Watanzania waishio Korea Kusini walipata bahati ya kutembelewa na Mh. Bernard Membe; Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa siku ya tarehe 8 Disemba 2013, katika Chuo Kikuu cha Dongguk jijini Seoul.
Katika mkutano huo, Waziri alifurahishwa sana na muamko, uelewa, na malengo kabambe ya Jumuiya ya Watanzania nchini Korea (TANROK) katika kujiendeleza na kuendeleza nchi yao.
Waziri alitoa taarifa ya hali ya uchumi, siasa, na kijamii nchini Tanzania na kuahidi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa wanadiaspora ili waweze kutumia vizuri elimu na ujuzi wanaopata ughaibuni katika kuendeleza nchi yao.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh. Bernard Membe akisaini kitabu cha Wageni alipotembelea Jumuiya ya Watanzania waishio nchini Korea Kusini jijini Seoul.
Mh. Bernard Membe (wapili toka kushoto) akijibu hoja mbalimbali za Watanzania waishio Korea Kusini. Katikati ni Mwenyekiti wa TANROK Bw. Rayton Kwembe, akifuatiwa na Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australia Balozi Mbelwa Kairuki, na wa mwisho kulia ni Katibu wa TANROK Bw. Innocent Lugendo. Wa kwanza kushoto ni afisa wa Ubalozi wa Tanzania nchini Japan anayeshughulikia Masuala ya Korea Kusini, Bw. Francis Mossongo.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh. Bernard Membe na Mkewe wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mkurugenzi wa idara ya Asia na Australia katika Wizara ya Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Mbelwa Kairuki wakipozi kwa picha ya pamoja na baadhi Watanzania Waishio nchini Korea Kusini.