Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110175 articles
Browse latest View live

nani kasema ze fulanazzzz kwishney?

$
0
0
Ankal akitafakari baada ya mwenyeji wake kutotokea...

konozzzz na missie popular

$
0
0
Ankal akipata selfie na Missie Popular a.k.a MP, mmoja wa mabloga wakubwa wanawake nchini. Hapa ni katika sherehe za uzinduzi wa nyumba za makaazi za Shirika la Nyumba (NHC) za Medeli mjini Dodoma. Dada huyu ni mwanalibeneke wa siku nyingi na anajua anachokifanya. Keep it up Missie! Mtembelee BOFYA HAPA
Pia BOFYA HAPA

Introducing LONKA - "Beautiful Smile" (Official Video)

$
0
0
BRAND NEW VIDEO LONKA- BEUTIFUL SMILE (Official Video) directed By JACKSON JOACHIM IVES ENTERTAINMENT

Ngoma azipendazo ankal - Kindly sponsored by Isumba Lounge

$
0
0
"I'm Wishing on a Star" - Rose Royce

ORIJINO KOMEDI KUJA KIVINGINE,KAA MKAO WA KULA

NHIF YAKUTANA NA KUTETA NA WASANII BASATA

$
0
0
2Meneja wa Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa NHIF tawi la Ilala Bw.Christopher Mapunda akizungumza na washiriki wa semina katika ya shirika hilo na Wasanii mbalimbali iliyofanyika kwenye ukumbi wa Baraa za la Sanaa nchini BASATA ili kupata elimu juu ya huduma za afya zinazotolewa na shirika hilo kwa vikundi mbalimbali na mashirika pamoja na taasisi mbalimbali za serikali, kulia ni Mkwabi Fikirini Meneja Udhibiti na ubora na Hans Mwankenja Ofisa Mwandamizi matekelezo.
9Msanii aliyeng'ara na Kundi la Wagosi wa Kaya, Fred Maliki 'Mkoloni'akichangia mada wakwati alipokuwa akiuliza swali katika semina hiyo10Baadi ya wanamuziki wa muziki wa dansi wakiwa katika semina hiyo.12Mwimbaji wa muziki wa taarabu Siza Mazongela alikuwa ni mmoja wa wasanii walioshiriki katika semina hiyo.

MWENYEKITI WA NCCR-MAGEUZI,JAMES MBATIA AKARIBISHWA KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA VUNJO

$
0
0
Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi taifa ,James Mbatia akipungungia wananchi wakati msafara wa pikipiki na magari ukipita katika maeneo mbalimbali ya jimbo la Vunjo.
Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi taifa ,James Mbatia akifurahia jambo akiwa na mjumbe wa mkutano mkuu wa NCCR,Hemed Msabaha,(kulia)
Umati wa wakazi wa mji wa Himo wakisiliza kwa makini hotuba zilizokuwa zikitolewa katika mkutano wa hadhara wa Mh James Mbatia aliofanya katika uwanja wa Ghalani.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

TAMASHA LA FIESTA 2014 LASAMBAZA UPENDO WA KUTOSHA KWA WAKAZI WA MUSOMA.

$
0
0
Wasaniii walioshiriki tamasha la Fiesta 2014 wakiwa na mishumaa jukwaani wakisambaza upendo na kuwafariji wale wote waliopotelewa na ndugu zao,waliojeruhiwa katika ajali iliyotokea  hivi karibuni wilayani Butiama mkoani Mara,ambapo watu zaidi ya 40 walipoteza maisha na wengine kujeruhiwa vibaya.
 Sehemu ya umati wa wakazi wa mji wa musoma wakiwa ndani ya uwanja wa Karume,wakati tamasha la Fiesta 2014,likiendelea huku shangwe za hapa na pale zikiwa zimetawala kila kona ya uwanja.
 Mmoja wa wasanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya,Barnaba ambaye kwa sasa anatamba na wimbo wake mpya ujulikanao kwa jina la Waharade akiwaimbisha wakazi wa mji wa musoma waliojitokeza kwa wingi kwenye tamasha la fiesta 2014
 Mmoja wa wasanii kutoka kundi la Weusi ,Nick wa Pili akiwarusha wakazi wa mji wa Musoma usiku huu kwenye tamasha la Fiesta 2014,lililofanyika ndani ya uwanja wa Karume.
 Sehemu ya wakazi wa Musoma waliojitokeza kwenye tamasha la Fiesta usiku huu ndani ya uwanja wa Karume.
  Mwanadada machachari awapo jukwaani,Shilole akiimba kwa madaha kabisa kwenye jukwaa la Fiesta ndani ya uwanja wa Karume mjini Musoma.
 Pichani kati ni msanii wa muziki wa kizazi kipya Rachael akiwa sambamba na madansa wake wakilishambulia jukwaa la fiesta vilivyo usiku huu ndani ya uwanja wa Karume mjini Musoma
 Mashabiki wakishangilia burudani iliyokuwa ikitolewa na wasanii mbalimbali jukwaani usiku huu
 Mmoja wa wasanii anaeokuja juu katika anga ya muziki wa hip hop,Young Killer a.k.a Msodoki akiimba jukwaani.
 Wakazi wa Musoma walivyojitokeza kwenye tamasha la Fiesta 2014 katika uwanja wa Karume usiku huu.
 Jicho la samaki  likiwa limewakusanya pamoja mashabiki wa tamasha la Fiesta lililokuwa likiendelea ndani ya uwanja wa Karume,mjini Musoma.
PICHA NA MICHUZI JR-MUSOMA

Rock City Marathon 2014 kuzinduliwa keshokutwa

$
0
0
UZINDUZI wa msimu wa sita wa mbio za Rock City Marathon 2014
zilizoanza mwaka 2009, zikiwa na lengo la kukuza Utalii wa Ndani
kupitia michezo, unatarajia kufanyika Septemba 10, kwenye Hoteli ya
New Afrika, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mratibu wa mbio hizo, Bi. Grace
Sanga, alisema kuwa baadhi ya wanariadha, viongozi wa vyama vya
riadha, viongozi wa Baraza la Michezo Tanzania na wadau mbali mbali wa
mchezo wa riadha nchini wanatarajiwa kuhudhuria uzinduzi huo.

Bi. Grace alisema kuwa pamoja na maandalizi ya mbio za mwaka huu za
Rock City Marathon kuboreshwa zaidi  ukilinganisha na miaka
iliyotangulia, wawakilishi wa wanariadha na viongozi mbali mbali
watapata fursa ya kuzungumzia changamoto zinazokumba mchezo wa riadha
nchini na jinsi ya kukabiliana nazo.

“Tuko tayari kwa mbio za Rock City Marathon 2014, zitakazofanyika
Oktoba 26. Kamati ya Maandalizi imeweka mikakati mizuri ili
kuhakikisha mbio za mwaka huu zinakuwa bora na zenye mafanikio
kulinganisha na misimu iliyopita,” alisema Bi. Grace.
Mratibu huyo alisema kuwa kwa kutokana na uendeshaji wa kuridhisha wa
mbio hizo, wadhamini wengi wamejitokeza kuwezesha kuzifanya mbio hizo
kuwa bora zaidi mwaka huu.

“Baada ya kufanya maandalizi ya Rock City Marathon kwa mafanikio kwa
miaka tano mfululizo na kuweza kupandisha kiwango chake, makampuni na
mashirika mengi yamejitokeza kudhamini mbio za mwaka huu kwa lengo la
kuiboresha zaidi. Miongoni mwa wadhamini wetu mwaka huu ni pamoja na
NSSF, TSN Group, African Barrik Gold, IPTL, TTB, TANAPA, New Mwanza
Hotel, Nyanza Bottling Company, Sahara Communications, New African
Hotel, Continental decoders, ATCL, PPF, Umoja Switch, and Bank M,”
alisema Bi. Grace.

Rock City Marathon zinaandaliwa na Kampuni ya Capital Plus
International (CPI), kwa ushirikiano na Chama cha Riadha Tanzania
(RT), pamoja na Chama cha Riadha mkoa wa Mwanza (MRAA), ambazo
zimewavutia washiriki wengi wa ndani na nje ya nchi.

Bi. Grace aliongeza kwamba, mbio hizo zitakuwa na vipengele vitano kwa
msimu huu, ambavyo ni mbio za kilometa 21 (wanawake na wanaume) na
zile za kilometa tano kwa wakimbiaji kutoka makampuni mbalimbali,
kilometa tatu kwa watu wenye ulemavu, kilometa tatu kwa watu wazima
(zaidi ya miaka 55) na kilometa mbili kwa watoto walio kati ya miaka 7
mpaka 10.

“Tunatarajia watu wengi kujitokeza mwaka huu, kwa kuwa tumejipanga
vizuri kwa msimu huu. Tumejifunza kupitia mbio za mwaka jana, hivyo
Kamati ya Maandalizi imekuja na mpango madhubuti utakaoboresha mbio
zetu kwa mwaka huu,” alisema Bi. Grace.

SEMINA YA FURSA YAWAONESHA DIRA WAKAZI WA SHINYANGA

$
0
0
 
 SEMINA ya Kamata Fursa Jitathimini,Jiamini,Jiongeze inayoendeshwa sambamba na burudani za Serengeti Fiesta 2014, jana imeendelea kwa kuwapatia dira ya maisha na namna ya kuwafanya wajikwamue kwenye shughuli mbalimbali za kiuchumi wakazi wa Mkoa wa Shinyanga mjini ndani ya Ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Uhuru iliyopo mjini humo.
Semina hiyo ambayo imeongozwa na Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba (pichani juu) ilikuwa ya aina yake, kwani baadhi ya vitu na mbinu alizowapatia wakazi wa Mkoa wa Shinyanga wengi wao wameonesha hali ya kuelewa baadhi ya mafunzo na mbinu hizo na kuaahidi kuzifanyia kazi ipasavyo ili waweze kujikwamua kiuchumi na kuyatimiza malengo yao waliojiwekea.
 Meneja wa Maxcom Africa, ‘Max malipo’,  Bernard Munubi  ambaye aliwapatia mbinu za mafanikio na namna ya kujikwamua kiuchumi kupitia mashine za Max Malipo ambazo kwa kiasi kikubwa sasa zimeweza kuwapatia ajira wakazi wengi nchini.
Naye mzungumzaji kutoka  kampuni ya GSI Tanzania,Afisa Mwanadamizi wa kampuni hiyo Tanzania,Pius Mikongoti akizungumza kwenye semina hiyo ya fursa ikiwemo na kuwapa mbinu za kujikwamua kupitia kampuni hiyo.

BREAKING NEWZZZZZZ: MKATABA WA YANGA, OKWI HAUPO NA SASA YUPO HURU KUCHEZEA TIMU YOYOTE AITAKAYO

$
0
0
Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imekutana leo (Septemba 7 mwaka huu) na kupitia masuala mbalimbali ikiwemo mgogoro wa kimkataba kati ya klabu ya Yanga na mchezaji Emmanuel Okwi (pichani kushoto akipokea jezi baada ya kusajiliwa na Simba). 
Mkataba huo ulipitiwa na Kamati ikiwemo kumsikiliza mchezaji mwenyewe pamoja na upande wa Yanga, na kuridhika kuwa mkataba kati ya pande hizo umevunjika. Ukiwa ni mkataba wa pande mbili, Yanga ilikiuka kipengele namba 8 kuhusu malipo ya ada ya usajili.
 Yanga ikiwa mwajiri, haikutekeleza kipengele hicho cha kimkataba hadi kufikia Juni 27 mwaka huu ilipoandika barua TFF kuomba mkataba huo uvunjwe. Kwa maana hiyo Okwi ni mchezaji huru, hivyo yuko huru kujiunga na timu yoyote. 
Mkataba ni uhusiano kati ya mwajiri (Yanga) na mwajiriwa (Okwi), ambapo Kamati imebaini kuwa uhusiano huo haupo, hivyo hakuna mazingira ya pande hizo mbili kuendelea kufanya kazi pamoja. 
Pamoja na Yanga kuwasilisha pingamizi la kuwepo mmoja wa wajumbe katika kikao kwa sababu za kimaslahi (conflict of interests), walifahamishwa kuwa kilichopo mbele ya kamati ni mgogoro wa kimkataba kati ya Yanga na Okwi, na si usajili. 
Pia lilijitokeza suala la Okwi kutakiwa na klabu ya Wadi Degla ya Misri. Kamati imeiagiza Sekretarieti ya TFF kulifanyia uchunguzi suala hilo na kulitolea taarifa katika kikao kijacho. 
Hata hivyo mjumbe huyo hakushiriki katika kuchangia hoja na kutoa maamuzi. Uamuzi wa kamati ulifanyika baada ya majadiliano, hivyo hakukuwa na suala la kupiga kura. 
Kuhusu pingamizi la Coastal Union kwa Abdi Banda, Kamati imebaini kuwa klabu hiyo imevunja mkataba kati ya pande hizo mbili kwa kushindwa kumlipa mchezaji huyo mshahara wa miezi mitatu mfululizo kama takwa la mkataba. 
Klabu ya Coastal Union iliwakilishwa na mmoja wa viongozi wake, wakati Banda aliwakilishwa na mwanasheria wake. 
Vilevile Kamati imekubaliana na pingamizi la Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Morogoro (MRFA) kuhusu wachezaji waliofanyiwa uhamisho kutoka katika mkoa wake bila kulipiwa ada za usajili, hivyo klabu husika zinatakiwa kulipa ada hizo. 
Pia Kamati imeagiza klabu zote zilizosajili wachezaji bila kuwafanyia uhamisho, kulipa ada za uhamisho kwa pande husika kabla ya kuanza ligi, vinginevyo leseni zao zitazuiwa hadi watakapolipa.
Mashauri mengine ya pingamizi yatasikilizwa baadaye kwa vile klabu husika hazikupata fursa ya kufika mbele ya kamati.Kamati inasisitiza kwa wanachama wa TFF kuheshimu mikataba.

BONIFACE WAMBURA
KAIMU KATIBU MKUU
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)


MWANAHARAKATI KHADIJA LIGANGA ATOA SEMINA YA UNYANYASAJI WA KIJINSIA NA UKATILI DHIDI YA WATOTO KWA VIJANA ZAIDI YA 100 JIJINI MWANZA

$
0
0
Mwanaharakati toka Shirika la Kutetea Haki za Wanawake la KIVULINI la jijini Mwanza, Bi. Khadija Liganga ametoa mafunzo ya siku moja kuhusu Unyanyasaji wa kijinsia na ukatili Dhidi ya watoto kwa vijana takribani 100 wa jiji la Mwanza ikiwa ni hatua za kuwajenga vijana katika misingi ya kuachana na mila, tamaduni na dhana potofu zinazowakandamiza wanawake na watoto katika jamii.

Semina hiyo iliyoandaliwa na Teen Club Mwanza, ililenga Kujenga uwezo wa kutambua ukatili na unyanyasaji wa kijinsia, kuelewesha na kutoa njia za namna ya kuripoti unyanyasaji na ukatili na kuwasihi vijana kutoendeleza tabia za unyanyasaji na ukatili dhidi ya wanawake na watoto.

Akizungumza mara baada ya kutoa mafunzo hayo Bi. Khadija Liganga alisema ni lazima jamii ichukue jukumu la makusudi kukomesha vitendo vyote vinavyowakandamiza na kuwanyanyasa wanawake na watoto kwani ni moja ya sehemu inayochangia kwa kiasi kikubwa kuleta umasikini na kurudisha nyuma gurudumu la maendeleo kwa haraka sana.

“Mwanamke akipigwa au kutukanwa hatoweza kufanyakazi zake, mtoto akiteswa na kunyanyaswa hatoweza kusoma vizuri shuleni, huwezi pata maendeleo. Ili vijana waweze kupeleka ujumbe sahihi wa masuala ya ukatili wa kijinsia wanatakiwa kujua na kufahamu masuala yanayohusiana na tofauti za kijinsia, kulingana na suala la ukatili wa kijinsia (GBV) na namna ya kuzikemea tabia hizo” alisema Bi. Khadija.

Kwa mujibu wa ripoti ya UNICEF ‘Watoto na Wanawake Tanzania’ ya mwaka 2010 inasema kuwa kuwekeza kwa watoto na wanawake ni moja ya njia bora kabisa kwa maendeleo ya Tanzania. Sensa ya watu na Makazi ya mwaka 2012 inaonesha Zaidi ya asilimia 50 ni watoto, ubunifu wao na umahiri wao katika kuzalisha ndio msingi mkubwa wa kufikia malengo ya Tanzania 2025.

Bi. Khadija aliendelea kusema kuwa bado katika jamii nyingi watoto hukatazwa kusema hadharani kwamba wananyanyaswa, mila nyengine watoto hawastahili kuzizungumzia, hivyo hivyo mwanamke anaona aibu au anaogopa kuzungumzia suala la ukatili wakati mwanaume anaweza kufanya kisema mbele za watu na wakati mwingine kwa kujidai /kujigamba amempiga mkewe. Hivyo basi ushiriki wa wa vijana ni muhimu sana kuelimishwa ili kujenga familia na jamii salama isiyo na ukatili Dhidi ya wanawake na watoto.

“Ni swali la kujiuliza kama sisi watu wazima tumeshindwa kujenga miji iliyo salama, kwanini tusiwekeza nguvu nyingi kwa hawa vijana, waswahili husema ‘ashakum si matusi’ni ngumu kumfundisha mbwa mzee mbinu mpya, hivyo naomba serikali, vyombo vya habari, mashirika ya kijamii, wazazi, pamoja na wanaharakati kuwekeza katika kuwapa kundi hili la vijana elimu ya ukatili wa kijinsia na haki za watoto ili kujenga kizazi bora” alimalizia kwa kusema Bi. Khadija.

Ripoti ya “Ukatili Dhidi ya Watoto Tanzania” ya UNICEF 2011, inasema kuwa karibu wasichana 3 kati ya 10 na mvulana 1 kati ya 7 wameripoti kutendewa walau tukio moja la ukatiliwa kijinsia kabla ya kutimiza umri wa miaka 18. Huku karibu asilimia 6 ya wasichana wamelazimishwa kujamiiana kabla hawajatimiza miaka 18. Marafiki, majirani, na watu wasiowafahamu walitajwa na wasichana na wavulana kama wakosaji wa ukatili wa kijinsia.
Kundi la vijana Zaidi ya 100 toka katika klabu ya Vijana (Teen Club) jijini Mwanza wakisikiliza kwa makini mafunzo toka kwa Bi. Khadija Liganga ya jinsi gani wanaweza kukabiliana na Unyanyasaji na Ukatili wa kijinsia lakini pia jinsi ya kuripoti matukio mbalimbali ya ukatili katika vyombo husika.
Bi. Khadija Liganga, Mwanaharakati wa kupigania Haki za Wanawake wa Shirika la Kutetea Haki za Wanawake KIVULINI akitoa semina ya siku moja kuhusu unyanyasaji wa kijinsia na ukatili dhidi ya watoto kwa vijana Zaidi ya 100 kutoka klabu ya vijana (Teen Club) ya jijini Mwanza.

NAPE ATOA DARASA KWA VIONGOZI WA CCM UINGEREZA

$
0
0
 Katibu wa NEC itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye akizungumza na viongozi wa mashina ya CCM Uingereza  ambapo aliwaambia matawi ya CCM nje ya nchi yawe mawakala wa kuleta mabadiliko ndani ya chama pamoja na kuwaunganisha watanzania kujikomboa kiuchumi
 Baadhi ya viongozi wa mashina ya CCM Uingereza wakifuatilia mafunzo kutoka kwa Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye aliyekuwa akitoa somo juu ya Wajibu wa Matawi ya CCM nje ya Nchi.
 Viongozi wa mashina wakisikiliza kwa makini.

TAARIFA KWA UMMA: BENKI KUU YATOA SARAFU MPYA YA SHILINGI MIA TANO, KUANZA KUTUMIKA OKTOBA MWAKA HUU

$
0
0
Benki Kuu ya Tanzania ndiyo chombo chenye jukumu la kutoa sarafu na noti halali (legal tender) zinazotumika nchini. Katika kutekeleza jukumu hili Benki Kuu hutengeneza noti na sarafu zenye uwiano mzuri wa thamani (denominations) unaozingatia uwezekano wa zile zenye thamani kubwa kuweza kugawika katika zile zenye thamani ndogo ndogo. 

Hii hulenga kurahisisha upatikanaji wa chenji na uwezekano wa wahitaji wa viwango mbalimbali vya bidhaa na huduma  kupata katika mafungu yatakayokidhi mahitaji yao. 

Katika kutekeleza jukumu hili, Benki Kuu imetoa toleo jipya la Sarafu ya Shilingi 500. Hatua hii imezingatia yafuatayo: 
kwamba noti ya shilingi mia tano (500), ndiyo inayotumika zaidi kwenye manunuzi ya kawaida ya kila siku ya wananchi wengi kuliko noti nyingine yoyote. Hivyo noti hiyo hupita kwenye mikono ya watu wengi katika kipindi cha muda mfupi sana na kuchakaa haraka. 

Noti hizi hukaa katika mzunguko kwa muda mrefu bila kurejeshwa kwenye mabenki kwa wakati muafaka ili zibadilishwe zinapokuwa zimefikia ukomo wake. 
Sarafu hukaa kwenye mzunguko kwa miaka mingi zaidi kuliko noti. 

Sarafu hii inatambuliwa kwa kuangalia yafuatayo:
Umbo lake ni la duara lenye michirizi pembezoni, kipenyo cha milimita 27.5 na uzito wa gramu 9.5 
Ina rangi ya fedha na imetengenezwa kwa madini aina ya chuma (Steel) na “Nickel” 
Kwa mbele ina sura ya Rais wa Kwanza wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Sheikh Abeid Aman Karume na kwa nyuma ina taswira ya mnyama nyati akiwa mbugani.
Ina alama maalum ya usalama iitwayo “latent image” iliyopo upande wa nyuma  ambayo ni kivuli kilichojificha. Kivuli hiki huonesha thamani ya sarafu ‘500’ au neno ‘BOT’ inapogeuzwa-geuzwa.

Sarafu hii mpya ya shilingi mia tano (500) inatarajiwa kuingizwa kwenye mzunguko kuanzia mwezi  Oktoba 2014. Sarafu hii, itakuwa ikitumika sambamba na noti zilizopo sasa za shilingi mia tano mpaka hapo noti hizo zitakapokwisha katika mzunguko. Pamoja na taarifa hii; tunawaomba wananchi kuendelea kufuatilia vipindi mbalimbali vitakavyokuwa vinaeleza jinsi sarafu hii ilivyo na namna ya kutunza noti na sarafu zetu kwa njia salama.

Ahsanteni Sana

Mkurugenzi Huduma za Kibenki kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Bw. Emmanuel Boaz(wa kwanza kulia) akiwaeleza waandishi wa habari(Hawapo   Pichani) sababu zilizopelekea kutoa toleo jipya la sarafu ya shilingi 500, ambapo alisema noti ya shilingi 500 inatumika zaidi kwenye manunuzi ya kawaida ya kila siku hivyo hupita kwenye mikono ya watu wengi na kuchakaa haraka,noti hizi hukaa katika mzunguko kwa muda mrefu bila kurejeshwa kwenye mabenki na sarafu hukaa kwenye mzunguko kwa muda mrefu kuliko noti. Katikati ni Mshauri wa Fedha kutoka ofisi hiyo Bw. Hassan Jarufu na Mwisho ni Meneja Msaidizi, Sarafu Bw. Abdul Dola.
Mkurugenzi Huduma za Kibenki kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Bw. Emmanuel Boaz (kulia) na Mshauri wa Fedha kutoka ofisi hiyo Bw. Hassan Jarufu wakiwaonesha waandishi wa Habari(Hawapo Pichani) Toleo jipya la sarafu ya Shilingi 500 inayotarajiwa kuingizwa kwenye mzunguko kuanzia mwezi Oktoba 2014. Picha na Hassan Silayo-MAELEZO

NEWS ALERT: BENKI YA CRDB KUJENGA TAWI LA KISASA KATIKA KIWANDA CHA DANGOTE, MTWARA

$
0
0
  Ndege ya Mwenyekiti na Mtendaji Mkuu wa Dangote Group of  Industries, Alhaji Aliko Dangote ikiwasili katika uwanja wa Mtwara.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dk. Charles Kimei (wa pili kushoto), akiwa na balozi wa Nigeria, Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Mtwara, Francis Kasoyaga (wa pili kulia) wakiwa uwanja wa Ndege wa Mtwara wakati wakimsubiri kumpokea Mwenyekiti na Mtendaji Mkuu wa Dangote Group of  Industries, Alhaji Aliko Dangote.
  Mwenyekiti na Mtendaji Mkuu wa Dangote Group of  Industries, Alhaji Aliko Dangote akishuka katika Ndege mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Mtwara.
 Mwenyekiti na Mtendaji Mkuu wa Dangote Group of  Industries, Alhaji Aliko Dangote akisalimiana na balozi wa Nigeria.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB akisalimiana na Mwenyekiti na Mtendaji Mkuu wa Dangote Group of  Industries, Alhaji Aliko Dangote.
Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

Tamasha la 'Handeni Kwetu' lapania kuvunja rekodi

$
0
0
MRATIBU Mkuu wa Tamasha la Utamaduni Handeni, maarufu kama ‘Handeni Kwetu’, Kambi Mbwana, ameapa kuhakikisha kuwa tamasha lao msimu wa 2014 linakuwa la aina yake na kuvunja rekodi ya mwaka jana lilipofanyika kwa mara ya kwanza wilayani Handeni, mkoani Tanga.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mbwana alisema kuwa hiyo ni kutokana na kutamani kushirikisha wasanii wengi kutoka Tanga na Tanzania kwa ujumla.

Alisema kwamba mwaka jana wasanii zaidi ya 200 walionyesha uwezo wao kutoka kwa vikundi mbalimbali vya wilayani Handeni na jijini Dar es Salaam.

“Mwaka jana vikundi zaidi ya 10 vyenye wasanii wasiopungua 15 walipata nafasi ya kupanda jukwaani kuonyesha vipaji vyao, ukiacha wasanii wanaotoka kwenye Kambi ya jeshi la Kujenga Taifa (JKT) wa Mgambo waliozidi 80.

“Wakati tunajivunia mafanikio haya, tunaamini msimu huu utakuwa mzuri zaidi tukiamini kuwa tutavunja rekodi ya mwaka jana, ambapo tulishuhudia burudani mbalimbali, ikiwamo hadithi zilizohusu watu wa Handeni, bila kusahau vyakula vya asili pamoja na michezo waliyokuwa wakicheza wazee wetu enzi hizo,” alisema Mbwana.

Kwa mujibu wa Mbwana, mipango ya kuboresha tamasha hilo imepamba moto ambapo kwa sasa utafiti wa ubora wa vikundi nje ya wilaya ya Handeni inafanywa ili kuhakikisha kuwa wasanii watakaopanda jukwaani wanakuwa na uwezo wa juu na kufanikisha kwa dhati kukuza sekta ya utamaduni pamoja na uchumi wa Tanzania.

SAFARI LAGER YATANGAZA ZAWADI ZA WASHINDI WA MCHEZO WA POOL TAIFA 2014

$
0
0
Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo akizungumza na waandishi wa habariu (hawapo pichani) wakati wa kutangaza zawadi na  maandalizi ya fainali za mashindino ya Safari National Pool Competition 2014 zinazotarajiwa kufanyika mkoani Kilimanjaro mwishoni mwa wiki.Kulia ni Katibu Mkuu wa Chama cha Pool Taifa (TAPA),Amos Kafwinga.
Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo (kushoto) akimkabidhi kwa Katibu Mkuu wa Chama cha Pool Taifa (TAPA),Amos Kafwinga zawadi zitakazo kabidhiwa kwa washindi wa fainali ya mashindino ya Safari National Pool Competition 2014 zinazotarajiwa kufanyika mkoani Kilimanjaro mwishoni mwa wiki.

BREAKING NEWZZZZ: JESHI LA POLISI MKOANI GEITA LAKAMATA BUNDUKI SABA ZILIZOPORWA KITUO CHA POLISI BUKOMBE, WATU WAWILI MBARONI NA MSAKO MKALI UNAENDELEA

$
0
0
 Habari zilizotufikia hivi punde zinasema Jeshi la polisi mkoani  Geita limekamata bunduki saba (pichani) na mabomu kadhaa ya machozi eneo la Ushirombo wilaya ya Bukombe ikisadikiwa kuwa ni kati ya bunduki kumi zilizoporwa na majambazi yaliyovamia kituo cha polisi Bukombe na kufanya mauaji ya askari polisi wawili waliokuwa zamu  jana. Bunduki hizo, nne zikiwa SMG na tatu aina ya Shotgun  pamoja na panga zimepatikana  katika tanuri la kuchomea matofali zikiwa zimefichwa pamoja na mabomu hayo.

Habari zinapasha pia kwamba katika msako huo mkali unaoendelea, Jeshi hilo pia limewatia mbaroni watu wawili wanaohisiwa kuwa ni  majambazi yaliyohusika na shabulio hilo, mmoja akiwa kakutwa  akiwa na bomu  juu ya mti, majira ya jioni ya leo. 

Jeshi la polisi nchini tayari limetangaza dau  la shilingi millioni 10 kwa mtu yeyote atakaye fanikisha kuwakamata au kuwabaini waliohusika na vitendo hivyo. Taarifa zaidi tutaendelea kuwaletea kwa kadri zitavyopatikana

SAMSUNG REWARDS E-WARRANTY WINNERS

$
0
0
SAMSUNG Electronics East Africa Tanzania has today rewarded its winners for its E-warranty draw for June at its Quality Centre Brand Shop, along Pugu Road.

Samsung Electronics introduced the SMS check off point buying system dubbed E- Warranty to enable customers identify genuine Samsung phones through the phone's IMEI Number.

Samsung Electronics Account Manager Mr. Ibrahim Kombo said ‘Since the introduction of the E-Warranty system in Tanzania, the response from customers has been great. Consumers are able to know whether: the Samsung phone has a 24 month warranty or not, if the Samsung Phone has been reported missing or stolen and if the Phone is new or used’.

Draw winners walk away with 1 of 10 prizes: 1 Samsung Galaxy Tab 10.1”, 3 Samsung Cameras, 1 Samsung TV 32”, 1 Samsung Home Theatre, 3 Samsung Microwaves, 1 Samsung Galaxy Grand.

To check for the authenticity of the phone, a prospective buyer simply needs to send an SMS with 'Check' followed by star(*) then IMEI number, then hush(#) button and send this to ‘15685’ a reply about the status of the Samsung phone is then automatically generated.

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LEO TAREHE 08.09.2014.

Viewing all 110175 articles
Browse latest View live




Latest Images