Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110133 articles
Browse latest View live

Utalii unavyoweza kuleta ajira kwa vijana

$
0
0
Kukua kwa biashara ya watalii kumeweza kutoa ajira kwa vijana wengi nchini,Huku ikikuza vipaji vya kazi za mikono ambapo zina soko kubwa kwa wageni kijana huyo alikutwa akichora picha ya mbuyu katika mitaa ya Hurumzi Stree Stone Town. Picha na Sabry Juma wa Zanzibar.

JARIDA LA WIKI LA NISHATI NA MADINI - TOLEO LA 31

WAZIRI MKUU ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI IRELAND

$
0
0
WAZIRI MKUU Mizengo Pinda ametumua salamu za rambirambi kwa Serikali ya Ireland kufuatia kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa zamani wa nchi hiyo, Bw. Albert Reynolds.

Hayati Reynolds ambaye amefariki akiwa na miaka 81, alikuwa Waziri Mkuu wa nane wa nchi hiyo kwa miaka mitatu kuanzia mwaka 1992. Atakumbukwa kwa kuanzisha mchakato wa kuleta amani Ireland Kaskazini dhidi ya kundi la IRA.

Waziri Mkuu Pinda ambaye aliwasili jana (Alhamisi, Agosti 28, 2014) jijini Dar es Salaam akitokea Dodoma, alikwenda moja kwa moja ubalozi wa Ireland na kusaini kitabu cha maombolezo cha kiongozi huyo.

Katika salamu za rambirambi, Waziri Mkuu amemwelezea Bw. Reynolds kuwa ni kiongozi atakayekumbukwa kwa kuleta amani duniani na misaada ya kimaendeleo nchini Tanzania. 

“Kwa niaba ya Serikali ya Tanzania, ninawapa pole sana kwa kufiwa na Kaka yetu na ndugu yetu, Waziri Mkuu wa zamani wa Ireland, Albert Reynolds. Tunashirikiana nanyi katika kipindi hiki cha majonzi. Tutaendelea kumkumbuka kwa kazi nzuri alizofanya kwa nchi yetu na duniani. POLENI SANA KWA MSIBA HUU MKUBWA,” inasomeka sehemu ya salamu za rambirambi alizotoa Waziri Mkuu.

Akipokea salamu hizo, Balozi wa Ireland nchini Tanzania, Bibi Fionnuala Gilsenan alimshukuru Waziri Mkuu Pinda kwa kufika ubalozini hapo na kuwapa pole kwa kifo cha Waziri Mkuu wao wa zamani. 

“Tutamkumbuka kiongozi wetu kwa mambo mengi aliyoifanyia nchi yetu… Tunafarijika kwa salamu hizi za rambirambi. Tutafikisha kitabu hiki cha salamu za rambirambi kwa familia yake, naamini nao watafarijika sana,” alisema Balozi Gilsenan.

Balozi Gilsenan alimweleza Waziri Mkuu kwamba kitabu cha maombolezo kitafungwa leo.

KUTOKA BUNGE LA KATIBA LEO

$
0
0
Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Samia Suluhu Hassan (aliyebeba mkoba) akiwasili Bungeni kuendelea na majukumu ya Bunge Maalum la Katiba. Aliyemtangulia mbele ni Mkuu wa Idara wa shughuli za Bunge John Joel.
Mwakilishi wa Watanzania waishio Marekani ambaye pia ni Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Bw. Kadari Singo (kushoto) akifurahia jambo akiwa pamoja na waandishi wa Habari leo 29 Agosti, 2014 Bunge Maalum la Katiba mjini Dodoma.
Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, kulia ni Mhe. Stella Manyanya akiwa amefuatana na Mhe. Reuben Matango wakielekea ndani ya Bunge Singo leo 29 Agosti, 2014 Bunge Maalum la Katiba mjini Dodoma.
Mwakilishi wa Watanzania waishio Marekani ambaye pia ni Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Bw. Kadari Singo (kushoto) akibadilishana mawazo na Mjumbe mwenzie, Mhe. Yusuph Singo leo 29 Agosti, 2014 Bunge Maalum la Katiba mjini Dodoma. (Picha zote na Benedict Liwenga, Maelezo-Dodoma)

4TH ANNIVERSARY OF VIJIMAMBO BLOG, PROMOTING TANZANIA TOURISM EXPO IN THE USA

$
0
0
Vijimambo Blog kwa ushirikiano wa pamoja na Ubalozi wa Jamhuri ya Muunagano wa Tanzania ikiwemo Jumuiya ya Watanzania DMV inawaletea miaka 4 ya Vijimambo ikiutangaza Utalii wa Tanzania na kukemea ujangili siku ya September 13, 2014. Njoo ujivunie maliasili na utalii wa nchi yako sote kwa pamoja yunaweza kuitangaza nchi yetu na kukemea ujangili kwa kauli moja yenye nguvu inayosikika kimataifa.
Juu na chini ni Ukumbi wa sharehe ya mchana kuanzia saa 4 asubuhi mpaka saa 11 jioni
add ni 3 Reserch  Court, Rockville, MD 20850 na baadae usiku ni Hall la Oxford 9700 Martin Lurthers King Jr HWY, Lanham, MD 20786 kuanzia saa 3 usiku mpaka saa 9 alfajiri
Vyakula vya kitanzania Burudani ya kila aina karibu tuitangaze Tanzania kimataifa. 

Kwa Wajasiliamali watakaopenda kuweka meza zao mwisho wa kujisajili ni Sept 5, 2014 tafadhali wasiliana na wanakamati Baraka Daudi 301 792 8562, Tuma Kaisi 301 433 4311, Iddi Sandaly 301 613 5165, Asha Nyang;nyi 301 793 2833, Mayor Mlima 301 806 8467 na Julius Katanga 202 400 4218

PSPF YAANDAA SEMINA YA SIKU MOJA KWA WATUMISHI WA SERIKALI NA TAASISI ZAKE

$
0
0
 Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Adam Mayingu, akitoa hotuba yake wakati wa ufunguzi wa semina ya siku moja kwa watumishi wa serikali na taasisi zake iliyofanyika jana Agosti 29, 2014 mjini Bagamoyo, mkoa wa Pwani.
 Constatina Martin Meneja Masoko, na Mawasiliano wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Constatina Martin, akizungumza kwenye semina ya siku moja ya watumishi wa serikali na taasisi zake iliyoandaliwa na Mduko huo mjini Bagamoyo mkoa wa Pwani, Ijumaa Agosti 29, 2014.
 Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Utumishi, George Yambesi(Wanne kulia waliokaa), na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Adam Mayingu, (Wanne kushoto), wakiwa katika picha ya pamoja na maafisa waandamizi wa Mfuko huo na wafanyakazi wa serikali na taasisi zake, wanaohudhuria semina ya siku moja iliyoandaliwa na Mfuko huo ili kuelezea huduma mbalimbali zitolewazo na Mfuko wa PSPFT.
 Mwanaasemina akipitia utaratibu wa semina ya siku moja ya watumishi wa serikali na taasisi zake iliyoandaliwa na Mfuko wa Pensheni wa PSPF, mjini Bagamoyo mkoa wa Pwani, Agosti 29, 2014.
 Constatina_Kuwite_Muro Mkurugenzi wa Operesheni wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Neema Muro, (Kulia), Meneja Masoko na Mawasiliano wa Mfuko huo, Constatina Martin ,Katikati) na Meneja Utawala, Neema Kuwite, wakibadilishana mawazo muda mfupi kabla ya mkuanza semina ya siku moja kwa watumishi wa serikali na taasisi zake iliyoandaliwa na Mfuko huo mjini Bagamoyo, mkoa wa Pwani Ijumaa Agosti 29, 2014
 Constantina_Mayingu_Yambesi Meneja Masoko, na Mawasiliano, wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Constatina Martin, (Kushoto), akiwaongoza Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais Utumishi, George Yambesi, (Kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko huo, Adam Mayingu, kuelekea ukumnbi wa semina ya watumishi wa serikali na taasisi zake mjini Bagamoyo mkoa wa Pwani, Ijumaa Agosti 29, 2014.


 Mayingu_Yambesi Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Utumishi, George Yambesi, (Kulia), akiongozana na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Adam Mayingu, wakati akiwasili kufungua semina ya siku moja ya watumishi wa serikali na taasisi zake mjini Bagamoyo mkoa wa Pwani Ijumaa Agosti 29, 2014.

JK aagiza Halmashauri zinunue nyumba NHC

$
0
0
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifungua mradi wa nyumba za gharama nafuu za NHC Mnyakongo zilizopo Kongwa mkoani Dodoma akiwa pamoja na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, George Tuguluvala Simbachawene na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu, Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai, Waziri wa Ujenzi Dk John Pombe Magufuli na Mbunge wa Afrika Mashariki Adam Kimbisa.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akishuhudia jiwe la msingi mara baada ya kufungua mradi wa nyumba za gharama nafuu za NHC Mnyakongo zilizopo Kongwa mkoani Dodoma wanaoshuhudia ni pamoja na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, George Tuguluvala Simbachawene na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu. 

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza wakati akitembelea mradi wa nyumba za gharama nafuu za NHC Mnyakongo zilizopo Kongwa mkoani Dodoma. Mradi huo una jumla ya nyumba 44.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akizungumza katika hafla hiyo jana.

JWTZ LATOA MSAADA KWA WAZEE NA MAYATIMA ZANZIBAR

$
0
0
MKUU wa Mkoa Mjini Magharib, Mhe. Abdalla Mwinyi Khamis akizungumza na Wazee wanaoishi katika nyumba za Wazee Sebleni mjini Zanzibar wakati wa hafla ya kukabidhi msaada wa vyakula na vifaa vya usafi vilivyotolewa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika kutimiza miaka 50 ya jeshi hilo tangu kuanzishwa kwake mwaka 1964.
WAZEE wanaoishi katika nyumba za wazee Sebleni wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa Mjini Magharib, Mhe. Abdalla Mwinyi (hayupo pichani) wakati akizungumza katika makabidhiano ya msaada wa vyakula uliotolewa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika kutimiza miaka 50 ya jeshi hilo.
KAIMU Kamanda wa Brigedi ya Nyuki Zanzibar, Kanali Shaban Ilangu Lissu (wa pili kulia) akimkabidhi Mkuu wa Mkoa Mjini Magharib, Mhe. Abdalla Mwinyi msaada wa vyakula na vifaa vya kufanyia usafi vilivyotolewa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ)kwa Wazee wanaoishi katika nyumba za Wazee Sebleni ikiwa ni kutimiza miaka 50 ya kuanzishwa kwa JWTZ.Kulia Naibu Katibu Mkuu Uwezeshaji na Ushirika, Nd. Ali Khamis .
MASISTA wanaowalea wazee wanaoishi katika nyumba za wazee welezo wakiwa katika hafla ya kumakabidhiano ya msaada wa vyakula uliotolewa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika kutimiza miaka 50 ya Jeshi hilo ambapo misaada kama hiyo ilitolewa kwa Tanzania nzima kwa wazee wasiojiweza na mayatima.
WANAJESHI wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wakishusha msaada wa vyakula na vifaa vya kufanyia usafi vilivyotolewa na jeshi hilo kwa Wazee wanaoishi katika nyumba za Wazee ziliopo Welezo Wilaya ya Magharib.Kushoto anaeshughudia Mkuu wa Mkoa Mjini Magharib, Mhe. Abdalla Mwinyi na Kaimu Kamanda wa Brigedi ya Nyuki Zanzibar, Kanali Shaban Ilangu Lissu.
MKUU wa Mkoa Mjini Magharib, Mhe. Abdalla Mwinyi Khamis akiwakabidhi msaada wa vyakula na vifaa vya kufanyia usafi Watoto yatima wanaoishi katika nyumba za mayatima Mazizini. Msaada huo ulitolewa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ) katika kutimiza miaka 50 ya kuanzishwa kwake.
MKUU wa Mkoa Mjini Magharib, Mhe. Abdalla Mwinyi Khamis na viongozi wengine wakiwa katika picha ya pamoja na watoto yatima wanaolelewa katika nyumba za mazizini, baada ya kuwakabidhi msaada wa vyakula vilivyotolewa na JWTZ katika kutimiza miaka 50 ya jeshi hilo.(Picha na Haroub Hussein).

DSTV KUENDELEA KUTOA BURUDANI KWA MASHABIKI WA SOKA WIKIENDI HII

WAZIRI MKUU,MIZENGO PINDA AFUNGUA MKUTANO WA MAWAZIRI WA MAZINGIRA JIJINI DAR LEO

$
0
0
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akifungua Mkutano wa Pamoja wa Mawaziri wa Mambo ya Nje na Mazingira wa Kamati ya Mabadiliko ya TABIANCHI kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere jijini Dar es salaam August 28, 2014.
Sehemu ya washiriki wa mkutano wa mabadiliko ya tabia nchi ulio wahusisha baadhi ya Mawaziri wa Mazingira na Mawaziri wa mambo ya nchi za nje kutoka katika baadhi ya nchi za afrika wakisikiliza hotuba kutoka kwa Waziri mkuu wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Mizengo Pinda (hayupo pichani) leo jijini dar es salaam.
Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya baadhi ya Mawaziri waliohudhuria mkutano wa mabadiliko ya tabia nchi ulio wahusisha mawaziri wa mazingira na mawaziri wa mambo ya nchi za nje kutoka katika baadhi ya nchi za Afrika leo jijini Dar es salaam.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya, Amina Mohamed (katikati) na Waziri wa Mazingira wa Msumbiji, Ana Paulo Chichava baada ya kufungua Mkutano wa Pamoja wa Mawaziri wa Mawaziri wa Mambo ya Nje na Mazingira wa Kamati ya Mabadiliko ya TABIANCHI kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere jijini Dar es salaam August 28, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

NEWS ALERT: WATU KUMI WAFARIKI DUNIA NA WENGINE SABA KUJERUHIWA KATIKA AJALI YA GARI JIJINI MBEYA LEO

$
0
0
WATU kumi wakiwemo watoto wawili wamefariki dunia papo hapo na wengine saba wamejeruhiwa vibaya katika ajali iliyohusisha magari mawili.

Ajali hiyo ilitokea jana majira ya saa nne asubuhi ikihusisha gari ndogo ya abiria maarufu daladala lenye namba za usajili T 237 BFB aina Toyota Hiace na gari kubwa aina ya Fuso lenye namba za usajili T 158 CSV.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo wamesema ajali hiyo ilitokea maeneo ya Mbalizi baada ya Hiace iliyokuwa ikitokea Mbeya mjini kuelekea Mbalizi kulivaa Fuso ilikuwa ikiingia barabarani.

Walisema inasemekana dereva wa Hiace gari yake ilimshinda kutokana na kutelemka mlima mkali wa Mbalizi inagawa pia walimtupia lawama dereva wa Fuso ambaye alikuwa akiingia barabarani bila kuchukua tahadhari.

Muuguzi Mkuu wa Hospitali teule ya Ifisi Mbalizi, Sikitu Mbilinyi, ambako Majeruhi na marehemu walikimbizwa hapo alithibitisha kupokea majeruhi 7 ambapo alisema kati yao ni wanawake 3 na wanaume 4.

Alisema kati ya majeruhi hao wawili wamepewa rufaa kwenda hospitali ya Rufaa Mbeya kutokana na kuhitaji msaada zaidi huklu wengine wakiendelea kupatiwa msaada wa haraka ili kunusuru hali zao.

Mbilinyi aliongeza kuwa pia wamepokea miili ya marehemu 10 wakiwemo watoto wawili na Wanawake wanne na Wanaume wanne.

Hata hivyo majina ya majeruhi na marehemu hayajaweza kupatikana mara moja kutokana na kuwa katika hali mbaya ambapo Dereva wa Fuso akitokomea mara baada ya tukio. NA MBEYA YETU BLOG
Hivi ndivyo ambavyo Daladala hiyo ilivyojibamiza muda mchache uliopita. 
Gari hilo aina ya Tata likiwa limepaki pembeni Muda mchache baada ya kupata ajali hiyo
Askari wa usalama wa Barabarani akiwa anatazama na kuchunguza zaidi ajali hiyo. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

kongamano la kupata maoni ya wadau kuhusu rasimu ya sera ya Petroli lafunguliwa leo jijini Dar

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro akifungua kongamano la siku moja la kupata maoni ya wadau kuhusu rasimu ya sera ya Petroli linalofanyika leo katika ukumbi wa mikutano uliopo Hoteli ya New Africa jijini Dar es Salaam. Kongamano hilo limejumuisha wadau wa mafuta na gesi, wabunge, viongozi wa dini na mikoa iliyofanyiwa utafiti wa mafuta na gesi na vyama vya siasa.
Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro (hayupo pichani) wakati akifungua kongamano la siku moja la kupata maoni ya wadau kuhusu rasimu ya sera ya Petroli linalofanyika katika ukumbi wa mikutano uliopo Hoteli ya New Africa jijini Dar es Salaam.
Wakuu wa mikoa ya Mbeya Abbas Kandoro (katikati) na Lindi Ludovick Mwananzila( kushoto) na Mjiolojia Mwandamizi kutoka Idara ya Nishati Adam Zuberi (kulia) wakisikiliza mada ya rasimu ya sera ya Petroli iliyokuwa inatolewa leo katika kongamano la siku moja la kupata maoni ya wadau kuhusu rasimu hiyo lililofanyika leo katika ukumbi wa mikutano uliopo Hoteli ya New Africa jijini Dar es Salaam.
Kamishna wa Nishati Eng. Hosea Mbise akiwasilisha mada kuhusu rasimu ya sera ya Petroli kwa wadau wa mafuta na gesi, wabunge, viongozi wa dini na mikoa iliyofanyiwa utafiti wa mafuta na gesi na vyama vya siasa wakati wa kongamano la kupata maoni ya wadau lililofanyika leo katika ukumbi wa mikutano uliopo Hoteli ya New Africa jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wadau wa mafuta na gesi, wabunge, viongozi wa dini na mikoa iliyofanyiwa utafiti wa mafuta na gesi na vyama vya siasa wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro (hayupo pichani) wakati akifungua kongamano la siku moja la kupata maoni ya wadau kuhusu rasimu ya sera ya Petroli linayofanyika jijini Dar es Salaam.
Waandishi wa mkutano (Rapporteur) wakiandika taarifa mbalimbali wakati wa kongamano la siku moja la kupata maoni ya wadau kuhusu rasimu ya sera ya Petroli linayofanyika leo katika ukumbi wa mikutano uliopo Hoteli ya New Africa jijini Dar es Salaam. Picha na Anna Nkinda- Maelezo

Rais Kikwete aagiza Halmashauri zinunue nyumba NHC

$
0
0
Na Sifa Lubasi, Kongwa
HALMASHAURI nchini zimetakiwa kununua nyumba za bei nafuu zinazojengwa na Shirika la Nyumba (NHC) ili kuwapangisha watumishi wake.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Rais Jakaya Kikwete alipokuwa akifungua mradi wa nyumba nafuu katika eneo la Mnyakongo wilayani Kongwa mkoani Dodoma.

Alisema kumekuwa na tabia ya baadhi ya maeneo watumishi wa halmashauri kukaa mbali na sehemu zao za kazi kwa visingizio vya kukosa makazi.

Alisema sababu hiyo sasa haina msingi katika maeneo ambayo NHC imejenga nyumba zao kwani halmashauri inaweza kununua nyumba hizo na kuwapangisha watumishi wake.

‘’ Hawa NHC wana utaratibu kwa kupitia mabenki wanayoshirikana nayo hivyo kwa kutumia utaratibu huo halmashuri mnaweza kwenda katika hizo benki na kuingia mkataba na kukopa nyumba hizo na kisa kuwapangisha watumishi…’’ alisema.

Aidha Rais Kikwete alisema shirika hilo linafanya kazi nzuri katika ujenzi wa nyumba hizo za bei nafuu huku akilitaka kuongeza zaidi idadi ya nyumba. Alisema ni vyema sasa halmashuri zikaongeza maeneo ya kujenga nyumba hizo ili wananchi wengi zaidi waweze kuishi katika nyumba bora.

Akizungumza katika ufunguzi huo Mkurugenzi Mtendaji wa NHC Nehemia Mchechu alisema mradi huo ni utekelezaji wa mpango wa ujenzi wa nyumba za gharama nafuu. Alisema mradi huo wenye nyumba 44 hadi kukamilika utakuwa umegharimu Shilingi bilioni 1.2.

Alisema nyumba hizo zinauzwa kwa gharama kati ya Sh milioni 35 hadi 40 kulingana na ukubwa wa nyumba husika.

Hata hivyo alisema bado kuna tatizo la kodi katika uuzaji wa nyumba hizo na ndio kinachofanya kuuzwa kwa bei kubwa.

Alimuomba Rais kusaidia katika kusukuma nia ya kushusha kodi ili nyumba hizo ziuzwe kwa bei nafuu na kila mwananchi aweze kununua.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifunua kitambaa kuashiria ufunguzi mradi wa nyumba za gharama nafuu za NHC Mnyakongo zilizopo Kongwa mkoani Dodoma wanaoshuhudia ni pamoja na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, George Tuguluvala Simbachawene na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akishuhudia jiwe la msingi mara baada ya kufungua mradi wa nyumba za gharama nafuu za NHC Mnyakongo zilizopo Kongwa mkoani Dodoma wanaoshuhudia ni pamoja na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, George Tuguluvala Simbachawene na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifungua mradi wa nyumba za gharama nafuu za NHC Mnyakongo zilizopo Kongwa mkoani Dodoma akiwa pamoja na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, George Tuguluvala Simbachawene na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu, Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai, Waziri wa Ujenzi Dk John Pombe Magufuli na Mbunge wa Afrika Mashariki Adam Kimbisa.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akizungumza katika hafla hiyo jana
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai akizungumza katika hafla hiyo jana
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akijadiliana jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu wakati akitembelea mradi wa nyumba za gharama nafuu za NHC Mnyakongo zilizopo Kongwa mkoani Dodoma. Mradi huo una jumla ya nyumba 44.

MASHINDANO YA SAFARI POOL NGAZI YA MKOA YAFUNGULIWA LEO MKOANI IRINGA

$
0
0
Afisa Utamaduni wa Manispaa ya Iringa, Carlous Mbinda akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi kiti cha kubebea wagonjwa kilichotolewa na kilichotolewa na Chama cha mchezo wa Pool Mkoa wa Iringa(IPA) katika hosptali Halimashauri ya Manispaa ya Iringa ikiwa ni sehemu ya uzinduzi wa mashindano ya mchezo wa Pool ngazi ya Mkoa yaliyoanza jana mkoani humoyajulikanayo kama “Safari Lager Pool Competition 2014” ngazi ya Mkoa.
Mganga mfawidhi wa Hospitali ya Halimashauri ya Wilaya ya Iringa, Mbaraka Mgangachuma(watatu kushoto) akipokea kiti cha kubebea wagonjwa kilichotolewa na Chama cha mchezo wa Pool Mkoa wa Iringa(IPA) katika hosptali hiyo jana wakati wa uzinduzi wa michezo huo ulioanza jana mjini Iringa ujulikanao kama “Safari Lager Pool Competition 2014” ngazi ya Mkoa.
Mganga mfawidhi wa Hospyali ya Haliamshauri ya Manispaa ya Iringa Mbaraka Mgangachuma akipanda mmmoja wa miche iliyofikishwa hospitalini hapo na wacheza pool wa Mkoa wa Iringa waliofika kwa lengo la utunzaji mazingira wakati wa siku ya ufunguzi wa fainali za mashindano ya Safari Pool ngazi ya mkoa yajukayo kama “Safari Lager Pool Competition 2014” ngazi ya Mkoa.
Afisa Utamaduni wa Manispaa ya Iringa, Carlous Mbinda akipanda mmmoja wa miche iliyofikishwa hospitalini hapo na wacheza pool wa Mkoa wa Iringa waliofika kwa lengo la utunzaji mazingira wakati wa siku ya ufunguzi wa fainali za mashindano ya Safari Pool ngazi ya mkoa yajukayo kama “Safari Lager Pool Competition 2014” ngazi ya Mkoa.

MAKABIDHIANO YA OFISI KATI YA WAZIRI WA AFYA NA WAZIRI WA MIUNDOMBINU,ZANZIBAR

$
0
0
Aliyekuwa Waziri wa Afya ambaye kwa sasa ni Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano Juma Duni Haji akimkabidhi Ripoti Waziri mpya wa Wizara ya Afya Rashid Seif Suleiman katika hafla ya kukabidhiana Ofisi iliyofanyika ukumbi wa Wizara ya Afya Mnazi mmoja mjini Zanzibar.
Mkurugenzi Utumishi na Uendeshaji wa Waizara ya Afya Juma Rajab Juma kulia akiwakaribisha Mawaziri wa Afya na Miundombinu katika hafla ya kukabidhiana Ofisi mawaziri hao baada ya kuteuliwa katika nafasi zao hivi karibuni.
Aliyekuwa Waziri wa Afya ambaye kwa sasa ni Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano Juma Duni Haji akizungumza na baadhi ya Watendaji wa Wizara ya Afya katika hafla ya kukabidhiana Ofisi iliyofanyika Wizara ya Afya Mnazi mmoja mjini Zanzibar.
Waziri wa Afya Rashid Seif Suleiman akizungumza na Watendaji wa Wizara hiyo mara baada ya kukabidhiwa Ofisi na Aliyekuwa Waziri wa Wizara hiyo Juma Duni Haji. Katika mazungumzo yake aliwaomba kushirikiana naye ili kutimiza malengo ya Wizara hiyo mpya kwake. picha na Abdallah Omar-Maelezo Zanzibar

Dkt. Shein aelekea Visiwa vya Samoa kwa ziara ya kikazi

$
0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiagana na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar,Balozi Seif Ali Idd katika Uwana wa Ndege wa Kimataia wa Abeid Amani Karume wakati akielekea katika Visiwa vya Samoa kwa ziara ya siku tano.Katikati ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar,Maalim Seif Sharif Hamad.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiagana na Viongozi mbali mbali katika Uwana wa Ndege wa Kimataia wa Abeid Amani Karume akielekea katika Visiwa vya Samoa kwa ziara ya siku tano.[Picha zote na Ramadhan Othman Ikulu.]

"WAUNGWANA" NA MIKIDADI MAHMOUD

RAIS KIKWETE ATEMBELEA SOKO LA NAFAKA LA KIMATAIFA LA KIBAIGWA, DODOMA

$
0
0
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitembelea soko la nafaka la kimataifa la Kibaigwa mkoani Dodoma katika siku ya kwanza ya ziara yake mkoani humo Agosti 28, 2014 , ambapo alijionea shehena kubwa sana ya mahindi iliyoletwa kutoka mashambani na kusafirishwa kila pembe ya nchi. Mwaka huu, kama ilivyokuwa mwaka jana, mavuno ya mahindi yamekuwa makubwa kiasi hata cha kupatikana kwa mavuno ya ziada yanayolemea maghala yaliyopo, ikiwa ni muendelezo wa mafanikio ya sera ya kilimo kwanza ambayo imekuwa ikileta matokeo mazuri kila mwaka.PICHA NA IKULU.
 

uzi wa manchester united watamba mkoani dodoma

$
0
0
Kinamama wa kundi la ngoma za  utamaduni la Simba kutoka kijiji cha Nhambi, Wilayani Mpwapwa, mkoani Dodoma wakitumbuiza kwa ngoma ya Kigogo huku wakiwa wamekula uzi wa Man U wakati wa sherehe za uzinduzi wa mradi wa maji uliofanywa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete Agosti 29, 2014 katika kijiji cha Chunyu.

MISS TANZANIA USA PAGEANT YAPAMBA MOTO, MAMISS WAANZA KUWASILI TAYARI KUWASHA MOTO LEO JUMAMOSI

$
0
0

 Kutoka kushoto ni Maria Rutayuga kuotoka Maryland, Jesca Kalemera kutoka New Jersey, Mercy Sakaya kutoka Michigan na Grace Mlingi kutaoka Maryland.
 Washiriki wakimsikiliza mmoja ya waratibu alipokua akiwaelekeza jambo kwenye hotel waliyofikia ya Double Tree iliyopo Dwntown Silver Spring.
PICHA ZAIDI BOFYA HAPA
Viewing all 110133 articles
Browse latest View live




Latest Images