Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110170 articles
Browse latest View live

BALOZI SEIF IDD AKUTANA NA VIONGOZI WA YANGA IKULU LEO ZANZIBAR

$
0
0
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd, amekutana na sekretarieti ya Yanga na kuzungumza masuala mbalimbali ya maendeleo ya klabu hiyo.

Kikao hicho kimefanyika leo Ikulu  ya Zanzibar na kuutaka uongozi kusimamia vyema rasilimali za Klabu na kudhibiti wadokozi wanaojinufaisha kwa maslahi yao. Balozi Idd ameweza kuupongeza uongozi wa Yanga kwa jitihada na mikakati ya kujikwamua kiuchumi ili kuepuka kuwa tegemezi kwa wafadhili. 

Amesema Yanga ni klabu kubwa lazima ionyeshe mfano kwa klabu zingine katika kila jambo na kwa upande atachangia Milioni 2 kwa ajili ya maendeleo ga klabu.Awali Mwenyekiti wa Yanga Dkt Mshindo Msolla alimueleza Balozi Idd juu ya miakati mbalimbali ya uongozi mpya wa Yanga katika kuijenga klabu iweze kujitegemea kiuchumi.

Pia, Dkt Msolla ameweka mkakati wa uongozi wao ni kuifanya Yanga kuwa timu yenye ushindani ndani na nje ya Tanzania. Yanga wamezindua wiki ya Mwananchi Visiwani Zanzibar hapo jana kwa kutembelea kaburi la muasisi wa Klabu hiyo na Rais wa Kwanza wa Zanzibar  Hayati Abeid Aman Karume pamoja na kucheza mechi ya kirafiki.

Matukio mengine ya wiki ya mwananchi yanaendelea kwenye maeneo tofauti tofauti, matawi na wanachama wa Yanga wakijitoa katika shughuli za Kijamii.Kileke cha siku ya mwananchi kinahitimishwa Agost 4 mwaka huu kwa Kikosi cha Yanga kutambulishwa rasmi kwa wachezaji wapya na kucheza mchezo wa Kirafiki na timu ya Kariobang Sharks ya nchini Kenya.
Makamu wa Pili za Zanzibar Balozi Seif Ali Idd akimkabidhi Mwenyekiti wa Yanga Dkt Mshindo Msolla kiasi cha shilling Milion 2 kama mchango wake katika klabu hiyo baada ya kukutana nao na kufanya mazungumzo kwa manufaa ya Klabu ya Yanga.

 Mwenyekiti wa Yanga Dkt Mshindo Msolla akielezea jambo kwa Makamu wa Pili wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd wakati wa mazungumzo yao walipokutana leo Ikulu Zanzibar.

 Makamu wa Pili wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd akizungumza na uongozi wa Yanga ukiongozwa na Mwenyekiti Dkt Mshindo Msolla baada ya kufanya nao mazungumzo ya kimaendeleo pamoja na kuwachangia shilling Milion 2
 Makamu wa Pili wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd akiwa kwenye picha ya pamoja na uongozi wa Klabu ya Yanga ukiongozwa na Mwenyekiti Dkt Mshindo Msolla.

MAHAKAMA YA TANZANIA YAINGIA MKATABA WA BILLIONI 4.2 NA TTCL KUUNGANISHA MAHAKAMA ZOTE NCHINI KATIKA MKONGO WA TAIFA

$
0
0
Na Karama Kenyunko, Globu ya jamii.

MAHAKAMA ya Tanzania imeingia mkataba wa sh. Bilioni 4.2 na shirika la mawasiliano Tanzania TTCL kwa ajili ya kuunganisha mahakama zote nchini katika mkongo Wa Taifa ili kuziwezesha kupatikana haki kwa urahisi na haraka zaidi.

Imeelezwa kuwa, kuunganishwa kwa Ofisi za Mahakama nchi nzima katika Mtandao Mpana (WAN) kwa kutumia mkongo wa Taifa kutapunguza gharama za uendeshaji wa shughuli na kusaidia shahidi kuwasilisha ushahidi wake bila kulazimika kufika mahakamani.

Mkurugenzi wa Tehama wa Mahakama ya Tanzania Kelege Enock, ameeleza hayo leo Julai 29,2019  jijini Dar es Salaam, wakati wa utilianaji saini wa mkataba huo kati ya Mahakamani na TTCL.

Akizungumza kabla ya kutiliana saini, Enock amesema, huduma hiyo ya mtandao  Itasaidia kurahisisha upatikanaji wa huduma za mahakama kwa kupitia mifumo, electroniki, kuwa na mazingira wezeshi ya kubadilishana taarifa kati ya Mahakama na taasisi wadau katika mfumo mzima wa utoaji haki nchini.

"aasisi wadau ni pamoja na Magereza, Polisi, Ofisi ya Mwendesha Mashitaka, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Wizara ya Katiba na Sheria, Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali na Chama Cha Mawakili (TLS),” alisema.

Aidha Kelege amesema, mkataba huo wenye lengo la kuunganisha majengo ya mahakama kuanzia Mahakama ya Rufani, Mahakama Kuu, Mahakama za Hakimu Mkazi, Mahakama za Wilaya na baadhi ya Mahakama za Mwanzo zenye majengo ya kisasa kwa kuanzia jumla ya majengo 157 yatapata Huduma hiyo.

"Mahakama zitakazo ingizwa kwenye mtandao ni, Mahakama ya Rufani moja, Mahakama Kuu 16, Mahakama Kuu Maalumu (Specialized Divisions) nne, Mahakama za Mkoa 29, Mahakama za Wilaya 112,  Mahakama za Mwanzo  10 hivyo  kufanya jumla ya majengo ya Mahakama 157 kwa kuanzia,” amesema Enock.

Ameongeza kuwa, katika mkongo huo wa Taifa  huduma za aina mbili zitapatikana ambazo ni mtandao wa ndani yaani ‘data’ pamoja na ‘Internet’ katika maeneo yote tajwa.

“Kwa kuzingatia unyeti na usalama wa shughuli za Mahakama huduma hii ya mtandao itawezeshwa na teknolojia ya “Virtual Private Network (VPN)” kupitia ‘‘Multiprotocol Labelling Switch (MPLS) ambapo jitihada za kuunganisha mahakama zilianza mwaka 2015 kwa kuwahusisha kikamilifu TTCL mpaka leo mafanikio yamepatikana" amesema.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa TTCL, Waziri Kindamba amesema shirika lao limekuwa likiuza data katika kampuni zingine za mawasiliano kutokana na hilo wanawahakikishia mahakama kuwa wataifanya kazi hiyo na kuimaliza kwa wakati.

“Tunajivunia kuwa sehemu ya watu watakaowasaidia watanzania kupata haki kwa haraka hivyo tunaishukuru mahakama kwa kutuchagua kwani kutokana na miradi hii ndio inayowezesha kuwepo kwa gawio linalorudi serikalini,” alisema.

Aidha alisema watanzania wanapaswa kutumia vitu vya nyumbani kwani kwa kufanya hivyo faidi inabaki nchini na kwenda kutumika katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo.
 Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Hussein Kattanga na Mkurugenzi Mkuu wa TTCL Waziri Waziri Kindamba wakikabidhiana Mkataba huo mara baada ya kuusaini.
 Picha ya pili Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Hussein Kattanga na Mkurugenzi Mkuu wa TTCL Waziri Waziri Kindamba wakikabidhiana Mkataba huo mara baada ya kuusaini.
Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania  Hussein Kattanga (katikati) na Mkurugenzi Mkuu wa TTCL, Waziri Waziri Kindamba (wa pili kulia) wakionesha kwa furaha Mkataba huo mara baada ya kuusaini. Wa pili kushoto ni  Mwenyekiti wa Bodi ya TTCL Bw. Mohamed Mtonga.
 Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) wa Mahakama ya Tanzania Bw. Kalege Enock akielezea kuhusu Mahakama kuingia kwenye Mkongo wa Taifa wakati wa Hafla ya kusainiwa kwa Mkataba kati ya Mahakama ya Tanzania na Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) leo jijini Dar es salaam.

NMB YATOA MSAADA WA VIFAA MBALIMBALI KUKUZA ELIMU RUANGWA MKOANI LINDI

$
0
0
Mkuu wa Idara ya Huduma za Serikali Vicky Bishubo akikabidhi vifaa mbalimbali vikiwemo kompyuta, madaftari, na madirisha ya aluminum kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Kassim Majaliwa kwenye shughuli iliyofanyika zahanati ya Nandangala wilayani Rukwa
Meneja wa Tawi la Ruangwa Abrahamu Eliakimu akimueleza Waziri Mkuu Mh. Kassim Majaliwa kuhusu vifaa mbalimbali vilivyokabidhiwa na Benki ya NMB, NMB imetoa msaada wa thamani ya TZS 25 milioni
………………………
Benki ya NMB imekabidhi msaada wa vifaa vya ujenzi, kompyuta, na Madaftari vyenye thamani ya Tsh. Milioni 25 kwa ajili ya kukuza sekta ya elimu na afya katika halmashauri ya Ruangwa Mkoani Lindi.
Vifaa hivyo vimekabidhiwa kwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ambae pia ni Mbunge wa jimbo hilo katika Zahanati ya Nandagala iliyopo katika Kijiji cha Nandagala Wilayani humo.

Kwa mujibu wa Mkuu wa Idara ya Huduma za Serikali Bi, Vicky Bishubo alisema Vifaa hivyo vilivyotolewa ni pamoja na Madilisha ya Aluminium kwa ajili ya Zahanati ya Nandagala yenye thamani ya Tsh. milioni 15, mabati 56 zikiwa na Mbao zake za kupaulia vyenye thamani ya Tsh. Milioni 3.3, Kompyuta 10 kwa ajili ya Shule ya Sekondari Kasimu Majaliwa pamoja na Madaftali yenye thamani ya Tsh. Milioni 5 kwa ajili ya Shule mbali mbali katika Wilaya hiyo ya Ruangwa.

Akikabidhi vifaa hivyo kwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Mkuu wa Idara ya Huduma za Serikali Bi, Vicky Bishubo kwa niaba Kaimu Mkurungezi Mkuu wa Benki hiyo Albert Jonkergouw alisema kuwa kwa NMB changamoto za sekta ya Afya na Elimu hapa Tanzania ni jambo la kipaumbele kutokana na umuhimu wa sekta hizo kuwa ndio nguzo kuu ya maendeleo kwa Taifa.

“Sisi kama NMB tumekuwa msitari wa mbele kuchangia huduma za kijamii kwa lengo la kurejesha sehemu ya faida yetu kwa jamii, ambapo kwa zaidi ya miaka saba mfululizo tumeweza kuchangia 1% ya faida yetu kama sehemu ya uwajibikaji kwa jamii inayotuzunguka” alisema Bishubo

Hata hivyo Bishubo aliongeza kuwa kwa mwaka 2019 Benki yao imetenga kiasi cha Tsh. Bilioni 1 kwa ajili ya kuchangia maendeleo ya jamii ikiwemo kusaidia sekta ya Elimu na Afya ambapo mpaka sasa tayari imeshatoa msaada wa zaidi ya Tsh. Milioni 600.
Akizungumza baada ya kupokea vifaa hivyo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliishukuru Benki ya NMB kwa kutoa msaada huo ikiwa ni moja ya kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Serikali ya awamu ya tano

Majaliwa alisema kama Serikali inatambua mchango mkubwa unaotolewa na Benki hivyo katika shughuli mbali mbali za maendeleo pamoja na majanga yanapotokea.

Waziri Mhagama afungua mafunzo ya ujasiriamali na usimamizi wa biashara kwa vijana

$
0
0

Na Charles James, MICHUZI TV

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu, Mhe Jenista Mhagama amefungua mafunzo ya ujasiriamali na usimamizi wa biashara kwa vijana na kuwataka kuwa wabunifu pamoja na kuitumikia nchi yao kwa uzalendo.

Akizungumza wakati wa ufunguzi huo jijini Dodoma, Waziri Jenista amesema Serikali imejipanga katika kufanikisha inatoa kipaumbele kwa vijana nchini ikiwemo kutunga Sera rafiki zitakazowawezesha kujikwamua kiuchumi katika ujasiriamali bila kusubiri kujitegemea.

Amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwezesha na kuboresha mbinu za uendeshaji na usimamizi wa biashara pamoja na urasimishaji wa shughuli za uzalimishaji zinazofanywa na vijana.

" Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais wetu mpendwa Dk John Magufuli inalenga kuwawezesha vijana wanaomiliki biashara katika Mikoa husika kukuza na kurasimisha biashara zao ili kuongeza ajira kwa vijana wenzao na watanzania kwa ujumla pamoja na kuchangia pato la Taifa.

" Lakini pia Serikali imepanga kuwaunganisha vijana na fursa za mitaji na mitandao ya huduma za biashara ikiwemo urasimishaji," amesema Waziri Jenista.

Aidha Mhe Jenista amewataka vijana kuepuka kukaa vijiweni na kuwa watu wanaolalamika bila ilihali Serikali ya Rais Magufuli imekua ikitoa mikopo isiyo na riba katika Halmashauri zake nchini.

" Niwaombe vijana muamke maana nyie ndio mnapaswa kuwa uti wa mgongo katika kuufikia uchumi wa kati. Hampaswi kulalamika, mna nguvu na wengine mna taaluma zenu, tuzitumie kuhakikisha tunaikomboa jamii yetu, sisi kama Serikali tunaahidi kuwaunga mkono na kuwatengenezea mazingira rafiki ya kuwawezesha kufanya biashara zenu bila kusumbuliwa na mtu," amesema Mhe Jenista.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Vijana, Mhe Anthony Mavunde amewataka vijana kuamka na kufanya kazi kwa bidii huku wakiamini wanaweza kufikia malengo na ndoto zao bila kikwazo chochote.

" Ondoeni dhana ya kushindwa katika akili zenu, ukiwa kijana unapaswa kufikiri chanya muda wote, Kama hutoamua kujituma na kufanya kazi kwa bidii huku ukiamini unaweza kufanikiwa basi hata aje nani kukwambia utafanikiwa huwezi kumuelewa. Kama vijana ni wakati wa kuamka kwa ari kubwa na kushinda, " amesema Mhe Mavunde.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi Vijana Ajira na Walemavu, Andrew Massawe amesema dira ya Serikali ya awamu ya tano ni kuipeleka Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa kati kupitia sekta ya viwanda ambayo itakua chachu ya kukuza pato la Taifa.

" Ili kufikia azma ya uchumi wa kati vijana ndio nguzo pekee yenye mchango mkubwa wa kufanikisha maono ya Serikali. Hivyo Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) wanaendesha mafunzo ya uwezeshaji kwa vijana ili kutengeneza tija katika shughuli za uzalimishaji wanazozifanya kila siku," amesema Bw Massawe.

Nae Katibu Mtendaji wa NEEC, Bi Beng'i Issa amesema mafunzo hayo yatawafikia moja kwa moja vijana wasiopungua 4000 katika Mikoa yote ya Tanzania bara lakini matokeo yake yanaweza kuwa zaidi ya namba hiyo kutokana na ajira mpya zitakazoibuliwa sambamba na uanzishwaji wa biashara nyingine.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu, Mhe Jenista Mhagama akizungumza na vijana wanaoshiriki mafunzo ya ujasiriamali n usimamizi wa biashara kwa vijana jijini Dodoma leo
 Sehemu ya vijana wanaoshiriki mafunzo ya ujasiriamali na usimamizi wa biashara kwa vijana yaliyofunguliwa leo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge Kazi Ajira Vijana na Walemavu, Mhe Jenista Mhagama
 Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Vijana, Mhe Anthony Mavunde akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu Bw Andrew Massawe akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo hayo ya vijana

Balozi Kijazi Aridhishwa Maandalizi Mkutano wa SADC

MAJALIWA AZUNGUMZA NA VIONGOZI WA CCM WA KATA ZA WILAYA YA RUANGWA

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikabidhiwa zawadi ya picha yake iliyochorwa na Mwalimu Elisha Simon wa Ruangwa (kulia) wakati alipozungumza na viongozi wa CCM na Jumuiya zake wa kata za wilaya ya Ruangwa, kwenye ukumbi wa Ofisi ya CCM ya wilaya ya Ruangwa, Julai 29, 2019.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na viongozi wa CCM wa wilaya ya Ruangwa wakati alipowasili kwenye ukumbi wa CCM wa wilaya hiyo kuzungumza na viongozi wa CCM na Jumuiya zake wa kata za wilaya hiyo, Julai 29, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na viongozi wa CCM na Jumuiya zake wa Kata za wilaya ya Ruangwa kwenye ukumbi wa Ofisi ya CCM ya wilaya ya Ruangwa, Julai 29, 2019.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikabidhiwa zawadi ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli ambayo ni picha ya Rais iliyochorwa na Mwalimu Elisha Simon wa Ruangwa (kulia), wakati alipozungumza na viongozi wa CCM na Jumuiya zake wa kata za wilaya hiyo, kwenye ukumbi wa Ofisi ya CCM ya wilaya ya Ruangwa, Julai 29, 2019.
Viongozi wa CCM na Jumuiya zake wa kata za wilaya ya Ruangwa wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza nao kwenye ukumbi wa Ofisi ya CCM ya wilaya ya Ruangwa, Julai 29, 2019.

375 wapima Homa ya Ini, 29 waambukizwa

$
0
0
Wataalam wa afya Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) wakisajili watu mbalimbali waliojitokeza kupima ugonjwa wa Homa ya Ini ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha siku ya Homa ya Ini ambayo hufanyika Julai 28 kila mwaka duniani kote.
 Baadhi ya watu wakiwa kwenye foleni ya kuandikishwa kabla ya kufanyiwa uchunguzi wa kubaini kama wameambukizwa ugonjwa wa Homa ya Ini.
Daktari Bingwa katika Kitengo cha Magonjwa ya Mfumo wa Chakula na Ini wa Muhimbili, Dkt. Eva Uisso akitoa ushauri kwa mgonjwa aliyefanyiwa uchunguzi kuhusu maambukizi ya ugonjwa wa Homa ya Ini.
Baadhi ya watu wakisubiri kuwaona madaktari kwa ajili ya kupatiwa matibabu na ushauri baada ya kufanyiwa uchunguzi kuhusu maambukizi ya ugonjwa wa Homa ya Ini.


Wataalam wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) wameadhimisha siku ya Homa ya Ini duniani kwa kutoa huduma ya upimaji wa afya kwa watu 375, huku 29 kati yao wakiwa wameambukizwa ugonjwa wa Homa ya Ini na 55 wakiwa wamepatiwa chanjo. 

MNH imetoa huduma ya kupima watu mbalimbali ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha siku ya Homa ya Ini duniani ambayo hufanyika tarehe 28 Julai kila mwaka.Kati ya watu 375 waliojitokeza wanaume ni 175 na wanawake ni 200 ambapo watu 346 hawana ugonjwa wa Homa ya Ini.

Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Mfumo wa Chakula na Ini wa Muhimbili, Dkt. Masolwa Ng’wanasayi amesema watu waliobainika kuwa na Homa ya Ini wameshauriwa kwenda hospitali kwa ajili ya kupatiwa matibabu. 
Dkt. Ng’wanasayi amesema lengo la kufanya uchunguzi wa afya kwa watu mbalimbali ni kuongeza uelewa katika jamii kuhusu ugonjwa wa Homa ya Ini wa aina ya Hepatitis B.

Mtaalamu amebainisha kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), watu 325 milioni duniani wanaishi na maambukizi ya Homa ya Ini na kwamba asilimia nane ya wakazi wanaoishi Kusini mwa Jangwa la Sahara wameambukizwa Homa ya Ini aina ya Hepatitis B.

“Hapa kwetu tafiti zinaonyesha asilimia 4.9 wameambukizwa ugonjwa wa Homa ya Ini aina ya Hepatitis B na asilimia 2 wameambukizwa Homa ya Ini aina ya Hepatitis C,” amesema Dkt. Ng’wanasayi.

Amesema kundi la watu wanaotumia dawa za kulevya ni miongoni mwa watu ambao wameambukizwa Homa ya Ini. “Tafiti zinaonyesha kwamba miongoni mwao asilimia 67 hadi 70 wameambukizwa Homa ya Ini,” amesema.

Mkataba Ujenzi Daraja la Kigongo Busisi Wasainiwa

$
0
0
Mtendaji Mkuu Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mhandisi Patrick Mfugale akisaini Mkataba wa ujenzi wa Daraja la Kigongo-Busisi mkoani Mwanza na Mwakilishi kutoka kampuni ya ujenzi ya China Civil Engeering Construction Coorporation, Zhang Jang, katika hafla iliyofanyika Makao makuu ya Mamlaka ya Bandari Tanzania TPA, Jijini Dar es Salaam, wanaoshuhudia ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe na Waziri wa TAMISEMI, Selemani Jaffo.
Mtendaji Mkuu Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mhandisi Patrick Mfugale na Mwakilishi kutoka kampuni ya ujenzi ya China Civil Engeering Construction Coorporation, Zhang Jang, wakionesha nakala za mkataba wa ujenzi wa Daraja la Kigongo- Busisi mara baada ya kusainiwa, ujenzi wake utagharimu TZS. Bilioni 592. (Picha Idara ya Habari-MAELEZO). 

Hatimaye historia imeandikwa nchini Tanzania kwa kusainiwa kwa mkataba wa ujenzi wa daraja la Kigongo Busisi katika Ziwa Victoria mkoani Mwanza lenye urefu wa kilometa 3.2, ambao utagharimu jumla ya fedha za kitanzania Bilioni 592. 

Akizungumza Jijini Dar es Salaam katika hafla ya utiaji saini mkataba wa ujenzi wa daraja hilo, Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isaac Kamwelwe, amesema mradi huo utatekelezwa kwa fedha za walipa kodi wa Tanzania bila kutegemea fedha za wafadhili. 

Waziri Kamwelwe alisema mradi wa Kigongo Busisi kama ilivyo miradi mingine ya kimkakati ulipigwa vita sana na baadhi ya watanzania na hata wahisani, amesema hata baadhi ya wanasiasa waliupinga wakidai ni mradi mkubwa sana kwa taifa na hauna tija kwa wakazi wa maeneo hayo na nchi kwa ujumla. 

“Serikali hii ikiamua jambo inalivalia njuga na inahakikisha linakamilika kwelikweli , huu ni mkonga wetu watanzania na haijawahi hata siku moja mkonga ukamshinda tembo hivyo tunafanya na tutafanikiwa kwa sababu tunatumia fedha zetu wenyewe ili hao waliotukatisha tamaa washangae ” Alisema Waziri Kamwelwe. 

Amesemakuwa ni wakati sasa kwa watanzania kutembea kifua mbele kwani sasa kodi zao zinatumika ipasavyo katika kuwaletea maendeleo, ndio maana mradi huo mkubwa unaanza kutekelezwa, sambamba na miradi mingine kama ya umeme wa mto Rufiji pamoja na kuendelea kununua ndege mpya ili kuimarisha shirika la ndege. 

Amesema wahisani wengi walikuwa na masharti kwamba wakikuletea fedha wanakuletea na mkandarasi wao, hivyo amesema kwa Tanzania ya sasa haitakubalika kwani kuna mgawanyo wa majukumu na wataalam wa mikataba, kuna wataalam wa manunuzi na hata washauri katika miradi mbalimbali hivyo serikali iko makini sana hasa katika masuala ya mikataba ili wasiingie mikataba ambayo itakuja kuwa kifungo kwa watanzania. 

Waziri Kamwelwe amesema wakati wa ujenzi wa daraja kutakuwa na ajira za kudumu zaidi ya elfu moja na ajira zisizo za kudumu zaidi ya elfu kumi, kwakua fedha ni za watanzania ni wajibu wa serikali kuhakikisha fedha zinawanufaisha watanzania. 

Hafla ya utiaji saini mkataba wa Ujenzi wa Daraja la Kigongo Busisi ulihudhuriwa pia na Waziri wa nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Suleiman Jaffo , wakuu wa mikoa ya Mwanza na Geita, wabunge kutoka katika mikoa hiyo pamoja na baadhi ya wajumbe wa kamati ya Kudumu ya Bunge ya miundombinu. 

Ujenzi wa daraja hilo unatekelezwa na kampuni ya China Civil Engineering Construction Cooperation kwa kushirikiana na kampuni ya China Railway 15 Bureau Group , na linatarajiwa kuwa na urefu wa kilometa 3.2 pamoja na barabara zenye urefu wa kilometa 1.66. mkoa wa Mwanza. 

Utiaji saini huo ulifanywa na Mhandisi Patrick Mfugale Mtendaji Mkuu wa Tanroads kwa niaba ya Serikali ya Tanzania na Bw.Zhan Jang kwa niaba ya makampuni ya China Civil Engineering Cooperation na China Railway 15 Bureau Group. 

MKATABA WA UJENZI WA DARAJA LA KIGONGO-BUSISI MKOANI MWANZA LA KM 3.2 WASAINIWA

$
0
0
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Isaack Kamwelwe akiongea kabla ya kusainiwa kwa Mkataba wa Mradi wa Ujenzi wa Darala la Kigongo-Busisi Mwanza wa Km 3.2 katika hafla iliyofanyika makao makuu ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) jijini Dar es salaam leo Julai 29, 2019.
Mtendaji Mkuu wa TANROADS Eng. Patrick Mfugale akiuelezea Mradi wa Ujenzi wa Daraja la Kigongo-Busisi la Mwanza wa Km 3.2 kusainiwa katika hafla iliyofanyika makao makuu ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) jijini Dar es salaam leo Julai 29, 2019.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Isaack Kamwelwe. Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Atashasta Nditiye. Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI) Mhe. Suleiman Jaffo wakishuhudia Mtendaji Mkuu wa TANROADS Eng. Patrick Mfugale wakiweka saini  na Mkandarasi China Civil Engineering Construction Corporation (CCECC) Mkataba wa Mradi wa Ujenzi wa Darala la Kigongo-Busisi Mwanza wa Km 3.2 kusainiwa katika hafla iliyofanyika makao makuu ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) jijini Dar es salaam leo Julai 29, 2019
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Isaack Kamwelwe. Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Atashasta Nditiye. Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI) Mhe. Suleiman Jaffo wakishuhudia Mtendaji Mkuu wa TANROADS Eng. Patrick Mfugale wakibadilishana nyaraka baada ya kuweka saini na Mkandarasi China Civil Engineering Construction Corporation (CCECC) Mkataba wa Mradi wa Ujenzi wa Darala la Kigongo-Busisi Mwanza wa Km 3.2 kusainiwa katika hafla iliyofanyika makao makuu ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) jijini Dar es salaam leo Julai 29, 2019
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela akizungumza katika hafla ya utiaji siani kwa Mradi wa Ujenzi wa Daraja la Kigongo-Busisi Mwanza wa Km 3.2 iliyofanyika makao makuu ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) jijini Dar es salaam leo Julai 29, 2019
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu Mhe. Hawa Mchafu Chakoma katika hafla ya uwekaji saini Mkataba wa Mradi wa Ujenzi wa Darala la Kigongo-Busisi Mwanza wa Km 3.2 kusainiwa katika hafla iliyofanyika makao makuu ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) jijini Dar es salaam leo Julai 29, 2019.
Mbunge wa Geita Mhe Joseph Kasheku Msukuma akitoa shukrani kwa serikali ya awamu ya Tano kwa Mradi wa Ujenzi wa Darala la Kigongo-Busisi Mwanza wa Km 3.2 kusainiwa katika hafla iliyofanyika makao makuu ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) jijini Dar es salaam leo Julai 29, 2019
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Isaack Kamwelwe. Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Atashasta Nditiye, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI) Mhe. Suleiman Jaffo, Mtendaji Mkuu wa TANROADS Eng. Patrick Mfugale na wabunge wa Kanda ya zaiwa katika picha ya pamoja na wawakilishi wa Mkandarasi China Civil Engineering Construction Corporation (CCECC) Mkataba wa Mradi wa Ujenzi wa Darala la Kigongo-Busisi Mwanza wa Km 3.2 kusainiwa katika hafla iliyofanyika makao makuu ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) jijini Dar es salaam leo Julai 29, 2019

MTOTO WA MFANYABIASHARA ANAYETUHUMIWA KUMUUA MJUKUU WAKE ATOA USHAHIDI MAHAKAMANI

$
0
0

Na Karama Kenyunko, Michuzi Tv

MTOTO wa mfanyabiashara Ester Lymo (47) , anayekabiliwa na tuhuma za kesi ya mauaji ya mjukuu wake Naomi John, Jackline Kessy (25) ameieleza 

Mahakama kuwa marehemu Naomi aliyefariki Machi, mwaka 2017 alipigwa na mama yake licha ya kuwa mtoto huyo hakuwa katika haki nzuri ya kiafya kwa siku hiyo.

Jackline ambae ni shahidi wa pili wa utetezi katika tuhumza za kesi hiyo ya mauaji ameeleza hayo leo Julai 29 mwaka 2019 wakati akitoa ushahidi kumtetea mama yake mzazi mshtakiwa Ester mbele

ya Msajili Pamela Mazengo wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam.

Wakati akijibu maswali ya Wakili wa Serikali Mwandamizi Cecilia Mkonongo, Jackline amedai, siku ya tukio kabla ya mama yake kumchapa Naomi, hakuwa katika hali yake ya kawaida, kwani alikuwa amelegea.Pia alikuwa hajanywa hata chai lakini mama yake alimchapa na ndipo baada ya kumchapa akalegea kabisa.

Ameidai kuwa wakati mama yake akiendelea kumchapa, Naomi aliishiwa nguvu, ambapo mama yake alikwenda duka la dawa, alishauriwa ampeleke hospitali mtoto kutokana na hali aliyokuwa nayo marehemu.

" Mimi ndio nilimbebe Naomi wakati tunaenda hospitali, tukiwa njiani nilisikia Naomi akiwa ana hema haraka haraka, sikujua kama alikuwa amekufa hadi tulipomfikisha hospitali, ambapo nilimsikia daktari akimwambia mama kuwa mgonjwa wao alikuwa ameishiwa damu", amedai Jackline 

Wakili huyo wa Serikali, Mkonongo alimpatia Jackline maelezo yake aliyoyatoa Polisi ili ayasome, kulinganisha na alichokisema mahakamani kama vinalingana au la.

Jackline akisoma maelezo yake aliyoyatoa polisi, alidai kuwa mama yake alikuwa mkali sana ndiyo maana walikuwa hawakai nyumbani, ambapo mwaka 2009, baba yake ndiyo aliwaomba wakae likizo nyumbani.Alidai Naomi alikuwa na vidonda mwilini na mkono wake ulikuwa kama umeteguka, alipomuuliza dada yake (Victoria John) alidai mama ndiyo kamchapa na kumfinya na hata yeye alishawahi kumshuhudia mama yake akifanya hivyo.

"Siku moja Victoria alikuwa anamuogesha Naomi alikuwa anasikia maumivu sehemu za siri, Victoria akampiga akasema anadeka.Mama na Victoria ndiyo walikuwa wanampiga Mimi sikuwahi kumpiga ," Nilimuona mama akitumia maji ya moto kumchoma Naomi. Naomi alipotoka Moshi alikuwa anamapunye kichwani na pia alikuwa hana tabia nzuri, "amedai Jackline mahakamani hapo.

Wakati Mkonongo alipomuuliza kuwa kati ya yeye na mama yake nani anayesema ukweli?, Kessy alidai kuwa ni yeye ambaye anazungumza ukweli, ambapo awali hilo lilitokana na mkanganyiko wa maelezo ya mama yake na yeye.

Katika utetezi wake, mshtakiwa Easter Lyimo ambae ni shahidi wa kwanza katika kesi hiyo amedai wakati anamchapa marehemu alimwambia amechoka lakini yeye alijua ni utani na akaendelea kumchapane Kessy (25).

Akiongozwa na Wakili wa utetezi, mshitakiwa Esther amedai mahakamani hapo kuwa vidonda na makovu katika mwili wa marehemu Naomi vilitokana na shuguli za kuchunga mbuzi kijijini kwao Moshi.

Amedai, Naomi na Andrew ni watoto dada yake na aliwachukua ili aishi nao baada ya kuombwa na Dada yake awasomeshe lakini tangu aishi na Naomi nyumbani kwake Tuangoma hadi siku ya siku anafariki, alikuwa na vidonda na makovu.

"Watoto hawa ni watundu sana, huwa wanakimbizana na kucheza vichakani hivyo ndio maana mwili wake ulikuwa na vidonda na makovu, sijamuua Naomi, nilikuwa nawapenda watoto hao kama watoto wangu wa kuwazaa naomba mahakama iniachie huru,"amedai

Amedai, siku ya tukio, Machi 25, mwaka 2016 wakati anatoka kufanya usafi Saloon kwake, alielezwa na Andrew kuwa Naomi ameamka, amejikojolea yupo barazani."Nilimwambia Naomi akapige mswaki, nikaingia ndàni, lakini aliendelea kukaa barazani, Andrew aliniambia hapigi mswaki anachezea maji, nikaongea kwa sauti kwamba nikitoka ndani nitàmchapa, nilipotoka Naomi akakimbia nikamwambia Andrew amkamate," amedai Esther.

Amedai alipoletwa alichuma fimbo katika mti wa Mparachichi na kumchapa kwa nia ya kumkanya kama mzazi."Wakati namchapa Naomi akasema amechoka, mi nilizani ni utani kwasababu ya kukimbia na ujeuri wake, nilimnyànyua na kumweka barazani, nikaenda kutafuta dawa, nilivyorudi nilikuta amelegea sana hivyo nikachukua gari ya jirani na kumpeleka hospitali Temeke," amedai.

Katika utetezi wake, Esther amedai daktari aliwaambia Naomi alikuwa amepungukiwa damu na baada ya muda akawaeleza kuwa ameshafariki.Amedai wakiwa hospitalini Polisi walikuja kumchukua na kupelekwa Kituo cha Polisi Maturubai na baadae Charambe na Aprili 4, mwaka 2016 akafunguliwa mashitaka ya mauaji.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi itakapopangiwa session nyingine.

TAASISI YA KUENDELEZA KILIMO AFRIKA YAKUTANA NA WIZARA TATU NCHINI

$
0
0
Timu ya wataalam kutoka katika Taasisi ya kuendeleza kilimo Afrika (AGRA) imekutana na viongozi wa wizara ya kilimo na wizara ya Viwanda na Biashara lengo likiwa ni kuajadiliana namna ya kuongeza uzalishaji na tija katika mazao ya kilimo pamoja na uongezaji wa thamani wa mazao hayo . 

mkutano huo ambao umehudhuriwa na Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Innocent Bashungwa, Naibu waziri wa Kilimo Mhe. Omar Mgumba na Naibu Waziri kilimo Mhe. Hussein Bashe,pamoja na Rais wa AGRA Afrika Dkt. Agnes Kalibata umefanyika leo 29.07.2019 katika ukumbi wa mikutano wa kilimo IV mjini Dodoma ambapo wamekubaliana 

kuimarisha uzalishaji wa mazao manne ambayo,ni alizeti, mahindi, mpunga pamoja na maharage ya soya ambayo yanahuitaji mkubwa katika soko. 

Akizungumza katika kikao kazi hicho Rais wa AGRA Dkt. Agnes Kalibata amesema kwamba Tanzania inaweza kuwa ghala la chakula afrika endapo itaendea kuwekeza kikamilifu katika sekta ya mbegu hapa nchini kwa kuwa wakulima wengi hawatumii mbegu bora za kilImo 

akizungumza katika mkutano huo Dkt. Kalibata amesema wakati umefika kuongeza uwekezaji katika sekta ya mbegu kwa kuimarisha miundombinu ya umwagiliaji katika mashamba ya mbegu ili ziweze kuzalishwa kwa uhakika na kuongeza tija kwa wakulima. 

hata hivyo ameshauri wizara ya kilimo kuandaa jukwaa maalum la wazalishaji wa mbegu (seed platform ) ambalo litasaidia kuongeza uhusiano baina ya wazalishaji wa mbegu wa serikalini na wa sekta binafsi katika kusaidia ukuaji wa viwanda hapa nchini. 

Tanzania ina viashiria vingi vinavyoweza kusaidia ukuaji wa viwanda vya kilimo kama wataongeza kiasi cha uzalishaji mbegu, kuongeza idadi ya wauzaji pembejeo za kilimo(agro- dealer) ,kuimarisha huduma za ugani kwa wakulima na kuongeza usajili wa makampuni ya mbegu. alisema Dkt. Kalibata 

Aidha mwenyekiti wa kikao hicho ambaye ni waziri wa viwanda na biashara Mhe. Innocent Bashungwa amesema wamekubalina na AGRA Kuweka mikakati madhubuti ya kuendeleza mazao ya mafuta ili kupunguza uagizaji wa bidhaa hiyo nje ya nchi. 

Hata hivyo Mhe. Bashungwa amesisitiza kwamba AGRA isaidie katika kuongeza uzalishaji wa mbegu hapa nchini ambapo uzalishaji huo utasaidia kuongeza malighafi za viwanda hapa nchini. 

Akitolea mfano viwanda vya alizeti Mhe. Bashungwa amesema kwamba hapa nchini kuna viwanda vya kusindika alizeti vipatavyo 29 lakini vyote vinazalisha chini ya asilimia 30 kwa kukosa malighafi za viwandani. 

Mhe. Bashugwa aliendea kumfafanulia Rais wa AGRA Afrika kwamba nchi zinazoizunguka tanzania zinauhitaji mkubwa wa mazao kama soya,mahindi,alizeti mpunga na Degu hivyo kwa ushirikiano huo utasaidia sana katika upatikanaji wa soko kwa wakulima wetu. 

akiongea kwa niaba ya serika Naibu Waziri Mh. Mgumba amesema makubaliano hayo yamelenga kuongeza tija na uzalishaji kwa wakulima na kuongeza ushindani katika soko kuwa na bei nzuri kwa wanunuzi. 

hata hivyo Mhe. Mgumba ameeleza kwamba wakuima wanatakiwa kulima kulingana na mahitaji ya soko na kutokana na makubaliano hayo kutasaidia wakulima kupunguza gharama za uzalishaji hivyo kusaidia kupungua bei za mazao ikilinganishwa na hali ilivyo sasa. 

Aidha, wamekubaliana kuimarisha sekta binafsi hususani katika uzalishaji wa mbegu, huduma za ugani na kuijengea mazingira mazuri ili kuweza kuongeza uzalishaji , na kutoa ajira kwa watanzania kwa kupunguza gharama za uwekezaji 

Naye Mh Naibu Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amesema wakulima wanakabiliwa na changamoto kubwa ya kiwango kidogo cha uzalishaji katika ekari na gharama kubwa ya uzalishaji hivyo kuwashauri AGRA kuangalia namna ya kuwasaidia wakulima kupunguza gharama ya uzalishaji na kuongeza kipato. 

kwa upande mwingine Naibu waziri Bashe amewaomba AGRA kusaidia uzalishaji wa mbegu hapa nchini, ili ziweze kupatikana kwa gharama ndogo na mkulima kupata matokeo chanya. 

katika kuimarisha ufuatiliaji wa shughuli za kilimo wamekubaliana kuhusu fedha zinazotoka kwa wafadhili zijulikane kila zinapokwenda ili kuhakikisha lengo lilikusudiwa linafikia alisema Mhe. Bashe 

Rais Magufuli amteua Dkt. Elirehema Joshua Doriye kuwa Mkurugenzi Mkuu wa NIC

KAMPUNI I ya Jatu PLC yaendesha mafunzo kwa vijana 100 kutokomeza umaskini

$
0
0
KAMPUNI I ya Jenga Afya Tokomeza Umaskini (Jatu PLC), imeendesha mafunzo kwa vijana 100 lengo likiwa ni kutokomeza umaskini kupitia rasilimali watu.

Meneja mkuu wa Jatu, Mohamed Simbano akizungumza wakati wa mafunzo hayo alisema mkakati wa taasisi yao ni kusaidia kuondoa kutu vichwani mwa vijana kwa kuacha kutegemea kuajiriwa na badala yake waangalie fursa zilizopo na kuweza kujiajiri.

“ Tukiwa hapa kwenye mafunzo, una diploma, degree weka pembeni kwa sababu hazina maana sana kama huna uwezo wa kubuni wazo na kutengeneza pesa,” alisema Simbano na kuongeza

“Aliyejaribu na akashindwa, anafaida kubwa kuliko asiyejaribu, kufeli haina maana umeshindwa bali utatafuta namna nyingine ya kujaribu.” Alisema

Akimnukuu mwanafalsafa Joseph Chilton Pearce aliyeelezea thamani ya ubunifu aliyosema, ‘to live a creative life we must lose our fear of being wrong’ kwa tafsiri isiyo rasmi alimanisha kuishi maisha ya ubunifu kunahitaji kuondoa hofu ya kukosea.

Simbano alisema elimu ambayo wanawapatia vijana hao itawaondoa katika dhana ya kusaka ajira au kubweteka majumbani na badala yake watachukua hatua na kujiikingiza kwenye ujasiriamali wa kilimo na masoko.Alisema mafunzo hayo ni bure kwa kila kijana mwenye ndoto za kujikwamua kiuchumi,bila kujali elimu.

Alisema mara baada ya mafunzo hayo watatoa nafasi kwa vijana katika masoko kwa kuwaajiri na kuimarisha kitengo chao cha masoko, hadi kufikia mwaka 2022 kila anayetumia soko bidhaa za Jatu aweze kupata manufaa na kwamba chakula kinacholiwa kiwe suluhisho la masoko.

“Mafunzo haya ni endelevu, vijana 100 tutakaowapa ajira ni fursa pekee kwao kwa kuimarisha kitengo cha masoko cha Jatu, na kazi yao kubwa ni kuhakikisha kila mwanachama wa jatu aweze kutumia bidhaa.” Alisema

Alisema mafunzo hayo yanaenda sambamba na mpango mkakati na kufikia malengo, waliojiwekea ikiwemo kutokomezaz umaskini kupitia rasilimali watu, kilimo na viwanda, ikiwa ni pamoja na kuingia kwenye soko la hisa (DSE) mwezi Septemba.

KAMPUNI ya Jatu PLC yaendesha mafunzo kwa vijana 100,yawaasa kuacha kutegemea kuajiriwa

$
0
0
KAMPUNI I ya Jenga Afya Tokomeza Umaskini (Jatu PLC), imeendesha mafunzo kwa vijana 100 lengo likiwa ni kutokomeza umaskini kupitia rasilimali watu.

Meneja mkuu wa Jatu, Mohamed Simbano akizungumza wakati wa mafunzo hayo alisema mkakati wa taasisi yao ni kusaidia kuondoa kutu vichwani mwa vijana kwa kuacha kutegemea kuajiriwa na badala yake waangalie fursa zilizopo na kuweza kujiajiri.

“ Tukiwa hapa kwenye mafunzo, una diploma, degree weka pembeni kwa sababu hazina maana sana kama huna uwezo wa kubuni wazo na kutengeneza pesa,” alisema Simbano na kuongeza

“Aliyejaribu na akashindwa, anafaida kubwa kuliko asiyejaribu, kufeli haina maana umeshindwa bali utatafuta namna nyingine ya kujaribu.” Alisema

Akimnukuu mwanafalsafa Joseph Chilton Pearce aliyeelezea thamani ya ubunifu aliyosema, ‘to live a creative life we must lose our fear of being wrong’ kwa tafsiri isiyo rasmi alimanisha kuishi maisha ya ubunifu kunahitaji kuondoa hofu ya kukosea.

Simbano alisema elimu ambayo wanawapatia vijana hao itawaondoa katika dhana ya kusaka ajira au kubweteka majumbani na badala yake watachukua hatua na kujiikingiza kwenye ujasiriamali wa kilimo na masoko.Alisema mafunzo hayo ni bure kwa kila kijana mwenye ndoto za kujikwamua kiuchumi,bila kujali elimu.

Alisema mara baada ya mafunzo hayo watatoa nafasi kwa vijana katika masoko kwa kuwaajiri na kuimarisha kitengo chao cha masoko, hadi kufikia mwaka 2022 kila anayetumia soko bidhaa za Jatu aweze kupata manufaa na kwamba chakula kinacholiwa kiwe suluhisho la masoko.

“Mafunzo haya ni endelevu, vijana 100 tutakaowapa ajira ni fursa pekee kwao kwa kuimarisha kitengo cha masoko cha Jatu, na kazi yao kubwa ni kuhakikisha kila mwanachama wa jatu aweze kutumia bidhaa.” Alisema

Alisema mafunzo hayo yanaenda sambamba na mpango mkakati na kufikia malengo, waliojiwekea ikiwemo kutokomezaz umaskini kupitia rasilimali watu, kilimo na viwanda, ikiwa ni pamoja na kuingia kwenye soko la hisa (DSE) mwezi Septemba.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE JULAI 30,2019


Waziri Biteko Aitaka halmashauri ya Uvinza kuratibu uanzishwaji soko la chumvi

$
0
0
Meneja wa kiwanda cha chumvi cha uvinza Ben Mwaipopo wa kwanza kushoto na Meneja Mkuu wa kuwanda hicho Mukash Mamlani Wa pili kulia wakimwonesha kitu Waziri wa Madini Doto Biteko wa kwanza kulia alipokuwa akikagua shamba la chumvi la uvinza.
Waziri wa Madini, Doto Biteko akizungumza na wachimbaji wadogo (hawapo pichani) wa madini katika ukumbi wa mkutano wa Uvinza alipofanya ziara ili kusikiliza changamoto zao na kuzitafutia ufumbuzi tarehe 29/July, 2019.
Waziri wa Madini, Doto Biteko akisikiliza jambo kutoka kwa wachimbaji walioshiriki mkutano baina yake na wachimbaji wadogo wa Madini wa Uvinza kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Uvinza Bi. Mwanamvua H. Mrindoko. 
Wachimbaji wadogo wa Madini Uvinza, wakimsikiliza waziri wa Madini Doto Biteko (hayupo pichani) wakati wa kikao baina ya waziri Biteko na wachimbaji wadogo wilayani Uvinza mkoani Kigoma.
Afisa Madini Mkazi wa Kigoma akitoa taarifa fupi ya madini wakati wa Mkutano baina ya Waziri wa Madini Doto Biteko na wachimbaji wadogo (hawapo pichani) wa madini katika ukumbi wa mkutano wa Uvinza alipofanya ziara ili kusikiliza changamoto zao na kuzitafutia ufumbuzi tarehe 29/July, 2019.

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameuagiza uongozi wa Halmashauri ya Uvinza ukishirikiana na kiwanda cha chumvi cha Uvinza, pamoja na ofisi ya Madini Mkoani Kigoma kujadili namna ya kuanzisha soko la chumvi katika halmashauri hiyo.

Maelekezo hayo yametolewa kufuatia maombi ya wananchi wa halmashauri hiyo ya uvinza kulalamikia ukosefu wa soko la kuuzia bidhaa hiyo na kuiomba serikali kufanya utaratibu wa kufungua soko ili kuwawezesha kufanya biashara yao mahali salama.

Agizo hilo limetolewa tarehe 29 July, 2019 katika ofisi za Kiwanda cha Chumvi cha Uvinza mara baada ya Waziri Biteko na ujumbe alioambatana nao kuwasili kwa lengo la kuzungumza na uongozi wa kiwanda hicho ili kuweka sawa mambo mbalimbali yaliyowasilishwa na wananchi wakati wa mkutano baina ya Waziri Biteko na Wachimbaji wadogo pamoja na wananchi wa Uvinza.

Moja kati ya malalamiko yaliyomfikia waziri Biteko ni malipo duni ya ujira kwa wafanyakazi wa kiwanda hicho ambapo aliutaka uongozi wa kiwanda hicho kujadili na kufikia maamuzi ya kuongeza ujira kwa wafanyakazi wa kiwanda hicho waliodai kulipwa ujira mdogo.

Aidha, Biteko aliutaka uongozi wa kiwanda hicho kufanya marekebisho hayo mpaka ifikapo tarehe mosi mwezi Agosti, 2019 mara baada ya Kiwanda kufanya mahesabu na kujiridhisha juu ya kiasi kinachobaki baada ya kutoa gharama za uwekezaji kiongezwe katika malipo hayo ya ujira.

Akijibu hoja ya baadhi ya wananchi wa Uvinza waliolalamikia uongozi wa kiwanda hicho kuuza chumvi inayozalishwa kiwandani hapo hiyo bei kubwa inayowafanya walanguzi hao kupata faida kidogo, Biteko aliutaka uongozi wa kiwanda hicho na wachimbaji wengine wa chumvi wilayani humo kupunguza bei hiyo ili kuiwezesha jamii inayowazunguka kunufaika na uwepo wa chumvi katika mji wao.

Biteko aliutaka uongozi wa kiwanda cha chumvi kuwapa wananchi sababu ya kuwapenda kwa kuwatendea mema. Aliendelea kwa kusema mtu mwenye kurekebisha bei ya chumvi kwa manufaa ya wafanyabiashara wadogo ni mwekezaji mkubwa. “ifanye jamii hii iugue siku ukiwa haupo, Ifanye jamii ikukumbuke kwa mema yako” Biteko alisisitiza .

Pamoja na hayo Waziri Biteko, aliutaka uongozi wa Halmashauri ya Uvinza, Ofisi ya Madini ya Mkoa wa Kigoma pamoja na uongozi wa kiwanda kukutana na kujadili namna na mahali patakapofaa kwa ajili ya kuanzisha soko la madini ili kuwaondolea adha ya soko la chumvi wananchi wa Uvinza.

Kufuatia malalamiko ya wananchi wa Uvinza ya kutozwa kiasi cha Tzs 500 ya ushuru kwa kila kilo 25 za chumvi, Waziri Biteko aliiagiza halmashauri ya Uvinza kufuta tozo hiyo na kueleza kuwa tozo hiyo haipo chini ya mamlaka yake na hivyo haitambui.

Akijibu kero ya mwananchi wa uvinza aliyejulikana kwa jina la Yona William Gwagula kwa niaba ya wanakikundi wa Twikome Salt Kinyo Chakuru juu ya watu waliokuwa wakiwatoza kodi kwa madai kuwa leseni iliyokuwa ikichimbwa na wanakikundi hao ni ya kwao jambo lililobainika kuwa si kweli, Waziri Biteko alimtaka Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Kigoma David William Ndosi, kuifuta leseni hiyo mara moja na kuwapa wachimbaji hao wadogo ili waweze kuendeleza shughuli zao.

Kwa upande wake, Katibu wa Wachimbaji Wadogo wa Wilaya ya Uvinza, Hamisa Omari Kambi akiwasilisha changamoto wanazokumbana nazo alisema ni pamoja na maeneo yao kuvamiwa, ukosefu wa vitendea kazi, halmashauri kutowapa kipaumbele wamiliki wa leseni kwenye tenda za Serikali pamoja na kuomba kurahisishwa kwa utolewaji wa vibali vya kusafirisha Madini nje ya nchi ambapo changamoto zote zimepatiwa ufumbuzi. 

Waziri Biteko atakuwepo Mkoani Kigoma kwa ziara ya siku mbili ambapo atafanya majadiliano na ofisi ya Mkoa wakishirikiana na Ofisi ya Tume ya Madini ili kujadili namna bora ya kuimarisha soko la Madini litakalowezesha kuweka mazingira rafiki na salama kwa ajili ya nchi jirani ya Kongo, kutokana na kuonesha nia ya kushirikiana na Tanzania katika biashara ya Madini kupitia masoko yaliyoanzishwa hususani mkoani Kigoma.

WATAALAMU WA MAABARA WAPIGWA MSASA USIMAMIZI WA VIMELEA HATARISHI

$
0
0
Mwezeshaji kutoka Wizara ya Afya,Zanzibar, Rukia Shani akiendelea kutoa mafunzo ya Usimamizi wa vimelea hatarishi vya kibaiolojia kwa wataalamu wa maabara wakati wa mafunzo hayo, yaliyowahusisha wataalamu hao kutoka sekta ya Afya ya Binadamu na Wanyama, Jijini Arusha, tarehe 29 Julai, 2019.
Baadhi ya wataalamu wa maabara wakifuatilia mafunzo ya Usimamizi wa vimelea hatarishi vya kibaiolojia wakati wa mafunzo hayo yaliyowahusisha wataalamu hao kutoka sekta ya Afya ya Binadamu na Wanyama, Jijini Arusha, tarehe 29 Julai, 2019.
Mratibu wa Afya Moja Kitaifa, Ofisi ya Waziri Mkuu, Harrison Chinyuka, akieleza umuhimu wa mafunzo ya Usimamizi wa vimelea hatarishi vya kibaiolojia kwa wataalamu wa maabara wakatia akifungua mafunzo hayo yaliyowahusisha wataalamu hao kutoka sekta ya Afya ya Binadamu na Wanyama, Jijini Arusha, tarehe 29 Julai, 2019.
Mwezeshaji kutoka Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto akiendelea kutoa mafunzo ya Usimamizi wa vimelea hatarishi vya kibaiolojia kwa wataalamu wa maabara wakati wa mafunzo hayo, Jijini Arusha, tarehe 29 Julai, 2019.
Mshiriki wa mafunzo ya Usimamizi wa vimelea hatarishi vya kibaiolojia kwa wataalamu wa maabara, Basilius Kilowoko, akichangia wakati wa mafunzo hayo, Jijini Arusha, tarehe 29 Julai, 2019.
Mshiriki wa mafunzo ya Usimamizi wa vimelea hatarishi vya kibaiolojia kwa wataalamu wa maabara, Fredy Makoga, akichangia wakati wa mafunzo hayo, Jijini Arusha, tarehe 29 Julai, 2019.
Washiriki wa mafunzo ya Usimamizi wa vimelea hatarishi vya kibaiolojia kwa wataalamu wa maabara, wakiwa katika picha ya pamoja na Mratibu wa Afya Moja Kitaifa, Ofisi ya Waziri Mkuu, Harrison Chinyuka (katikati walio kaa) mafunzo hayo yaliyowahusisha wataalamu hao kutoka sekta ya Afya ya Binadamu na Wanyama, Jijini Arusha, tarehe 29 Julai, 2019.




Na. OWM, ARUSHA

Wataalam wa maabara nchini kwa kutumia Dhana ya Afya moja ambao ni wataalam wa maabara kutoka sekta ya Afya ya binadamu, Afya ya wanyamapori na mifugo pamoja na mazingira wameendelea kupewa mafunzo ya Msingi ya Usimamizi na udhibiti wa vimelea hatarishi vya kibailojia kwa kuimarisha ulinzi na usalama wa sampuli za vimelea hivyo.

Vimelea hatarishi vya kibailojia vinaweza sambaza magonjwa kwa wanyama na binadamu iwapo ulinzi na usalama wake hautaimarishwa wakati wa kuvichukua kwa wanyama, binadamu na mimea au wakati wa kusafirisha vimelea hivyo na kuvipeleka maabara kwa ajili ya Uchunguzi pia wakati kuvifanyia uchunguzi pamoja na wakati wa kuviharibu mara baada ya kuvifanyia uchunguzi.

Akiongea wakati wa kufungua mafunzo hayo, leo tarehe 29, Julai, 2019, Mratibu wa Afya Moja Kitaifa, Ofisi ya Waziri Mkuu, Harrison Chinyuka amefafanua kuwa Mafunzo hayo ni mwendelezo wa mafunzo ya msingi ambayo wataalam hao tayari walishafundishwa mafunzo ya awali ya Usimamizi na Usalama wa vimelea hatarishi vya kibailojia mnamo mwezi Machi, mwaka huu.

“Lengo la mafunzo haya ni kuiwezesha nchi yetu kuwa na wataalamu wa maabara wenye uelewa kuhusu dhana za vihatarishi vya kibaiolojia, ikiwemo wakati wa kusafirisha vimelea hivyo na kuvipeleka maabara kwa ajili ya Uchunguzi pia wakati kuvifanyia uchunguzi pamoja na wakati wa kuviharibu mara baada ya kuvifanyia uchunguzi” amesema Chinyuka

Wakiongea kwa nyakati tofauti washiriki wa mafunzo hayo wamebainisha kuwa baada ya mfunzo hayo, mienendo na matendo yao wakiwa maabara itazingatia usalama wa afya zao na usalama wa jamii inayowazunguka pamoja na Usalama wa watanzania, kwa kusimamia na kudhibiti vihatarishi vya kiulinzi na usalama vitokanavyo na vimelea hatarishi amabavyo wataalamu hao wamepewa dhamana ya kuvifanyia kazi.

Mafunzo hayo ya siku tano, yameandaliwa na DTRA na Sandia National Laboratories na wawezeshaji wa hapa nchini kutoka wizara ya Afya, maendeleo ya Jamii,Jinsia , Wazee na watoto pamoja na Wizara ya Uvuvi na Mifugo, chini ya Uratibu wa Ofisi ya Waziri Mkuu.

Afya Moja ni dhana ni dhana inayojumuisha sekta ya afya ya binadamu , wanyamapori, mifugo na mazingira katika kujiandaa , kufuatilia na kukabili magonjwa yanayoathiri binadamu ,wanyamapori na mifugo.

TCRA KUHAKIKISHA HUDUMA BORA NA ZA UHAKIKA ZA MAWASILIANO KWENYE UJENZI MRADI WA UMEME MTO RUFIJI

$
0
0
NA K-VIS BLOG/Khalfan Said, Rufiji

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeagiza kuwepo kwa huduma bora za Mawasiliano katika eneo la Mradi wa ujenzi wa bwawa la kufua umeme wa maji Mto Rufiji Mkoani Pwani.

Akizungumza wakati wa ziara ya Wajumbe wa Bodi na Menejimenti ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA, kwenye eneo la Mradi huo Julai 28, 2019, Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Mhandisi James M. Kilaba alisema, Mradi huo mkubwa ni mradi wa kimkakati na TCRA kama msimamizi wa sekta ya Mawasiliano hapa nchini inaamini hakuna uwekezaji unaotendeka bila ya uwepo wa mawasiliano, jamii na watu watakaokuwa wanatekeleza ujenzi wa mradi huo wanapaswa kuwa na mawasiliano ya uhakika wakati wote wakiendelea na kazi ya ujenzi.

Ujenzi wa Mradi huo wenye thamani ya Shilingi za Kitanzania Trilioni 6.5 fedha za Serikali, ulizinduliwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli juzi Ijumaa Julai 26, 2019 na utakamilika mwaka 2022 ambapo utakuwa na uwezo wa kuzalisha umeme Megawati 2115.

Akieleza zaidi Mhandisi Kilaba alisema, Shirika la TTCL kama Shirika la Serikali pamoja na watoa huduma wengine ya mawasiliano wanaowajibu wa kuhakikisha mawasiliano yapo na TCRA wajibu wake ni kuhakikisha watoa huduma wanafanya yale wanayopaswa kufanywa.

“Hapa umesema zaidi ya wafanyakazi 6,000 watakuwa kwenye eneo hili, lakini pia hata watakaokuwa wanakuja kufanya utalii kwenye National Park ya Nyerere ni lazima wawe na mawasiliano na mawasiliano ya sasa ni Data, kwahiyo tunachoweza kuagiza hususan TTCL ni kuhakikisha wanaenda kwa kasi kubwa kuweka mawasiliano katika eneo hili na mawasiliano tunayotaka sisi kama wadhibiti ni 4G as Minimum.” Alifafanua Mhandisi Kilaba na kuongeza

“Kwa hiyo 4G siyo isubiri mpaka turbines (mitambo ya kufua umeme)zianze kuzunguka, la hasha, ujumbe tunaowapa kwakweli mwisho wa mwezi wa Nane (Agosti) mwaka huu, watu waanze kupata huduma za 4G katika maeneo haya.” Alisisitiza.

Aidha Mwenyekiti wa Bodi ya TCRA, Dkt. Jones Killimbe alisema Mradi huo utakuwa na faida kubwa kwa nchi na kwamba TCRA imekuwa ikitembelea miradi mikubwa (Flagship Project), kama vile ujenzi wa SGR, Jengo la tatu la abiria la kiwanja cha ndege cha Julius Nyerere Terminal III na leo tumekuja hapa kutembelea mradi huu mkubwa wa kimakakati wa bwawa kubwa la kufua umeme wa maji ambao utachangia kwa kiasi kikubwa ukuaji wa uchumi, alifafanua Dkt. Kilimbe.

Alimshukuru Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa juhudi kubwa anazofanya kuhakikisha nchi inaelekea kwenye uchumi wa viwanda kwa uhakika zaidi kwa kuimarisha miundombonu wezeshi kama vile nishati ya Umeme wa uhakika na wa bei nafuu.

Nae Mhandsi Mkazi wa ujenzi wa bwawa hilo, Eng.Mushubila Kamuhambwa kutoka kampuni ya TECU, ambayo ni kampuni tanzu ya TANROADS, alisema bwawa hilo litakuwa ni miongoni mwa mabwawa makubwa yaliyotengenzwa na binadamu na litakuwa na urefu wa kilomita 100.

Akieleza faida za bwawa hilo licha ya kuzalisha umeme, pia shughuli za uvuvi wa samaki katika maeneo yatakayoainishwa, ongezeko la Mamba na Viboko ambao wanapatikana kwenye mto Rufiji lakin I pia kuwa kivutio cha utalii.

Hata hivyo alieleza changamoto za mawasiliano ya simu inayowakabili eneo la mradi na kuomba TCRA kuyahimiza makampuni ya simu kuboresha huduma zao."Umbi letu, tunaomba muwasukume hawa wanaotoa huduma za mawasiliano ya simu, kwakweli mawasiliano ni changamoto kubwa sana kwenye eneo hili." Alisisitiza Mhandisi Kamuhambwa.
Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Dkt. Jones Killimbe (kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo, Mhandisi James M. Kilaba (wapili kushoto) na mmoja wa wajumbe wa bodi, wakiwa kwenye eneo la Mto Rufiji ambako kunajengwa bwawa la kufua umeme wa maji Megawati 2115.
Baadhi ya wajumbe wa bodi na menejiment ya TCRA wakiwa kandokando ya Mto Rufiji Julai 28, 2019 wakati wa ziara ya kutembeela ujenzi wa Mradi wa umeme wa Mto Rufiji. 
Mwenyekiti wa Bodi, TCRA, Dkt. Jones Killimbe akifafanua jambo.
Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Mhandisi Jmes M. Kilaba, akizungumza mwanzoni mwa ziara hiyo.
Msafara wa TCRA ukipatiwa maelezo ya utekelezaji wa Mradi.
Msafara wa TCRA ukiwa eneo la mradi

Mamia waendelea kujitokeza uchunguzi homa ya ini Ocean Road

$
0
0
NA MWANDISHI MAALUM  - ORCI

WATU 481 wamejitokeza kupima Afya zao kutambua Iwapo wamepata maambukizi ya virusi vya homa ya ini katika Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI).

Akizungumza na waandishi wa habari mapema leo, Mkurugenzi wa Idara ya Huduma za Kinga ya Saratani Ocean Road, Dk. Crispin Andrew  Kahesa amesema idadi hiyo imeongezeka kutoka watu 150 ilivyokuwa jana.

Dk. Kahesa alikuwa akizungumza kuhusu kambi maalum ya uchunguzi wa virusi vya homa ya ini bila malipo iliyoanza kufanyika Julai 27 ambayo itamalizika  Julai 31, mwaka huu.

Amesema kambi hiyo inafanyika ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Homa ya Ini Duniani inayofanyika Julai 28, kila mwaka, kauli mbiu mwaka huu ikisema 'Tafuta mamilioni ya watu wenye maambukizi ya homa ya ini'.

Dk. Kahesa amesema kauli mbiu hiyo inalenga kila nchi kuhakikisha inawatambua watu wenye maambukizi ya homa hiyo ili wapate matibabu na kuwapa chanjo wale wasio na maambukizi ili kuwakinga.

Dk. Kahesa amesema kati ya watu wote 481 waliochunguzwa katika kampeni hii hadi sasa ni watu 18 wamekutwa na maambukizi.

"Mwitikio ni mkubwa kwa kundi la wanawake kuliko wanaume, nawasihi wanaume wenzangu nao wajitokeze kuchunguza, tumekusudia kuchunguza watu 1,000," ametoa rai.

Ameongeza "Tangu mwaka 2018 ORCI ilipoanza kufanya uchunguzi na kutoa chanjo dhidi ya ugonjwa huo, wameona watu wapatao 7,000 na 279 sawa na asilimia 3.9 kati yao walikutwa na maambukizi.

"Hii inamaanisha katika kila watu 100 nchini watu wanne wamepata maambukizi ya ugonjwa huu, aidha, takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO), zinaeleza kila mwaka watu wapatao milioni 10 duniani hugundulika kupata maambukizi kila mwaka," amesema.

Ameongeza "Hii inamaanisha kwamba watanzania wapo hatarini kupata maambukizi ya homa ya ini, virusi hivi vinaenezwa kwa njia mbalimbali hasa kupitia mfumo wa maisha.

"Kwa mfano kugusana na majimaji ya mwili kama damu, kutoka kwa mama (mwenye maambukizi) kwenda kwa mtoto wakati wa  kwa njia ya mama kujifungua, kushirikiana vitu vyenye ncha kali kama sindano, viwembe na hususani wale wanaotumia dawa za kulevya, kujamiiana pasipo kutumia kondomu.

"Ndiyo maana tunatoa rai kwa jamii waje tuwafanyie uchunguzi ni vizuri kugundua mapema na kuanza tiba kuliko kuchelewa ,"  na wale ambao hawana maambukizo wahakikishe wana pata chanjo tatu amesisitiza.
Mkurugenzi wa Idara ya Huduma za Kinga ya Saratani Ocean Road, Dk. Crispin Andrew  Kahesa

MBUNGE TARIME AKABIDHI MIFUKO YA SARUJI UJENZI WA CHOO CHA WANAFUNZI SHULE YA MSINGI BUHEMBA

$
0
0
Mbunge wa Jimbo la Tarime Mjini Mhe Esther N. Matiko amekabidhi mifuko 20 ya Saruji kwa ajili ya ujenzi wa Choo cha Wanafunzi kitakachokuwa na Matundu 21.

Mifuko hiyo ya Saruji imekabidhiwa na Katibu wa Mbunge (Peter Magwi Michael) mbele ya kikao cha Wazazi na Walezi wa watoto wanaosoma Shuleni hapo.

Akiwa ameambatana na Mhazini wa CHADEMA Jimbo la Tarime Mjini (Esther Nyaburiri) na Mwenyekiti wa CHADEMA Kata ya Bomani Ndg Mwita Joseph (White) aliyechangia Mifuko 2 ya Saruji kuunga juhudi za Mhe Matiko kushirikiana na wananchi wake katika kujiletea Maendeleo, Katibu wa Mbunge amewahasa Wazazi hao kwa niaba ya Mbunge kujitoa kwa hali na Mali kukamilisha ujenzi wa Choo hicho ili kuhepukana na dhahama inayoweza kujitokeza kwa kufungwa kwa Shule hiyo.

Itakumbukwa kuwa Mhe Matiko alipata kufanya ziara 19/07/2019 Shuleni hapo na kujionea tatizo la Choo cha Wanafunzi kinachotumika jinsi kilivyojaa na kusababisha kuzibwa kwa Matundu mengine na kuachwa matundu 2 tu yanayotumika.

Akizungumza kwa niaba ya wazazi waliokuwa kwenye kikao hicho, Mwenyekiti wa Kamati ya Shule amemshukuru Mhe Matiko kwa mchango wake huo na kuwaomba viongozi wengine waige mfano wa Mhe Matiko wakasaidiane nao katika kukamilisha ujenzi wa Choo hicho.

Wazazi wa Wanafunzi hao wakizungumza kwa nyakati tofauti tofauti waliokuwa kwenye kikao hicho wameuomba uongozi wa Kamati ya Shule kwenda kutafuta wadau wengine wajitokeze nao kusaidia ujenzi wa Choo hicho, “Tunaomba Mwenyekiti wa Kamati na Katibu tafuteni viongozi wengine waige mfano wa Mbunge wetu Esther Matiko, nendeni kwa Mkuu wa Wilaya, Diwani wa Kata yetu na Wafanyabiashara waje kutusaidia japo nasie tutaendelea kuchangishana kama kawaida yetu wala hatutochoka” alisema Ostadhi Ramadhani.

Katibu wa Mbunge alitumia nafasi hiyo pia kuwambia wananchi hao kuwa mchango wa Mhe Matiko wa Mifuko hiyo ya Saruji sio mwisho wa Mbunge kushirikiana na wazazi hao, “katika ujenzi wa Choo hiki tambueni kabisa Mhe Matiko ni sehemu yake, tuendelee kupeana taarifa kadri ujenzi utakavyokuwa unakwenda na Mhe Matiko hatosita kutoa kingine chochote kwa ajili ya Maendeleo ya watoto wetu” alisema Katibu wa Mbunge.
Viewing all 110170 articles
Browse latest View live




Latest Images