Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110186 articles
Browse latest View live

WATOTO CHINI YA MIAKA 5 KUPATA CHETI CHA KUZALIWA BURE

$
0
0
Na.Farida Saidy,Morogoro

Wakala Wa Usajili Ufilisi Na Udhamini (RITA) Kupitia Wasajili Wa Huduma Ya Uandikishaji Watoto Chini Ya Umri Wa Miaka Mitano Wametakiwa Kutofanya Urasimu wa kuwatoza Watu Fedha kwa ajiri ya malipo ya ya cheti cha kuzaliwa, Ikiwa Mkakati Uliopo sasa Ni Kusajiliwa Bure, Na Kwa Atakaebainika Kufanya Hivyo Hatua Kali za kisheria Zitachukuliwa Dhidi Yake.

Kauli Hiyo Imetolewa Na Mkuu Wa Mkoa Wa Mororgoro Bw.Loata Ole Sanare Wakati Wa Ufunguzi Wa Semina Ya Wakala Wa Usajili Ufilisi Na Udhamini (RITA) Uliowahusisha Viongozi Mbalimbali Wa Kimkoa Wenye Dira Ya Kufikia Lengo La Kusajili Watoto Zaidi Y Asilimia 90 Ya Watoto Wote Bure , Wenye Umri Chini Ya Miaka Mitano Mkoani Morogoro.

Kwa Upande Wake Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu Kutoka RITA Bi. Emmy Hudson Amesema Ili Kukamilisha Majukumu Kwa Watendaji Kuhusu Mpango Huo,Wameandaa Mafunzo Kwa Wahusika Wote ,Wakiwemo Watumishi Sita Kutoka Kila Halmashauri Mkoani Morogoro ,Pamoja Na Mtumishi Mmoja Mmoja Kutoka Idara Ya Usalama Na Idara Ya Uhamiaji .

Nao Baadhi Ya Washiriki Wa Semina Hiyo Wakiwemo Viongozi Mbalimbali Wa Kiserikali Na Kidini Wameusifu Mpango Huo Wa Usajili Bure Wa Watoto Wenye Umri Chini Ya Miaka Mitano Unaoendelea Kuifikia Mikoa Mbali Mbali Nchini Na Kusema Kuwa Utawasaidia Katika Kuharakisha Upatikanaji Wa Haraka Wa Vyeti Hivyo.

Ikumbukwe Kuwa Kundi La Awali La Watoto Walio Chini Ya Umri Wa Miaka Mitano Limekwishaanza Utekelezaji Wake Ambapo Ni Mikoa Ya Mbeya Songwe Mwanza Njombe Iringa Geita Shinyanga Lindi Mtwara Mara Simiyu Dodoma Na Singida Ambapo Kwa Sasa Ni Zamu Ya Morogoro Pamoja Na Pwani.

MADIWANI HALMASHAURI YA KINONDONI WAMPONGEZA MKURUGENZI ARON KAGURUMJULI UFAULU WA DARASA LA SABA

$
0
0
Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni kwa pamoja limempongeza Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo , Aron Kagurumjuli kwa jitihada zake zakuwezesha kufanya vizuri katika matokeo ya darasa la saba.

Wakizungumza katika kikao cha robo ya mwaka cha baraza la madiwani lililofanyika leo, madiwani hao wameeleza kuwa Mkurugenzi kagurumjuli amekuwa na ushirikiano mzuri na watendaji wake na hivyo kufanikisha kufanya vizuri kwenye matokeo ya darasa la saba.

Naibu Meya wa Halmashauri hiyo, Mhe. George Manyama amesema kuwa kama halmashauri imejipanga kuhakikisha kuwa wanafunzi wote waliomaliza darasa la saba wanapata nafasi ya kusoma na kwamba hakuna atakaye kaa nyumbani.

Amefafanua kuwa ushindi huo uliopatikana ni dira inayoonyesha kuwa hata matokeo ya kidato cha nne yatakuwa mazuri na kwamba Halmashauri ya Kinondoni itaongoza.

“ Niseme tu haya ni matokeo mazuri kwetu, baraza limepitisha maadhimio ya kubadili shule ya msingi Kijitonyama kuwa Sekondari, huu ni mpango uliofanywa na wataalamu wa Halmashauri yetu, lakini pia bado tunaendelea kufanya upembuzi yakinifu kuangalia shule nyingine ambazo tunaweza kuzigeuza kuwa Sekondari.

Diwani wa Kata ya Mwananyamala Mhe.Songoro Mnyonge amesema kuwa Halmashauri ya Kinondoni katika matokeo yake ya darasa la saba mwaka huu imeshika nafasi ya tatu kitaifa huku kimkoa ikishika nafasi ya kwanza.

Mhe. Songoro amefafanua kuwa,matokeo hayo yanatokana na jitihada za Mkurugenzi Kagurumjuli kwani amekuwa akiwasimamia vyema watendaji wake sambamba na kutoa ushirikiano jambo ambalo limewezesha kupata matokeo hayo mazuri.

Amesema kuwa kama madiwani watashirikiana kuhakikisha kuwa wanafunzi wote waliofaulu wanapata nafasi ya kuingia kidato cha kwanza kwakuwa shule zipo na kwamba hakuna mwanafunzi ambaye atakaa nyumbani kwakukosa nafasi.

“ Pamoja na pongezi hizi, ni wakati sasa wakuhakikisha kuwa wote wanakwenda kusoma , kama baraza leo hii tumeadhimia kuwa shule ya msingi Kijitonyama itabadilishwa na kuwa Sekondari, shule hii inavyumba 20 vya madarasa , hivyo wote watapata nafasi ya kusoma” amefafanua Mhe. Chongolo.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Kunduchi Michale Urio , amesema kuwa suala la elimu bure lililotolewa na Mhe. Rais Dk. John Magufuli, limewezesha kuwa na idadi kubwa ya watoto wanaosoma, hivyo Halmashauri itaendelea kuweka jitihada za kuhakikisha kuwa wanapata nafasi za kusoma.

BODI YA URATIBU WA NGOs YATEMBELEA MASHIRIKA KANDA YA ZIWA

$
0
0
Mwenyekiti wa Bodi ya Uratibu wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Dkt. Richard Faustine Sambaiga (wa pili kulia) akizungumza katika kikao kati ya Shirika la Plan International na Bodi hiyo ilipokuwa inatembelea Mashirika yaliyopo Kanda ya Ziwa mkoani Mwanza kufuatilia mwenendo wa utekelezaji wa miradi katika Mashirika hayo.
Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Bi. Vickness Mayao (kulia) akifafanua jambo katika kikao kati ya Shirika la Plan International na Bodi hiyo ilipokuwa inatembelea Mashirika yaliyopo Kanda ya Ziwa mkoani Mwanza kufuatilia mwenendo wa utekelezaji wa miradi katika Mashirika hayo.
Meneja Miradi kutoka Shirika la Plan International Bw. Nicodemas Gachu akielezea kuhusu utekelezaji wa Miradi inayotekelezwa na Shirika hilo katika kikao kati ya Shirika hilo na Bodi ya Uratibu wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ilipotembelea Mashirika yaliyopo Kanda ya Ziwa mkoani Mwanza kufuatilia mwenendo wa utekelezaji wa miradi katika Mashirika hayo.
Mjumbe wa Bodi ya Uratibu wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Dkt.Zena Mabeyo (katikati) akieleza jambo katika kikao kati ya Shirikala Plan Internationla na Bodi hiyo ilipotembelea Mashirika yaliyopo Kanda ya Ziwa mkoani Mwanza kufuatilia mwenendo wa utekelzaji wa miradi katika Mashirika hayo.
Mjumbe wa Bodi ya Uratibu wa Yasiyo ya Kiserikali Dkt.Alli Mcharazo (katikati) akielezea jambo katika kikao kati ya Shirika la Plan International na Bodi hiyo ilipotembelea Mashirika yaliyopo Kanda ya Ziwa mkoani Mwanza kufuatilia mwenendo wa utekelezaji wa miradi katika Mashirika hayo.
Mjumbe wa Bodi ya Uratibu wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Hassan Samli (kulia) akielezea jambo katika kikao kati ya Shirika la Plan International na Bodi hiyo ilipotembelea Mashirika yaliyopo Kanda ya Ziwa mkoani Mwanza kufuatilia mwenendo wa utekelezaji wa miradi katika Mashirika hayo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Uratibu wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Dkt. Richard Faustine Sambaiga (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Bodi na Meneja wa Miradi kutoka Shirika la Plan International Bw. Nicodemas Gachu mara baada ya kumaliza kikao kati ya Bodi na Shirika hilo kilicholenga kufuatilia utekelezaji wa Miradi katika Shirika hilo jijini Mwanza.Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini WAMJW

DK.BASHIRU AZINDUA MAGHARIB YA KIJANI

$
0
0
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Dkt.Bashiru Ally Kakurwa,akitembelea vikundi vya wajasiriamali walioshiriki katika hafla ya uzinduzi wa Magharibi ya Kijani Zanzibar.
MWENYEKITI wa CCM Mkoa wa Magharibi kichama ndugu Mohamed Rajab Soud, akizungumza katika hafla hiyo ya uzinduzi wa kampeni ya magharib ya kijani iliyofanyika Bububu Chuo cha kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Zanzibar.
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Dkt.Bashiru Ally Kakurwa, akiwahutubia Wana CCM katika uzinduzi wa kampeni ya Magharibi ya Kijani iliyozinduliwa katika ukumbi wa Chuo cha kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Bububu Zanzibar.
…………………..

NA IS-HAKA OMAR,ZANZIBAR.

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt.Bashiru Ally Kakurwa, ameyaonya mashirika ya kimataifa yanayowakilisha nchi zao Tanzania kuacha kuingilia siasa za ndani ya nchi.

Alisema kuna baadhi ya wawakilishi wa nchi hizo za kigeni wameanza kutoa kauli zisizofaa na vipeperushi kupitia nchi za mitandao wakibeza na kuhoji kuhusu Uchaguzi wa Serikali za mitaa uliofanyika hivi karibuni.

Hayo aliyasema wakati akizindua kampeni ya Magharibi ya kijani huko katika ukumbi wa Chuo cha kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Zanzibar.

Alisema ajenda ya uchaguzi huo tayari imefungwa na chama cha mapinduzi kimeibua mshindi kwa asilimia zaidi ya 99 na kwa sasa kinajipanga na Uchaguzi Mkuu ujao wa mwaka 2020.

Alisema watu hao wanaojadili uchaguzi katika mitadao ya kijamii ni kupoteza muda kwani mitandao haipigi kura wala kubadilisha uhalisia wa ushindi wa CCM.

“Naendelea kuwakumbusha hawa wenzetu wanaojadili uchaguzi katika mitandao kuwa Whatsapp na Instagram na facebook hazipigi kura na hazijasajiliwa katika daftari la kudumu la wapiga kura”, amesema Dkt.Bashiru.

Katika maelezo yake Dkt.Bashiru alisema kuna baadhi ya watu wanadhani demokrasia ipo katika uchaguzi tu jambo ambalo sio sahihi kwani hata kutokuwa na tama ya kukandamiza uhuru wa wengine pia ni demokrasia.

Akizungumzia kampeni hiyo iliyozinduliwa alisema kampeni ya kijani iliyoasisiwa na UVCCM imesaidia kwa kiasi kikubwa kuimarisha shughuli za kisiasa ndani ya Chama na Jumuiya zake.

Alisema kampeni hiyo ya Magharibi ya kijani inatakiwa kutoa matokea chanya yanayoendana na malengo yaliyokusudiwa na kuimarisha shughuli za kisiasa chama ndani ya mkoa huo kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.

Alieleza kuwa Mapinduzi ya Zanzibar ya Januari 12 mwaka 1964 ndio yaliyofanikisha nchi kujitawala na kufikia maendeleo endelevu yaliyopo hivi sasa.

Akizungumzia Utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2015-2020,alisema imetekelezwa kwa ufanisi mijini na vijiji wanapata huduma bora za kijami,kiuuchumi na kimaendeleo bila ubaguzi.

Dkt.Bashiru, alihoji wanaobeza uongozi wa Rais wa Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein ambaye anamaliza muda wake mwaka ujao akiwa na historia nzuri na iliyotukuka ya uchapakazi na uadilifu.

Alisema Dk.Shein ni kingozi mwenye uzoefu na uwezo mkubwa kiuongozi kwani amehudumu kwa muda mrefu ndani ya ngazi za juu za Chama na Serikali.

Alisema Rais ajaye wa Zanzibar anatakiwa kuwa na sifa kama za Rais wa sasa Dk.Ali Mohamed Shein ambaye ni muadilifu,mpole na mchapakazi.

“ Nawashangaa baadhi ya wanasiasa eti wanatathimini Dk.Shein na Serikali anayoiongoza nawambia kuwa Rais huyu ni wa kuigwa kwani mambo ya maendeleo aliyoyafanya Zanzibar yanaonekana kwa kila mtu”, alieleza na kuongeza kuwa Rais huyo hadi hivi sasa hana kashifa za rushwa wala ufisadi.

Pamoja na hayo Dkt.Bashiru, aliwasihi Wana CCM kuendelea kushikamana na kulinda uhuru ulioasisiwa na Waasisi wa Chama hicho kwa gharama yoyote bila hofu.

Katibu huyo alisema ushindi uliopatikana katika uchaguzi wa serikali za mitaa Tanzania bara ni sehemu ya kutesti mitambo na kwa sasa anatumia ziara yake kuendelea kufunga mitambo katika Mikoa yote ya Zanzibar ili 2020 CCM ipate ushindi wa kihistoria.

Aliahidi kwamba akiwa Mkurugenzi wa Uchaguzi ndani ya CCM kwa Tanzania nzima atahakikisha CCM inashinda Zanzibar na Tanzania bara katika uchaguzi mkuu ujao.

Naye Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Mwl.Kombo Hassan Juma, alisema CCM inaimarika kisiasa kutokana na Serikali kutekeza vizuri Ilani ya CCM .

Mapema akizungumza Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Magharib ndugu Mohamed Rajab Soud,alisema kampeni hiyo imezinduliwa kwa lengo la kusafisha njia ya kisiasa kuelekea 2020.

Wafanyakazi wa Benki ya NBC wajitolea damu kusaidia wenye mahitaji

$
0
0
Watanzania wamehimizwa kushiriki zoezi la kuchangia damu kwa hiari ili kukidhi mahitaji makubwa ya damu na kuokoa maisha ya wenzao pamoja na kusaidia huduma za afya nchini.

Hayo yamesemwa jana jijini Dar es Salaam na Ofisa Fedha Mkuu wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) Waziri Barnabas akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Bbenki hiyo, Theobald Sabi wakati wa tukio la kuchangia damu kwa hiari lililondaliwa na NBC akisema kwamba huo ni utamaduni wa benki hiyo wa kuchangia damu kwa kujitolea.

Alisisitiza kwamba ni muhimu kwa watanzania kuanza kujitokeza na kujitolea damu kwa hiari ili kuendelea kuokoa maisha ya wenye mahitaji. "Hii ni mara ya tatu kwa benki hii na wafanyakazi wake kushiriki kwenye kampeni ya uchangiaji damu ili kuokoa maisha ya wakinamama wanaojifungua, waliopata ajali na watu wengine wenye mahitaji ya damu nchini,” aliongeza.

Barnabas aliongeza kwamba kwamba mahitaji ya damu bado yapo juu kwenye mahospitali hasa kwenye upasuaji na bado mwamko upo chini kwa wananchi kama uchangiaji wa damu kwa hiari.

"Ni muhimu sana kwa watanzania wenzetu kuungana nasi katika shughuli ya kujitolea ya kuchangia damu ambayo inatarajiwa kumalizika kesho,” alisema.

Alisema kwamba kwenye shughuli hiyo wanatarajia kukusanya takriban chupa 100 kutoka kwa wafanyakazi wa benki hiyo na watu wengine kutoka maeneo mbalimbali ya jiji ili kupunguza mahitaji makubwa ya damu nchini na alisisitiza kuwa kampeni hiyo inapaswa kuwa endelevu kukidhi matarajio ya nchini.

Kwa upande wake, Kaimu Ofisa Rasilimali watu wa benki hiyo, Grace Mgondah alisema kwamba wanatarajia wafanyakazi 500 kutoka kwenye matawi mbalimbali watashiriki katika zoezi hilo la siku mbili ya kujitolea damu kwa hiari.

"Hii ni sehemu ya huduma kwa jamii ambayo benki yetu ya NBC inasikia fahari kuwahudumia na ninatoa wito kwa watanzania wenzetu kujitokeza kwa wingi kuja kutuunga mkono,” alisisitiza.

Fatuma Mjungu kutoka Kitengo cha Taifa cha Damu Salama (NBTS) alisema kwamba mwaka huu wanatarajia kukusanya chupa 450,000 za damu kutoka kwenye taasisi mbalimbali na watu wanaojitolea kwa hiari. "Mahitaji ya damu kwa sasa nchini ni chupa 520,000 lakini asilimia moja tu ya watanzania wote wakichangia damu tunaweza kukidhi mahitaji ya damu kwa taifa,” aliongeza

Mjungu pia ametoa wito kwa taasisi na makampuni nchini kuinga mkono benki hiyo ya NBC kwa kuhamasisha wafanyakazi wake na wananchi wengine kwa ujumla kujitolea damu kwa ajili ya watu wenye uhitaji.
  Ofisa Fedha Mkuu wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Waziri Barnabas (katikati), akihojiwa na waandishi wa habari, Dar es Salaam leo, wakati yeye na mwenzake, Fanuel Jenga (kushoto), wakijitolea damu katika zoezi lililoandaliwa na benki hiyo kwa wafanyakazi wake kujitolea damu kusaidia wenye mahitaji kupitia Mpango wa Taifa wa Damu Salama.

 Ofisa Fedha Mkuu wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Waziri Barnabas (kulia), pamoja na Mhasibu wa benki hiyo, Fanuel Jenga (kulia kwake) wakichukuliwa vipimo vya damu kabla ya kujitolea damu jijini Dar es Salaam leo, katika zoezi liloandaliwa na benki hiyo kwa wafanyakazi wake pamoja na wakazi wengine wa jiji hilo kusaidia wenye mahitaji kupitia Mpango wa Taifa wa Damu Salama. Kushoto ni Evelyn Dielly kutoka Mpango wa Taifa wa Damu Salama.

  Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) wakijitolea damu  katika zoezi liloandaliwa na benki hiyo kwa wafanyakazi wake pamoja na wakazi wengine wa Jiji la Dar es Salaam leo kujitolea damu kusaidia wenye mahitaji kupitia Mpango wa Taifa wa Damu Salama.
 Mkazi wa Chalinze, Joshua Mjuni akijitolea damu katika zoezi liloandaliwa na NBC kwa wafanyakazi wake pamoja na wananchi wengine leo, kujitolea damu kusaidia wenye mahitaji kupitia Mpango wa Taifa wa Damu Salama. Anayemhudumia ni muuguzi kutoka Damu Salama, Peter Chami.
 Ofisa Uhamasishaji wa Mpango  wa Taifa wa Damu Salama, Fatuma Mjungu, akihojiwa na waandishi wa habari katika zoezi la uchangiaji damu wa hiari lililkoandaliwa na Benki ya NBC jijini Dar es Salaam leo.

FORUMCC, WADAU WATOA USHAURI KWA WATALAAM,WAFANYA MAAMUZI KUWEKA MGAWANYO SAWA MAENEO YENYE UHITAJI IKIWEMO MIRADI YA MABADILIKO YA TABIANCHI

$
0
0
Na Said Mwishehe, Michuzi  Globu ya jamii

WATAALAMU na wafanya maamuzi wa miradi mbalimbali nchini Tanzania  wameshauriwa kuweka mgawanyo sawa  katika maeneo yenye uhitaji wa miradi ikiwemo ya mabadiliko ya tabianchi na kuongeza rasilimari ili kuweza kupunguza kasi ya uhitaji.

Akizungumza Dar es Salaam leo Novemba 28,mwaka 2019 katika mkutano wa wadau wa masuala ya Mabadiliko ya tabianchi chini ya Mradi wa Uwajibikaji katika masuala ya mabadiliko ya tabianchi (ACATI) unaofadhilia na Umoja wa Ulaya ,Mkurugenzi wa Shirika la ForumCC,Rebecca Muna  amesema dhana ya uwajibikaji katika  mambo ya mabadiliko ya tabianchi yanapaswa kuangalia  kwa namna  gani rasilimari zinaelekezwa  mahali ambapo kuna uhitaji zaidi katika jamii inayoathirika zaidi na mabadiliko ya tabianchi.

Muna ameongeza wataalamu hao wanaopanga miradi iende wapi wanapaswa kuzingatia mahali ambapo kuna uhitaji zaidi na kuwa wawazi kuliko kuvutia miradi hiyo kupeleka katika maeneo yenye watu maarufu na wenye nguvu ya kuvuta rasilimali.

"Katika suala la uwajibikaji wa mabadiliko ya tabianchi yanapaswa kuangalia ni maeneo yapi yanapata changamoto hiyo na miradi inawafikia walengwa ipasavyo bila kubaguliwa.Kunahitajika kufanya ushawishi na utetezi kwa Serikali kuhakikisha katika bajeti zinaelekezwa katika vipaumbele vya uhimili wa mabadiliko ya tabianchi na kuangalia ni rasilimari zinawafikia watu walioathirika zaidi  na mabadiliko ya tabianchi,"amesema.

Ameongeza ni  wakati muafaka kuondoa mambo ya kupeleka miradi katika eneo moja bali ihakikishe inaangalia wapi kuna uhitaji zaidi ya uhimili wa mabadiliko ya tabianchi  ili kupunguza uongezwaji wa athari za mabadiliko ya tabianchi katika maeneo ambayo yameathirika zaidi.
  
Wakati huo Ofisa Mazingira na Mratibu wa Masuala ya Mabadiliko ya Tabianchi kutoka Baraza la Taifa la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira nchini(NEMC),Fredrick Mulinda  amefafanua baraza hilo ndilo linaosimamia mazingira na ni taasisi ilipochini ya Ofisi ya Makamu wa Rais na ndio yenye dhamana ya kuratibu  masuala ya mabadiliko ya tabianchi Tanzania.

"Baraza hili  linawakilisha nchi kama taasisi iliyopewa dhamana ya kupokea fedha za kuhimili mabadiliko ya tabianchi kutoka Mfuko wa Dunia wa Kuhimili mabadiliko ya tabianchi kwa nchi zinazoendelea.Baada ya kukamilisha kwa michakato mwaka  2017  kwa nchi zinazoendelea zinapata fursa ya kupata fedha Dola Milioni10 katika kutekeleza miradi iliyoathiriwa zaidi na mabadiliko ya tabianchi kwenye nchi husika,"amesema.

Ameongeza kwamba Serikali kupitia ofisi ya Makamu wa Rais tayari imetekeleza mradi mmoja kwa moja ya shirika ambalo iligharimu Sh. Dola million tano na  tayari kumefanyika  mchakato wa kuandika miradi kwa baadhi ya taasisi za mabadiliko ya tabianchi  ambapo takribani  taasisi nne zimepita na zipo katika mchakato wa mwisho wa kupewa fedha hizo na kutekeleza miradi.

Kwa mujibu wa Mulinda amesema fedha hizo zinawafikia wananchi moja kwa moja katika kutelezewa miradi ya mabadiliko ya tabianchi katika maeneo husika ambapo kunaathari kubwa ya mabadiliko hayo na athari zinaonekama. 
 Wadau wa mabadiliko ya tabianchi wakiwa katika majadiliano kuhusu athari za mabadiliko ya tabianchi na hatua zinazostahili kuchukuliwa kukabiliana na mabadiliko hayo. Wadau hao wamekutana chini ya Mradi wa Uwajibikaji katika Mabadiliko ya Tabianchi(ACATI) kupitia ufadhili wa Umoja wa Ulaya 
 Mmoja wa wadau akitoa mada katika kikao cha majadiliano kuhusu athari za mabadiliko ya tabianchi na hatua zinazostahili kuchukuliwa .Wadau wao wamekutana chini ya Mradi wa Uwajibikaji katika Mabadiliko ya Tabianchi(ACATI) unaofadhiliwa na Umoja wa Ulaya 
Wadau wa mabadiliko ya tabianchi wakiwa katika picha ya pamoja leo jijini Dar es Salaam wakati wa kikao cha majadiliano kuhusu mabadiliko ya tabianchi chini Mradi wa Uwajibikaji katika Mabadiliko ya Tabianchi(ACATI)unaofadhiliwa na Umoja wa Ulaya

BODI YA NYAMA TANZANIA YAKUTANA NA WAFANYABIASHARA YA NYAMA JIJI LA DODOMA, YAWAKUMBUSHA KUFUATA SHERIA,KUANZA KUWASAJILI KUANZIA KESHO... WATUMIA VIGOGO BUCHANI KUKIONA

$
0
0
Na Said Mwishehe,Michuzi Globu ya jamii-Dodoma

BODI ya Nyama Tanzania imekutana na wadau mbalimbali wanajihusisha na biashara ya nyama katika Mji wa Dodoma ambapo imewakumbusha hatua mbalimbali zinapaswa kufuata kwa watoa huduma hiyo ikiwa pamoja na kiheshimu sheria huku ikitangaza kuanza kuwasajili wadau wote.

Wamekumbushwa umuhimu wa mnyama kupumzishwa kati ya saa 12 hadi saa 24 kabla ya kuchinjwa ikiwa ni sehemu ya kumpunguzia mnyama mawazo huku wakikumbushwa nyama ubora wa nyama kwa uthibitisho wa daktari. 

Akizungumza leo Novemba 24 mwaka 2019 Mjini Dodoma Kaimu Msajili wa Bodi ya Nyama nchini Imani Paulo Sichalwe amewaaambia wanaojihusisha na biashara hiyo kuifanya kwa mujibu wa taratibu kwa kuafuata sheria na sio mazoea.

" Bodi ya Nyama leo tumeamua kukutana nanyi ili kutoa elimu kwa wadau wote wa nyama Dodoma kuhusu namna bora ya ubebaji nyama na taratibu za ufanyaji biashara ya nyama.Tunayo majukumu mengi na baadhi ya majukumu hayo ni kusimamia biashara ya nyama nchini kwa kuhakikisha sheria zote zinafuatwa, kwa ujumla ni kusimamia taratibu zote na watakaokiuka kuna adhabu zake ingawa huko kwenye adhabu sio mara nyingi .

"Ni mara ya kwanza kukutana na wadau wa sekta hiyo ya ufanyaji wa biashara ya nyama katika Jiji la Dodoma kwa wingi namna hii. Kazi ya tatu ni kuendeleza tasnia ya nyama ikiwa pamoja na kutoa elimu ambayo itawawezesha wadau kuwa na nyama iliyokidhi viwango,"amesema na kuongeza kuwa lengo la bodi ya nyama kuwepo na wadau hao ni kuzungumza na wadau hao na kukumbusha.

Sichwale amesema kuwa kwa hiyo wanatoa elimu hiyo kama sehemu ya kuakumbusha yanayotakiwa kufanywa na wadau wa nyama na kutambua mnyonyoro wote kuanzia nyama inapoanzia hadi inakwenda kwa mlaji.

Akizungumzia usafirishaji mnyama amesema ni muhimu kuzingatiwa kwa sheria ya mnyama kwani anayo sheria inayomlinda na anahaki zake na kwamba mnyama hatakiwi kuumizwa kwa kupigwa fimbo na anaposafirishwa mnyama lazima apumzike kila baada ya kilometa 300.Mnyama anaposafirishwa biashara nyama yake inakuwa sio nzuri na matokeo yake huonekana mwishoni.

Ameongeza kuwa pia wanyama nao wana mawazo na yanatokana na sababu mbalimbali ,kwani kuna wanyama ambao hawajawahi kuona gari wala kupandisha,hivyo huwa na mawazo."Tunashauri mnyama hatakiwi kupigwa kwani kunaharibu nyama kwani inakuwa ngumu kuihifadhi.Pia mnyama anapopigwa nyama inakuwa ngumu."

Kuhusu kuchinja nako kuna hatua zake ambazo lazima zifuatwe na kutoa mfano mnyama ambaye ni mgonjwa au amekonda sana hatakiwi kuchinjwa na kwamba katika kukidhi hatua hizo kuna wataalaam wakiwamo madaktari ambao kazi yao ni kuangalia ubora wa mnyama na nyama yenyewe."Mnyama kabla ya kuchinjwa anatakiwa kumpumzika kati ya saa 12 na saa 24 .Kumpumzisha mnyama kunamuondolewa mawazo."

Pia amesema wakati mnyama amepumzika hatakiwi kupewa chakula cha aina yoyote zaidi ya maji.Ameongeza katika kumchinja mnyama lazima awe amepoteza fahamu kwani naye anaogopa kufa na kwa mazingira hayo mnyama anatakiwa kupigwa shorti ya umeme na kwamba sifa mojawapo ya machinjio ni kuwa na sehemu ya kumpunguzia maumivu.

"Baada ya kuchinjwa damu inadibi iachwe ichuruzike na kuna sababu zake,mojawapo ni kuua balteria na kama inavyofahamika katika damu kuna vitu vingi na ndio maana machinjioni kuna harufu ya damu .Kwa hiyo baada ya mnyama kuchinjwa damu itaachwa itoke na wakati huo huo daftari wanafanya kazi yao ya kuangalia ubora wa nyama.Baada ya nyama kukaguliwa hatua inayofuata ni usafirishaji.Wanatoa huduma hiyo lazima wawe wamepimwa afya, wawe na sare nyeupe,"amesema.

Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Mifugo Jiji la Dodoma Mwesiga Gration amesisitiza umuhimu wa wafanyabiashara ya nyama kuhakikisha mabucha yao yanakuwa salama ili kuwa na nyama iliyobora hasa kwa kuzingatia Jiji la Dodoma wageni ni wengi na lazima wahakikishiwe usalama wa nyama wanayokula na si wageni tu bali na kwa wananchi wote kwa ujumla.

"Leo nipo hapa kuwaomba kwa lugha ya upole kabisa,tuheshimu utaratibu uliopo, nyama iuuzwe katika mazingira safi na salama. Lazima bucha ziwe safi.kuna bucha ukienda unakuta kuna Kigogo kinatumika wakati wa kupata nyama,hii hapana sasa,tubadilike.Dodoma nchi yote iko hapa siko tayari kupoteza kazi kwa ajili ya.kutosimamia yale ambayo natakiwa kusimamia,"amefafanua.

Wakati huo huo Ofisa Usajili Mifugo Bodi ya Nyama Tanzania Geofrey Kakuru amezungumzia usaji wa mifugo na nyama ambapo amesema usajili huo unafanyika kwa mujibu wa sheria iliyoanzisha Bodi ya Nyama Tanzania ambapo wahusika na kusajili maeneo yote yanayohusika na biashara ya mifugo na nyama na hivyo wote ambao wanafanyabiashara hiyo wanatakiwa kusajiliwa na kuna aina nyinyi za wadau ambao wanapaswa kusajiliwa na bodi hiyo.

Ameongeza kwamba sababu za kuwasajili mojawapo ni kuwatambua wadau na wakati huo huo kuwa na nafasi nzuri ya kutatua changamoto zao na kwamba ametoa rai wadau kujisajili. Pia umuhimu mwingine wa kusajili ni kupata takwimu sahihi za masuala yanayohusu sekta ya nyama, kwani hiyo inasaidia hata Serikali inapotaka kufanya jambo lolote katika eneo hilo lazima kuwepo na takwimu sahihi na lengo jingine kusajili kunasaidia katika kuchangia pato la taifa

Hata hivyo amesema kuanzia kesho wataanza kusajili wadau wa nyama na kwamba ni jukumu la kila anayehusika na sekta hiyo kuhakikisha anasajiliwa kwani wasiojisajili watachukuliwa hatua kwani watakuwa wanakiuka sheria
 Wadau wa sekta ya nyama katika Jiji la Dodoma wakiwamo wafanya biashara ya nyama na wamiliki mabucha na wachinjaji nyama wakiwa katika kikao cha kukumbushwa umuhimu wa kufuata sheria katika kutoa huduma ya nyama jijini Dodoma. Kikao hicho kimeandaliwa na Bodi ya Nyama Tanzania ambacho kimefanyika leo   Novemba 28,mwaka 2019
 Ofisa Usajili Mifugo Bodi ya Nyama Tanzania Geofrey Kakuru akifafanua jambo wakati wa kikao cha bodi hiyo na wafanyabiashara ya nyama wakiwamo wamiliki wa mabucha katika Jiji la Dodoma
 Kaimu  Msajili   Bodi ya Nyama Tanznaia Iman Paul Sichwele akizungumza na wafanyabiashara ya nyama na wadau wa sekta hiyo leo Jijini Dodoma
Baadhi ya maofisa kutoka Bodi ya Nyama Tanzania, maofisa Afya na wakuu wa Idara ya Nyama Jiji la Dodoma.wakiwa katika kikao kati yao na wadau wa biashara ya nyama katika Jiji hilo.



Mshindi wa promosheni ya Tigo Chemsha Bongo apatikana

$
0
0

Mtaalam wa Huduma za ziada-Tigo, Fabian Felician na Jehud Ngolo- Afisa Mwandamizi Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania. wakimpigia simu Shaban Khamis Ali,mkaazi wa Zanzibar, mshindi wa promosheni ya Tigo Chemsha bongo
Mtaalam wa Huduma za ziada-Tigo, Fabian Felician na Jehud Ngolo- Afisa Mwandamizi Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania. wakimpigia simu Shaban Khamis Ali,mkaazi wa Zanzibar, mshindi wa promosheni ya Tigo Chemsha bongo

Droo ya mwisho ya promosheni ya ‘Tigo Chemsha Bongo’ imefanyika jijini Dar es Salaam ambapo mkaazi wa Zanzibar, Shabani Khamis Ali (48) amejishindia gari mpya aina ya Renault KWID yenye thamani ya 23m/-. Khamis akiongea baada ya kupigiwa simu na Mtaalam wa Huduma za Ziada kutoka Tigo, Fabian Felician, kumfahamisha kuwa ameibuka mshindi, alisema anayo furaha kufanikiwa kuwa miongoni mwa washindi kupitia promosheni hiyo kwa kujishindia gari mpya.

“Sikutegemea kabisa kuwa ningeibuka mshindi katika promosheni hii, Habari hizi naziona kama ndoto kwangu, nashukuru Tigo kwa kunifungia mwaka vizuri na kutimiza ndoto yangu ya kumiliki gari, kwani itanisaidia katika mizunguko yangu ya kibiashara “alisema kwa furaha.

Mtaalam wa Huduma za Ziada kutoka Tigo, Fabian Felician, alimpongeza mshindi huyo na kutumia fursa hiyo kuwashukuru wateja wote wa kampuni ambao walishiriki na baadhi yao kujishindia zawadi mbalimbali ikiwemo zawadi za fedha taslimu ambayo yalitolewa na kampuni hiyo.

“Tunayo furaha kubwa katika kipindi hiki tunachoelekea katika msimu wa sikukuu kumpata mshindi wetu wa gari ya aina Renault Kwid,yenye thamani ya 23m/-, gari hili ni jipya kabisa, baada ya kumpata mshindi taratibu zengine zitafata ili tuweze kumkabidhi Shaban Khamis Ali gari lake jipya. Tunawashukuru wateja wetu kutoka nchini pote walioshiriki kwenye promosheni hii ya miezi mitatu ambayo imemalizika mwishoni mwa mwezi wa Novemba 2019”. alisema Felician.

Aliongeza kuwa, promosheni hii ambayo ilianza jijini Mwanza katika msimu wa Tigo Fiesta 2019-Saizi Yako imepata mafanikio makubwa kutokana na wateja wengi kujitokeza kushiriki na baadhi yao kufanikiwa kujishindia zawadi(fedha taslim) mbalimbali na hivyo Tigo kufanikisha lengo lake ambalo lilikuwa ni kuwashukuru wateja kwa kuiunga mkono kampuni kupitia kununua bidhaa zake mbalimbali.

Kwa kumalizia Felician aliwashukuru wateja wote wa Tigo kwa kuendelea kuunga mkono kampuni na kuahidi kuwa promosheni mbalimbali za kunufaisha wateja wa kampuni hiyo zinatendelea kubuniwa katika siku za usoni.

TANZANIA YASEMA WAKIMBIZI ZAIDI YA LAKI TATU WAMEPATA HIFADHI, KUENDELEA KUTOA HUDUMA MUHIMU

$
0
0

Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

JUMLA ya wakimbizi 33,765 kutoka Rwanda, Burundi, Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo (DRC) na wengine kutoka nchi 15 wamepata hifadhi nchini pamoja na kupata huduma muhimu ikiwemo elimu na afya.

Akizungumza leo Novemba 28,2019 jijini Dar es Salaam katika maadhimisho ya siku ya takwimu duniani Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango amesema mwaka 2018 Serikali kwa kushirikiana na Shirika linaloshughulikia wakimbizi (NHCR) lilianzisha mfumo rasmi kwa utoaji kwa elimu ya msingi ambapo asilimia 90 ya watoto kutoka Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo na asilimia 79 ya watoto kutoka Burundi waliandikishwa kupata elimu ya msingi.

Mpango amesema Tanzania itaendelea kuwagharamia wakimbizi na wale wenye uhitaji wa hifadhi na kueleza kuwa hadi sasa jumla ya wakimbizi laki mbili wakiwemo wake, waume na watoto wamepewa uraia wa Tanzania.

Aidha amewataka watakwimu wote katika Halmashauri zote nchini kuripoti kwa Mtakwimu mkuu wa Serikali na hiyo ni  kutokana na uwepo wa wakimbizi wengi katika halmashauri nyingi hivyo hitaji kupata takwimu ni kubwa hasa kwa kujua na kutambua mahitaji yao ya muhimu.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Takwimu ya Taifa Albina Chuwa amesema  maadhimisho hayo ya siku ya takwimu hufanyika kila mwaka  Novemba 28, na kwa mwaka huu maadhimisho hayo yataende sambamba na kujadili changamoto zinazozikumba Chama cha takwimu nchini na  tasnia hiyo kwa ujumla.

Amesema, wamekuwa wakikusanya takwimu mbalimbali kupitia sensa za watu na makazi na baadaye kupima na kutoa takwimu sahihi kulingana na mahitaji muhimu.

"Siku ya takwimu inayoadhimisha kila mwaka imewalenga wananchi, wapate kujifunza kuhusiana na takwimu na leo  tutajadili changomoto mbalimbali na wadau wakiwemo wananchama wa chama cha takwimu duniani lakini pia tutajadili namna ya kuboresha tasnia hii" ameeleza.

Ameeleza kuwa wananchi wanahitaji kupata takwimu sahihi na Ofisi hiyo itaendelea kutoa elimu ya takwimu kupitia majukwaa mbalimbali kwa manufaa ya jamii kwa ujumla. 
Mwandishi wa Habari wa Gazeti la Jamvi la Habari Veronika Mrema,akipokea zawadi kutoka kwa Waziri wa Fedha na Mipango Dkt Philip Mpango ,Veronika amekuwa mshindi wa pili katika tuzo za Waandishi wa Kitakwimu zilizotolewa leo Novemba  28,2019 na Ofisi ya Takwimu ya Taifa.

 Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt.Philip Mpango akizungumza na Washiriki wa Mkutano wa Siku ya Takwimu Afrika uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam, Waziri ametoa maagizo kwa Ofisi ya Takwimu (NBS), na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA)  kufanya kazi kwa kushirikiana. 
 Mwenyekiti wa Bodi ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Dkt. Amina Msangi Akizungumza katika Mkutano wa Siku ya Takwimu Afrika uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam, ambapo kauli mbiu ilikuwa ni ‘Kila mmoja wetu ana umuhimu kwa takwimu bora, kwa usimamizi bora wa watu wanaolazimika kuyakimbia makazi yao barani Afrika’
Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Dkt. Albina Chuwa akizungumza katika na Washiriki wa Mkutano wa Siku ya Takwimu Afrika uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam, ambapo kauli mbiu ilikuwa ni ‘Kila mmoja wetu ana umuhimu kwa takwimu bora, kwa usimamizi bora wa watu wanaolazimika kuyakimbia makazi yao barani Afrika’ 
  Mkurugenzi Msaidizi-Idara ya Ajira na Ukuzaji Ajira, Ofisi ya Waziri Mkuu, Bw.Ahmed Makbel akichangia mada katika Mkutano wa Siku ya Takwimu Afrika uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam, ambapo kauli mbiu ilikuwa ni ‘Kila mmoja wetu ana umuhimu kwa takwimu bora, kwa usimamizi bora wa watu wanaolazimika kuyakimbia makazi yao barani Afrika’. 
 Sehemu ya meza kuu akifuatilia yaliyokuwa yakijiri ukumbini humo 

 Sehemu ya Wadau wa Watakwimu kutoka Sehemu mbalimbali nchini wakifuatilia Mkutano wa Siku ya Takwimu Afrika uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam leo Novemba 28, 2019, kauli mbiu ilikuwa ni ya Mkutano huo ni ‘Kila mmoja wetu ana umuhimu kwa takwimu bora, kwa usimamizi bora wa watu wanaolazimika kuyakimbia makazi yao barani Afrika’
 
Wanafunzi kutoka Chuo cha Takwimu cha Mashariki mwa Afrika waliohudhuria katika Siku ya Takwimu Afrika iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam wakifuatilia Mkutano huo

SERIKALI YATOA ONYO KWA WATU WANAOENDELEZA UKATILI WA KIJINSIA

$
0
0
SERIKALI imetoa onyo kwa wale wote wanaojihusisha na vitendo vya ukatili wa kijinsia na kwamba haitomvumilia yeyote ambaye ataendeleza vitendo hivyo ambavyo vimekua vikiathiri maendeleo nchini.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Afya Maendeleo ya jamii Jinsia Wazee na Watoto, Mhe Ummy Mwalimu leo jijini Dodoma katika uzinduzi wa kampeni ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.Waziri Ummy mesema serikali imeweka mikakati mbalimbali ya kukabiliana na vitendo hivyo kwa kutumia sheria zilizopo ambapo atakaebainika kuendeleza ukatili wa kijinsia hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Amesema serikali imekuwa ikitumia gharama nyingi katika kushughulikia waathirika wa vitendo vya ukatili ambapo fedha hizo zingeweza kutumika katika kutoa huduma nyingine za kijamii.

"Kwa mujibu wa benki ya Dunia baadhi ya nchi hutumia hadi asilimia 3.5 ya pato ghafi la taifa kugharamia ukatili wa kijinsia, serikali ya awamu ya tano haiwezi kuvumilia vitendo hivi kwa kuwa vinaathiri maendeleo," Amesema.

Ameagiza walimu wakuu wa shule msingi na sekondari nchini kutoa idadi ya mimba kila baada ya miezi mitatu."Kuwepo kwa ukatili wa kijinsia hapa nchini kunachangia Taifa kutofikia uchumi wa kati wa Viwanda kwa sababu nguvu kazi nyingi inapotea kwa kutofikia malengo yao," Amesema.

Aidha, ametoa wito kwa wadau kutumia kampeni hiyo kufanya tathmini maeneo yote yanayohusiana na vitendo vya ubakaji ili kubainisha kiwango cha tatizo hilo na kupendekeza mikakati ya kushughulikia suala hilo.

Awali, Mratibu wa Kitaifa wa Shirika la Wanawake katika Sheria na Maendeleo Barani Afrika(WiLDAF), Anna Kulaya, ameomba serikali kutunga sheria maalum inayoshughulikia masuala ya ukatili wa kijinsia na mahakama ya familia ili kuharakisha kesi za ubakaji ambazo zimekuwa zikikwama kwa kukosa ushahidi.

"Kwa mujibu wa taarifa ya uhalifu wa kibinadamu iliyotolewa na jeshi la polisi kwa mwaka 2018, inaonesha kati ya matukio 11,759, matukio ya ubakaji yalikuwa ni 7,617 sawa na asilimia 64.7," Amesema

Amesema kumekuwapo na mitazamo tofauti kwa jamii hasa ya kutoa taarifa na ushahidi pale matukio ya ubakaji yanapotokea kutokana na wanaofanya vitendo hivyo ni watu wa karibu na wakuaminika.Naye, Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Wanawake (UN-Women), Hodan Addou, amesema mwanamke mmoja kati ya watatu duniani wanafanyiwa ukatili wa kijinsia.

"Inakadiriwa wasichana milioni 15 duniani wamekumbana na vitendo vya ubakaji huku kwa Tanzania asilimia 17 ya watu wamefanyiwa ukatili wa kijinsia," Amesema.Amesema vitendo vya ubakaji kwa tafiti mbalimbali ambazo zimekuwa zikifanyika vinashamiri na kugharimu fedha nyingi.

"Ukiweza kuzuia kila ubakaji wowote zaidi ya Dola za Kimarekani 122,000 huokolewa na katika nchi nyingi za Afrika zaidi ya nusu ya gharama za ubakaji hulipwa kupitia vyanzo vya mapato vya serikali ikiwemo Afya, Huduma za jamii, na mfumo wa mahakama nchini,"Amesema.
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto,Mhe Ummy Mwalimu akizungumza kwenye mkutano wa uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia. Tukio hilo limefanyika leo jijini Dodoma.
Sehemu ya wanafunzi kutoka Shule mbalimbali jijini Dodoma ambao wamejitokeza katika uwanja wa Jamhuri kushuhudia uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia ambapo mgeni rasmi alikua Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe Ummy Mwalimu.

WAKURUGENZI WA HALMASHAURI WAPEWA SIKU SABA KUWASILISHA TAARIFA YA MIKOPO YAO

$
0
0


WAKURUGENZI WA HALMASHAURI WAPEWA SIKU SABA KUWASILISHA TAARIFA YA MIKOPO YAO



Charles James, Michuzi Blog

HALMASHAURI zilizochukua mikopo kutoka katika mabenki ya kibiashara na bado hawajazitumia wametakiwa kuzirejesha ndani ya wiki moja.

Pia Halmashauri ambazo zilichukua mikopo kwenye mabenki hayo zimetakiwa kuwasilisha taarifa zao kwa Ofisi ya Rais-TAMISEMI ndani ya wiki moja na wote watakaokaidi watachukuliwa hatua.

Agizo hilo limetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe Selemani Jafo leo jijini Dodoma kwenye mkutano wake na wandishi wa habari huku pia akimuagiza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo kuhakikisha anafuatilia taarifa zote bila kupepesa macho.

Waziri Jafo amesema kuwa wale wote waliyochukua mikopo na hawajaanza kuitumia wairudishe haraka ipasavyo kwani Taasisi zote za Serikali zikiwemo mamlaka za Serikali za Mitaa hazitakiwi kuchukua mikopo kutoka mabenki ya kibiasha.

“Hayo ni maelekezo kutoka katika walaka wa Barua ya Katibu Mkuu Hazina barua ya tarehe 13 /12/2016 barua yenye kumbu kumbu namba CBC.155/233/01 kuwa taasisi zote za serikali na mamlaka za serikali hazipashi kuchukua mkopo kutoka benki za kibiashara” Ameeleza Mhe Jafo.

Ametoa onyo kwa Wakurugenzi wa Halmashauri zote ambazo zitawasilisha taarifa ambazo siyo sahihi au mikopo yao kutokua na sura yenye mashiko na kusema kwamba watachukuliwa hatua.

Ametoa wito kwa wakurugenzi wa halmashauri kuhakikisha wanawasilisha taarifa sahihi kulingana na mikopo waliyochukua na wasijaribu kufanya udanganyifu wowote.

" Kama ikatokea taarifa ya halmashauri ikawa ba na mashaka halafu Mkurugenzi alishaondoka bado haiwapi uhalali wa mikopo hiyo, haya ni maagizo na wanapaswa kutekeleza," Amesema Waziri Jafo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe Selemani Jafo akizungumza na wandishi wa habari kuhusiana na agizo lililotolewa kwa Wakurugenzi wa Halmashauri kuwasilisha taarifa ya mikopo waliyochukua kwenye mabenki ya kibiashara.
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Selemani Jafo akizungumza na wandishi wa habari ofisini kwake jijini Dodoma leo.

MKURUGENZI JIJI LA DODOMA AWATAKA WENYEVITI WA MITAA KUWEKA UZALENDO MBELE

$
0
0
Charles James, Michuzi TV

WENYEVITI wa Mitaa na Wajumbe wao wametakiwa kufanya kazi kwa uadilifu na uzalendo katika kuwatumikia wananchi ili kuendana na azma ya Mhe Rais Magufuli ya kuwaletea watanzania maendeleo.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dodoma na Mkurugenzi wa Jiji hilo, Godwin Kunambi wakati akizungumza na wenyeviti wa mitaa na wajumbe baada ya zoezi la kuwaapisha kufanyika.

Kunambi amesema wananchi wana changamoto na kero nyingi ambazo zinapaswa kutatuliwa hivyo ukiwa kiongozi unapaswa kushughulika na mambo ya wananchi waliokuchagua bila kujali itikadi za vyama na Dini zao.

Amesema wenyeviti wa serikali za mitaa na wajumbe ndio viongozi ambao wanakutana na wananchi na kugundua changamoto zao hivyo ni jambo la ajabu kuona mwananchi anaenda ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Wilaya au kwa Mkurugenzi ilihali mtaa una viongozi wake.

" Ndugu zangu kama anavyosemaga Mhe Rais hizi kazi za watu siyo lelemama, tumeomba wenyewe ridhaa ya kuwatumikia watanzania basi tuwatumikie kwa moyo wote na tusiweke maslahi yetu mbele.

Nafahamu kumekuepo na tabia ya wenyeviti kutaka pesa pale mwananchi anavyofika kwake kuhitaji huduma fulani, nitoe rai kwenu kuwa wazalendo na kuishi katika uongozi ambao Rais Magufuli amekua akiuishi kwa kuwa muadilifu, mchapakazi na mzalendo kwa watu wetu waliotuchagua," Amesema Kunambi.

Amewataka kwenda kufanya kazi kwa kufuata Katiba ya Nchi na miongozo ya kiutendaji ya Serikali za Mitaa lakini pia akawasihi kushirikiana na watendaji wao katika kuwaletea wananchi maendeleo na kuzifikia changamoto zao kwa wakati.

Pia amesema Jiji la Dodoma litaandaa utaratibu wa kuwafanyia semina viongozi hao ya kuwapitisha kwenye sheria, kanuni ili waweze kujua mamlaka waliyonayo.

" Tutaanzisha pia utaratibu wa kutoa zawadi nono kwa mitaa 10 bora ambayo itafanya vizuri katika nyanja mbalimbali kwenye Jiji letu, rai yangu kwenu nendeni mkafanye kazi bila kubagua na mjue wananchi wamewaamini," Amesema Kunambi.

Jumla ya wenyeviti 222 na wajumbe wa serikali za mitaa 1110 ndani ya Jiji la Dodoma wameapishwa leo baada ya uchaguzi uliofanyika Novemva 24 mwaka huu ambapo viongozi wote hao wanatokana na Chama cha Mapinduzi.
 Wenyeviti na wajumbe wa serikali za mitaa jijini Dodoma wakila kiapo cha uongozi leo tayari kwa kuanza majukumu ya kuongoza mitaa yao kwa kipindi cha miaka mitano inayokuja.
 Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi akizungumza na wenyeviti wa serikali za mitaa na wajumbe wao katika mkutano wa pamoja baada ya kuapishwa leo jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi akizungumza na wenyeviti wa mitaa 222 pamoja na wajumbe 1110 waliochaguliwa katika uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika Novemba 24 mwaka huu.

Nimemiss uchawi wa Gaucho na ‘bangi’ za Roy Keane

$
0
0
Charles James

USIKU flani wa zamani. Usiku wa Ulaya katika dimba la Stanford Bridge. Ronaldinho Gaucho alikua akiionesha Dunia maajabu yake. 

Machi 7 mwaka 2005. Chelsea ya Mropokaji Jose Mourinho walikua wakiikaribisha Barcelona ya Frank Rjikaard katika raundi ya pili ya Ligi ya Mabingwa.

Dakika ya 38 ya mchezo, Chelsea wakiwa wanaongoza 3-1 ndipo Gaucho alipotuonesha uchawi wake.Anapokea pasi kisha kwa maringo makubwa huku Ricardo Carvalho, John Terry wakimuangalia anaanza kucheza ‘sankoro’ kabla hajapasia mpira wavuni.

Licha ya Chelsea kushinda 4-2 goli lile la Gaucho linabakia kuwa miongoni mwa magoli bora ya muda wote kwenye michuano ya Ulaya.
Tusogee hapa: Zinedine Zidane Yazid, alikua bora hewani na miguuni, aliuchezea mpira alivotaka. 

Alijawa na kiburi cha miguu kilchotawaliwa na ubabe wake dimbani, Zidane aliujua mpira bwana. Ballon d'Or tatu ziko kabatini kwake.Alichowafanya wa-Brazil wedi kapu ya 1998 wanabaki kusimualiana wenyewe kwa wenyewe. 

Goli mbili za dhahabu ziliwapa ubingwa Ufaransa mbele ya wanamajinuni wa Kibrazil. Zidane alikua fundi wa ukweli.Zimeenda wapi faulo za kidigitali katika zama za Analojia kutoka kwa Samba Boy, Juninho Pernambucano?

Juninho anatajwa kuwa mkali wa mipira iliyokufa ‘free kick’ kuwahi kutokea Duniani. Leo hii mchezaji akifunga goli la faulo inakua gumzo.David Beckham kuna nyakati aliweza kupiga kona ikaenda moja kwa moja nyavuni. 

Una muda gani hujaona ajabu kama hilo? Najua utaniletea kumbukumbu ya Shiza Kichuya dhidi ya Yanga. Achana na hizo stori wewe.Shiza aliotea tu. Ukitaka kuamini ni bahati hajawahi kurudia tena. Haikua mikato yake.

Ebwana umaridadi wa Ronaldo de Lima mbele ya lango la adui umekwenda wapi siku hizi?Mbona Dunia haina tena washambuliaji wa aina yake? Tumepoteza wanaume wenye uwezo wa kufunga na miguu yote miwili na mwenye matumizi mujarabu kichwani.

De Lima hajawahi kuwa na mfanano wake, tunammiss na tunapoelekea tunapoteza watu hodari mbele ya maadui.Nani hakumbuki goli tatu za kitemi alizomtungua Fabian Barthez na Manchester United yake pale Old Trafford?

Wakati anatolewa wahuni wa Kiingereza wakasimama kumpigia makofi mtu aliewachapa tatu mzuka.Ni kitambo kirefu sijashuhudia tukio kama hilo katika ardhi ya Malkia Elizabeth. Tukio la heshima mbele ya Mshambuliaji wa kifahari.

Temana na Ronaldo. Kisanga cha Philipo ‘Pippo’ Inzaghi, Rud Van Nestorooy hakikua na mfanano wake.Mbobezi Alex Ferguson aliwahi kunukuliwa akisema “ Pippo amezaliwa kuwa mviziaji”.

Hawa ni washambuliaji waliopachikwa jina la ‘poacher’ walifunga magoli ya ajabu katika mazingira magumu ambayo wangewaacha mabeki wa Timu pinzani wakinyoosha mikono juu kuomba ‘offside’.

Dunia ya sasa haiwataki tena waviziaji, watu wanaosubiri mjisahau wawape adhabu ya kifo.Haishangazi tunapomuona Lukaku akionekana bora mbele ya mhafidhina Javier Hernandez Chicharito.

Makocha wengi wanapenda washambuliaji viungo, Bobby Firmino anamfanya Klopp asifikirie kusajili namba Tisa  pale Liverpool. Maajabu haya.

Ghafla nimezikumbuka bangi za waapolo Roy Keane na Patrick Vieira. Dunia ilisimama kila Man U walipovaana na Arsenal.Ubabe ulitamalaki katikati, ngumi, karate na Judo zilihusika, viatu vilichapwa kisawa-sawa. 

Leo hii pale Arsenal kuna Mateo Gundeouzi, United kuna Fred hakuna hata ishu. Soka limeenda wapi jameni?Gennaro Gattuso angeweza kumchapa mtu vibao uwanjani bila sababu yoyote. Ubabe tu ubayani ubayani. Mambo mbaya.

Kulikua na refa anaitwa Corina huyu alikua mbabe wa watukutu kama Keane na Gattuso.Sura yake mpalazo, macho yake ya Paka na kipara chake kichwani viliwatisha hata wale wachezaji waliojiona wababe.

Eti Martin Athkson leo ndo tunamuona bora na wa mechi ngumu. Futbol imepoteza mvuto.Diego Maradon alikua bora sana, kijitu kifupi hivi, chenye nguvu kuanzia juu hadi chini. Mfalme wa chenga za maudhi haswa.

Goli lake la mkono dhidi ya Waingereza mwaka 1986 linabaki katika historia ya Dunia. Siyo refa wala lezman ambaye aliona Diego ameshika ule mpira. Ladha ya soka ilionekana. Ule ubishi wa alishika au hakushika ulikuepo.

Leo tuna ‘goal technology na VAR, hakuna mikwaruzano ya vibandani ‘lile siyo goli, ni goli mara aliotea yule’. Soka limekua la kisayansi sana. Inatukera sisi.

Hebu nambieni hamjamiss Higuanita? Yule Golikipa ambaye angeruka sarakasi kabla hajadaka mpira. Kipindi flani Juma Kaseja alifanya hii michezo.

Upiganaji wa kutokata tamaa kutoka kwa Liverpool je? Hawa jamaa ungewafunga tatu bila lakini bado wangepambana kuhakikisha wanarudisha magoli yote.

Fainali yao ya UEFA na AC Milan 2005 na ile ya FA na West Ham 2006 zinabaki kuwa kielelezo chao angalau mchezo wa pili wa nusu fainali dhidi ya Barcelona kwenye Ligi ya Mabingwa msimu ulioisha walitukumbusha sifa yao.

Wapi mchuano wa kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa Dunia? Eti siku hizi ni rahisi kutabiri kwamba asipobeba Lionel Messi atatwaa Cristiano Ronaldo, huyu Modric kaokota dodo tu.

Miaka 10 wanapokezana wenyewe kwa wenyewe. Fikiria wakati Luis Figo anashinda mwaka 2000 Ballon d'Or washindani wake walikua Zidane, Raul Gonzalez.

Pavel Nedved anashinda 2003 akiwapiku akina Lampard, Gaucho. Ushindani ulikuepo bwana.Messi na Ronaldo unafikiri wangeshinda vipi mfululizo kama wangekutana na akina Nesta, Gattuso, Keane au Hierro dimbani?

Wangeshinda vipi mara tano mfululizo mbele ya uchawi wa Gaucho, De Lima, Nedved au Thienry Henry?

Wanangu wa Chelsea mnaangaika baada ya Eden Hazard kuondoka hamjamiss ile Zola Zone ya Giafranco Zola? Wenyewe wataliano waliita Traquartista.

Bwana ee nyakati zime-expire soka limebadilika ladha haipo kama zamani sasa kuna biashara tu.

Ngoja nikalale napoona nafasi ya Rashid Yekin anacheza Iwobi pale Nigeria, siyaoni matege ya Mohammed Aboutrika kule Misri.

Kwamba Afrika imeshindwa kuzalisha George Weah mwingine wa kuwapa homa Wazungu? Ujuha huu. Afrika haina Jay Jay Okocha tena. Tumebaki kujisifia na Pierre Aubameyang.

Uko wapi Ukompyuta wa Sunday Manara katika ubongo wa Ibrahim Ajib Migomba? ‘Football is Dead’

0683 015145

RIDHIWANI ATAFUNA MFUPA ULIOWASHINDA WENGI.

$
0
0
Na Shushu Joel.

MBUNGE wa jimbo la chalinze Ridhiwani Kikwete amefanikiwa kuwapa heshima ya uhakika wa kufanikiwa kwa wananchi wa jimbo lake.

Mfupa huo uliwashinda watangulizi wake katika jimbo hilo ni kufanikiwa kwa kupata kwa hati miliki za maeneo kwa baadhi ya wanachalinze mara baada ya kutoa elimu ya kutosha kwa wananchi hao. 

Akizungumza na wananchi wakati wa makabidhiano ya hati kwa wale waliokamilishi kulipia hati hizo Kikwete alisema kuwa hati ni muhimu sana kuwa nayo kwani mbali na kukopesheka unakuwa umepandisha thamani ya kiwanja chako. 

"Nimefurahishwa sana kwa kitendo cha wananchi wangu kupata hati za viwanja vyao kwani huu ni mwanzo wa mafanikio katika maisha yao"Alisema Kikwete.

Aidha ameipongeza kamati ya watu 12 iliyoundwa kwa ajili ya kuhamasisha wananchi waweze kujitokeza kupimiwa maeneo yao ili yaweze kupanda thamani ya ardhi."Nimefanikiwa kukabidhi hati 48 kwa wananchi ķati 100 waliolipia hivyo ni wakati wa kuchangamkia fursa hii ili kuondokana na kuwa na maeneo ambayo hayajapimwa"

Aluongeza kuwa katika kata ya Bwilingu mpaka sasa viwanja 10000 vimepimwa na wananchi wapo kwenye mchakato wa malipo ili nao waweze kupatiwa hati.Hivyo sasa chalinze itaingia kwenye moja ya halmashauri zitakazoongezea kipato serikali kupitia kodi za ardhi.

Pia ametoa wito kwa wananchi wake kuendelea kujitokeza ili waweze kupimiwa maeneo yao.Naye mwenyekiti wa kamati ya ufuatiliaji na hamasa kwa wananchi Shamba Msakamali amempongeza mbunge kwa ushirikiano wake wa dhati katika kuhamasisha wananchi ili wajitokeze kwenye zoezi.

Msakamali aliongeza kuwa msaada uliotolewa na mbunge Kikwete ni mkubwa na wenye tija kwa wanakamati.Kwa upande mwanana Ally ambaye ni miongoni mwa wale waliokabidhiwa hati alisela kuwa watu wamekuwa wakikata tamaa juu ya mwenendo wa awali kwa ajili ya upatikanaji wa hati.

Hivyo amewataka wananchi kujitokeza ili nao waweze kupata hati zao kama wengin nye.


AGAPE YAENDESHA KIKAO KUJADILI KUTENGENEZA MUONGOZO WA KUPAMBANA NA UKATILI SOKONI SHINYANGA

$
0
0
Shirika lisilo la kiserikali Agape Aids Control Programme limeendesha kikao cha kujadili namna ya kutengeneza muongozo ambao utatumika kwenye masoko ya Shinyanga Mjini, kwa ajili ya kuzuia na kupambana na ukatili wa kijinsia kwenye Masoko.

Kikao hicho kimefanyika leo Novemba 28, 2019, kwenye ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Liga, ambacho kimeshirikisha viongozi wa masoko sita ya Shinyanga mjini, maofisa ustawi, maendeleo ya jamii, wanasheria, dawati la jinsia, pamoja na wajumbe wa kutokomeza ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto Mtakuwwa. Akizungumza wakati wa kufungua kikao hicho, Mwansheria kutoka Shirika la Agape Felix Ngaiza, akimwakilisha mkurugenzi wa Shirika hilo John Myola, amesema, utengenezaji wa muongozo huo wa kuzuia na kupambana na ukatili kwenye masoko, utasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza matukio ya ukatili wa kijinsia masokoni. Amesema Shirika hilo limekuwa likitekeleza mradi wa kupambana na matukio ya ukatili wa kijinisa sokoni, uitwao Mpe Riziki Si Matusi, ambapo sasa wameamua watengeneze muongozo ambao utatumika kuzuia na kupambana na matukio hayo ya ukatili wa kijinsia sokoni, ili pawe mahali salama pa kufanyia biashara. 

“Muongozo huu ni muhimu sana ambao utasaidia kuzuia na kupambana na matukio ya ukatili wa kijinsia masokoni, na ndio maana leo tumeamua kufanya kikao na viongozi wa masoko, maofisa ustawi jamii, maendeleo, dawati la jinsia, wanasheria, na wajumbe wa Mtakuwwa, ili tupate kuutengeneza na kuanza kutumika,”amesema Ngaiza. Aidha amesema muongozo huo wa kuzuia na kupambana na ukatili wa kijinsia kwenye Masoko, utakuwa ukitoa faini na adhabu mbalimbali kwa watu ambao watakuwa wakifanya matukio hayo ya ukatili kwenye masoko. 

Naye Afisa mradi wa kutokomeza ukatili sokoni wa ‘Mpe Riziki Si Matusi’ Helena Daudi, amesema mradi huo umeanza kutekelezwa tangu mwaka Novemba 2018 ambao unakoma mwaka huu 2019, ambapo mpaka sasa wamefanikiwa kupunguza ukatili huo kwa kiwango kikubwa. Amesema mradi huo unafadhiliwa na Shirika la UN WOMEN kupitia shirika la Equality for Growth (EFG), ambao umedhamiria kutokomeza ukatili kwenye masoko sita ya manispaa ya Shinyanga dhidi ya wanawake na wasichana, ambayo ni Kambarage, Soko kuu, Nguzonane, Ngokolo, Majengo mapya, na Ibinzamata. Nao baadhi ya wenyeviti wa masoko akiwemo Alex Stephen kutoka soko kuu la Shinyanga, wamebainisha matukio ya ukatili ambayo yamekuwa yakitendeka ikiwamo kutolewa kwa lugha chafu za matusi ya nguoni, kushikwa maumbile kwa wanawake bila ya ridhaa yao, kutakwa kimapenzi kwa nguvu, kudhulumiwa pamoja na vipigo. TAZAMA PICHA HAPA CHINI Mwanasheria wa Shirila la Agape Felix Ngaiza akizungumza wakati wa kufungua kikao cha kujadili namna ya kutengeneza muongozo wa kuzuia na kupambana na ukatili wa kijinsia sokoni. Picha zote na Marco Maduhu - Malunde 1 blog Afisa mradi wa kutokomeza ukatili sokoni wa ‘Mpe Riziki Si Matusi’ kutoka Shirika la Agape Helena Daudi, akielezea umuhimu wa masoko kuwa na muongozo huo wa kuzuia na kupambana na ukatili wa kijinsia sokoni, ambapo utasaidia kutokomeza ukatili huo. Mwanasheria kutoka Shirika la Agape Emmanuel Nyalada akiwasilisha mada kuhusu muongozo wa kuzuia na kupambana na ukatili kijinsia sokoni. Meneja miradi kutoka Shirika la Agape Peter Amani, akizungumza kwenye kikao hicho. Mwanasheria wa manispaa ya Shinyanga Mushi Josephat akieleza kuwa muongozo huo wa kuzuia na kupambana na ukatili wa kijinsia sokoni utasaidia kumalizana kesi wao kwa wao zinazohusu ukatili, kuliko kupelekana kwenye vyombo vya Sheria ambapo matukio yote ya ukatili ni Makosa ya Jinai. Wajumbe wakiwa kwenye kikao cha kujadili utengenezaji wa muongozo ambao utasaidia kuzuia na kupambana na matukio ya ukatili wa kijinsia sokoni. Wajumbe wakiwa kwenye kikao cha kujadili utengenezaji wa muongozo ambao utasaidia kuzuia na kupambana na matukio ya ukatili wa kijinsia masokoni. Wajumbe wakiwa kwenye kikao cha kujadiri utengenezaji wa muongozo ambao utasaidia kuzuia na kupambana na matukio ya ukatili wa kijinsia masokoni. Wajumbe wakiendelea na kikao. Wajumbe wakiendelea na kikao. Wajumbe wakiendelea na kikao. Mwenyekiti wa Soko kuu la Shinyanga Alex Stephen akichangia mada kwenye kikao hicho. Mhasibu wa Soko la Ibinzamata Juliana Francis akichangia mada kwenye kikao hicho. Msaidizi wa kisheria kutoka Soko kuu la Shinyanga Zera Semuguruka, akichangia mada kwenye kikao hicho. Mwakilishi wa Soko la Nguzo Nane Hilda Athanas, akichangia mada kwenye kikao. Mchungaji wa kanisa la KKKT Makedonia Harold Mkaro, ambaye pia ni mjumbe wa MTAKUWWA, akichangia mada kwenye kikao. Wajumbe wakiwa kwenye kazi ya makundi. Wajumbe wakiwa kwenye kazi ya makundi. Wajumbe wakiwa kwenye kazi ya makundi. Mwenyekiti wa Soko la Kambarage Seif Mtete akiwasilisha kazi ya kikundi. Wajumbe wakiendelea kuwasilisha kazi ya kikundi. Wajumbe wakiwasilisha kazi ya kikundi. Picha zote na Marco Maduhu- Malunde 1 Blog

MBUNGE BALOZI ADADI AISHUKURU SERIKALI KUWEKA LAMI MJI WA MUHEZA

$
0
0
MBUNGE wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu akizungumza wakati wa halfa ya utiliaji saini  ya kati ya Halmashauri ya Muheza na Mkandarasi wa Kampuni ya ujenzi ya SIMAC Limited kutoka Dar kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara za mita 800 kwenye mji huo kwa kiwango cha lami kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Muheza Nassib Mbaga na kushoto ni Meneja wa Tarura wilaya hiyo Mhandisi Joseph Kahoza
 Mkurugenzi wa Halmashauri ya Muheza Nassib Mbaga akizungumza wakati wa halfa hiyo kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu kulia ni Katibu  wa CCM wilaya ya Muheza Mohamed Moyo 
 Meneja wa Tarura wilaya hiyo Mhandisi Joseph Kahoza akizungumza wakati wa halfa hiyo kulia ni Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajab
 MBUNGE wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu akimkabidhi nyaraka na michoro mkandarasi wa kampuni ya ujenzi SIMAC LTD kutoka Dar Felix Chawe mara baada ya kusaini nae mkataba kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara za mita 800 katika mji wa Muheza

 MBUNGE wa Jimbo la Muheza kushoto Balozi Adadi Rajabu (aliyevaa suti) akisisitiza jambo kwa mkandarasi wa ujenzi huo mara baada ya kutembelea eneo ambalo ujenzi huo utafanyika 
 MBUNGE wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu kushoto akimsikiliza Katibu wa CCM wilaya ya Muheza Mohamed Moyo kulia wakati walipotembelea barabara ya sokoni wilayani humo 



MBUNGE wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu ameishukuru serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt John Magufuli kuwasaidia kuweka lami baadhi ya barabara zilizopo kwenye mji huo.

Huku akiwataka wananchi wilayani humo kumpa ushirikiano mkandarasi ambaye anatekeleza ujenzi huo ili aweze kutekeleza kazi yake kwa wakati kutokana na kwamba amepewa muda wa miezi saba. 



Balozi Adadi aliyasema hayo wakati wa halfa ya utiaji wa saini kati ya kati ya Halmashauri ya Muheza na Mkandarasi wa Kampuni ya ujenzi ya SIMAC Limited kutoka Dar kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara za mita 800 kwenye mji huo. 



Alisema kwamba utiliaji saini huo umeonyesha namna serikali ya awamu ya tano imedhamiria kuhakikisha inaboresha miundombinu kwenye miji mbalimbali hapa nchini.

Mbunge huyo alisema kwamba barabara ni kilomita ya pili ambayo itaanzia Kilimanjaro Bar, Darajani, relini mpaka hospitali ya Teule Muheza na baadae kufika mpaka kwenye kipande ambacho kinatumika na wananchi kwenye maeneo ya karibu na soko la Muheza.

“Serikali ya awamu ya tano imeweza kutusaidia kuweka lami ni jambo kubwa na la faraja kubwa kwetu hivyo kwa sababu lami itawekwa kwenye mji wetu hakikisheni mnapa ushirikiano na niwaombe msimpe vikwazo vya namna yoyote ile “Alisema Balozi Adadi. 



Awali akizungumza wakati wa halfa hiyo Meneja wa Tarura wilaya ya Muheza Mhandisi Joseph Kahoza alisema kwamba mkandarsi aliyekabidhi mkataba huo ni wa barabara za mita 800 kwa ajili ya kuweka lami kwa mji wa muheza.

Alisema mkandarasi huyo ataanza kufanya kazi hiyo kuanzia barabara ya Kilimanjaro darajani, relini mpaka teule ambao utakuwa na thamani ya milioni 386 huku akieleza barabara nyengine ya mita 200 zinazokarabatiwa mjini humo zitatumia zaidi ya milioni 60..

Naye kwa upande wake Mkandarasi wa kampuni ya ujenzi SIMAC LTD kutoka Dar Felix Chawe ambao wamekabidhiwa barabara hiyo alisema kwamba anajisikia furaha kupata nafasi ya ujenzi huo huku akihitaji ushirikiano na kuhaidia kufanya kazi kwa uwezo wake wote na maelekezo yaliyopo kwenye mkataba.

SBL yashauri mfumo wa pamoja wa kodi kwa nchi za Afrika Mashariki kuharakishwa

$
0
0

· Asema utofauti wa kodi za ndani unasababisha kuongezeka bidhaa bandia za pombe

 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) Mark Ocitti, ameshauri kuharakishwa kwa utaratibu wa kuoanisha mfumo wa kodi kwa nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

Ocitti amesema, pamoja na kwamba hatua nzuri na kubwa imefikiwa, vikwazo vya kibiashara vilivyopo havina budi kushughulikiwa ili kuongeza kasi ya uwekezaji pamoja na kurahisisha biashara ya bidhaa na huduma miongoni mwa nchi wanachama

Akizungumza katika mkutano wa Biashara na Uwekezaji wa Wakuu wa Nchi za EAC uliofanyika jijini Arusha, Ocitti alisema tafsiri tofauti za vipengele vya kisheria kama ‘bidhaa za nje’ imesabisha kuwepo kwa kodi kubwa kwa bidhaa zinazotoka ndani ya nchi wanachama jambo ambalo limepunguza kasi ya ukuaji wa biashara.

“Utekelezaji wa kuoanisha mfumo wa kodi miongoni mwa nchi wanachama umekuwa hauendi vizuri sana kwa sababu mbali mbali ikiwamo utofauti ya kiuchumi pamoja na kufikiria suala la mapato, viwanda vya ndani, ushindani na nyinginezo,’ alisema

Akizungumzia athari zake kwenye sekta ya uzalishaji wa bia, alisema utofauti wa kodi za ndani miongoni mwa nchi wanachama, umesababisha kuongezeka kwa pombe haramu na kuongeza kuwa bado kuna changamoto katika utekelezaji wa kanuni itayoweka mfumo wa kodi unaofanana kutokana na utofauti wa maendeleo ya kiuchumi na pia hakuna msukumo wa kisheria unatoa msisitizo kwa jambo hilo.

“Kasi ndogo ya upitiaji wa Itifaki ya Ushuru wa Forodha kwa nchi wanachama wa EAC unaathiri baadhi ya shughuli pamoja na kuzifanya bajeti za nchi hizi kutegemea kwa kiasi kikubwa ushuru wa forodha. Hata hivyo, kuanzia mwaka 218 kumekuwa na mfumo mzuri kati ya nchi wanachama kwa kukuliana muundo wa 0%, 10%, 25% na 35.

Akizungumzia namna kampuni ya Bia ya Afrika Mashariki (EABL) ambayo ni kampuni mama ya SBL ilivyoathirika alisema imekuwa ni bahati nzuri kuwa makampuni yaliyo chini ya EABL yamesajiliwa kama makapuni ya ndani kwa nchi wanachama na hivyo hayajaathirika sana kwa kuwa bidhaa zake zinazalishwa ndani ya nchi hizo.

“Hata hivyo, uwekaji wa viwango vya pamoja kwa bidhaa ambazo zipo tayari kwa ajili ya kutumika (RTD) imeleta shida kwa mfano kwenye biashara ya bidhaa hizo zinazotoka Kenya kuja Tanzania,” alisema

 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni Bia ya Serengeti Mark Ocitti (wa pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watoa mada na wachangiaji muda mfupi baada ya kumalizika kwa mkutano wa Baraza la Biashara la Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika jijini Arusha leo.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni Bia ya Serengeti Mark Ocitti akizungumza wakati wa mkutano wa Baraza la Biashara la Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika jijini Arusha leo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni Bia ya Serengeti Mark Ocitti (wa pili kulia) akizungumza wakati wa mkutano wa Baraza la Biashara la Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika jijini Arusha leo. Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Ushuru na Biashara wa Sekretariati ya EAC Kenneth Bagamuhunda akifuatiwa na Meneja wa kanda wa Coca cola  na wa kwanza kulia ni David Tarimo kutoka kampuni PWC.

NCHI SITA KUSHIRIKI MASHINDANO YA GOFU YA TANZANIA OPEN 2019 ARUSHA

$
0
0

Wachezaji wa Gofu 150 wakiwemo kutoka Kenya,Uganda, Malawi, Zambia ,Burundi na Rwanda na Wenyeji Tanzania wanatarajia kuingia Viwanjani katika Mashindano ya Taifa ya Mchezo wa Gofu ya Tanzania Open Mwaka 2019 yanayotarajiwa kuanza kutimua vumbi kesho (leo) katika Uwanja wa Kili Jijini Arusha.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Mwenyekiti wa Chama cha Gofu Tanzania TGU Criss Martin alisema ri maandalizi yote yamekamilika na kinachosubiriwa ni kuanza kwa mashindano na zawadi Nono ikiwemo ya gari itatolewa.

“ Tuna Zawadi nono na kubwa Zaidi ni Gari aina ya rav 4 ambayo itakwenda kwa Mchezaji atakayefanikiwa kupiga mpira mmoja na kuingiza Shimoni Hole in One” alisema Martin.

Aliongeza kuwa wachezaji wa kulipwa ndio watakaoanza sambamba na Kundi A na kufuatiwa na kundi B na Mashindano yanatarajiwa kumalizika Jumapili .

Pia alisema mashindano haya hayahusishi Wanawake wala Watoto na makundi ni A na B ambao ndio wanakidhi ushiriki wa Mashindano hayo huku wachezaji wa kulipwa wakoiwa kama wanogeshaji.

Kwa upande wake Mwanakamati wa mashindano hayo Kapteni Japhet Masai alisema Mashindano haya ni ya Gross Mikwaju ya Jumla kwa kujumlisha siku zote.

Aliongeza pia kuwa Sheria zitatumika za Kitaifa ambazo zimeainishwa katika karatasi ya kuandikia matokeo sambamba na sheria za Kimataifa.

Klabu za Tanzania zinazoshiriki mashindano haya yaliyodhaminiwa na Oryx, Super Doll, Garda word, Coca Cola, Tanfoam na Serengeti ni Lugalo Gofu Klabu na Dar es Salaam Gymkhana zote za Dar es Salaam, Morogoro Gymkhana, Arusha Gymkhana, Mufindi na Zanzibar sea Cliff na am.

CHAMA CHA WAAJIRI ATE: KUJISAJILI WCF NI LAZIMA SIO HIARI

$
0
0

NA K-VIS BLOG/Khalfan Said

MKURUGENZI Mtendaji wa Chama Cha Waajiri Tanzania (ATE), Dkt. Aggrey Mlimuka amewaambia waajiri nchini kuwa kujisajili na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi sio hiari bali ni lazima.

Dkt. Mlimuka ameyasema hayo Alhamisi Novemba 28, 2019 jijini Dar es Salaam wakati akifungua mafunzo ya siku moja yaliyoandaliwa na ATE na kuwaleta pamoja waajiri kutoka sehemu mbalimbali nchini ili kujifunza kuhusu masuala ya Fidia kwa Wafanyakazi.

“Naomba tuelewane toka mapema, siyo hiari kujiunga na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi hilo ni takwa la kisheria Mfuko huu uko pale kisheria na ni vema likaeleweka mapema.”Alisema Dkt. Mlimuka

Alisema Chama Cha Waajiri Tanzania (ATE) kiko kwa maslahi ya waajiri lakini pia kwa maslahi ya waajiriwa (wafanyakazi) kwani wameajiriwa ili kufanya shughuli mbalimbali na wanaweza kuumia au kupatwa na madhara yoyote wakati wakitekeleza majukumu yao na ndio maana upo Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi ambao umeundwa maalum kushughulikia masuala hayo.

“Niwashukuru sana viongozi wa WCF kwa kuja hapa leo kutupatia mafunzo, sisi waajiri tutanufaika vya kutosha na mafunzo haya ambayo yataweza kujibu maswali yaliyo mengi kutokana na changamoto mbalimbali.” Alibainisha Dkt. Mlimuka.

Alisema,hapo zamani malipo ya Fidia kwa Mfanyakazi aliyeumia yalikuwa kidogo sana, na ndio maana Serikali ikaanzisha Mfuko huu ambao umesaidia sana katika kutatua changamoto zilizokuwa zikitukabili kutokana na masuala ya Fidia.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Tathmini, Dkt. Abdulsalaam Omary alisema, Waajiri wanao wajibu wa kuhakikisha usalama wa wafanyakazi wao unapewa umuhimu wa kwanza na ndio maana WCF inatoa elimu mara kwa mara.

“Ifahamike kuwa sisi WCF wajibu wetu wa msingi ni kulipa fidia stahiki na kwa wakati kwa mfanyakzi aliyeumia, kuugua au kufariki wakati akitekeleza wajibu wake wa kazi… kusajili na kupokea michango kutoka kwa waajiri walio katika sekta ya umma na binafsi Tanzania Bara, lakini pia tunalo jukumu la kisheria la kukuza mbinu za kuzuia ajali na vifo kazini kwa kutoa elimu kwa waajiri lakini pia wafanyakazi wenyewe na hiki ndicho tunachokifanya hapa leo.” Alisema Dkt. Omary wakati akiwasilisha mada yake ya namna ya kudai Fidia.

Washiriki hao walipatiwa mafunzo mbalimbali yakiwemo Sheria iliyoanzisha Mfuko, Kujisajili na jinsi ya kuwasilisha michango WCF na namna ya kuwasilisha madai ya Fidia, lakini pia Mafao yanayotolewa na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Chama Cha Waajiri Tanzania (ATE), Dkt. Aggrey Mlimuka, akitoa hotuba ya ufunguzi wa mafunzo kuusu masuala ya Fidia kwa Wafanyakazi yaliyotolewa kwa Waajiri kutoka sehemu mbalimbali nchini na kufanyika jijini Dar es Salaam Novemba 28, 2019.
Mkurugenzi Mtendaji wa Chama Cha Waajiri Tanzania (ATE), Dkt. Aggrey Mlimuka (kushoto), akisalimiana na Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Tathmini, Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dkt. Abdulsalaam Omary, mara baada ya kutoa hotuba. 
Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Tathmini, Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dkt. Abdulsalaam Omary, akizungumza mwanzoni mwa mafunzo ya siku moja kuhusu masuala ya Fidia kwa Wafanyakazi kwa wanachama wa Chama Cha Waajiri Tanzania (ATE) jijini Dar es Salaam Novemba 28, 2019. 
Bw, Deo Ngowi kutoka kitengo cha Sheria Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), akiwasilisha mada kuhusu Sheria iliyoanzisha Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi.
Bw.Pascal Rischard kutoka Kitengo cha Usajili na Uwasilishaji Michango WCF, akiwasilisha mada kuhusu namna ya kujisajili na kuwasilisha michango kupitia Portal ya WCF
Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Tathmini, Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dkt. Abdulsalaam Omary, 
Meneja Madai Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Bi. Rehema Kabongo, akiwasilisha mada kuhusu Mafao yatolewayo na WCF.
Baadhi ya washiriki w asemina wakifuatilia mafunzo hayo.
Baadhi ya washiriki w asemina wakifuatilia mafunzo hayo.
Baadhi ya washiriki w asemina wakifuatilia mafunzo hayo.
Maafisa wa juu wa WCF, kutoka kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano, Bi. Laura Kunenge, Bw. Deo Ngowi kutoka Kitengo cha Sheria na Bw. Pascal Richard kutoka Kitengo cha Usajili na Uwasilishaji Michango WCF
Baadhi ya washiriki w asemina wakifuatilia mafunzo hayo.

PWANI YAFANYA MNADA WA KWANZA WA KOROSHO NA KUUZA KILO 156,257-NDIKILO

$
0
0

NA MWAMVUA MWINYI,MKURANGA

Mkoa wa Pwani wa Pwani, umefanya mnada wa kwanza wa korosho kwa mfumo wa stakabadhi ghalani na kufanikiwa kuuza korosho yote iliyokuwa katika maghala makuu, kilo 156,257 kwa daraja la kwanza na la pili. 

Aidha baadhi ya waendesha maghala wamekewa kuacha kupokea cha juu kwa viongozi wachache wa AMCOS ambao sio waaminifu ,wakitaka wapokee korosho zisizo na viwango ama kupewa stakabadhi za ghala wakati hakuna korosho zilizopelekwa kwenye maghala yao.

Akizindua mnada huo huko Mkuranga ,mkuu wa mkoa wa Pwani, mhandisi Evarist Ndikilo alisema, daraja la kwanza limeuzwa kwa bei ya sh.2,571 ambapo korosho hizo zimenunuliwa na kampuni ya Alpha Choice.

Alieleza, daraja la pili limenunuliwa kwa bei sh.2,300 na korosho hizo zimenunuliwa na kampuni ya CDJKL.Hata hivyo, Ndikilo aliwataka wakulima kukausha korosho zao ili ziwe kavu na zenye ubora na wakati wa msimu wa kilimo kupalilia na kufufua mikorosho ya zamani ili kujiongezea kipato.

Ndikilo hakusita kubainisha kwamba ,licha ya juhudi zote hizo mapokezi ya hali ya korosho kwenyw maghala hairidhishi hivyo ukusanyaji uongezeke ili kufanya mnada wa pili na mingine yenye mafanikio kwa wakulima.

"Lindi imeshafika mnada wa saba,sisi ndio tumeanza ,tusifanye mchezo katika masuala ya uchumi ama lenye manufaa kwetu kama hili"alisisitiza .Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Rufiji, Juma Njwayo alisema wilaya hiyo ina korosho kilo 107,592 na ubora ni STD na UG na uhakiki unaendelea.

Nae mrajisi wa mkoa wa Pwani, Angela Nalimi aliweka bayana kuwa, mkoa unapendekeza korosho zenye ubora stahili zitaendelea kupokelewa kwenye maghala makuu.

Alisema korosho nyingi pia bado zipo katika maghala ya AMCOS ambapo yatasimamiwa na kuratibiwa na chama kikuu (CORECU).Angela alieleza ,halmashauri kupitia ofisi za ushirika zitasimamia malipo ya wakulima wote waliokusanya korosho kupitia AMCOS.

Viewing all 110186 articles
Browse latest View live




Latest Images