Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110186 articles
Browse latest View live

new anti-theft tech


UZEE MWISHO CHALINZE..

uzushi wa kifo feki cha muigizaji Will Smith watikisa dunia

$
0
0
Taarifa za kifo cha mwigizaji nguli wa Marekani Will Smith zilisambaa kama moto nyikani mapema wiki hii, na kusababisha mtafaruku kwa mashabiki wake duniani kote. Hata hivyo taarifa ya jana Ijumaa February 21, 2014 zimethibitisha kuwa habari hizo za uzushi na uwongo ni mojawapo ya nyingi zinazohusisha watu maarufu. 
Kwa mujibu wa uchunguzi wa kina uliofanywa na Globu ya Jamii, ukweli ni kwamba mwigizaji huyo aliyetamba katika filamu kadhaa ziiwemo The Pursuit of Happyness, Men in Black orThe Fresh Prince of Bel-Air bado anadunda. 
 Uzushi wa kifo cha Will Smith unasemekana ulianzia kwenye ukursa mmoja katika mtandao wa jamii wa Facebook siku ya Alhamisi uliokuwa na kichwa cha habari ‘R.I.P. Will Smith’ n kuvutia wasomaji takriban milioni moja. 
Waliosoma ukurasa huo walishawishika kuamini taari hiyo iliyosomeka: “Mnamo majira ya saa 11 a.m. ET siku ya Alhamisi (February 20, 2014), mwigizaji wetu kipenzi Will Smith alitangulia mbele ya haki. Will Smith alizaliwa September 25, 1968 huko Philadelphia. Tutamkosa lakini hatutomsahau. Tafadhali onesha kuguswa kwako kwa ku ‘like’ ukurasa huu.
Ghafla tu mamia ya mashabiki wakaanza mara moja kuandika ujumbe wa rambirambi kwenye ukurasa huo wa Faceboook, wakionesha kusikitishwa kwao kwa kifo cha muigizaji na mwanamuziki huyo mwenye umri wa miaka 45. 
Kwenye twitter nako taarifa hiyo ilivuma balaa. Wakati baadhi ya mashabiki waliiamini taarifa hiyo, wengine waliguna na kujiuliza mara mbilimbili bila shaka wakichukulia uzoefu wa taarifa feki za aina hiyo zilizopata kutokea miezi ya karibuni. Wengine pia waliuliza iweje habari ya kifo cha mtu kama Will Smith isitangazwe kwenye vyombo vikubwa vya habari. 
Utafiti pia ukaonesha kuwa asilimia 80 ya waliohojiwa kuhusu uzushi wa kifo cha Will Smith sio za kufurahisha kidogo. Ndipo Ijumaa hii (Februari 21) wawakilishi wa Will Smith walithibitisha kuwa hajafa. 
“Anajiunga katika orodha ndefu ya watu maarufu walioathirika na uzushi kama huo. Yeye bado yu hai na buheri wa afya, acha kuamini unachokiona mitandaoni”, walisema. 
 Baadhi ya mashabiki walielezea hasira zao kwa taarifa hiyo feki, wakisema ni ya kuhamanisha na kujeruhi hisia zao. Wengine walisema taarifa hiyo inaonesha ni jinsi gani Will Smith anavyojulikana ulimwenguni kote, ikiwemo Tanzania ambako nako taarifa za kifo hicho feki zimezagaa kwenye mitandao ya jamii. 
 Hivi tunavyoongea kituo maarufu cha TV cha Home Box Office (HBO) iko katika hatua za mwisho kuandaa onesho la kuchekesha litalomhusisha Will Smith (kulia) pamoja na mwanamuziki mahiri Jay Z (wa pili toka kulia). Wawili hawa (wanaoonekana pichani na wake zao Beyonce na Jada Pinckett-Smith)  pia kwa pamoja wanatengeneza filamu iitwayo ‘Annie’ inayotegemewa kuzinduliwa mwezi Desemba mwaka huu. Vile vile kampuni ya Will Smith ya Overbrook Entertainment imeungana na kampuni ya Jay Z Roc Nation kuandaa filamu ya ‘Free Angela & All Political Prisoners’.

Will Smith na mkewe Jada Pinckett-Smith walizuru Tanzania mwishoni mwa mwezi Agosti mwaka 2008, na kutembelea Zanzibar na Arusha, wakati huo akiwa kama Balozi wa Hisani wa kupambana na malaria duniani. Globu ya Jamii ilirekodi ujio huo kama picha zinavyoonesha hapa chini.
Will Smith akiongea na Rais wa Zanzibar wakati huo (Agosti 30, 2008) Dkt Amani Abeid Karume alipomtembelea Ikulu, Zanzibar katika ziara yake ya Tanzania akiwa kama Balozi wa Hisani wa kupambana na Malaria duniani
Will Smith akimpa zawadi ya kitabu Dkt Karume
Will Smith na mkewe Jada Pinckett-Smith wakipozi na Dkt Karume na Mama Shadya Karume Ikulu, Zanzibar
Will Smith na mkewe wakiwasili hoteli ya Kilimanjaro jijini Dar es salaam Siku ya Jumanne ya Agosti 26, 2008
Will Smith na mkewe pamoja na mlinzi wao wakifurahia kamera ya Globu ya Jamii mara baada ya kuwasili Kilimanjaro hotel
Mhudumu wa hoteli ya Kilimanjaro akiwapokea Will Smith na mkewe pamoja na mlinzi wao
Will Smith akiwa na Mtendaji Mkuu wa kiwanda cha kutengeneza Vyandarua cha A to Z jijini Arusha, Bw. Anuj Shah, alipotembelea siku ya Jumatatu ya Septemba 1, 2008 

ngoma azipendazo ankal

$
0
0
 Jabali la muziki Marijani Rajab linakupa 'Georgina' halisi

Article 17

KAMPUNI YA MONABAN YAKABIDHI MSAADA WILAYA YA HAI KWA AJILI YA WAHANGA WA MAAFA

$
0
0
DSCF2880Mkurugenzi wa kiwanda cha kuzalisha unga kilichopo jijini Arusha Bw.Philemon Mollel akimkabidhi Mkuu wa wilaya ya Hai Mh.Novatus Makunga msaada wa Tani nne za unga  wenye thamani ya shilingi Milioni 4.2,baada ya wilaya yake kupata maafa yaliyotokana na mvua zilizoambatana na upepo mkali na kusababisha badhii ya watu kukosa nyumba za kuishi
DSCF2878Mkurugenzi wa kiwanda cha kuzalisha unga Arusha Philemon Mollel akiongea mbele ya wanakijiji(hawapo pichani)namna alivyoguswa na maafa hayo yaliyopelekea kutoa msaada huo huku kiwataka wafanyabishara,makampuni,watu binafsi kujitokeza kuwasaidia waanga wa maafa hao,mbali na msaada huo wa tani nne za unga pia alitoa shilingi Milioni moja kwaajili ya waanga.
DSCF2866Kina mama ambao ndio waathirika wa kubwa wa maafa hayo wakisubiria zoezi la kugawiwa chakula cha msaada 
DSCF2870Mtendaji wa kijiji Bi.Trea Ramadhani akitoa shukrani zake za dhati kwa mmiliki wa kiwanda cha kuzalisha unga kilichipo Arusha
DSCF2882Mkuu wa wilaya Novatus Makunga akimkabidhi msaada uliotolewa na kampuni ya Monaban ,mtendaji wa kijiji cha  kwa sadala Bi.Trea Ramadhani msaada uliogharimu zaidi ya milioni 4,Kushoto ni kaimu mkurugenzi Bw.Zabdieli Moshi.

Nyumba ya familia ya Bibi Aziza Mohammed baada ya kuezuliwa paa
 Bibi Aziza Mohammed kama anavyooneka katika picha baada ya mvua kusababisha mafaa makubwa kwake hali iliyosababisha yeye kuishi chooni na mjuuku wake.(Picha na Pamela Mollel wa jamiiblog).
PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

Article 15

WAKIWEZESHWA WANAWEZA.!


SEMINA YA WASANII WA MBALIMBALI WA MUZIKI NA FILAMU YAFANYIKA JIJINI DAR

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji Kampuni ya Chief Promotion,Amoni Mkoga akizungumza wakati wa semina ya wasanii wa Muziki pamoja na wale wa Filamu iliofanyika katika ukumbi wa Vijana Kinondoni jijini Dar es Salaam 21 Februari-2014. lengo la semina hiyo ilikuwa ni kuzungumzia hakimili kwa wasanii pamoja na kujiunga na mifuko ya jamii ili kujiwekea akiba ya baadae (kushoto), Afisa Mwandamizi wa Huduma kwa Mlipa Kodi TRA, Msafiri Mbibo (watatu kulia), Kaimu Afisa Kumbumbuku COSOTA Bw Philemon Kilaka na wakwanza kulia Kaimu Mwanasheria COSOTA Bw,Zephania Lyamuya.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasilano,Promosheni na Uhamasishaji wa Mfuko wa Uthibiti wa Mifuko ya  Hifadhi za Jamii Nchini (SSRA), Sarah Kibonde akiwaelezea wasanii kuhusiana na mifuko mbalimbali ya hifadhi ya jamii kama NSSF,PSPF ,LAPF,GEPF,PPF,NHIF juu ya faida pale watapofikia muda wakustaafu kazi kisanii au kupatwa na matatizo mbalimbali. (katikati), Mwanasheria COSOTA Bw,Zephania Lyamuya (kusho), Kaimu Afisa Kumbumbuku COSOTA Bw Philemon Kilaka.
Afisa Mwandamizi wa Huduma kwa Mlipa Kodi TRA, Msafi Mbibo akiwaelezea wasanii mwongozo wa utumiaji mashine maalumu za kodi za kielekitroniki (EFDs), wakati wa semina ya hatimiki kwa sanii mbalimbali wa bongo movie pamoja na muziki.
Kaimu Afisa Kumbumbuku COSOTA Bw Philemon Kilaka.akiwaezea wasanii jinsi hakimiliki na mikataba katika kazi za sanaa.

RT WAMPONGEZA WAZIRI MEMBE KWA KUUNGA MKONO KUENDELEZA RIADHA TANZANIA

$
0
0
Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Anthony Mtaka , akizumgumza na Waandishi wa Habari mjini Morogoro kutoa pongezi na kumshukuru Waziri Membe .

Na John Nditi, Morogoro

RAIS wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Anthony  Mtaka  amemshukuru Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe  kwa kuanzisha diplomasia ya michezo na nchi za nje pamoja  na kufadhili maandalizi ya wanariadha 40 na makocha sita.

Wanamichezo  na makocha hao wanapelekwa nje kwa ajili ya kujinoa  ili kuwa tayari kwa ajili ya Mashindano ya Jumuiya ya Madola  yanayotarajiwa kufanyika kuanzia Julai 23 hadi Agosti 3, mwaka huu , Glasgow , Scotland. 

Rais huyo wa RT alimshukuru Waziri Membe, alipozungumza  na waandishi wa habari Mjini Morogoro , Februari  21, 2014 na kusema  kitendo  cha kuanzisha diplomasia ya mchezo  na nchi za  nje  kimetoa  majawabu kwa wanamichezo na viongozi wa Tanzania wanalodeni  la kurejea na  medali za kutosha kutoka kwenye  mashindano hayo. 

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LEO TAREHE 22 .02.2014

IN LOVING MEMORY OF OUR BELOVED MOTHER ESTHER NYIMBO BADI

$
0
0

No words can express the pain we felt when we lost you on Wednesday 22nd February 2012 at 6.30 p.m. Over the two years, precious memories of your beautifully life have been our only comfort.

We remember your affectionate smile, the sweet sound of your voice, your kind and most generous heart that would have a place for everyone.

We count our self lucky to have held a mother like you, and we thank GOD for the incredible times we shared. We miss you greatly, but we know you are happy in Heaven watching over us, and praying for us.

Affectionately remembered by your children, Blandina, Bertha, Stella, Gern, Lilian, John and Upendo. You’re in laws Cashmir, Modestus, James, Kenny and Afro and Your Grandson’s Joakim, Jeff, Abraham, Faith, Deborah, Caleb, Karen, Sara, Brandon, Dillan, Esther, Hilary, Suzana and Edson.  

Rest in Peace Mummy.

DAKIKA 90 ZA DUNIA: Kwanini Facebook imetumia dola bilioni 19 kununua WhatsApp?

$
0
0
Kama wewe ni mmoja wa wanaotumia njia ya mawasiliano iliyojipatia umaarufu ya WhatsApp, basi ujue kuwa nawe ni miongoni mwa wateja takribani nusu bilioni walioufanya mtandao huo kuwa maarufu zaidi duniani kwa kipindi kifupi tu.
Ni umaarufu huu uliofanya kampuni kubwa ya mawasiliano ya Facebook wiki hii kuona umuhimu wa kutumia dola za kimarekani bilioni 19 kununua WhatsApp.
Lakini kwanini kampuni itumie kiasi hicho kikubwa kwa kampuni kama hii?
Hii ni sehemu ya ripoti ya Jamii Production kwenye kipindi cha DAKIKA 90 ZA DUNIA kinachorushwa na kituo cha Radio cha Capital FM cha Dar Es Salaam Tanzania kila Jumamosi kuanzia saa moja na nusu asubuhi (7:30 AM).
Hii ilikuwa ripoti ya Februari 22, 2014

KENYA, TANZANIA, UGANDA MEETING ON TOURISM AND WILDLIFE MANAGEMENT ISSUES CONCLUDES IN ARUSHA

$
0
0
East African Community

East African Community Secretariat Arusha; 21 February 2014: The meeting of the Ministers/Cabinet Secretary responsible for Tourism, Wildlife Management, and EAC Affairs of the Republic of Kenya, the United Republic of Tanzania, and the Republic of Uganda to resolve their ongoing differences in tourism and wildlife management under the auspices of the EAC Secretariat concluded 20 February, 2014 at the EAC Headquarters in Arusha, Tanzania

The 17 to 20 February 2014 meeting was held to discuss among others, Partner States denying entry of tourist vehicles registered in other Partner States; harassment of driver guides at the border crossings; disparities in fees charged; cross border cooperation in wildlife law enforcement; and cooperation and support in addressing multi-lateral environment agreements. 
For more of this and other EAC news today
CLICK HERE

WAZIRI MKUU,MIZENGO PINDA AFUNGUA SEMINA YA JUMUIYA WAZAZI NGAZI YA TAIFA,MKOANI DODOMA LEO

$
0
0
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akihutubia wakati wa ufunguzi semina ya viongozi na watendaji wa Jumuiya ya Wazazi Ngazi ya Taifa, mikoa na Wilaya nchini iliyofanyika kwenye ukumbi wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM mjini Dodoma Februari 22, 2014wakimsikiliza Waziri Mkuu, Mizengo Pinda wakati alipofungua semiana hiyo.
Washiriki wa Semina ya viongozi na watendaji wa Jumuiya ya Wazazi Ngazi ya Taifa,mikoa na Wilaya nchini iliyofanyika kwenye ukumbi wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM mjini Dodoma Februari 22, 2014.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiongozana na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania,Abdallah Majura Bulembo (kulia) na Makamu wake Dogo Idd Mabrouk (Wapili kushoto) na Mjumbe wa Kamati yaUtekelezaji ya Jumuiya hiyo,Mohammed Sif Khatib (wapili kulia) kutoka kwenye ukumbi wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM mjini Dodoma baada ya kufungua semina viongozi na watendaji wa Jumuiya ya Wazazi Ngazi ya Taifa,mikoa na Wilaya nchini ,Februari 22, 2014.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizuzungumza na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania, Abdallah Majura Bulembo (kulia) na Makamu wake Dogo Idd Mabrouk (Wapili kushoto) na Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya hiyo, Mohammed Seif Khatib (wapili kulia) baada ya kufungua semina viongozi na watendaji wa Jumuiya ya Wazazi Ngazi ya Taifa,mikoa na Wilaya nchini , kwenye ukumbi wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Februari 22, 2014. Kushoto ni Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya hiyo Adam Malima. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

Mtanzania mwenzetu,elisha bahunde apata ajali na kuvunjika miguu yote miwili

$
0
0
Mtanzania Elisha Bahunde jina maarufu Eric ambaye siku ya Jumamosi Feb 15, 2014 alipata ajali Jimbo la Indiana iliyopelekea kukatika kwa miguu yote miwili na mkono wa kulia na baadae kuhamishiwa Jimbo la Maryland kwa matibabu zaidi kwa sasa yupo University Of Maryland Medical Center iliyopo 22 S Greene St, Baltimore, MD Ghorofa ya 6 chumba # 8 na anatumia jina la Elisha Bahunde.ama kweli hujafa hujaumbika na Mwenyezi Mungu ndiye mueza wa kila jambo,Mdau huyu wiki iliyopita alishiriki kwenye Kijiwe cha Ughaibuni (muangalie kwenye video hapo chini) ameva shati la njano na amekaa karibu na Ally Bambino


Video streaming by Ustream
 Elisha Bahunde akiwa chumba # 8 ghorofa ya 6 alipolazwa tangia siku ya Jumatano Feb 19, 2014 alipoletwa Maryland kwa matibabu zaidi
 Elisha Bahunde au Eric akiwa hana miguu wa mkono kama picha inavyoonyesha.
 Rais wa Jumuiya DMV, Bwn. Idd Sandaly akiwa Hospitalini hapo kumjulia hali mgojwa
 Abdi Makeo amkimjulia hali Elisha Bahunde
 Said Mwamende akimjulia hali Bwn. Eric huku akilengwa na machozi
 Wanajumuiya waliofika kumjulia hali wakiwa hawaamini walichokiona.
Kutoka kushoto ni Abdi Makeo, Saidi Mwamende, Rais wa DMV Idd Sandaly na Jabir Jongo wakiwa chamba cha mapumziko baada ya kumaliza kumjulia hali Elisha Bahunde kwa jina lingine Eric

YANGA YAINYOA RUVU SHOOTING BAO 7-0 UWANJA WA TAIFA JIJINI DAR LEO

$
0
0
 Mchezaji wa Yanga, Juma abdul akimtoka beki wa Ruvu Shooting, Said Madega.

 Mshambuliaji wa Yanga, Emmanuel Okwi akimpiga chenga kipa wa Ruvu Shooting, Abdalah Ramadhan na kuipatia timu yake bao la 3 kwa timu yake.
 Dogo huniwezi.................
 Sasa naenda kufunga......
Golikipa wa Ruvu Shooting, Abdalah Ramadhani akiwa ameshika kiuno baada ya Okwi kupachia bao.
Washambuliaji wa Yanga, Emmanuel Okwi (kulia), na Hamis Kiiza wakishangilia moja ya magoli waliyoifungia timu yao wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara dhidi ya Ruvu Shooting uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Yanga ilishinda 7-0 (Picha zote na Francis Dande)

DKT. SHEIN MGENI RASMI KATIKA HAFLA YA CHAKULA CHA MCHANA KWA WAPIGANAJI WALIOFANIKISHA SHEREHE ZA MIAKA 50 YA MAPINDUZI

$
0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Brigedia Jenerali Sharif Sheikh Othman,pamoja na viongozi wengine alipowasili viwanja vya Kambi ya JKU kama katika hafla ya Chakula cha mchana kwa Maaskari na Makamanda wa Vikosi vya Ulinzi waliofanikisha katika sherehe za Miaka 50 ya Mapinduzi Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akifuatana na Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Abdalla Mwinyi Khamis,(wa pili kulia) na Brigedia Jenerali Sharif Sheikh Othman,pamoja na viongozi wengine alipowasili viwanja vya Kambi ya JKU kama katika hafla ya Chakula cha mchana kwa Maaskari na Makamanda wa Vikosi vya Ulinzi waliofanikisha katika sherehe za Miaka 50 ya Mapinduzi Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein(katikati) Waziri wa Ofisi ya Rais na Utawala Bora Dk.Mwinyihaji Makame,(kulia) akifuatiwa na Brigedia Jenerali Sharif Sheikh Othman,Mkuu wa JKU Kanali Sudi Haji Khatibu,(kushoto) akifuatiwa na Mkuu wa Kikosi cha KMKM Komodoo Hassan na Mkuu wa Mkoa w Mjini Maharibi Abdalla Mwinyi Khamis,wakisimama wakati wimbo wa Taifa ukipiga kabla ya hafla ya chakula kwa wapiganaji wa Vikozi vya Ulinzi katika ufanikishaji wao katika sherehe za kilele cha Miaka 50 ya Mapinduzi.
Baadhi ya Makamanda na wapiganaji wa Vikosi vya Ulinzi na Usalama wakiwa katika hafla ya Chakula cha mchana kilichoandaliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,katika kufanikisha sherehe za miaka 50 ya Mapinduzi Zanzibar hafla ilifanyika jana katika kambi ya JKU kama, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
Brigedia Jenerali Sharif Sheikh Othman,alipokuwa akimkaribisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein katika hafla ya chakula kilichoandaliwa kwa wapiganaji wa vikosi vya ulinzi kwa ufanikishaji wao katika sherehe za kilele cha miaka 50 ya Mapinduzi,sherehe zilizofanyika uwanja wa Amaan Studiuam, 12 januari 2014.
Baadhi ya Makamanda na wapiganaji wa Vikosi vya Ulinzi na Usalama wakiwa katika hafla ya Chakula cha mchana kilichoandaliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,katika kufanikisha sherehe za miaka 50 ya Mapinduzi Zanzibar hafla ilifanyika jana katika kambi ya JKU kama. [Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]

Dkt. Salim Ahmed Salim akutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri

$
0
0
Waziri Mkuu Mstaafu,Dkt. Salim Ahmed Salim akiwa katika mazungumzo na mgeni wake ambaye ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri,Balozi Nabil Fahmy wakati alipomtembelea nyumbani kwake leo Jumamosi 22 Februari 2014.
Waziri Mkuu Mstaafu,Dkt. Salim Ahmed Salim na mgeni wake Wakiangalia picha za ukumbusho. Picha ya pili juu kushoto Dr Salim akiwakilisha credentials zake kwa Rais wa Zamani wa Misri, Gamal Abdul Nasser akiwa kama balozi wa Kwanza wa Tanzania nchini humo.

KAGERA SUGAR YASHINDA RHINO RANGERS 1- 0, SELEMAN KIBUTA AITUNGUA RHINO AKITOKEA BENCHI

$
0
0

Timu zikisalimiana
Na Faustine Ruta, Bukoba
Timu ya Kagera Sugar wakiikaribisha timu ya Rhino Ranger leo kutoka Tabora kwenye Ligi  kuu ya Vodacom (VPL) wameifunga bao 1-0. katika mchezo huo ulio pigwa hii leo jumamosi katika kipindi cha kwanza timu zote mbili zilienda mapumziko zikiwa 0-0. Kipindi cha pili Kagera Sugar walifanya mabadiliko kwa kumuingiza mchezaji wao Seleman Kibuta na katika dakika ya 52 kipindi hicho hicho cha pili mchezaji huyo aliwapachikia bao la pekee. Bao hilo limepatikana baada ya kupigwa frii kiki na Hussein Mohamed(Shabalala) na kugonga posti upande wa juu na hatimaye  Seleman Kibuta kuumalizia mpira huo ndani ya lango la Rhino Rangers.
Bao hilo limedumu mpaka dakika za mwisho wa kipute hicho na Kagera Sugar kumaliza mtanange huo na ushindi wa pointi tatu muhimu kwenye uwanja wao wa Nyumbani Kaitaba. Ushindi huu wa Kagera Sugar umewapandisha hadi nafasi ya tano wakiwa na pointi 26 huku Rhino Rangers wakiendelea kushika nafasi ya mwisho kwenye ligi hiyo wakiwa na pointi 13.
Picha ya waamuzi na timu kapteni wakiteta jambo muda mfupi kabla ya mtanange kuanza
Picha ya pamoja
Viongozi wa timu ya Rhino Rangers pamoja na wachezaji wa akiba
Sehemu ya Kagera Sugar, Viongozi na wachezaji wa akiba
Patashika kwenye lango la Kagera Sugar.
Viewing all 110186 articles
Browse latest View live




Latest Images