Mbunge wa Viti maalum Jimbo la Iringa akizungumza na wananchi hawapo pichani kuelezea kazi alizofanya katika jimbo la Iringa katika mkutano uliofanyika katika kiwanja cha Mwembetogwa.
Baadhi ya wananchi waliohudhuria mkutano wa ccm katika kiwanja cha mwembetogwa
Baadhi ya wanachama vijana wa chadema waliorudisha kadi wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa ccm wilaya katika mkutano uliofanyika katika viwanja vya mwembetogwa. (picha zote na Denis Mlowe)
========= ======== ===========
MBUNGE LITA KABATI AELEZA ALIYOYAFANYA HADI SASA KATIKA UBUNGE
Na Denis Mlowe,Iringa
Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa Rita Kabati ameeleza kazi mbali mbali alizozifanya katika jimbo la Iringa mjini ikiwa ni pamoja na kujenga kituo cha polisi kilichoko jirani na chuo Kikuu cha Iringa(Tumaini).
Kabati alisema hayo wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Mwembetogwa kuwa ataendelea kutatua kero za wananchi wa Iringa mjini kila anapopata nafasi za kuwahudumia wananchi hao.
Alisema kuwa kamwe hatarudi nyuma katika utendaji na kuwa siku zote atawapigania wananchi wa jimbo la Iringa mjini na kuwa kuwa siku zote kwake atahakikisha anatenda zaidi na amekuwa akijenga hoja za kusaidia Jimbo la Iringa mjini na sio kutoa kejeli kwa serikali akiwa mbungeni .
Akielezea mambo ambayo amepata kutekeleza alisema ni pamoja na kusaidia sekta ya elimu vitabu na kompyuta pamoja na kusaidia vikundi vya vikoba katika jimbo hilo la Iringa mjini kusaidia vijana katika harakati za kujikwamua kiuchumi kwa kuanzisha mashindano ya Kabati Star Search.
Kwa upande wake katibu wa CCM Iringa mjini Hassan Mtenga alisema yeye alikuwa jimbo la Freeman Mbowe ambae sasa anatangaza kutogombea jimbo la Hai.
Alisema zama za ubunge wa Mchungaji Peter Msigwa katika jimbo la Iringa mjini umekwisha na sasa atake ataondoka na asipotaka ataondoka.
"Mwambieni mbunge Msigwa wakati wa kuwadanganya wananchi umekwisha na lazima sasa awaeleze wananchi wa jimbo la Iringa mjini wapi anapelekea fedha za mfuko wa jimbo ambazo zinatolewa kila mwezi na Rais Jakaya Kikwete"
Hata hivyo alimuagiza meya kupambana ili fedha kiasi cha Tsh milioni 15 zinazotolewa na rais Kikwete kuona zinafanya kazi gani katika ofisi ya mbunge pia kutembelea Hospital na vituo vya afya ili kuona changamoto mbali mbali ndani ya wiki tatu kupeleka majibu katika ofisi yake.
Aidha aliwataja vijana kuleta maendeleo ya mji wa Iringa na sio vijana wa kutumiwa kuvuruga maendeleo ya mji wa Iringa.
" Nawaombeni wananchi kuwa tayari tumemshika pua mbunge Msigwa na naomba wananchi tusaidiane kumnywesha panado na ninamuomba Msigwa fedha za kiinua mgogo zake asije tena katika jimbo la Iringa mjini atumie kwa kazi nyingine ....tumeanza mkakati huu kwa ajili ya kumng’oa Msigwa