Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110171 articles
Browse latest View live

Article 9

$
0
0
COMMUNIQUÉ OF THE DOUBLE TROIKA SUMMIT OF HEADS OF STATE AND GOVERNMENT OF THE SOUTHERN AFRICAN DEVELOPMENT COMMUNITY (SADC) ADDIS ABABA, REPUBLIC OF ETHIOPIA 17TH  JANUARY 2019


1.The Double Troika Summit (Summit) of the Heads of State and Government of the Southern African Development Community (SADC) was held in Addis Ababa, in the Federal Democratic Republic of Ethiopia on 17th January 2019.

2.The Summit was officially opened by H.E President Dr. Hage G. Geingob, the Chairperson of SADC.

3.Summit was attended by the following Double Troika Heads of State and Government or their representatives:

Angola:H.E. President João Lourenço, Out-going Chairperson of the Organ on Politics, Defence and Security Cooperation

Namibia:H.E President Dr Hage G. Geingob, Chairperson of SADC


South Africa:H.E. President Cyril Ramaphosa, Out-going Chairperson of SADC

Zambia:H.E. President Edgar Chagwa Lungu, Chairperson of the Organ on Politics, Defence and Security Cooperation

Tanzania:H.E. Dr. Augustin P. Mahiga, Minister of Foreign Affairs and East African Co-operation, representing the In-coming Chairperson of SADC

Zimbabwe:H.E. Mr. Raphael Faranisi, Ambassador of the Republic of Zimbabwe to the Democratic Republic of Congo, representing the In-coming Chairperson of the Organ on Politics, Defence and Security Cooperation

4.Summit was also attended by the Executive Secretary of SADC, H.E. Dr. Stergomena Lawrence Tax, and was briefed by H.E Leonard She Okitundu, Deputy Prime Minister and Minister of Foreign Affairs and International Co-operation of the Democratic Republic of Congo (DRC).

5.Summit reviewed the political and security situation in the Democratic Republic of Congo (DRC) following the Presidential, Legislative and Provincial Elections that were conducted in the country on 30th December 2018.

6.Summit congratulated the Government of the Democratic Republic of Congo and Independent National Electoral Commission (CENI) for organising and conducting generally peaceful elections, notwithstanding some incidences and the logistical challenges, coupled with the impediments brought about by the devastating Ebola outbreak and security insurgencies.

7.Summit commended the Congolese people and all Political Stakeholders for ensuring that the elections were conducted in a peaceful manner.


8.Summit commended H.E. President Joseph Kabila for his leadership in holding the elections.

9.Summit noted that that due to the outbreak of the Ebola Virus in Beni and Butembo areas, combined with security challenges, Legislative and Provincial elections in Beni, Butembo and Yumbi were postponed to March 2019.


10.Summit encouraged the Government of the Democratic Republic of Congo to continue maintaining peace and security in the country.

11.Summit took note of the election petition filed in the Constitutional Court challenging the provisional results of the Presidential Election and called upon all the Congolese People and all the concerned Political Stakeholders to remain calm and act in a way that consolidates democracy and preserves peace, and to address any electoral

grievances in line with the Democratic Republic of Congo’s Constitution and relevant electoral laws.


12.Summit called upon the international community to respect the sovereignty and territorial integrity of the Democratic Republic of Congo in accordance with the AU Constitutive Act, and the SADC Treaty.

13.Summit recognized and underscored the role of the Constitutional Court of the DRC and called upon the international community to respect the Constitution of the Democratic Republic of Congo and the internal legal and political processes for the finalization of the electoral process.


14.Summit also called upon the international community to support the Government of the Democratic Republic of Congo to maintain a peaceful and stable environment following the landmark elections, and avoid actions that are prejudicial to the electoral process.

15.Summit further called for the continued implementation of the Peace, Security and Co- operation Framework in the Democratic Republic of Congo and the Region.

16.Summit reaffirmed its commitment to continued support to the Democratic Republic of Congo’s political processes, and with respect to neutralizing the negative forces and other armed groups operating in Eastern Democratic Republic of Congo, and to remain seized with the matter.

17.Summit expressed its appreciation for the support rendered to the SADC Electoral Observation Mission (SEOM) by the Government of the Democratic Republic of Congo and the United Nations Organization Stabilization Mission in the DRC (MONUSCO).

18.Summit commended H.E. President Hage G. Geingob, Chairperson of SADC for convening the Double Troika Summit.


Done at Addis Ababa, Federal Democratic Republic of Ethiopia, 17th January 2019


FEMINA HIP YATIMIZA MIAKA 20 TANGU KUANZISHWA KWAKE, YATOA ELIMU KWA WANAHABARI

$
0
0
Mkurugenzi wa Masuala ya Habari katika shirika lisilo la kiserikali linaloshughulika na masuala ya vijana la Femina Hip, Amabilis Batamula (kulia) akizungumza kuhusiana na miaka 20 ya shirika hilo wakati wa semina na wanahabari, jijini Dar es Salaam juzi. Picha na Joseph Zablon
Baadhi ya wanahabari wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zinawasilishwa kuhusiana na miaka 20 ya Shirika lisilo la kiserikali la Femina Hip, Dar es Salaam juzi. Picha na Joseph Zablon
Mkurugenzi wa Masuala ya Habari katika shirika lisilo la kiserikali ya Femina Hip, Amabilis Batamula akifafanua jambo mbele ya wanahabari baada ya semina na waandishi wa habari kuhusiana na miaka 20 ya shirika hilo, Dar es Salaam juzi. Picha na Joseph Zablon

AFISA ELIMU ASIMAMISHWA KAZI ARUSHA

$
0
0
Na. Vero Ignatus, Arusha. 

Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amemsimamisha kazi Ofisa elimu wa mkoa huo Gift Kyando kwa madai ya kuzuia wanafunzi waliochaguliwa kuingia kidato cha kwanza huku akilazimisha kila darasa kuwa na wanafunzi 40 tu.

Pia anadaiwa kusababisaha wanafunzi hao kukosa nafasi za masomo kwa kukataa kusajiliwa kwa shule mbili mpya za Oldonyowasi na Losikito kwa madai ya kukoda mahabara.

Gambo amesema kitendo hicho ni cha kukwamisha juhudi za serikali kupitia ilani ya chama cha mapinduzi kwa kuwa uamuzi aliouchukua Ofisa huyo haukumuhusisha kiongozi yeyote yule wa serikali ngazi ya wilaya au mkoa

Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Arusha Dk. Wilson Mahera amesema kitendo hicho alichokifanya ofisa huyo kiliwachanganya na kusababisha ugomvi kati yao na wazazi wa wanafunzi hao

Amesema ofisa huyo angesababisha wanafunzi 6,819 kukosa elimu wakati yapo madarasa ambayo yaliachwa na wanafunzi waliohitimu kidato cha nne ambayo yangeweza kutumiwa na wanafunzi hao

'' Madarasa yaliyopo yangeweza kuchukua wanafunzi kwa kipindi kifupi wapatao 55 kwa darasa moja '' alisema Mahera.Dkt. Mahera amesema kuhusu mapokezi wanafunzi kati ya shule 4239 wameshapokelewa katika shule 28 za halmashauri ya Arusha wakiwemo wavulana 1,853 na wasichana 2,386 ambao ni sawa na asilimia 62 huku waliobakia wakiendelea kuripoti na wengine wakichukua fomu za kujiunga.

Kwa upande wake Mwenyakiti wa CCM mkoa Loata Sanare amesema alichokiona ni hujuma za waziwazi kwa ofisa huyo dhidi ya serikali na kutaka kuzuia wanafunzi wasianze masomo.Sanare anasema alianza kupokea simu za malalamiko kutoka kwa wazazi wawanafunzi hao na alipompigia ofisa elimu huyo alimjibu majibu ambayo hayakumridhisha ndipo alipoamua kuwasikiana na mkuu wa mkoa. 

SABABU ZINAZOFANYA WASANII WA KIKE WA TANZANIA BARA KUTOTOBOA KIMUZIKI

$
0
0
Na Khadija Seif, Globu ya jamii

Malkia wa Bongofleva kwa upande wa Tanzania Visiwani (Zanzibar) Jamila a.k.a Baby J amewataka wasanii wa miondoko hiyo kwa upande wa Tanzania Bara hasa wanawake kupeana ushirikiano katika kazi ili kuendelea kuzalisha vipaji kwa wingi hasa kwenye muziki na kuendelea kukuza tasnia hiyo nchini kote

Baby J amesema jina lake linaendelea kutambulika na kung'ara vizuri kimuziki kutokana na jitihada, kuamini kile wanachokifanya pamoja na kujichanganya na kushirikiana na wasanii wengi mbalimbali ili kuendelea kujifunza mambo mengi yahusuyo muziki.

Hata hivyo Baby J ameeleza jinsi mitandao ya kijamii ilivyo na nguvu kwa sasa katika kuendesha shughuli za kimuziki na kuutangaza, inasaidia kuwapa fursa mashabiki kufahamu upo wapi, una kazi ipi na unajiandaa na lipi kitendo hiko kimekua kigumu kwake kutokana na kutopenda maisha ya mitandaoni.

 "Nitarudi tena kufanya kazi za kimuziki kwani nina kipaji, muziki ni kilevi changu ila kwa sasa naendelea na majukumu ya familia hasa kumlea mtoto wangu mpya. "Amesema Baby J

Pia ameeleza kuwa kwa wanamuziki wa Zanzibar wengi hawajiamini katika kile wanachokifanya kutokana na kukatishwa tamaa kwani hata yeye aliyekuwa akisimamia kazi zake alishamkatisha tamaa lakini aliweza  kujiamini kwa kuendelea kufanya vizuri kwa upande wa Bara.

Na amemtaja Mwanamuziki Diamond Platnumz kuwa ni mtu ambae anamshauri na kushirikiana nae vizuri katika kazi za muziki kwani anaamini mchango wake ni mkubwa katika tasnia ya muziki wa Bongofleva.

INTRODUCING Mbosso - Tamu (Official Music Video)

MLELA AWAPONGEZA WAANDAJI WA TAMASHA LA FILAMU "SZIFF"

$
0
0
Na Khadija Seif, Globu ya jamii

MSANII wa filamu nchini, Yusuph Mlela amewapongeza waandaji wa tamasha la filamu za kitaifa    (SZIFF) kwa kuwapa fursa wasanii kujifunza kupitia masoko ya nje. Mlela ameeleza fursa waliyoipata katika mchakato wa tuzo ikiwa wazi kwamba bado wanafanya jitihada katika kuboresha na kukuza tasnia ya filamu nchini hasa kuonyesha filamu za nje na kukutanisha watu wanaofanya vizuri kutoka nchi za nje kutoa elimu kwa wasanii wa nchi zingine.

"Kuna utofauti mkubwa sana ukiangalia filamu za mataifa mengine na za kwetu hasa kwenye mtiririko wa matukio, ubora, uvaaji wa uhusiano, sisi bado tuko nyuma sana". Alisema mlela

Hata hivyo amefafanua kupitia tamasha hilo tasnia itaimarika na kupanuka na kupata masoko ya nje na kujitangaza kwani sanaa ni ya watu wote, ni wakati wa wasanii kushirikiana kwa pamoja.

Aidha Mlela amesema kwa mwaka jana filamu ya kesho iliingia sokoni na kufanya vizuri  aliyomshirikisha msanii Gabo Zigamba na kwa mwaka huu kajipanga na vitu vizuri ambavo viko jikoni na kuwasihi mashabiki wakae mkao wa kushudia vitu vizuri.

Pia ametoa rai kwa waandaji wa Tuzo hizo kufanya kitu cha kipekee na tofauti katika kuboresha na kunogesha msimu huu wa pili japo ni changa kwa sasa, anaamini katika jambo lolote zuri lazima mawazo na maoni ni muhimu kuwasilishwa sehemu husika kufanyiwa ufumbuzi.

TAIFA BADO LINAHITAJI WATUMISHI WENYE UJUZI UNAOKWENDA SAMBAMBA NA MABADILIKO YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA - BALOZI SEIF ALI IDDI

$
0
0
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema Taifa bado linahitaji kuwa na Watumishi wenye ujuzi ili kwenda sambamba na mabadiliko mbali mbali ya sayansi na Teknolojia itakayoweza kuzikabili changamoto tofauti zilizopo Ulimwenguni hivi sasa.

Alisema Watumishi hao wakiandaliwa vyema katika maadili bora ya Utumishi wa Umma uliojaa Ubunifu, weledi na uchungu wa Rasilmali za Taifa ndio watakaokuwa tayari kuibadilisha Zanzibar kufikia Maendeleo yanayokusudiwa na Jamii.

Balozi Seif Ali Iddi alisema hayo wakati akizungumza na Wahitimu wa Chuo cha Utawala wa Umma Zanzibar wa ngazi na Fani mbali mbali za Elimu pamoja na Walimu na Wananchi kwenye Mahafali ya Kumi na Moja ya chuo hicho yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Dr. Ali Mohamed Shein SUZA Tunguu Mkoa wa Kusini Unguja.

Alisema kwa vile Mtumishi wa Umma ndio Rasilmali ya msingi na nguvu kazi ya Maendeleo ya Taifa lolole, Chuo cha Utawala wa Umma kina dhima ya kumuandaa na kumuendeleza Mtumishi wa Umma ili amudu kutekeleza majukumu aliyopangiwa kwa ueledi, uaminifu, upendo na Uzalendo.

Balozi Seif alisema Chuo hakina budi kujikita katika kufanya tafiti mbali mbali zitakazosaidia kuandaa Programu za mafunzo ya muda mrefu na mfupi zitakazokwenda sambamba na mahitaji ya Wanajamii ili kuisaidia Serikali kuwa na Watumishi Bora wanaotoa huduma kwa vigezo na viwango kulingana na matarajio makubwa ya Wananchi.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alitoa wito kwa Uongozi wa Chuo hicho kuendelea kuongeza Uwezo wa kubadili Wanafunzi wengi zaidi lakini kwa kuzingatia vigezo na masharti yanayowekwa na Tume ya Vyuo Vikuu Nchini pamoja na mahitaji ya sasa na baadae ili kufikia malengo ya Nchi iliyojiwekeza.

“ Tukumbuke kuwa Taifa linahitaji wasomi walioandaliwa vyema na kushiba Maadili bora ya Utumishi wa Umma, Weledi wenye Uchungu wa Rasilmali za Nchi”. Alieleza Balozi Seif.

Alielezea faraja yake kuona jinsi Chuo kinavyoendelea kutanua wigo wake wa kutoa Mafunzo mafupi ya kujenga uwezo kwa Watumishi wa Umma ikiwemo kuijengea uwezo Idara husika kwa kuandaa Programu Maalum ya Mafunzo iliyotokana na ziara ya kujifunza uendeshaji katika vyuo mbali mbali vya Zanzibar na Tanzania Bara.

Balozi Seif alisema kitendo cha kutoa mafunzo kwa Watumishi Wastaafu watarajiwa pamoja na watumishi wapya ni ishara tosha ya namna Chuo kinavyopiga hatua ya kutekeleza majukumu yake ya msingi ya maandalizi ya Watumishi Wastaafu.

Alisema wakati umefika sasa wa kukithamini na kukiheshimu Chuo cha Utawala wa Umma na kukitumia ipasavyo kama alivyosema Muasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar ywa Mwaka 1964 Marehemu Mzee Abeid Amani Karume ya kutukuza chake Mtu mpaka asahau cha mwenzake.

Alieleza kwamba Taasisi za Umma na hata zile binafsi wajenge Utamaduni wa kukitumia Chuo cha Utawala wa Umma katika kuwaendeleza Watendaji wao chenye Walimu waliobobea wenye uwezo wa kuwabadilisha wanafunzi wao Kimaadili, Kitaaluma, Kifrikra, Kimawazo na Utendaji .

Kwa upande wa Wahitimu hao, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliwakumbusha kuitumia Taaluma wanapokwenda eneo lolote ili kubadilisha utendaji kazi wa mazoea kwenda kwenye Utumishi wenye kuzingatia uweledi, tija na utoaji huduma wa wakati kwa Wananchi.

Alisema Taifa linafurahia siku muhimu na adhimu ya ongezeko la Wataalamu wa fani mbali mbali wanaoingia kwenye tanuri la uwajibikaji utakaotegemewa katika kuleta mabadiloko ya Maendeleo endelevu Nchini.
Mapema Mkurugenzi wa Chuo cha Utawala wa Umma Dr. Mwinyi Talib Haji Alisema Chuo hicho ni Taasisi inayojitegemea na kupewa dhamana ya kutoa Mafunzo yanayohusiana na masuala ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Nchini.

Dr. Mwinyi alisema Watumishi wa Umma ni Rasilmali muhimu inayopaswa kuenziwa kwa kupatia nyenzo ya kuwajibika Kitaaluma ambayo ni Elimu inayohusiana na Fani yao.Alisema Chuo kimepata maendeleo makubwa tokea kuasisiwa kwake kwa kuzalisha Wahitimu wenye hadhi ya kukubalika katika ajira za Taasisi tofauti ambapo kwa sasa tayari kinawanafunzi 1,510 wanaoendelea kupata mafunzo katika fani tofauti.

Dr. Mwinyi alifahamisha kwamba Mwaka huu Chuo hicho kimezalisha Wahitimu wapatao 746 wa Ngazi ya Stashahada na Cheti katika fani mbali mbali sambamba na Wafanyakazi 2,675 wa Taasisi za Umma waliopatiwa Mafunzo.Mkurugenzi huyo wa Chuo cha Utawala wa Umma Zanzibar alieleza kwamba Uongozi huo tayari umeshafungua Tawi lake Kisiwani Pemba linaloendelea kuwafinyanga Wanafunzi 235 hivi sasa.

Licha ya Mafanikio hayo Dr. Mwinyi alieleza kwamba zipo changamoto zinazokikabili chuo hicho akizitaja baadhi kuwa ni pamoja na uhaba wa Ofisi za Watendaji na Uzio unaotia hofu ya kuvamiwa na wahalifu hasa nyakati za Usiku.Akimkaribisha Mgeni rasmi kuzungumza na Wahitimu hao Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora Zanzibar Mh. Haroun Ali Suleiman alitoa wito kwa Viongozi na Wafanyakazi wa Taasisi za Umma kujipangia utaratibu wa kupata mafunzo ya Kazi chuoni hapo.

Waziri Haroun alisema Chuo kimebarikiwa kuwa na Walimu wenye uwezo mkubwa wa kutoa mafunzo yenye muelekeo wa kumuwezesha Manafunzi kufikia ngazi ya Stashahada kwa hivi sasa.

Kabla ya Mwaka 2007 Chuo cha Utawala wa Umma Zanzibar kilikuwa kikitoa Mafunzo kwa Watumishi wa Kada ya Chini, lakini kwa sasa kinadahili Wanafunzi wa ngazi ya Shahada ya Kwanza katika Kada tofauti zikiwemo Utunzaji wa Kumbukumbu na Nyaraka, Uhusiano wa Kimataifa na Diplomasia na Usimamizi wa Rasilmali Watu.

Wengine ni Teknolojia ya Mawasiliano ya Habari, Uongozi wa Biashara, ununuzi na Ugavi, Mipango ya Maendeleo, Utawala wa Serikali za Mitaa, Uhazili, Uongozi wa Elimu na Utawala pamoja na Menejimenti ya Utumishi wa Umma.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akipokea Gwaride la Wahitimu wa Chuo cha Utawala wa Umma Zanzibar katika mahafalio yaliyofanyika katika Ukumbi wa Dr. Ali Mohaed Shein uliopo ndani ya Viunga vya Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar {SUZA}kiliopo Tunguu Mkoa Kusini Unaguja.Kulia ya Balozi Seif ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba, Sheria na Utawala Bora Mh. Haroun Ali Suleiman Waziri wa Elimu Mh. Riziki Pembe Juma, Kushoto ya Balozi ni Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo Bibi Fatma Said Ali,Waziri wa Vijana Balozi Ali Karume na Mkuu wa Mkoa Kusini Unguja Mh. Hassan Khatib.
Baadhi ya Wahitimu wa Chuo cha Utawala wa Umma Tunguu wakiingia ndani ya ukumbi wa Dr. Ali Mohamed Shein SUZA kukamilisha mahafali yao ya 11.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akihutubia kwenye Mahafali ya 11 ya Chuo cha Utawala wa Umma Tunguu Mkoa Kusini Unguja.
Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Utawala wa Umma Zanzibar Bibi Fatma Said Ali akitoa salamu wakati wa kuanza kwa Mahafali ya 11 ya Chuo hicho hapo Tunguu.
Baadhi ya Wahitimu wa Chuo cha Utawala wa Umma Zanzibar wakifuatilia matukio mbali mbali yaliyokuwa yakifanyika kwenye Mahafali yao ya 11 kwenye Ukumbi wa SUZA.
Muhitimu Abass Bakari Yakoub akipokea zawadi ya Mwanafunzi Bora wa {DRM} kutoka kwa Mgeni Rasmi Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi.
Muhitimu Maryam Said Omar akipokea zawadi ya Mwanafunzi Bora wa {DSS} kutoka kwa Mgeni Rasmi WA Mahafali yao Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi.Picha na – OMPR – ZNZ.

GAVANA SHILATU AAGIZA MADARASA KUFUNGULIWA MARA MOJA

$
0
0


Na Mwandishi wetu Mihambwe

Afisa Tarafa Mihambwe Gavana Emmanuel Shilatu ameagiza Madarasa mawili mapya yaliyojengwa Shule ya Sekondari ya Mkoreha kumaliziwa vyema na kufunguliwa Mara moja ili Wanafunzi waanze kusomea Mara moja.

Agizo hilo amelitoa Leo Ijumaa Januari 18, 2019 alipotembelea na kukagua ulipofikia ujenzi wa Madarasa hayo akiwa amembatana na Mtendaji Kata Mkoreha pamoja na Mwalimu Mkuu Sekondari ya Mkoreha ambao pia ni Wajumbe kamati ya ujenzi Madarasa hayo.

*"Madarasa yanapendeza kiukweli. Naagiza yakamilishwe vyema kabisa na Mara moja yaanze kutumika kuanzia wiki ijayo. Nisisikie hadithi nyingine, nataka kuona Wanafunzi wanaanza kusomea Mara moja."* Aliagiza Gavana Shilatu.

Wakati huo huo Gavana Shilatu ameongea na kuwapongeza Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Mkoreha ambao wamekwisha ripoti na kuanza kusoma na kuwasihi kuzingatia zaidi elimu na kupeleka salaam kwa waliochelewa kuripoti kufika shuleni haraka.

*"Nawapongeza nyote kwa kuripoti shuleni, msome kwa bidii. Pia fikisheni salaam kwa wenzenu ambao bado wapo nyumbani waje shuleni haraka iwezekanavyo."* alisema Gavana Shilatu wakati akiongea na Wanafunzi hao.
 


WIMBO MPYA MTAANI: Mwenyekiti - Ni kweli..

MAARIFA YA TEHAMA YAENDELEA KUONGEZEKA KUELEKEA UCHUMI WA VIWANDA –DKT YONAZI

$
0
0
WAKATI jamii mbalimbali duniani wakiendelea kutumia mfumo wa teknolojia habari na Mawasiliano (TEHAMA) imeelezwa kuwa maarifa zaidi yataendelea kuongezeka katika kuelekea uchumi wa viwanda. .

Moja ya mafanikio ya  Tehama ni kubuniwa kwa mfumo wakufuatilia madereva wanaoendesha mwendo wa haraka ambapo mfumo huo umesaidia kupunguza ajali ikilinganishwa na kipindi cha nyuma.

Hayo aliyasema Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Mawasialiano) Dk.Jim Yonazi amesema Tehama imesaidia kutatua matatizo mengi ya kijamii na kiuchumi.

Dk. Yonazi aliyasema hayo juzi wakati wa semina ya siku mbili juu ya umuhimu wa Tehama katika kujiletea maendeleo iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam.“Tehama ina mchango mkubwa sana katika maendeleo ya mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla hivyo hatunabudi kuhimiza wananchi kutumia Tehama ili kujiletea maendeleo na kutatua changamoto mbalimbali,”alisema

Dk. Yonazi alisema Tehama ikitumiwa vizuri inaweza okoa maisha ya mama mja mzito kwakufuatilia programu mbalimbali za lishe na malezi bora kupitia simu ya kiganjani.Kwa upande wake Mkuu wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) Profesa Tadeo Satta alisema  tehama ikitumiwa vzuri huongeza ubunifu na maarifa hivyo aliwataka wananchi kutumia Tehama kujiletea maendeleo.

“Tehama hadi sasa inaendelea kusaidia kuongeza ubunifu na maarifa ambapo wengi wamenufaika ili kufanikisha hilo IFM tumeandaa washa ya siku mbili kwa watumishi na wanafunzi wa IFM kama sehemu yakujuzana umuhimu wa Tehama,”alisema.Profesa Satta alisema semina hiyo itawajengea uwezo watumishi wa IFM ikizingatiwa kuwa muongoza mada katika washa hiyo ni mbobevu katika masuala ya Tehama ambaye ni Profesa Henk Sol wa Chuo Kikuu cha Groningen cha nchini Uholanzi.

“Tumekuwa tukibadirishana uzoefu na vyuo vya kimataifa ili kuweza kuleta maendeleo katika Taifa letu kwakuwa ukiwajengea uwezo wanataaluma umeelimisha Taifa zima hususani katika mmatumizi bora ya teknolojia katika kuboresha huduma na ufanisi,”Naye Muongozaji wa mada mbalimbali zihusuzo Tehama katika washa hiyo Profesa  Henk Sol alisema nchi za magaharibi ikiwemo Uholanzi zimepiga hatua kubwa sana kutokana na matumizi ya Tehama.

"Ugunduzi wa Tehama ulianzia katika nchi za mabara ya Ulaya na Marekani lakini lakini umekuwepo ukweli kwa watu wake ambao wamechangamkia fursa na wameweza kujiletea maendeleo kikubwa nikuwa wabunifu nakuitumia Tehama kama injini yakujiletea maendeleo." 

 Maprofesa na Madaktari wakifatilia mjadala wa Profesa Henk Sol wa Chuo Kikuu  cha Groningen nchini Uholazi warsha hiyo iliandaliwa na Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) .
Mkuu wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) Profesa Tadeo Satta akizungumza kuhusiana na Ujio wa Profesa Henk Sol wakati uwasilishaji wa maandiko mbalimbali.

SABABU ZINAZOFANYA WASANII WA KIKE WA TANZANIA BARA KUTOTOBOA KIMUZIKI

$
0
0
Na.Khadija seif,Globu ya jamii.

Malkia wa Bongofleva kwa upande wa Tanzania Bara Jamila a.k.a Baby J awataka wasanii wa Bara hasa wanawake kupeana ushirikiano katika kazi ili kuiendelea kuzalisha vipaji kwa wingi hasa kwenye muziki wa bongofleva na kuendelea kukuza tasnia ya muziki .

baby j amesema jina lake linaendelea kutambulika na kung'ara vizuri kimuziki kutokana jitihada ,kuamini kile wanachokifanya pamoja na kujichanganya na kushirikiana na wasanii wengi mbalimbali ili kuendelea kujifunza mambo mengi yahusuyo muziki.

Hata hivyo baby j ameeleza jinsi mitandao ya kijamii ilivo na nguvu kwa Sasa katika kuendesha shughuli za kimuziki na kuutangaza inasaidia kuwapa fursa mashabiki kufahamu upo wapi ,una kazi ipi na unajiandaa na lipi kitendo hiko kimekua kigumu kwake kutokana na kutopenda maisha ya mitandaoni.

" Nitarudi tena kufanya kazi za kimuziki kwani nina kipaji ,muziki ni kilevi changu ila kwa Sasa naendelea na majukumu ya familia hasa kumlea mtoto wangu mpya. "Amesema Baby J

Pia ameeleza kuwa kwa wanamuziki wa Zanzibar wengi hawajiamini katika kile wanachokifanya kutokana na kukatishwa tamaa kwani hata yeye aliyekuwa akisimamia kazi zake alishamkatisha tamaa lakini aliweza kujiamini kwa kuendelea kufanya vizuri kwa upande wa Bara.

Na amemtaja Mwanamuziki Diamond platnum kuwa ni mtu ambae anamshauri na kushirikiana nae vizuri katika kazi za muziki kwani anaamini mchango wake ni mkubwa katika tasnia ya muziki wa Bongofleva.

MLELA AWAPONGEZA WAANDAJI WA MATAMASHA YA FILAMU

$
0
0
Na.Khadija seif,Globu ya jamii

MSANII wa filamu nchini Yusuph Mlela amewapongeza waandaji wa tamasha la filamu za kitaifa (SZIFF)kwa kuwapa fursa wasanii kujifunza kupitia masoko ya nje.

Mlela ameeleza hayo leo,kuwa fursa waliyoipata katika mchakato wa tuzo ikiwa wazi kwamba bado wanafanya jitihada katika kuboresha na kukuza tasnia ya filamu nchi hasa kuonyesha filamu za nje na kukutanisha watu wanaofanya vizuri kutoka nchi za nje kutoa elimu kwa wasanii wa nchi zingine.

"Kuna utofauti mkubwa sana ukiangalia filamu za mataifa mengine na za kwetu hasa kwenye mtiririko wa matukio,ubora, uvaaji wa uhusiano , sisi bado tuko nyuma sana". Alisema mlela

Hata hivyo amefafanua kupitia tamasha hilo tasnia itaimarika na kupanuka na kupata masoko ya nje na kujitangaza kwani sanaa ni ya watu wote ni wakati wa wasanii kushirikiana kwa pamoja.

Aidha Mlela amesema kwa mwaka jana filamu ya kesho iliingia sokoni na kufanya vizuri aliyomshirikisha msanii Gabo zigamba na kwa mwaka huu kujipanga na vitu vizuri ambavo viko jikoni na kuwasihi mashabiki wakae mkao wa kushudia vitu vizuri.

Pia ametoa rai kwa waandaji wa Tuzo hizo kufanya kitu cha kipekee na tofauti katika kuboresha na kunogesha msimu huu wa pili japo ni changa kwa sasa , anaamini katika jambo lolote zuri lazima mawazo na maoni ni muhimu kuwasilishwa sehemu husika kufanyiwa ufumbuzi.

MAAFISA MADINI WATAKIWA KUTOBAGUA MIGODI

$
0
0
Na Asteria Muhozya, Mbinga 

Maafisa Madini nchini wametakiwa kutobagua migodi midogo kwa kuelekeza nguvu kwenye migodi mikubwa tu huku wakisisitizwa kutatua migogoro kwenye maeneo yao ya kazi na kuelezwa kuwa, watakaobainika wakibagua migodi hiyo na kutotatua migogoro wataondolewa kwenye nafasi zao. 

Hayo yalibainishwa Januari 17 na Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo wakati akizungumza na wachimbaji wadogo wa madini aina ya Sapphire wakati wa ziara yake katika kijiji cha Masuguru, Wilayani Mbinga mkoa wa Ruvuma. 

Naibu Waziri Nyongo alifanya ziara hiyo ikilenga kukagua shughuli za uchimbaji madini wilayani humo pamoja na kusikiliza kero za wachimbaji katika migodi hiyo, ambapo wachimbaji waliwasilisha kero za kutaka kutengewa maeneo kwa ajili ya shughuli za uchimbaji, bei elekezi za madini ikiwemo kuunganishwa na huduma ya umeme kwenye migodi yao. 

Akizungumza kijijini hapo, alimtaka Afisa Madini mkoa wa Ruvuma hukakikisha anaishughulikia kero hiyo na kuitatua mara moja na kuongeza kuwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano anataka wachimbaji nchini wachimbe madini, hivyo, maafisa madini kote nchini wahakikishe wanashughulikia kero katika maeneo yao ya kazi ikiwemo kusuluhisha migogoro. 

“Sisi ni matajiri, tumebarikiwa madini ya vito. Wachimbaji chimbeni lakini mchimbe katika maeneo yaliyoruhusiwa kuchimbwa”.alisisitiza. 

Alisema kuwa, kama mgogoro ni mkubwa wapo viongozi wa vyama vya wachimbaji wahakikishe kuwa wanafikisha migororo hiyo na kusema “tuleteeni na sisi lakini usipoishughulikia migogoro hiyo tutakuondoa. 

Aliongeza kwamba, serikali inalenga katika kuwatoa wachimbaji wadogo kutoka katika uchimbaji mdogo kwenda uchimbaji wa kati na hatimaye mkubwa na ndiyo sababu inaendelea na ujenzi wa vituo vya umahiri katika maeneo mbalimbali nchini ikilenga katika kutoa elimu ya uchimbaji bora, uchenjuaji bora, biashara ya madini na ujasiliamali ili kuhakikisha kwamba wachimbaji wadogo wanakua. 

Aliongeza kuwa, elimu ya ujasiliamali ni muhimu kwa wachimbaji wadogo kwa kuwa itawaandaa kuwa na uchimbaji endelevu na wenye tija. 

Akijibu ombi la ruzuku, aliwataka wachimbaji wadogo kujiunga katika vikundi vidogo vidogo ili iwe rahisi kwa wachimbaji hao kufikiwa ikiwemo kupatiwa huduma za leseni, elimu, vifaa, kuwamilikisha, kuwapatia mikopo na kuwafuatilia jambo ambalo litapelekea wafanye kazi kwa urahisi na kwa kulipa kodi za serikali na wao kubaki na kipato kitakachowezesha maisha bora. 

Alisema uwepo wa mazingira mazuri migodini utasaidia vijana kufanya kazi na hivyo kuwa na taifa lenye watu wanaofanya kazi. Aliwataka maafisa madini wote kuhakikisha wanashughulikia migogoro ya wachimbaji wadogo na kueleza kwamba, endapo serikali itakuta migogogoro ya wachimbaji wadogo katika maeneo yao wataondolewa. 

Aliongeza kwamba, wizara imejipanga na tayari kuna baadhi ya maeneo yametengwa kwa ajili ya wachimbaji na kuwasisisitiza kuhakikisha wanauza madini wanayoyachimba katika maeneo rasmi. 

Akizungumzia suala la broker, aliwataka kuhakikisha wanakuwa na leseni ya kufanya shughuli hizo ikiwemo vifaa vya kupimia madini na kuwataka kulipa kodi. Pia, aliwatahadharisha wachimbaji wanaoshirikiana na broker wasiokuwa na leseni kuacha kwani kwa kufanya hivyo ni kwamba kwamba wote wanaliibia taifa.” Maafisa madini hakikisheni mnawajua ma broker wote na wawe na leseni na walipe kodi, “ alisisitiza Nyongo. 

Akijibu ombi la ruzuku lililowasilishwa kwake, alisema fedha za ruzuku zilizokuwa zikitolewa awali hazikuwafikia walengwa wote na kueleza kuwa, wapo waliopata ruzuku hizo lakini hawakuwa wachimbaji na kuongeza kwamba, hivi sasa wizara inaangalia namna bora ya kuwasaidia wachimbaji. 

Kwa upande wake, Afisa Madini Mkoa wa Ruvuma Abraham Nkya alisema kuwa, mkoa huo tayari umetenga maeneo kwa ajili ya wachimbaji wadogo na kwamba watashirikiana na wachimbaji hao ili suala hilo liweze kuwasilishwa Tume ya Madini kwa ajili ya hatua zaidi. 

Awali , kiongozi wa wachimbaji aliwasilisha ombi kwa Naibu Waziri la wachimbaji kupatiwa ruzuku. Alisema mkoa huo umebarikiwa madini ya ujenzi, nishati, viwanda huku eneo la Masuguru likibariwa madini ya Sapphire. Alisema eneo hilo liliombwa kwa ajjili ya uchimbaji mdogo lakini mpaka sasa bado halijatengwa. 

Pia, alisema ipo changamoto ya kukosekana elimu kwa watendaji vijijini ambao wamesababisha mgizo mkubwa wa kodi kwa wachimbaji. 
Sehemu ya Wachimbaji Wadogo wa Madini ya Saphire wakiwa wameshika mabango yenye ujumbe Maalum kwa Naibu Waziri Stanslaus Nyongo baada ya kuwasili katika kijiji cha Masuguru Wilaya ya Mbinga Mkoani Ruvuma.
Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo mwenye sweta (nyekundu) katika picha ya pamoja na baadhi ya wachimbaji wadogo wa madini ya Sapphire katika kijiji cha Masuguru Wiaya ya Mbinga mkoa wa Ruvuma
Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo akisamiliana na baadhi ya wachimbaji wa madini ya Sapphire katika kijiji cha Masuguru mara baada ya kuwasili kijijini hap wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za uchimbaji madini wilayani humo
Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Cosmas Ishenyi akizungumza jambo wakati wa mkutano wa hadhara katika kijiji cha Masuguru. Katikati ni Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo.
Mmoja wa wachimbaji wananwake katika kijiji cha Masuguru akiwasilisha kero yake kwa Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo na Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Cosmas Ishenyi ( hawapo pichani) wakati wa ziara ya viongozi hao kijijini hapo.
Sehemu ya wachimbaji na wananchi katika kijiji cha Masuguru wakimsikiliza Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo hayupo pichani wakati wa ziara yake kijijini hapo kukagua shughuli za uchimbaji madini.

WABUNGE CCM WAMPONGEZA CAG KUITIKIA WITO WA KAMATI YA BUNGE

$
0
0
Mbunge wa Jimbo la Mbinga Mjini, Sixtus Mapunda. 

UNHCR – Distribution of Clothing to Refugee, Local Communities in Tanzania


WAZIRI KIGWANGALLA AKUTANA NA WAKALA ATAKAYELETA WATALII 10,000

$
0
0
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt.Hamisi Kigwangalla amekutana na kufanya mazungumzo  na Wakala wa watalii kutoka  Beijing nchini China, Bw.He Liehui ambaye kwa mwaka huu amepanga kuwaleta watalii 10,000 nchini Tanzania na kwa sasa yupo nchini kwa ajili ya kufanya maandalizi ya watalii hao.

Mazungumzo hayo kati yao  yamefanyika katika ofisi ndogo ya Wizara hiyo Mpingo House jijini Dar es Salaam

Aidha,  Wakala huyo Bw.He  anatarajia pia leo  kuonana na Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe.Kassim Majaliwa.

WANANCHI KATA YA BITURANA KIBONDO WAUFURAHIA UCHAGUZI MDOGO WA UDIWANI

MWANAMITINDO WA MAREKANI AFURAHISHWA NA VIVUTIO HIFADHI YA TAIFA TARANGIRE.

$
0
0
Anaandika Dixon Busagaga, Tarangire. 

MWANAMITINDO na muigizaji maarufu Marekani aliyewahi kung’ara katika taji la Miss Universe, Marisela De Montecristo aliwasili nchini hivi karibuni ametembelea Hifadhi ya Taifa ya Tarangire na kupokelewa na Mkuu wa Idara ya Utalii katika Hifadhi hiyo.

Muda mfupi baada ya kuwasili Mwanamitindo huyo aliyekuwa ameongozana na Mama yake mazazi pamoja na anayetajwa kuwa mchumba wake ,alikabidhiwa zawadi mbalimbali yakiwemo mavazi maalumu yanayotumiwa na Jamii ya Maasai.

Marisela baada ya kutembelea mane mbalimbali ya Hifadhi hiyo wakiwemo wanyama alieleza furaha yake huku akiahidi kuwa balozi wa vivutio vya utalii atakavyotembelea hapa nchini .

Mrembo huyo ambaye kwa sasa anaishi Los Angels amesema lengo la kuja nchini kutembelea vivutio vya utalii ni pamoja na kuangalia fursa mpya ipatikanayo katika sekta ya Utalii Duniani pamoja na kuvitangaza.

Mwanamitindi huyo anaendelea na ziara yake hiyo ya kitalii katika Hifadhi ya Ngorongoro ambako atashuhudia maajabu ya wanyama katika Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) na Bonde la ufa la Ngorongoro (Ngongoro Creator).”

Hospitali ya Bugando kuajiri Madaktari na wauguzi kutoka nchini Cuba

$
0
0

Hospitali ya Kanda ya Bugando inatarajia kuajili Madaktari na wauguzi 13 kutoka nchini Cuba katika kuhakikisha wanatoa huduma bora za afya kwa wananchi kutokana na kuongeza idadi hiyo ya madaktari.

Akizungumza Balozi wa Cuba nchini Tanzania Profesa Lucas Polledo amesema ziara yake katika hospitali Bugando ni kutokana ushirikiano uliopo kati ya Bugando na nchi ya Cuba.

Balozi amesema kuwa lengo ni kuangalia utoaji wa huduma za afya kwa wananchi. Aidha amesema kuwa wanaendelea kushirikiana na hospitali hiyo katika maeneo mengine ambayo yana changamoto katika utoaji wa huduma za afya.

Nae Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Kanda Bugando Profesa Abel Makubi amesema kuwa Madaktari saba wanakuja mwezi ujao na wengine watakuja.
Amesema kuna ushirikiano wa karibu kati ya hospitali ya Bugando na Cuba hivyo wanatarajia kupata mengi katika nchi hiyo.

Profesa Makubi mesema Madaktari wataokuja Madaktari Bingwa wa Mfumo wa Mkojo,Koo-pua na masikio (ENT),Wataalamuwa usingizi ,mionzi,na madaktari bingwa wa huduma za dharula pamoja na madaktari bingwa wa magonjwa ya ubongo na uti wa mgongo.


Balozi wa Cuba nchini Tanzania Profesa Lucas Polledo akitia saini kitabu cha wageni katika hospitali ya Kanda ya Bugando jijini Mwanza wakati alipotembelea hospitali hapo akiwa na familia yake.
Balozi wa Cuba nchini Tanzania Profesa Lucas Polledo akizungumza na menejimenti ya Hospitali ya Bugando wakati alipofanya ziara akiwa familia yake ikiwa na mahusiano yaliyopo katika ya hospitali nan chi ya Cuba.

WAZIRI MKUU KUWAPOKEA WATALII 300 KUTOKA CHINA

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameahidi kupokea kundi la watalii wasiopungua 300 ambao wanatarajiwa kuwasili nchini Machi, mwaka huu.

Watalii hao ni kundi la kwanza miongoni mwa watalii 10,000 wanaotarajiwa kuwasili nchini katika mwaka 2019 chini ya mpango unaosimamiwa baina ya Wizara ya Maliasili na Utalii, Bodi ya Utalii Tanzania na kampuni ya TouchRoad International Holding Group ya China.

Ametoa ahadi hiyo leo (Jumamosi, Januari 19, 2019) alipokutana na Mwenyekiti wa Touchroad Group, Bw. Liehui He na Mwenyekiti wa Bodi ya Utalii, Jaji Thomas Mihayo ofisini kwake Mlimwa, jijini Dodoma.

Waziri Mkuu amefikia uamuzi huo baada ya kuelezwa na Bw. He huyo kwamba kundi hilo la watalii likiwa Djibouti litapokelewa na Waziri Mkuu wa nchi hiyo na likienda Zimbabwe, litapokelewa na Rais wa nchi hiyo.

“Tanzania imeamua kuweka mkakati wa kuongeza idadi ya watalii nchini kwa kuboresha miundombinu ya usafiri na kukuza utalii kupitia vivutio vya vyakula vya asili, mavazi ya asili, wanyama, fukwe za bahari na milima. Kwa hiyo, ujio wa kundi hili kubwa, unatoa fursa mpya ya kutangaza vivutio vya nchi yetu,” amesema.

“Nitoe wito kwa Watanzania wanaoishi maeneo ya jirani na vivutio vyetu, wachangamkie fursa ya ujio wa watalii hawa katika maeneo mbalimbali. Wakifika Dar es Salaam, wanaweza kwenda Kigoma kuona Ziwa Tanganyika, mbuga zilizoko Nyanda za Juu Kusini, Arusha au vivutio vya Zanzibar. Tujiandae, tuwe tayari kuwauzia bidhaa mbalimbali,” amesema.

Pia amesema amefurahishwa na wazo lao la kuifanya Dar es Salaam iwe kitovu cha utalii (tourist hub) kwa makundi ya watalii ambayo yatakuja Tanzania na baadaye kutoka Tanzania kwenda Lusaka, Harare, Johannesburg na Djibouti.

Mwenyekiti huyo ambaye aliwasili nchini juzi, ameambatana na ujumbe wa watu 31 ambao unajumuisha waandishi wa habari, wasanii, wanamuziki na watu mashuhuri.

Akiwa Beijing, China, wakati akishiriki mkutano wa Jukwaa la Biashara baina ya Tanzania na China lililofanyika Septemba mwaka jana, Waziri Mkuu alikutana na uongozi wa kampuni ya TouchRoad ambayo ilionesha nia ya kutangaza fursa za utalii zilizopo hapa nchini.Ziara ya Bw. He ni sehemu ya utekelezaji wa makubaliano yaliyoingiwa kati ya kampuni ya TouchRoad na Bodi ya Utalii ya Tanzania, Novemba 2018.

Mapema, Bw. He alimweleza Waziri Mkuu nia ya kampuni hiyo kutekeleza makubaliano yao ya kutangaza vivutio vya utalii vya Tanzania katika soko la China ili kuvutia watalii wapatao 10,000 waitembelee Tanzania katika mwaka 2019.

“Tumepanga kuleta watalii 10,000 kwa mwaka huu wa 2019 na tumeweka lengo la kuongeza idadi hiyo kwa asilimia 20 kila mwaka kwa muda wa miaka mitano. Pia tuna lengo la kuitumia ndege ya ATCL ili ilete watalii moja kwa moja kutoka Shanghai, China,” alisema.Akielezea ujio wa kundi la kwanza la watalii, Bw. He alisema kundi hilo litakaa Djibouti kwa siku moja, Tanzania siku nne (tatu za kulala) na Zimbabwe siku tatu (mbili za kulala) na kisha kurejea China.

Alisema wanapanga kila mwezi wawe na kundi kubwa la watalii ambao watakuwa wanafikia Tanzania na kupelekwa nchi nyingine kwa sababu Wachina wengi hupenda kufanya utalii kwa siku walau 10, lakini wapelekwe maeneo matatu au manne tofauti kuona vivutio vya aina nyingine badala ya kukaa sehemu moja kwa kipindi chote hicho.

“Watalii hawa wakija kwa siku tatu au nne, wana uhakika wa kutumia dola za Marekani zaidi 2,000, wakienda eneo jingine watatumia fedha pia, namna hiyo tuna uhakika wa kuongeza pato la Taifa, lakini pia tuna uhakika wa kutengeneza ajira kwa Watanzania,” alisema.


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 980,
41193 – DODOMA, 

JUMAMOSI, JANUARI 19, 2019.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mwenyekiti wa Kampuni ya Touchroad Group ya China, Bw. He Liehui, ofisini kwa Waziri Mkuu, jijini Dodoma, Januari 19, 2019. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mwenyekiti wa Kampuni ya Touchroad Group ya China, Bw. He Liehui, ofisini kwa Waziri Mkuu, jijini Dodoma, Januari 19, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
Viewing all 110171 articles
Browse latest View live




Latest Images