Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110171 articles
Browse latest View live

WAZIRI MKUU: TUTAIBADILI SHULE YA LIUGURU IWE YA WASICHANA TU

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na viongozi wakati alipowasili kwenye Shule ya Sekondari ya Liuguru wilayani Ruangwa kukagua majengo ya Shule hiyo na kuzungumza na wananchi, Julai 29, 2019.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua darasa wakati alipotembelea Shule ya Sekondari ya Liuguru wilayani Ruangwa Julai 29, 2019. Wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Ruangwa, Andrew Chezue. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na wananchi kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari ya Liuguru wilayani Ruangwa, Julai 29, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).



*Asema itakuwa ya bweni ili wasichana wengi zaidi wasome

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema amekuwa na ndoto ya muda mrefu ya kuona shule ya sekondari Liuguru inabadilishwa na kuwa shule ya bweni kwa ajili ya wasichana pekee.

“Ndoto yangu ni kuona shule hii inakuwa ya wasichana peke yao. Na tukifanikiwa, tutatengeneza akinamama wasomi, wanaojitambua, wenye maadili mema na wachapakazi,” alisema.

Alikuwa akizungumza na wakazi wa kijiji cha Liuguru, kata ya Narungombe, wilayani Ruangwa jana jioni (Jumatatu, Julai 29, 2019) mara baada ya kukagua shule hiyo.Waziri Mkuu ambaye ni mbunge wa jimbo la Ruangwa, alisema amechagua shule za Mnacho na Liuguru ziwe ni za bweni kwa ajili ya wanafunzi wa kike tu kama njia ya kuwaongezea fursa za masomo katika wilaya hiyo.

“Leo nimekuja kuwaeleza ndoto yangu. Tunahitaji kuona kila mtoto anayeenda shule, anakuwa na uhakika wa kumaliza masomo yake ya elimu ya juu. Wilaya hii tuna shida ya idadi kubwa ya mimba kwa watoto wa kike, na mimi hili jambo linanikera sana,” alisema.

“Tulikubaliana tuwe na kaulimbiu yetu kwamba ‘Ruangwa kwa maendeleo inawezekana’, lakini kwenye elimu tumekwama kuleta maendeleo kwa sababu dada zetu hawamalizi shule na sisi ndiyo wasababishaji. Tumeweka sheria ya kuwafunga watu wanaowapa mimba wanafunzi, lakini bado haisaidii.”

“Njia pekee ya kuondokana na tatizo hili ni kufanya shule hizi ziwe za bweni ili wakae hapa shuleni, wafundishwe bila kupoteza muda wa kwenda nyumbani au kukutana na vikwazo wawapo njiani kuja shule au kurejea nyumbani,” alisema.

“Kwa wenzetu kwenye mikoa mingine, mtoto wa kike akianza shule ya awali, atamaliza ya msingi, ataenda sekondari hadi chuo kikuu. Akimaliza kusoma, anarudi nyumbani kuja kufanya kazi kwao na kuwasaidia wengine waliokosa fursa.”

“Tunahitaji mabweni kwa ajili ya watoto wetu wa kike kuanzia kidato cha kwanza hadi cha nne, tunahitaji nyumba za walimu ili wake hapa na kuwalea wanafunzi wetu. Yakikamilika, tutawahamisha wavulana wanaosoma hapa na kuwapeleka shule za jirani au za bweni, ili hapa tuwaachie wasichana peke yao,” alisema Waziri Mkuu.

Alisema kwa kuanzia zitatumwa sh. milioni 100 ili zitumike kujenga nyumba nne za walimu, kisha atatafuta fedha nyingine ajili ya ujenzi wa mabweni, bwalo la chakula, jiko na mahitaji mengine kadri fedha zitakavyopatikana.

Aliwataka wanafunzi wa shule hiyo wahakikishe wanakazania masomo kwani hakuna muujiza wa kufaulu mitihani kama hawatasoma kwa bidii. “Wanangu wa Form 2 na Form 4 hakuna muujiza wa kufaulu mitihani iliyo mbele yenu. Ni lazima msome kwa bidii. Na msikubali kuishia Form 4, lazima mwende Form 6 na mkimaliza hakikisheni mnafika chuo kikuu,” alisisitiza.

Mapema, akiwasilisha taarifa mbele ya Waziri Mkuu, Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Bw. Samuel Diwani alisema shule hiyo iliyoanzishwa mwaka 2007, hivi sasa ina walimu 11 ambapo watatu kati yao wanafundisha masomo ya sayansi na wanane waliobakia wanafundisha masomo ya lugha na sanaa.

Alisema shule hiyo yenye wanafunzi 109 ambapo 51 kati yao ni wavulana na 59 ni wasichana, inakabiliwa na changamoto nyingi zikiwemo ukosefu wa nyumba tisa za walimu, ukosefu wa maabara mbili na iliyopo moja haijakamilika kwa asilimia 100.

Nyingine ni ukosefu wa mabweni, maabara ya kompyuta, mfumo wa umemejua, maktaba, jengo la utawala na stoo.

Agra inavyosaidia Tanzania kubadili kilimo chake

$
0
0
WAKATI taasisi ya kimataifa ya mapinduzi ya kijani barani Afrika (AGRA) ikitekeleza miradi mbalimbali nchini inayohusiana na maendeleo ya kilimo na masoko, Shirika hilo leo Jumatatu limefikia makubaliano na serikali ya Tanzania ya namna ya kuwezesha mabadiliko katika kilimo hivyo kuwakomboa wakulima kwa kuongeza tija na kuipeleka Tanzania katika uchumi wa viwanda.

Makubaliano hayo yamefikiwa baada ya mkutano ulioshirikia mawaziri watatu wa Tanzania na ujumbe wa taasisi hiyo ukiongozwa na Rais wake Dk Agnes Kalibata. Ujumbe wa Tanzania uliongozwa na Waziri wa Viwanda na Biashara, Innocent bashungwa. Mawaziri wengine ni manaibu wawili wa wizara ya Kilimo Hussein Bashe naOmar Mgumba.

Katika makubaliano hayo, serikali na Agra wameafikiana kuangalia namna ya kusukuma mbele ASDP ll na pia kuwezesha mazao ya kimkakati ya viwanda kama alizeti, mahindi na maharage ya soya am,bayo yanaweza kupelekwa kiwandani katika msim u mmoja yanasaidiwa kupunguza gharama na pia kuongezwa tija ili kutumika katika viwanda vilivyopo nchini.
Rais wa AGRA , Dk Kalibata (wa pili kulia-mbele) akizungumza 
Waziri wa Viwanda na Biashara Innocent Bashungwa akiongoza mkutano 


Aidha Agra watatoa ruzuku ya dola 600,000 kwa ajili ya kuimarisha utekelezaji wa ASDPll kwa kusaidia serikali katika masuala ya kiufundi yanayohusu program mbalimbali za kilimo.

Kabla ya kufika Dodoma jana ujumbe wa Rais huyo wa AGRA ulikuwa Iringa kwa siku 2 akifanya mazungumzo na wadau wa sekta ya kilimo waliopo katika mradi unaosimamiwa na AGRA wa Ihemi Ludewa.

Mradi huo ni sehemu ya juhudi za AGRA katika kuinua hali ya wakulima kwa kuwashirikisha wadau wote ikiwemo sekta binafsi na serikali ya mitaa, mkulima akiwa ndio mtu wa kati anayetakiwa kuhudumiwa huku serikali ikihakikisha kwamba hakuna fedha zinazotumika kwa kazi moja kutoka kila idara au ufadhili.
Muuza pembejeo za kilimo Zabibu akizungumza dukani kwake 


Kabla ya mkutano wake na wadau wanaosaidia mradi wa Ihemi Ludewa, Rais huyo aliendesha mkutano wa kimataifa wa nchi 11 zinazosaidiwa na AGRA kutekeleza miradi mbalimbali ya kuinua kilimo na kuwezesha masoko.

Nchi hizo ni pamoja na Mali, Burkina fasso, Ghana, Nigeria, Ethiopia, Kenya, msumbiji, Rwanda na Tanzania.Mkutano huo ulikuwa kubadilishana uzoefu wa uendeshaji wa majukwaa huru yanaounganisha wadau muhimu katika sekta ya kilimo kuwezesha kila mmoja kutekeleza wajibu wake.

Katika mkutano huo wadau wa Tanzania walielezea umuhimu wa vyama vya ushirika kuweza kupata elimu ya kilimo,kuunganisha sauti katika soko na pia kujifunza mambo mapya katika teknolojia ya kisasa ya kilimo.

Aidha mataifa mengine yalielezea haja ya kuungana kwa nchi za Afrika katika kuinua sekta ya kilimo kwa serikali kushirikiana na mashirika mbalimbali yanayochangia kilimo ili kuwezesha utekelezaji wa sera za kwenda vizuri.

“ Serikali ndio yenye wataalamu wa kilimo na ndio wasimamizi wa teknolojia ya kisasa, tusiposhirikiana tutafanyakazi ya kuwianua wakulima kuwa ngumu” alisema Rais wa AGRA, Dk Kalibata.
Dk Kalibata wakizungumza na mkulima Victory wakati alipomtembelea shambani kwake 
Josephine kutoka taasisi ya uelimishaji Briten akizungumzana mfanyabiashara wa mahindi na mkulima Christina 

Aidha katika ziara yake kuwaona wadau wa sekta ya wakulima, Dk Agnes Kalibata ametaka elimu zaidi kutolewa kwa wakulima ili kufanya kilimo cha ushindani kitakachohimili mabadiliko ya soko duniani.

Dk Kalibata alisema kwamba bila kuwaandaa wakulima, kukitokea shida katika bei wakulima watakuwa wanakata tama na kuona kilimo chao hakilipi.

Alitoa hoja hiyo baada ya kutaka kununua soya kutoka kwa mkulima Victory Mhanga wa Magulilwa halmashauri ya Iringa, mkoani Iringa ambaye alitaka kumuuzia bidhaa hiyo kwa bei ya Sh 2000.

Dk Kalibata alisema kwamba bei hiyo ni kubwa kulinganisha na soya inayolimwa Brazil.Hata hivyo wataalamu wa masoko waliokuwapo katika ziara hiyo walisema kwamba bei ya juu ilikuwa sh 800 katika mnada wa Songea uliofanyika hivi karibuni ingawa bei ya rejareja Dar es salaam ni Sh 2,500.

Alipouliza zaidi sababu ya bei hiyo kubwa kutozwa na mkulima huyo wakati katika soko la dunia ni dola 0.63 aliambiwa kwamba mkulima huyo anauza kwa nguvu la soko inayomzunguka na kwamba hana tatizo la soko katika eneo lake.

Magulilwa wameanza kulima soya mwaka huu na ingawa wanafahamu faida yake wakulima wachache ndio wamechukua maamuzi ya kulima soya.

Hata hivyo, Rais huyo alisema wakulima lazima waandaliwe kulima na kuzalisha kwa kiwango kikubwa na kupambana na bei ya soko la dunia ambalo huenda likawa chini kuliko wanavyofikiri, lakini wakiwa na mazao ya kutosha bei hiyo ya chini inaweza kabisa isiwaharibie kazi yao na hivyo kuendelea kulima kwa tija kuliko kuwa na bei kubwa na soko finyu.

“ Tusitazame bei tu inayotuzunguka kwa kiasi kidogo. Tukitaka kuwa matajiri katika kilimo ni lazima kutazama kwa upana wake na viongozi wa wakulima lazima wawaeleze wakulima bei ya dunia kitaifa , kimkoa na maeneo yao na kujua manufaa yake,” alisema Rais huyo.

Alisema kwa kuangalia mihimili mitatu inayofanyiwa kazi na AGRA ya uwezeshaji, mfumo na uwekezaji suala la masoko na mauzi ni suala ambalo linatakiwa kuzingatiwa ili mkulima aone faida ya kilimo chake.

Akizungumza kuhusu wauza pembejeo, aliwataka kuwasaidia wananchi kutambua mahitaji halisi na kuyafanyia kazi ili kuweza kuwasaidia kuwa na kilimo cha kisasa hasa matumizi ya pembejeo na mbegu.

Pamoja na kumsifu mkulima huyo na wakulima wengine katika halmashauri ya iringa na Ilolo, Dk kalibata alisifu wakulima kwa kuongeza uzalishaji kufikia hadi magunia zaidi ya 20 kwa ekari na kusema wakiendelea kubadilika watafikisha maguni hata 30.

Rais huyo ambaye pia alipata nafasi ya kutembelea mashamba ya mbegu ya Silverland na kiwanda cha kusaga nafaka cha Seki wanaotengeneza sembe yenye virutubisho, amesema ushiriki wa AGRA katika maeneo ambayo serikali inataka kufanyiwa kazi kumeleta neema kwa wakulima.

Kiwanda cha seki kimekuwa kikinunua mahindi kutoka kwa wakulima na vyama vyao vya msingi na Sliverland ambao pia hununua soya na mahindi kwa ajili ya kutengeneza chakula cha mifuigo pia wana dhamana ya kulima mbegu kwa mujibu wa mkataba wake na kampuni ya mbegu ya Seed Co, wanasaidia kutanuka kwa soko la wakulima, shughuli muhimu inatyofanywa na AGRA kuwezesha taasisi nyingine kusaidia wakulima kupata soko.

Mwaka 2014 AGRA ilianzisha mradi wa miaka mitatu wa kusaidia shughuli mbalimbali za kuinua kilimo kwa wakulima wadogo na kuongeza tija wenye thamani ya dola za Marekani milioni 4.25.

Mradi huo uliotekelezwa na Netherlands Development Organization (SNV), Rural Urban Development Initiative (RUDI), Women in Social Entrepreneurship (WISE) na Dunduliza Network of Savings And Credit Co-operatives (SACCOs) waliwezesha miradi mbalimbali iliyokuwa na lengo la kusaidia kuongeza tija, pato na soko kwa mkulima mdogo kwa maeneo ya ukanda wa SAGCOT.

Mradi huo ambao baadae ulifuatiwa na mradi wa Pata Tija yaani tengeneza utajiri, ulifundisha haja ya matumizi ya mbegu bora na pembejeo katika kuilimo, kufunza wauza pembejeo teknolojia mpya na nakuwuanga wakulima na taasisi za fedha.

Katika mradi huo pia wadau wlaipata nafasi ya kujifunza menejimentiya udongo.Wilaya ambazo zilifadikika na mradi huo ni opamoja na Ifakara, Kilombero, Kilolo, Kyela, Ludewa, Mbarali, Mbeya, Mbozi, Momba, Namtumbo, Songea na Sumbawanga.

AGRA ikiwa imelenga kubadili maisha ya wakulima na vipato vyao katika bara la Afrika jana iliingia katika makubaliano na serikali ya Tanzania kwa kutia saini hati ya maridhiano (MOU) inayoonesha majukumu ya serikali na taasisi hiyo katika lengo la kuinua ushiriki wa kila mdau katika kuinua sekta ya kilimo kuipa tija kwa uzalishaji wa uhakika na soko la uhakika huku mazingira yakilindwa.

Huku bara la Afrika likiwa na asilimia 25 ya eneo la ardhi lenye uwezo wa kuzalisha, sekta ya kilimo barani Afrika inaweza kupanda kama hatua kadha zitachukuliwa kuimarisha tija .

Taarifa ya Shirika la Chakula Duniani ( FAO) ya mwaka 2016 kuhusu usalama wa chakula, inasema kwamba watu milioni 153 ikiwa ni asilimia 26 ya watu waliochi ya miaka 15 Kusini mwa Jangwa la Sahara wamekabiliw ana upungufu mkubwa chakula kwa mwaka 2014/15.

TAEC yawaomba Wananchi kanda ya ziwa kujitokeza kwa wingi maonesho ya nane nane simiyu

$
0
0
Wananchi wanaoishi mikoa ya kanda ya Ziwa na mikoa ya jirani ,wametakiwa kuhudhuria kwa wingi katika maonesho ya Nane Nane Kitaifa yanayofanyika katika uwanja wa Nyakibindi, ili kujipatia elimu ya namna ambavyo teknolojia ya nyuklia inavyotumika katika sekta mbali mbali hapa nchini ikiwemo kilimo, mifugo, maji pamoja na afya.

Akizungumza katika banda la Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC) ,Afisa mwandamizi wa Utafiti wa TAEC, Bwana Yesaya Sungita amesema kuwa wananchi watapata elimu ambayo itawawezesha kupata uelewa juu ya masuala ya matumizi salama ya teknolojia ya Nyuklia na udhibiti wake hapa nchi ili kutokuleta madhara kwa wananchi pamoja na mazingira.

Sungita amesema kuwa TAEC imekuwa ikihakikisha teknolojia ya Nyuklia inatumika ipasavyo katika sekta muhimu kama vile Maji, Mifugo na Kilimo.

Hata hivyo SUNGITA amesema mbali na wananchi kujua kuhusiana na teknolojia ya Nyuklia pia wataweza kufahamua namna TAEC inavyofanya kazi ya Kusimamia na kuthibiti matumizi ya salama ya mionzi nchini.
Timu ya Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania(TAEC) katika picha ya pamoja kwnye banda lao lilipo katika uwanja wa Nyakabindi Wilayani Bariadi mkoani Simiyu ,ambapo wameanza kutoa elimu kuhusiana na masuala mbali mbali ikiwemo namna ya teknolojia ya Nyuklia inavyotumika katika sekta ya Kilimo,Mifugo,maji na Mazingira,pia inavvyosimamia na kudhibiti matumizi salama ya mionzi.

Halmashauriya wilaya ya Tunduru yaanzisha msako wa kuwatafuta wagonjwa wa kifua kikuu waliokatisha matumizi ya Dawa

$
0
0
Mganga Mkuu wa Halmashauriya wilaya ya Tunduru, Dkt Wendy Robert akimwanzishia Dawa za kifua kikuu mtoto Rashid Salum mwenye umri wa miaka 3 wa kijiji cha Nandembo Tunduru ambaye wazazi wake walimkimbizia shambani ili asinywe dawa hizo kutokana na imani potofu,anayeshuhudia katikati Mratibu wa kifua kikuu na Ukoma wa Hospitali ya wilaya Tunduru Dkt Mkasange Kihongole.
HALMASHAURI ya wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma,kupitia Idara ya Afya imeanza msako wa kuwatafuta wagonjwa wa kifua kikuu waliokatisha matumizi ya Dawa ili waendelee kunywa, kama  mkakati wa kumaliza  tatizo hilo na kupunguza vifo vitokanavyo na ugonjwa  huo.

Msako huo unaoongozwa na Mganga mkuu wa Halmashauri Dkt Wendy Robert, na mratibu wa kifua kikuu na ukoma Dkt Mkasange Kihongole, unawashirikisha  viongozi wa serikali za vijiji, umewezesha kuokoa  watu kadhaa ambao walisitisha matumizi ya dawa  nan a hivyo kuwa katika hatari ya kupoteza maisha.

Akiongea  na  wazazi  katika kijiji cha Nandembo Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Tunduru Dkt Wendy Robert alisema, msako huo unalenga wale wote ambao walibainika kuwa  na vimelea vya ugonjwa wa kifua kikuu wakiwemo watoto wadogo walioibuliwa kupitia kampeni ya uchunguzi  wa vimelea vya TB katika maeneo mbalimbali na walianzishiwa dawa lakini waliamua kukatisha.

Dkt Wendy alisema,Serikali inatumia fedha nyingi kuagiza dawa kwa ajili ya watu wanaobainika  kuugua kifua kikuu hasa ikizingatia kuwa  ugonjwa huo ni kati ya magonjwa 10 Duniani yanayoongoza kuuwa watu wengi na Tunduru  ni kati ya wilaya iliyoathirika sana  maradhi hayo.

Alisema,  madhara  ya kukatisha kunywa dawa ya kifua kikuu ni kubwa mno kwani mgonjwa mwenye homa hiyo asiyepata tiba sahihi anaweza kuambukiza watu wengine zaidi ya 15 kwa wakati mmoja ndiyo maana  Serikali imeweka utaratibu wa kutoa dawa za ugonjwa huo bure.


Kwa mujibu wa Wendy,kumkimbiza mtoto mbali na huduma za Afya ni unyanyasaji, kumnyima haki  na ukatili dhidi ya mtoto na kutompatia dawa mtoto mwenye maambukizi ni kukiuka sheria ya Afya ya Jamii ya  mwaka 2009.

“mtu anayejua ana ugonjwa fulani lakini hampeleki kwenye matibabu ni kosa kisheria na kuna adhabu ambayo muhusika atakabiliana nayo,nasisitiza wazazi na walezi wahakikishe wana wapeleka wagonjwa kwenye maeneo ya kutolea huduma ili wapate tiba sahihi na kufuatilia hali ya afya zao”alisema, Wendy.

Kwa upande wake mratibu wa kifua kikuu na ukoma wa Hospitali ya wilaya Dkt Mkasange Kihongole alisema,ugonjwa wa TB unatibika kwa mgonjwa kutumia dawa  kwa miezi sita bila kuacha.

Mkasange alisema, idara ya Afya kupitia kitengo cha kifua kikuu na ukoma  itaendelea  na kampeni ya uchunguzi  na kutoa elimu  kwa jamii ili wafahamu chanzo,madhara,tiba na hatua  ya kuepuka kupata kifua kikuu.

Alisema, wazazi ndiyo wenye wajibu wa kufuatilia Afya za watoto na kuhakikisha matumizi sahihi ya dawa za  kifua kikuu ili kuokoa maisha yao.

Pia ameiomba jamii,kutowatenga watu wenye maradhi ya kifua kikuu,badala yake kuwapa ushirikiano ikiwemo kuwashirikisha katika kazi zote za kiuchumi ili kupata nguvu ya pamoja itakayosaidia kuongeza kipato katika familia.

Mmoja wa watu wanaofanya kazi ya kukusanya  sampuli za makohozi  na kupeleka hospitalini kwa ajili ya uchunguzi  katika kijiji cha Nandembo Joseph Hyera alisema,katika kampeni ya mwezi Juni mwaka huu jumla ya watu 12 waligundulika kuwa na TB katika kijiji hicho.

Alisema, kati yao watu watano walifuatilia matumizi sahihi ya dawa, sita hawakuwa makini na mgonjwa mmoja alikimbia na hivyo jitihada za kumtafuta zinafanyika ili aweze kuendelea kunywa dawa.

Mwenyekiti wa kijiji  cha Nandembo Omari Mkumbi alisema, katika kijiji hicho kuna watu wakiwemo watoto walio na umri chini ya miaka mitano waliobainika kuwa na ugonjwa wa kifua kikuu,hata hivyo baadhi walioanzishiwa dawa waliacha kunywa.

Alisema, serikali ya kijiji inafanya jitihada ya kuwatafuta na katika msako huo wamefanikiwa kuwapata watu wawili ambao walikimbilia mashambani na tayari wamerudishwa kwenye utaratibu wa kunywa dawa.

Amepongeza jitihada zinazo fanywa na  hospitali ya wilaya chini ya kitengo cha kifua kikuu na ukoma kufanya kampeni ya uchunguzi wa vimelea vya ugonjwa huo kwa watoto walio na umri chini ya miaka mitano na watu wazima katika maeneo mbalimbali.

TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA YAWAALIKA WANANCHI KUPATA HUDUMA KATIKA MAONESHO YA NANENANE 2019, SIMIYU

$
0
0
Naibu Mrajis wa Vyama vya Ushirika nchini, Bw. Charles Malunde anatoa wito kwa wanaushirika na wananchi wote kufika katika Maonesho ya Nanenane yanayofanyika Kitaifa katika viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu. Maonesho yameanza rasmi tarehe 28 Julai, 2019 na yatafikia kilele chake tarehe 8 Agosti 2019.

Kauli mbiu ya mwaka huu ni “Kilimo, Mifugo na Uvuvi katika Ukuaji wa Uchumi wa Nchi”. Wito huo umetolewa wakati Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC) ikikamilisha maandalizi ya ushiriki wa maonesho hayo katika viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu.

Bw. Malunde amesema Tume imejiandaa vyema kuhudumia wananchi viwanjani hapo. Aidha, Tume pia ipo katika kukamilisha maandalizi ya ushiriki katika maonesho ya Nanenane Kanda ya Kati yanayofanyika katika Viwanja vya Nanenane (Nzuguni) Jijini Dodoma.

Katika Maonesho hayo, Vyama vya Ushirika wa aina mbalimbali vitashiriki: Ushirika wa Mazao (Pamba, Tumbaku, Kahawa nk) Ushirika wa Umwagiliaji, SACCOS, Ushirika wa Maziwa, Ushirika wa Wafugaji Nyuki na Ushirika wa Wavuvi.

“Nichukue fursa hii kuwakaribisha wananchi kufika kwa wingi kujionea, kupata huduma pamoja na kujifunza masuala mbalimbali ya ushirika katika maonesho haya ya Nanenane. Tume imejiandaa vyema na maandalizi yote yamekamilika ili kukidhi mahitaji na matarajio ya wadau wetu,” alisema Malunde.

Tume katika maonesho hayo imepanua wigo wa upatikanaji wa elimu na huduma za ushirika kwa kushirikisha wadau mbalimbali katika sekta hii ili kuhakikisha kuwa wananchi wanapata fursa ya kujifunza mengi kuhusu ushirika.

Wadau wengine wa Ushirika watakaoshiriki ni pamoja na Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU), Shirikisho la Vyama vya Ushirika nchini (TFC), Chama Kikuu cha Ushirika wa Akiba na Mikopo (SCCULT), Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama vya Ushirika nchini (COASCO) na Mfuko wa Udhamini wa Sekta ya Fedha (FSDT).

Wanachama na Wananchi kwa ujumla watajifunza kuhusu Mfumo Jumuishi: Ushirika Afya kwa Wanaushirika, Ufunguzi wa Akaunti za benki kwa Wakulima/ Wanaushirika, Bima ya Mazao na Upatikanaji wa Mitaji kwa Wanaushirika.

Vilevile, katika banda la Ushirika kutakuwa na madarasa ambapo Wanachama, Viongozi na Watendaji wa Vyama vya Ushirika watapa fursa ya kujifunza masuala muhimu ya Kiushirika.

Rais Magufuli atoa pole kwa familia kifo cha Meja Jen Mstaafu Albert Lameck Mbowe

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mhe. Freeman Mbowe Mbunge wa Hai na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambaye pia ni kaka wa marehemu Meja Jenerali Mstaafu Albert Lameck Mbowe aliyefariki dunia julai 28,2019 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam, mara baada ya kuwasili nyumbani kwa Marehemu Salasala kwa ajili ya kutoa pole kwa Familia Julai 30,2019.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa pole kwa Familia ya Marehemu Meja Jenerali Mstaafu Albert Lameck Mbowe aliyefariki dunia julai 28,2019 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam ikiongozwa na Mhe. Freeman Mbowe Mbunge wa Hai na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambaye pia ni kaka wa Marehemu nyumbani kwao Salasala Dsm. Julai 30,2019.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akizungumza na Mhe. Freeman Mbowe Mbunge wa Hai na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambaye pia ni kaka wa Marehemu mara baada ya kutoa pole kwa Familia ya Marehemu Meja Jenerali Mstaafu Albert Lameck Mbowe aliyefariki dunia julai 28,2019 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akizungumza na Familia ya Marehemu Meja Jenerali Mstaafu Albert Lameck Mbowe aliyefariki dunia julai 28,2019 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam ikiongozwa na Mhe. Freeman Mbowe Mbunge wa Hai na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambaye pia ni kaka wa Marehemu nyumbani kwao Salasala Dsm. Julai 30,2019.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akiomba dua maalumu na Familia ya Marehemu Meja Jenerali Mstaafu Albert Lameck Mbowe aliyefariki dunia julai 28,2019 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam iliyoongozwa na Mhe. Freeman Mbowe Mbunge wa Hai na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambaye pia ni kaka wa Marehemu nyumbani kwao Salasala Dsm. Julai 30,2019. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akizungumza baada ya kuomba dua maalumu na Familia ya Marehemu Meja Jenerali Mstaafu Albert Lameck Mbowe aliyefariki dunia julai 28,2019 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam iliyoongozwa na Mhe. Freeman Mbowe Mbunge wa Hai na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambaye pia ni kaka wa Marehemu nyumbani kwao Salasala Dsm. Julai 30,2019.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akizungumza na Mhe. Freeman Mbowe Mbunge wa Hai na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambaye pia ni kaka wa Marehemu pole kwa Familia ya Marehemu Meja Jenerali Mstaafu Albert Lameck Mbowe aliyefariki dunia julai 28,2019 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam alipowatembelea nyumbani kwao Salasala Dsm kwaajili ya kutoa pole kufuatia msiba huo. Julai 30,2019. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akiagana na Waombolezaji wengine akiwa ameambatana na Mhe. Freeman Mbowe Mbunge wa Hai na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambaye pia ni kaka wa Marehemu Meja Jenerali Mstaafu Albert Lameck Mbowe aliyefariki dunia julai 28,2019 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam mara baada ya kutoa pole kufuatia msiba huo nyumbani kwao Salasala Dsm. Julai 30,2019. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akiagana na Mhe. Freeman Mbowe Mbunge wa Hai na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambaye pia ni kaka wa Marehemu Meja Jenerali Mstaafu Albert Lameck Mbowe aliyefariki dunia julai 28,2019 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam mara baada ya kutoa pole kufuatia msiba huo nyumbani kwao Salasala Dsm. Julai 30,2019.

WAZIRI WA KILIMO AWASILI MKOANI SIMIYU, ARIDHISHWA NA MAANDALIZI YA NANENANE KITAIFA

$
0
0
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) akikagua mazao mbalimbali katika banda la maonesho la Jeshi la kujenga Taifa JKT mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Nyakabindi katika Halmashauri ya mji wa Bariadi Mkoani Simiyu kwa ajili ya kujionea maandalizi ya Maadhimisho 26 ya sikukuu ya wakulima maarufu kama (Nane Nane) tarehe 29 Julai 2019.
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) akikagua mashine za kisasa za kilimo kwenye banda la maonesho la Jeshi la kujenga Taifa JKT mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Nyakabindi katika Halmashauri ya mji wa Bariadi Mkoani Simiyu kwa ajili ya kujionea maandalizi ya Maadhimisho 26 ya sikukuu ya wakulima maarufu kama (Nane Nane) tarehe 29 Julai 2019.
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) akikagua banda la maonesho la Mkoa wa Simiyu mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Nyakabindi katika Halmashauri ya mji wa Bariadi Mkoani Simiyu kwa ajili ya kujionea maandalizi ya Maadhimisho 26 ya sikukuu ya wakulima maarufu kama (Nane Nane) tarehe 29 Julai 2019. (Picha Zote Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo)
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) akikagua banda la maonesho la Mkoa Shinyanga mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Nyakabindi katika Halmashauri ya mji wa Bariadi Mkoani Simiyu kwa ajili ya kujionea maandalizi ya Maadhimisho 26 ya sikukuu ya wakulima maarufu kama (Nane Nane) tarehe 29 Julai 2019.
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) akikagua zoezi la ufugaji samaki  kwenye banda la maonesho la Jeshi la kujenga Taifa JKT mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Nyakabindi katika Halmashauri ya mji wa Bariadi Mkoani Simiyu kwa ajili ya kujionea maandalizi ya Maadhimisho 26 ya sikukuu ya wakulima maarufu kama (Nane Nane) tarehe 29 Julai 2019.

Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Simiyu


Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga tarehe 29 Julai 2019 amewasili Mkoani Simiyu kwa ajili ya kujionea maandalizi ya Maadhimisho 26 ya sikukuu ya wakulima maarufu kama (Nane Nane) yenye lengo la kuwatambua na kuwaenzi Wadau Wakuu wa Sekta ya Kilimo ambao ni Wakulima, Wafugaji, Wavuvi, Wanaushirika, Wasindikaji wa mazao ya kilimo, mifugo, uvuvi na maliasili kwa mchango wao mkubwa wanaoutoa katika kuendeleza uchumi wa nchi yetu. 


Mwaka huu wa 2019, sherehe hizi zinafanyika Kitaifa mjini Bariadi katika Viwanja vya maonesho ya kilimo Nyakabindi katika Mkoa wa Simiyu hivyo Mhe Hasunga amepongeza Uongozi wa mikoa ya Simiyu, Shinyanga na Mara kwa juhudi zao za kufanikisha kuingiza uwanjani huduma za msingi ambazo ni maji na umeme.


Alisema kuwa jukumu hilo kwa Serikali na Wadau wa Sekta Binafsi ni kuendeleza viwanja hivyo vya Nyakabindi kwa kujenga mabanda ya maonesho ya kudumu na kuboresha huduma muhimu za kijamii ili kuwe na maonesho endelevu yenye sura ya Kitaifa na Kimataifa.


Alisema kuwa Serikali kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali, imeendelea kuongeza na kuboresha viwanja vya maonesho katika Kanda mbalimbali hapa nchini, kwa sasa kuna viwanja nane (8) vya maonesho ya kilimo ambavyo ni Themi (Arusha) Kanda ya Kaskazini inayohusisha mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Manyara;  Mwl. J.K.Nyerere (Morogoro) Kanda ya Mashariki ambayo mikoa yake ni Dar es Salaam, Pwani, Morogoro na Tanga;na John Mwakangale (Mbeya) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini inayojumuisha mikoa ya Iringa, Mbeya, Ruvuma, Njombe, Katavi, Songwe na Rukwa; 


Vingine ni Nzuguni (Dodoma) katika Kanda ya Kati yenye mikoa ya Dodoma na Singida; Nyakabindi (Bariadi) Kanda ya Ziwa Mashariki yenye mikoa ya Simiyu, Shinyanga na Mara; Nyamuhongolo (Mwanza) Kanda ya Ziwa Magharibi yenye mikoa ya Mwanza, Kagera na Geita; Ngongo (Lindi) Kanda ya Kusini inayojumuisha mikoa ya Mtwara na Lindi na Fatma Mwasa (Tabora) Kanda ya Magharibi yenye mikoa ya Tabora na Kigoma.


Akizungumza na mtandao wa Wazo Huru Blog, Waziri huyo wa kilimo ameeleza kuwa Wakati wa sherehe hizo za Nane Nane, Wakulima, Wafugaji, Wavuvi, Wanaushirika na Wadau wengine katika Sekta za Kilimo; watapata fursa nzuri zaidi ya kuona na kujifunza mbinu na teknolojia sahihi za uzalishaji na usindikaji wa mazao ya kilimo, mifugo, uvuvi, maliasili na bidhaa nyinginezo kupitia Maonyesho ya Kilimo yanayoandaliwa. 


Aidha, kwa Wafanyabiashara itakuwa ni fursa nzuri ya kutangaza bidhaa zao hususani pembejeo na zana mbalimbali za uzalishaji na usindikaji wa mazao ya kilimo, mifugo, uvuvi na maliasili.


Aliitaja Kaulimbiu ya sherehe za Nane Nane Mwaka huu ni kuwa ni “Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa ukuaji wa Uchumi wa Nchi”.  Kaulimbiu hii imechaguliwa baada ya kutafakari kwa undani suala zima la Uchumi wa Viwanda unavyoweza kuchangia katika kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja, pato la Taifa na wakati huo huo kupambana na Umaskini.


"Ni ukweli ulio dhahili kuwa Kilimo ni Sekta kubwa na muhimu kwa maendeleo kutokana na mchango wake katika uchumi wa Taifa. Mfano katika mwaka 2017, Sekta ya Kilimo ilitoa ajira kwa Watanzania kwa asilimia 65.5, ikichangia asilimia 28.7 ya pato la Taifa. Sambamba na hilo Sekta ya Kilimo inachangia asilimia 65 ya malighafi za viwandani. Takwimu zinaonesha kuwa katika robo ya kwanza ya mwaka 2018 ukuaji wa Sekta ya Kilimo ulifikia asilimia 7.1" Alikaririwa Mhe Hasunga


Ameongeza kuwa Kaulimbiu ya mwaka huu inahamasisha Wakulima, Wafugaji, Wavuvi na Wanaushirika kuleta mapinduzi katika Sekta za Kilimo kwa kuzalisha kwa tija ili kukuza uchumi wa Mkulima, Mfugaji, Mvuvi mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.


Kadhalika, ametoa wito kwa Wananchi na Wadau wote kushiriki kikamilifu na kuhudhuria kwa wingi maonesho hayo kuanzia tarehe 1 hadi 8 Agosti, 2019.


MWISHO.

Makamu wa Rais azindua mradi wa kutokomeza unyanyasaji dhidi ya Wanawake

$
0
0
Na Charles James, MICHUZI TV

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amezindua mradi wa kutokomeza vitendo vya unyanyasaji na udhalilishaji dhidi ya Wanawake na Watoto kwenye masoko na kushauri elimu iendelee kutolewa kupitia mikutano ndani ya Mitaa na Kata.

Hayo ameyasema leo jijini Dodoma wakati wa uzinduzi huo ambapo amesema katika kupambana na vitendo hivyo vya kikatili Serikali imeimarisha utendaji wa madawati 417 ya jinsia na watoto yaliyopo katika vituo vya Polisi nchini kwa lengo la kuwezesha huduma stahiki kwa watu wanaofanyiwa ukatili wa kijinsia.

Mama Samia ameitaka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto pamoja na Ofisi ya Rais-TAMISEMI kushirikiana na Jumuiya ya Tawala za Mitaa ambao ndio waratibu wa mradi huo katika kuhakikisha afua zinazotekelezwa kupitia mradi huo zinakua endelevu hata pale utekelezaji wa mradi unapofikia mwisho.

" Ndugu zangu kila mmoja wetu ana haki ya kupinga na kutokomeza ukatili wa kijinsia, hivi vitendo havikubaliki na wala haviruhusiwi kisheria. Yeyote atakayethubutu kumdhalilisha mwanamke au mtoto tutamchukulia hatua kali.

" Ni jambo la aibu kuona tunatumia viungo vya wanawake kama matusi, huyu mwanamke unayemdhalilisha tukumbuke ni kama mama zetu majumbani mwetu, hatuwezi kuwa na Taifa lenye amani kama tutaruhusu vitendo hivi, tuungane katika kupiga vita na kutokomeza ukatili wa kijinsia, " amesema Mama Samia.

Akizungumzia ombwe la watoto wadogo kufanya biashara kwenye masoko, Mama Samia amezitaka kamati za masoko kuhakikisha zinashirikiana na mamlaka husika katika kuzuia watoto kufanya biashara sokoni na badala yake wawahimize kwenda shule na kuwaripoti wazazi wanaowatuma watoto wao kufanya biashara.

" Serikali yenu ya awamu ya tano iliwaahidi elimu bure kwa shule ya msingi hadi kidato cha nne. Tunapoona watoto wetu hawaendi shule na wanafanya biashara sokoni tunakua hatumtendei haki Rais wetu Dk John Magufuli kwa zawadi ya elimu bure aliyotuletea. Tuwazuie watoto kufanya biashara sokoni na tushirikiane kuwapeleka shule," amesema Mama Samia.

Aidha katika kutekeleza mradi huo, Mhe Makamu wa Rais amekabidhi Pikipiki 14 kwa ajili ya wataalam wa Maendeleo ya Jamii wa Mkoa wa Dodoma kwa Kata za Halmashauri ya Chamwino na kuielekeza Wizara kuendeleza utaratibu huo wa kupatia wataalamu hao usafiri ili iwe rahisi kwao kuwafikia wanawake wengi hususani wa vijijini na kuwaunganisha na fursa za kiuchumi.

Kwa upande wake Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe Ummy Mwalimu amemshukuru Makamu wa Rais kwa kuzindua mradi huo ambao utakua msaada mkubwa katika mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia.

" Mhe Makamu wa Rais kama Wizara tumejipanga katika kuhakikisha tunaongeza elimu zaidi kwa wananchi iki tuzidi kupunguza wimbi la vitendo hivi, lengo letu ni kutokomeza kabisa vitendo hivi ili kuwa na Taifa imara ambalo litakua na mshikamano na amani baina yetu bila kujali huyu ni Mwanaume au Mwanamke," amesema Waziri Ummy.

Nae Mwenyekiti wa ALAT Mhe Gulamhafeez Mukadam amesema kuna changamoto kwenye dira ya pamoja juu ya utokomezaji wa vitendo vya ukatili wa kijinsia jambo ambalo linaleta athari ya maendeleo ya wanawake na hivyo kuzorotesha uchumi wa Nchi.

" Nimpongeze Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Mhe Godwin Kunambi kwa namna ambavyo amekua msaada kwa akina Mama wa Jiji hili kwa kuwapatia mikopo inayowawezesha kufanya biashara zao. Serikali za Mitaa jukumu lao ni kuwawezesha wananchi wao kuzipata fursa.

" Lakini pia kuna changamoto ya masoko, lugha chafu kwa wanawake sokoni hizi changamoto zinapaswa kushughulikiwa na kutokomezwa kabisa. Tukiwawezesha wanawake na kuwaepusha na vitendo vya unyanyasaji tutakua tunatengeneza Taifa imara na madhubuti na kuweza kufikia azma ya Mhe Rais ya uchumi wa kati kupitia viwanda," amesema Mhe Mukadam.
 Makamu wa Rais Mhe Mama Samia Suluhu Hassan akikata utepe kuashiria ufunguzi wa mradi wa kutokomeza vitendo vya unyanyasaji na ukatili dhidi ya wanawake na watoto katika maeneo ya masoko. Uzinduzi huo umefnyika jijini Dodoma.
 Wananchi waliohudhuria uzinduzi wa mradi wa kutokomeza vitendo vya kikatili dhidi ya wanawake wakimsikiliza mgeni rasmi ambaye ni Makamu wa Rais Mhe Mama Samia Suluhu Hassan (hayupo pichani) jijini Dodoma.
Maafisa Maendeleo ya jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino wakiwa na pikipiki walizokabidhiwa na Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan jijini Dodoma. Pikipiki hizo zimelenga kuwasaidia katika kuwafikia kundi kubwa la wanawake ambao wanafanyiwa unyanyasaji wa kijinsia.

ANAYETUHUMIWA KUUA MKE WAKE NA KISHA KUMCHOMA MOTO KWA GUNIA MBILI ZA MKAA AFIKISHWA KORTINI

$
0
0
*Ni yule mfanyabiashara anayeishi Kigamboni jijini Dar ,ajificha sura yake kwa kujifunika kofia ili asionekane 

Na Karama Kenyunko, Michuzi Tv

MFANYABIASHARA Khamis Luwonga maarufu kwa jina la Meshack (38), anayedaiwa kumuua mkewe na kisha kumchoma na moto kwa kutumia magunia mawili ya mkaa, amefikishwa katika Mahakama Hakimu Mkazi Kisutu kujibu tuhuma hizo za mauaji ya mke wake, Naomi Marijani.

Akisoma hati ya mashtaka Wakili wa Serikali Mwandamizi Wankyo Simon amedai leo mahakamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi Salum Ally kuwa mshtakiwa anatuhumiwa kwa kosa moja la mauaji  kinyume cha Sheria ya kanuni ya adhabu namba 196 sura 16 kama kilochofanyiwa marejeo mwaka 2002.

Katika kesi hiyo ya mauaji namba 4 ya mwaka 2019, mshtakiwa Luwonga Mkazi wa Kigamboni, Dar es Salaam anadaiwa Mei 15,mwaka huu wa 2019 akiwa Gezaulole eneo la Kigamboni alimuua Naomi Marijani.

Hata hivyo, mshtakiwa hakuruhusiwa kujibu kitu chochote mahakamani hapo kwa kuwa mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu haina mamlaka ya kusikiliza kesi za mauaji ambazo kwa kawaida zinasikilizwa mahakama kuu.Kwa mujibu wa upande wa mashtaka upelelezi katika kesi hiyo bado haujakamilika na kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 13, mwaka huu kwa ajili ya kuangalia kama upelelezi utakuwa umekamilika au la.

Mshtakiwa huyo pindi anatolewa mahabusu na kupandishwa mahakamani, alifunika sura yake kwa kutumia kofia ya koti lake kwa lengo la kutokuonekana sura yake.Mwanzoni mwa Julai mwaka huu, mshtakiwa Meshack alisambaza tangazo magazetini na kwenye mitandao ya kijamii kuwa anamtafuta mkewe ambaye alitoweka ghafla lakini baadae Jeshi la Polisi kupitia Mkuu wa Upepelezi wa kanda hiyo, Camillius Wambura alitangaza kumshikilia Luwonga akidaiwa kumuua na kisha aliuchoma moto mwili wa mkewe. 

WAZIRI LUGOLA ATANGAZA VITA KWA YEYOTE ATAKAYEMCHUKUA MTOTO AU MTU MZIMA KWA KUMDANGANYA NA KUMFANYA MTUMWA

$
0
0
*Asema Serikali ipo macho, wahusika watafikiwa na kupewa adhabu kali kwa mujibu wa sheria

Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

WAZIRI wa mambo ya ndani Kangi Lugola ametangaza vita kali dhidi ya watu wanaowarubuni na kuwadanganya watoto na watu wazima kwa kigezo cha kuwapatia maisha mazuri na mwishowe kuwapa malipo duni, mateso na kufanywa watumwa.

Akizungumza leo katika maadhimisho ya siku ya kupinga biashara ya usafirishaji haramu wa binadamu duniani yenye kauli mbiu ya "Ungana na Serikali Kutokomeza Biashara Haramu ya Usafirishaji wa Binadamu, Wahanga Sio Wahalifu Walindwe" yalikofanyika katika viwanja wa Mnazi mmoja jijini Dar es Salaam Waziri Kangi amesema madhara ya usafirishwaji wa binadamu na kuwatumikisha ni makubwa na hayawezi kufumbiwa macho na hatua kali za kisheria dhidi ya wahusika zitachukuliwa ikiwepo kutumikia vifungo gerezani.

Amesema ikiwa ni mara ya pili taifa likiadhimisha siku hiyo, malengo kwa mwaka huu ni kuadhimisha siku hiyo kwa kupinga vikali usafirishwaji haramu wa binadamu, kuelimisha jamii kuhusiana na madhara ya usafirishwaji wa binadamu na hatua zinazochukuliwa dhidi ya wahusika pamoja na kutoa shukrani hasa kwa shirika la uhamiaji la IOM kwa kutoa ushirikiano wa karibu zaidi na Serikali katika kuhakikisha vitendo vya namna hiyo vinakoma.

Waziri Lugola amesema katika kuhakikisha janga hilo linakoma kuanzia Januari 2017 hadi Juni 2019 mafunzo maalumu yametolewa kwa wadau wapatao 600 wakiwemo walezi wa vituo vya waathirika wa usafirishwaji huo, maaskari, mawakili na mahakimu katika kuhakikisha wanapambana na janga hilo katika maeneo yao ya kazi.

Imeelezwa kuwa waathirika wa janga hilo ni vijana, watoto, na wanawake wenye umri kati ya miaka 13 hadi 24 ambao huchukuliwa kutoka ngazi za Wilaya, Mikoa na taifa na wengine kupelekwa nje ya nchi wakihaidiwa kupewa maisha bora kwa familia zao lakini huishia katika utumwa, kubebeshwa dawa za kulevya, kuuza pombe haramu ya gongo pamoja na kutumikishwa kingono.

Pia ubalozi wa Marekani umetuma ujumbe wa kuipongeza Tanzania kwa kuendelea kupambana na janga hilo la usafirishaji haramu wa binadamu na kuahidi kushiriki katika kutokomeza kabisa janga hilo linaloathiri jamii hasa vijana na watoto katika masuala ya kijamii na uchumi.

Ujumbe huo umeeleza kwamba; "upepo utapita, kwa kuwa usafirishwaji ni wa ndani na nje ya nchi huku asilimia 70 ya waathirika wakiwa ni kutoka ndani ya nchi husika hivyo lazima tupambane kwa kuwalinda vijana na watoto wetu" umeeleza.

Vilevile ubalozi huo umeshauri adhabu kali dhidi ya wahusika na wao kama balozi hapa nchini wapo pamoja katika kupinga janga hilo ambalo sio la asili bali hutengenezwa na kutekelezwa na watu.

Kwa upande wake Mkuu wa shirika la kuwahudumia  wahamiaji nchini (IOM) Dkt. Qasim Sufi amesema kuwa usafirishaji haramu wa binadamu umeathiri nchi nyingi hasa katika sekta za kiuchumi huku waathirika wakipata majanga kama magonjwa, vifo na maumivu yanayotokana na harakati za kutengeneza maisha bora kwa familia zao.

Amesema wanawake na watoto wamekuwa waathirika wakubwa wa janga hilo na amezishauri nchi mbalimbali kuwapokea wahamiaji na kuwapa haki zao za msingi na kibinadamu katika nchi wanazofanya kazi.

Aidha amesema kuwa juhudi zinazofanywa na serikali ya Tanzania zinatia moyo na tatizo hilo linaweza kumalizwa kabisa kutokana na uwepo wa wadau wengi wanaopinga usafirishwaji haramu wa binadamu, na kueleza kuwa tafiti zaidi zinaendelea kufanywa  zitaisadia Serikali katika kutatua tatizo hilo.

Awali akitoa taarifa ya kamati ya kupambana na usafirishwaji haramu wa binadamu, mwenyekiti wa kamati hiyo Adatus Magere amesema kuwa wahanga wa janga hilo sasa wanajikwamua kupitia fursa zilizopo nchini ambapo tangu kuanzishwa kwake mwaka 2008 mapambano yameshika kasi na waharifu waliokutwa na hatia wengi wao wapo gerezani wakitumikia kifungo.

Ametoa mwito kwa jamii kutohadaika na mafanikio ya muda mfupi na kuwashauri vijana kutumia fursa za nyumbani katika kujipatia maendeleo.
 Jeshi la uhamiaji nchini likiwa katika maandamano katika kuadhimisha siku ya kupinga Biashara haramu ya usafirishaji wa binadamu duniani yaliyofanyika leo katika viwanja vya Mnazi mmoja jijini Dar es Salaam.
Waziri wa mambo ya ndani Kangi Lugola akizungumza wakati wa maadhimisho ya siku ya kupinga biashara haramu ya usafirishaji wa binadamu ambapo amewaonya wote wenye tabia ya kuwarubuni watoto na watu wazima na hatimaye kuwafanya watumwa kuwa sheria inasimamia makali yake, leo jijini Dar es Salaam.

 Mwenyekiti wa kamati ya taifa ya kuzuia na kupambana na biashara haramu ya usafirishaji wa binadamu Adatus Magere akizungumza katika maadhimisho hayo na kuishauri jamii kutohadaika na mafanikio ya muda mfupi, leo jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa mambo ya ndani Kangi Lugola akisalimiana na wageni mbalimbali waliohudhuria  maadhimisho ya siku ya kupinga biashara haramu ya usafirishaji wa binadamu ambapo mabalozi na wawakilishi wamevutiwa na kasi ya Tanzania katika kupambana na kukomesha biashara hiyo haramu ya kusafirisha binadamu, leo jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa mambo ya ndani Kangi Lugola akipata maelekezo kutoka kwa washiriki wa maonesho walioshiriki maadhimisho ya siku ya kupinga biashara haramu ya usafirishaji wa binadamu duniani ambapo wadau wengi wakiwemo mabalozi wamehaidi kushirikiana na Tanzania katika kupinga janga hilo, leo jijini Dar es Salaam.

JESHI LA POSLI LASEMA MWANDISHI ERICK KABENDERA HAKUTEKWA,YAMNASA ASKARI FEKI

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Michuzi TV

Jeshi la Polisi Kanda Maalum limesema kuwa Mwandishi wa Erick Kabendera hakutekwa bali Polisi ndio limemkamata kwa mahojiano.

Akizungumza na Waandishi habari Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Razaro Mambosasa amesema kuwa Mwandishi huyo Polisi walimwita akaikadi wito wa Jeshi hilo na kuamua kwenda kumkmata.

Amesema wito wa Polisi kwa Kabendera ilikuwa ni kuhoji uraia wake ambapo kwa mujibu  wa Jeshi la Polisi linalomamlaka ya kufanya hivyo na kwenda mbele katika idara ya uhamiaji.

Kamanda Mambosasa amesema kuwa taarifa mbalimbali katika mitandao ya jamii  lakini sio Michuzi Blog zilikuwa zikidai kuwa katekwa wakati hakuna ukweli huo.

Wakati huo Jeshi la Polisi limemkamata Askari  Feki Daud Ramadhan katika maeneo ya Tabata kwa kujiweka nyota moja ya cheo.

Kamanda Mambosasa amesema Askari Feki huyo alikuwa akifanya njia ya kutapeli watu kwa kutumia sare za Polisi, simu ya mawasiliano ya upepo,pamoja na pingu.Kamanda Mambosasa amesema watampandisha kizimbani kujibu tuhuma hizo.
 Askari feki aada ya kunaswa na jeshi la Polisi
 Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam Razaro Mambosasa akizungumza na waandishi habari kuhusiana taarifa mbalimbali ikiwemo ya Mwandishi wa Habari Erick Kabendera. 
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam Razaro Mambosasa akimuonesha Askari Feki Daud Ramadhan kwa waandishi habari.

Mimba za Utotoni Tabora Bado ni Tatizo

$
0
0
Na, Editha Edward-Tabora 

Katika Kukabiliana na tatizo la mimba za utotoni ambalo limekuwa chanzo kikubwa cha kukwamisha ndoto za Watoto wa kike, wadau mbalimbali weendelea kuunga mkono jitihada za Serikali za Kukabiliana na tatizo hilo lengo ni kumuwezesha mtoto wa kike aweze kupata elimu

Akikabidhi Magodoro yatakayoyumika katika mabweni ya wasichana wilayani Uyui mkoani Tabora, Naibu Katibu Mkuu chama cha kutetea haki za maslahi ya walimu Tanzania Sosipeter Ndabagoye ametoa wito kwa jamii kuona umuhimu wa kuunga mkono jitihada za Serikali katika kuboresha Elimu

Nae mkuu wa Wilaya ya uyui Gift Msuya amesema Lengo la wilaya hiyo ni kuhakikisha linaondokana na changamoto hiyo ya mimba za utotoni kwa kuwatengenezea mazingira Mazuri ili kuwawezesha Wanafunzi kufikia Malengo yao. 

Aidha changamoto ya mimba za utotoni kwa wanafunzi wa kike ambapo katika wilaya hiyo ni karibu nusu ya wanafunzi wanaohitimu Elimu ya Msingi hushindwa kuendelea na Masomo ya sekondari kutokana na kupata mimba hali iliyosababisha Serikali ya Wilaya hiyo kuanzisha kampeni ya "Nishike Mkono Tuwavushe Salama " lengo likiwa ni kuboresha mazingira yatakayomuwezesha mtoto wa kike kupata Elimu.
Pichani ni Naibu Katibu Mkuu wa chama cha kutetea haki za maslahi ya walimu Tanzania Sosipeter Ndabagoye akikabidhi Magodoro katika mabweni ya wasichana wilayani Uyui.

 Pichani ni Mkuu wa Wilaya ya Uyui Gifti Msuya akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.
 Wanafunzi wa kike wa shule ya sekondari Wasichana uyui wakimsikiliza naibu  katibu  mkuu wa chama cha  kutetea haki za maslahi ya walimu Tanzania( pichani hayupo).

IGP SIRRO APOKEA MSAADA WA MAGARI MAWILI NA PIKIPIKI KUMI.

$
0
0
Inspekta Jenerali wa Polisi IGP Simon Sirro akikata utepe pamoja na maafisa wawakilishi wa Shirika la Upelelezi la Ujerumani (BKA) Bwana Rene Becker (kulia) na Bwana Harald Gessner (kushoto) kuashiria makabidhiano ya msaada wa magari mawili na pikipiki kumi kwa Polisi kutoka Shirika la Upelelezi la Ujerumani (BKA). Hafla ya kupokea msaada huo imefanyika leo Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Jijini Dar es Salaam. Picha na Jeshi la Polisi. 
Inspekta Jenerali wa Polisi IGP Simon Sirro akipokea pikipiki miongoni mwa msaada wa magari mawili na pikipiki kumi kutoka kwa maafisa wawakilishi wa Shirika la Upelelezi la Ujerumani (BKA) Bwana Rene Becker (kushoto) na Bwana Harald Gessner. Hafla ya kupokea msaada huo imefanyika leo Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Jijini Dar es Salaam. Picha na Jeshi la Polisi.
Inspekta Jenerali wa Polisi IGP Simon Sirro akiwasha gari miongoni mwa msaada wa magari mawili na pikipiki kumi kutoka kwa maafisa wawakilishi wa Shirika la Upelelezi la Ujerumani (BKA) Bwana Rene Becker (kulia) na Bwana Harald Gessner. Hafla ya kupokea msaada huo imefanyika leo Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Jijini Dar es Salaam. Picha na Jeshi la Polisi. 

MWENGE WA UHURU WAZINDUA MRADI WA MAJI KATA YA MUHEZA ,KIBAHA UTAKAONUFAISHA WAKAZI 2,541

$
0
0
NA MWAMVUA MWINYI,KIBAHA

MWENGE Wa Uhuru ,umezindua mradi wa maji kata ya Muheza,Mjini Kibaha ,Pwani wenye thamani ya milioni 359.5, ambao chanzo chake cha maji ikiwa ni mto Ruvu kupitia DAWASA,huku ukitarajiwa kunufaisha wakazi 2,541.

Mhandisi wa maji halmashauri ya mji huo,Grace Lyimo alimweleza kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa,Mzee Mkongea Ali kuwa ,mradi huo ni mkombozi kwa wakazi hao.

Alisema ,mradi huo ni kati ya miradi iliyopo chini ya programu ya Taifa ya maji na usafi wa mazingira vijijini ambapo ulichelewa kukamilika kutokana na uhaba wa fedha.

Grace alieleza ,ulisanifiwa na kusimamiwa na mhandisi mshauri M/S Netwas (T) Ltd wa Dar es salaam mwaka 2009/2010 ,Halmashauri na jamii ilishirikishwa katika hatua zote za kuibua mradi mpaka usanifu wake.

"Ujenzi ulianza mwaka wa fedha 2013/2014 chini ya mkandarasi M/S Federick company Ltd wa Dar es salaam kwa gharama ya sh.mil 359.577.570 "

Grace alibainisha ,kutokana na uhaba wa fedha kutoka serikali kuu ,mradi huu ulisimama kwa muda wa takriban miaka 2 mwaka 2015/2016 na kuendelea tena na ujenzi mwanzoni mwa mwaka 2017 na kukamilika mwezi agosti 2018.

"Mradi huo ulikuwa na vituo vya jamii vya kuchotea maji Tisa ambavyo vilikabidhiwa kwa uongozi wa watumia maji Muheza kwa ajili ya usimamizi.Hii iliweza kuongeza vituo viwili na kufanya jumla ya vituo vya jamii kuwa 11 na wateja binafsi 240 pamoja na kupeleka maji mtaa jirani wa Lumumba"

"Baada ya mradi kutanuka na maeneo mengine kupata huduma uongozi wa jumuiya ya watumiaji maji uliomba mradi ukabidhiwe DAWASA ili kusaidia huduma kuwa endelevu na kupunguza gharama za huduma ya maji"alifafanua Grace.

Mkongea aliukubali mradi huo na kusema maji ni haki ya kila mtu ,na aliiomba jamii kutunza vyanzo vyake ili miundombinu ya maji iweze kudumu.

Alisema, serikali inatekeleza kauli mbiu ya KUMTUA MAMA NDOO YA MAJI KICHWANI na kutekeleza sera ya maji ya mwaka 2002 ya kuhakikisha wananchi wanapata maji safi na salama katika umbali usiozidi mita 400 kila upande kwa kila kaya pamoja na utunzaji wa vyanzo vya maji.

Awali mkuu wa wilaya ya Kibaha, Assumpter Mshama alisema ,mwenge wa Uhuru umepitia miradi 11 ,yenye thamani ya sh .bilioni 2.464.Assumpter alielezea, mradi mmoja umezinduliwa,mmoja umefunguliwa,miwili imewekwa mawe ya msingi na miradi saba imetembelewa.


MAJALIWA AZUNGUMZA NA WACHEZAJI TIMU YA SOKA YA NAMUNGO NA KUWAKABIDHI MIPIRA

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa leo Julai 30, 2019 amekabidhi   mipira ipatayo 30 kwa timu ya soka ya Namungo. Pichani, Mheshimiwa Majaliwa akimkabidhi kocha Mkuu wa timu hiyo, Mroki Chrisswa , moja kati ya mipira hiyo baada ya kuzungumza na wachezaji kwenye hoteli ya Sea View mjini Lindi.  Wa pili kushoto ni Mke wa Waziri Mkuu, Mama Mary Majaliwa na wa pili kulia ni Mkuu wa wilaya ya Lindi Mjini,na kaimu Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Shaibu Ndemanga. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na wachezaji wa timu ya soka ya Namungo, baada ya kuzungumza nao kwenye hoteli ya Sea View mjini Lindi Julai 30, 2019. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na wachezaji wa timu ya soka ya Namungo, baada ya kuzungumza nao kwenye hoteli ya Sea View mjini Lindi Julai 30, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

MAMIA WAJITOKEZA MAZISHI YA DADA WA MBUNGE WA JIMBO LA SINGIDA MAGHARIBI

$
0
0
Waombolezaji wakishusha kaburini jeneza lenye mwili wa Lucylight Ndekeja ambaye ni dada yake Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi, Elibariki Kingu wakati wa mazishi yake yaliyofanyika katika makaburi ya Kanisa la Katoliki Parokia ya Sepuka wilayani Ikungi mkoani Singida jana.
Waombolezaji wakiwa kwenye ibada ya mazishi nyumbani kwao na marehemu Kata ya Sepuka.
Baadhi ya wafanyakazi wenzake na marehemu na waombolezaji wengine wakiwa kwenye ibada hiyo.
Waombolezaji wakiwa kwenye ibada ya mazishi nyumbani kwao na marehemu Kata ya Sepuka.
Ndugu jamaa na marafiki wakiwa kwenye ibada hiyo. Wa tatu kutoka kulia ni mume wa marehemu.
Mjomba wa marehemu akiwa ameshika tama kwenye ibada hiyo.
Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Singida, Elekizandya Katabi (kushoto) na Katibu wa CCM Wilaya ya Ikungi, Novatus Kibaji wakiomba kabla ya kushiriki sakramenti takatifu katika ibada hiyo.
Mbunge Mteule wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu akitoa salamu za rambirambi katika ibada hiyo.
Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Ikungi, Mika Likapakapa alitoa salamu za rambirambi.Wengine ni viongozi kutoka kata zote za jimbo hilo wakisubiri kutoa rambirambi zao.
Katibu wa CCM Mkoa wa Singida, Elekizandya Katabi akikabidhi rambirambi kwa mmoja wa wanafamilia ya Marehemu.
Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi, Elibariki Kingu akitoa shukurani kwa niaba ya wanafamilia kabla ya kufanyika mazishi hayo.
Mazishi yakifanyika
Padre wa Kanisa Katoliki Parokia ya Yoseph Mfanyakazi ya Mandewa, Paterine Mangi, akisimika msalaba juu ya kaburi la marehemu Lucylight Ndekeja baada ya kukamilika kwa mazishi.
Mama wa marehemu akiweka shada la maua kwenye kaburi la mtoto wake.
Mume wa marehemu akiwa shada la maua kwenye kaburi na mke wake.
Watoto wa marehemu wakiweka shada la maua kwenye kaburi la mama yao. 
Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi na Singida Mashariki, Elibariki Kingu na Miraji Mtaturu (kulia) wakiweka kaburini shada la maua.

KATIBU MKUU SEKTA YA UJENZI AFANYA ZIARA MKOANI SONGWE

$
0
0
Jengo la ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Songwe likiwa katika hatua ya awali ujenzi.
 Muonekano wa jengo la hospitali ya wilaya ya Tunduma pindi ujenzi wake utakapokamilika. Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.
Katibu Mkuu wa Sekta ya Ujenzi Arch. Elius Mwakalinga, akikagua maendeleo ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Tunduma mkoani Songwe.
Msimamizi wa ujenzi wa mradi huo Mhandisi Fidelis Cosmas, akimuonesha Katibu Mkuu Arch. Elius Mwakalinga, vipimo vilivyotumika kwenye mradi wa ujenzi wa hospitali ya wilaya ya tunduma. Ujenzi huu unasimamiwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA).
Katibu Mkuu wa Sekta ya Ujenzi Arch. Elius Mwakalinga, akikagua jengo la Mkuu wa Mkoa wa Songwe linalosimamiwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA).
Katibu mkuu wa sekta ya ujenzi arch. Elius Mwakalinga, akitoa maelekezo kwa meneja wa wakala wa majengo (tba) mkoani songwe, arch. Christina Shayo kuhusu marekebisho kwenye mradi wa ujenzi wa ofisi ya mkuu wa mkoa songwe.

WAKANDARASI WATAKIWA KUZINGATIA MAELEKEZO YA MIKATABA YAO

$
0
0
Na Woinde Shizza Michuzi Tv,Arusha


Wakandarasi mbalimbali wanaotengeneza Barabarani kwa kiwango cha Lami katika jiji la Arusha, wametakiwa kuzingatia maelekezo ya mikataba yao inayowataka kutoa kipaumbele cha ajira kwa wananchi wanaoishi maeneo ya mradi.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Tarafa wa kata ya Themi ,Felisiani Mtahengerwa wakati wa ziara ya Kamati ya siasa ya CCM kata ya Levolosi ya kutembelea na kusimamia miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali.

Miradi waliotembelea ni pamoja na kukagua Barabara zenye urefu mita 585 zinazojengwa katika kata hiyo na kampuni ya ujenzi ya Ravji ya Mjini Moshi,Mkoani Kilimanjaro,Soko la Kilombero pamoja na ukarabati wa kituo cha Polisi cha Kilombero alichobaini kuwa na changamoto kubwa ya kuvuja wakati wa mvua

Felician aliitaka kampuni hiyo ya ujenzi wa barabara kuwapatia ajira vijana waliopo katika eneo la miradi katika kata hiyo bila kujali itikadi zao za kisiasa pamoja na kuikata kampuni hiyo kukamilisha mradi huo kwa wakati na kwa ubora unaohitajika

Akiongea wakati akiwa kwenye soko la Kilombero alisema kuwa serikali inaomba wadau wa maendeleo kuona umuhimu wa kukirabati kituo cha Polisi cha Kilombero kwa kujitolea thamani za ofisi sanjari na ukrabati wa paa na kusaidia ulipaji wa deni la maji kwani kituo hicho kinasaidia katika suala zima la usalama katika eneo hilo.

"Unajua suala hili sio la lazima ni hiyari ya wadau wa maendeleo kuona umuhimu wake kwani kituo hiki kinasaidia sana katika kulinda Mali zao na usalama katika eneo hili hivyo waone umuhimu wa kuisaida serikali kujitolea"

Naye msimamizi wa kampuni hiyo ya ujenzi ya Ravji ,Peter Mahushi alisema atahakikisha kampuni yake inamaliza Kazi katika muda uliopangwa na kwamba ifikapo September 14 mwaka huu watakabidhi Miradi huo.

Alisema kuwa wamejipanga kuhakikisha wanatoa kipaumbele kwa vijana wa kata hiyo kwa kuanza na vijana watano na kuwataka viongozi hao kuwapelekea majina wao wataangalia na kuona wanauwezo kiasi gani na kuahidi kuwa changamoto zote watazifanyiakazi ndani ya muda uliopangwa.

Kwa upande wake mwenyekiti wa CCM kata ya Levolosi,Tabu Simile amesema kuwa chama cha mapinduzi kimeridhishwa na ujenzi wa miradi ya Barabara kwa kuona thamani ya fedha inayotolewa ikitumika kama ilivyokusudiwa.

Alisema kuwa wao kama chama wameridhishwa kwa kiasi kikubwa na utekelezaji wa ilani na changamoto ndogo walizokutana nazo wanawataka serikali kuhakikisha inazitatua kama ilivyoahidi ndani ya muda kuokoa na kwenda sambamba na kasi ya ujenzi wenye viwango vinavyokubalika.

Miradi hiyo ya ujenzi wa barabara za lami katika jiji la Arusha inatekelezwa kwa kiwango kikubwa na serikali chini ya wakala wa barabara za mijini na Vijijini (Tarura ) jambo ambalo linazidi kuung'arisha mji wa Arusha ,ambapo wananchi wanafurahi kuona kodi wanazotoa zinatumika kuwaletea maendeleo ipasavyo.
Kamati ya siasa ya chama cha mapinduzi CCM kata ya Levolosi wakitembelea baadhi ya barabara zinazojengwa kwa kiwango cha lami katika kata hiyo  inayotekelezwa na serikali.



WAZIRI WA NISHATI AAGIZA MKANDARASI KUTOA AJIRA 50 KWA VIJANA WA KARATU

$
0
0
Na Woinde Shizza Michuzi Tv, Arusha

WAZIRI wa Nishati Dk.Medard Kalemani amemwagiza Mkandarasi wa Kampuni ya Nipo Group Mhandisi Shija Magese kuhakikisha anatoa ajira kwa vijana 50 wa Kijiji cha khusumay Wilayani Karatu, ili wasaidie kazi za uwekaji umeme kwenye Vijiji 39 vya wilaya hiyo.

Alitoa agizo hilo jana alipotembelea Wilaya hiyo na kuzindua Rea awamu ya tatu, iliyofanyika kiwilaya katika Shule ya Sekondari ya Baray Khusumay na kuhudhuriwa na wananchi wa Wialaya hiyo.

Alisema ameagiza utoaji wa ajira hiyo kwa sababu mkandarasi huyo amepewa kumaliza kazi ya uwekeaji miundombinu ya umeme na kuwaunganishia wananchi nishati hiyo kwa muada wa miezi 24, lakini mpaka sasa bado nusu ya kazi hajamaliza.

“Sasa naagiza ajiri vijana 50 wa eneo hili ili muda wako tuliowekeana mkataba umalize ni Juni mwaka 2020, lakini nataka umalize kazi hii Desemba 30 mwaka huu, sasa hawa vijana watakusaidia na wakati huo watanufaika na ajira na Meneja wa Wilaya simamia hawa,”alisema

Dk.Kalemani aliahidi kurudi kijijini hapo kufuatilia kama kazi hiyo imeisha kwa wakati muafaka ili wananchi wapate umeme na kuzalisha viwanda vidogovidogo.

Aidha aliagiza Meneja wa Wilaya hiyo Tanesco, Edward Mwakapuja kufungua vituo kwenye vijiji husika ili wananchi wapate unafuu wa kuwafikia na kulipa Sh.27,000 ili waunganishiwe umeme huo wa Rea.

Pia aliwataka Wafanyakazi wa Tanesco kuhakikisha wanafanya kazi za kuhudumia wananchi na kuepuka kuvaa suti kama wanakwenda Kanisani.

“Nimepiga marufuku wafanyakazi Tanesco kuvaa suti labda kama mnaenda kanisani Jumapili, sababu hapa kazi tu, suti na kazi wapi na wapi acheni kabisa pigeni kazi,”alisema Aliwasisihi pia wanachi hao kutunza miundombinu ya umeme wakiwekewa ili waendelee kunufaika nao na kupata maendeleo.

Dk.Kalemani aliwaagiza wanafunzi wa Shule yya Sekondari ya Baray Khusumay kuhakikisha wanafanya vizuri masomo yao na kufaulu vizuri kwa sababu umeme wameshapata.“Someni usiku na msachan lakini pia umeme huu utawamulika msifanye maovu maana shule hii ya wavulana na wasichana mkisimama kwa yale mambo yenu umeme huu utawamulika, someni mfaulu na shule hii mpya,”alisema

Kuhusu suala la kukatika kwa umeme aliagiza Tanesco kuhakikisha wanamaliza tatizo hilo harka, sababu umeme upo wa kutosha hadi ziada.

Mkuu wa Wilaya ya Karatu Theresia Mahongo alishukuru serikali kwa kuwafikishia umeme kijiji hicho ambacho tangu Uhuru hakijawahi pata umeme, lakini aliomba Waziri kufuatilia changamoto ya kukatika kwa umeme mara kwa mara wilayani humo.

“Tunaamini tatizo hili litaisha baada ya uzinduzi wa Rea awamu ya tatu kufanyika, sababu kukiwa na umeme tunaamini usalama utakuwa juu na hata ufaulu kwenye shule utaongezeka,”aisema

Akijibu suala la kukatika kwa umeme, Meneja wa Tanesco Mkoa wa Arusha, Mhandisi Herin Mhina alisema sababu ya kukatika kwa umeme huo kulitokana na utengenezaji wa nguzo zaidi ya 600 ambazo zimewekwa mpya.

Kwa upande wake Mkandarasi wa kampuni ya Nipo Group Shija Magese, aliahidi kumaliza kazi hiyo Desemba mwaka huu na mpaka sasa kati ya Vijiji 39 anavyotakiwa kuweka umeme wa Rea, vijiji 23 ameshajenga miundombinu ya kuweka umeme na kati ya hivyo nane ameshawasha umeme. 
Wafanyakazi kutoka kampuni ya Booygues Energies &services wakiendelea na Mradi wa ujenzi wa njia za kusafirisha umeme Kenya-Tanzania Power Interconnection (KTIPIP)ZTK wa laini kubwa ya msongo wa kilovolti 400 inayoanzia Singida unapita Babati nakuja mkoa wa Arusha hadi Namanga ,ujenzi huo unaendelea katika kijiji cha Kisongo jijini Arusha (Picha na Woinde Shizza, Arusha 
WAZIRI wa Nishati Dk.Medard Kalemani akiongea na wananchi .
WAZIRI wa Nishati Dk.Medard Kalemani alipotembelea Wilaya ya Karatu na kuzindua Rea awamu ya tatu, iliyofanyika kiwilaya katika Shule ya Sekondari ya Baray Khusumay 
WAZIRI wa Nishati Dk.Medard Kalemani akiongea na viongozi wa Tanesco pamoja na mkuu wa wilaya ya karatu wakati alipotembelea kituo cha Tanesco cha wilaya hiyo .

MAKAMU WA RAIS AONYA MATUSI NA VITENDO VYA UDAHALILISHAJI MASOKONI

$
0
0

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akionesha Bango Juu kama ishara ya Uzindua rasmi Mradi wa kutokomeza vitendo vya Unyanyasaji na Udhalilishaji Dhidi ya Wanawake na Watoto katika maeneo ya Masoko pamoja na ugawaji wa Pikipiki 14 kwa Maafisa wa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya wilaya ya Chamwino Dodoma kwa ajili ya kuongeza kurahisisha Usafiri katika kufanikisha kutokomeza Ukatili na Unyanyasaji kwa Wanawake na watoto . Hafla hiyo imefanyika leo Julai 30,2019 katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma. Katikati Mwenyekiti wa ALAT Taifa na Meya wa Manispa ya Shinyanga Mhe. Gulamhafeez Z. Mukadam na Waziri wa Afya na Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akimkabidhi Funguo ya Pikipiki Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith S. Mahenge Baada ya kuzindua rasmi Mradi wa kutokomeza vitendo vya Unyanyasaji na Udhalilishaji Dhidi ya Wanawake na Watoto katika maeneo ya Masoko kwa ajili ya kuongeza Chachu ya kurahisisha Usafiri katika kufanikisha zoezi hilo, Jumla ya Pikipiki 14 zilitolewa kwa Mkoa wa Dodoma . Hafla hiyo imefanyika leo Julai 30,2019 katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiangalia Bidhaa mbalimbali zinazotengenezwa na Wajasiriamali Wanawake katika Mkoa wa Dodoma alipotembelea Mabanda ya Maonesho kwenye Uzinduzi wa Mradi wa kutokomeza vitendo vya Unyanyasaji na Udhalilishaji Dhidi ya Wanawake na Watoto katika maeneo ya Masoko. Hafla hiyo imefanyika leo Julai 30,2019 katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma. 
Baadhi ya Wafanyabiashara wa Masokoni Wanawake na Wanancho wa Dodoma, wakimsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, alipokuwa akihutubia kwenye Hafla ya Uzinduzi wa Mradi wa kutokomeza vitendo vya Unyanyasaji na Udhalilishaji Dhidi ya Wanawake na Watoto katika maeneo ya Masoko. Hafla hiyo imefanyika leo Julai 30,2019 katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Mratibu wa Umoja wa Mataifa Tanzania Alvaro Rodriquez walipokutana kwenye Hafla ya Uzinduzi wa Mradi wa kutokomeza vitendo vya Unyanyasaji na Udhalilishaji Dhidi ya Wanawake na Watoto katika maeneo ya Masoko. Hafla hiyo imefanyika leo Julai 30,2019 katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Mwakilishi Mkazi wa kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshuhulikia Usawa wa Kijinsia na Uwezeshaji wanawake (UN WOMEN) Bibi. Hadon Addou walipokutana kwenye Hafla ya Uzinduzi wa Mradi wa kutokomeza vitendo vya Unyanyasaji na Udhalilishaji Dhidi ya Wanawake na Watoto katika maeneo ya Masoko. Hafla hiyo imefanyika leo Julai 30,2019 katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma. 
Mwenyekiti wa ALAT Mhe Gulamhafeez Mukadam,akizungumza na Wafanyabishara Wanawake wa Masokoni na Wananchi wa Dodoma kwenye Hafla ya Uzinduzi wa Mradi wa kutokomeza vitendo vya Unyanyasaji na Udhalilishaji Dhidi ya Wanawake na Watoto katika maeneo ya Masoko. Hafla hiyo imefanyika leo Julai 30,2019 katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akihutubia Wafanyabishara Wanawake wa Masokoni na Wananchi wa Dodoma kwenye Hafla ya Uzinduzi wa Mradi wa kutokomeza vitendo vya Unyanyasaji na Udhalilishaji Dhidi ya Wanawake na Watoto katika maeneo ya Masoko. Hafla hiyo imefanyika leo Julai 30,2019 katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma. 

Waziri wa Afya ,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akizungumza na Wafanyabishara Wanawake wa Masokoni na Wananchi wa Dodoma kwenye Hafla ya Uzinduzi wa Mradi wa kutokomeza vitendo vya Unyanyasaji na Udhalilishaji Dhidi ya Wanawake na Watoto katika maeneo ya Masoko. Hafla hiyo imefanyika leo Julai 30,2019 katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akikata Utepe kuzindua rasmi Mradi wa kutokomeza vitendo vya Unyanyasaji na Udhalilishaji Dhidi ya Wanawake na Watoto katika maeneo ya Masoko pamoja na ugawaji wa Pikipiki 14 kwa Maafisa wa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya wilaya ya Chamwino Dodoma kwa ajili ya kuongeza kurahisisha Usafiri katika kufanikisha kutokomeza Ukatili na Unyanyasaji kwa Wanawake na watoto . Hafla hiyo imefanyika leo Julai 30,2019 katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma. 
Makamu wa Rais wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema watu wanatumia matusi ni watu waliokosa malezi kwa namna tofauti tangu wakiwa wadogo hivyo kuitaka Jamii ya Watanzania kutumia nguvu nyingi katika malezi ya watoto ili kuepukana na athari za ukosefu wa malezi ukubwani. 

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema hayo leo jijini Dodoma katika hotuba yake ya uzinduzi wa Mradi wa Kutokomeza vitendo vya unyanyasaji na udhalilishaji dhidi ya wanawake na watoto katika maeneo ya masoko na zoezi la ugawaji wa pikipiki kwa waataalam wa maendeleo ya Jamii leo Jijini Dodoma. 

Aidha Makamu wa Rais amekemea wanaume wanaotumia lugha ya matumisi katika maeneo ya masoko kuwa yanasabababisha wakina mama wafanya biashara Sokoni kukosa uhuru na hata kushindwa kuleta watoto wao sokoni kwa ajili ya kuwasaidia kwa kutopenda vijana wao kusikia lugha isiyokuwa na maadili. 

“Mnawazalilisha wanawake kwa kuwatukana matusi kwa kutumia viungo vyao, kuwashika au kuwapapasa bila idhini yao kwanini nyie wanaume msishikane wenyewe vitendo vya kuwazalilisha wanawake havikubaliki kabisa’’. Alisisitiza Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan. 

Katika hotuba yake hiyo Makamu wa Rais wa Tanzania amesema vitendo hivyo vya ukatili havikubaliki na ndio maana ya ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ibala ya 168 c inasema wanawake wanayo haki ya kulindwa dhidi ya unyanyasaji wa aina yoyote ile hivyo hatua za kukomesha vitendo vya ukatili dhidi yao ni utekelezaji wa ilani hiyo. 

Pamoja na kukemea vitendo hivyo Makamu wa Rais wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewataka wanaume wanaonyanyaswa Kijinsia wasione aibu bali watoe taarifa kwenye dawati la Jinsia la Jeshi la Polisi ili Serikali iweze kupata takwimu sahihi ili iweze kufanyia kazi chanagamoto hiyo. 

Aidha Makamu wa Rais amehoji wanawake walio katika Kamati ya Soko kwanini wanafumbia macho vitendo vya ukatili ili hali wao ni viongozi watoa maamuzi sokoni hapo na kuonya kuwa uenda na wao wanachangia kuendelea kuwepo kwa ukatili katika maeneo ya sokoni. 

Makamu wa Rais amewataka viongozi wa masoko nchini kuhakikisha wanafanyia kazi tabia ya watoto wadogo kufanya biashara sokoni kwa lengo la kusaidia familia na kuutaka uongozi wa soko kuwahoji na kuwarudisha shuleni ili kusaidia kukata mnyororo wa umasikini wa familia kwani mtoto akipata elimu inamsaidia kutumia elimu yake kupambana na umasikini. 

Kwa upande wake Waziri wa Afya, MAendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amemwomba Makamu wa Rais kuagiza Halmashauri zote nchini kuacha kutoa kiwango kidogo cha mikopo kwa akina na mama na waongeze kiwango cha fedha ili wakinamama wapate miradi ya maana ya biashara kupitia makato ya 4% ya mapato ya kwa Halmashauri. 

“Unakuta kikundi cha akina mama watano wapewa mkopo wa laki tano nakugawana fedha kidogo hii ni pesa gani ndio maana wakina mama wanaishia kuila na kushindwa kufanya marejesho kwa kuwa fedha hii inakuwa haitoshi kufanya chochote’’ Aliongeza Waziri Mwalimu. 

Naye Katibu Mkuu Wizara ya Afya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii Dkt. John Jingu amesema Wizara kwa kushirikiana na wadau wataendelea kutafuta na kugawa Pikipiki kwa Mikoa mingine baada ya Mkoa wa Dodoma ili kuwawezesha Maafisa Maendeleo nchini kutoa elimu kwa jamii kuhusu vitendo vya ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto. 

Dkt. Jingu amesema kuwa Wizara imetoa pikipiki 25 kwa mkoa wa Dodoma na mapema mwezi ujao itatoa pikipiki kumi na tano kama hizo kwa Mkoa wa Rukwa ili kuwawezesha Maafisa Maendeleo Mkoani humo kutumia usafiri huo kuelimisha wananchi kuhusu ukatili na unyanyasaji dhidi ya Wanawake na Watoto. 

Naye Beatrice Siame ambaye ni Mwakilishi wanawake Soko la Majengo ameiomba Serikali kusimamia usawa wa kijinsia katika maeneo ya kazi ili wanawake waweze kunufaika na kuwezeshwa kiuchumi lakini pia akibainisha kuwa changamoto ya soko ya bidhaa zao ni kikwazo katika kumwendeleza mwanamke kiuchumi. 

Uzinduzi wa Mradi wa kupinga unyanyasaji na udhalilishaji wanawake kijinsia katika Masoko ni hatua muhimu ya utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa Kutomeza Vitendo vya Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto unaolenga kutokomeza vitendo vya ukatili Nchini kwa 50% ifikapo 2022.
Viewing all 110171 articles
Browse latest View live




Latest Images