Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110170 articles
Browse latest View live

DHARAU HAZITOSAIDIA KUTATUA MGOGORO WA GESI

$
0
0

Baada ya majibizano ya hapa na pale kuendelea kwa muda mrefu baina ya Serikali, Wanaharakati na Wananchi wa Mikoa ya Kusini sasa inaonekana mgogoro huo kukua zaidi siku hadi siku. Ililipotiwa hapo kabla kuhusu Naibu Waziri wa Nishati kwenda usiku huko Msimbati na kufukuzwa, ingawaje Serikali kwa upande wake ilikanusha habari hiyo na kudai ni maneno ya kizushi na udanganyifu wa watu kujitafutia umaarufu.

Katika kile kinachoonekana kuwa ni hatari, asubuhi ya leo tumepata taarifa kwamba gari lililoenda kwa ajili ya kumbeba Bibi kwenda naye kusikojulikana limechomwa moto. Taarifa zinasema, watu kadhaa akiwemo kijana mmoja mwenye asili ya ukaazi wa kijiji hicho walikamatwa jana usiku na wanakijiji cha Msimbati wakidai wameagizwa kuja kumchukua Bibi huyo ili wakafanye maongezi na Wakubwa ambao pia hawakuweza kuwekwa bayana ni Wakubwa gani hao. Kinachoelezwa ni kwamba, baada ya mtafaruku huo, watu hao walichoropoka na kukimbia kitu kilichowapa hasira Wananchi na kuamua kuchoma gali hilo ambalo walikuja nalo.

Ni hatari, kwasababu mbali na propaganda za viongozi wetu wa Kitaifa kwamba suala la gesi ni la Wanamtwara Mjini tu, eti kwamba wenyewe wa Msimbati na Mtwara Vijijini kwa ujumla wako tayari gesi hiyo kupelekwa Dar es salaam, kumbe si kweli. Leo hii, wale wanaodaiwa kuwa tayari kuruhusu gesi hiyo wameteketeza gari, je wale wasio tayari kwa hilo kesho watafanya nini? Wananchi hao wamesema wako tayari kumlinda Bibi huyo usiku na mchana kwa kuhofia kurubuniwa na Serikali ili abadili simamo wake.

Serikali isidharau wananchi na wale wenye matakwa mema na nchi hii, kwani mbali na mamlaka ambayo serikali imepewa katika kusimamia rasilimali za nchi bado uhalali wa wamiliki asilia wa rasilimali hizo ambao ni wananchi hauwezi kuporwa. Wananchi wanaozungukwa rasilimali husika ndio wamiliki halali wa rasilimali hizo kabla ya Serikali na jamii zingine za nchi. Hivyo wanufaika wa kwanza wa rasilimali husika ni lazima wawe ni wale wenye uhalali wa Ki-asili na si vinginevyo.

Tuache dharau, leo gari limechomwa na kama hii hali itaendelea kuwa hivi tusishangae kuambiwa kunamtu pia kachomwa au kapoteza maisha kwasababu hizihizi zinazofanyiwa masihara na viongozi wetu. Tuweni wazalendo jamani, tutetee maendeleo ya nchi na watu wake kwa vitendo, tuache porojo.

Hassani Samli, Mtwara.

Minister Membe to brief APRM meeting on governance status

$
0
0
By Hassan Abbas, Addis Ababa

The Tanzanian Minister of Foreign Affairs and International Cooperation, Bernard Membe is on Friday expected to brief governance experts from all over the African region on his country's implementation of the African Union governance assessment instrument-the African Peer Review Mechanism (APRM Tanzania).

Minister Membe whose portfolio includes facilitating the APRM process in Tanzania will have the opportunity to brief more than 100 APRM officials from 31 African countries participating in the Mechanism as a Pre-Summit meeting before President Jakaya Kikwete presents the country’s report to his peers on Saturday.

Speaking in Addis Ababa today (Thursday) the APRM Tanzania Executive Secretary, Ms Rehema Twalib said the APRM Pre-Summit meeting will act as preparatory stage for the countries of Zambia and Tanzania which are expected to be reviewed on Saturday.

“Minister Membe is expected to use the meeting to brief other APRM Ministers and senior officials on the preparedness of Tanzanian President, Jakaya Kikwete to face his peers,” she said.

According to the program of events released by the Continental APRM Secretariat in the meetings which take place in the margins of the AU Ordinary Summit here, Presidents of Tanzania, Jakaya Kikwete and his Zambian neighbour, Michael Sata will be reviewed on Saturday, 26th January, 2013.

APRM is mandated to periodically review progress on good governance through wide consultations of the people at the national level and then a country is finally reviewed by its peers-the rest of the African Heads of States and Governments for constructive discussions on how to move ahead.

The President Jakaya Kikwete confirmed his participation in the review meeting after a meeting with officials from the APRM Tanzania- a local secretariat of the Continental wide body at State House in Dar es Salaam on Thursday last week in Dar es Salaam.

Tanzania signed the Memorandum of Understanding (MoU) to join the APRM on the 26th May, 2004 and secured formal admission into the process on the 8th July 2004. On the 1st February, 2005 the Tanzanian Parliament ratified the APRM Memorandum of Understanding.

A team of APRM Tanzania led by the chairmen of National Governing Council, Prof. Hasa Mlawa, Member of APRM Tanzania Governing Council representing the National Assembly, MP John Magale Shibuda and other APRM Tanzania senior officials are already in Addis Ababa for the meetings.

DR FENELLA AKUTANA NA UJUMBE WA KILI MARATHON,PIA APOKEA UJUMBE KUTOKA KOREA

$
0
0
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fennela Mukangara akiwa katika mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Executive Solution,Agrey Mareale na Mkurugenzi wa Uhusiano na Jamii wa Kampuni ya TBL,Steven Kilindo walipomtembelea ofisini kwake kwa nia ya mazungumzo ya hapa na pale ambapo walimuomba awe mgeni Rasmi katika mashindano ya Kilimanjaro Marathon yanayotarajiwa kufanyika mjini Moshi tarehe 3/3/2013
Rais wa Kampuni ya Young Poong Ecoenergy kutoka Korea Bwana JaeJong Moon akiteta jambo na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fennela Mukangara walipokutana Ofisini kwa Mheshimiwa Waziri Jijini Dar es Salaam jana (Leo).

DK. SHEIN AHUDHULIA SIKU YA KILELE CHA WIKI YA UWEZESHAJI UKUMBI WA SALAMA BWAWANI ZANZIBAR

$
0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(katikati) akimkabidhi Fatma Abdalla Issa,wa Kikundi cha "Tanaweza Coop " Ole Kaskazini Pemba,Mfano wa Cheki ya Shilingi za Kitanzania Millioni Mia tatu na Laki Saba,kwa niaba ya Vikundi vya Ushirika na Wajasiriamali wa Mikoa Mitano ya Zanzibar,wakati wa sherehe za Kilele cha Wiki ya Uwezeshaji wananchi Kiuchumi katika Ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Zanzibar,(kushoto) Waziri wa Kazi,Uweshaji, Wananchi Kiuchumi na Ushirika Haroun Ali Suleiman.
Baadhi ya Viongozi wa Taasisi mbali mbali Serikali,na Wajasiriamali waliohudhuria katika sherehe za Kilele cha Wiki ya Uwezeshaji wananchi Kiuchumi katika Ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Zanzibar,wakiksikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, alipokuwa akizungumza nao leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(katikati) akizungumza na wananchi na Wajasiriamali ,wakati wa sherehe za Kilele cha Wiki ya Uwezeshaji wananchi Kiuchumi katika Ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Zanzibar,(kutoka kushoto )Makamo wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi, Waziri wa Kazi,Uweshaji, Wananchi Kiuchumi na Ushirika Haroun Ali Suleiman,na (kulia) Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Wakfu na Mali ya Amana,Abdalla Twalib.
Baadhi ya Viongozi wa Taasisi mbali mbali Serikali,na Wajasiriamali waliohudhuria katika sherehe za Kilele cha Wiki ya Uwezeshaji wananchi Kiuchumi katika Ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Zanzibar,wakiksikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, alipokuwa akizungumza nao leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(katikati) akimkabidhi Cheti cha Shukurani Bibi Nuru Hafidhi Mzee,Mstaafu katibu Muhtasi Wizara ya Kazi,Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi na Ushirika,wakati wa sherehe za Kilele cha Wiki ya Uwezeshaji wananchi Kiuchumi katika Ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Zanzibar,(kushoto) Waziri wa Kazi,Uweshaji, Wananchi Kiuchumi na Ushirika Haroun Ali Suleiman.[Picha na Ramadhan Othman,IKULU.]

Simba yashindwa kutamba kwa Black Leopard leo,yalala kwa bao 1-0

$
0
0
 Mshambuliaji wa Timu ya Simba,Masoud Kaheza akijaribu kutaka kuwatoka Mabeki wa timu ta Black Leopard ya nchini Afrika ya Kusini,wakati wa mchezo wa kirafiki uliochezwa jioni ya kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.Simba imepigwa bao 1-0.
 Winga wa kushoto wa timu ya Simba,Ramadhan Singani akiwania mpita na beki wa timu ya Black Leopard ya nchini Afrika ya Kusini,Thulan Ntshingila wakati wa mchezo wa kirafiki uliochezwa jioni ya kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.Simba imepigwa bao 1-0.
 Mshambuliaji wa Timu ya Black Leopard ya nchini Afrika ya Kusini,Bafana Sibeko akiingia langoni mwa timu ya Simba huku Beki wake akiangalia namna ya kumzuia.
Beki wa Simba akiondoa hatari iliyokuwa ikielekea langoni kwake.

The United States Ambassador Alfonso E. Lenhardt with course members of National Defense College

$
0
0
On 22 January 2013, The United States Ambassador Alfonso E. Lenhardt (center) pose for a group photo with course members of National Defense College. The National Defense College Commandant, Lt. Gen. Charles Makakala invited His Excellency Alfonso Lenhardt, the United States Ambassador to Tanzania, to present a lecture on United States national strategy for Africa and Tanzania, to the professional National Defense College students. Ambassador Lenhardt provided an overview of United States policy in Africa focusing the June 2012 Presidential Policy Directive - the United States guiding policy doctrine for sub-Sahara Africa that outlines four United States objectives for Africa which are (1) Strengthen democratic institutions; (2) Spur economic growth, trade and investment; (3) Advance peace and security; and (4) promote opportunity and development. Ambassador Lenhardt then focused on U.S. bilateral assistance to Tanzania, stating that "Presently, the United States is the largest donor to Tanzania, contributing over $740 million in bilateral assistance during 2012. We share a commitment to focus on addressing needs and priorities identified by Tanzanians, to improve life here in Tanzania. But that is only part of the story in our bilateral relationship. The strength of our partnership lies in mutual respect and the common goals we share. Together we are building trade relationships that will benefit Tanzania, East Africa and the United States. And, through our joint efforts in international institutions, such as peacekeeping operations, we together are helping to build a more prosperous and stable world."

Clouds Media Group yaukaribisha mwaka kwa hafla ya kukata na shoka usiku huu

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Clouds Media Group,Bwa.Joseph Kusaga akiwa sambamba na mke wake,ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa kampuni bingwa ya burudani hapa nchini,ya Prime Time Promotions Ltd,Johayna Kusaga,akizungumza mbele ya wafanyakazi mbalimbali wa kampuni hiyo waliokutana usiku huu kwenye hafla fupi (hawapo pichani) ya kuukaribisha mwaka na kuzungmza mambo mbalimbali ikiwemo na mafanikio yaliyopatikana mwaka jana,pia kuwashukuru kwa ushirikiano wao mkubwa ambao wamekuwa wakionesha kwenye kampuni hiyo kwa ammoja.
Boss Joe akiwaomba wafanyakazi wote wazinyanyue glassi zao za vinywaji juu na kuzigonganisha kwa pamoja kuonesha upendo,mshikamano na ushirikiano.Baada ya hapo Wafanyakazi walipewa ruksa ya kula kunywa na kujimwaya mwaya.
 Shampeni ikimiminwa baada ya kufunguliwa.
 Eprahim Kibonde akimminia kinywaji aina ya Shampeni meneja wa vipindi Sebastian Maganga baada ya kufunguliwa,ikiashiria kuwa hafla ya kunywa,kula imefunguliwa rasmi usiku huu huku baadhi ya wafanyakazi wa Clouds Media wakishuhudia tukio hilo.
 Mtangazaji wa kipindi cha power breakfast,Gerald Hando akizungumza jambo mbele ya Wafanyakazi wenzake usiku huu kabla ya kufungua shampeni,wa pili kulia ni Barbra Hassan,B Dozen,Ephrahim Kibonde,Millard Ayo pamoja na Dina Marious.
Dj Zero akiangusha ngoma live ndani ya kiota cha maraha cha Escape 2 usiku huu.Picha zaidi bofya JIACHIE BLOG.

Kamati ya Bunge ya Maliasili na Mazingira yakutana na Watendaji wa Ofisi ya Makamu wa Rais

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Dk Terezya Huvisa akitoa Maelezo ya Matumizi ya Bajeti ya Nusu Mwaka wa Fedha 2012/2013 Mbele ya Kamati ya Bunge ya Maliasili na Mazingira Kwenye Ofisi za Bunge Jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Charls Kitwanga akizungumza Jambo na Mbunge wa Jimbo la Pangani Saleh Mbamba Mara Baada ya Kikao cha Bajeti ya Nusu Mwaka kwa Ofisi ya Makamu wa Rais Kulia Mkurugenzi wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais Dk Julias Ningu.(Picha na Ali Meja)

MWAKIFWAMBA AZUNGUMZIA TAMASHA LA WASANII DAR LIVE JUMAMOSI HII

$
0
0
Rais Shirikisho la Filamu Tanzania (TFF), Simon Mwakifwamba akiongea mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani).
Msanii Vitalis Maembe akionyesha mfano atakavyokamua siku hiyo.
Dude akitoa kionjo cha nyimbo yake atakayoitambulisha kwa mara ya kwanza siku hiyo.
Baadhi ya wasanii hao wakisikiliza mawaidha kutoka kwa rais wao.
Waandishi wa habari wakichukua matukio ya ishu hiyo.

RAIS wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TFF), Simon Mwakifamba, leo amezungumzia juu ya maandalizi ya tamasha la wasanii wa filamu Bongo, walivyojiandaa kwa makamuzi ya nguvu Jumamosi hii ndani ya Ukumbi wa Dar Live uliopo Mbagala-Zakhem jijini Dar es Salaam.

Akizungumza mbele ya wanahabari, katika viwanja vya Leaders Club leo, Mwakifwamba alisema maandalizi ya tamasha hilo yamekamilika na kila kilichopangwa kitafanyika. Katika upande wa burudani, kutakuwa na wasanii mbalimbali waliojitolea kusapoti tamasha hilo ambao ni Vitalis Maembe, Mrisho Mpoto, Scorpion Girls, Dude, Mtunisi, Radon, Ray, JB, Wema, Jack Wolper, Uwoya, Dk Cheni, na wengine kibao.
(Habari/Picha: Musa Mateja/GPL)

APPLICATION FOR POSTGRADUATE SPONSORSHIP 2013/14

TASWA kufanya mdahalo na Wagombea wa nafasi za Juu TFF,Februari 15

$
0
0

CHAMA cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) kimepanga kufanyika mdahalo kwa wagombea wa nafasi za juu za uongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Februari 15 mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Uamuzi wa kuendesha mdahalo huo ulifikiwa kwenye kikao cha Kamati ya Utendaji ya TASWA kilichofanyika jana (Januari 23, 2012), ambapo pia kilijadili masuala mbalimbali yahusiyo chama hicho.

Tayari kikao kimeiagiza Sekreterieti ya TASWA ifanye maandalizi ya mdahalo huo kwa kuzungumza na vituo vya televisheni ili uweze kuoneshwa moja kwa moja kwenye vituo hivyo ili wananchi waweze kuwasikia wagombea hao.

Pia mazungumzo ya awali na wadhamini mbalimbali yameanza kuweza kufanikisha tukio hilo la kuendesha mdahalo wa 'live' kwenye televisheni. Nafasi ambazo wahusika watafanyiwa mdahalo ni Rais na Makamu wa Rais.

TASWA imekuwa ikifanya mdahalo kwa wagombea wa nafasi za juu kwenye uchaguzi wa TFF, ilifanya hivyo mwaka 2001 na mwaka 2004 ingawa haukuwa wa live, ikafanya wa live mwaka 2008, ambapo yote ilikuwa ya mafanikio makubwa, hivyo itafanya mawasiliano na TFF ili iweze kupata msaada wa karibu kufanikisha jambo hilo.

Tunaamini ushirikiano uliopo kati ya TFF  na TASWA utasaidia kwa namna fulani kufanikisha jambo hilo, ambapo mdahalo utahusisha waandishi wa habari waandamizi wa michezo, wahariri wa baadhi ya michezo na wadau wachache wa soka.

Kutokana na hali hiyo Kamati ya Utendaji ya TASWA imemteua mwandishi wa habari mkongwe ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Redio ABM, Abdallah Majura kuwa mwendeshaji wa mdahalo huo kutokana na uzoefu wake katika masuala ya habari na mambo ya michezo.TASWA inaamini Majura ambaye ni mwanachama wa TASWA akiwa pia amepata kuwa Katibu wa TASWA FC na Mhazini wa TASWA ni mtu makini, asiyeyumba na mwenye kutenda haki.

Pia Kamati ya Utendaji imesisitiza katika kikao chake kwamba uchaguzi wa TFF haimuungi mkono mgombea yeyote na haina mpango wa kumuunga mkono mgombea yeyote, hivyo TASWA inaonya kama kuna baadhi ya wagombea wenye ndoto za kutaka kutumia mgongo wa TASWA kwamba chama kinawaunga mkono ili wapate mteremko kufikia malengo yao hazitatimia.

Kama kuna kiongozi au mwanachama wa TASWA ambaye anamuunga mkono mgombea yeyote wa TFF, huo utakuwa msimamo wake binafsi si wa chama na kama atahusisha chama kwa namna yoyote atakuwa anakosea na hatutasita kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa katiba ya chama.

Tunawaomba waandishi wa habari za michezo nchini kuzidisha umakini kipindi hiki cha uchaguzi wa TFF na kujiepusha na makundi ya aina yoyote ambayo yatatia doa taaluma ya habari kwa namna yoyote ile.

Nawasilisha

Amir Mhando
Katibu Mkuu TASWA

MABALOZI JOB LUSINDE NA IBRAHIM KADUMA WATOA MAONI YA KATIBA MPYA

$
0
0
Waziri mstaafu na Mwanasiasa mkongwe nchini, Balozi Job Lusinde akitoka nje ya ukumbi wa mikutano wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba,alhamisi januari 24, 2013 ambapo alikutana na wajumbe wa Tume hiyo kutoa maoni na uzoefu wake kuhusu uandishi wa Katiba Mpya. Anayemwongoza ni Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Joseph Warioba na wa kushoto ni Makamu Mwenyekiti, Jaji Mkuu mstaafu Augustino Ramadhani.
Waziri mstaafu na Mwanasiasa mkongwe nchini, Balozi Ibrahim Kaduma akibadilishana mawazo na Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Dkt. Salim Ahmed Salim mara baada ya kumalizika kwa mkutano baina yake na Tume hiyo, alhamisi januari 24, 2013 ambapo alitoa maoni na uzoefu wake katika uandishi wa Katiba Mpya. Kushoto ni Mwenyekiti wa Tume, Jaji Joseph Warioba na kulia ni Mjumbe wa Tume, Profesa Mwesiga Baregu.
Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba akiagana na Waziri mstaafu na mwanasiasa mkongwe nchini, Balozi Job Lusinde mara baada ya kumalizika kwa mkutano baina yake na Tume hiyo, ambapo alitoa maoni na uzoefu wake katika uandishi wa Katiba Mpya.
Waziri mstaafu na Mwanasiasa mkongwe nchini, Balozi Ibarahim Kaduma akibadilishana mawazo na Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba mara mara baada ya kumalizika kwa mkutano baina yake na Tume hiyo, ambapo alitoa maoni na uzoefu wake katika uandishi wa Katiba Mpya. . Mwingine ni Mjumbe wa Tume hiyo, Dkt. Salim Ahmed Salim. (PICHA NA TUME YA KATIBA)

SOPHIA SIMBA AMFUNDA DIWANI WA CHADEMA KATA YA NYANDIRA

$
0
0
MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake Taifa ( UWT), Sophia Simba (aliesimama), ambaye pia ni Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto,ameshangazwa na kitendo cha Diwani wa Kata ya Nyandira kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo ( CHADEMA), Luanda Zengwe ,kushindwa kuwaondolea wananchi wake kero mbalimbali tangu achanguliwe ikiwemo kushirikiana na Halamshauri ya Wilaya a Mvomero kuwezesha kupatikana kwa kitanda maalumu cha kubeba wagonjwa. 

 Badala yake amekuwa mstari wa mbele kuwahamisha vijana na wanachama wa chama hicho  na pia kuzomea na kuwaletea fujo viongozi wa Serikali ya chama Tawala ( CCM) wanaotembelea kwenye Kata hiyo kwa madhumuni ya kukutana na wananchi ili kupata kero zao mbalimbali na kuzitolea majawabu ya msingi. 

Mwenyekiti wa Taifa wa UWT, alishangazwa na hatua hiyo ya kushindwa kutatua kero hizo na badala yake kuondoka eneo la meza kuu Chadema na kwenda kuwahamasisha wafuasi wake wafanye fujo wakati wa  mkutano ulioanmdaliwa na UWT kwa wananchi wa Kata ya Nyandira. 

 Diwani Luanda alipandwa na munkari, baada ya Diwani wa zamani wa CCM wa Kata hiyo , Modesta Lubasije kuwasilisha kero kwa Mwenyekiti wa Taifa wa UWT juu ya ukosefu wa kitanda cha kubeba wagonjwa ‘ Strecha ‘ hasa akina mama wajawazito kwenye Zahanati ya Kijiji cha Nyandira hali inayosababisha kutumia machela za miti. 

 Kutokana na hoja hiyo, Mwenyekiti wa UWT Taifa na Waziri alimgeukia Diwani waliyekuwa ameketi pembezoni mwa meza kuu na kumtaka wakati ukifika awezekujibu kero za wananchi na wapigakura wake , alitolee majibu huku akimsisitizia kuwa suala hilo si la Waziri bali lipochini ya uwezo wa Diwani kwa kushirikiana na Diwani wa Viti maalumu wa Tarafa ya Mgenta pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero. 

 Hata hivyo kufuatia kuelezwa suala hilo, Diwani huyo alinyanyuka ghafla kutoka meza kuu na kuanza kutoa maneno makali ya kejeri na kumshutumu Waziri Simba kwa kudai swali hilo lililenga kuchafua na hivyo kusababisha kuzuka kwa tafrani za dakika kadhaa na baadaye mkutano kuendelea kama kawaida.

 Kutokana na kitendo chake cha kutoa lugha chafu mbele ya Waziri Simba, alimua kunyanyuka na kuindoka meza kuu na kwenda kwa wafuasi wake ambao walijipanga kufanya fujo na kuanza kupiga mayowe na kurushiana vijembe hali iliyowafanya baadhi ya Viongozi wa CCM na UWT chini Katibu wa CCM Wilaya ya Mvomero,Sadakati Kimati kwenda kumdhibiti Diwani huyo wakisaidiwa na Askari Polisi wa eneo hilo.

 Waziri Simba akiendelea na mkutano huo, aliwataka wananchi kuona umuhimu wa kuchangua viongozi wenye busara na hekima , kwani kitendo cha utovu wa nidhamu uliooneshwa na Diwani wa Kata hiyo ni kuonesha ni namna gani siasa ya Vyama vya Upinzani zilivyo hapa nchini. 

 Akizumza kama Mwenyekiti wa Taifa wa UWT, Simba aliwahimiza wana CCM na wananchi wa Kata hiyo kutofanya makosa wakati wa uchaguzi mkuu ujao na badala yake warejeshe uongozi wa CCM katika Kata hiyo.

 “ Wananchi wa Nyandira hii ndiyo siasa za wenzetu hawa , baada ya kujionea mwenyewe, ninaahidi panapo majaliwa mwaka 2015 nitatia timu hapa kuendesha kampeni ya nguvu ili Kata hii isiendelee kuwa chini ya watu walevi , ambao hawataki maendeleo ya wananchi “ alisema Simba. 

 Hata hivyo alisema, maendeleo lazima yaletwe na wananchi kwa kushirikiana na viongozi , hivyo burasa inahitajika pale viongozi wanapofika kwenye eneo kama hilo na wananchi wanayo haki ya kutoa kero zao na kuzipatia majawabu ya msingi. 

 Kufuatia ombi hilo , Waziri Simba aliahidi kutoa fedha za kununua kitanda maalumu cha kubeba wagonjwa katika Zahanati hiyo ya Kijiji na kuwataka wananchi wenye kupenda amani wampuuze Diwani huyo pamoja na wafuasi wake ambao wao hekima na busara zimewashinda. 

 Kwa upande wake Diwani Luanda, alidai kuwa , ziara ya Waziri Simba haikuwa ya kiserikali na badala yake ililalia kwenye Chama chake zaidi na yeye kama Diwani wa Chadema wa Kata hiyo alikuwa na wajibu na haki ya kuona wanachama na Chama chake hakichafuliwi. 
Zengwe lilianzia hapa ambapo Diwani wa Kata ya Nyandira kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo ( CHADEMA), Luanda Zengwe (katikati) aliponyanyuka na kuanza kujibizana na Diwani wa zamani wa CCM wa Kata hiyo ,Modesta Lubasije aliyekuwa akiwasilisha kero mbali mbali kwa Mwenyekiti wa Taifa wa UWT,Mh. Sophia Simba (kushoto).
Katibu wa Chama cha Mapinduzi ( CCM) Wilaya ya Mvomero, Sadakati Kimati akimdhibiti vilivyo Diwani wa Kata ya Nyandira, kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo ( CHADEMA ), Luanda Zengwe, (mwenye skafu), mbele ya Askari Polisi, Sajini Taji aliyefahamika kwa jina la S .E Mndeme kutoka Kituo cha Polisi Mgeta , mara baada ya kutoa maneno ya lugha chafu kwa Waziri wa Maendeleo ya Jamii , Jinsia na Watoto, Sophia Simba ambaye pia ni Mwenyekiti wa UWT Taifa ( hayupo pichani) alipokuwa akiwahutubia wananchi wa Kata hiyo , Januari 19, mwaka huu, Diwani Luanda alikaribishwa akiwa ni mwakilishi wa wananchi kuketi meza kuu.
Diwani wa Kata ya Nyandira kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo ( CHADEMA), Luanda Zengwe akiingilia mkutano huo na kuanza kuongea na Wananchi wa Kata hiyo.

President Kikwete and Tony Blair attend meeting on Mobilising Private Sector investment in African Energy

$
0
0
President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete (right) speaks during a World Economic Forum session on “Mobilizing Private Sector Investment in African Energy,” held at World Food Programme Tent in Davos, Switzerland. On the left is USAID administrator Dr. Rajiv Shah and second left is former British Prime Minister Tony Blair.
President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete and former British Prime Minister Tony Blair leaves World Food Programme tent in Davos, Switzerland after participating in a meeting on “Mobilizing Private Sector Investment in African energy,” yesterday
Photos by Freddy Maro

MUALIKO WA MAULID NABII Toronto,Canada

$
0
0
Assalam Alaykum:

Nachukua fursa hii adhimu kuwataarifu ndugu katika Uislamu kwa niaba ya Madrasatul Al-Amin iliyokuweko katika Jiji la Toronto Canada katika anuani ifuatayo:
256 Eddystone Ave
North York, Ontario
M3N-1H7

Inawaalika nyote katika shughuli ya Maulid pamoja na kuja kusikiliza na kuona kile watakachokionyesha wanafunzi wao kile wanachokipata katika (Elimu) kutoka kwa Walimu wao.

Shughuli itaongozwa na Al-Ustadh Abdullah Abubakar (Mtawa) na itafanyika mnamo tarehe 16/02/1213 muda wa kuanza shughuli yetu ni 9:45 jioni na kumalizia saa 3:30 usiku katika anuani ifuatayo:

Lawrence height
5 Replied Rd
Toronto, Ontario
M6A

Nimatumaini yetu tutakuwa pamoja katika kufanikisha shughuli yetu hii kubwa zaidi kuja kuwasikiliza vijana wetu nini? wamepata na kufaidika katika yale aliyokuja nayo Bwana Mtume Muhammad (S.A.W)...

Na nachukuwa fursa hii kwa mara ya pili tena kuwaomba wale wote watakao changia kwa upande wa vinywaji au chakula basi tunawakaribisha na kwa kile mtu atakachojaaliwa kuja nacho.

Mwisho kabisa nitoe shukrani kwa niaba ya Madrasatul Al-Amin kwa wale wote watakao fanikisha shughuli hii kwa kila hali pia tusisite kutoa ushirikiano wetu kwa kupiga simu namba hizi zifuatazo ni (647 994-3028, 647 774-1133).

Nawataki kila la kheri na afya njema pamoja na kuja kujumuika pamoja katika siku hiyo ya shughuli yetu sote tunakaribishwa wa Toronto na Vitongoji vyake.

Imetolewa na Uongozi

Madrasatul Al-Amin
Toronto,Canada.

Article 2

$
0
0

SERENGETI FREIGHT FORWARDERS LTD
WAZEE WA KAZI
  TUMESHUSHA BEI ZA MAKONTENA!
40'HC TO DAR/MOMBASA NOW £1,950
20' CONTAINER TO DAR/MOMBASA £1,350
THIS IS MORE THAN £200 DISCOUNT!
HII BEI NI KWA MAERSK LINE, CMA-CGM, WEC LINE NA SAFMARINE

RATIBA YA MELI MPYA FEBRUARY 2013
 
FROM TILBURY 06/02/2013
FROM SHEERNESS 08/02/2013
BOOKINGS ZOTE SASA ZINAFANYIKA ONLINE
PLEASE VISIT OUR IMPROVED WEBSITE
TUNATOA HUDUMA ZA UKAGUZI WA MAGARIMOT/VOSA OFISINI KWETU
VEHICLE INSPECTION FOR KENYA AND UGANDA NOW CAN BE DONE IN OUR OFFICES
JUST DROP YOUR  CAR IN OUR OFFICE AND WE WILL INSPECT IT AND DELIVER IT TO THE PORT FOR YOU

kama unataka kuagiza kitu au kufanya booking yoyote ingia kwenye website yetu au tupigie kwenye namba zifuatazo

WAZIRI ABOUD AZUNGUMZA NA KAMPUNI INAYO SHUGHULIKIA UJENZI NA UCHUMI WA NJE YA CHINA

$
0
0
Waziri wa Nchi ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais Mohamed Aboud Muhamed akizungumza na ujumbe wa Kampuni inayo shuhulikia Ujenzi na Uchumi wa nje(ANHU)Group co,LTD ya China kulia yake ni Makamo wa Rais wa Kampuni hiyo Wang Hao,huko ofisini kwake Vuga mjini Zanzibar.
Katibu Mkuu Wizara ya Kazi Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi na Ushirika Bi. Asha Abdalla akiwa na Katibu wa Makamu wa Pili wa Rais Khalid Salum akiuliza suali kwa Makamu wa Rais wa Kampuni inayo shuhulikia Ujenzi na Uchumi wa nje(ANHU)Group co,LTD ya China Wang Hao hayupo pichani huko ofisini kwake Vuga mjini Zanzibar.
Makamu wa Rais wa Kampuni hiyo Wang Hao akionyesha baazi ya Viwanja mbali mbali vya mpira vilivyojengwa na Kampuni hiyo huko Vuga mjini Zanzibar.
Makamu wa Rais Wang Hao wa Kampuni inayo shuhulikia Ujenzi na Uchumi wa nje(ANHU)Group co,LTD ya China akimkabidhi zawadi Waziri wa Nchi ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mohamed Aboud Muhamed huko ofisini kwake Vuga mjini Zanzibar. Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar.

DKT. SHEIN AONGOZA WAUMINI WA KIISLAM KWENYE MAULID YA MTUME MUHAMMAD (S.A.W) VIWANJA VYA MAISARA,ZANZIBAR

$
0
0

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maulid EL Nabii Zanzibar Sheikh Khamis Haji Khamis,alipowasili katika viwanja vya Maisara katika sherehe za Maulid ya kuzaliwa Bwana Mtume Muhamad (S.A.W) yaliyofanyika jana.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Jaji Mkuu wa Zanzibar Omar Othman Makungu, alipowasili katika viwanja vya Maisara katika sherehe za Maulid ya kuzaliwa Bwana Mtume Muhamad (S.A.W) yaliyofanyika jana, na Rais Mstaafu wa Zanzibar Dk.Amani Abeid Karume,(katikati).
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,(wa tatu kulia) akitiwa Marashi wakati wa kumswalia Mtume (S.A.W) wakati wa sherehe ya Maulid ya Kuzaliwa kwake katika viwanja vya Maisara Mjini Zanzibar jana.
Baadhi ya Waumini wa Dini ya Kiislamu waliohudhuria katika sherehe za Maulid ya Kuzaliwa kwa Bwana Mtume Muhammad (S.A.W) yaliyofanyika jana katika viwanja vya Maisara Mjini Zanzibar.

news alert: vurugu zaendelea mtwara

$
0
0
Habari zilizotufikia punde zinasema vurugu zinaendelea mjini Mtwara ambapo leo wananchi wamechomamoto mahakama ya Mwanzo na kuvunja vioo vya Nyumba ya Mhe. Hawa Ghasia Waziri wa Tamisemi na ya Mhe. Mohamed Sinani Mwenyekiti wa CCM mkoa zilizopo mtaa wa Sinani.

Wakiwa katika mahakama ya mwanzo Polisi walizingirwa na vijana waliokuwa wamebeba mawe na kufunga barabara zote za kuingia na kutoka kituo kikuu cha mabasi na soko kuu, licha ya kufyatua hewani mabomu ya machozi.Baadhi ya barabara za mji huo zimezibwa kwa kuchomwa matairi ya gari, na kuongeza hofu kwa wananchi…Bado haijajulikana chanzo ama sababu ya vurugu hizo, nasi tunafuatilia kwa karibu n tutawapasha yanayojiri kwa kadri tutapopata taarifa
Baadhi ya watuhumwa wa vurugu hzo wakiwa chini ya ulinzi
Askari wa FFU wakiwa katika harakati za  kuzuia vurugu hizo

Used Desktop Computers, Printers, Badge Printers, Office Furniture for sale in Dar

$
0
0
1. HP Color LaserJet 2550L printer - $300

2. HP LaserJet 1022 printer (Black and White)
- $250

3. HP LaserJet 4250DTN printer (prints  in Black only)
-$400

4. Minolta CS Pro 4000/5000 (printsin Black only)
- $350

5. Canon - NP 1820 Copier/Printer (prints in Black only)
- $400

6. Fargo DTC525 Color Double-Sided ID Badge Card Printer (2 units)
-$1250 each

7. Lot of 10 used Dell GX745 desktop computers with peripherals
- $250 each

8. Office furniture: 15 used office chairs and 8 used PC desks
- $1050 for whole lot

9. ID Badge photo/passport photo

cameras, tripod, background screen)
- $450
Please contact 0715 455 346 or computersDAR@gmail.com
Viewing all 110170 articles
Browse latest View live




Latest Images