwa na wakulima wanaofanya uzalishaji wenye tija,lakini bahati mbaya wakulima wengi waliopo wanaendesha kilimo kisicho cha kitaalamu huku wakiwa wanakabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwemo kukosa utaalamu wa kilimo,kukosa taarifa za masoko ya kuuzia mazao yao,kutokuwa na mbimu za biashara ,kutokuwa na sifa za kukopesheka kutoka taasisi za fedha na kuuza mazao yao kwa bei ndogo kutokana na kutokuwa na uwezo wa kuyasafirisha mpaka kwenye sehemu yenye soko kubwa.”Alisema Zambi. 
 Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Rene Meza alisema kuwa ikiwa na mtandao ulioenea kwa asilimia 90 ya Tanzania Vodacom imedhamiria kuwakwamua wakulima vijijini kupitia Kilimo Klub Rene alisema, “Kupitia Kilimo Klub wakulima watanufaika kwa namna mbalimbali na maisha yao kuwa murua kwa kuwa wataweza kupata mikopo rahisi na isiyo na urasimu,wataweza kupata taarifa za masoko na hali ya hewa na kupata ushauri wa kilimo na haya yote yanafanyika kwa njia rahisi kupitia simu zao za mkononi na nina imani wakulima wengi hususani wanaoishi vijijini watabadilika kutoka hali duni na kuwa na maisha bora zaidi” Meza aliongeza kusema kuwa mtandao wa Vodacom umesambaa asilimia 90 ya Tanzania na asilimia 40 ya vituo vyake vya kurusha mawasiliano vipo maeneo ya vijijini na huu ni mmoja ya mkakati wa kampuni wa kusambaza huduma za mawasiliano vijijini na kubuni huduma za kuwarahisishia maisha wakazi wa maeneo hayo ambao wanakabiliwa na changamoto mbalimbali katika maisha yao ya kila siku na nia na uwezo wa kufanya hivyo upo. 
 Alisema hivi sasa maelfu ya wakulima nchini kupitia Kilimo Klub wanaweza kutuma na kupokea fedha kupitia huduma ya M-Pesa na kujiwekea na kupata mikopo nafuu kutoka huduma ya M-Pawa “Huduma hii ya M-Pawa ni tumaini jipya la wakulima vijijini na hadi kufikia sasa tangu ianzishwe mapema mwaka jana maelfu ya wakulima wamejiunga nayo na zaidi ya bilioni 2.5 zimewekwa kama akiba na zaidi ya milioni 500 zimekuwa zikitolewa kwa mkopo kila mwezi. Mpango wa Kilimo Klub ambayo umelenga kubadilisha maisha ya wakulima kuwa murua unaendeshwa kwa ubia kati ya Vodacom Tanzania na taasisi za Connected Farmers Alliance na Techno Serve.
 Naibu Waziri wa Kilimo na Chakula,Mh.Godfrey Zambi(kushoto)akipeana mikono na na Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania, Rene Meza wakati wa kuzindua warsha ya Kilimo Klub iliyoandaliwa na kampuni hiyo iliyolenga kushirikisha wadau mchango wa kampuni hiyo katika kuendeleza sekta ya kilimo kupitia mtandao wake na kujenga msingi wa ushirikiano kati ya wadau hao ili kuendeleza  sekta hii muhimu nchini.Warsha hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam ilishirikisha wadau mbalimbali wa sekta hiyo.
 Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania, Rene Meza(kushoto)akimwelezea jambo Naibu Waziri wa Kilimo na Chakula,Mh.Godfrey Zambi,wakati akiwasili kufungua warsha ya Kilimo Klub iliyoandaliwa na kampuni hiyo iliyolenga kushirikisha wadau mchango wa kampuni hiyo katika kuendeleza sekta ya kilimo kupitia mtandao wake na kujenga msingi wa ushirikiano kati ya wadau hao ili kuendeleza  sekta hii muhimu.Warsha hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam ilishirikisha wadau mbalimbali wa sekta hiyo.
 Naibu Waziri wa Kilimo na Chakula,Mh.Godfrey Zambi akifafanuliwa jambo  na  Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania, Rene Meza(kushoto) kuhusiana na huduma ya M Pawa alipofika kuzindua warsha ya Kilimo Klub iliyoandaliwa na kampuni hiyo iliyolenga kushirikisha wadau mchango wa kampuni hiyo katika kuendeleza sekta ya kilimo kupitia mtandao wake na kujenga msingi wa ushirikiano kati ya wadau hao ili kuendeleza  sekta hii muhimu nchini.Warsha hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam ilishirikisha wadau mbalimbali wa sekta hiyo.
Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania, Rene Meza(kulia) akiteta jambo na Naibu Waziri wa Kilimo na Chakula,Mh.Godfrey Zambi,wakati warsha ya Kilimo Klub iliyoandaliwa na kampuni hiyo iliyolenga kushirikisha wadau mchango wa kampuni hiyo katika kuendeleza sekta ya kilimo kupitia mtandao wake na kujenga msingi wa ushirikiano kati ya wadau hao ili kuendeleza  sekta hii muhimu.Warsha hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam ilishirikisha wadau mbalimbali wa sekta hiyo.

 Naibu Waziri wa Kilimo na Chakula,Mh.Godfrey Zambi,akizungumza na wadau mbalimbali wa Kilimo nchini wakati wa warsha ya Kilimo Klub iliyoandaliwa na Vodacom Tanzania iliyolenga kushirikisha wadau mchango wa kampuni hiyo katika kuendeleza sekta ya kilimo kupitia mtandao wake na kujenga msingi wa ushirikiano kati ya wadau hao ili kuendeleza  sekta hii muhimu.Warsha hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wadau walioshiriki warsha ya Kilimo Klub iliyoandaliwa na Vodacom Tanzania,wakijadiliana jambo wakati wa warsha hiyo iliyolenga kushirikisha wadau mchango wa kampuni hiyo katika kuendeleza sekta ya kilimo kupitia mtandao wake na kujenga msingi wa ushirikiano kati ya wadau hao ili kuendeleza  sekta hii muhimu nchini.Warsha hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam ilishirikisha wadau mbalimbali wa sekta hiyo.

uzinduzi cha chama NETEVE kinachojihusisha na mambo ya utamaduni wa Afrika nchini Ubelgiji

$
0
0
 Mheshimiwa Tim Vandenput Meya wa kitongoji cha Hoeilaart nchini Ubelgiji akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa chama cha NETEVE,wa kwanza kushoto ni Rais wa chama hicho Madame Oliva Butoyi akishuhudia uzinduzi huo.wengineo ni wanachama wanaounda umoja huo,Neteve ni chama kinachojihusisha na mambo ya tamaduni za nchi mbalimbali toka barani Africa.
Wanachama wa Neteve wakipiga makofi kushangilia uzinduzi rasmi wa umoja wao pale Mheshimiwa Tim Vandenput alipokata utepe kukizundua chama hicho rasmi.
Kikundi cha ngoma cha Amahoro kutoka Rwanda kikitumbuiza kwenye sherehe za uzinduzi wa chama cha Neteve nchini Ubelgiji. Picha zaidi BOFYA HAPA

Ziara ya mafunzo kutoka U.S. Army War Collage ofisi za Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania umoja wa mataifa

$
0
0
Mhe. Balozi Tuvako Manongi mwishoni mwa wiki alikutana na ujumbe wa wanawajeshi wanafunzi kutoka chuo cha Kijeshi (U.S. Army War Collage) ambao walikuwa katika ziara ya mafunzo. Miongoni mwa wanafunzi yupo Luteni Kanali Juma Sipe kutoka JWTZ. Ungeni huo ulitumia ziara hiyo kujifunza masuala mbalimbali yanayoihusu Tanzania kitaifa na kimataifa na uwepo wake kama nchi mwanachama wa Umoja wa Mataifa,
Mhe. Balozi akielezea jambo mbele ya  kikundi  cha wanajeshi wanafunzi  ambao wapo katika  mafunzo  katika chuo cha U.S Army War Collage, wanafunzi hao walipata fursa ya kumuuliza Balozi maswali mbalimbali na ambayo yalijibiwa kwa ufasaha na  Mhe. Balozi
Kiongozi wa Msafara akitoa zawadi yao kwa Mhe. Balozi kama kumbukumbu  na shukrani yao kwa kupokelewa na kwa Balozi kutenga muda wake kukutana nao.
Mhe. Balozi Tuvako  Manongi akiwa katika picha ya pamoja na Wanajeshi kutoka U.S Army War Collage,  miongoni mwa wanafunzi hao ni Mtanzania Luteni Kanali Juma Sipe kutoka JWTZ
Mhe. Balozi Manongi akiteta jambo na Luteni Kanali Juma Sipe  kutoka JWTZ ambayo  yuko mafunzoni U.S Army War Collage hapa Marekani

TASWIRA KUTOKA UMOJA WA MATAIFA JIJINI NEW YORK

$
0
0
Wajumbe wanaohudhuria Mkutano wa 59 wa Kamisheni kuhusu Hadhi ya Wanawake, kwa wiki kuanzia jumatano hadi Ijumaa wameendelea na jukumu kubwa la kujadiliana, kuhabaridha,a kubadilishana uzoefu, kuelimisha na hata kujifunza namna ya kuzikabilia changamato mbalimbali ambazo mwanamke na mtoto wea kike wanaendelea kukabiliana nazo. 
Mkutano huu wa mbao ni wa waki mbili unafanyika sambamba na maadhimisho ya miaka 20 tangu kufanyika kwa mkutano wa kihistoria wa wanawake uliofanyika mwaka 1995 huko Beijing, China. 
 Ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wenye wajumbe kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar unaongozwa na Mhe. Sophia Simba ( Mb) Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto na umekuwa ukishiriki majadiliano ya jumla na mikutano ya pembezo iliyobeba maudhui mbalimbali lakini yote yakilenga katika usawa wa jinsia na uwezeshwaji wa mwanamke.
 Mhe. Waziri   Simba akisalimiana na  First Lady wa Kenya Mama Margaret Kenyatta, First Lady huyu   hukimbia mbio za marathon kama njia moja wapo ya kufatua  raslimali za kuwasaidi akina mama wenzie na watoto walio katika mazingira magumu.
Mhe. Waziri  Simba  na  Balozi Tuvako Manongi wakibalishana mawazo
Pamoja na kuhudhuria mbalimbali inayohusianana Kimesheni   Kuhusu Hadhi ya Wanawake,   Mwakilishi wa Kudumu wa wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa,  alipata fursa ya kuwapokea na kuzungumza na wageni mbalimbali waliofika katika Uwakilishi wa Kudumu. Balozi Manongi akiwa na Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao walikuwa  Jijini  New York  kwa shughuli za Kikazi.  
" Utanzania na uzalendo kwanza" ndivyo anavyoelekea kusema Mhe. Susan Lymo wakati yeye na wabunge wenzie   walipofika katika Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataif.
Mhe. Waziri Sophia Simba  akiwa na  Mbunge wa Kawe Mhe. Halima Mdee,  Katibu Mkuu Anna Maembe, na Balozi  Tuvako Manongi katika moja wa  mikutano ya pembezoni iliyokuwa  inakwenda sambamba na  majadiliano  ya jumla ya Kamisheni ya 59. Mkutano huu  uliandaliwa na  Mke wa Rais wa  Kenya Mama, Margaret Kenyata,  ambapo alitumia fursa hiyo kuelezea shughuli anazozifanya  za kuwasaidia wanawake  na watoto wa nchi mwake hasa wale walio katika mazingira magumu. Kampeni yake inayoitwa Beyond Zero inalenga katika kufikisha huduma za afya  
Viewing all 110170 articles
Browse latest View live




Latest Images