Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110185 articles
Browse latest View live

Vodacom yarekebisha mfumo wa M-Pesa kwa soko la Afrika ya Kusini

$
0
0
Kampuni ya Vodacom imerekebisha mfumo wa M-Pesa kwa soko la Afrika Kusini ili kuleta mafanikio kama yaliyopatikana katika nchi za Kenya na Tanzania.

M-Pesa ilianzishwa Kenya mwaka 2007 na leo hii inatumiwa na watu zaidi ya  milioni 18 katika nchi zipatazo 13 kwa ajili ya kutuma pesa na za kibenki kwa kutumia simu ya mkononi.M-Pesa ilianzishwa Afrika ya Kusini mwaka 2011 ikiwa na wateja wa mwanzoni zaidi ya milioni moja lakini hadi leo haijaonyesha kukua kwa soko kama ilivyo kwa nchi za Kenya na Tanzania,taarifa kutoka ndani ya kampuni zimeeleza.

Taarifa zimeendelea kueleza kwamba kutoka kipindi cha miaka miwili iliyopita Vodacom Afrika ya Kusini, imeunda jopo jipya la kushughulikia huduma ya M-Pesa na kuingiza utaalamu wa kutoka nje kuhusu shughuli za benki na malipo kwa njia ya simu,pia kuangalia ni mambo gani yamesababisha huduma hiyo kuzorota Afrika ya Kusini na kuangalia mafanikio katika nchi nyingine yametokana na nini.

Kutokana na tathmini iliyofanyika huduma mpya ya M-Pesa imezinduliwa ikiwa na marekebisho katika maeneo manne yakiwemo usambazaji,usajili,matumizi na imani katika mfumo wa M-Pesa.

Kuhusu usambaji,huduma mpya ya M-Pesa imeanzishwa kwa kuwa na mawakala wapatao 8,000 kukiwemo wadogo wadogo na mawakala wakubwa “idadi hii ni zaidi ya mara 10 ikilinganishwa na mawakala waliokuwepo wakati M-Pesa ilipozinduliwa Afrika ya Kusini mwaka 2011 na lengo ni kukua hasa katika sekta isiyo rasmi ili kufikia angalau mawakala 30,000 ifikapo mwisho wa mwaka huu”.Alisema Shameel Joosub,Mtendaji Mkuu wa makampuni ya Vodaccom Afrika Kusini.

‘’Upanuzi huu utatuweka mbele ya wengine katika shughuli za usambazaji kwa kuhakikisha kuna wakala wa M-Pesa kwa kila mita zisizozidi mamia mengi kutoka walipo wateja na pia kutakuwepo na ongezeko la ajira”.Aliendelea kueleza Joosub.

Kwa upande wa usajili M-Pesa ya Afrika Kusini imerekebisha taratibu za usajili kusudi wateja wajisajili kwa kutumia simu ya mkononi na kitambulisho tofauti na hapoo mwanzo ambapo mteja alilazimika kwenda mwenyewe kwenye kituo wakati vituo vya mawakala vilikuwa vichache.Kwa wateja wanaopenda  kubadili matumizi na kiwango cha kutuma fedha katika akaunti zao,wanachohitaji ni kwenda na vitambulisho vyao na kujisajili katika vituo maalumu zaidi ya 1,000 nchini vikiwemo maduka ya Vodacom,maduka mengine maalumu na vituo vingine vinavyohusika.

“Ingawa usajili na usambazaji ni muhimu lakini kubwa zaidi ni matumizi ya M-Pesa na tunafurahi kuona kwamba tumeshirikiana na benki ya Bidvest  inayotoa huduma za Visa vilevile ambayo imetupatia ushauri tukafanya marekebisho makubwa katika mfumo wa matumizi “Amesema Joosub.
Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa benki ya Bidvest Japie van Niekerk,   amesema kuwa taasisi yake inajivunia kufanya kazi na taasisi kubwa ya Vodacom katika kutoa huduma za kibenki kwa wananchi na ana imani wananchi watanufaika na huduma zitakazotoolewa kwa kutumia wataalamu wa taasisi yake na Vodacom.

Aliongeza kwamba ana imani kubwa kutokana na mabadiliko haya ya kuboresha huduma za M-Pesa wananchi wengi watafaidika na huduma hii ambayo tayari imerahisisha maisha kwa mamilioni ya wananchi wanaoutumia kutumiana pesa na kupata huduma mbalimbali katika nchi mbalimbali za Afrika mojawapo ikiwa ni Kenya na Tanzania.

kikao cha baraza la madiwani chafanyika mkoani iringa leo

$
0
0
 Mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Pudenciana Kisaka akizungumza wakati wa kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika katika ukumbi Siasa ni Kilimo, kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Steven Mhapa.
 Baadhi ya madiwani wakifuatilia majadiliano katika kikao hicho yakiendelea katika kikao cha baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Iringa katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo.
 Baadhi ya wakuu wa idara wa halmshauri ya wilaya ya Iringa wakifuatilia majadiliano katika kikao hicho yakiendelea katika kikao cha baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Iringa katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo(picha na Denis Mlowe)
 Madiwani wakichangia majadiliano.

UNRWA official breaks down on live TV

Serikali ya Comoro yakabidhi eneo kwa Ubalozi Tanzania nchini humo

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje wa Muungano wa Visiwa vya Comoro,Mhe. El-Anrif Said Hassane amekabidhi rasmi eneo lililototewa na Serikali ya Comoro kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ajili ya ujenzi wa Ubalozi wa Tanzania mjini Moroni. 

Hafla ya makabidhiano hayo imefanyika Wizara ya Mambo ya Nje ya Comoro ambapo Mhe. Waziri El-Anrif amemkabidhi Mhe. Chabaka F. Kilumanga, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Comoro, funguo za majengo matatu yaliyopo katika eneo hilo. Tukio hilo lilishuhudiwa pia na Mhe. Ahamada El-Badaoui Mohamed Fakih, Balozi wa Comoro nchini Tanzania.

Sambamba na kukabidhiana eneo hilo, Mhe. Balozi Kilumanga na Mhe. Waziri El-Anrif walipata fursa ya kuzungumzia masuala mbalimbali yanayohusu namna ya kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Comoro kwa maslahi ya pande zote mbili.
Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Comoro, Mhe. Chabaka F. Kilumanga (katikati) akionyesha funguo aliyokabidhiwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Muungano wa Visiwa vya Comoro,Mhe. El-Anrif Said Hassane (kulia) ikiwa ni ishara ya kukabidhiwa eneo lililototewa na Serikali ya Comoro kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ajili ya ujenzi wa Ubalozi wa Tanzania mjini Moroni
Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Comoro, Mhe. Chabaka F. Kilumanga (kushoto) akiwa katika mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Muungano wa Visiwa vya Comoro,Mhe. El-Anrif Said Hassane

KAMPUNI YA BIMA YA RESOLUTION ILIVYOKUTANA NA WATEJA WAKE

$
0
0
Kampuni ya Bima ya Resolution mwishoni mwa wiki iliyoisha iliaanda hafla ya kufuturisha wateja wake katika hoteli ya Serena, jijini Dar es Salaam. Hafla ilihudhuriwa na Sheikh Msaidizi wa Dar es Salaam, Sheikh Athuman Makumbaku.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa hafla hiyo, Meneja Mkuu wa Resolution Insurance nchini Tanzania, Bwana Oscar Osir alisema, "Tunawashukuru sana kwamba mmehudhuria hafla hii na tunawapongeza kwa uvumilivu wenu katika mwezi huu mkuu wa Ramadhan.”.

Naye Sheikh Makumbaku alisema, "Kwa niaba ya ndgug zangu Waislamu ningependa kuwashukuru Resolution Insurance kwa kutukumbuka wakati wa Mwezi huu Mtukufu wa Ramadhan. Pia ningependa kuwahimiza Waislamu wenzangu kutia maanani amri wakati wa Mwezi Mtukufu. Tuonesha upendo na uvumilivu kwa wote, kusameheana na kuwasaidia wale ambao hawana uwezo wa kujisaidia”.

Bwana Osir alimaliza kwa kusema, "Tunashukuru sana kwa ushirikiano wenu kwani ndiyo inatupa motisha ya kuendelea kuwapa huduma bora zaidi. Katika shughuli za kuwapa Huduma zilizo bora zaidi na zinazoweza kuwahudumia ukiwa hapa nchini na hata sehemu yeyote duniani. Ningependa pia kuwahakikishia kuwa tutaendelea kuwapa bidhaa bora na kuwasikiliza ili tutimize mahitaji yenu".
Meneja Mkuu wa Resolution Insurance, Oscar Osir akizungumza na wageni waalikwa wakati wa Futari iliyoandaliwa na Resolution Insurance iliyofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Sheikh Mkuu msaidizi wa Mkoa wa Dar es Salaam, Athuman Mkambaku akizungumza na wageni waalikwa wakati wa Futari iliyoandaliwa na Resolution Insurance iliyofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Wageni waalikwa wakipata Futari iliyoandakliwa Resolution Insurance iliyofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Baadhi ya wageni waalikwa wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya futari iliyoandaliwa na Resolution Insurance iliyofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

Mkurugenzi wa Idara ya Habari atembelea Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali Wizara ya Mambo ya Nje

$
0
0
Mkurugenzi wa Idara ya Habari-MAELEZO, Bw. Assah Mwambene akizungumza na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali cha Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Mkumbwa Ally alipotembelea Kitengo hicho kwa ajili ya kujionea shughuli mbalimbali zinazofanyika.
Bw. Mwambene akiangalia moja ya machapisho aliyopatiwa na Bw. Mkumbwa kuhusu Wizara.
Picha na Reginald Philip

TAARIFA KWA UMMA: MABADILIKO YA MUDA WA SAA ZA KAZI KATIKA OFISI ZA MFUKO WA TAIFA WA BIMA YA AFYA

GURU G LOVER ALONGA NA VIJIMAMBO AFUNGUKA KUHUSU YEYE NA ALI KIBA NI KWANINI WALISHINDWANA

$
0
0
Dj G Lover Dj wa siku nyingi katika anga ya muziki Tanzania na Dj anaepambana na kuupaisha muziki wa kizazi kipya kila kukicha leo Ijumaa Aug 1, 2014 alifanya mahajiano ya simu na VIJIMAMBO  aliongelea mambo mengi kuhusu wasanii na sababu gani walishindwana yeye na Ali Kiba MSIKILIZE
Picha juu na chini Dj G Lover akiwa na wasanii mbambali wa Bongo Flava

Top African stars join ONE in Washington DC for Historic US-Africa Leaders Summit

$
0
0
WASHINGTON—Africa’s top artists, including Nigeria’s Femi Kuti and D’Banj, South Africa’s Judith Sephuma and Congo DRC’s Fally Ipupa will be traveling with Manchester City soccer star Yaya Toure to Washington D.C. 4-7 August with The ONE Campaign to play an active role in shaping the conversation about the US-Africa relationship at the historic US-Africa Leaders Summit.
The full list of artists are: A.Y. (Tanzania), Buffalo Souljah (Zimbabwe), D’Banj (Nigeria), Fally Ipupa (DRC), Femi Kuti (Nigeria), Judith Sephuma (South Africa), Omawumi (Nigeria), Victoria Kimani (Kenya) and Wax Dey (Cameroon).
President Barack Obama will welcome leaders from across the African continent to the nation’s capital for a three-day summit beginning 04 August, marking the largest gathering any U.S. president has ever held with African heads of state and government. The summit aims to strengthen ties between the United States and Africa, one of the world’s most dynamic and fastest growing regions.
During the US trip, the artists will hold advocacy meetings with high-level US officials, Washington Fellows from the Obama administration’sYoung African Leaders Initiative (YALI), and Members of Congress. They will also perform the on 04 August during an event at the Newseum, including the song ‘Cocoa Na Chocolate’.
These artists represent a portion of a larger group, led by D’banj, who came together earlier this year during the official African Union Year of Agriculture to record the number one hit song, “Cocoa na Chocolate” in support of ONE’s pro-agriculture campaign in Africa, Do Agric, It pays.
Their collaboration and advocacy work tapped into the dynamic African youth culture, prompting more than 2 million African citizens to take action and sign ONE’s Do Agric petition. The US summit takes place only weeks after June’s African Union Heads of State and Government Summit in Malabo, Equitorial Guinea where leaders heeded the call of the petition signers in the Malabo Declaration, pledging to increase investments in agriculture, double agriculture production, and create millions of agribusiness opportunities for its large youth population in the Malabo Declaration.
Speaking about the artists’ involvement in the historic summit, Dr. Sipho S. Moyo, Africa Director for ONE, said:
 “These amazing artists and soccer star Yaya Toure represent a new era of hope, where Africans take responsibility for their own destiny. They joined ONE across the continent to play a major role in ensuring a positive agriculture outcome for agriculture in Malabo and they will be in Washington D.C. with us this week to remind African leaders about the need to implement their commitments. And we at ONE, along with our CSO partners, will continue to work with policy makers to ensure this continent wide promise is implemented country-by-country.
The artists will also be meeting with American policy makers to strengthen our ties and ensure that African citizens are taking an active role in writing the continent’s next chapter. For a summit whose theme is "Investing in the Next Generation,” these ONE ambassadors truly are the next generation of African leaders.”
ONE launched the Do Agric campaign in January in support of the official 2014 African Union Year of Agriculture. Growth in agriculture in Sub-Saharan Africa  today is estimated to be 11 times more powerful at reducing poverty than growth in other sectors such as  mining and utilities.
The continent-wide campaign urged African leaders in the months ahaed of the AU meeting in Malabo that the time had come to adopt better agricultural policies that will help tackle youth unemployment, boost the productivity of  African small holder farmers, and help lift millions of Africans out of extreme poverty.

Rais Kikwete awasili Washington kuhudhuria Mkutano wa Viongozi wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Amerika na Africa (US-Africa Leaders summit)

$
0
0
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na baadhi ya maafisa waliofika kumpokea wakati akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dulles tayari kwa Mkutano wa Viongozi wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Amerika na Africa (US-Africa Leaders summit) uliondaliwa na Rais Barack Obama wa unaotaraji kuanza Agosti 4-hadi 6, 2014, ambao utatanguliwa na mikutano mingine ya maendeleo ya sekta mbalimbali na uwekezaji (2-3 Agosti, 2014) jijini Washington DC. Kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Marekani,Balozi Liberata Mulamula.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mkewe Mama Salma Kikwete wakisalimiana na baadhi ya maafisa wa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani wakati walipowasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dulles.PICHA NA IKULU.

Dkt. Shein afungua Maonesho ya Nane Nane Mkoani Lindi leo

$
0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akikata utepe kama ishara ya uzinduzi wa Maonesho ya kilimo ya nane nane kitaifa mwaka huu katika viwanja vya Ngongo Mkoani Lindi leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Viongozi mbali mbali wakati alipowasili katika Viwanja vya Ngongo yanapofanyika maonesho ya Kilimo ya nane nane kitaifa Mkoani Lindi.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akipata maelezo katika banda la Benki kuu ya Tanzania BOT katika maonesho ya kilimo ya nane nane kitaifa Mkoani Lindi katika viwanja vya Ngongo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akipata maelezo katika banda la sekta ya Afya katika maonesho ya kilimo ya nane nane kitaifa yanayofaanyika Mkoani Lindi katika viwanja vya Ngongo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akipata maelezo kutoka kwa Dk.Geoffrey Mkamito Mtafiti wa Mazao ya Mizizi, katika banda la Bodi ya Korosho katika maonesho ya kilimo ya nane nane kitaifa yanayofaanyika Mkoani Lindi katika viwanja vya Ngongo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akipata maelezo kutoka kwa Meneja Biashara na Masoko Numwagile A.Mwaijumba wa Shirika la Nyumbu kuhusu mashine ya utengenezaji wa matofali ya udongo katika maonesho ya kilimo ya nane nane kitaifa yanayofaanyika Mkoani Lindi katika viwanja vya Ngongo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na wananchi wa manispaa ya Lindi Mjini na Vitongoji vyake baada ya kuzindua rasmi maonesho ya kilimo ya nane nane kitaifa katika viwanja vya Ngongo leo Mkoani Lindi. [Picha na Ramadhan Othman Lindi.]

HOTUBA YA MHE DKT.JAKAYA MRISHO KIKWETE KWA WANANCHI, 31 JULY 2014

HOTUBA YA MHESHIMIWA DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KWA WANANCHI, TAREHE 31 JULAI, 2014

WIKI TATU KUELEKEA FAINALI YA SHINDANO LA TANZANIA MPVIE TALENTS (TMT), WASHIRIKI WENGINE WAWILI WAAGA SHINDANO WIKI HII

$
0
0
 Waendeshaji wa Show ya Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) Joti na Lulu wakiwa kwa steji, tayari kwa kuendelea na show hiyo iliyofanyika katika Ukumbi wa Mkaumbusho ya Taifa Jijini Dar Es Salaam.
 Mshiriki Ally Kiwendo ambae alikuwa ni mmoja kati ya washindi watatu kutoka kanda ya Kusini mkoani Mtwara akitoa maneno ya shukrani kwa Kampuni ya Proin Promoitons ambao ndio waandaaji na waendeshaji wa Shindano la TMT mara baada ya kutangazwa kuaga shindano hilo kutokana na Kura kuwa chache, huku pia akiwashukuru watazamaji na wote waliompigia kura
 Joyce Kalinga Mshiriki wa Shindano la TMT ambae apia alikua mshindi kutoka Kanda ya Kati Mkoani Dodoma akitoa maneno yake ya shukrani na pia kuwashukuru wadau, Kampuni ya Proin Promotions na watazamaji na waliompigia kura japokuwa bahati haikuwa yake kutokana na kutolewa kwenye kinyanganyiro hiko kutokana na uchache wa kura kutoka kwa watazamaji
 Lulu na Joti wakitoa maelekezo kwa washiriki wawili wa Shindano la TMT ambao waliweza kutolewa katika kinyanganyiro hiko kutokana na kupata kura chache kutoka kwa watazamaji wa Kipindi cha TMT kinachorushwa Kila Jumamosi saa Nne usiku.

BOFYA HAPA KWA HABARI KAMILI

MAFUNZO YA AWALI KWA WATUMISHI WA HUDUMA ZA MKOBA WA UZAZI YAMALIZIKA JIJINI DAR

$
0
0
Mkurugenzi Mkazi wa Marie Stopes Tanzania, Ulla Muller (kushoto) akielezea jambo wakati akifunga mafunzo ya awali ya IT kwa watumishi wa huduma za MKOBA wa uzazi wa mpango kutoka Mikoa mbalimbali nchini Tanzania.hafla hiyo ya ufungaji mafunzo ilifanyika 2 Agositi 2014 katika chuo cha CBE jijini Dar es Salaam, wakwanza kulia Mhadhiri Msaidizi (ICT), Godfrey Mwandosya, Mkuu wa Idara ya Tekenolojia ya Habari na Mawasiliano.Alex Mwijika, Kaimu Mkuu wa Idara Mathematics (ICT), Nzomwe Mazana.
Mhadhiri Msaidizi ICT, Ogakhan Nyamu akisisitiza jambo wa hafla hiyo.
watumishi huduma za MKOBA wa uzazi wa mpango kutoka Mikoa mbalimbali nchini Tanzania walioitimu mafunzo ya IT wakisikiliza Mkurugenzi Mkazi wa Marie Stopes Tanzania, Ulla Muller, wakati akifunga mafunzo hayo. PICHA NA PHILEMON SOLOMON

FIBA Africa yapata Rais Mpya

$
0
0
Mkutano Mkuu wa Shirikisho la mpira wa kikapu Barani Africa umemalizika nchini Madagascar,ambapo katika mkutano huo alichaguliwa Rais mpya wa FIBA Africa ambaye ni Ndg. Humane Niang kutoka nchini Mali, pia Ndg. Hisham El Hariri kutoka Misri alichaguliwa kuwa Rais wa FIBA Africa zone V.
Pichani Ndg. Niang akipongezwa na baadhi ya Wajumbe waliohudhulia Mkutano huo akiwepo Ndg. Phares Magesa (katikati).

WAKE WA VIONGOZI WAMTEMBELEA MAMA MARIA NYERERE NYUMBANI KWAKE MSASANI

$
0
0
Mke wa Waziri Mkuu,Mama Tunu Pinda (kulia) ambaye ni mlezi wa kikundi cha Wake waViongozi (NEW MELLENIUMWOMEN GROUP) akimsikiliza kwa makini Mama Maria Nyerere wakati walipo mtembelea nyumbani kwake kwa ajili yakumjulia hali pamoja na kumpatia zawadi mbalimbali kutokana na mchango wake mkubwa aliokuwa anampa Baba wa Taifa ambao ulisaidia kuleta amani utulivu na maendeleo ndani ya nchi na nje ya Tanzania.
Mama Maria Nyerere na MamaTunu Pinda wakiangali picha zao walizo pigwa na Mama Othmani kwenye simu ya kiganjani wakati kikundi cha wake wa viongozi (NEW MELLENIUMWOMEN GROUP) walipo mtembelea Mama Nyerere nyumbani kwake Msasani kumjulia hali.
Kikundi cha wake wa viongozi wakiwa katika picha ya pamoja na Mama Maria Nyerere walioketi (katikati) Mama Tunu Pinda Mama (wa pili kushoto walioketi) Mama Regina Lowasa (kushoto) Mama Sophia Kawawa (wa pili kulia walioketi) akifuatiwa na Mama Sumaye.Picha na Chris Mfinanga.

Uongozi na wachezaji wa Timu ya Soka ya African Coast wamuomba radhi Balozi Seif Ali Idd

$
0
0
Uongozi na wachezaji wa Timu ya Soka ya African Coast ya Kijiji cha Upenja umemuomba radhi Mbunge wa Jimbo la Kitope Balozi Seif Ali Iddi kufuatia uamuzi wa Timu hiyo kuruhusu kufanyika kwa Mkutano wa Hadhara wa Chama cha Upinzani uliozaa kashfa na matusi dhidi ya mbunge huyo.

Wachezaji hao waliomba radhi hiyo Mbele ya Mbunge huyo hapo katika Ukumbi wa Tawi la CCM la Kijiji cha Upenja kilichomo ndani ya Jimbo la Kitope Wilaya ya Kaskazini “B “ mkutano uliohudhuriwa pia na Wazee na baadhi ya viongozi waasisi wa CCM wa Kijiji hicho.

Akiwasilisha salamu hizo za kuomba radhi Msemaji wa Timu hiyo ya Soka ya African Coast Juma Mshamba alisema wachezaji na Viongozi wa clabu hiyo walifikia uamuzi wa kukutana na Uongozi wa Wazee wa Tawi hilo kwa lengo la kuomba radhi baada ya tukio hilo la mvua za matusi dhidi ya Viongozi wao.

Juma Mshamba alisema pamoja na nia safi ya Viongozi na Wachezaji hao ya kuruhusu Mkutano huo, lakini pia zilitumika mbinu za hadhaa kwa Viongozi wa upinzani kuahidi kuwapatia fedha za kuendesha klabu yao pamoja na kuwatengenezea uwanja wao mambo ambayo hakuna hata moja hadi sasa lililotekelezwa na chama hicho cha upinzani.

Akizungumza na Wazee, Viongozi na wachezaji hao wa African Coast Mbunge wa Jimbo la Kitope Balozi Seif Ali Iddi alisema tayari ameshawasamehe tokea wakati wa mshindano ya Jimbo la Kitope ya Kombe la ZAWEDA ambapo timu hiyo iliidhinishwa kushiriki kwenye mashindano hayo.

Balozi Seif ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliwaasa wanamichezo hao kujiepusha na vitendo vyote vinavyoashiriadalili za uvunjifu wa amani katika maeneo yao.

Naye Mke wa Mbunge huyo wa Kitope Mama Asha Suleiman Iddi aliwatanabahisha wanamichezo hao kuwa mbali na udanyanyifu wa baadhi ya watu wanaowatumia wanamichezo katika kushiriki kufanya maovu mitaani.
Mzee wa Timu ya African Coast Ali Soud akipokea mchango wa Mbunge wa Kitope Balozi Seif kwa ajili ya kulipa deni ya kambi ya timu hiyo pamoja na ada ya timu, kadi za wachezaji pamoja na Mrajisi wa michezo.
Mbunge wa Jimbo la Kitope Balozi Seif Ali Iddi akimkabidhi Kepteni ya Timu ya Soka ya African Coast ya Upenja Ali Hassan Mipira,seti ya Jezi pamoja na Fulana za mazoezi kwa ajili ya wachezaji wa timu hiyo iliyomo ndani ya Jimbo lake.

Msemaji wa Timu ya Soka ya African Coast ya Upenja Wilaya ya Kaskazini “ B” Juma Mshamba akiomba radhi kwa Mbunge wa Jimbo la Kitope Balozi Seif hayupo pichani kufuatia uamuzi wa timu hiyo kuruhu uwanja wao kutumika kwa mkutano wa hadhara wa chama cha upinzani ulioporomosha matusi dhidi ya mbunge huyo.

Neno La Leo: Mkwamo Wa Katiba Na Msafara Wa Tembo..

$
0
0
Ndugu zangu,

Msafara wa tembo huwa na kawaida ya kutokurudi nyuma,ndio maana porini huzioni nyayo za tembo zenye kwenda mbele na kurudi nyuma.

Ni ukweli, kuwa tembo ndiye mnyama mkubwa porini, na ni mfalme wa pori. Lakini tembo hufika mahali akasumbuliwa na siafu kiasi cha kuweweseka na hata kutamani kulihama pori. Ni kwa kosa la tembo kukanyaga kichuguu cha siafu. Naam, siafu mia tano ni wengi kuliko tembo mmoja, pamoja na ukubwa wa tembo.

Na adili ya jambo hilo ni ukweli kuwa duniani hapa mkubwa anapaswa kumuheshimu mdogo, na mdogo pia kumuheshimu mkubwa.Hivyo, wanadamu tunapaswa kuheshimiana.

Kwenye hili la hofu ya mkwamo wa mchakato wa Katiba nayaona mapungufu mawili kwa pande zinazohusika; KUTOHESHIMIANA na KUTOAMINIANA.

Kwenye awamu ya kwanza ya Bunge Maalum la Katiba mawili hayo yalijidhihiri. Hakika UKAWA na CCM kwa pamoja wamebeba dhamana kubwa ya hatma ya nchi yetu. Kuna makosa yameshafanyika tangu kuanza kwa mchakato huu. Hatupaswi kama taifa kuwa kama tembo kwenye msafara wao, kwamba hawarudi nyuma.

Kabla ya kuendelea na mchakato huu wa Katiba, kama taifa, na kwa kupitia viongozi wakuu wa UKAWA na CCM. Viongozi hao, kwa namna yeyote ile, wana lazima ya kujiandalia au kuandaliwa mazingira ya kukaa meza moja kama Watanzania. Kuendelea kufanya vikao vya siri na kuyapitia mapungufu yaliyojitokeza kwenye Awamu ya kwanza, kisha watoke kwa pamoja na kwa kauli moja ya namna ya kwenda mbele.

Wakishindwa kukaa meza moja,basi,ni heri mchakato mzima ukahairishwa kusubiri wakati muafaka, kuliko kusonga mbele kwa staili ya msafara wa tembo, maana, huko njiani kutakuwa na vichuguu vingi vya siafu vitakavyokanyagwa, na tembo pamoja ukubwa wao, wataweweseka sana porini, na hata kusababisha pori lichafuke. Pori kukosa amani.

RAI YANGU: Kinachoonekana kwa sasa ni kwamba CCM hawako tayari kwa Serikali Tatu, kuna mengine basi, ya muhimu kwa nchi, ambayo CCM wako tayari nayo. Na UKAWA nao hawako tayari kurudi bungeni kwa kujadili Serikali Mbili, kuna mengine pia UKAWA wako tayari nayo na muhimu sana kwa taifa. Na katika dunia hii, si yote anayotaka mwanadamu anayapata katika wakati huo huo anapoonyesha kuyataka, mengine husubiri.

Na kubaki kuelekeza lawama kwa Rais wa nchi na hata kumtaka aombe radhi kwa wananchi hilo nalo haliwezekani na ni kuendelea kupoteza muda. Pamoja na kuwa Urais ni taasisi, lakini, Rais naye ni mwanadamu kama wengine, si malaika, na ni MwanaCCM pia, si Mwana UKAWA.

Na katika dunia tunayoishi, yumkini kuna UKAWA ndani ya CCM na CCM ndani ya UKAWA. Hivyo,yawezekana haya tunayoyashuhudia si mepesi sana. Si mepesi maana hata kuamini kuwa Bunge liendelea na UKAWA warudi Bungeni ina maana ya kuendelea kwa malumbano na ushindani wa CCM na UKAWA. Ni kwa vile itakuwa na tafsiri ya kuendelea kuwepo Bungeni kwa wajumbe wa ' Umoja wa Kutetea Katiba ya Wananchi' dhidi ya ' CCM'. Nao watakuwa wakitetea Katiba ya nani? Ni mazungumzo tu ya pande mbili katika mazingira ya kuheshimiana na kuaminiana ndiyo yanapaswa kuandaa mazingira ya wajumbe wa Barazala Katiba kurudi Bungeni kwa maslahi ya taifa na si makundi yao.

Na zaidi, tumwamini Rais wetu katika dhamira yake ya kuanzisha mchakato wa kupata Katiba Mpya. Tumsaidie pia, maana, yumkini, Katiba Mpya ni moja ya mambo anayotaka kuyaacha nyuma yake na akumbukwe nayo-legacy.

Hivyo, tulikofikia ni mahali ambapo kila mzalendo wa nchi hii anapaswa kujisikia huzuni na hata kujutia. Tulikofikia hakuna mshindi, sote tumeshindwa, kama taifa. Maana, tumetumia rasilimali nyingi kama taifa, muda na fedha . Mchakato huu kukwamia hapa ni aibu kwa taifa. Na wahenga walisema; majuto ni mjukuu, na kwamba yaliyopita si ndwele, tugange yajayo.

Kongamano la Kitaifa la Katiba lililoandaliwa na Baraza la Vyama Vya siasa, liwe ni fursa ya kutukwamua kutoka tulikokwama, hivyo, kusonga mbele kwa KUHESHIMIANA na KUAMINIANA. Ndio,kongamano hilo litoke na ' AZIMIO LA DODOMA' la kusonga mbele kama taifa.

Ni Neno La Leo.

OLD IS GOLD NA SPICE MODERN TAARAB KUFUNIKA NDANI YA SAFARI CARNIVAL LEO

$
0
0
WAPENZI wa nyimbo za zamani za taarabu asilia nchini, leo wanatarajiwa kupata burudani safi na ya aina yake  kutoka kundi la Spice Modern Taarab,  ndani ya ukumbi wa  Safari Carnival uliopo Kawe, (opposite) na Clouds fm katika gate la kuingilia Escape 1.

Kwa kiingilio cha sh 5000 tu, kuanzia saa mbili usiku mpaka majogoo.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Fabak Fashions, Asia Idarous Khamsin, ambao ni miongoni mwa wadhamini wa onyesho hilo, amewasihi wadau kujitokeza kwa wingi kuuenzi usiku huo kwa kukumbushiana enzi.

Asia Idarous alisema onyesho hilo maarufu kwa jina la ‘Old is Gold na Spice Modern Taarab,’  tayari limeanza kujizolea umaarufu kwa wadau ambapo wanakutana kwa pamoja na kufurahia shoo hizo.
“Kwa kiingilio cha sh 5,000 tu, wadau watafurahia shoo kabambe kutoka kwa Spice Modern Taarab kwa kupata nyimbo za mwambao hasa zile zilizokuwa zikipendwa, kuanzia saa 2 usiku hadi saa 8 usiku,” alisema Asia Idarous.

Spice Modern taarab wanatamba na nyimbo mbalimbali ambapo watapiga na nyimbo zilizowahi kutamba miaka ya zamani kama ambazo zimekuwa gumzo kipindi hicho ni pamoja na ‘Pendo kitu cha hiari’, ‘Dunia ina fisadi,’ ‘Kasha’ na nyingine nyingi.
Aidha aliwataja Wadhamini wengine katika usiku huo wa taarabu asilia ni Times FM, Fabak Fashions na Safari Carnival.
Viewing all 110185 articles
Browse latest View live




Latest Images