Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110170 articles
Browse latest View live

KORTI YAUTAKA UPANDE WA SERIKALI KUWASILISHA KIAPO KINZANI AGOSTI 5 MWAKA HUU KUJIBU HOJA KUKAMATWA MWANDISHI ERICK KABENDERA

$
0
0
Na Karama Kenyunko, Michuzi TV

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imeutaka upande wa Serikali kuwasilisha kiapo kinzani mahakamani hapo Augusti 5, mwaka 2019 kujibu hoja kuhusu kukamatwa kwa mwandishi wa habari za uchunguzi, Erick Kabendera.

Hakimu Mkazi Mkuu, Augustine Rwizile ametoa maagizo hayo leo Agosti Mosi, 2019 baada ya Wakili kutoka Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC), Shilinde Swedy kuwasilisha maombi ya kutaka Kabendera afikishwe mahakamani kwa sababu Jeshi la Polisi linamshikilia tangu Julai 29, 2019 hadi leo.

Katika maombi hayo namba 14 ya mwaka 2019 yaliyofunguliwa Julai 30, wakili huyo amedai kuwa hadi sasa saa 24 zimeshapita, hivyo anapaswa kufikishwa mahakamani dhidi ya tuhuma zozote zinazomkabili kwa ajili ya haki zake za msingi ikiwemo dhamana kwani kosa lake linadhaminika.

Akijibu hoja hizo, Wakili wa Serikali Mwandamizi Wankyo Simon ameiomba Mahakama iwape muda mpaka August 7 mwaka 2019 kwa ajili ya kuwasilisha kiapo kinzani katika maombi hayo, lakini upande wa utetezi ulipinga na kuomba wafanye hivyo, Agosti 2, mwaka 2019.

Hata hivyo baada ya mabishano na kusikiliza hoja za pande zote mbili mahakama imeamuru majibu hayo yaletwe Agosti 5,mwaka 2019 saa saba mchana.Hakimu Rwizile ameutaka upande wa Serikali kuwasilisha kiapo kinzani Agosti 5, mwaka 2019.
 Wakili kutoka kituo cha utetezi wa haki za binadamu, THRDC,  Shilinde Swedy akizungumza na wanahabari nje Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu juu ya kilichojiri mahakamani hapo kufuatia maombi  dhidi ya kushikiliwa kwa mwandishi wa Habari za uchunguzi Erick Kabendera.
 
Wakili kutoka kituo cha utetezi wa haki za binadamu, THRDC,  Shilinde Swedy akijadili jambo na wakili wa kujitegemea Gebra Kambore Mahakamani hapo.

NEWS ALERT:MSANII WA BONGOFLEVA NA DIWANI KATA YA MWANGA KASKAZINI AHUKUMIWA MIEZI 5 JELA

$
0
0
Na Editha Karlo wa michuzi tv Kigoma .

 Msanii wa Bongo Fleva na Diwani wa kata ya Mwanga kaskazini kupitia cha cha ACT Wazalendo katika Manispaa ya Kigoma Ujiji,Revocatus Kipando maarufu kama Baba Levo amehukumiwa leo kifungo cha miezi mitano kwa kosa la kumshambulia Askari wa Usalama Barabarani wakati akitimiza majukumu yake ya kazi. 

Akisoma hukumu hiyo Hakimu Frolence Ikorongo wa mahakama ya Mwanzo mwandiga alisema mshtakiwa amekutwa na kosa katika kesi iliyo kuwa inamkabili hivyo mahakama inampa adhabu ya kutumikia kifungo cha miezi mitano jela. Baba Levo alikuwa na kesi ya kumshambulia askari wa barabarani wakati akiwa kwenye majukumu yake ya kazi. 

Tukio la kumshambulia askari lilitokea July 15 majira ya saa moja usiku katika eneo la kwabela ambapo baba Levo alimshambulia askari wa barabarani anayefahamika kwa jina la Msafiri Ponera wakati akiwa kwenye eneo lake la kazi. 

Inadaiwa kuwa mtuhumiwa alilazimisha kupita kwa pikipiki eneo la watembea kwa miguu wakati askari huyo ameshawaruhusu watembea kwa miguu kuvuka,baada ya hapo baba levo alimua kumshambulia askari huyo. Diwani wa kata ya Kigoma mjini kupitia chama cha ACT Wazalendo Hussein Kaliyango amesema kuwa tayari wameshaanza mchakato wa kukata rufaa ili haki ya baba Levo ipatikane.

 "Tunashukuru maamuzi ya mahakama tunakata rufaa leo hii tunaingiza rufaa tunaamini haki ya Baba levo itapatikana, Niwatoe hofu wananchi wa kata ya mwanga kaskazini kuwa tunakata rufaa tunaimani mahakama itatenda haki"alisema Diwani huyo Alisema Baba levo ni mtetezi wa Bodaboda,Bajaji na wanyonge wajasiliamali katika Manispaa ya Kigoma amewapambania vya kutosha leo amepatikana na hatia kwa nia ya kuwatetea wananchi wa mji mzima ndio alivyozaliwa baba levo hii ndio safari ya kuwa mwanasiasa mkubwa nchini.
Msanii wa Bongo Fleva na Diwani wa kata ya mwanga kaskazini kupitia chama cha ACT Wazalendo Revocatus Kipando maarufu Baba Levo akitoka mahakama ya mwanzo ya Mwandiga baada ya kuhukumiwa kifungo cha miezi mitano jela kwa kosa la kumshambulia askari wa usalama barabarani akiwa kazini.

MASAUNI AKAGUA UANDIKISHWAJI VITAMBULISHO VYA TAIFA NA UTOLEWAJI WA PASI ZA KUSAFIRIA ZANZIBAR

$
0
0
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akizungumza na wananchi waliofika Makao Makuu ya Uhamiaji Visiwani Zanzibar leo kupata pasi za kusafiria za kielektroniki, wapili kulia ni Kamishna wa Uhamiaji Johari Suluhu.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) Zanzibar, Hassan Hassan ,akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (wapili kulia),alipofika ofisi za mamlaka hiyo leo kukagua zoezi la utolewaji vitambulisho kwa wananchi.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Mkazi wa Unguja Salma Ali, akizungumza wakati wa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (hayupo pichani), alivyofika Ofisi za Uhamiaji Zanzibar leo kukagua zoezi la utolewaji wa pasi za kusafiria za kielektroniki linavyoendelea.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Mkazi wa Unguja Salim Hassan Makame, akizungumza wakati wa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni(hayupo pichani), alivyofika Ofisi za Uhamiaji Zanzibar leo kukagua zoezi la utolewaji wa pasi za kusafiria za kielektroniki linavyoendelea.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

*************

Na Mwandishi Wetu

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhandisi Hamad Masauni amewataka watumishi wa Idara ya Uhamiaji na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa(NIDA) kuwahudumia wananchi walioiweka serikali madarakani ili kuepuka baadhi ya mbinu zinazotumiwa na watu wasio na nia njema kuvuruga amani ya nchi.

Ameyasema hayo Makao Makuu ya Uhamiaji Zanzibar baada ya kukagua zoezi la utolewaji vitambulisho vya taifa na ubadilishaji wa pasi za zamani za kusafiria baada ya kupokea malalamiko mbalimbali kutoka kwa wananchi waliofika katika ofisi hizo

“Kuna sauti zinatembea katika mitandao ya kijamii zikieleza ubaguzi unaofanyika katika kutoa pasi na vitambulisho, bado siamini kama kweli watumishi wetu mnafanya hivyo. Muhimu fanyeni kazi kuhudumia wananchi hawa bila kubagua mtu yoyote yule muhimu awe na nyaraka zote muhimu zinazomtambulisha,” alisema Masauni

“……wananchi hawa wamezichagua serikali hizi mbili lazima tuwahudumie maana ndio waajiri wetu,hatuwezi kuwa tupo katika serikali kisha hatuhudumii wananchi ipasavyo au tunahudumia kwa ubaguzi” aliongeza Masauni

Wakizungumza mbele ya Naibu Waziri Masauni wananchi waliofika katika ofisi hizo waliiomba wizara kuongeza idadi ya watumishi hasa katika kipindi hiki cha kukaribia mwisho wa kubadilisha pasi za kusafiria ili kupunguza kupoteza muda mrefu kufuatilia pasi hizo za kusafiria.

“Tangu asubuhi saa mbili tuko hapa na huduma zimekua zikienda taratibu sana,tunaomba kuwepo na uharaka wa kupata huduma hizi,wiki nzima tunakuja hapa lakini utolewaji umekua auridhishi sana,nadhan watumishi waongezwe” alisema Abdallah Kheri Said Mkazi wa Vuga

Akizungumza katika ziara hiyo Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa(NIDA),Hassan Hassan alisema matarajio mpaka mwisho wa mwaka huu ni kusajili watu Laki Nane Thelathini Sita Elfu huku akiweka wazi changamoto za wingi wa watu wanaofika kwa ajili ya kuchukua vitambulisho ambavyo vimekua vinatumika katika kupata pasi za kusafiria na usajili wa laini za simu

“Tutaletewa mashine 15 kutoka Tanzania Bara ili tuweze kuhudumia watu wengi kwa wakati mmoja ili kupunguza foleni na kuharakisha utolewaji wa vitambulisho hivyo” alisema Hassan

Nae Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar Johari Suluhu alitaja changamoto ya kipato kwa raia walowezi ambao gharama ya kupata kibali cha kuishi ambayo ni milioni mbili kuwa ni kubwa huku wakilalamika vipato vyao vikiwa vidogo.

POLISI TZ FC YAMTAMBULISHA MDHAMINI WAKE MKUU LODHIA GROUP

$
0
0
Mwenyekiti wa timu ya Polisi Tanzania Kamishna wa Polisi
Charles Mkumbo (Kulia) na Mwenyekiti wa Kampuni za Lodhia
Bw. Harun Lodhia wakisaini mkataba wa udhamini ambapo
kampuni ya Lodhia itakuwa mdhamini mkuu wa timu hiyo katika
kipindi cha mwaka mmoja. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es
Salaam. (Picha na Polisi Tanzania FC).
Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi Mhe. Kangi Lugola
akizungumza na Mwenyekiti wa Makampuni ya Lodhia Bw. Harun
Lodhia ambaye ndiye mdhamini mkuu wa timu ya Polisi Tanzania
wakati wa hafla ya kutambulishwa kwake jijini Dar es Salaam.
(Picha na Polisi Tanzania FC).
Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi Mhe. Kangi Lugola
akizungumza katika hafla maalumu ya kumtambulisha mdhamini
mkuu wa timu ya Polisi Tanzania inayoshiriki Ligi kuu Tanzania
bara Kampuni ya Lodhia. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam.
(Picha na Polisi Tanzania FC).
Mwenyekiti wa timu ya Polisi Tanzania Kamishna wa Polisi
Charles Mkumbo (Kulia) na Mwenyekiti wa Kampuni za Lodhia
Bw. Harun Lodhia wakisaini mkataba wa udhamini ambapo
kampuni ya Lodhia itakuwa mdhamini mkuu wa timu hiyo katika
kipindi cha mwaka mmoja. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es
Salaam. (Picha na Polisi Tanzania FC).

iMES, Imekuja kwa wakati Muafaka

$
0
0
Mataalam kutoka OR-TAMISEMI, Fatma Yusuph, akitoa msaada wa kiutaalam kwa wataalam wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela, wakati wa zoezi la uingizaji wa taarifa katika mfumo wa iMES.
Mtaalam wa TEHAMA, kutoka Mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma nchini, Milton Ndosi, akitoa ufafanuzi wa jambo wakati wa zoezi la uwandani kwenye Jiji la Mwanza.
Limi George, Afisa Ugavi Manispaa ya Ilemela, akiwa anaingiza takwimu katika mfumo wa iMES wakati wa zoezi la uwandani katika Manispaa hiyo. (Picha zota na Atley Kuni-TAMISEMI).
Afisa Takwimu kutoka OR-TAMISEMI, akitoa maelezo ya awali juu ya Mfumo wa iMES, kwa wataalam wa Jiji la Mwanza.

**********

Na. Atley Kuni- Mwanza

Wataalam kutoka Idara na Vitengo wa Manispaa ya Ilemela mkoani Mwanza, wamesema Mfumo jumuishi wa Ufatiliaji na Tathimini (integrated Monitoring and Evaluation System-iMES), umekuja kwa wakati na enzi muafaka, wakati huu ambao matumizi ya takwimu ni hitaji la kila nyanja katika kusukuma gurudumu la maendeleo.

Wakiwa katika zoezi la pamoja za uingizaji wa takwimu katika mfumo, wataalam hao wamesema, ile hali yakukimbizana na taarifa pindi zinapo hitajika sasa litakuwa mwanzo na mwisho wake.

Limi George, Afisa Manunuzi katika Manispaa hiyo anasema kwamba, kwakuwa mfumo ni web base, haita malazimu mtaalam kuanza kutembea kutoka ofisi moja kwenda ofisi nyingine kusaka taarifa bali kwakupitia mfumo wa iMES kila kitu mtu atafanya akiwa mezani kwake.

“Kwakuwa sisi watumiaji wote tumesha tengenezewa akaunti za kutuwezesha kuingia katika mfumo, hata kama kuna hoja za ukaguzi ambazo zilijitokeza kutoka kwa Mkaguzi Mkuu na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali, nikiwa kwenye dawati langu nitaweza kuzifatilia na kuzifanyia kazi bila yakutembea toka Ofisi moja hadi nyingine cha msingi hapa nikwa wataalam kuutumia mafumo kwakuweka data kwa wakati” alisema Limi.

Naye Rose Nyemele, Afisa Muuguzi katika Manispaa hiyo, yeye anasema, pamoja na kutumia mfumo wa (Data Health Information System-DHIS-2) katika masuala ya mipango ya bajeti na MTUHA, ambayo yalianzia ngazi ya Kijiji bado anaona iMES imekuja kwa wakati mujarabu kujibu masuala mtambuka kutoka sekta zote.

“Kwetu sisi watu wa Afya data ni kila kitu, Masuala kama Mipango ya bajeti katika Dawa, Rasilimaliwatu, pamoja na vifaa tiba na vitendanishi vingine hutegemea sana uwepo wa taarifa sahihi na kwawakati, hivyo iMES tunaiona kama suluhu yakudumu, alisema Nyemele.

Mtazamo wa Nyemele, hautofautiani na Afisa TEHAMA katika Halmashauri hiyo Isac Tenguye, ambaye anasema katika Dunia ya sasa kuwa na Mfumo kama huo ni muarobaini wa matatizo ya taarifa. 

“Huu ni mfumo utakao kuwa na chanzo kimoja cha taarifa na utaepusha takwimu kutofautiana kama kipindi cha nyuma, mnaweza kwenda kwenye mkutano mmoja na wadau lakini wewe mtendaji na mdau taarifa zenu mkakuta zinakinzana, lakini kwa iMES tunaona kabisa kila mmoja atajikita kupata taarifa kutoka katika mfumo na hivyo kuondoa tofauti” alisema Tenguye.

Hata hivyo Wataalam hao, hawakusika kuipongeza Serikali pamoja na Wadau wa Maendeleo nchini USAID, chini ya Maradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma PS.3 kutokana na juhudi wanazo zifanya za uimarishaji wa mifumo ya Sekta za Umma.

“Uzalendo nikuwa na mapenzi mema na nchi yako hivyo tunawapongeza sana OR TAMISEMI pamoja na PS.3, kwa ushirikiano huu ambao unaonesha matunda ya wazi wazi kwa nchi hususan ni katika kipindi hiki cha serikali ya awamu ya tano ambayo imejipambanua katika kumjali mwananchi” alisema Nelson Rugaimukamu Daktari wa Mifugo katika Manispaa hiyo. 

Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Manispaa ya Ilemela pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza, zimekuwa Mamlaka za mwanzo kabisa za majaribio ya mfumo huo wa iMES huku lengo likiwa nikuzifikia Halmashauri zote 185 nchini lakini pia kujumuisha Wizara za kisetakta kote nchini.

Jumla ya wagonjwa 10 wenye matatizo ya umeme wa moyo wafanyiwa matibabu kambi maalum ya matibabu inayoendelea katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)

$
0
0
Madaktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete(JKCI) na wenzao kutoka Shirika la Madaktari Afrika la nchini Marekaniwakimwekea mgonjwa ambaye mapigo yake ya moyo yako chini kwa asilimia 25kifaa maalum cha kuongeza utendaji kazi wa moyo (Cardiac resynchronizationtherapy implantable cardioverter defibrillator – CRTD).

Na Mwandishi Maalum

Jumla ya wagonjwa 10 wenye matatizo ya umeme wa moyo ambao mapigo yake yanadunda haraka kuliko kawaida na wengine yako chini ya asilimia 30 wamefanyiwa matibabu kwenye kambi maalum ya matibabu inayoendelea katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI).

Matibabu ya wagonjwa hao yamefanyika katika kambi maalum ya matibabu ya moyo inayofanywa na madaktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa shirika la Madaktari Afrika la nchini Marekani.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Idara ya Magonjwa ya Moyo Dkt. Peter Kisenge amesema kati ya wagonjwa 10 waliofanyiwa upasuaji katika kambi hiyo, wagonjwa wanne ambao mioyo yao ilikuwa imechoka na mapigo ya moyo kuwa chini ya asilimia 30 wamewekewa kifaa maalum cha kuongeza utendaji kazi wa moyo kijulikanacho kwa jina la kitaalamu la “Cardiac Resynchronization Therapy implantable cardioverter Defibrillator” (CRTD).

Dkt. Kisenge aliongeza kuwa kwa mara ya kwanza JKCI imeanza kuziba maeneo ambayo yanapitisha umeme wa moyo kwa wingi na kuleta shida katika moyo kwa kutumia mashine maalum (Electrophysiology machine) iliyotolewa hivi karibuni na Serikali ya Jamhuri ya watu wa China kwa ajili ya matibabu ya moyo hapa nchini.

“Mashine hii ya Electrophysiology inakazi ya kupima umeme wa moyo kama kuna mahali ambapo unapita bila kufuata njia ya kawaida pataonekana na baada ya hapo inatumika kuziba njia hizo. Tatizo hili huwatokea zaidi wagonjwa wenye shinikizo la juu la moyo la muda mrefu, wagonjwa wanaopata mstuko wa moyo, na wagonjwa wenye hitilafu ya umeme wa moyo katika baadhi ya vyumba vya moyo,” alisema Dkt. Kisenge.

Daktari huyo bingwa wa magonjwa ya moyo alisema matibabu ya kuziba maeneo yanapitisha umeme wa moyo bila kufuata njia yake awali hayakuwepo hapa nchini hivyo kupelekea wagonjwa wenye shida hiyo kupelekwa nje ya nchi kwa ajili ya matibabu lakini kuanzia Julai 22 mwaka huu matibabu hayo yameanza kutolewa hapa nchini.

Naye Mtaalamu wa mashine ya kuchunguza, kutathmini na kutibu umeme wa moyo unaoenda kwa haraka (Electrophysiologist) kutoka Shirika la Madaktari Afrika la Nchini Marekani Prof. Mathew Sachest alisema Madaktari Afrika wamekuwa wakishirikiana na madaktari wa JKCI kwa kipindi cha miaka mitatu sasa ambapo utoaji wa huduma za matibabu ya moyo umekuwa kwa kasi ya hali ya juu hivyo kupunguza uhitaji wa wagonjwa kwenda kutibiwa nje ya nchi.

Prof. Sachest alisema kupitia kambi maalum za matibabu wanazozifanya JKCI madaktari , wauguzi na mafundi sanifu wa moyo wanapata uzoefu wa kutoa huduma za matibabu zinazohitaji ujuzi wa hali ya juu na kuweza kutoa huduma hizo kwa wagonjwa.

RAIS DKT. MAGUFULI AFUNGUA KIWANDA CHA 21st CENTURY FOOD AND PACKAGING LTD JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano waTanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwana Mkewe Mama Janeth Magufuli wapili kutoka kushoto,
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda,Mkurugenzi wa Kiwanda hicho Mohamed Dewji, Waziri waViwanda Innocent Bashungwa, akikata utepe kuashiriaufunguzi wa Kiwanda cha 21 st Century Food andPackaging kilichopo jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano waTanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuliakizungumza na Mkurugenzi wa Kiwanda cha 21 st CenturyFood and Packaging Mohamed Dewji mara baada yauzinduzi wa kiwanda hicho.
Rais wa Jamhuri ya Muungano waTanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuliakisikiliza maelezo ya kutoka kwa Mkurugenzi waKiwanda cha 21 st Century Food and Packaging MohamedDewji kuhusu ubora wa bidhaa mbalimbali za kiwandahicho jijini Dar es Salaam.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuliakizungumza na wananchi mara baada ya kufunguakiwanda hicho jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU.

Jaji Kiongozi Dkt. Eliezer Feleshi ataka vifungo vya nje vitumike ili kupunguza msongamano magerezani.

$
0
0
Jaji Kiongozi Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi akitoa mada kwenye kikao kazi cha wataalam kutoka taasisi mbalimbali wanaofanya Maboresho ya Mfumo wa Haki Jinai nchini ili uendane na wakati. Wataalam hao ambao ni kundi la pili wanapitia mnyororo wa haki jinai na kubainisha changamoto katika mfumo na kupendekeza hatua za namna ya kutatua changamoto hizo na hivyo kuwa na mfumo mpya wa haki jinai ambao utazingatia utoaji haki kwa wananchi.

Dkt. Feleshi ameyasema hayo alipotembelea kikosi kazi cha Maboresho ya Mfumo wa Haki Jinai kinachoendelea na maboresho hayo jijini Dodoma ambapo wataalam kutoka taasisi mbalimbali wanakutana ili kuona namna bora ya kuboresha mfumo mzima wa haki jinai ili kuwawezesha wananchi kupata haki zao.

“Makosa yote ambayo hayahitaji kifungo cha mda mrefu, maisha na kunyongwa yangepewa vifungo vya nje, huu mfumo ulianzia Uingereza karne ya 17 ambapo magereza yao yalijaa wafungwa wakapelekwa Australia na baade wakaanzisha huu mfumo. Ni vyema ukatumika ili kupunguza msongamano magerezani ”, amesema.

Vilevile aliongeza kuwa Mashauri yote mahakamani yana ukomo wa kuyasikiliza nakuyatolea maamuzi ambapo Mahakama za chini ni mwaka mmoja na Mahakama kuu ni miaka miwili hivyo ni vyema mashauri yakaisha kwa wakati ili kuepuka mlundikano wa mahabusu magerezani.

Ameongeza, Ili kuwa na mwelekeo mzuri wa mfumo wa haki jinai, Polisi, Uhamiaji,TAKUKURU, Idara za Wanyamapori, TRA, nawengineo ni lazima wafanye kazi kwa ukaribu na kwa kushirikiana na ofisi ya Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali na sio kila kimoja kufanya kazi zake bila kuwa na ushirikiano na ofisi hii muhimu na hii itaharakisha umalizaji wa mashauri Mahakamani.

Dkt. Feleshi ametembelea kikosi kazi cha wataalam wanaoshiriki katika majadiliano ya kuboresha mfumo wa haki jinai nchini na kutoa mada kuhusu kibali cha Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali kufungua na kuendesha mashtaka na Usikilizaji wa awali wa shauri kwa mahakama za chini.

MWENGE WA UHURU WAZINDUA HUDUMA ZA UPASUAJI HOSPITAL YA MSOGA

$
0
0
NA MWAMVUA MWINYI,MSOGA

RAIS Mstaafu wa awamu ya nne ,dkt.Jakaya Kikwete ameimwagia sifa wizara ya afya kutokana na kuboresha sekta ya hiyo pamoja na kupandisha hadhi kituo cha afya Msoga kuwa hospital ya wilaya.

Akizungumza baada ya mwenge wa uhuru kuzindua huduma za upasuaji katika hospital ya wilaya ya Msoga,Chalinze,Bagamoyo mkoani Pwani,alisema hospital hiyo ilianza kama zahanati hivyo anashukuru kuongezwa hadhi.

Kikwete alieleza, jitihada za kuimarisha sekta ya afya zinazofanywa na serikali chini ya wizara hiyo zinahitaji kupewa pongezi.

"Mimi ni mzaliwa wa Msoga, kitovu changu kilidondokea hapa, nimefarijika kituo hiki kupandishwa hadhi naimani itakuwa mkombozi kwa wananchi wa Msoga na maeneo jirani kupata huduma ya matibabu ya karibu na kuondokana na kero ya kufuata huduma umbali mrefu, "alisema Kikwete.

Awali mganga mfawidhi hospital ya Msoga ,dokta Nelson Luoga alisema,hospital hiyo ilianza kutoa huduma za tiba kama zahanati tangu mwaka 1943 .

"Ilipandishwa hadhi kuwa kituo cha afya mwaka 2016 baada ya Rais mstaafu Jakaya Kikwete kujenga majengo mapya ndani ya eneo la zahanati ya Msoga."alifafanua Luoga.

Nae kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa 2019, Mzee Mkongea Ali alizindua mradi huo na kusema, serikali inaendelea kuboresha sekta ya afya ili kutoa huduma bora kwa jamii.

Wakati huo huo mwenge huo ulizindua mradi wa josho la mifugo na mradi wa uhifadhi wa chanzo cha maji(lambo) ,ambapo mke wa Rais mstaafu ambae pia ni mbunge wa kuteuliwa mama Salma Kikwete aliwataka wakulima na wafugaji kuwa kitu kimoja na kuepukana na migogoro baina yao.

Alisema ,washirikiane na kuheshimiana badala ya kuingiliana katika shughuli zao.Awali akipokea mwenge wa uhuru kutoka halmashauri ya Kibaha,mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Zainab Kawawa alisema ,mwenge huo umepitia miradi 15 yenye thamani ya zaidi ya sh.milioni 945.1.

Mwenge wa uhuru ulipokelewa mkoani Pwani Julai 24 na kukimbizwa kwenye wilaya saba ,halmashauri Tisa ambapo miradi 95 imepitiwa yenye thamani ya zaidi ya sh.bilioni 40.436.6:', kati ya miradi hiyo miradi 61 imekaguliwa,17 ilipaswa kuwekwa jiwe la msingi,9 kuzinduliwa na 8 kufunguliwa huku agost 2 ukitarajiwa kupokelewa mkoa wa Morogoro.



RAIS WA ZANZIBAR DK. SHEIN AFUNGUA MAONESHO YA KILIMO KIZIMBANI ZANZIBAR LEO.

$
0
0
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akifurahia wakati akivuna mboga aina ya spinachi katika kitalu cha maoneshi ya JKU , kulia Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Balozi Seif Alim Iddi.(Picha na Ikulu).
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Mwanafunzu wa Chuo cha Kilimo Kizimbani Ndg. Faki Ali Faki na kulia Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Balozi Seif Ali Iddi.(Picha na Ikulu).
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akiponyeza kitufe kuashiria kuyafungua Maonesho ya Kilimo Zanzibar katika viwanja vya Kizimbani Wilaya Magharibi “A” Unguja kulia Kaimu Waziri wa Kilimo Maliasili, Mifugo na Uvivi Waziri wa Ujenzi Usafirishaji na Mawasiliano,Mhe. Dkt Sira Ubwa Mwamboya.*(Picha na Ikulu).
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akiwa katika moja ya Trekta lililotolewa Mkopo na Benki ya TAD kwa Vikundi vya Ushirika Zanzibar, wakati wa hafla ya maonesho hayo yaliofanyika katika viwanja vya Kizimbani Wilaya ya Magharibi”A” Unguja leo.(Picha na Ikulu).
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akimkabihi Ufungo wa Treka Mwenyekiti wa Ushirika wa Kilimo Mkombozi cha Mkokotoni Ndg. Haji Mashaka Omar,wakati wa hafla ya Maonesho ya Kilimo yaliofanyika katika viwanja vya Kizimbani Wilaya ya Magharibi”A” Unguja.(Picha na Ikulu)

VIJANA 24 WA KIMASAI WAANZA MAFUNZO YA UFUNDI WASHI SIMANJIRO NA KITETO

$
0
0
Na Novatus Makunga,Simanjiro Agosti 01,2019

Vijana 24 wa jamii ya kabila la Kimasai katika wilaya za Simanjiro na Kiteto wameanza mafunzo ya ufundi uashi baada ya kukamilika kwa chuo pekee za ufundi katika wilaya hizo kilichojengwa kwa gharama ya shilingi milioni 531.

Chuo hicho kilichopo katika kata Emboret wilayani Simanjiro ambacho kimejengwa na shirika lisilokuwa la kiserikali la ECLAT Development Foundation kwa ufadhili wa shirika la Upendo Society la nchini Ujerumani,kimekabidhiwa kwa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi Nchini(VETA).

Akizungumza wakati wa kuwapokea wanafunzi , mwenyekiti wa shirika la ECLAT,Peter Toima alisema kuwa hiyo ni awamu ya kwanza inayohusisha madarasa,bweni moja,jiko,vyoo,kisima kirefu cha maji,umeme wa nishati ya jua na vifaa vya kufundishia uashi.

“Tuliamua kujikita katika ujenzi wa Chuo hiki kwa lengo la kuunga mkono mpango wa serikali wa kujenga vyuo vya ufundi stadi kwa kila wilaya huku tukizingatia kipaumbele cha wananchi wenyewe wa Simanjiro,”alisema.

Naye mwenyekiti wa shirika la Upendo la Ujerumani ambao ndiyo wafadhili wa mradi huo,Dk.Fred Heimbach aliwataka wanafunzi hao wa awali kusoma kwa bidii kwani wamepata fursa ambayo inawahakikishia ajira na baadaye kuweza kuendesha maisha ya.

Kwa upande wake Mratibu wa VETA kanda ya kati,Abdulkadiri Yussuf alisema kuwa chuo hicho kimeanza mafunzo ya fani ya uashi kutokana na mahitaji ya wananchi wa wilaya ya Simanjiro na wilaya ya jirani ya Kiteto ya mafundi wa ujenzi wa majengo.

“Kwa ujumla katika wilaya ya Simanjiro hivi sasa kuna kasi kubwa ya ujenzi wa nyumba lakini kuna changamoto kubwa ya mafundi wanatoka mjini Arusha kuja kujenga nyumba hapa”alisema.

Yussuf alisema kuwa katika awamu ya pili ya chuo hicho,kitaanzisha fani nyingine zikiwemo ufundi seremala,ufundi umeme na bomba,ushonaji wa nguo pamoja na ufundi wa zana na mitambo ya kilimo.

Alisema chuo hicho ambacho mpaka kitakapokamilika kitakuwa na wanafunzi 250 pia kitaanzisha mafunzo ya ufugaji wa kisasa na wa kibiashara wa ng’ombe,mbuzi,kondoaa na kuku pamoja na wanyamakazi kama vile punda.

Aidha alisema kuwa katika mwaka huu wa fedha wameshatenga shilingi milioni 81 kwa ajili ya kujenga bweni lingine litakalokuwa na uwezo wa kuchukuwa wanafunzi 24 katika eneo hilo lenye ukubwa wa ekari 100.

Diwani wa kata ya Emboret,Christopher Kuya alisema chuo hicho kitakuwakomboa vijana wengi wanaozurura mitaani kutokana na kushindwa kuendelea na elimu ya juu baada ya kuhitimu darasa la saba na kidato cha nne.

Alisema kuwa kuhitimu kwao katika fani mbalimbali za ufundi kutawawezesha kujiajiri na pia kuajiriwa kama mafundi wa ngazi ya kati hivyo kuingia katika mwelekeo wa serikali ya sasa ya Tanzania ya viwanda

Kuya alisema kuwa hivi sasa katikan maeneo ya Umasaini kuna kasi kubwa ya ujenzi wa nyumba za kisasa na ununuzi wa pikipiki maarufu kama bodaboda na hivyo mafundi wengi wanahitajika
Mkufunzi wa chuo cha ufundi cha VETA Simanjiro,David Mrutu(kulia) akitoa maelezo ya vifaa vya kufundishia uashi kwa mwenyekiti wa shirika la ECLAT,Peter Toima(katikati) na Mwenyekiti wa Shirika la Upendo Society la Ujerumani Dkt.Fred Heimbach(kushoto).
Mwenyekiti wa shirika la ECLAT,Peter Toima na mwenyekiti wa Shirika la Upendo Society la Ujerumani,Dkt.Ferd Heimbach wakitoa nasaha kwa baadhi ya wanafunzi walioanza masomo katika chuo cha ufundi cha VETA Simanjiro.
Mwenyekiti wa ECLAT,Peter Toima(kushoto) na Mwenyekiti wa Shirika la Upendo Society la Ujeruman Dkt.Fred Heimbach(kulia) wakitoa maelekezo kwa msimamizi wa miradi inayotekelezwa na mashirika hayoMasham Bakiri(katikati)
Mkufunzi wa chuo cha ufundi VETA Simanjiro,David Mrutu akikagua vifaa vya kufundishia ufundi uashi katika chuo hicho
Mwenyekiti wa ECLAT,Peter Toima(kushoto) na Mwenyekiti wa Shirika la Upendo Society la Ujeruman Dkt.Fred Heimbach(kulia) wakikagua vifaa vya kufundishia ufundu uashi katika chuo cha VETA Simanjiro
Mratibu wa Mamlaka ya Elimu na Ufundi Studi(VETA) katika kanda ya kati Abdulkarimu Yussuf akizungumza na waandidhi wa habari(hawapo pichani) nje ya moja ya jengo la chuo cha ufundi VETA Simanjiro.(Picha na Novatus Makunga)

DC Mtanda awatahadharisha kinababa wenye tabia ya kunyonya maziwa ya mama

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Mh. Said Mtanda amewatahadharisha kinababa wenye tabia ya kunyonya maziwa ya kinamama wanaonyonyesha kwani hicho ni chakula maalum kwaajili ya mtoto aliyezaliwa na yeyote anayefanya hivyo anadhulumu haki ya mtoto ambaye hutegemea maziwa ya mama kwa muda wa miezi sita bila ya kula chakula cha aina yoyote.

Amesema kuwa kazi kubwa ya kinababa ni kuwawezesha kinamama kupata lishe bora ili wawe na afya thabiti kutoa maziwa ya kutosha na kuweza kuwanyonyesha watoto wao na kuongeza kuwa katika mkoa wa Rukwa asilimia 81 ya watoto wenye umri chini ya miezi sita wanalishwa vyakula vingine vya ziada, jambo ambalo halikubaliki kwa maendeleo ya mtoto.

“Ujumbe wa Leo ni kwamba watoto wadogo chini ya Miezi Sita ndio wanaotakiwa kunyonyeshwa, kwahiyo kinababa na wao wenye kupenda maziwa ya baba waache kwasababu hicho sio chakula chao ni lishe kwa watoto wachanga, tusidhulumu haki za watoto za unyonyeshaji, tuache tabia ya kunyonya maziwa ya mama kwa wasiohusika,” Alisisitiza.

Aidha alisema kuwa tafiti zinaonesha kuwa asilimia 17 ya watoto wenye umri chini ya miezi 6 wananyonyeshwa maziwa ya mama pekee bila kupewa kinywaji au chakula kingine kama inavyoshauriwa na Shirika la Afya Duniani. Hii ina maana kuwa asilimia 83 ya watoto wenye umri huo hawanyonyeshwi ipasavyo.

Mh. Mtanda aliyasema hayo katika uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji kimkoa katika Kijiji cha Kisumba, kilichopo Wilaya ya Kalambo akimwakilisha aliyetakiwa kuwa mgeni rasmi wa uzinduzi huo Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo.

Kwa upande wake Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa Albinus Mgonya aliisifu timu ya afya ya Mkoa kwa kuwezesha kufanyika uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji katika Kijiji cha kisumba kutokana na Kijiji hicho kuwa na kinamama wengi wanaonyonyesha.

“Katika Kijiji hiki Mheshimiwa mgeni rasmi kuna Kaya 1300, na kwa takwimu ambazo tunazo kupitia idara yetu ya afya kinamama wanaonyonyesha watoto katika Kijiji hiki cha Kisumba ni 234, hivyo utaona kwamba tumekuja kuhakikisha kuwa ujumbe huu unafika kwa wadau kwa njia muafaka,” Alieleza.

Halikadhalika alisema kuwa maadhimisho hayo yankwenda sambamba na utekelezaji wa mradi wa Lishe Endelevu unaolenga kuongeza idadi ya watoto wenye umri kati ya miezi 6 – 23 kuhakikisha kwamba wanapata vyakula vyenye mchanganyiko sahihi na kusisitiza kuwa ni muhimu kinababa kushiriki katika maadhimisho hayo ili wawe msaada mkubwa kwa kinamama.

Wakati akitoa neno la Shukrani Meneja wa Mradi wa Lishe Endelevu Ali Omar alishukuru ushirikiano anaoupata kutoka serikalini na kuwasisitizakinamama kuwa unyonyeshaji wa maziwa ya mama huchangia kwa kiasi kikubwa katika kuboresha afya, kulinda uhai na maisha ya mtoto.

Asilimia 67 ya watoto wa umri kuanzia miezi 6 – 23 wanapewa vyakula ambavyo havina mchanganyiko wa kutosha, yaani mlo usiokamilika, hali inayodhihirisha kuwa, taratibu duni za ulishaji watoto ni mojawapo ya sababu za utapiamlo katika Mkoa wa Rukwa.
Baadhi ya kinamama wanaonyonyesha wakipita kwa maandamano maalum mbele ya mgeni rasmi katika uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya Unyonyeshaji iliyofanyika katika kijiji cha Kisumba Wilayani Kalambo. 
Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Mh. Said Mtanda. 

TANZANIA KUPOKEA WAGENI TOKA NCHI 15 ZA SADC

$
0
0
Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Profesa Joseph Buchweishaija amewataka watanzania wote kujitokeza kwa wingi kushiriki katika maadhimisho na maonyesho ya nne ya wiki ya Viwanda ya Jumuia ya Maendeleo ya Kusini mwa Africa (SADC) Maadhimisho na Maonesho hayo yatafanyika kuanzia tarehe 5 hadi 8 Agosti 2019 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC); Viwanja vya Karimjee na Gymkhana jijini Dar es Salaam.

Profesa Bucheishaija amesema kuwa Serikali kupitia Wizara ya Viwanda na Biashara inawaalika wananchi kufika kwa wingi kwani tunatarajia jumla ya nchi 15 wanachama wa SADC zitashiriki,

Aidha, ameongeza kuwa wiki hii ya SADC itawawezesha wananchi kuona fursa mbalimbali ikiwemo kuweza kupata malighafi za kilimo ambazo viwanda utumia kuzalisha bidhaa za viwandani. Miongoni mwa faida watakazozipata watanzania kupitia maonesho ya Viwanda kwa nchi za Kusini mwa Afrika ni pamoja na kujifunza au kubadilishana uzoefu na nchi nyingine za SADC ambazo zitashiriki katika maonesho hayo pamoja na kuongeza wigo wa masoko ya ndani na nje ya nchi. 

Nafasi imetolewa kwa kila mtanzania kujisajiri bado ipo mpaka tarehe 2 August, 2019 na wale ambao watakuwa hawajajisajiri wasiwe na wasiwasi maana nao watatembelea maeneo ya maonesho kama wengine na kuweza kuona bidhaa za nchi nyinyine, hivyo watu wote wanakaribishwa sana kwa ajili ya tukio la kihistoria ambalo kutokea tena mpaka ipite miaka kumi na mitano.

Naye Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara ndugu Ludovick Nduhiye ametoa ufafanuzi kuwa lengo kuu ni kuweka utayari kwa wananchi hususani kwa Tanzania kuweza kushiriki kwa wingi na kuweza kujionea fursa lukuki ambazo zitaonekana katika maoshesho hayo. 

Aidha bwana Nduhiye amewakaribisha wananchi kufika kwa wingi lengo likiwa ni kuangailia fursa muhimu zitakazopatikana kwenye wiki hiyo ya viwanda ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa masoko pamoja na ubadilishaji wa mawazo namna ya kuanzisha viwanda mbalimbali pamoja na kupata fursa mbalimbali kwenye nchi hizo za SADC. 

Naye mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya maonesho na maadhimisho ya Wiki ya Viwanda kupitia Wizara ya Viwanda na Biashara bwana Ally Gugu ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Mtengamano na Biashara amewahimiza wananchi kujisajili kupitia anuani zinazopatikana katika tovuti ya Wizara ya Viwanda na Biashara ambayo ni www.mit.go.tz na kisha kubofya katika linki mbili za haraka (quick link) ambazo ni Usajili Wiki ya Viwanda na Usajili Mkutano wa 39 wa SADC.

Gugu aliongezea kuwa haya maonesho ya viwanda ni fursa ya watanzania wote kuanzia wajasiriamali wadogo, wajasiriamali wa kati pamoja na wenye viwanda vikubwa ili tuweze kutimiza azima ya Serikali ya awamu ya tano inayosisitiza maendeleo kupitia uchumi wa Viwanda ili Tanzania iweze kufikia uchumi wa kati.

MAKAMU WA RAIS AFUNGUA MAONYESHO YA 26 YA NANE NANE MKOANI SIMIYU, AZINDUA MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI MAZAO BAADA YA KUVUJA

$
0
0
Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan akionyesha vitabu kuashiria uzinduzi rasmi wa  Mkakati wa Taifa wa Usimamizi wa Mazao baada ya Kuvuna, wakati alipoyafungua rasmi maonyesho ya 26 ya kilimo na mifugo (Nane Nane 2019), katika viwanja vya Nyakabindi, Bariadi Mkoani Simiyu.  Kauli mbiu katika Maonyesho ya 26 nane nane 2019 ni "KILIMO, MIFUGO NA UVUVI KWA UKUAJI WA UCHUMI WA NCHI” Maonyesho haya yanawapa wakulima fursa ya kuonyesha bidhaa zao pamoja na kujifunza mbinu tofauti za kuboresha mazao yao na mifugo kwa ujumla.
Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka, Mkakati wa Taifa wa Usimamizi wa Mazao baada ya Kuvuna, uliozinduliwa leo Agosti 1, 2019 wakati alipoyafungua rasmi maonyesho ya 26 ya kilimo na mifugo (Nane Nane 2019), katika viwanja vya Nyakabindi, Bariadi Mkoani Simiyu. Kulia ni Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga.
Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga, Mkakati wa Taifa wa Usimamizi wa Mazao baada ya Kuvuna, uliozinduliwa leo Agosti 1, 2019 wakati alipoyafungua rasmi maonyesho ya 26 ya kilimo na mifugo (Nane Nane 2019), katika viwanja vya Nyakabindi, Bariadi Mkoani Simiyu. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka.
Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan akitoa hotuba yake katika ufunguzi rasmi maonyesho ya 26 ya kilimo na mifugo (Nane Nane 2019), katika viwanja vya Nyakabindi, Bariadi Mkoani Simiyu.
Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga, akitoa hotuba yake na mpango wa wizara yake katika ufunguzi rasmi maonyesho ya 26 ya kilimo na mifugo (Nane Nane 2019), katika viwanja vya Nyakabindi, Bariadi Mkoani Simiyu.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka, akitoa hotuba yake katika ufunguzi rasmi maonyesho ya 26 ya kilimo na mifugo (Nane Nane 2019), katika viwanja vya Nyakabindi, Bariadi Mkoani Simiyu.
Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe akizungumza katika hafla ya ufunguzi rasmi maonyesho ya 26 ya kilimo na mifugo (Nane Nane 2019), katika viwanja vya Nyakabindi, Bariadi Mkoani Simiyu.
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega akizungumza katika hafla ya ufunguzi rasmi maonyesho ya 26 ya kilimo na mifugo (Nane Nane 2019), katika viwanja vya Nyakabindi, Bariadi Mkoani Simiyu.
Mbunge wa Jimbo la Bariadi na Mwenyekiti wa Wabunge wa Simiyu, Andrew Chenge akizungumza katika hafla ya ufunguzi rasmi maonyesho ya 26 ya kilimo na mifugo (Nane Nane 2019), katika viwanja vya Nyakabindi, Bariadi Mkoani Simiyu.




















MSANII STEVE RNB AWAPA SOMO WASANII CHIPUKIZI

$
0
0
Na.Khadija seif, Michuzi tv.

MSANII wa muziki wa Bongo fleva nchini, Stephen William a.k.a Steve RNB' ametoa somo kwa wasanii chipukizi katika kuboresha Muziki wao.

Steve rnb ambaye alitamba na nyimbo mbalimbali kama 'One Love'na 'Jambo' na nyingine nyingi ambazo zimefanya vizuri katika soko la Muziki nje na ndani ya nchi.

Msanii huyo amesema kuwa wasanii wanaochipukia katika sanaa wanapaswa kuongeza juhudi kwa kile wanachofanya.

"Hakuna msanii aliyepata urahisi katika katika muziki ili uwe muimbaji mzuri unatakiwa kuongeza juhudi kwa kile unachofanya hasa kujua shabiki zako wanataka uwe vipi kuanzia mavazi pamoja na utumbuizaji". alisema SteveRNB.Pia amesema wasanii hao wanatakiwa kutoa nyimbo zenye ujumbe mzuri katika Jamii kwa ajili ya kukuza kuelimisha, kuburudisha na kukuza soko la muziki.

Aidha amefafanua kuwa wasanii wengi chipukizi wanaiga muziki kutoka kwa watu ambao wameshafanya vizuri kimuziki na matokeo yake mashabiki wanapata ukakasi kwenye kugundua yupi Ni yupi hasa pale wanaposikiliza wimbo kwenye vituo vya redio au hata kumpelekea Msanii huyo kutotambulika haraka kwenye jamii yake kutokana na kuiga kwake kulikopitiliza hasa kwa upande wa sauti.

MAONESHO YA NANENANE TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA TANZANIA

$
0
0
Mwenyekiti wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Dkt. Titus Kamani akijadiliana masuala mbalimbali ya uendelezaji wa Sekta ya Ushirika alipotembelea mabanda katika maonesho ya Nanenane Mkoani Simiyu kulia Bw. Agustino Mbulumi Mkurugenzi wa uendeshaji wa Soko la Bidhaa Tanzania (TMX), kushoto ni Bw. Mombeki Baregu Mkuu wa Kilimo na Huduma za Fedha Vijijini wa Mfuko wa Kuendeleza Sekta ya Fedha Tanzania (FSDT).
Mrajis Msaidizi wa Mkoa wa Simiyu Bw. Ibrahim Kadudu akitoa maelezo kuhusu kazi na majukumu ya Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania kwa wananchi waliotembelea banda la Tume, pamoja nae ni watumishi wa Tume katika siku ya uzinduzi rasmi wa maonesho ya sikukuu ya wakulima Nanenane kwenye viwanja vya Nyakabindi Mkoani Simiyu.
Afisa Ushirika wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Bw. Boniface Moshi akitoa mafunzo ya masuala ya ushirika katika maonesho ya Nanenane Kitaifa yanayofanyika kwenye viwanja vya Nyakabindi Mkoani Simiyu

RAIS MAGUFULI: SISI WATANZANIA TUMEAMUA NA TUNAO UWEZO WA KUTEKELEZA MIRADI MIKUBWA YA MAENDELEO

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wananchi katika uzinduzi huo.


RAIS Dkt. John Magufuli amesema Tanzania imeamua na ina uwezo mkubwa wa kutekeleza miradi mikubwa ya maendeleo nchini pasipo kutegemea fedha zenye masharti zinazotolewa kutoka kwa wafadhili na wadau wa kimataifa wa maendeleo.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa Jengo la 3 la Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam, leo Alhamisi (Agosti 1, 2019), Rais Magufuli alisema uzinduzi wa Jengo la Uwanja huo ni ushahidi wa wazi wa usimamizi na nidhamu ya matumizi ya fedha za Serikali zinazotokana na kodi ya wananchi.

Aliongeza Jengo la Uwanja huo limejengwa kwa asilimia 100 kutokana na kodi za Watanzania, na hivyo kuiagiza Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano pamoja na Wakala wa Barabara Nchini (TANROAD) kusimamia vyema miundombinu ya Uwanja huo kwa kuhakikisha kuwa inatunzwa ili kuakisi vyema taswira ya Jiji la Dar es Salaam na Watanzania kwa ujumla.

Kwa mujibu wa Rais Magufuli alisema jengo hilo litakalokuwa na uwezo wa kuhudumia jumla ya abiria Milioni 6 kwa mwaka limeigharimu Serikali kiasi cha Tsh Bilioni 722 ambazo ni fedha zilizotolewa na Serikali, limeweza kuifanya Serikali kuaminika na kuwa na udhubutu wa kutekeleza miradi ya Maendeleo kupitia fedha za ndani.

“Ipo miradi mingi ya Maendeleo tunayoisimamia kwa fedha zetu za ndani ikiwemo Ujenzi wa reli ya kisasa, mradi wa kufua umeme Mto Rufiji, Barabara za Juu Ubungo, Daraja la Kigongo-Busisi, Daraja la Salender, Ujenzi na ukarabati wa Viwanja vya ndege 15, kujenga rada 4 katika Viwanja vya Ndege vya Dar Salaam, Mwanza, Mbeya na Kilimanjaro, huu ni ushahidi wa usimamizi imara wa fedha zetu za ndani” alisema Rais Magufuli.

Aidha Rais Magufuli alisema kuwa Serikali itaendelea kuimarisha miundombinu ya sekta ya anga nchini, kwa kuwa sekta hiyo imekuwa kiungo muhimu katika maendeleo ya sekta ya Utalii, kwani kila siku takribani watu Milioni 12 duniani hutumia usafiri wa anga kutokana na kuwa njia ya haraka na ya uhakika kwa ajili ya usafirishaji wa abiria na mizigo.

Akifafanua zaidi Rais Magufuli aliitaka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kutoa kipaumbele kwa makampuni ya kitanzania yanapewa nafasi katika maduka yatakayofunguliwa ndani ya Uwanja huo ili kuwawezesha kufaidi matunda ya kodi yao sambamba na kuweza kuchangia kikamilifu katika maendeleo ya uchumi.

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi huo, Mtendaji Mkuu wa TANROADS, Mhandisi Patrick Mfugale alisema tangu mwaka 2004-2011 Serikali imechukua hatua mbalimbali kwa ajili ya kuimarisha miundombinu ya majengo ya Uwanja wa ndege vyaJulius Nyerere ikiwemo ujenzi wa Jengo jipya la tatu la abiria katika uwanja huo, kutokana na majengo ya sasa ya jengo la I na II kukabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo uwezo mdogo wa kuhudumia abiria.

Anaongeza kuwa ujenzi wa Jengo hilo la tatu la abiria lilisimama ujenzi wake mwaka 2016 kutokana na mkandarasi kudai Tsh Bilioni 29, ambapo awali alishapokea kiasi cha Tsh Bilioni 380 kati ya Tsh Bilioni 560 zilizohitajika kwa ajili ya ukamlishaji wa jengo hilo hapo awali, lakini mwaka 2017 Serikali ilitoa zabuni ya ujenzi wa mradi huo kwa mkandarasi mwingine kutokana mkandarasi aliyepita kuwa na kasi ndogo ya utekelezaji wa mradi.

Kwa mujibu wa Mhandisi Mfugale alisema kutokana na kasoro zilizojitokeza, shughuli za ujenzi wa jengo hilo zilipelekwa kwa kampuni ya TECU na mshauri mwelekezi kampuni ya Arab Contractor ambapo hadi kufikia Mei 29 mwaka huu zilikamilisha ujenzi wa jengo hilo na kusubiri kukabidhiwa kwa Serikali kwa ajili ya kuanza kutumika kwake.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Nchini (TAA), Mhandisi Julius Ndyamukama alisema hadi kufikia sasa jumla ya makampuni 18 kati ya 23 ya kimataifa tayari yamehamishia shughuli zao katika Uwanja huo kwa ajili ya kuanza kutoa huduma za usafiri kwa abiria wanaosafiri kwenda nje ya nchi.

Aliongeza kuwa katika kuimarisha usimamizi bora wa Jengo la Uwanja huo, Mamlaka hiyo pia imewapatia mafunzo watumishi wake kwa ajili ya kupata uelewa wa pamoja wa namna bora ya kulinda miundombinu ya Uwanja huo na hadi sasa imepokea Tsh Milioni 500 kutoka Serikalini ilizozilipa kwa mkandarasi wa ujenzi wa mradi huo kwa ajili ya kutoa mafunzo hayo.

MAONESHO YA NANENANE NYAKABINDI SIMIYU: RC ANTHONY MTAKA AIPONGEZA WCF

$
0
0
NA K-VIS BLOG/Khalfan Said, Simiyu
MKUU wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka, ameupongeza Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi WCF, kutokana na ushiriki wake katika mpango wa Mkoa huo kuanzisha kiwanda cha vifaa tiba kwa kutumia malighafi ya pamba.
Mhe. Mtaka ametoa pongezi hizo kwenye viwanja vya Nyakabindi Mkoani Simiyu wakati alipotembelea banda la WCF linaloshiriki maonesho ya Nanenane. mwaka  2019.
“Mimi kama kiongozi wa serikali ya Mkoa, ninawashukuru sana WCF kama partner (washirika) wakubwa sana kwenye mkoa wetu hususan kwenye ujenzi wa kiwanda cha vifaa tiba.” Alifafanua.
Alisema WCF kupitia Mkurugenzi Mkuu wake, Bw. Masha Mshomba na wakurugenzi wengine wamekuwa wakishirika wakubwa katika vikao vingi vya mkoa vinavyohitaji washirika (partners).
Mkuu huyo wa mkoa alisema, tayari site clearance imefanyika na wizara inaelekea kutangaza zabuni ili mradi uanze kutekelezwa.
Maonesho ya Nanenane kitaifa yanayofanyika kwenye viwanja vya Nyakabindi nje kidogo ya mji wa Bariadi yamefunguliwa rasmi leo Agosti 1, 2019 na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan ambapo kaulimbiu ya mwaka huu inasema “Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa ukuaji wa uchumi wa nchi.”
Akizungumzia ushiriki wa WCF kwenye maonesho hayo, Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Mfuko huo Bw. Anselim Peter amesema, maonesho hayo ni fursa nzuri kwa Mfuko kuelimisha waajiri, wafanyakazi na wananchi kwa ujumla kuhusu kazi na majukumu ya Mfuko.
“Tupo hapa ili kutoa elimu kwa wafanyakazi, elimu kwa waajiri namna gani wanaweza kuwasilisha madai yao pale mfanyakazi anapopata madhara kutokana na kazi ili hatimaye aweze kupata fidia stahiki na kwa wakati.” Alisema.
Amewakaribisha wananchi wakiwemo waajiri kutoka Simiyu na mikoa jirani ya Shinyanga na Mara kufika kwenye banda la WCF namba 13 lililo jirani na lango kuu la kuingia viwanja vya Nyakabindi ili kupata elimu zaidi kuhusu huduma mbalimbali zitolewazo na WCF.
“Katika banda letu, tunatoa huduma mbalimbali zikiwemo za waajiri kujisajili na Mfuko, kwani tunatambua Mkoa wa Simiyu unakuja juu katika uwekezaji wa viwanda kwahivyo tunategemea waajiri wapya wengi kutoka hapa.” Alisema.
 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (kulia) akizungumza jambo na Katibu Mkuu wizara ya Mifugo na Uvuvi, Profesa Elisante Ole Gabriel kwenye viwanja vya Nyakabindi kwenye maonesho ya Nanenane kitaifa mkoani Simiyu.
Mhe. Mtaka akisaini kitabu cha wageni kwenye banda la WCF
 Mkuu wa Mkoa Mhe. Mtaka, akiongozana na Afisa Uhusiano Mwandamizi wa WCF, Bw. Sebera Fulgence baada ya kutembelea banda la Mfuko huo.
 Mkurugenzi wa Uendeshaji Mfuko wa  Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), Bw. Anselim Peter, (kulia), akitoa maelezo kuhusu shughuli za Mfuko kwa mwananchi huyu aliyetembelea banda la WCF.

Afisa Matekelezo Mwandamizi (WCF), Bw. Musa Mwambujule (kushoto), akimuhudumia mwananchi huyu aliyetembelea banda namba 13 la WCF kwenye viwanja vya Nanenane Nyakabindi Simiyu leo Agosti 1, 2019.
 Mkurugenzi wa Uendeshaji Mfuko wa  Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), Bw. Anselim Peter.
Afisa Uhusiano Mwandamizi wa WCF, Bw. Sebera Fulgence (kulia), akitoa elimu kwa mwananchi huyu aliyetembelea banda la Mfuko huo.

BENKI YA CRDB NA KAULI MBIU YA “KILIMO CHETU, VIWANDA VYETU, UCHUMI WETU” MAONYESHO YA NANE NANE SIMIYU

$
0
0
Benki ya CRDB imeendelea kudhihirisha kuwa Benki kinara katika kuwezesha sekta mbalimbali za maendeleo nchini ambapo katika maonesho ya mwaka huu ya nane nane ambayo kitaifa yanaadhimishwa mkoani Simiyu Benki hiyo imekuja na kauli mbiu ya “Kilimo chetu, Viwanda vyetu, Uchumi wetu”.

Akizungumza katika maonesho hayo ambayo yamezinduliwa rasmi leo hii na Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Boma Raballa alisema Benki ya CRDB inaamini kuwa uwezeshaji wa sekta ya kilimo utasaidia kuongeza malighafi katika viwanda nchini na hivyo kuchochea ukuaji wa uchumi wa taifa.

“Tukiwa Benki ya kizalendo nchini tupo tayari kushirikiana na Serikali yetu kujenga uchumi wa kati unaoshamirishwa na viwanda. Ambavyo kwa uhalisia vinategemea sana mazao ya kilimo kama malighafi zake,” alisema ndugu Boma Raballa.

Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe aliipongeza Benki ya CRDB kwa kuwa mstari wa mbele kuwezesha sekta ya kilimo kupitia huduma na bidhaa mbalimbali inazozitoa Benki hiyo kwa ajili ya kilimo ikiwamo mikopo ya pembejeo za kilimo.

"Nimefurahishwa sana na kauli mbiu yenu ya 'Kilimo Chetu, Viwanda Vyetu, Uchumi wetu' hii inaonyesha ni jinsi gani Benki hii imejipanga vilivyo kuboresha sekta hii muhimu ambayo ni kichocheo kikubwa katika kufikia uchumi wa kati wa viwanda", alisema Hussein Bashe.

Akimueleza Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe juu ya mchango wa Benki ya CRDB katika maendeleo kilimo nchini ndugu Boma Raballa alisema Benki ya CRDB inatoa zaidi ya asilimia 40% ya mikopo yote itolewayo kwa ajili ya kilimo nchini.

Ambapo kwa kipindi cha mwaka 2018/2019, zaidi ya shilingi bilioni 650 zimeshatolewa. Katika hizo, shilingi bilioni 150 yaani asilimia 23% , zimeelekezwa katika kilimo cha mazao ya biashara na malighafi za viwanda, utengenezaji wa pembejeo, usindikaji na usambazaji.

Raballa alisema pia Benki ya CRDB imekuwa ikishirikiana na kwa karibu wadau wadau mbalimbali wa sekta ya kilimo nchini ikiwamo Benki Kuu ya Tanzania, Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB), Shirika la Uwezeshaji wa Kilimo (PASS), Mfuko wa Afrika Gurantee (AGF), Shirika la Uwezeshaji Kifedha la Kimataifa (IFC), Benki ya Maendeleo Afrika (AFDB), Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO), Ushirikiano wa Maendeleo ya Viwanda (IDC) na Kampuni ya ETC Agro katika kuwawezesha wakulima nchini kupitia mafunzo mbalimbali juu ya ufahamu wa masuala ya fedha, uwekezaji , utafutaji masoko na mikopo ya kilimo.
Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe, akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Wateja wa Kati na Wadogo wa Benki ya CRDB, Boma Raballa wakati alipotembelea banda la Benki ya CRDB katika maonyesho ya 26 ya kilimo na mifugo (Nane Nane 2019), yaliyofunguliwa rasmi leo na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan kwenye viwanja vya Nyakabindi, Mkoani Simiyu.
Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe, akisaini kitabu cha wageni wakati alipotembelea banda la Benki ya CRDB katika maonyesho ya 26 ya kilimo na mifugo (Nane Nane 2019),  yaliyofunguliwa rasmi leo na Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan kwenye viwanja vya Nyakabindi, Mkoani Simiyu. Katikati ni Mkurugenzi wa Wateja wa Kati na Wadogo wa Benki ya CRDB, Boma Raballa.
 Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe, akisalimiana na Afisa Masoko Mwandamizi wa Benki ya CRDB, Nassib Kalamba wakati alipotembelea banda la Benki ya CRDB katika maonyesho ya 26 ya kilimo na mifugo (Nane Nane 2019), katika viwanja vya Nyakabindi, Bariadi Mkoani Simiyu.
 Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima akizungumza na Meneja wa Biashara wa Benki ya CRDB, Felix Kisenha wakati alipokuwa akipatiwa huduma za kibenki katika Tawi la Benki ya CRDB linalotembea, katika maonyesho ya 26 ya kilimo na mifugo (Nane Nane 2019), katika viwanja vya Nyakabindi, Bariadi Mkoani Simiyu.
 Afisa wa Benki ya CRDB, Maregesi Shaaban akieleza jambo kuhusu huduma ya Malkia Akauti kwa baadhi ya wateja wa Benki hiyo waliotembelea banda lao, wakati wa maonyesho ya 26 ya kilimo na mifugo (Nane Nane 2019), katika viwanja vya Nyakabindi, Bariadi Mkoani Simiyu.














Rais Magufuli afungua Jengo la 3 la JNIA leo jijini Dar

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikata utepe akishuhudiwa na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa na viongozi wengine kuashiria ufunguzi rasmi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Alhamisi Agosti 1, 201
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa wakifurahia baada ya kuingia kwenye ndege ya ATCL aina ya Dreamliner iliyotua kutokea Mumbai wakati wa sherehe ya ufunguzi rasmi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Alhamisi Agosti 1, 2019
Wapiga picha wakifurahia kupigwa picha na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ndani ya ndege ya Dreamliner ya AITCL iliyowasili kutoka Mumbai wakati wa sherehe ya ufunguzi rasmi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Alhamisi Agosti 1, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na wapiga picha wa vyombo mbalimbali vya habari wakipigwa picha na Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa wakiwa ndani ya ndege ye ATCL ya Dreamliner iliyotua kutoka Mumbai wakati wa sherehe ya ufunguzi rasmi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Alhamisi Agosti 1, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa na Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeiry bin Ally wakitembezwa sehemu mbalimbali wakati wa sherehe ya ufunguzi rasmi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Alhamisi Agosti 1, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea kwa furaha na wafanyakazi wa Tawi la Benki ya NMB lililoko ndani ya Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam baada ya kuufungua rasmi leo Alhamisi Agosti 1, 201
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na marubani wa ndege ye ATCL ya Dreamliner waliotua kutoka Mumbai wakati wa sherehe ya ufunguzi rasmi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Alhamisi Agosti 1, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa wakiondoka baada yakuhitimisha sherehe ya ufunguzi rasmi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifawa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Alhamisi Agosti 1, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa akiagana na Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama baada ya sherehe ya ufunguzi rasmi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Alhamisi Agosti 1, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipiga Push Up na wasanii wa Tanzania One Theatre (TOT) wakati wa sherehe ya ufunguzi rasmi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Alhamisi Agosti 1, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza kwa kazi nzuri ya kutumbuiza msanii wa Tanzania One Theatre (TOT) Plus Khadija Omar Kopa wakati wa sherehe ya ufunguzi rasmi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Alhamisi Agosti 1, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa wakifunua pazia kama ishara ya ufunguzi rasmi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Alhamisi Agosti 1, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipungia wananchi kwa furaha akiwa na Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa na Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeiry bin Ally na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Katoliki la Dar es salaam Muadhama Polycarp Kardinali Pengo wakati wakielekea kukata utepe wakati wa sherehe ya ufunguzi rasmi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Alhamisi Agosti 1, 2019.


Viewing all 110170 articles
Browse latest View live




Latest Images