Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Iringa na kamanda wa vijana ccm Iringa Salim Abri Asas Abri akiwa katika moja ya matukio ya kuwahudumia wananchi kulia ni RTO SP Panfil Honono
========== ======== =========
SALIM ABRI ASASI AWAPA SOMO UVCCM IRINGA
Na Denis Mlowe, Iringa
KAMANDA wa umoja wa Vijana wa CCM Mkoa wa Iringa, Salim Asas ameunga mkono wito wa Mwenyekiti wa UVCCM mkoani humo, Tumaini Msowoya la kutaka vijana wa jumuiya hiyo wasikubali kugawanywa kwenye mambo ya siasa na watu wanaotaka kuwania nafasi mbalimbali za uongozi ikiwemo ubunge,udiwani ili kulinda heshima ya jumuiya hiyo na chama kwa ujumla.
Akifunga mkutano wa uchaguzi wa Chipukizi wa mkoa huo, Abri alisema heshima ya jumuiya hiyo ni vijana kufanya kazi kwa mujibu wa kanuni na taratibu na sio mapenzi ya mtu bali ni sera ya chama ndio wanayotakiwa kuifuata na kuepuka ushawishi kutoka kwa watu wenye nia ya kuwagawanya.
Alisema ni jukumu ya UVCCM mkoa wa Iringa ni kuhakikisha vijana hawafanyi kazi kwa maslahi ya watu wanaotaka uongozi mwaka 2015, jambo ambalo likiachwa liendelee linaweza kuimega na kuidhoofisha jumuiya yao inayojitegemea katika maamuzi kwa upande wa vijana.
Awali, akimkaribisha Kamanda huyo, Mwenyekiti wa UVCCM mkoani Iringa, Tumani Msowoya alitoa wito kwa CCM na wanachama wanachama wake kuhakikisha kuwa, wanaiacha jumuiya yao ifanye kazi kwa mujibu wa kanuni na taratibu zilizopo kwa manufaa ya chama hicho na sio mtu au watu wenye nia ya kujinufaisha kupitia umoja wao.
Aliwaagiza viongozi wa UVCCM kwa ngazi zote kutoa taarifa ya kuwepo kwa baadhi ya watu wenye nia ya kuwania nafasi za uongozi, ambao wanataka kuitumia jumuiya yao kama njia ya mafanikio yao kiuongozi.
“UVCCM ya sasa haitakubali kuyumbishwa wala kugawanywa na mtu yeyote mwenye nia ya kuomba madaraka, itafanya kazi kwa mujibu wa kanuni, taratibu na sheria zilizowekwa na katiba ya chama hicho kwa upande wa vijana” alisema Msowoya.
Msowoya aliwataka vijana kufanya kazi kwa juhudi zote kwa lengo lakujiongezea kipato ikiwepo kujiunga kwenye vikundi vidogo vidogo kuweza kupatiwa mikopo ya riba nafuu kuliko kuwa mmoja mmoja na kushindwa kupata mikopo katika taasisi zinazohusika katika kutoa mikopo.
“Vijana wenzangu tuepuke kuchagua kazi kwa maisha ya sasa ebu jiulieze kama tutachagua kazi, tutaendelea kugawanywa kwani watatupatia fedha ili tulinde maslahi yao, nawaomba sana tusikubali kuwatetemekea wenye fedha wanaotaka madaraka kwa njia ya kuhonga badala yake kila mmoja afanye kazi kwa bidii ili kuwa na uhakika wa kipato anachokipata kwa kazi halali kuliko fedha ya muda mfupi majuto baadaye,”alisema Msowoya
Akizungumzia uchaguzi wa chipukizi mkoani humo, Katibu wa UVCCM mkoani humo Alawi Haidar alisema umefanyika kwa amani na utulivu na kwamba, watoto hao wameweza kuwapata viongozi bora walioona wanawafaa.
Akitangaza matokeo hayo, Haidar alisema Mwenyekiti mpya wa chipukizi mkoani humo, Enock Luhala alifanikiwa kushindwa kwa kura 18 kati ya 33 zilizopigwa na kuwashinda wenzake, Ashraf Mpogole aliyepata kura 12 na Magreth Lusingo kura nne.
Katika nafasi ya mkutano mkuu wa chipukizi taifa, Junior Mlelwa alishinda kwa kura 26 na kuwabwaga wenzake, Halid Aziz na Christopher Dalu.
Wengine walioshinda ni Tausi Mgambo, Rukia Kimweli na Amina Kimweli kuwa wajumbe wa kamati ya uendeshaji mkoa.