Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110091 articles
Browse latest View live

Twanga kupiga na Msondo Jukwaa moja

$
0
0
Bendi za Muziki wa Dansi za African Stars "Twanga Pepeta" na Msondo Ngoma Music, Jumapili tarehe 19 Januari zimepanga kufanya onyesho moja kwa ajili ya kuukaribisha Mwaka mpya wa 2014.

Onyesho hilo limepangwa kufanyika katika ukumbi wa C.C.M kata ya 14 wilayani Temeke na maandalizi yote yamekwisha malizika.

Bendi hizo ambazo zipo kwenye mahusiano mazuri ya muda mrefu, zimeamua kufanya onyesho hilo ili kuwapa burudani mashabiki wao kwa kuukaribisha Mwaka mpya wa 2014.

Kwa Upande wa Twanga Pepeta ambao kwa sasa wanatamba na albamu yao ya "Nyumbani ni Nyumbani" watatumia onyesho hilo ili kuwaonjesha mashabiki ladha mpya za 2014 wakiwa na wakali wao wote wakiongozwa na Kiongozi wao Luizer Mbutu.

Kwa Upande wa Msondo wao wanataraji kumualika aliyekuwa Kiongozi wao Mkuu Mzee Ngurumo ili aje kutoa sapoti ya kuukaribisha Mwaka mpya wa 2014.

Onyesho litaanza mapema saa 12 kwa Msondo kuanza kutoa burudani Kabla ya kuwaachia vijana wao kuendeleza kutoa burudani.

SIMBA NA MTIBWA SUGER KUKIPIGA KESHO UWANJA WA TAIFA JIJINI DAR

$
0
0
MABINGWA wa michuano ya mtani Jembe, timu ya Simba, kesho inashuka katika Uwanja wa Taifa kuvaana na timu ya Mtibwa Sugar, huku kiingilio cha chini kikiwa sh.5000.

Mchezo huo utakaoanza saa 10 jioni, ukiwa wa kirafiki, kwa ajili ya kuziweka timu hizo sawa kabla ya kuanza kwa Ligi Kuu tanzania Bara, inayoanza kutimua vumbi wiki ijayo.

Simba inaingia dimbani ikiwa inatoka kwenye mashindano ya Mapinduzi, ambapo Simba ilichukua ushindi wa pili. Katika mchezo huo Simba iliyopo chini ya kocha Zdravko Logarusic akisaidiana na Suleiman Matola, imepanga kutumia wachezaji wake, wote ili kiwe kipimo tosha kabla ya Ligi Kuu.

Timu hiyo inayoshika nafasi ya nne katika msimamo wa Ligi, imejipanga kuhakikisha inavuka mpaka nafasi ya kwanza huku kocha wao Logarusic, akisema ana uhakika kikosi chake kitaibuka na ushindi.

Logarusic, alisema kuwa mchezo huo ni moja ya mtihani wake wa kutambua kikosi chake, kabla ya kuanza kwa ligi kuu. Alisema ameambiwa kuwa Mtibwa Sugar, ni moja ya timu nzuri hivyo anajua kwake ni kipimo kizuri.

"Nina amini mchezo wetu na Mtibwa Sugar, utakuwa mzuri , kutokana na ubora wa timu hiyo, ninajua itasaidia timu yangu kupata mazoezi mazuri"alisema Logarusic.

Nae kocha wa Mtibwa Sugar, Mecky Mexime, alisema ana amini mchezo huo utakuwa mzuri kwake kutokana na wapinzani wao kutoka katika mashindano.

Mexime alisema kuwa amepata nafasi ya kucheza na timu kubwa, ambayo itampa mazoezi mazuri.

"Nina amini mchezo huo utakuwa mzuri kwangu kwa kuwa nacheza na timu kubwa ambayo imetoka kwenye mashindano"alisema Mexime. Katika mchezo huo viingilio vitakuwa shilingi 20,000 VIP A, shilingi 10,000 katika VIP B, wakati VIP C itakuwa shilingi 7,000 na sehemu ya viti vya orange na bluu itakuwa shilingi 5000.

MWENGE WA JUMUIYA YA MADOLA KUTEMBELEA HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI JIJINI DAR

$
0
0
Mwenge wa Jumuiya ya Madola (Queens Baton Relay) utatembelea Hospitali ya Taifa Muhimbili jumapili ya tarehe 19, Januari, 2014 kuanzia saa tatu kamili hadi saa nne asubuhi. 

Mwenge huo unatarajia kufika Hospitali ya Taifa Muhimbili ukiongozwa na Mheshimiwa Balozi wa Uingereza nchini Tanzania Bi. Dianna Melrose.

Dhumuni la Mwenge huo kimataifa ni kutembelea nchi zote ambazo ni wanachama wa Jumuiya ya Madola katika kuhamasisha maandalizi ya Tamasha la Nne la Michezo na Utamaduni la Jumuiya ya Madola. 

Mwenge huu unakimbizwa kilomita 190,000 kupitia nchi 70 ambazo ni wanachama wa Jumuiya ya Madola. Safari ya mwisho ya Mwenge huu itakuwa Julai 23, 2014, Glasgow, Scotland kwa ajili ya ufunguzi wa sherehe za michezo ya 20 ya Jumuiya ya Madola.

Hii ni mara ya tano Mwenge huu kufika nchini Tanzania na utakuwa nchini kwa siku tatu ukisaidia kuhamasisha ushirikiano, kuimarisha umoja na, kuongeza ari ya wananchi hususani vijana waweze kuelewa nini maana ya michezo ya jumuiya ya madola.

Nia ya mwenge huu kuja Hospitali ya Taifa Muhimbili ni kutembelea watoto wanaougua saratani mbalimbali ili kuwapa matumaini ya kuishi na kwamba jamii inawanathamini. Watoto hawa watapata fursa ya kuushika mwenge huu na kupiga picha kama kumbukumbu muhimu katika maisha yao.

Zanzibar’s Sauti Za Busara festival announces special line-up of DJ events and workshops

$
0
0
Stone Town, Zanzibar – The Santuri Project, a three-year plan to revitalize the music industry in East Africa, funded and coordinated byHIVOS, announces a special line-up of DJ-centered workshops, performances, and networking opportunities to be held in conjunction with the Sauti za Busara festival 12-16 February, 2014.

“We are really excited to open the Santuri Project at Sauti za Busara this year. It’s a chance to take a look at what’s happening with DJ culture in East Africa right now, and should provide some exciting pointers to how the scene and music will develop from here. 

It’s clear the role of DJs and electronic music is growing all the time in the region, and this is a great time to celebrate that fact”, said Project Coordinator David Tinning. “It’s also a opportunity to bring together musicians and DJs to work together, and begin to develop a truly contemporary East African sound for the dance floor”.

Two workshops will be held concurrently 12-14 February: the first workshop, is geared toward industry professionals interested in learning more about new music technologies and new marketing strategies. SoundThread’s Sam Jones will lead the second workshop, aimed at DJs, producers and sound engineers. 

Participants in this workshop will learn more about ways to create DJ-centric tracks that reflect a local identity, style or culture. Specialist input from internationally renowned musicians, producers, DJs and singers who have gathered for the Sauti za Busara festival will be provided for the benefit of all participants in both workshops.

In addition to the workshops, several events will be held at the festival, including Sunset Sessions (DJ performances at sunset each evening that will be live-streamed to the web) and official after-parties designed to showcase East African and global DJ culture to Sauti za Busara festival audiences. DJs participating in the Santuri Safari will have the chance to spin at one of our many festive events, alongside internationally renowned guests.

Produced by the cultural NGO Busara Promotions, Sauti za Busara is widely recognized as one of East Africa’s biggest and best-loved festivals, known for showcasing emerging local and regional talents alongside Africa’s top established acts. The 11th edition will take place during 13-16 February 2014 in Stone Town’s historic Old Fort. 

This year, the festival is headlined by Ebo Taylor (Ghana), Jupiter and Okwess International (DRC), and Sona Jobarteh (Gambia/UK). Tanzanian/Zanzibari acts include Reggae star Jhikoman, Hoko Roro, Seven Survivor, Tausi Women’s Taarab, Swahili Vibes, and many more. Tickets are available online at www.busaramusic.org.

With special thanks to Sauti za Busara 2014 sponsors and donors:  The Royal Norwegian Embassy, Hivos, Goethe Institut, the Embassy of the United States of America, Swiss Agency for Development and Cooperation, African Music Festivals Network, Zanzibar Unique, Memories of Zanzibar, Ultimate Security, the Embassy of France, Southern Sun Hotel, Azam Marine, the Embassy of Germany, SMOLE II, and more…

We also thank our 2014 Media Partners: Times Radio FM, RFI-Kiswahili, and Hits FM Radio & Zanzibar Cable Television

Tanzania: World Bank Supports Land Ownership Reform and Better Access to Financial Services

$
0
0
Today the Government of United Republic of Tanzania and the World Bank signed the Financial Agreement for additional financing to the Private Sector Competitiveness Project (PSCP) for a total amount of US$60.2 million.

The Private Sector Competitiveness Project (PSCP) supports the implementation of Tanzania’s program to develop the private sector by lowering the cost of doing business. Today’s funds support the scaling up of two components: strengthening the country’s business environment and improving access to financial services.

The US$60.2 million PSCP is financed by a credit from the World Bank’s International Development Association (IDA)*.

“During the past decade, Tanzania has experienced high rates of economic growth, due to economic reforms, sound macroeconomic policies, and an expanding public sector,” said Philippe Dongier, World Bank Country Director for Tanzania. “The PSCP’s focus on securing land ownership and improving access to finance will facilitate increased flows of private investment into the country’s industries, light manufacturing firms and farms, while boosting shared growth and jobs and improving the quality of life for Tanzanians.”

The PSCP supports activities designed to improve land registration, land use planning and regularization of tenure rights. The project has already piloted a faster land demarcation and registration approach to replace the traditional high cost registration, (which is about 10 times more expensive.) Today’s project will help to further advance land administration reform, complete business registration reform, and help implement the Government’s Big Results Now initiative to speed up delivery of priority programs such as agriculture, education, energy, transport and water.

Already PSCP activities have helped 166,000 households participate in microfinance, benefiting more than one million people. Another 35,000 people have benefitted by participating in Village Savings and Loan Associations and Village Community Banks. The additional financing aims to build on this success by strengthening the legal and regulatory framework for the financial sector, improving the capacity of financial regulators, and supporting the development of products such as finance leasing and savings bonds.

Twice as fast as Concorde: The supersonic jet that will fly from London to New York in TWO HOURS

WAZIRI MUHONGO KATIKA WARSHA YA UZINDUZI WA HIGH RESOLUTION AIRBONE GEOPHYSICAL DATA

$
0
0
Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo akizungumza na wadau wa sekta ya madini (hawapo pichani) wakati wa ufunguzi wa warsha ya uzinduzi wa Mfumo wa Utafiti wa Geofizikia data leo jijini Dar es salaam.
Mwakilishi wa Kampuni ya Geotech Airborne Limited Malcolm Moreton akielezea namna kampuni yake ilivyoshirikiana na Serikali ya Tanzania kuhakikisha mfumo wa Utafiti wa Geofizikia unafanikiwa.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Geological Survey Tanzania(GST) Abdulkarim H. Mruma akifafanua jambo wakati wa warsha ya uzinduzi Mfumo wa Utafiti wa Geofizikia data leo jijini Dar es salaam.
Baadhi ya wadau wa sekta ya Jeolojia wakifuatilia mada kutoka kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Geological Survey Tanzania(GST) Abdulkarim Mruma (hayupo pichani) leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo (waliokaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa Warsha ya uzinduzi wa mfumo wa Utafiti wa Geofizikia Data iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam. Picha zote na Benjamin Sawe - MAELEZO.

NEW YORK YAJADILI UFANISI WA SHERIA ZINAZODHIBITI BIASHARA YA PEMBE ZA TEMBO

$
0
0
Mwenyekiti wa Kamati ya Hifadhi ya Mazingira ya Bunge la New York, Bw. Robert K. Sweeney akiongoza mkutano ( public hearing) aliouandaa kujadili na kubadilishana mawazo kuhusu ufanisi wa sheria na kanuni zinazodhiti biashara ya pembe za tembo katika New York, mkutano huo ulifanyika siku ya Alhamis. New York ndiyo inayoongoza katika Marekani kwa kuwa kituo cha Biashara ya pembe za tembo na biadhaa zake katika mwaka 2012 pembe za tembo zenye thamani ya dola milioni mbili zilikamatwa.
Muwakilishi wa kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi akizungumza katika mkutano huo ambapo pamoja na mambo mengine alielezea jitihada zinazofanywa na serikali katika kudhibiti ujangili na biashara haramu ya pembe za tembo.
Bw. William C. Woody ( mwenye tai ya njano) Naibu Mkurugenzi kutoka Ofisi inayosimamia sheria akiwa na Bw. Richard G. Ruggiero Mkuu wa Kitengo cha Afrika, Uhusiano wa Kimataifa , huduma za Samaki na Wanyamapori nchini Marekani. Wakitoa ushuhuda wao kuhusu changamoto wanazokabiliana nazo katika udhibiti na usimamizi wa sheria zinahusu biashara ya pembe za tembo na wanyama wengine walio katika hatari ya kutoweka.


MKUU WA MKOA WA RUKWA AKUTANA NA TIMU MAALUUM YA KUHAKIKI MAENEO MAPYA YA UTAWALA KUTOKA TAMISEMI

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akizungumza na timu maalum inayohakiki maeneo mapya ya utawala kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Pichani kulia na timu yake ya Mkoa iliyokuwa ikiratibu maeneo hayo ofisini kwake leo tarehe 17 Januari 2014. Timu hiyo kutoka TAMISEMI inaongozwa na Mwanasheria wa TAMISEMI Ndugu Eustard Ngatale (watatu kulia).

 Katika kikao hicho kifupi Mkuu huyo wa Mkoa ameiomba mamlaka husika kupitia timu hiyo kuangalia upya vigezo vinavyotumika katika kugawa maeneo mapya ya utawala na upandishaji wa madaraja kutoka kijiji, kata, Tarafa, Halmashauri, Miji na Manispaa. 

Alisema kuwa kuna maeneo mengine ambayo yakiangaliwa kwa kigezo kimoja cha wingi wa watu bila kuangalia umbali wa huduma na giografia ya eneo husika unakuta wananchi wanakosa huduma zao za msingi na kupata tabu kubwa katika kuzipata.

 Alitolea mfano vijiji vikubwa vya mwambao ambavyo kupata huduma katika kata zao ni lazma wavuke upande mmoja wa Ziwa kwenda upande mwingine jambo ambalo ni hatarishi kama ilivyotokea kwa wananchi wa Kijiji cha Kipwa Mwambao mwa Ziwa Tanganyika ambao hivi karibuni walipoteza watu 15 katika ajali ya boti walipokwenda kupata huduma ya afya. Wengi ya waliofariki katika ajali hiyo mbaya walikuwa ni watoto chini ya umri wa miaka 5.  
Kikao kikiwa kinaendelea ambapo kwa upande wake Mwanasheria wa TAMISEMI Ndugu Eustard Ngatale alisema kuwa kubariki na kuhalalisha uanzishwaji wa maeneo mapya ya Utawala vipo vitu mbalimbali vya kuzingatia ambavyo ni pamoja na kuwepo kwa makubaliano ya wananchi na viongozi wa maeneo husika kupitia mihutasari ya vikao maalumu vya kisheria vya WDC, Halmashauri, DCC na RCC katika ngazi ya Mkoa.(Na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa @Rukwareview.blogspot.com)

RAIS KIKWETE AFANYA UTEUZI WA KAMISHNA WA MADINI NCHINI

SHIRIKA LA NYUMBA LATOA MAFUNZO KWA VIKUNDI VYA VIJANA,LENGO NI KUBADILI MAISHA YAO

$
0
0
1Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Nyumba nchini (NHC), Bw. Nehemia Kyando Mchechu akizungumza wakati wa maadalizi ya ufungaji wa mafunzo ya vijana wawakilishi wa vikundi kutoka mikoa mbalimbali kuhusu utengenezaji wa matofali ya udongo yenye teknolojia ya Interlocking Blocks yaliyoanza Januari 6 mpaka 17 mwaka huu ambayo yanatarajiwa kufungwa wiki ijayo na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Mizengo Pinda, Mkurugenzi huyo amesema Shirika la nyumba badala ya kwenda kutoa msaada wa sabuni na vyakula katika vituo vya watoto yatima au kusaidia biskuti limeamua kubadilisha maisha ya vijana wa Tanzania kwa kuwapa mafunzo na kuwapatia mashine za kutengeneza matofali ya udongo ambayo wao NHC watakuwa ndiyo wateja wakuu wa kununa matofali hayo, lakini pia shirika hilo linatoa mashine za kufyatulia matofali zipatazo 640 katika wilaya 160 mikoa yote ya Tanzania bara na kiasi cha shilingi 500,000 kila mkoa kama mtaji wa kununulia saruji kwa vikundi hivyo, Katikati ni Injinia Kwanama Elias Mkurugenzi wa Utafiti na Maendeleo kutoka Nation Housing&Building Research Agency (NHBRA) na kushoto ni Bw.Julius Njelwa kutoka VETA, mafunzo hayo yameratibiwa kwa pamoja na (NHC), (VETA) na (NHBRA) kwa pamoja.3Injinia Kwanama Elias Mkurugenzi wa Utafiti na Maendeleo kutoka Nation Housing&Building Research Agency (NHBRA) akifafanua masuala ya kitaalamu kuhusu teknolojia hiyo ya matofali kwa waandishi wa habari.4Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo.7Baadhi ya maofisa wa Shirika la Nyumba NHC wakiwa katika maadalizi hayo kushoto ni Suzan Omary Meneja Mawasiliano NHC, Muungano Saguya Meneja huduma kwa jamii NHC na Ephraim Kibonde mtangazaji wa Clouds Radio.

wito kwa waheshimiwa wabunge wote

NEWS ALERT: KIKAO CHA KUKAMILISHA "UKAGUZI MAALUM "EXIT MEETING" CHA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI,CHAMFUTA KAZI MEYA WA BUKOBA LEO

$
0
0
Katibu tawala Mkoa, Mkuu wa mkoa Kagera Mh. Fabian Massawe, Naibu Waziri wa TAMISEMI Mhe. Agrey Mwanri na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kutoka Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bw. Ludovick Utouh wakiingia ukumbini leo Bukoba.Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kutoka Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bw. Ludovick Utouh akitoa taarifa ya ukaguzi maalum alioufakatika katika  mkoa huo leo mjini Bukoba.Naibu Waziri wa TAMISEMI Mhe. Agrey Mwanri akitoa Maelezo ya Serikali. Kuhusu Suruhisho hilo ambapo yamebainika Makosa ya Meya Anatory kufanya makubaliano bila idhini ya Madiwani na Taratibu za serikali, Basi ajipime Mwenyewe na Kujiudhuru mara moja kwa Maslahi ya Manispaa ya Bukoba.Mstahiki Meya wa Manispaa ya Bukoba Anatory Amani (kulia) kushoto ni Mzee Rwangisa, Ukumbuke pia Mzee huyo Rwangisa ndiye aliyemwachia nafasi Meya Anatory Amani.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI ZA KIKAO HICHO LEO

WAZIRI MKUU AKAGUA ATHARI ZA MAFURIKO MPWAPWA

$
0
0
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akitazama sehemu ya jengo la Kituo cha Polisi cha kijiji cha Chipogoro wilayani Mpwapwa ambayo imeporomoka kufuatia mafuriko yaliyokikumba kijiji hicho kufuatia mvua kubwa zianazoendelea kunyesha mkoani Dodoma januari 17, 2014. Kulia kwake ni Mkuu wa mkoa wa Dodoma, Dr. Rehema Nchimbi.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akikagua athari za mafuriko yaliyokikumba kijiji cha Chipogoro wilayani Mpwapwa Januari 17, 2014. Kulia kwake ni Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara na Mbunge wa Mpwapwa, Gregory Tewu na kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Dodoma, Dr. Rehema Nchimbi.
Waziri Mkuu,Mizengo Pinda akikagua daraja ambalo lilizibwa na maporomoko ya maji yaliyoambatana na magogo , mawe na udongo na kusababisha mafuriko katika kijiji cha Chipogoro wilayani Mpwapwa januari 17,20134.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akikagua athari za mafuriko katika kijiji cha Fufu wilayani Chamwino, Dodoma, Januari 17, 2014.Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rehema nchimbi na kulia kwake ni Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

EAC COMMITTEE ON CUSTOMS MEETS IN ARUSHA TO STRATEGIZE ON THE IMPLEMENTATION OF THE SINGLE CUSTOMS TERRITORY

$
0
0
Pursuant to the Summit directive to commence the implementation of a Single Customs Territory, the Committee of Customs comprising of Commissioners General and Commissioners of Customs held a one-day meeting at the EAC Secretariat, Headquarters in Arusha today  17th January 2014 to strategize on  the implementation of the Single Customs Territory.

The Commissioner General of Kenya Revenue Authority, Mr John Njiraini, who chaired the meeting, reiterated the commitment of the Revenue Authorities to the integration process and particularly the implementation of the Single Customs Territory. He noted the initiatives under the Trilateral arrangement by Kenya, Uganda and Rwanda will be harmonized within the wider EAC Single Customs Territory.

On behalf of the Secretary General of the EAC, the Director Customs Mr. Kenneth Bagamuhunda   noted that the Single Customs Territory (SCT) is one of the key regional integration priority policy interventions adopted by both the Council and the Summit to consolidate the EAC Customs Union. He said that ‘It is imperative that the Revenue Authorities take full responsibility to ensure the SCT is fully implemented as per the approved roadmap by the Council’.

The Committee established five technical working teams that will put in place operational requirements and procedures for the SCT. The meeting also agreed on the schedule of activities for the implementation of the SCT.

A pilot based approach segmented on the central and northern corridors was adopted which will progressively cover all goods cleared at the first ports of entry. The meeting agreed to integrate the ongoing activities on SCT on the Northern Corridor into the EAC wide SCT framework. A proactive, practical and result based method of work was agreed on as a way of work on the SCT.

The meeting was attended by the Commissioner General Kenya Revenue Authority, Mr John Njiraini; The Commissioner General Rwanda Revenue Authority, Mr Ben Karugarama; The Commissioner General Burundi, Mr Kieran Holmes; The Director of Customs Mr Kenneth Bagamuhunda, the Commissioners of Customs and experts from the EAC Partner States.

TAARIFA TOKA SHIRIKISHO LA SOKA NCHINI (TFF) LEO

MTEMVU ATOA MADAWATI 500 YATAKAYOGAWIWA SHULE ZA MSINGI JIMBONI TEMEKE

$
0
0
 Madiwani wakipiga makofi ikiwa ni ishara ya kumpongeza Mbunge wa Jimbo la Temeke, Abbas Mtemvu (wa pili kushoto)  kukata utepe  wakati wa hafla ya kukabidhi madawati 500 yenye thamani ya sh. mil. 67.5 yatakayogawiwa katika Shule za msingi katika Kata 13 za jimbo hilo. Hafla hiyo imefanyika leo Chuo cha Ufundi Chang'ombe, Dar es Salaam. 
 Mbunge wa Jimbo la Temeke, Abbas Mtemvu akizungumza baada ya kukabidhi madawati 500 yenye thamani ya sh. mil. 67.5 yatakayogawiwa katika shule zilizopo katika Kata 13 za Jimbo hilo. Madawati hayo yaliyonunuliwa kwa fedha za Mfuko wa Jimbo yalikabidhiwa kwa madiwani wa Kata hizo katika hafla iliyofanyika Chuo cha Ufundi Chang'ombe, Dar es Salaam
 Naibu Meya wa wa Manispaa ya Temeke, Juma Mkenga akitoa shukurani kwa Mbunge Mtemvu kutoa madawati hayo.
 Naibu Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Zena Mgaya akimpongeza Mtemvu kwa juhudi za kuinua kiwango cha elimu wilayani Temeke.
 Ofisa Elimu wa  Shule za Msingi Manispaa ya Temeke, Honorina Mumba akieleze furaha ya kupata madawati hao 500 yatakayopunguza tatizo la madawati wilayani Temeke.
Fundi akiendelea kupiga msasa baadhi ya madawati hayo yalitotengenezwa VETA Chang'ombe.(PICHA ZOTE NA KAMANDA WA MATUKIO BLOG)

Balozi Seif Ali Idd amjulia hali Mh. Haroun Ali Suleiman aliyelazwa Muhimbili

$
0
0
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akimkagua na kumpa pole Waziri wa Kazi na Utumishi wa Umma Zanzibar Mh. Haoun Ali Suleiman aliyelazwa katika Hospitali ya Rufaa kitengo ya MOI Muhimbili Jijini Dar es salaam. Waziri Haroun amelazwa Hospitalini hapo karibu wiki moja sasa akikabiliwa na tatizo la ugonjwa wa Moyo.
 Picha na Hassan Issa wa – OMPR – ZNZ

MAPENDEKEZO 9 YA JINSI YA KUCHAGUA JINA LA KUTUMIA KAMA MSANII

$
0
0
stage_name_hd
Kama mwandishi na mmiliki wa blog kama hii ya BC [mahali ambapo vipaji huibuliwa na majina kutambulishwa] mojawapo ya majukumu yangu ya kawaida kila siku au kila wiki ni pamoja na kupokea kazi mbalimbali za wasanii. Mara nyingi,kazi hizo zinakuwa bado hazijasikika katika masikio ya wapenzi na mashabiki wa muziki. Hivyo basi,ni jukumu langu pia kuzisikiliza nyimbo hizo, kuzifafanua na kuzielewa ili kupata maudhui yanayofaa katika kuitambulisha nyimbo na msanii mwenyewe.

Kuna wanaochipukia na kuna wanaoanza safari ndefu ya kuelekea kwenye umaarufu au kujikimu na maisha. Kuna wanaokuwa wanarejea baada ya mapumziko na tafakuri na kuna ambao wanakuwa wameogopa kwamba wanaanza kusahauliwa na hivyo wanajifaragua kurejea kilingeni.

Hivi sasa, kila jua linapozama,maelfu ya vijana wanajisogeza vitandani mwao kupumzisha mwili na akili huku ndoto zao zikilenga kwenye “kutoka” kwa maana ya kuwa msanii superstar ajaye. Kazi ya kuwaza ni kazi.Kazi ya kufanya kinachotakiwa kufanyika ili kutimiza lengo au malengo ni kazi zaidi.

Sanaa inalipa. Sanaa ni kazi. Sina takwimu halisi lakini bila shaka tunakubaliana kwamba sanaa inatoa ajira kwa maelfu [kama sio mamilioni] ya vijana nchini mwetu.Na ni kweli kwamba ingelipa zaidi endapo taratibu na sheria mbalimbali [ambazo zipo] zingetumika vyema. Kuna wanaofaidi Jasho la hawa vijana na ndio maana kuna “mgando” katika utekelezaji wa sheria hizo. Hii ni mada ambayo natumaini kuifanyia kazi zaidi katika siku za usoni. 

Flora Mbasha jukwaani

$
0
0
Mwimbaji gwiji wa nyimbo za Injili Flora Mbasha na kundi lake katika onesho lililofanyika PTA Hall Dar es salaam.
Viewing all 110091 articles
Browse latest View live




Latest Images