Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110181 articles
Browse latest View live

ULEGA ATOA MIFUKO 50 YA SARUJI KUSAIDIA UJENZI ZAHANATI YA MITARANDA

$
0
0
Wakazi wa Kijiji cha Mitaranda kata ya Kitombondo wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani, wametakiwa kujitolea kwa hali na mali katika ujenzi wa Zahanati ya kijijini hicho ili kuondokana na changamoto za huduma za kiafya zinazowakabili.

Wito huo umetolewa leo na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi ambaye pia ni Mbunge wa jimbo Mkuranga,Abdallah Ulega wakati akitoa msaada wa mifuko 50 ya saruji na fedha taslim laki tatu kwa ajili ya kuharakisha ujenzi huo.

Amesema ni muhimu kwa jamii kuwajibika kwa pamoja kwa maslahi yao na taifa kwani, kufanya hivyo kutawarahisishia upatikaji wa huduma hiyo kwa haraka.

Wakati akisoma risala mbele ya naibu waziri Ulega Afisa Mtendaji wa kijiji cha Mtaranda Jembe Ndembo amesema sanjari na ujenzi wa Zahanati hiyo pia wanamkakati wa kuinua kilimo ambapo kufikia msimu ujao kila Raia mwenye umri wa kuanzia miaka 18 awe na Ekari zisizopungua 2 ikiwemo ya mazao ya biashara na chakula , kuondokana na balaha la njaa na kuwainua wananchi kiuchumi.

Akizungumzia changamoto ya zahanati katika kijiji hicho Ndembo amesema kuwa kijiji hicho mpaka sasa hakina zahanati hali inayopelekea kinamama kujifungulia njiani."mpaka sasa tunatofari 2100 yaliyopatikana kwa nguvu za wananchi na halmashauri ,kupatikana kwa msaada huu tutapiga hatua sana katika ujenzi huu"alisema .

Naye Mwenyekiti wa halmashauri ya mkuranga,Juma Abeid amabye pia ni Diwani wa kata ya Magawa amempongeza mbunge huyo katika kufanikisha miondombinu ya umeme,Elimu na hata afya kwani amefanikisha katika kuleta maendeleo kwa haraka."wakati anaingia madarakani 2015 Ulega kulikuwa nachangamoto kubwa ikiwemo barabara na zahanati,lakini mpaka sasa ameshajenga zahanati zaidi ya Kumi kwakweli haijawahi kutokea kwa viongozi waliopita" Alisema Abeid

Katika hatua nyingine Waziri Ulega amefungua bonanza la michezo ndani ya wilaya ya Mkuranga lililowashirikisha timu mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu na wa pete huku akiwataka wachezaji hao na jamii kushiriki kikamilifu katika sekta ya michezo hatua ambayo itaongeza ushirikiano kwa jamii na kusaidia kuimarisha afya na upendo na kupelekea chachu ya maendeleo kwa mustakabali wa taifa.

Naibu Waziri wa Mifugo an Uvuvi ambaye pia ni Mbunge wa jimbo Mkuranga,Abdallah Ulega akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mitaranda kata ya Kitombondo katiaka mkutano huo wanachama wapya 50 walijiunga na Chama cha Mapinduzi kutoka Chama cha Wananchi (CUF)
Naibu Waziri wa Mifugo an Uvuvi ambaye pia ni Mbunge wa jimbo Mkuranga,Abdallah Ulega akiwa katika picha ya pamoja na wanachama wapya 50 walijiunga na Chama cha Mapinduzi kutoka Chama cha Wananchi (CUF)
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdalla Ulega akikabidhi mifuko ya Saruji 50 kwa wanakijiji wa Mitaranda kata ya Kitombondo kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa jengo la Zahanati ya Mitaranda.
Naibu Waziri wa Mifugo an Uvuvi ambaye pia ni Mbunge wa jimbo Mkuranga,Abdallah Ulega akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa mpira pete.
Naibu Waziri wa Mifugo an Uvuvi ambaye pia ni Mbunge wa jimbo Mkuranga,Abdallah Ulega akizungumza na wachezaji wa mpira wa miguu ambapo aliwaomba wachezaji hao na jamii kushiriki kikamilifu katika sekta ya michezo hatua ambayo itaongeza ushirikiano kwa jamii na kusaidia kuimarisha afya.

MAJALIWA MGENI RASMI MAADHIMISHO YA ZINJANTHROPUS JULAI 22 MWAKA HUU ENEO LA OLDUVAI

$
0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa 


Na Ahmed Mahmoud Arusha 

Waziri Mkuu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa anatarajiwa kuwa Mgeni rasmi katika sherehe za maadhimisho ya miaka 60 ya ugunduzi wa fuvu la zinjanthropus tarehe 22 julai mwaka huu na miaka 60 ya hifadhi ya Serengeti. 

Akizungumza na vyombo vya habari jijini Arusha Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya sherehe hizo Prof. Audax Mabula amesema kuwa sherehe za awali ambazo zilikuwa zifanyike julai 17 sasa zitafanyika julai 22 mwaka huu eneo la Olduvai ndani ya mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro. 

Amesema kuwa pia kuna mabadiliko ya warsha iliyokuwa inaandaliwa kufanyika Tarehe 16 julai sasa itafanyika tarehe 20 julai mwaka huu katika ukumbi wa mikutano wa AICC Jijini Arusha. 

“Kutoka na sababu zisiweza kuzuilika sherehe za ugunduzi wa fuvu la kale ambazo zilikuwa zifanyike julai 17 sasa zitafanyika Julai 22 eneo la Olduvai na Mh.Kassim Majaliwa atakuwa mgeni rasmi katika sherehe hizo hivyo wananchi wote mnakaribishwa kuja kujionea fuvu la mwanadamu wa kale siku hiyo” 

Amesema kuwa kutakuwa na ofa maalumu ya kutembelea makumbusho ya olduvai pamoja na maonyesho maalumu kutoka sehemu mbali mbali nchini yenye urithi wa kiutamaduni yataendelea kama yalivyopangwa kuanzia tarehe 17 hadi 22 juali mwaka huu. 

Ameeleza kuwa Kutokana na maadhimisho hayo watafiti kutoka sehemu mbali mbali duniani wanatarajiwa kukutana jijini Arusha kuanzia julai 17 na watalii wakiwamo wa ndani wanatarajiwa kutembelea maeneo hayo ambapo fuvu hilo kwa Mara ya kwanza litatolewa hadharani na kuonyeshwa ambapo watu mbalimbalinwatapata fursa ya kujionea. 

Amesema kuwa kauli mbiu ya siku hiyo “Tujivunie urithi na chimbuko letu” ambapo aliwataka wananchi wote kpenda kutembelea hifadhi hiyo ya Ngorongoro kujionea maajabu ya binadamu wa kale na kuweza kuutangaza utalii wa ndani. 

Alisema kuwa ili kuhamasisha Watazania na watalii kufuatilia maadhimisho hayo ya miaka 60 ya Olduvai na Serengeti taarifa zinapatikana kwenye mitandao kwa anuani #Tanzaniazinjanthropus60years na #tanapa@60. 

Ugunduzi w zinjanthropus katika tafiti za chimbuko la mwanadamu wa kale pamoja na fuvu ni moja ya rasilimali za kutangazwa kote ulimwenguni na siku hiyo kwa mara ya kwanza fuvu hilo litawekwa Olduvai Gorge ni faida yetu kiuchumi na kiutalii.

MAJALIWA AKAGUA MWENENDO WA UUZAJI WA PAMBA WILAYANI IGUNGA

$
0
0

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua pamba wakati alipotembelea ghala la Chama cha Msingi cha cha Ushirika cha kijiji cha Mwabakima wilayani Igunga akiwa katika ziara ya siku moja wilayani humo ya kukagua mwenendo wa ununuzi wa zao hilo, Julai 15, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
Waziri Mkuu, Kasism Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Katibu na Meneja wa Chama cha Msingi cha Ushirika cha kijiji cha Mwabakima wilayani Igunga kuhusu pamba iliyokusanywa na wakulima kwenye ghala la ushirika huo, Julai 15, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua mikokoteni iliyosheheni pamba wakati alipotembelea ghala la Chama cha Msingi cha Ushirika cha kijiji cha Mwabakima wilayani Igunga alikofanya ziara ya siku moja ya kukagua mwenendo wa ununuzi wa zao hilo, Julai 15, 2019. Kushoto ni Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga na wa pili kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
Wananchi wa kijiji cha Mwabakima wilayani Igunga wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipowahutubia akiwa katika ziara ya siku moja wilayani humo ya kukagua mwenendo wa ununuzi wa zao la pamba, Julai 15, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akihutubia mkutano wa hadhara katika kijiji cha Mwabakima wilayani Igunga akiwa katika ziara ya siku moja wilayani humo ya kukagua mwenendo wa ununuzi wa zao la pamba, Julai 15, 2019. Kushoto ni Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga na kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

CSP KUPAMBANA NA UKEKETAJI MANYARA

$
0
0
Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la Civil Social Protection Foundation (CSP) Nemency Iriya akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mikakati ya kupambana na vitendo vya ukeketaji. 
Waandishi wa habari wa Mkoa wa Manyara, wakimsikiliza Mkurugenzi wa CSP, Nemency Iriya akizungumza nao juu ya mikakati ya kupambana na vitendo vya ukatili vya ukeketaji. 

*************** 


KATIKA kupambana na ukeketaji ulioenea Mkoani Manyara, shirika lisilo la kiserikali la Civil Social Protection Foundation (CSP) limeanzisha mradi wa mwaka mmoja wa kubadili vikwazo vya kiutamaduni na kutokomeza vitendo hivyo. 

Mkurugenzi wa CSP Nemence Iriya akizungumza na waandishi wa habari mjini Babati alisema wameanzia wilayani Hanang’ kisha watafuata wilaya nyingine za mkoa huo. 

Iriya alisema watawatumia wazee wa kimila wa eneo hilo katika kikao chao ili kuhakikisha wanatokomeza vitendo hivyo vya kikatili ambavyo mkoa wa Manyara unaongoza nchini kwa asilimia 58. 

Alisema wameazimia kutumia mijadala kwa jamii ili kutokomeza vitendo hivyo kuliko kuwashurutisha kwani ni bora kubadili fikra zao wenyewe na kuongeza uelewa wa moja kwa moja. 

“Ukeketaji umejikita kwenye kanuni na taratibu za kijamii, imani za utamaduni na vichocheo vya kiuchumi na unatumika kama njia ya kudhibiti ashki ya kujamiiana kwa wanawake,” alisema Iriya. 

Alisema katika jamii nyingi inachukuliwa kama jambo la muhimu kwenye shughuli za jando na unyago na simulizi potofu za ukeketaji zimekuwa zinajirudia mara kwa mara. 

Mwezeshaji wa mafunzo ya kupinga ukatili wa kijinsia, Charles Odero alisema wamewajengea waandishi wa habari uwezo zaidi ili jamii izidi kufaidika kupitia vyombo vyao. 

Odero alisema kupitia taarifa za waandishi hao jamii itazidi kupata uelewa wa madhara ya vitendo vya kikatili vya ukeketaji ambapo mkoa wa Manyara unaongoza kwa vitendo hivyo kwa hapa nchini.  

Alisema waandishi hao wataeleza hali ipoje, nani anahusika, inasababishwa na nini, sheria, mipango, mikataba ya kimataifa inaelezeaje juu ya hayo na kusikiliza jamii pia ikizungumza juu ya hilo. 

Makamu Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa habari wa mkoa wa Manyara, (Mamec) Mary Margwe alisema hivi sasa baada ya serikali kuongeza nguvu za kupambana na ukeketaji jamii imebadili mtindo kwa kuwakeketa watoto wachanga kwa kutumia kucha. 

“Elimu inapaswa kuendelea kutolewa kwa jamii ili kuhakikisha vitendo hivi vinamalizika kwani vimepitwa na wakati na wanapaswa kubadilika tofauti na miaka iliyopita,” alisema Margwe. 

Kuendelea kuwepo kwa vitendo vya ukeketaji nchini, kumeelezwa kama eneo lenye kuleta wasiwasi wa utekelezaji wa mikataba ya haki za binadamu ambayo Tanzania imeridhia.

SERIKALI,BUZWAGI KUSHIRIKIANA KULINDA ULINZI NA USALAMA KAHAMA

$
0
0

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni,akipokea zawadi ya kitabu cha kuhifadhia kumbukumbu kutoka kw Kaimu Meneja Mkuu wa Mgodi wa Dhahabu wa Buzwagi ,Arthur Mgongo wakati Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilayani Kahama ilipotembelea mgodi huo ikiwa ni ziara ya kuimarisha Ulinzi katika wilaya hiyo.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni,akionesha zawadi ya kitabu cha kuhifadhia kumbukumbu alichopokea kutoka kwa Kaimu Meneja Mkuu wa Mgodi wa Dhahabu wa Buzwagi ,Arthur Mgongo(kushoto), wakati Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilayani Kahama ilipotembelea mgodi huo ikiwa ni ziara ya kuimarisha Ulinzi katika wilaya hiyo.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akiongozana na Kaimu Meneja Mkuu wa Mgodi wa Dhahabu wa Buzwagi , Arthur Mgongo (kulia) wakati Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilayani Kahama ilipotembelea mgodi huo ikiwa ni ziara ya kuimarisha Ulinzi katika wilaya hiyo.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza wakati Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilayani Kahama ilipotembelea mgodi huo ikiwa ni ziara ya kuimarisha Ulinzi katika wilaya hiyo.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Kaimu Meneja Mkuu wa Mgodi wa Dhahabu wa Buzwagi ,Arthur Mgongo akizungumza mbele ya Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia), wakati Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilayani Kahama ilipotembelea mgodi huo ikiwa ni ziara ya kuimarisha Ulinzi katika wilaya hiyo.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MAPAMBANO YA RUSHWA YANG’ARISHA OFISI YA RAIS NA OFISI YA WAZIRI MKUU

$
0
0

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema juhudi za Serikali za kupambana na
rushwa, kudhibiti upotevu wa mapato, matumizi ya fedha za Serikali na
kusimamia uwajibikaji kwa watumishi wa umma ni sababu zilizowezesha Ofisi yaRais pamoja na Ofisi ya Waziri kuaminika zaidi. 

Ameyasema hayo mwishoni mwa wiki wakati akizungumza na viongozi wa Umojawa Wanake Tanzania (UWT) akiwa katika ziara yake ya kikazi mkoani Kigoma.Amesisitiza kuwa vita dhidi ya rushwa ni endelevu. Waziri Mkuu amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Tano, inayoongozwa na Rais
Dkt. John Magufuli imepiga hatua kubwa katika vita dhidi ya rushwa ambapo kwaAfrika Tanzania inaongoza kwa mujibu wa ripoti ya taasisi ya TransparencyInternation iliyotolewa hivi karibuni. 

Ripoti hiyo mpya iliyotolewa Julai 11, mwaka huu inaonesha kwamba kwa sasa Tanzania inaongoza katika nchi 35 za Afrika baada ya kupungua kwa vitendo vyarushwa katika sekta nyingi, ambapo Ofisi ya Rais na Ofisi ya Waziri Mkuu zimeonekana kuaminika zaidi. Kadhalika, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwatahadharisha watumishi waumma kwamba Serikali kamwe haitomvumilia mtumishi atakayebainikaanayejihusisha na vitendo vya rushwa na aliwataka wahakikishe kuwawanatekeleza majukumu yao ya kuwatumikia wananchi bila ubaguzi. 

Waziri Mkuu amesema Serikali imejipanga vizuri katika mapambano dhidi ya rushwa, hivyo amewataka wananchi wasisite wakati wote kutoa taarifa kwa vyombo husika pale watakapobaini uwepo wa watumishi wanaojihusisha na vitendo vya kuomba na kupokea rushwa. “Watumishi wa umma wanatakiwa kutambua kwamba jukumu lao kubwa nikuwatumikia wananchi kwa kuzingatia maadili na kanuni za utumishi wa umma 

zilizowekwa kwa mujibu wa sheria na kanuni na si vinginevyo. Serikali hii kamwehaitowaonea haya au kuwafumbia macho watumishi wa hovyo.” 
Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema kuwa suala la kuwaondoa kazini watumishi wazembe, wasiotimiza wajibu wao ipasavyo pamoja na wale wasiozingatia maadili ya utumishi wa umma ni endelevu kwa sababu Serikali inahitaji watumishiwa umma wenye heshima na nidhamu ya kazi. 

Suala la kuwapokea, kuwasikiliza na kuwahudumia wananchi katika maeneo mbalimbali ya kutolea huduma kwa wananchi zikiwemo ofisi za Serikali kuanziangazi ya kijiji hadi Taifa ni miongoni mwa vipaumbele vya Serikali ya Awamu yaTano, hivyo watumishi wa umma wanapaswa kuzingatia jambo hilo.

MSAJILI AZITOA HOFU NGOs AZITAKA ZILIZOKUWA NJE YA SHERIA KUJITOKEZA KUJISAJILI

$
0
0
Mwanasheria kutoka Ofisi ya Msajili wa NGOs Bi. Idda Kombe akitoa huduma kwa mmoja wa wadau kutoka Taasisi na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ambayo awali yalisajiliwa chini ya Sheria nyingine akipata huduma ya kusajili Taasisi yake chini ya Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Na. 24 ya mwaka 2002 kama ilivyofanyiwa marekebisho na Sheria Na. 3/2019 katika zoezi linaloendelea kufanyika kwenye Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam kwa Kanda ya Mashariki. 
Mwanasheria kutoka Ofisi ya Msajili wa NGOs Faki Shaweji akifafanua jambo kwa mmoja wa wadau kutoka Taasisi na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ambayo awali yalisajiliwa chini ya Sheria nyingine akipata huduma ya kusajili Taasisi yake chini ya Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Na. 24 ya mwaka 2002 kama ilivyofanyiwa marekebisho na Sheria Na. 3/2019 katika zoezi linaloendelea kufanyika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam kwa Kanda ya Mashariki. 
Afisa kutoka Ofisi ya Msajili wa NGOs Bi. Irene Mayala akitoa huduma kwa mmoja wa mdau kutoka Taasisi na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ambayo awali yalisajiliwa chini ya Sheria nyingine akipata huduma ya kusajili Taasisi yake chini ya Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Na. 24 ya mwaka 2002 kama ilivyofanyiwa marekebisho na Sheria Na. 3/2019 katika zoezi linaloendelea kufanyika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam kwa Kanda ya Mashariki. 
Wadau kutoka Taasisi na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ambayo awali yalisajiliwa chini ya Sheria nyingine akipata huduma ya kusajili Taasisi yake chini ya Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Na. 24 ya mwaka 2002 kama ilivyofanyiwa marekebisho na Sheria Na. 3/2019 katika zoezi linaloendelea kufanyika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam kwa Kanda ya Mashariki. 



Msajili na Mkurugenzi wa Idara ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Vickness Mayao amewatoa hofu wadau wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali nchini kuwa Serikali haina nia mbaya na Mashirika hayo ila inataka iwe na utaratibu mzuri wa kuyaratibu Mashirika hayo. 

Ameyasema hayo leo jijini Dar Es Salaam wakati alipozungumza na waandishi wa habari kuhusiana na zoezi la usajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali linaloendelea jijini Dar es Salaam kwa Kanda ya Mashariki. 

Amesema kuwa utaratibu wa usajili umerahisishwa sana hasa ule wa Mashirika yaliyokuwa yamesajiliwa katika Sheria nyingine. 

Ameongeza kuwa Wadau wameridhishwa na huduma zinazotolewa na Ofisi yake na kusema wanapata mrejesho mzuri kutoka kwa wadau kupitia fomu za mrejesho wa zoezi hilo. 

Kwa upande wake mdau kutoka Taasisi ya Solidame Ifakara Bw. Ali Mzava ametoa rai kwa wadau wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali yaliyosajiliwa chini ya Sheria nyingine kujitokeza kwa wingi kujisajili chini ya Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali kwani usajili umeboreshwa na hakuna tatizo lolote katika zoezi hilo. 

Naye Mkurugenzi wa Shirika la Tanzania Community Development Assistant Bw. Denis Mchunguzi amesema kuwa wadau wameyapokea vizuri mabadiliko ya Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Na. 3 ya Mwaka 2019 kwani wameitikia wito na kujitokeza kwa wingi na hawana tatizo na utekelzaji wa marekebisho ya Sheria hiyo. 

Ofisi ya Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali inaendelea na zoezi la usajili wa Mashirika yaliyosajiliwa awali chini ya Sheria nyingine kama vile “Societies Act Cap 337” (Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nch); “Trustees’ Incorporation Act Cap. 318 (RITA); na The Companies Act Cap 212 (Msajili wa Makampuni-BRELA) ambazo zinatakiwa kujisajili chini ya Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Na. 24 ya mwaka 2002 kama ilivyofanyiwa marekebisho na Sheria Na. 3/2019. 

Usajili huu umeanza katika Kanda ya Mashariki (Dar es Salaam, Lindi, Mtwara, Pwani na Morogoro) na Kituo kitakuwa Ofisi za Wizara ya Afya-Dar es Salaam kuanzia tarehe 10-19/07/ 2019.

WIZARA YAJA NA MFUMO WA KIMTANDAO KUPATA TAARIFA ZA WANAWAKE NCHINI

$
0
0
Bi. Sylivia Siriwa akiongea na wajumbe wa kikao kazi kuhusu mfumo maalum wa mtandao utakaowezesha kupata wasifu wa wanawake wasomi, wanasiasa na wale wanaofanya kazi za kitaalam nje ya nchi. 
Mkurugenzi Mkuu toka TGNP Mtandao Bi. Lilian Liundi akiongea na wajumbe wa kikao kazi kuhusu mfumo maalum wa mtandao utakaowezesha kupata wasifu wa wanawake wasomi, wanasiasa na wale wanaofanya kazi za kitaalam nje ya nchi. 
Baadhi ya Washiriki wa kikao kazi kuhusu mfumo maalum wa mtandao utakaowezesha kupata wasifu wa wanawake wasomi, wanasiasa na wale wanaofanya kazi za kitaalam nje ya nchi wakifuatalia mada kuhusu namna mfumo huo utakavyokuwa ukifanya kazi. 
Bi. Jennifer Mwengwa toka TGNP Mtandao akiongea na wajumbe wa kikao kazi kuhusu mfumo maalum wa mtandao utakaowezesha kupata wasifu wa wanawake wasomi, wanasiasa na wale wanaofanya kazi za kitaalam nje ya nchi. 
…………………… 
Na Mwandishi wetu Morogoro. 

Wizara ya Afya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii kwa kushirikiana na TGNP Mtandao inatayarisha mfumo maalum wa mtandao utakaowezesha kupata wasifu wa wanawake wasomi, wanasiasa na wale wanaofanya kazi za kitaalam nje kwa kuweka taarifa zao kwenye mfumo ili iwe rahisi kwao kupata fursa za ajira ikiwemo na uteuzi katika nafasi mbalimbali. 

Akiongea wakati wa mapitio ya mfumo huo mapema leo mjini Morogoro Afisa Maendeleo Mkuu kutoka Wizara ya Afya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii Bi. Sylivia Siriwa amewaambia wajumbe wa Mkutano huo kuwa lengo la Mfumo huo nikuwezesha wanawake wenye vipaji, ubunifu na elimu kuweza kufahamika wapi walipo na kutumia taarifa binafsi au wasifu wao kama taarifa muhimu ya kuwangaunisha na fursa mbalimbali zilizopo na katika uteuzi wa nafasi za uongozi na kutoa maamuzi. 

Aidha Bi. Siriwa aliongeza kuwa mfumo huu utasaidia mwajiri na wenye kuhitaji kuajiri mwanamke mwenye sifa, uzoefu na taaluma anayotaka kutumia mfumo huu kumpata kwa kuwa unakuwa na wasifu na taarifa za mhusika tofauti na sasa ambapo waajiri wanakuwa hawana taarifa za wanawake wenye sifa zinazohitajika kukidhi sifa zinazotakiwa na mwajiri. 

Naye Mkurugenzi wa TGNP Mtandao Bi. Lilian Liundi aliwambia wajumbe wa kikao kazi hao kuwa baada ya kuanza kutumika na kuweka taarifa za wanawake kwenye mfumo huo ndipo wataweza kuona mapungufu yaliyopo na kuyafanyia kazi ikiwemo kutoa ushauri kwa vyombo vya maamuzi na kuwezesha wanawake pia kuwa katika sehemu za maamuzi na nafasi nyinginezo. 

Aidha Bi. Liundi aliongeza kuwa ukienda katika Taasisi binafsi kama Azam na Makampuni ya Mo Enterprises unakuta wanawake ni wachache lakini pengine wamiliki wa kampuni hizo hawana taarifa za uwepo wanawake wenye ujuzi hivyo mifumo kama hii itawezesha wamiliki wa makapuni haya kutoa nafasi kwa wanawake zaidi katika sekta binafsi. 

Bi. Liundi aliongeza kuwa pamoja na mfumo huu kuwepo Taasisi yake pamoja na Wizara watafanya uchambuzi wa bodi mbalimbali kuangalia uwiano wa kijinsia kwa kuangalia idadi ya wanawake na wanaume na kutoa ushauri kwa mamlaka za uteuzi kwa kuwasilisha taarifa za wanawake wenye sifa ili kuona kama wanawake wanaweza kuwa sehemu uteuzi wa nafasi zinazotakiwa kulingana na sifa. 

Aidha Bi. Liundi alisema kuwa wakati wa uwekaji taarifa katika Mfumo huo wataweza kuona viwango vya wanawake akiwataja kuwa wa viwango vya chini kati na juu jambo litakalo wawezesha kufanya uchambuzi wa namna ya kusaidia kuwainua kiutendaji na kitaaluma kwa wale walio na elimu ya chini kuwapatia fursa za masomo na wale wakati wenye elimu kuwapatia fursa za juu zaidi. 

Kuanzishwa kwa mfumo huu kunatokana na azimio la Siku ya Kimataifa ya Wanawake ya mwaka 2017 ambapo Waziri wa Afya Ummy Mwalimu aliagiza kuanzishwa kwa mfumo huu utakaowezesha kuwepo kwa taarifa za wazi kwa wanawake wenye sifa ili waweze kupatikana na kutumiwa kwa Maendeleo ya Taifa.

CCM ARUSHA WAMCHAGUA KATIBU MWENEZI MPYA

$
0
0
Na Woinde Shizza Michuzi Tv,Arusha

WAJUMBE wa kikao cha Halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi CCM,Mkoa w Arusha kimemchagua Gerad Munisi kuwa Katibu Mwenezi wa mkoa huo kujaza nafasi hiyo iliyokuwa wazi kutokana na aliyekuwa Katibu Uenezi Shaban Mdoe kuteuliwa kuwa Katibu wa CCM wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro.

Ushindi huo haukuwa rahisi ilibidi kuingia awamu ya pili kutokana na awamu ya kwanza mshindi kutokuvuka nusu ya kura .Ambapo awamu ya Kwanza Gerad Munisi alipata Kura 26 ,Bakari Rahib Msangi alipata kura 21 na Elipokea Urio alipata kura 7

Katika awamu ya Pili Gerad Munisi alizoa kura 33 na Bakari Rahm Msangi alipata kura 19 na Ndipo msimamizi wa Uchaguzi huo Katibu wa ccm mkoa wa Arusha, Mussa Matoroka, alipomtanga Gerad Munisi kuwa mshindi baada ya kuvuka nusu ya kura .

Akitoa Nasaha zake Munisi, ameahidi utumishi uliotukuka na pia atashirikiana na kila mmoja kwa ajili ya kazi za chama .Amesema siku za hivi karibuni kumekuwa kukitolewa taarifa za upotoshaji na vyama vya upinzani kutokana na miradi inayotekelezwa na serikali maeneo mbalimbali ambapo wanakuwa wakidai wao ndio wameileta jambo ambalo sio la kweli.

Akiahirisha uchaguzi msimamizi wa uchaguzi Mussa Matoroka, amewasisitiza wajumbe kuhakikisha wanasimama kidete kuhakikisha wananchi wanajitokeza kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa ambao utafanyika hivi karibuni nchini kote.

UVCCM yatamba kumpa kura za heshima JPM

$
0
0
Makamu Mwenyekiti wa UVCCM, Tabia Mwita akiwa ameshika zawadi ya picha ya Rais Dk. John Magufuli. 
Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Dar es Salaam, Mussa Kilakala, akiendesha mnada wa keki ambayo ilinunuliwa kwa Sh milioni 1.8 Kulia ni mgeni rasmi Makamu Mwenyekiti wa UVCCM, Tabia Mwita.
Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Dar es Salaam, Mussa Kilakala, akizungumza katika uzinduzi wa Ilala ya Kijani. 


UMOJA wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), umesema kuwa sasa unajipanga kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020 kwa kuhakikisha unampatia kura za heshima Rais Dk. John Magufuli. 

Pamoja na hali hayo, UVCCM imesema ni vema chama kikatoa fursa kwa vijana kuwania nafasi mbalimbali za uongozi kama njia ya kumuenzi Rais Magufuli ambaye ameamua kuwaamini katika nafasi mbalimbali za uongozi serikalini. 

Akizungumza Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa Ilala ya Kijani, Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Dar es Salaam, Mussa Kilakala, amesema wao kama vijana kwa sasa wanatembea kifua mbele kutokana na kazi kubwa inayofanywa na Rais Magufuli pamoja na wasaidizi wake, wakiwamo Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na mawaziri. 

Kilakala amesema viongozi hao wamekuwa wakijenga heshima kwa nchi na chama kwa kuhakikisha wanasimamia falsafa na misingi ya CCM kwa kuimarisha mshikamano kwa Watanzania. 

“Ndugu Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Taifa (Tabia Mwita), sisi vijana wa Dar es Salaam tunatembea kifua mbele kwani Rais Magufuli amekiheshimisha chama na taifa letu kwa ujumla na mwaka 2020 tutampatia kura za heshima. 

“Lakini pia kama kiongozi wa nchi (Rais Magufuli), ameweza kuwaamini vijana basi na uchaguzi wa mwaka huu tunakiomba chama kitoe tamko la kutokata majina ya wagombea vijana ambao muda wote wamekuwa wakikijenga chama kwa kuimba ‘hiyena hiyena’ na sasa nao waweze kuingia katika uongozi wa Serikali za Mitaa, udiwani na hata ubunge,” amesema Kilakala. 

Mgeni rasmi katika mkutano huo wa ndani, Makamu Mwenyekiti wa UVCCM, Tabia Mwita, amesema kuwa ili kijana aweze kutimiza wajibu wake, ni lazima ahahakikishe anajiandikisha na kuwa na kitambulisho cha kupigia kura. 

Tabia alisema hatua hiyo itahakikisha ushindi mnono wa CCM kwa kushinda viti vya mitaa, vijiji na vitongoji pamoja na Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020. 
Amesema agizo la CCM ni kuhakikisha inashinda nafasi zote za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa pamoja na Serikali Kuu. 

“Kama kuna mtendaji yeyote atakayekwamisha uandikishaji kwenye Daftari la Kudumu la Wapigakura toeni taarifa haraka ili tumpe taarifa Mwenyekiti wa CCM Rais John Magufuli,” amesema Tabia. 

Pia ametoa onyo kwa mataifa yanayojaribu kuisemea demokrasia ya nchi na kuwataka watatue matatizo yanayowakabili badala ya kushughulika na Tanzania. Pia aliwataka viongozi wa chama hicho kushirikiana na kuepuka migogoro ya ndani inayokigawa chama hicho kipindi cha uchaguzi. 

“Tuacheni tabia za kubomoana wenyewe kwa wenyewe, tunahitaji ushirikiano na muelekezane kwa utaratibu uliowekwa na chama,” amesema Tabia. Mwenyekiti wa UVCCM, Wilaya ya Ilala, Amani Pazi, amesema wamefanya uchunguzi na kubaini kwamba asilimia 80 ya wapigakura ni vijana, hivyo ili kuweza kushinda uchaguzi wagombea vijana wapewe kipaumbele zaidi. 

Katika mkutano huo, wanachama 200 walijiunga na CCM akiwamo aliyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha) upande wa Vyuo Vikuu, Jackson Nzinza.

MSAJILI AZITOA HOFU NGOs AZITAKA ZILIZOKUWA NJE YA SHERIA KUJITOKEZA KUJISAJILI

SERIKALI YAPIGA MARUFUKU TAASISI ZA FEDHA KUSHIKILIA KADI ZA BENKI KUTOKA KWA WALIMU NA WATUMISHI WENGINE WA UMMA

$
0
0
Na Mwandishi Wetu,Tunduru

SERIKALI mkoani Ruvuma, imepiga marufuku taasisi za fedha ambazo hazijasaliwa na zinawakopesha walimu na watumishi wengine wa Umma katika mkoa huo, kuacha mara moja kuchukua vitambulisho na kadi za benki kama dhamana.

Kwani taasisi hizo zinakwenda kinyume na mifumo ya ukopeshaji, na zina wadhalilisha sana walimu na kupelekea baadhi yao kuhaathirika kisaikolojia na hivyo kushindwa kutekeleza wajibu wao.

Kauli hiyo imetolewa jana na Mkuu wa mkoa huo Christina Mndeme, alipokuwa anaongea na walimu wa shule za msingi na sekondari na waratibu Elimu kata, wakati wa hafla ya kuwapongeza Walimu wa mkoa huo kufuatia na matokeo mazuri katika mitihani ya darasa la saba 2018 na kidato cha sita 2019.

Pia,amewaasa Walimu kuishi kwa maadili mema na kujiepusha na madeni kupita kiasi na kwa kuwa tabia hiyo inawafanya washindwe kufundisha watoto madarasani.

“taasisi za fedha zilizopo mitaani ziache kuchukua kadi za benki na vitambulisho vya watumishi, tabia hii sitaki kusikia katika mkoa wangu kwani inawadhalilisha na kuwaibia watumishi,siko tayari kuona walimu wanaendelea kuumia”alisema Mndeme.

Sambamba na hilo amewashauri walimu wasiwe wapesi wa kutoa kadi za benki na kutokubali kuingia katika mikataba ambayo haina masilahi kwa familia.

Alisema, hawezi kuzui mwalimu kukopa fedha,lakini ni muhimu kutumia taasisi zinazo fuata sheria,kanuni na taratibu za nchi.
Amewataka walimu wakuu kuwa na ushirikiano mkubwa na walimu walio chini yao,kuwapenda na kuwa kama familia ili kutoathiri taaluma.

Aidha,amewapongeza Walimu wa wilaya ya Tunduru na mkoa mzima wa Ruvuma kwa kupandisha taaluma ya mkoa ambayo imepelekea mkoa huo kupata tuzo sita kwa shule za Msingi,kati ya tuzo hizo Halmashauri ya wilaya Tunduru imefanikiwa kupata tuzo nne.

Alisema, mafaniko hayo ni matokeo ya mshikamano mkubwa uliopo kati ya walimu wenyewe na viongozi wa wilaya ambao ndiyo wanao simamia sekta ya Elimu.

Kwa mujibu wa Mndeme,jitihada hizo si za kubeza kwani pamoja na upungufu mkubwa waWalimu lakini ukweli ni kwamba ufaulu unazidi kuongezeka mwaka hadi mwaka na hiyo ni hatua madhubuti na makusudi ya wilaya ya Tunduru kuongeza ufaulu ili kufikia malengo ya Chama cha Mapinduzi ya kufaulisha kwa asilimia 90 ifikapo Mwaka 2020.

Alisema, Serikali imeendelea kuleta walimu ambapo jumla ya walimu 111 kati yao Walimu wa Sekondari 15 na Msingi 96 wamepelekwa katika wilaya ya Tunduru.

Amewaomba Walimu,waendelee kuchapa kazi na kuwapuuza wale wote wanao wakatisha tamaa kwa lengo la kuwavunja moyo.Kwa upande wake,katibu Tawala wa mkoa huo Profesa Rizik Shemdoe alisema,wilaya ya Tunduru imefanya vizuri katika skta ya Elimu kwa hiyo inastahili kupewa heshima kubwa.

Alisema, licha ya wilaya hiyo kuwa na idadi kubwa ya shule za Msingi,hata hivyo jambo la faraja kuona ndiyo wilaya yenye mafaniko makubwa katika mkoa huo kwa kipindi cha miaka miwili mfululizo.

Awali Afisa Elimu msingi wa wilaya ya Tunduru Mwalongo alisema,katika matokeo ya kidato cha nne ufaulu wake umekuwa ukiongezeka mwaka hadi mwaka kutoka wastani wa asilimia 76 hadi 100 ambapo shule 19 zilifanikiwa kuingia kuwa shule Bora Kitaifa.

Mwalongo alisema, kwa upande wa shule za msingi shule 54 zilifaulisha kwa asilimia 94 hadi 100 na mafanikio hayo yametokana na ushirikiano kutoka kwa wadau wote wa sekta ya Elimu.

Pia alisema, mwaka 2019 Halmashauri kupitia idara ya Elimu imefanikiwa kulipa madeni yote ya walimu sambamba na kulipa stahiki zote za wastaafu kwa kipindi cha miezi sita pamoja na alimu 506 wamepandishwa madaraja.

DC Kigamboni aipongeza UBA Tanzania, yagawa vitabu

$
0
0
MKUU wa Wilaya ya Kigamboni, Sara Msafiri, ameipongeza Benki ya UBA Tanzania kwa mchango mkubwa ambao inatoa kwenye sekta ya elimu kwa kutoa vitabu zaidi ya 15,000 kwa shule za sekondari zote zenye uhitaji wa vitabu zilizopo wilaya humo.

UBA Tanzania kupitia UBA Foundation chini ya mpango wa ‘Read Africa Initiative’, imetoa vitabu hivyo vya fasihi kwenye shule za Serikali zilizopo wilaya mpya ya Kigamboni.

Shule ambazo UBA imetembelea ni Nguva Sekondari, Aboud Jumbe Sekondari na Pemba mnazi Sekondari zote zipo ndani ya wilaya hiyo.

Wengine waliokuwepo kwenye tukio hilo ni Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Kigamboni, Ng’wilabuzu Ludigija na Ofisa Elimu wa Wilaya, ambapo uongozi wa benki hiyo uliongozwa na Geofrey Mtawa ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha Biashara ndogondogo na za Kati, Mkuu wa Kitengo cha Dijitali, Asupya Nalingigwa na Ofisa Mawasiliano, Anitha Pallangyo.

“Vitabu hivi vilivyotolewa na Benki ya UBA Tanzania, vitasaidia katika kuwajengea vijana wetu kupenda kujisomea na kujiwekea utaratibu wa kujisomea mara kwa mara, pamoja na kuwaongezea uwezo katika masomo yao,” amesema Msafiri.

Geofrey alisema vitabu hivyo ni vya hadhi ya juu Afrika, ambavyo vimeboreshwa zaidi ili kuwawezesha wanafunzi na walimu kuvielewa kwa lugha rahisi na yenye kuelimisha.

Mbali na kutoa vitabu hivyo, UBA imekuwa ikisaidia sekta ya elimu kwa kutoa vitabu kwenye shule mbalimbali ikiwa ni pamoja na wilaya za Ilala, Temeke nkoani Dar es Salaam na Kisarawe mkoani Pwani, pamoja na kutoa elimu ya ujasiriamali bure kwa vijana na wanawake kupitia mpango wao wa ‘Each one teach one’.

Baadhi ya vitabu vilivyotolewa na benki hiyo ni vile vinavyotumika kwenye mitaala ya Tanzania kama ‘Things Fall Apart’, ‘The Girl That Can’, ‘The Fisherman’ na vinginevyo vingi kutoka kwa waandishi mashuhuri kutoka Nigeria ambavyo pia hutumika kwenye mitaala ya shule mbalimbali Afrika.



MBARAWA AFANYA UTEUZI WA WAKURUGENZI WATENDAJI WA MAMLAKA ZA MAJISAFI NA USAFI WA MAZINGIRA

RAIS DKT.MAGUFULI MGENI RASMI MAADHIMISHO YA MIAKA 80 KANISA LA TAG NA HITIMISHO LA MIAKA 10 YA MAVUNO MKOANI ARUSHA.

$
0
0
Askofu Mkuu wa Kanisa la TAG Dkt.Barnabas Mtokambali akizungumza na waandishi wa habari leo katika ukumbi uliopo hoteli ya Cordo Spring Jijini Arusha.
Mhubiri wa Kimataifa Johannes Amritzer
akizungumza na waandishi wa habari leo katika ukumbi uliopo hoteli ya Cordo Spring Jijini Arusha.
Mwenyekiti wa Maandalizi ya Sherehe hizo na Askofu wa TAG Mkoani Arusha O.Sosi akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari kuhusiana na ratiba ya shughuli nzima itakavyokuwa katika Sherehe hizo za miaka 80 ya kanisa la.TAG Tanzania.
Waimbaji wa Muziki wa Injili watakaohudumu katika Mkutano kutoka kushoto ni Julia Wilkander akiwa na Muimbaji Miriam Mauki kutoka nchini Tanzania
Askofu Mkuu wa Kanisa la TAG Dkt.Barnabas Mtokambali akiteta jambo na Mhubiri wa Kimataifa Johannes Amritzer.
Baadhi ya Timu itakayoshiriki katika sherehe hizo pamoja na mkutano mkuu wa Injili utakaoanza tar 17julai 2019 wakiwa tayari katika maandalizi.
Baadhi ya Timu itakayoshiriki katika sherehe hizo pamoja na mkutano mkuu wa Injili utakaoanza tar 17julai 2019 wakiwa tayari katika maandalizi.


Na.Vero Ignatus,Arusha.

Maadhimisho ya sherehe za kutimiza miaka 80 ya Kanisa la TAG pamoja na hitimisho la miaka 10 ya mavuno yaataandimishwa wiki hii Jijini Arusha .

Dkt.Barbanas Mtokambali ni Askofu Mkuu wa Kanisa la TAG nchini amesema katika mkutano wake na waandishi wa habari kuwa kanisa hilo likianza kazi nchini mwaka 1939, Igale mbeya ambapo hivi sasa yapo makanisa 9,986,vyuo vya Biblia,8 vyuo vya kupanda makanisa ,shule za sekondari,vyuo vya ualimu ambavyo vinakaribia kukamilika,vituo vya Radio,vyuo vya ualimu,vituo vya Afya na vituo vya huduma za jamii kwa watoto yatima.

Dkt.Mtokambali anasema mpango mkakati wa awamu ya kwanza ya mafanikio ya kanisa wameyapata katika miaka 10 ya mavuno kwani majimbo yameongezeka kutoka 10-69,makanisa 2,619-9,986,wachungaji 2,616-10,085,washirika kuongezeka 200,069-13,326,vyuo vya Biblia 4-8 ambapo Idara ya kujenga shule za sekondari na nyingine zitaanza kuandikisha wanafunzi mwezi Januari 2020.

Maadhimisho hayo yanaambatana uwekaji wa Jiwe la msingi wa Kanisa la kwanza la TAG kanda ya kaskazini Calvary Temple,Uzinduzi wa visima viwili maeneo ya Ngaramtoni,Makuyuni mmkoani hapa,Upimaji wa na Matibabu ya macho itakayofanyika kwa mMrmombo na Levolosi mkoani hapa 

Askofu huyo amesema hadi sasa kanisa hilo limeweza kutoa vitendea kazi mbalimbali kwa Maaskofu na waangalizi wa majimbo,pamoja na makatibu wa Kanisa hilo la TAG.“Kanisa letu hivi sasa linaonekana katika kila wilaya na kila kata ya Tanzanzania” Alisema Dkt.Mtokambali.

Ameeleza mwezi April 2019 wamekuwa na mfululizo wa sherehe za maadhimisho kuanzia kanisa la mahali pamoja,Jimbo,Idara na vyuo vya Biblia wakiwa na kauli mbiu isemayo “Ebenezer,hata sasa Bwana ametusaidia.”

Kwa upande wake Muhubiri huyo wa Kimataifa Johannes Amritzer amesema wao wanafanya ya uhubiri wa Injili inayogusa kila nyanja ya Jamii,kwani kuimba nyimbo.za kidini na kusoma maandiko hayabadilishi maisha ya mtu hadi mtu apate badiliko la ndani ya moyo.

Amesema yeye alilelewa maisha ya mtaani bila kuwa na uangalizi wa kutosha kutoka kwa wazazi kwani alikuwa mtukutu hadi pale Mungu alipoamua kuyabadilisha maisha yake na kuwa mtu mwingine na kuanza hatua mpya ya mabadiliko.

Amesema wiki hii ya kilele cha maadhimisho hayo kutakuwa na matukio mbalimbali kama Mkutano mkuu wa Halmashauri siku ya kesho,Baraza la waangalizi wote ,Mkutano wa wachungaji utafanyika chuo cha Ufundi Arusha pamoja na mkutano mkubwa wa Injili utakaoongozwa na Muhubiri wa Kimataifa Johanes Amritzer utakaofanyika uwanja wa Stadium wa Shekh Amri Abeid.

Aidha amesema julai 21 ndiyo itakuwa kilele cha maadhimisho ya sherehe hizo ambapo mgeni Rasmi anatazamiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli. 
Ambapo kwa pamoja wanasema “Miaka 10 ya mavuno -Kazi tuliyoianzisha.


Ikumbukwe kuwa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG) lilianzaishwa mnamo mwaka 1939 Igale Mkoani Mbeya ambapo mwaka 2019 linatimiza miaka 80.

Oxford yaongeza nguvu upandikizaji ULOTO Muhimbili

$
0
0
Mkuu wa Kitengo cha Mafunzo, Ushauri na Utafiti, Dkt. Faraja Chiwanga wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) akizungumza kabla ya kufungua mafunzo ya upandikizaji ULOTO ambayo yanafanyika MNH kwa mudawa wiki mbili.
Baadhi ya wataalam wakifuatilia mafunzo ya jinsi ya kuwahudumia wagonjwa watakaopandikizwa ULOTO. Huduma hii inatarajiwa kuanza nchini mwishoni mwa mwaka huu katika hospitali hii.
Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Ndani, Dkt. John Rwegasha akizungumza baada ya mafunzo kufunguliwa rasmi na Dkt. Chiwanga. 
Wataalam wakifuatilia wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo leo katika Hospitali ya Muhimbili.
Mtaalam wa Tiba ya Magonjwa ya Saratani kutoka Hospitali ya Chuo Kikuu cha OXFORD nchini Ungereza, Finn Tysoe akitoa mafunzo wa wataalam mbalimbali wa MNH leo.

Wataalam kutoka Hospitali ya Chuo Kikuu cha Oxford nchini Uingereza wameanza kutoa mafunzo kwa madaktari bingwa wadamu, madaktari wasaratani na wauguzi ambao watatoa Huduma kwa wagonjwa watakaopandikizwa ULOTO mwishoni mwa mwaka huu. 

Akizungumza kabla ya kufungua rasmi mafunzo ya wiki mbili, Mkuu wa Kitengo cha Mafunzo, Ushauri na Utafiti, Dkt. Faraja Chiwanga amesema kwamba mafunzo haya ni mwendelezo wa maandalizi ya kutoa Huduma ya upandikizaji ULOTO (bone marrow transplant) ambayo ilikuwa haipatikani hapa nchini kutokana na kutokuwapo kwa wataalam na ukosefu wa vifaa vya kutoa Huduma husika. 

‘’Mafunzo haya yanajumuisha wauguzi zaidi ya 30 pamoja na madaktari bingwa 20 wa magonwa ya damu na saratani wa Hospitali ya Taifa Muhimbili,’’ amesema Dkt. Chiwanga kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa MNH. 

Dkt. Chiwanga amefafanua kwamba mwezi Juni, mwaka huu hospitali ilipeleka wataalam 11 nchini India katika Hospitali ya Apollo iliyopo Chennai kwa kipindi cha mwezi mmoja ili kujifunza kwa vitendo jinsi ya kupandikiza ULOTO (bone marrow transplant). 

Takwimuza MNH zinaonyesha kwamba wagonjwa takribani 130 hadi 140 wanahitaji Huduma ya upandikizaji ULOTO kwa mwakana kwamba zaidi ya theluthi mbili ya wagonjwa wenye tatizo la saratani hufariki dunia kwa kukosa Huduma hii. Uwapo wa Huduma hii utasaidia wananchi wengi kutibiwa hapa nchini, kujenga uwezo kwa wataalam wa ndani na kupunguza gharama kwa Serikali kupeleka wagonjwa nje ya nchi.

Majaji wa shindano la East Africa Got Talent watangazwa leo ofisi ya Coca Cola jijini Nairobi.

$
0
0

  Jopo la majaji hao linamjumuisha Jeff Koinange, ambaye ni maarufu zaidi katika vyombo vya habari nchini Kenya ambaye pia amefanya kazi katika vyombo mbalimbali vya habari Duniani.

Mwingine ni Gaetano Kagwa, mwigizaji wa Uganda na mtangazaji ambaye amejizolea umaarufu mkubwa zaidi katika eneo hilo ambaye pia anatangaza katika kituo cha Capital FM, akiongoza kipindi cha Tusker Project Fame na alikuwa mshiriki wa Big Brother Africa.

Jaji mwingine ni Vanessa Mdee, mwimbaji wa Kitanzania na mtunzi wa nyimbo na Mtanzania wa kwanza MTV VJ, mwenyeji wa Epic Bongo Star Search na pia alishiriki kwenye shoo ya runinga ya Coke Studio Africa 2019 kati ya nyota wengine wa muziki wa Afrika.

Pia yumo Makeda Mahadeo aliyebobea katika vyombo vya habari nchini Rwanda na DJ wa kwanza wa kike nchini Rwanda.

Majaji watakuwa na jukumu muhimu katika kuidhinisha washiriki ambao wanatakiwa kuendelea kwa hatua inayofuata mwishoni mwa kila hatua na kutoa maoni au kukosoa juu ya waliyoshuhudia jukwaani. Washiriki wataondolewa ikiwa hawapati kura nyingi kutoka kwa majaji wanne.

Hii ni shoo ambayo itakuwa kinyumbani zaidi kufuatana na soko ambapo itatangazwa katika nchi nne za Afrika Mashariki ikiwemo Kenya, Tanzania, Uganda na Rwanda. Vyombo vya habari vishiriki vitakuwa ni Citizen TV, Clouds Tv, NBS na RTV.

Kampuni ya Coca-Cola pia itakuwa na jukumu la kutoa huduma mbalimbali zikiwemo ushauri wa ushiriki wa fursa katika kanda nne zilizoshiriki.

"Mfumo wa Coca-Cola unaamini kusaidia sekta ya ubunifu nchini na kutoa jukwaa ambapo watu wanaweza kuonyesha na kuendeleza vipaji vyao katika kanda. Tunaamini kwamba majaji waliochaguliwa wana uwezo wa kuchagua vipaji bora kwa wasikilizaji wetu wa Afrika Mashariki, ili waweze kufahamu na kufurahia shoo, "alisema Beatrice Nyamari, Meneja Mwandamizi wa Mawasiliano wa Coca-Cola Kanda ya Biashara Kusini na Mashariki mwa Afrika (SEABU).

Wanajiunga na Safaricom PLC ambao ni wadhamini wa shoo hiyo Kenya na moja wa wafadhili wa Afrika Mashariki kupitia huduma yao ya M-PESA; na Challenge Access, ambayo inaongoza Kampeni ya Moja kwa Moja, kwa msaada wa Programu ya Huduma za Afya Duniani na Mpango wa UHC wa Kenya, Afya Care.

"Afrika ya Mashariki ina vipaji vya kuonyesha ambavyo vinatoa fursa kwa Waafrika Mashariki kuonyeshea talanta zao na kampuni yetu inaamini katika kutoa majukwaa ya watu kustawi, tunafurahi sana kuwa sehemu ya shoo,"alisema Sitoyo Lopokoiyit, Afisa Mkuu wa Huduma za Fedha, Safaricom.

Jukwaa hilo litaonyesha vipaji mbalimbali kutoka kwa watu wote wa umri tofauti wa Afrika Mashariki, na litajumuisha vipaji vinavyotokana na kuimba, kucheza, maigizo na aina nyingine nyingi za vipaji.

"Sisi tunafarijika kuleta msisimuko huu wa kidunia nyumbani. Tunaamini kuwa jukwaa hili litaamua wafuatiliaji wa kimataifa kwa vipaji vya kipekee vya Afrika Mashariki, "alisema Joseph Kusaga, Mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Media International na mmiliki wa Franchise.

Majaji wanne watakuwa na vitufe vyao vyekundu ambavyo vinaweza tu kubonyezwa mara moja, pale jaji anapoona imetosha na inapotokea wakati mmoja, vikabonyezwa vyote basi kinachoendelea itapasa kisitishwe.

Kila mshiriki anahitaji kupokea idhini tatu kutoka kwa majaji kwenda kwenye duru ijayo.

Kutokana na kuanzia mwezi wa Agosti mwaka huu, kuonyesha EAGT itakuwa na vipindi 10, pamoja na nusu fainali na finali kubwa kuishi eneo moja nchini Kenya. Mshindi wa shooo atajinyakulia fedha za Kenya milioni tano (dola 50,000) kwa kupigiwa kura na watazamaji, ambayo itamuwezesha kuingia ubia wa kufanya kazi muda mrefu na mafunzo ya ujasiriamali.

Vipindi vitahaririwa katika vipengele sita ambavyo vitaanza kurushwa kuanzia Jumapili ya Agosti 4 saa mbili usiku (saa moja usiku Rwanda) katika sehemu zote nne za ukanda.
Meneja Mwandamizi wa Chapa ya Coca-Cola nchini Tanzania, Kabula Nshimo (kushoto) akitambulishwa na mshereheshaji rasmi wa mashindano makubwa ya kuibua vipaji kwa ukanda wa Afrika Mashariki (East Africa’s Got Talent) Anne Kansime wakati hafla ya kuwatambulisha majaji wa mashindano hayo iliyofanyika katika makao makuu ya Coca-Cola jijini Nairobi hivi karibuni.


Meneja Mwandamizi wa chapa ya Coca-Cola nchini Tanzania, Kabula Nshimo akizungumza kuhusu ushirikiano baina ya Coca-Cola na mashindano makubwa ya kuibua vipaji kwa ukanda wa Afrika Mashariki ya East Africa’s Got Talent kwa Tanzania wakati wa hafla ya kuwatambulisha majaji wa mashindano hayo iliyofanyika katika makao makuu ya Coca-Cola jijini Nairobi hivi karibuni.

Vijiji Vyote Nchini Kufikiwa na Umeme Ifikapo Juni 2021 No views

DIRA YA DUNIA JUMATATU 15/07/2019

SWAHILIFLIX YAJIPANGA KULETA CHACHU NA MABADILIKO KATIKA SOKO LA TASNIA YA FILAMU NCHINI

$
0
0
Na.Khadija Seif, Michuzi TV

KAMPUNI ya kuuza na kusambaza filamu mtandaoni (SWAHILIFLIX) imepania kuwapa kipaumbele wasanii kutengeneza kazi zenye ubora ili kijitangaza duniani.

Akizungumza na wanahabari jijini Dar es salaam (pichani chini) muwakilishi kutoka Kampuni ya Swahiliflix Nazir Atul amesema kutokana na kukua kwa teknolojia katika utandawazi katika kila sekta shughuli nyingi zinafanywa na mitandao ili kusaidia kufikia mahitaji ya watumiaji.

"Kwa sasa wapenzi,mashabiki ,wakereketwa wa tasnia ya filamu wataona  filamu wazipendazo kupitia Swahiliflix kwa haraka na kwa nafuu ,"

Pia Atul amesema rasmi Kampuni hiyo inatarajia kufanya uzinduzi julai 31 mwaka huu katika ukumbi wa Mlimani city jijini Dar es salaam. 

Kwa upande wake Msanii wa Bongomovie nchini Aunt Ezekiel  amesema wakati mwengine wasanii wamekua wakiboresha,kukuza sanaa kwa pamoja na kujitahidi kuwa tofauti lakini bado changamoto inabaki katika upatikanaji wa soko la kuuza kazi zao.

"Wadau wa filamu ni wakati wa kuburudika na filamu za kitanzania viganjwani mwao kupitia Swahiliflix, kwani imekua changamoto sana kwa shabiki kuhitaji kazi zako kupitia mtandao wa youtube na muda mwingine haipati kazi yako ikiwa kamili ,"

Aidha,Mkwere ameeleza hapo awali kulikua na tatizo la wasanii wakongwe kutoonekana kwenye kazi mpya kutokana na kukosekana kwa wadau  wanaosambaza na kuuza kazi za sanaa .

"Swahiliflix italeta Mapinduzi ya tasnia ya filamu kutokana na kazi zetu kuzitangaza zenyewe mtandaoni na wadau kutokana na kuwepo kwa Swahiliflix kuleta chachu na mabadiliko makubwa kwa wasanii kurudi kwa wingi,"

Viewing all 110181 articles
Browse latest View live




Latest Images