Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110028 articles
Browse latest View live

RAIS KIKWETE AMTEMBELEA RAIS MSTAAFU WA ZANZIBAR DKT SALMIN AMOUR

$
0
0
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Rais Mstaafu wa Zanzibar Dkt Salmin Amouralipomtembelea kumjulia hali nyumbani kwake Zanzibar Jumatatu Januari 13, 2014 baada ya kuhudhuria sherehe za miaka 50 ya Mapinduzi.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiagana  na Rais Mstaafu wa Zanzibar Dkt Salmin Amouralipomtembelea kumjulia hali nyumbani kwake Zanzibar Jumatatu Januari 13, 2014 baada ya kuhudhuria sherehe za miaka 50 ya Mapinduzi. PICHA NA IKULU

cristian Ronaldo amwaga chozi jukwaani baada ya kutangazwa manasoka bora wa FIFA 2013

$
0
0
 Cristiano Ronaldo  akimwaga chozi baada ya kutangazwa mwanasoka bora wa FIFA  kwa mwaka 2013 usiku wa kuamkia leo jijini Zurich, Uswisi huku mwanae Cristiano Junior  na Pele pamoja na Rais wa Chama cha Soka cha Ufaranza Francois Moriniere wakishuhudia.
Cristiano Ronaldo na mwandani wake, Lionel Messi na Mwandani wake wakati wa sherehe hizo. 
CHEKI VITUZZZZ VYA RONALDO HAPO CHINI
...JAMAAA NI NOMA!

Burudani ya taarab halisi katika sherehe za miaka 50 ya mapinduzi zanzibar

$
0
0
Kundi la Taarab la Taifa la Zanzibar likitumbuiza wakati wa kilele cha sherehe za miaka 50 ya Mapinduzi uwanja wa Polisi wa Ziwani mjini Zanzibar Januari 12, 2013

Cheki makomandoo wetu walivyo fiti

$
0
0
Kikosi cha Makomandoo kikionesha nidhamu na ukakamavu wa hali ya juu wakati wa kilele cha sherehe za miaka 50 ya Mapinduzi Zanzibar katika Uwanja wa Amani

Wanafunzi na walimu wa International School of Tanganyika watembelea watoto yatima wa kituo cha Guardian Angels

$
0
0
Wanafunzi na walimu wao kutoka shule ya kimataifa ya International School of Tanganyika leo wametembelea watoto wa kituo cha Guardian Angels katika kuwatakia heri ya mwaka mpya. Wanafunzi hawa wamekuwa marafiki wa watoto wa Guardian Angels kwa muda sasa na wamekuwa wakiwasaidia vifaa vya michezo,chakula na mahitaji mengine. 
Picha hizi mbalimbali ni wakati wakicheza katika viwanja vya kituo hicho. Tunawashukuru sana kwa upendo. Tunawakaribisha wadau wengine wenye mapenzi na watoto kuja kutembelea kituoni kwetu Mbezi-Temboni karibu na Sinon Collage. Tembelea www.angelstz.org
Wanafunzi na walimu wao kutoka shule ya kimataifa ya International School of Tanganyika wakicheza na watoto yatima wa kituo cha Guardian Angels
Wanafunzi na walimu wao kutoka shule ya kimataifa ya International School of Tanganyika na watoto wa Guardian Angels
Haya tucheze kidali pooo..
Nani aanze...
Wanafunzi na walimu wao kutoka shule ya kimataifa ya International School of Tanganyika katika picha za pamoja na watoto wa Guardian Angels

Kali TV: This week's Around Town

Rais Kikwete aagana na Mwakilishi mkazi wa Umoja wa Mataifa ikulu jijini Dar

$
0
0
Mwakilishi mkazi na Mratibu wa Shughuli za Umoja wa Mataifa nchini(Resident Coordinator of the UN System) Bwana Alberic Kacou akimkabidhi Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete nakala ya Ripoti ya mwaka Utendaji ya (UNDP) 2012-2013 wakati mwakilishi huyo alipokwenda kumuaga Rais Kikwete ikulu jijini Dar es Salaam leo. Bwana Kacou anaondoka baada ya muda wake wa utumishi kumalizika hapa nchini(picha na Freddy Maro)

MKUSANYIKO WA MABINGWA WA KUCHOMA NA KUTAFUNA NYAMA KUFANYIKA JIJINI DAR

$
0
0
Kwa mara ya kwanza kabisa mwaka huu 2014, lile tamasha kubwa la Nyama choma linalofahamika kama The Nyama Choma Festival (TNCF) limepangwa kufanyika siku ya Jumamosi ya tarehe 8 mwezi Machi mwaka 2014. 

Nani alifikiria kuwa Nyamachoma ingeweza kuwaleta maelfu ya watu pamoja? Toka lilipoanzishwa,  tamasha la nyama choma ambalo limesajiriwa kisheria limekuwa ni sehemu ya kipekee ya kuweza kufurahia aina mbalimbali za nyama choma na pia ni eneo linalowakuwakutanisha watu kutoka sehemu mbalimbali wanaofika kufaidi nyama zinazochomwa na wataalamu wa kuchoma nyama kutoka katika kona mbalimbali za jiji la Dar salaam kwa kiingilio cha shilingi 10,000 tu.

Ukiachana na aina mbalimbali ya nyama zinazokuwepo katika tamasha hili, hii pia ni sehemu mojawapo ya kufurahi na marafiki ikiwa ni pamoja na “mtoko” kwa familia kwani huduma zinazotolewa zimezingatia umri wa watu wote yaani kuanzia watoto hadi watu wazima. Kuna eneo maalumu limetengwa kwa ajili ya michezo ya watoto, vinywaji vya ain azote na burudani nzuri ya muziki. Si hivyo tu wapo watu wengine wanaotoa huduma za kahawa, ice cream, michoro ya usoni, vyakula vya kawaida na michezo ya nje ya watuwazima kama pool n.k

Tupo katika dunia ambayo inatulazimu kuwa katika mtandao mkubwa na watu wenye weledi tofauti, The Nyama Choma Festival inakuwezesha kuingia katika mtandao huu kwa urahisi zaidi. Kwani kwa siku hii moja tu watu wote wanaweka vyeo na nafasi zao kitaaluma pembeni na kuchanganyika na watu wote huku wakifurahi kwa pamoja. Katika hali hii watu wanabadilishana uzoefu na kupeana mawasiliano kwa ajili ya siku za usoni.


MPIGIE KURA MUIGIZAJI JUMA RAJAB AWEZE SHINDA TUZO YA AFRIKA MAGIC

$
0
0
Kumbuka kumpigia kura Muigizaji Juma Rajab Rashid a.k.a Cheche ili aweze kushinda tuzo ya Muigizaji Bora wa Kiume kwenye Tamthilia kwa kutuma ujumbe mfupi kwenda namba +2783142100415 au kwenye mtandao- huu  http://goo.gl/o72lu5 !  Kumbuka kuwa unaweza kupiga kura mara nyingi zaidi kila baada ya saa moja. Umoja wetu ni Ushindi kwa Mtanzania mwenzetu

SCHOLARSHIP FOR STUDYING AT THE PRESBYTERIAN UNIVERSITY OF EAST AFRICA

$
0
0

Umoja wa Wanawake Makanisa ya Dar es Salaam (UWAMAKDA), an interdenominational committee of the Umoja wa Makanisa ya Dar es Salaam, is announcing to Tanzania women, a full scholarship for studying Bachelor of Business Administration at the Presbyterian University of East Africa, Kenya.

The scholarship has been offered by the Moderator of the 20th General Assembly of the Presbyterian Church of East Africa whose Headquarters are in Nairobi.

UWAMAKDA members are all women of the churches and institutions which are members or are affiliated with the Tanzania Episcopal Council/Roman Catholic, Christian Council of Tanzania (CCT) and the Pentecostal Churches in Tanzania/PCT.

ELIGIBILITY CRITERIA FOR THE SCHOLARSHIP AND STUDIES

·         Age: less than 40 yrs

·         GenderFemale

·         Nationality: Tanzanian

Education:

·         Division II …..Form VI with a science  or commercial orientation

·         Division I…..Form IV with a science or commercial orientation or C+ in Maths and C+ in English

·         Must be fluent in writing and speaking English.

DEADLINE

·         February 28, 2014

PLEASE FORWARD YOUR APPLICATIONS, WRITTEN IN ENGLISH TO:


The Chairlady, 
UWAMAKDA, 
P.O Box 6783, 
Dar es Salaam 
OR Deliver to the Matron, YWCA Headquarters, 
Ghana Avenue opposite St Alban’s Anglican Church on same street, Dar es Salaam.

Article 23

EAC ISSUES SQMT REGULATIONS TO FACILITATE REGIONAL TRADE

$
0
0
The East African Community has issued regulations to enhance the operationalization of the EAC Standardization, Quality Assurance, Metrology and Testing Act (SQMT) of 2006. The SQMT regulations are geared towards facilitating regional trade.

The Regulations were approved by the Council of Ministers in November 2013 and are issued in line with Article 6 of the Protocol on Establishment of the EAC Common Market, with reference to Free Movement of Goods. 

Article 6 of the Protocol stipulates among others laws that the free movement of goods shall be governed by EAC SQMT Act, 2006 and regulations made there under. The regulations include: The EAC SQMT (Product Certification in Partner States) Regulations, 2013; The EAC SQMT (Designation of Testing Laboratories) Regulations, 2013; and The EAC SQMT (Enforcement of Technical Regulations in Partner States) Regulations, 2013. 

The EAC SQMT (Product Certification in Partner States) Regulations, 2013; provides for certification bodies in the Partner States on the basis of Product Standards. The regulations will facilitate the issuance of quality marks on products conforming to regional and international standards and provide consumer confidence of the products traded in the region. The regulations also provide for emphasis on recognition of each Quality Marks issued by other Partner States Quality Marks in conformity assessment of goods moving across borders. 

The EAC SQMT (Designation of Testing Laboratories) Regulations, 2013; provides for the Ministers responsible for Trade in the Partner States to designate Testing Laboratories to be recognized in the region. The regulation will facilitate an organized recognition of testing laboratories to test goods for conformity assessment of goods in the region.

The EAC SQMT (Enforcement of Technical Regulations in Partner States) Regulations, 2013; provides for Partner States to declare or notify  a technical regulation which may create barriers to trade and obliges Partner States upon request to explain the justification for that technical regulation.
The above mentioned regulations are expected to be approximated and/or aligned to the existing National Laws as required by the Treaty establishing the East African Community.

Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana inavyompa Kijana Fursa ya Kujitambua na kujiamini

$
0
0
Na Benjamin Sawe,WHVUM

“Vijana ni nguvu kazi ya Taifa”. Hii ni kweli na kwa mujibu wa utafiti wa Nguvu Kazi Nchini ya mwaka 2006 asilimia 68% ya nguvu kazi nchini ni Vijana ambao idadi yao kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 ni 15,587,621 sawa na asilimia 34.7% ya idadi ya watu wote nchini. Kati yao Vijana wa kike ni 8,273,505 sawa na asilimia 35.9% na Vijana wa kiume ni 7,314,116 sawa na asilimia 33.4%.

Kutokana na umuhimu huu, kumekuwa na jitihada mbalimbali za Serikali zinazolenga katika masuala ya maendeleo ya Vijana nchini hii ikiwa ni pamoja na kuwa na Sera, Mipango na Mikakati inayokidhi mahitaji mbalimbali ya vijana kama vile, Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana 2007,Sera ya Taifa ya Ajira 2008 (Iliyo chini ya Wizara ya Kazi na Ajira), Mpango Kazi wa Taifa wa Ajira kwa Vijana 2007 na Programu ya Kukuza Ajira zenye Staha kwa Vijana nchini inayoratibiwa kati ya Wizara Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo na Shirika la Kazi Duniani (ILO).

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Vijana Bw. James Kajugusi anasema Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana 2007 ni matokeo ya maboresho ya Sera ya Vijana ya mwaka 1996 ambapo, maboresho ya Sera hiyo yanatokana na mabadiliko, mahitaji au changamoto mbalimbali zinazojitokeza za kijamii, kiuchumi na kisiasa.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

ETON STUDENTS TO PROMOTE SPORTS IN TANZANIA

$
0
0
Tanzania has taken the first step towards producing their first Premier League player -- thanks to Eton College, England's premier public school. Together with Safarihub and charity organisation ACE Africa, Eton are sending Glen Pierce, head of sports, plus Ali Lyon, 19, Nicholas Zafirios, 18, and Tom Pearson,18, who are on a gap year before starting university, to Tanzania to teach local children the finer arts of football.

Maisha Plus / Mama Shujaa wa Chakula imerudi tena.

$
0
0
Zimebaki siku 9 tu za kujaza fomu ya ushiriki.

1. Kijana wa Tanzania, Burundi, Rwanda, Kenya, Uganda mwenye umri wa kati ya miaka 21 - 26, jaza fomu ya kushiriki shindano la Maisha Plus moja kwa moja mtandaoni kwa kubofya hapa
--> http://maishaplus.tv/MaishaPlusFomu2014.html

2. Kama wewe ni mkulima mwanamke mwenye umri wa miaka 18 mkazi wa Tanzania ama unamfahamu yeyote, jaza fomu moja kwa moja kwa kubofya hapa --> http://maishaplus.tv/MamaShujaaFomu2014.html

Tunawatakia kila la Kheri.

VODACOM ILIVYOZIKUTANISHA TIMU ZA WABUNGE WA ZANZIBAR,MUUNGANO NA UGANDA MIAKA 50 YA MAPINDUZI ZANZIBAR

$
0
0
Ofisa Mkuu wa Mauzo na Usambazaji wa Kampuni ya Vodacom Hassan Saleh akimkabidhi Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Pandu Ameir Kificho kombe lililotolewa na Vodacom kwa ajili ya mshindi wa mechi maalum kati ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na Wabunge wa Bunge la Tanzania kuadhimisha miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Mchezo huo ulichezwa kwenye Uwanja wa Amaan Mjini Zanzibar na kufadhiliwa na Vodacom Tanzania.
Spika wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar Pandu Ameir Kificho akimkabidhi Nahodha wa Timu ya Soka ya Wabunge wa Bunge la Tanzania Amos Makala amabe pia ni Naibu Waziri wa Habari,Vijana Utamduni na Michezo kombe kufuatia kuichapa timu ya Baraza la Wawakilishi kwenye mechi maalum ya kuadhimisha miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Katikati ni Ofisa Mkuu wa Mauzo na Usamabazaji wa Vodacom Hassan Saleh waliodhamini mechi hiyo iliyopigwa kwenye Uwanja wa Amaan Mjini Zanzibar.
Ofisa Mkuu wa Mauzo na Usamabazaji wa Vodacom Hassan Saleh akimpongeza mchezaji wa timu ya Wabunge wa Bunge la Tanzania Adam Malima ambae pia ni Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika mara baada ya kumalizka kwa mechi yao dhidi ya Wajumbe wa Baraza La Wawakilishi kuadhimisha miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar kwenye uwanja wa Amaan Mjini Zanzibar. Mechi hiyo ilidhaminiwa na Kampuni ya Vodacom.
Kikosi cha Timu ya soka ya Wabunge wa Bunge la Tanzania kikiwa na kombe muda mfupi mara baada ya kukabidhiwa baada ya kuifunga timu ya Baraza la Wawakilishi bao moja kwa bila kwenye mechi maalum ya kusherehekea mika 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Mchezo huo ulidhaminiwa na kampuni ya Vodacom.
Kikosi cha Timu ya Netiboli kinachoundwa na Wabunge wa Bunge la Uganda kikiwa katika picha ya pamoja muda mfupi kabla ya kushuka uwanjani kuvaana na kombaini ya Zanzibar ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Katikati ni Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AWAJULIA HALI MAWAZIRI WALIOLAZWA MUHIMBILI, CLEOPA MSUYA NA HARUNA ALI SULEIMAN

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Waziri Mkuu Mstaafu, Cleopa Msuya, aliyelazwa katika jengo la Moyo Hospitali ya Taifa Muhimbili, wakati alipofika kumjulia hali leo, Jan 15, 2014. Kulia ni mke wa Makamu, Mama Zakia Bilal (kushoto) ni Meneja wa Jengo hilo la Moyo, Sr. Salome Kassanga.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Waziri Mkuu Mstaafu, Cleopa Msuya, aliyelazwa katika jengo la Moyo Hospitali ya Taifa Muhimbili, wakati alipofika kumjulia hali leo, Jan 15, 2014. Kushoto ni mke wa Makamu, Mama Zakia Bilal.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimjulia hali Waziri wa Kazi na Utumishi wa Umma wa Zanzibar, Haruna Ali Suleiman, aliyelazwa katika jengo la Moyo Hospitali ya Taifa Muhimbili, wakati alipofika kumjulia hali leo, Jan 15, 2014. Katikati ni mke wa Makamu, Mama Zakia Bilal (kushoto) ni Meneja wa Jengo hilo la Moyo, Sr. Salome Kassanga. Picha na OMR Meneja wa Jengo hilo la Moyo, Sr. Salome Kassanga. Picha na OMR

Rais Kikwete awajulia hali Waziri Mkuu Mstaafu Cleopa David Msuya na Waziri Haroun Ali Suleiman wa Zanzibar

$
0
0
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimjulia hali Waziri Mkuu Msaafu Mzee Cleopa David Msuya aliyelazwa katika hospitali ya Taifa Muhimbili jana jijini Dar es Salaam.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete wakimjulia hali Waziri wa nchi Afisi ya Rais Kazi na Utumishi wa Umma wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar(SMZ) Bwana Haroun Ali Suleiman aliyelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam, Jana (Jumanne)(picha na Freddy Maro).

EPZA yavuka malengo 2013, yaimarisha uwekezaji Tanzania

$
0
0
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Ukanda Maalumu wa Uwekezaji (EPZA),Dkt. Adelhelm Meru, akimkabidhi zawadi maalumu mafanyakazi wa muda mrefu na mwenye umri mkumbwa wa mamlaka hiyo, Bi. Easter Mkumbwa (kulia)kwenye hafla ya kuuaga mwaka 2013 na kuukaribisha mwaka 2014 kwenye Hotel ya Land Mark hivi karibuni jijini Dar es salaam.
Wageni waalikwa wakichukua chakula wakati wa hafla iliyo andaliwa na Mamlaka ya Ukanda Maalumu wa Uwekezaji (EPZA), ya kuuaga mwaka 2013 na kuukaribisha mwaka 2014 kwenye Hotel ya Land Mark hivi karibuni jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Ukanda Maalumu wa Uwekezaji (EPZA),Dkt. Adelhelm Meru, akiwaongoza wafanyakazi na wageni waalikwa kulisakata Rhumba kwenye hafla ya kuuaga mwaka 2013 na kuukaribisha mwaka 2014 kwenye Hotel ya Land Mark hivi karibuni jijini Dar es salaam.

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LEO

Viewing all 110028 articles
Browse latest View live




Latest Images