Jeneza lililobeba mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Mbinga Magharibi na Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM marehemu John Damiano Kumba ukipokelewa katika uwanja wa ndege wa Songe na umati mkubwa wa waombolezaji wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma,Mhe.Mwambungu,Mhe.John Nchimbi,Mbunge wa Songea Mjini,na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais(Kazi Maalum)Mark Mwandosya,kulia. Marehemu anatarajiwa kuzikwa kijijini kwake Lituhi, Wilaya ya Nyasa, Kesho.
mwili wa hayati kepteni John Damiano Komba wawasili Songea
↧
↧
Benki ya Exim yakarabati kituo cha watoto wenye ulemavu Morogoro
Meneja wa Benki ya Exim Tawi la Morogoro, Bi Anna Wesiwasi (wapili kulia) akipeana mkono na Mkurugenzi wa Kituo cha Amani cha watoto wenye ulemavu, Padri Beatus Sewando (watatu kulia) mara tu baada ya kuzindua jengo la kituo hicho kilichokarabatiwa na benki hiyo jana mkoani Morogoro. Akishuhudia ni Afisa Mauzo wa Benki hiyo Vick Haji (Kulia).
Na Mwandishi wetu, Morogoro
BENKI ya Exim Tanzania imefanya ukarabati wa majengo ya kituo cha watoto wenye ulemavu cha Amani kilichopo eneo la Chamwino mkoani Morogoro ikiwa ni muendelezo wa jitihada za benki hiyo kuboresha maisha ya jamii.
Kupitia sera yake ya kurudisha sehemu ya faida yake kwa jamii, benki hiyo pia imejipanga kutoa misaada zaidi ikilenga mipango yenye kuleta maendeleo kwa jamii hapa nchini hususani katika maeneo ambayo benki hiyo tayari imefungua matawi yake.
Akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi vifaa vya ukarabati wa majengo ya kituo hicho iliyofanyika mkoani humo mwishoni mwa wiki iliyopita, Meneja wa tawi la benki hiyo mkoani Morogoro, Bi Anna Wesiwasi alisema msaada huo pia unalenga uboreshaji wa maisha ya watoto wanaoishi kwenye kituo hicho kwa kuwa wataishi kwenye makazi salama, safi na bora kwa afya zao.
“Benki ya Exim siku zote tunaamini kuwa watoto wenye ulemavu wanahitaji kupewa matumaini zaidi na kwa kushiriki kwetu kwenye mipango ya maendeleo kama huu ndio tunatekeleza hiyo imani yetu kwa vitendo na zaidi tunazidi kuwa karibu na jamii inayotuzunguka jambo ambalo ni muhimu katika ulimwengu wa kibiashara kwa sasa kuona kwamba benki inarudisha sehemu ya faida yake kwa watu inao wahudumia,'' alisema Bi Wesiwasi
Kwa mujibu wa Bi Wesiwasi, benki hiyo inaamini kuwa watoto ndio wateja wao wa kesho kama sio wa sasa na hivyo basi benki hiyo itajitoa kwa hali na mali kuhakikisha kwamba wanapata maisha bora kwa sasa .
Akizungumza mara baada ya kupokea msaada huo, Mkurugenzi wa kituo hicho, Padri Beatus Sewando alisema uamuzi wa benki hiyo kusaidia kituo cha watoto wenye ulemavu ni kitendo kinachotakiwa kuigwa na taasisisi, mashirika na watu mbalimbali hapa nchini.
“Tunashukuru sana kuona wenzetu wa benki ya Exim wameonyesha mfano kwa kuitikia kilio chetu.Msaada huu utawahakikishia watoto wetu hapa kituoni kuwa na makazi bora na salama kwaa afya zao…naomba wengione waige mfano huu,’’ alitoa wito
↧
MAKALA YA SHERIA: USIFANYE MAKOSA, HUU NDIO UTARATIBU WA KUNUNUA NYUMBA ILIYOWEKWA REHANI/DHAMANA BENKI
Na Bashir Yakub
Nimewahi kuandika mara kwa mara kuhusu utaratibu mzuri wa kumwezesha mtu kununua nyumba huku akiwa ameepuka mgogoro. Nilitahadharisha sana kuhusu migogoro ya ardhi ambayo sasa imekuwa janga la kitaifa hapa kwetu. Nakumbuka moja kati ya mambo niliyoeleza ni kuwa utaratibu wa manunuzi ya nyumba/viwanja unatofautiana.Nikasema kwamba tofauti zake zinatokana na ukweli kuwa kila nyumba ina mazingira yake. Hata hivyo sikusema utofauti wa mazingira hayo ila sasa naweza kueleza kwa ufupi utofauti wa mazingira ya kila nyumba unapokuwa katika taratibu za ununuzi.
1.UTOFAUTI WA KITAALAM KATIKA UNUNUZI NYUMBA.
Usikurupuke unapohitaji kununua ardhi. Unapaswa kujua kuwa nyumba na viwanja zina taratibu tofauti unapohitaji kununua. Ukikurupuka utalipia gharama ya kukurupuka kwako. Kutokana na hilo ni muhimu tujue kuwa kuna nyumba inayouzwa kwa utaratibu wa kawaida wa mmiliki mwenyewe kumuuzia mnunuzi. Hii mara nyingi huwa haina shida sana kwakuwa unahitaji tu kujiridhisha na baadhi ya mambo ya msingi kama kufanya upekuzi rasmi ( official search) katika mamlaka za ardhi n.k.
Pili kuna nyumba inayouzwa na wasimamizi wa mirathi. Hii uuzwaji wake hauko sawa na ile inayouzwa na mmiliki halisi. Hawa ni wasimamizi wa mirathi hivyo hata uuzaji wao si uuzaji kama wa mmliki halisi. Utofauti wao upo katika namna ya kuandika mkataba( sale agreement) na nyaraka ambazo wanapaswa kukuonesha wewe mnunuzi . Pia kuna ununuzi wa nyumba ya mkopo ambao sasa ndio mada ya leo. Ununuzi wa nyumba ya mkopo nao si ununuzi kama wa nyumba ya kawaida. Haufanani na nyumba ya kawaida na haufanani na wa nyumba ya mirathi. Unazo tarati bu zake tofauti kabisa na ununuzi mwingine.
2.UMUHIMU WA KUZINGATIA UTARATIBU UNAPONUNUA NYUMBA YA DHAMANA.
Tatizo kubwa linakuja kuwa unaponunua bila kuzingatia utaratibu pia uwe tayari kupoteza. Ieleweke kuwa nyumba au ardhi yoyote ni kitu ambacho hudumu milele. Hivyo kama utakosea utaratibu hata kwa kiwango kidogo basi ya kutosha kuishi bila amani maisha yako yote. Kama si wewe watakuwa watoto wako na kama si watoto wako watakuwa wajukuu wako. Kati ya hawa kuna mmoja mgogoro utamkuta kwa makosa uliyoyafanya wewe. Na ubaya wa mgogoro unapotokea mahakama kikubwa inachokifanya ni kuangalia nani alikosea taratibu. Inaangalia hilo kwasababu yenyewe inakuwa haipo wakati mnauziana na hivyo nyote haiwajui na haijui kati yenu nani mkweli na nani muongo.
Kwahiyo kama ni wewe mnunuzi uliyekosea taratibu wakati wa kununua basi hakuna kingine ila kupoteza bila kujali gharama ulizotumia katika manunuzi. Lakini ikiwa ulifuata taratibu kwa umakini kwanza ni vigumu kuingia katika mgogoro lakini hata bahati mbaya uingie katika mgogoro basi ushindi utakuwa ni wa kwako. Huu ndio umuhimu wa kuhakikisha unafuata taratibu. Zingatia maeneo mawili kwanza uandaaji wa mkataba na pili ukaguzi na uhakiki wa nyaraka.
↧
DKT. TITUS KAMANI ATEMBELEA MAONESHO YA KIMATAIFA YA KILIMO NCHINI UFARANSA
Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi,Mhe. Dkt. Titus Kamani akitembelea mabanda ya maonesho ya kimataifa ya kilimo yanayofanyika katika Jiji la Paris nchini Ufaransa,na kujionea aina ya mifugo inayoshindanishwa. Hapa anaangalia ng'ombe wa nyama aina ya Charolaise.
Mhe. Dkt. Kamani akiangalia kondoo wa sufi waliopo kwenye mabanda ya maonesho.
Umati wa watu kutoka mataifa mbalimbali duniani waliohudhuria maonesho hayo. Takriban watu milioni moja wametembelea maonesho hayo kwa mwaka huu 2015 ambayo hufanyika kwa muda wa siku tisa.
Mhe. Dkt. Kamani pamoja na ujumbe wa watanzania wakisikiliza kwa makini maelezo ya maendeleo ya sekta ya mifugo nchini Ufaransa na mfumo wa uendeshaji wa maonesho ya kimataifa ya kilimo kabla ya kupata fursa ya kutembelea mabanda mbalimbali.
↧
USIKOSE KUFATILIA MICHEZO YA LIGI KUU YA UINGEREZA KUPIA SUPERSPORT NDANI YA DSTV
↧
↧
RAIS KIKWETE AAGANA NA BALOZI WA JAPAN
↧
KATIBU MKUU WA CCM NDUGU ABDULRAHMAN KINANA AWASILI MKOANI RUVUMA KUSHIRIKI MAZISHI YA MAREHEMU KAPTENI KOMBA
↧
MESSAGE ON WORLD WILDLIFE DAY
The United Nations General Assembly has proclaimed 3 March – the anniversary of the adoption of the Convention on International Trade in Endangered Species of Wild Fauna and Flora (CITES) – as World Wildlife Day. On this second observance of the Day, the UN system, its Member States and a wide range of partners from around the world are highlighting the simple yet firm message that “It’s time to get serious about wildlife crime”.
Illegal trade in wildlife has become a sophisticated transnational form of crime, comparable to other pernicious examples, such as trafficking of drugs, humans, counterfeit items and oil. It is driven by rising demand, and is often facilitated by corruption and weak governance. There is strong evidence of the increased involvement of organized crime networks and non-State armed groups.
Illegal wildlife trade undermines the rule of law and threatens national security; it degrades ecosystems and is a major obstacle to the efforts of rural communities and indigenous peoples striving to sustainably manage their natural resources. Combatting this crime is not only essential for conservation efforts and sustainable development, it will contribute to achieving peace and security in troubled regions where conflicts are fuelled by these illegal activities.
Getting serious about wildlife crime means enrolling the support of all sections of society involved in the production and consumption of wildlife products, which are widely used as medicines, food, building materials, furniture, cosmetics, clothing and accessories. Law enforcement efforts must be supported by the wider community. Businesses and the general public in all countries can play a major role by, for example, refusing to buy or auction illegal ivory and rhinoceros horn, and insisting that products from the world’s oceans and tropical forests have been legally obtained and sustainably sourced.
On this World Wildlife Day, I urge all consumers, suppliers and governments to treat crimes against wildlife as a threat to our sustainable future. It’s time to get serious about wildlife crime.
↧
MAONYESHO YA SIKU YA WANAWAKE YA MKOA WA MOROGORO YAINGIA DOSARI BAADA YA MVUA KUBWA KUNYESHA
Mkurugenzi wa manispaa ya Morogoro, Bi. Theresia Muhongo akisikiliza maelezo kutoka kwa Haji Sajilo ambaye ni Kiongozi msimamizi wa Mipango wa NGO,s ya MOYODEI wakati alipotembelea kwenye mabanda yaliyoharibwa vibaya na mvua iliyonyesha jana jioni. Haya mabanda yalikuwa ni kwa ajili ya maadhimisho ya siku ya wanawake duniani iliyotakiwa kuanza leo jumanne lakini kutokana na maafa hayo maonyesho hayo yamesogezwa mpaka tarehe 5/03/2014 kwa ajili ya ukarabati wa mabanda hayo.(Picha na Pamoja Blog)
Mkurugenzi wa manispaa ya Morogoro, Bi. Theresia Muhongo akipata maelezo kutoka kwa mama kuhusu mabanda yaliyoezuliwa na mvua iliyokuwa na upepo mkali
Baadhi ya Mabanda yakiwa yameharibika vibaya
↧
↧
Hayati John Komba enzi za uhai wake akihojiwa na Salama Jabir katika kipindi cha mkasi pale pale amaya beauty spa jijini Dar es salaam
↧
HOTUBA YA RAIS JAKAYA KIKWETE YA MWISHO WA MWEZI WA FEBRUARI,2015
↧
WATU WANNE MBARONI AKIWEMO M/KITI WA KIJIJI CHA IHANDA WILAYANI KONGWA DODOMA KWA TUHUMA ZA MAUAJI YAKIHUSISHA IMANI ZA KISHIRIKINA
Na. Sylvester Onesmo/Dorice Kigombe wa Jeshi la Polisi Dodoma.
Watu watatu wameuawa Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma katika matukio mawili tofauti yanayohusisha imani za kishirikina.
Akizungumzia matukio Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi DAVID MISIME – SACP amesema tukio la kwanza limetokea tarehe 01/03/2015 majira ya saa 01:00hrs katika kitongoji cha Golani, kijiji cha Masinyeti, kata ya Iduo, tarafa ya Mlali Wilaya ya Kongwa Mkoani Dodoma ambapo mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la SAIDIA S/O CHAKUTWANGA mwenye miaka 80, kabila Mkaguru, Mkulima Mganga wa kienyeji aliuawa na watu waliojichukulia sheria mkononi kwa kupigwa na kitu kizito kichwani na kutobolewa macho.
Kamanda MISIME amesema uchunguzi wa awali unaonyesha chanzo cha mauaji hayo ni imani za kishirikina wakimtuhumu marehemu kuwa anazuia mvua kunyesha katika eneo hilo.
Pia Kamanda MISIME amesema katika tukio lingine limetokea tarehe 01/03/2015 majira ya saa 02:00hrs katika kitongoji cha Majengo, kijiji cha Ihanda, Kata na Tarafa ya Mlali Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma ambapo mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la PETER S/O KALULI mwenye miaka 85, kabila Mkaguru akiwa na mkewe aitwaye KAILA W/O KALULI mwenye miaka 80, Mkaguru wote wakulima na wakazi wa Kitongoji cha Majengo wakiwa wamelala ndani ya nyumba yao ya tembe, waliuawa na watu wasiofahamika kwa kuangushiwa ukuta wa nyumba yao kisha kuchoma moto na kubomoa nyumba mbili za tembe.
Watu hao walifanya uharibifu mwingine kwa kuwaua nguruwe mmoja na ng’ombe mmoja kumkata miguu.
Aidha Kamanda MISIME amesema uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa chanzo cha mauaji na uharibifu huo ni imani za kishirikina wakiwatuhumu marehemu kuwa wanazuia mvua kunyesha. Watuhumiwa wanne akiwemo M/Kiti wa Kijiji cha Ihanda na wazee wawili wa kimila wa kijiji wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kuhusiana na tukio hili kwani taarifa zinaonyesha waliandaa vikao vya kutekeleza mauaji haya. Upelelezi wa matukio yote mawili unaendelea ikiwa ni pamoja na kuwatafuta watuhumiwa wengine waliohusika na matukio haya.
Kamanda MISIME ametoa wito kwa wananchi kutochukua sheria mkononi na kujiepusha na imani za kishirikina zinazopelekea kuleta hofu na mashaka kwa jamii. Alisema ni jambo la aibu kwa jamii hadi karne hii watu kuamini kuwa kuna watu wanaoweza kuzuia mvua isinyeshe. Pia amewataka viongozi wa maeneo mbalimbali kutoa taarifa mapema polisi pale wanapoona mipango ya kihalifu kama hiyo ikipangwa.
↧
WATOTO WANAOISHI KWENYE MAZINGIRA MAGUMU JIJINI ARUSHA KUJENGEWA HOSTEL
Watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu jijini Arusha wanatarajiwa kujengewa Hostel zitakazowasaidia kuondokana na adha ya kupata sehemu za malazi hivyo kulazimika kulala maeneo ya stendi za mabasi na masoko.
Mkurugenzi wa shirika la Gola linalojihusisha na masuala ya watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu jijini Arusha,Sawale Maghema amesema kuwa mpango huo utasaidia watoto hao kuondokana na mazingira magumu yanayowapelekea kujiingiza katika vitendo vya uhalifu na matumizi ya madawa ya kulevya.
Sawale alisema kuwa iwapo watoto hao watatelekezwa na jamii bila kusaidiwa wanaweza kugeuka na kuwa mwiba kwa jamii ya Watanzania hivyo amewataka Watanzania kujitokeza kuwasaidia watoto hao .
"Watoto hawa tuna mpango maalumu wa kuwakusanya na kuwakutanisha pamoja kujua mahitaji yao ,malengo na matarajio waliyonayo ili kuwasaidia kwa kushirikiana na jamii hata kwa hili la ujenzi wa Hostel litasaidia kuwaweka pamoja tukiwaacha waendelee kukaa mitaani hawatabadilika wataendelea kuwa na maisha mabaya" Alisema Sawale
Mdau wa Masuala ya utalii Mustafa Panju alijitolea kuwasaidia watoto hao kwa kuchangia kiasi cha shilingi milioni 20 ili waweze kupata mahitaji muhimu ,Ameeleza kuwa jamii inapaswa kuamka na kuwasaidia watoto hao badala ya kuwaacha waendelee kukaa kwenye mazingira hatarishi.
Mwenyekiti wa Baraza la Watoto Arusha ,Hassan Omari akizungumza kwa niaba ya watoto wa mitaani anaeleza kuwa watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu wana ndoto nyingi,vipaji na uwezo wa hali ya juu hivyo wakisaidia wanaweza kufika mbali na kulisaidia taifa .
Chanzo:libeneke la kaskazini blog
Kikundi cha ngoma cha watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu wakitumbuiza katika shughuli ya kuwakusanya watoto wa mitaani iliyofanywa na taasisi ya GOLA Foundation inayolenga kuwasaidia watoto hao kukabiliana na changamoto za ukosefu wa malazi,chakula,mavazi na pia elimu.Jamii inaombwa kujitokeza kusaidia watoto hao
Baadhi ya Watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu jijini Arusha waliokusanywa na taasisi ya GOLA Foundation inayolenga kuwasaidia watoto hao kukabiliana na changamoto za ukosefu wa malazi,chakula,mavazi na pia elimu.Jamii inaombwa kujitokeza kusaidia watoto hao
Chanzo:libeneke la kaskazini blog
↧
↧
MKUU MPYA WA WILAYA YA NGORONGORO AAPISHWA
Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro Hashimu Shaibu akila kiapo cha utumishi mbele ya Mkuu wa mkoa wa Arusha Daudi Felix Ntibenda jana katika hafla iliyofanyika katika Ofisi za Mkuu wa Mkoa huyo
chanzo libeneke la kaskazini blog |
↧
Halmashauri ya mji wa Kahama yapokea ushuru wa asilimia 0.3 kutoka mgodi wa Buzwagi
Kampuni ya ACACIA kupitia mgodi wake wa Buzwagi uliopo kwenye halmashauri ya mji wa Kahama,imeipatia ushuru wa asilimia 0.3 (0.3%) ya mapato ghafi halmashauri hiyo,ikiwa ni ushuru kwa kipindi cha miezi sita (Julai - Disemba,2014) ambayo ni zaidi ya shilingi za kitanzania millioni 800,uliokabidhiwa kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Kahama.
Kaimu Meneja Mkuu wa mgodi wa Buzwagi ulio chini ya Kampuni ya ACACIA,Ing. Mutereko Muganda (wa pili kushoto) akikabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya zaidi ya shilingi za kitanzania millioni 800 kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Kahama Bw. Felix Kimaryo (kulia) nje ya ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kahama,Mh. Benson Mpesya (wenye tai).
↧
TAASISI ya kifedha ya Bayport Financial Services yazindua tawi lake jipya wilayani Kwimba jijini Mwanza
TAASISI ya kifedha ya Bayport Financial Services inayojihusisha na mambo ya mikopo imepongezwa na serikali kwa hatua yake ya kufungua tawi wilayani Kwimba mkoani Mwanza.
Meneja Mauzo wa Taasisi ya Kifedha ya Bayport Financial Services Kanda ya Ziwa, Lugano Kasambala, akimuelekeza jambo Katibu Tawala wa Wilaya Kwimba, Vicent Emmanuel, katika uzinduzi wa tawi jipya wilayani humo, uliofanyika Machi 2 mwaka huu. Wengine ni maofisa wa taasisi hiyo, Ramadhan Hanafi na Monica Mwangoka. Picha na Mpigapicha Wetu.
Shughuli za uzinduzi huo zilifanyika Machi 2 mwaka huu, huku mgeni rasmi akiwa ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Kwimba, Vicent Emmanuel, akiongozana na viongozi mbalimbali wa serikali wilayani humo.
Katibu Tawala wa wilaya ya Kwimba, Vicent Emmanuel, kushoto akikata utepe kuashiria kuzindua rasmi tawi jipya la taasisi ya kifedha ya Bayport Financial Services, wilayani Kwimba, mkoani Mwanza. Kulia ni Meneja Mauzo wa taasisi hiyo Kanda ya Ziwa, Lugano Kasambala. Picha na Mpigapicha Wetu.
Akizungumza katika uzinduzi huo, Katibu Tawala huyo wa wilaya Kwimba, Emmanuel alisema kwamba kufunguliwa kwa tawi hilo kutatoa huduma karibu na wananchi, kama njia ya kukuza uchumi wao kwa ujumla, zikiwapo fursa za kukopeshwa bidhaa mbalimbali, vikiwamo vyombo vya usafiri.
Alisema kwamba awali watu wa Kwimba walilazimika kusafiri umbali mrefu kupata huduma za mikopo, lakini sasa wamesogezewa huduma karibu, hivyo ni jukumu lao kutumia fursa hiyo kwa ajili ya kujinufaisha kwa ajili ya maisha yao.
↧
WAFANYAKAZI WA SEKTA YA AFYA ZANZIBAR WAPEWA MAFUNZO JINSI YA KUKABILIANA NA UGONJWA WA EBOLA
Mshauri wa mambo ya Afya kutoka Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa (WHO) Dk. Andemichael Ghirmay akitoa hutuba yake ya ufunguzi wa kuwajengea uwezo wafanyakazi wa sekta ya Afya Zanzibar kukabiliana na ugonjwa wa Ebola, mafunzo hayo ya siku tatu yanafanyika Hoteli ya Zanzibar Beach Resort na yamezaminiwa na WHO.
Mgeni rasmin Katibu Mkuu Wizara ya Afya Zanzibar Dkt. Mohammed Jidawi akifungua mafunzo ya siku tatu ya kuwajengea uwezo wafanyakazi wa sekta ya Afya Zanzibar kukabiliana na ugonjwa wa Ebola.
↧
↧
MAKALA YA SHERIA: JE UMENYANYASWA NA MWAJIRI, HII NI NAMNA YA KUMFUNGULIA MASHTAKA
NA BASHIR YAKUB
Makuzi ya biashara hasa biashara za kimataifa yameleteza utitiri wa makampuni. Karibia kila biashara kubwa au ya kati kwa sasa hufanywa na makampuni. Baadhi ya ndani na mengine ya nje.
Hatua hii njema kwa kiasi fulani imeongeza ajira japo ajira zenyewe hazina vigezo vya kuitwa ajira. Yatosha ziitwe kazi tu. Ajira hizi ambazo nyingi ni za umanamba zimekuwa zikifanywa na wazawa. Upande mmoja zimekuwa neema na upande mwingine zimekuwa laana.
Ni neema kwakuwa baadhi wanaweza kuishi japo kwa pato la mlo tu na kusiwe na akiba yoyote lakini pia zimekuwa laana kwakuwa ukihadithiwa baadhi ya mambo yanayoendelea huko waweza toa chozi.
Sio pote ila yapo maeneo yaliyoshindikana kama viwandani, migodini, miradi ya barabara na kwingineko waliko wawekezaji hasa wa kigeni. Hili ndilo limenituma kuandaa makala haya ili basi wenye fursa wasome na waelewe na wenye kutaka msaada waweza kuwasiliana nami na kuona la kufanya.
Nianze hivi, kampuni kwa mujibu wa sheria ni mtu( legal person). Kuna tofauti kubwa kati ya kampuni na mmiliki wake. Kisheria kampuni ikifanya kosa yatakiwa ishitakiwe kampuni na sio wamiliki au mfanyakazi kama mameneja, mkurugenzi n.k.
Nimewaona wengi hasa vijana ambao huyadai makampuni haki zao hufungua kesi wakiwashitaki wamiliki au mabosi wao. Hili ni kosa kubwa na wengi wao huwa wanashindwa zile kesi na badala yake kuanza kulalamikia mfumo wa nchi , mahakama au viongozi na hata chama tawala.
Ndugu hili halikusaidii. Hili sio la serikali wala rais wala nani ni suala ka kisheria. Kampuni yako imekukosea unataka kudai fidia umemshtaki mmilki au viongozi badala ya kampuni, ni lazima utashindwa kesi usimtafute mchawi wala kulalama kwa tuhuma za rushwa. Unapokosea taratibu sheria haina huruma inakata. Upo msemo usemao ( A law is a merciless sword) yaani sheria ni upanga usio na huruma unamkata yeyote anayeuchezea. Kampuni kama kampuni inao uwezo wa kushtaki kwa jina lake na kushtakiwa kwa jina lake,namna gani tutaona hapo chini.
↧
NGOMA AFRICA BAND KUTUMBUIZA LIVE MJINI STUTTGART,GERMANY
Bendi ya maarufu barani ulaya Ngoma Africa Band aka FFU-Ughaibuni aka Anunaki aliens bendi hiyo inatarajiwa kutumbuiza katika onyesho maalumu la AFRICA UNITE PARTY litakalofanyika katika ukumbi wa VTS uliopo mtaa wa Augusburger Str.442 D-70327 mjini Stuttgart,nchini Ujerumani.Onyesho hilo limeandaliwa na shirika la Afrikaktiv e.V wakishirikiana na shirika la Cabaret du Monde, Ngoma Africa band iliyozoeleka kwa kuwatia kiwewe washabiki wake kila kona duniani wataporomosha muziki moto moto na mdundo wao maarafu kama " Extraordinary Bongo Dansi" mdundo unaotingisha bila ya kuwa na mpinzani huko ughaibuni, bendi hiyo inadumu katika medani ya muziki kwa muda wa miaka 23 na kufanikiwa kujizolea washabiki kila kona. Ticket za onyesho hilo zinapatikana kwa simu ( booking): Call9+49 0)152 12091242 au +49(0)152 106106137 Mnakaribishwa wote,pia usikose kuwasikiliza FFU-Ughaibuni at www.ngoma-africa.com
↧
KAMATI YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI YAFANYA ZIARA KATIKA MITAMBO YA KUFUA UMEME YA KINYEREZI 1
Mkurugenzi wa Sera na Mipango kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Wanja Mtawazo ( kulia) akisalimiana na Mbunge wa Lulindi- Masasi, Jerome Bwanausi ( kushoto) ambaye ni mmoja wa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini mara baada ya kamati hiyo kuwasili katika eneo la mtambo wa kufua umeme wa Kinyerezi I. Kamati hiyo inafanya ziara katika miradi ya umeme katika mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma, Singida, Arusha na Kilimanjaro pamoja na kuzungumza na wadau wa madini ya tanzanite katika mkoa wa Manyara ili kujionea maendeleo ya sekta hizo.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini (Madini), Charles Kitwanga (kulia) akimsikiliza kwa makini Meneja Mradi Mkazi wa Kampuni ya Yakobsen Elektro ya Norway inayojenga mtambo wa Kinyerezi I Markkli Repo ( wa pili kutoka kushoto) mara baada ya kuwasili katika eneo la mtambo huo ili aweze kuwaongoza wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwenye ziara katika mitambo hiyo.
↧
More Pages to Explore .....