Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110171 articles
Browse latest View live

WAKUU WA MIKOA WAIMBA WIMBO WA UZALENDO MRADI WA SGR ,MREMA ASEMA JPM NI JASIRI


MWENDO MDUNDO,USIMIKAJI NGUZO ZA UMEME KUENDESHA TRENI YA KISASA (SGR) WAANZA

$
0
0

Kazi ya Usimikaji wa Nguzo za Umeme utakaotumika Kuendesha treni za Kisasa zitakazotumia Umeme na Reli ya kisasa - SGR imeanza eneo la Soga nje Kidogo ya Kambi ya Ujenzi wa Reli ya  Kisasa liyopo Soga   mkoani  Pwani  mapema  Desemba  2018. Nguzo hizo zinajengwa umbali wa Mita 500 kutoka nguzo moja hadi nyingine, urefu wa nguzo moja ni Mita 9.5 huku uzito wa nguzo Moja ukiwa Tani 2.4, zina uwezo wa kudumu kwa kipindi cha Miaka 120 pia zimewekewa madini ya Zinki kwa ajili ya kuzuia kutu.

DC ILALA ATEKELEZA AGIZO LA RAIS KWA KUGAWA VITAMBULISHO KWA WAMACHINGA

$
0
0
Na Heri Shaban

MKUU wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema jijini Dar es Salaam ameanza kukabidhi vitambulisho vya wafanyabiashara wadogowadogo maarufu kama Wamachinga waliopo Kariakoo.

Mjema amegawa vitambulisho hivyo Dar es Salam ikiwa ni siku mbili tu zimepita baada agizo la Rais John Magufuli kuwagiza wafanyabiashara wote watambulike wakiwa na vitambulisho hivyo vinavyotolewa vya Wajasiriamali wadogo.

"Katika Wilaya yangu ya Ilala leo(jana) nimegawa vitambulisho 5000 kwa Wamachinga wa Kariakoo ambao tulikuwa tunawatambua katika mfumo maalum, zoezi hili baadae litahamia kwa Mama lishe wote waliopo wilayani Ilala ambao mtaji wao chini ya shilingi milioni nne," alisema Mjema

Amesema katika wilaya ya Ilala mchakato huo umekwenda vizuri kwani wamachinga walishawekwa pamoja katika mfumo maalum ambao wanatambulika rasmi na Serikali. Aliwataka Wamachinga na wafanyabiashara wote kufuata utaratibu na wote watapewa vitambulisho hivyo katika ofisi za Halmashauri zilizopo jengo la Anatogluo.

Aidha amesema wote waliopewa vitambulisho wanatambulika na biashara zao na maeneo kama sio mfanyabishara hawezi kupewa.Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala Elzabeth Thomas amesema Manispaa ya Ilala wamejipanga vizuri katika juhudi za kumsaidia Rais na tayari wameanza na Wamachinga wa Kariakoo wote.

Thomas amesema mpango huo wa kugawa vitambulisho ni endelevu mpaka wote wapewe vitamburisho Watendaji wake wa Manispaa hiyo wanasimamia. Naye Makamu Mwenyekiti wa Wamachinga Kariakoo Yusuph Namoto amesema wao ni wazalendo wanaungana na Serikali yao tukufu katika juhudi za kumsaidia Rais katika kukuza uchumi.Yusuph amesema kwa sasa wanahitaji kukuza uchumi biashara zao kila wakati zinabadilika hivyo wanaitaji uwezeshaji ili waweze kupiga hatua. 
Mkuu wa wilaya ya Ilala sophia Mjema akimkabidhi kitambulisho mfanyabiashara mmachinga Ramadhan Said Dar es Salam jana ,wengine OFISA Masoko Ilala na Ofisa Biashara wa Manispaa wakishudia tukio hilo.Picha na Heri Shaaban.
 Makamu Mwenyekiti wa Wafanyabiashara wamachinga Yusuph Namoto akionyesha KITAMBURISHO chake mara baada kukabidhiwa na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema Dar es Salam

PROFESA MBARAWA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA OFISI ZA WIZARA YA MAJI IHUMWA

$
0
0
Waziri wa Maji, Mhe. Profesa Makame Mbarawa amefika eneo la Ihumwa kukagua maendeleo ya ujenzi wa ofisi za Wizara ya Maji katika mji wa Serikali kwa nia ya kujionea hatua iliyofikiwa ya ujenzi huo.

Profesa Mbarawa amemsisitiza mkandarasi kufanya kazi usiku na mchana ili kumaliza ujenzi wa ofisi hizo kwa wakati ifikapo Januari 31, 2019 kulingana na maagizo ya Serikali.

Ujenzi wa Ofisi za Wizara ya Maji Ihumwa ulianza rasmi Disemba 7, 2018 na unatarajiwa kukamilika ndani ya siku 60.Kwa sasa ujenzi upo katika hatua ya msingi na unatekelezwa na Mkandarasi SUMA JKT kikiongozwa na Mhandisi Juma Ibrahimu chini ya Mtaalam elekezi Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) wakisaidiana na Wataalam kutoka Wizara ya Maji wakiongozwa na Mhandisi Tamim Katakweba.

Profesa Mbarawa amesema Wizara ya Maji imejipanga kuhakikisha upatikanaji wa huduma ya uhakika ya maji muda wote, ambapo Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira jijini Dodoma (DUWASA) imeweka vituo maalum kwa ajili ya kusambazia maji wakati wote wa ujenzi unaoendelea kwenye mji wa Serikali.

Aidha, amesema utekelezaji wa ujenzi wa Mradi wa Maji Ihumwa ambao utahudumia mji huo wa Serikali chini ya usimamizi wa DUWASA unaendelea vizuri, ambapo mpaka sasa ujenzi wake umefikia asilimia 75.

Huku ujenzi wa tenki la maji litakalotumika kuhifadhi maji kwa ajili ya kusambaza maji katika maeneo ya mji huo lenye ujazo wa lita milioni moja ukiwa katika hatua nzuri na kazi ya ulazaji mabomba ikiwa imeanza. Mradi huo unatarajiwa kukamilika kufikia miwshoni mwa mwezi Januari, 2019.

Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi akimpa maelezo Waziri wa Maji, Mhe. Profesa Makame Mbarawa kuhusu ujenzi wa tenki la maji Ihumwa unaoendelea lenye ujazo wa lita milioni moja.
Waziri wa Maji, Mhe. Profesa Makame Mbarawa akisikiliza maelezo ya maendeleo ya ujenzi wa ofisi za Wizara ya Maji katika mji wa Serikali, Ihumwa kutoka kwa Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi alipotembelea kuangalia hatua ya ujenzi wa ofisi za wizara yake.
Waziri wa Maji, Mhe. Profesa Makame Mbarawa akionyeshwa ramani ya ujenzi wa ofisi za Wizara ya Maji katika mji wa Serikali, Ihumwa na Mratibu wa Mradi kutoka Wizara ya Maji, Mhandisi Tamim Katakweba alipotembelea kufuatilia maendeleo ya ujenzi wa ofisi za wizara yake.
Mafundi wakiendelea na ujenzi wa ofisi za Wizara ya Maji katika eneo la mji wa Serikali, Ihumwa ambapo ujenzi wake unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Januari, 2019.

WABANGUAJI KOROSHO WAMPA KONGOLE RAIS MAGUFULI

$
0
0

Uamuzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, kununua korosho za wakulima na kuzibangua nchini umepongezwa na Umoja wa Wabanguaji Wadogo wa Korosho Tanzania (UWWKT).

Akisoma risala mbele ya Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhandisi Stella Manyanya, Mwenyekiti wa umoja huo Bi. Tumpale Magehema amesema uamuzi wa Rais Magufuli una nia ya kuwapa ajira wanachama wake wapatao 2881, jambo ambalo ni la kupongezwa.

Licha ya kutoa ajira Bi. Tumpale ameueleza uamuzi huo wa kijasiri uliofanywa na Rais Magufuli utaongeza ari ya kufanya kazi na kuchochea ukuaji wa uchumi hasa kwenye mikoa inayolima korosho kwa wingi.

Akitoa taarifa kwa mgeni rasmi, Katibu wa umoja huo Bw. Audax Mkongi, alimueleza mhandisi Manyaya kuwa umoja huo ni asasi mwamvuli ya kitaifa ya wabanguaji wadogo yenye jumla ya vikundi 183 kutoka wilaya tisa za mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani na Morogoro. Baadhi ya wilaya hizo ni Ulanga, Tandahimba, Kisarawe, Liwale na Ruangwa.

Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhandisi Stella Manyanya, akisisitiza jambo kwenye kikao na wawakilishi wa Umoja wa Wabanguaji Wadogo wa Korosho Tanzania(UWWKT) kilichofanyika kwenye hoteli ya Lindi Sea View. Pembeni ya Naibu Waziri ni Mkuu wa Wilaya ya Lindi, mhehsimiwa Shaibu Ndemanga, Mkurugenzi Mkuu wa SIDO Profesa Sylvester Mpanduji na kulia ni Mwenyekiti wa UWWKT Tumpale Magehema 
Baadhi ya wanachama wa Umoja wa Wabanguaji Wadogo wa Korosho Tanzania (UWWKT) wakimisikiliza mgeni rasmi (hayupo pichani) Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, mhandisi Stella Manyanya. Umoja huo wa wabanguaji wadogo wa korosho umeonesha nia ya kubangua korosho iliyonunuliwa na serikali. 
Mwenyekiti wa Umoja wa Wabanguaji Wadogo wa Korosho Tanzania (UWWKT) Bi. Tumpale Magehema akisoma risala mbele ya Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, mhandisi Stella Manyanya alipofanya kikao na baadhi ya wanachama wa umoja huo mjini Lindi. 
Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, mhandisi Stella Manyanya(katikati walioketi) kwenye picha ya pamoja na wawakilishi wa wanachama wa Umoja wa Wabanguaji Wadogo wa Korosho Tanzania (UWWKT). Wengine walioketi kuanzia kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa SIDO, Profesa Sylvester Mpanduji, Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Shaibu Ndemanga, Mwenyekiti UWWKT Tumpale Magehema na Mkurugenzi Mtendaji wa ANSAF, Audax Rukonge. 

Halmashauri Msitoze kodi Zilizofutwa kwenye Madini ya Chumvi- Nyongo

$
0
0
Na Greyson Mwase, Mtwara 

Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo amezitaka halmashauri zote nchini kutokutoza kodi zilizofutwa kwenye madini ya chumvi ili wazalishaji wa madini hayo waweze kufanya kazi katika mazingira mazuri na kulipa kodi stahiki serikalini. 

Naibu Waziri Nyongo ameyasema hayo leo Desemba 12, 2018 kwenye mkutano wake na wazalishaji wa madini ya chumvi kutoka katika Chama cha Wazalishaji wa Madini katika Mkoa wa Mtwara (MTWAREMA) kilichofanyika kwenye Ofisi ya Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Mtwara mjini Mtwara ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku mbili katika mkoa huo yenye lengo la kukagua shughuli za uchimbaji wa madini pamoja na kusikiliza na kutatua kero za wachimbaji wa madini. 

Alisema kuwa, Serikali ya Awamu ya Tano kupitia Wizara ya Madini iliamua kufuta baadhi ya kodi walizokuwa wanatozwa wazalishaji wa madini ya chumvi ambazo zilikuwa ni mzigo kwao na kushindwa kufikia malengo waliyojiwekea. “Ninaziagiza halmashauri zote nchini kutoza kodi kwa kuzingatia sheria zilizopo huku zikihakikisha kodi zilizofutwa kisheria hazitozwi tena.” Alisema Naibu Waziri Nyongo. 

Akielezea mikakati ya Serikali kupitia Wizara ya Madini katika kuwasaidia wazalishaji wa madini ya chumvi katika mkoa wa Mtwara, Naibu Waziri Nyongo alieleza kuwa ni pamoja na kuangalia namna ya uanzishwaji wa kiwanda cha chumvi katika mkoa wa Mtwara kwa ajili ya kuongeza ubora na thamani ya madini ya chumvi. 
Kutoka kushoto, Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo, Kaimu Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Mtwara, Mhandisi Ephraim Mushi, Msaidizi wa Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo, Mhandisi Noel Baraka wakipata  maelezo kutoka kwa Mhandisi Migodi Mwandamizi kutoka Ofisi ya Madini ya Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Mtwara, Mhandisi Aidan Mhando kwenye eneo la uchimbaji wa mchanga la Ziwani lililopo Wilayani Mtwara mkoani Mtwara. 
Afisa Tarafa wa Ziwani, Fransis Mkuti (kushoto) akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (kulia) kwenye eneo la uchimbaji wa mchanga la Ziwani lililopo Wilayani Mtwara mkoani Mtwara.

Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (katikati) akichimba mchanga pamoja na wachimbaji wa madini ya mchanga kwenye eneo la uchimbaji wa mchanga la Ziwani lililopo Wilayani Mtwara mkoani Mtwara. 
Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo akikagua madini ya chumvi katika ghala la kuhifadhi madini hayo kwenye shamba la chumvi linalomilikiwa na Jeshi la Magereza la Kiwanda Chumvi lililopo wilayani Mtwara mkoani Mtwara. 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>

Prof. Ndalichako aahidi kushughulikia uchakavu wa miundombinu ya vyuo vya VETA

$
0
0
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako ameahidi kushughulikia changamoto ya uchakavu wa miundombinu katika vyuo vya ufundi stadi vinavyomilikiwa na VETA ili kuwezesha utoaji wa mafunzo bora sambamba na mabadiliko mbalimbali ya teknolojia viwandani na kukidhi viwango vya mahitaji ya waajiri.

Prof.  Ndalichako alitoa ahadi hiyo kufuatia ombi la Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), Dkt. Pancras Bujulu wakati akitoa maelezo mafupi kabla ya kumkaribisha kutoa hotuba kwenye sherehe za mahafali ya 33 ya Chuo cha VETA Moshi yaliyofanyika chuoni hapo Jumatano, 12 Desemba 2018.

Katika maelezo yake, Dkt. Bujulu alisema kuwa baadhi ya vyuo vya VETA ni vikongwe mno na miundombinu yake imechakaa sana, hivyo ukarabati wake kwa kutumia fedha ambazo VETA imekuwa ikipatiwa na serikali umekuwa ni mgumu. Alisema pamoja na uchakavu wa miunndombinu kwa ujumla vifaa na mashine zinazotumika kwenye karakana kwa ajili ya kufundishia pia zimechakaa na zingine  zimepitwa na wakati kutokana na mabadiliko ya kiteknolojia hivyo hazifai kutumika kufundishia ili kutoa mafundi wanaokidhi mahitaji ya wakati huu.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako akitoa hotuba kwenye mahafali ya 33 ya Chuo cha VETA Moshi yaliyofanyika chuoni hapo Jumatano, tarehe 12 Desemba 2018.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), Dkt. Pacras Bujulu akitoa Maelezo kuhusu mipango na mikakati ya VETA katika kutoa na kusimamia mafunzo ya ufundi stadi.
 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako akitazama nyaraka za kampuni ya LES Inspection iliyoanzishwa na wahitimu wa VETA ambao wamefuzu na kupata leseni za kutoa ithibati ya kazi za uungaji vyuma kwa kiwango cha kimataifa wakati akitembelea maonesho ya wahitimu kwenye mahafali ya 33 ya Chuo cha VETA Moshi, Jumatano, tarehe 12 Desemba 2018. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa VETA, Dkt. Pancras Bujulu na anayefuatia ni Mwenyekiti wa Chemba ya Madini na Nishati, Balozi Ami Mpumbwe.
  Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako akisikiliza maelezo kutoka kwa mhitimu wa fani ya Ufundi wa Kaanga Mvuke (Boiler Mechanics) juu ya mfumo wa kaanga mvuke (Boiler) unavyofanya kazi kwenye mahafali ya 33 ya Chuo cha VETA Moshi, Jumatano, tarehe 12 Desemba 2018. Kulia kwa Waziri ni Mkurugenzi Mkuu wa VETA, Dkt. Pancras Bujulu.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Gulamali aachiwa huru, baada ya kukutwa hana kesi ya kujibu

$
0
0
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi mkoa wa Singida imetupilia mbali kesi ya kupokea rushwa iliyokuwa ikimkabili mfanyabiashara, Haidar Hussein Gulamali baada ya kutopatikana na kesi ya kujibu.

Uamuzi huo umetolewa na Hakimu Mkazi Mfawidhi, Consolata Singano baada ya upande wa Jamuhuri  kifungo kesi Kwani kutoa mashahidi 9. Na kusema amezingatia ushahidi wa mashahidi 9 wa upande wa Jamuhuri waliofika mahakamani hapo kutoa ushahidi was lakini kati yao wote  hakuna ushahidi unaomgusa Gulamali moja kwa moja.

Akisoma Uamuzi huo,  Hakimu Singano amesema upande wa mashtaka wameshindwa kuthibitisha kesi yao na kutoka Sababu moja wako Ni kutofautiana kwa mashahidi watatu kuhusu bahasha iliyobeba fedha.

Amesema katika ushahidi wao kila shahidi ametaja rangi tofauti ambapo mmoja ametaja Kaki, mwingine nyeupe, huku wa mwisho akitaja Brown jambo ambalo mahakama imeshindwa kuelewa bahasha ipi ilibeba fedha.

Pia amesema hata hatua za ukamataji hazikuanishwa vizuri kwani hakuna mahali iliyoonyesha Pesa ziliwahi kutaifishwa hadi zilipofikishwa mahakamani, pia namna zilivyotunzwa mpaka kufikishwa kama ushahidi.
Kutokana na hatua hiyo, Hakimu Singano amesema anatupilia mbali kesi hiyo na kumuachia Huru a

Katika kesi hiyo Gulamali alikuwa akitetewa na wakili Godfrey Wasonga,  

Miongoni mwa mashahidi waliofika kutoa ushahidi mahakamani hapo Ni pamoja na  Ofisa Usalama mkoa wa Singida, Kiseo Nzowa anayedaiwa kupewa rushwa hiyo ambapo amedai anafanya kazi kwa mujibu wa sheria.

Shahidi huyo Katika ushahidi wake alidai Gulamali alimpa Sh.Milioni 2 ili amsaidie kupitisha jina lake kwenye kinyang’anyiro cha ubunge Singida Kaskazini na kwamba yeye hakuwa Mjumbe Kamati ya Siasa Wilaya.

NAIBU WAZIRI CONSTANTINE KANYASU ATEMBELEA HIFADHI YA TAIFA YA KISIWA CHA RUBONDO

$
0
0
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Constantine Kanyasu (kulia) akipewa maelezo kutoka kwa Mkuu wa Hifadhi ya Kisiwa cha Rubondo, Ignas Gara (katikati) mara baada ya kuwasili katika hifadhi ya kisiwa hicho ambapo  ambapo aliweza kuzungumza na watumishi wa Hifadhi hiyo  iliyopo wilayani Chato mkoani Geita. Kushoto ni Afisa wanyamapori wa Hifadhi hiyo, Emmanuel Kaaya. 
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Constantine Kanyasu (katikati) akipewa maelezo kutoka kwa Meneja wa Hoteli ya Asilia, Adam Juma (wa pili kulia) akiwa pamoja na Mkuu wa Hifadhi hiyo, John Gara (wa pili kushoto) wakati alipofanya ziara katika hifadhi ya Taifa  ya  kisiwa cha Rubondo    ambapo aliweza kutembelea  hoteli hiyo iliyopo ndani ya  Hifadhi hiyo  iliyopo wilayani Chato mkoani Geita. Kulia ni Afisa wanyamapori wa Hifadhi hiyo, Emmanuel Kaaya na kulia ni Adrian William
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Constantine Kanyasu akiwa pamoja na Mkuu wa Hifadhi hiyo, John Gara (kulia) wakiangalia baadhi ya picha kwenye simu ya Sokwe wakati Naibu Waziri huyo alipofanya ziara katika hifadhi ya Taifa  ya  kisiwa cha Rubondo, Kushoto ni Katibu wa Naibu Waziri huyo,Bw. Zulu Ng’ondya.
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,  Constantine Kanyasu (katikati) akiwa pamoja na Mkuu wa Hifadhi hiyo, John Gara (kulia) wakiwa kwenye boti wakivuka  wakati Naibu Waziri huyo alipofanya ziara katika hifadhi ya Taifa  ya  kisiwa cha Rubondo, Kushoto ni Katibu wa Naibu Waziri huyo,Bw. Zulu Ng’ondya
Baadhi ya sehemu za kupumzika katika hifadhi ya Taifa  ya  kisiwa cha Rubondo.

(PICHA ZOTE NA LUSUNGU HELELA-WMU)

WAZIRI LUGOLA ATOA ONYO KALI KWA WANAOJIPENYEZA KUPITIA TAASISI ZA DINI KUHUBIRI SIASA, UCHOCHEZI, KUVURUGA AMANI NCHINI

$
0
0
Na Felix Mwagara, (MOHA), MARA.
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amesema wapo baadhi ya watu ambao wanajipenyeza kupitia mgongo wa taasisi za dini nchini kujifanya wahubiri kumbe ni wachochezi na wanajiingiza katika masuala ya kisiasa.

Amesema Wizara yake ipo makini katika kusajili Makanisa na Misikiti yote nchini na mpaka sasa wana maombi mengi ambayo yametumwa wakiomba kusajiliwa ambapo baadhi yao bado hayajasajiliwa kwasasababu wanahitaji umakini mkubwa katika kufanya uchunguzi wa kina kabla hawajatoa usajili ikiwa na lengo la kuepusha baadhi ya taasisi za dini zenye mpango mbaya na maendeleo ya  nchi.  

Akizungumza na mamia ya wananchi wa Kijiji cha Sunsi, Kata ya Nampindi, Jimbo la Mwibara, Wilaya ya Bunda, Mkoani Mara, jana, Lugola ambaye ni Mbunge wa Jimbo hilo, alisema taasisi za dini zina mchango mkubwa nchini na uwepo wao ni muhimu katika maendeleo ya nchi, na serikali inawathamini mchango wao katika kuimarisha amani na pia kuwaweka watu pamoja lakini kuna baadhi ya dini hizo zinakiuka utaratibu wa usajili na kuvunja sheria za nchi kwa kuacha kuhubiri masuala ya kiroho wanajihusisha na masuala ya kisiasa pamoja na uchochezi. 

“Serikali ya Rais Dk. John Magufuli ya Awamu ya Tano haitakua tayari kwa mwananchi yeyote kutumia mwavuli wa dini, au kufanya misikiti na makanisa kuwa kichaka kwa kufanya uchochezi katika nchi hii, kuhatarisha amani ya nchi hii, tupo makini na hatuwezi kuchezewa na mtu yeyote au taasisi yoyote,” alisema Lugola.
 AZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akizungumza na wananchi wa Kata ya Nampindi, Mwibara, Wilaya ya Bunda, Mkoani Mara, katika Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Sunsi Wilayani humo leo. Katika hotuba yake, alitoa onyo kwa baadhi ya watu wanajipenyeza kupitia mgongo wa taasisi za dini kujifanya wahubiri kumbe ni wachochezi na wanajiingiza katika masuala ya kisiasa.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kushoto), akicheza na Wanakwaya wa Kijiji cha Busambu, Kata ya Nampindi, jimboni kwake Mwibara, Bunda kabla ya kuanza mkutano wake wa kwanza kati ya minne na wananchi wa Kata hiyo, mkoani Mara. Lugola aliwataka wananchi wa Kijiji hicho kufanya maandalizi ya kilimo ili wasije kukumbwa na njaa kwa hapo baadaye endapo hawatalima. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

BALOZI SEIF AFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA FALME ZA KIARABU(UAE)

$
0
0
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif AliIddi alisema Zanzibar itaendelea kuwa karibu na Muungano wa Falme za Kiarabu {UAE} katika dhana nzima ya kuimarisha Sekta ya Uchumi na Ustawi wa Jamii wa Wananchi wa pande zote mbili. Alisema hatua hiyo inakuja kufuatia mafungamano makubwa yaliyopo kati ya Zanzibar na Muungano wa Mataifa hayo hasa katika Sekta ya Biashara kwa usafirishaji wa bidhaa za Matunda na Viungo.

Balozi Seif Ali Iddi alieleza hayo wakati wa mazungumzo yake na Balozi Mpya wa Muungano wa Falme za Kiarabu {UAE} Bwana Khalifa Abdulrahman Mohamed Al – Marzooqi aliyefika Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar kujitambulisha rasmi. Alisema kutokana na utulivu mkubwa uliopo Zanzibar ulioambatana na Miundombinu sahihi ya Uwekezaji Wawekezaji wa Mataifa hayo wana fursa nzuri ya kutumia nafasi hiyo ikiwa ni njia ya kuendeleza uhusiano wa muda mrefu uliopo kwa sehemu hizo mbili.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alimueleza Balozi huyo wa Muungano wa Falme za Kiarabu { UAE} kwamba wakati umefika kwa watendaji wake kufuatilia kwa kina mambo yaliyokubalika katika Mikutano na Vikao kufuatia ziara ya Rais wa Zanzibar aliyoifanya katika Mataifa hayo rafiki miezi michache iliyopita.

Balozi Mpya Bwana Khalifa Abdulrahman Mohamed Al – Marzooqi wa Muungano wa Falme za Kiarabu {UAE} kati kati akisabahiana na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alipofika Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar kujitambulisha rasmi.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akisisitiza umuhimu wa Wawekezaji wa Muungano wa Falme za Kiarabu kutumia fursa za Uwekezaji zilizopo Tanzania kuanzisha Miradi yao.
Balozi Khalifa Abdulrahman Mohamed Al – Marzooqi wa Muungano wa Falme za Kiarabu {UAE}akimueleza Balozi Seif shauku ya Wafanyabiashara wa Mataifa ya Muungano wa Falme za Kiarabu kutaka kuwekeza Zanzibar kutokana na mazingira mazuri ya Miradi ya Kiutalii. Picha na – OMPR – ZNZ.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA


DKT. MWANJELWA AITAKA TAKUKURU KUHAKIKISHA INADHIBITI MIANYA YA RUSHWA

$
0
0
Serikali imeitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU)  kuelekeza nguvu zaidi kuhakikisha mianya ya rushwa ndani ya taasisi za umma na jamii kwa ujumla inadhibitiwa ipasavyo ikiwa ni pamoja na kutowaonea haya wanaobainika kujihusisha na vitendo vya rushwa bila kujali vyeo vyao. Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) wakati akifunga mkutano mkuu wa siku mbili wa mwaka wa viongozi wa TAKUKURU nchini uliofanyika katika ukumbi wa Bunge wa Pius Msekwa, jijini Dodoma.
Mhe. Mwanjelwa amesema, watumishi wote wa TAKUKURU wamekula kiapo na wamepewa dhamana ya kuzuia na kupambana na rushwa, hivyo wametakiwa kutomuogopa mtu yeyote anayejihusisha na rushwa na kumshughulikia ipasavyo kwa mujibu wa sheria.
Mhe. Mwanjelwa ameongeza kuwa, katika kutekeleza azma ya serikali kufikia uchumi wa kati wa viwanda, TAKUKURU ikiwa ni taasisi iliyopewa dhamana na serikali ya kupambana na rushwa, haina budi kudhibiti vitendo vya rushwa katika sekta zilizopewa kipaumbele katika Mkakati wa Kitaifa Dhidi ya Rushwa na Mpango wa Utekelezaji Awamu ya Tatu (NACSAP III).
Mhe. Mwanjelwa ameziainisha sekta zilizopewa kipaumbele, kuwa ni pamoja na sekta ya manunuzi ya umma, ukusanyaji wa mapato, maliasili na utalii, madini, gesi, afya, elimu na ardhi, hivyo TAKUKURU kuanzia ngazi ya wilaya inapaswa kutoa mchango kufikia uchumi wa kati wa viwanda. Aidha, Mhe. Mwanjelwa amerejea maelekezo ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George Mkuchika (Mb) kwa TAKUKURU alipokuwa akifungua mkutano huo ya kuwataka wadhibiti mianya ya rushwa katika uchaguzi ujao wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika mwakani ambapo nae amesisitiza vitendo vya rushwa vidhibitiwe kikamilifu kwani ni kikwazo cha upatikanaji wa viongozi wenye sifa na uadilifu.
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akizungumza na viongozi wa TAKUKURU nchini wakati akifunga mkutano mkuu wa mwaka wa siku mbili wa viongozi hao uliofanyika katika ukumbi wa Bunge wa Pius Msekwa, jijini Dodoma.
Viongozi wa TAKUKURU nchini wakimsikiliza Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) wakati akifunga mkutano mkuu wa mwaka wa siku mbili wa viongozi hao uliofanyika katika ukumbi wa Bunge wa Pius Msekwa, jijini Dodoma.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Uchaguzi DRC 2018: Majengo ya tume ya uchaguzi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo yateketea

$
0
0

Majengo yanayotumiwa na tume ya taifa ya uchaguzi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo yameshika moto na kuteketea mjini Kinsasa.

Moto huo ulizuka mwendo wa saa nane usiku wa manane na kuzua taharuki ikizingatiwa kwamba ni siku 10 zilizosalia kabla ya uchaguzi mkuu kufanyika nchini humo.

Moshi mweusi ulitanda angani na uliweza kuonekana kutoka mbali asubuhi kulipopambazuka, shirika la AFP limeripoti.

Moto huo unadaiwa kuathiri majengo ambayo yamekuwa yakitumiwa kuhifadhi vifaa vya uchaguzi.

Mradi Uzalishaji Umeme Bonde la Mto Rufiji Kuleta Neema Nchini

NAIBU WAZIRI KWANDIKWA AAGIZA UKARABATI DOM – MORO KUKAMILIKA HARAKA

$
0
0
Na Siti Said
Naibu Waziri wa Ujenzi, Elias Kwandikwa, amemtaka mkandarasi wa kampuni CGI Contractors Limited anayekarabati barabara ya Dodoma- Morogoro sehemu ya Magubike na Gairo kuhakikisha anakamilisha kazi hiyo mapema ili kupunguza adha ya msongamano wa magari katika eneo hilo.
Agizo hilo amelitoa leo wilayani Gairo mkoani Morogoro akiwa katika ziara ya kikazi ya kukagua miundombinu inayosimamiwa na sekta yake katika mikoa ya Dodoma na Morogoro ili kujionea maendeleo yake.

Aidha, Naibu Waziri Kwandikwa amemsisitiza mkandarasi huyo kuchukua tahadhari katika kipindi hiki cha mvua ikiwa ni pamoja na kuhakikisha ujenzi wa barabara hiyo unakuwa imara hususan katika sehemu za miinuko ili kuzuia ajali zinazoweza kutokea katika maeneo hayo. "Hakikisheni mnamaliza haraka ukarabati wa barabara hii, magari hapa yamekuwa mengi na msongamano ni mkubwa, mnachotakiwa kufanya kwa sasa ni kufuatilia taarifa za hali ya hewa ili muweze kukabiliana na mvua na huku mkipanga ratiba zenu kuhakikisha mnakamilisha kazi hii mapema", amesema Naibu Waziri Kwandikwa.

Akiwa njiani kuelekea mkoani Morogoro katika eneo la Kibaigwa (panda mbili) mjini Dodoma, Naibu Waziri Kwandikwa amekagua madaraja yanayojengwa na Wakala wa Barabara ( TANROADS), mkoani humo na kuwapongeza kwa ujenzi wa madaraja hayo ili kudhibiti maji yanayotuama hapo hususan katika kipindi cha mvua na kusababisha kero kwa watumiaji wa barabara hiyo. Ameongeza kuwa kwa mwaka huu wa fedha 2018/ 2019, Serikali imetenga fedha kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu kuhusu ujenzi wa barabara ya Dodoma - Morogoro kutokana na mahitaji ya barabara hiyo kuonekana kuwa ni makubwa kutokana na ongezeko la watu na magari mara baada ya Serikali kuhamia Dodoma.
 Naibu Waziri wa Ujenzi, Elias Kwandikwa, akitizama uimara wa kingo mojawapo iliyopo katika moja ya madaraja yanayojengwa eneo la Kibaigwa mjini Dodoma. Madaraja hayo yanajengwa kwa ajili ya kuzuia maji ambayo hutuama na kusababisha mafuriko katika eneo hilo. 
 Naibu Waziri wa Ujenzi, Elias Kwandikwa, akitoa maelekezo kwa Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), Mkoa wa Dodoma, Mhandisi Leonard Chimagu, kuhusu namna ya kuboresha ujenzi wa madaraja yanayojengwa na Wakala huo eneo la Kibaigwa mjini Dodoma.
 Muonekano wa sehemu ya barabara ya Dodoma – Morogoro eneo la Gairo ambalo linakarabatiwa na Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoa wa Morogoro.
 Naibu Waziri wa Ujenzi, Elias Kwandikwa, akikagua moja ya jengo lililopo kwenye mzani mpya wa Dakawa Magereza mkoani Morogoro. Wa Kwanza kulia ni Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), Mkoa wa Morogoro Mhandisi Dorothy Mtenga. 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Mbunge wa Njombe mjini Edward mwalongo akikagua ujenzi wa miradi mbalimbali jimboni kwake

$
0
0
Akizungumza wakati wa ziara ya Kamati ya Mfuko wa Jimbo iliyofanywa kwa lengo la kukagua na kupitisha miradi itakayosaidiwa na Mfuko huo, Mbunge wa Jimbo la Njombe Kusini Edward Mwalongo amesema kuwa kiasi cha shilingi milioni 40 kitatumika kununulia vifaa vya ujenzi kulingana na mahitaji ya mradi husika na vitagawiwa kwenye Kata 13 za jimbo hilo ili kuweza kuchochea na kuchangia kasi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Mwalongo amesema kuwa vipaumbele vya Mfuko wa Jimbo ni kusaidia miradi ya afya, elimu pamoja na utawala mara baada ya kufanyika upembuzi yakinifu na kubaini mahitaji ya vifaa kwenye miradi iliyoibuliwa na wananchi na ambayo ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji.

Kwa mwaka huu wa fedha 2018/2019 mfuko wa jimbo umefanikiwa kufanya jambo la upekee katika sekta ya elimu tofauti na vipindi vingine jambo ambalo limepokelewa kwa furaha na wanafunzi na uongozi wa Ruhuji shule ya Msingi.

“Kitu cha pekee ambacho Mfuko wa Jimbo umefanya katika mwaka huu wa fedha 2018/2019 ni kusaidia ujenzi wa jiko maalumu katika Shule ya Msingi Ruhuji ambalo litakua linatumia kuni kidogo, na rafiki wa Mazingira lakini pia ununuzi wa sufuria aina ya “Stainless steel”ambayo ni imara na haipati kutu na itatumika kwa muda mrefu. Hii itaonesha njia kwa Shule nyingine za Msingi na Sekondari katika Jimbo la Njombe kwamba jiko bora na sufuria bora liko Ruhuji Shule ya Msingi na wanaweza kufika pale kujifunza.”Alisema Mbunge wa Jimbo la Njombe Kusini Mhe. Mwalongo.
Mbunge wa Njombe mjini Edward Mwalongo(wa kwanza kulia) akikagua ujenzi wa miradi mbalimbali wakati wa ziara ya Kamati ya Mfuko wa Jimbo iliyofanywa kwa lengo la kukagua na kupitisha miradi jimboni kwake.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

RPC ARUSHA AWAPA “TANO” ASKARI WA KIKE, SASA KUBISHA HODI KWENYE “MABOMA”

$
0
0
Na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha
Polisi wanawake mkoa wa Arusha kupitia Mtandao wao (TPF NET) wamepongezwa kutokana na utendaji bora wa kazi zao za kila siku hasa katika suala zima la kudumisha nidhamu na kufanya kazi kwa uaminifu.

Pongezi hizo zimetolewa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACP) Ramadhani Ng’anzi wakati wa kuhitimisha maazimisho ya Siku 16 za kupinga Ukatili yaliyoanza rasmi Novemba, 25 mwaka huu.  Kamanda Ng’anzi alisema kwamba, askari wa kike wamekuwa mstari wa mbele katika kuwahudumia wananchi lakini pia kudumisha nidhamu kwa kiwango cha hali ya juu katika utendaji wao wa kazi.

“Natoa pongezi kwa viongozi wenu wa TPF NET kwa kuwasimamia vyema na kuwaweka kwenye mstari mnyoofu na wale ambao walikuwa na dalili za kwenda kinyume na kazi walirudishwa kwenye njia kuu”. Alisema Kamanda Ng’anzi.

Alisema ubora wao wa utendaji kazi umekuwa kivutio kwa baadhi ya taasisi na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali mkoani hapa ambapo wamekuwa wakifanya kazi pamoja nao hasa katika Madawati ya Kijinsia na Watoto kupitia harakati za kupinga ukatili na unyanyasaji na kuahidi kujenga ofisi kubwa ya Dawati mkoa itakayotoa nafasi ya faragha kwa wateja.
 Kaimu Mwenyekiti wa Mtandao wa askari wanawake (TPF NET) mkoa wa Arusha Mrakibu Msaidizi wa Polisi Edith Makweli akikabidhi vifaa vya usafi kwa wafanyakazi wa hospitali ya rufaa ya Mount Meru wakati wa maazimisho ya siku 16 za kupinga ukatili yaliyofanyika mkoani hapa.
 Baadhi ya askari wa kike mkoa wa Arusha ambao ni wanachama wa TPF NET mkoa wa Arusha wakijiandaa kugawa Khanga kwa wagonjwa waliolazwa katika moja ya wodi wa wazazi iliyopo hospitali ya rufaa ya Mount Meru wakati wa maazimisho ya siku 16 za kupinga ukatili
Kaimu Mwenyekiti wa Mtandao wa Polisi wanawake mkoani Arusha Mrakibu Msaidizi wa Polisi Edith Makweli akimsalimia mtoto aliyelazwa katika hospitali ya rufaa ya Mount Meru pamoja na kumpa zawadi wakati wa maazimisho ya siku 16 za kupinga ukatili yaliyofanyika jana.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

DK. MABODI AKABIDHI TREKTA KIJIJI CHA BUMBWISUDI

$
0
0
NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimesema kinaendelea kuimarisha upatikanaji wa huduma bora za Pembejeo za kilimo katika maeneo mbali mbali nchini. Hayo ameyasema Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla 'Mabodi katika hafla ya kukabidhi Trekta moja lililonunuliwa na Mwakilishi wa Jimbo hilo Machano Othman Said kwa ajili ya wakulima wa kijiji cha Bumbwisudi kilichopo Wilaya Magharibi "A' Unguja.

Dk.Mabodi ameeleza kuwa hatua hiyo ya kuwapatia Pembejeo za kilimo wakulima zitarahisisha shughuli za kilimo, kwani mazao yatapandwa kwa muda mwafaka na kupatikana mavuno mengi. Kupitia hafla hiyo Dk.Mabodi amewapongeza Mbunge wa Jimbo la Mfenesini Mhe.Mhe.Col.Mstaafu Masoud Khamis pamoja na Mwakilishi wa Jimbo hilo Mhe. Machano Othman Said kwa utendaji wao mzuri wa kutatua kwa wakati changamoto zinazowakabili wananchi.

Aliwambia Viongozi wa Majimbo mengine kuiga utendaji huo wa viongozi wa Jimbo la Mfenesini kwani wameendelea kutekeleza kwa ufanisi Ilani ya CCM ya mwaka 2015/2020, kwa nia ya kutimiza ahadi walizotoa kwa wapiga kura wao katika Uchaguzi Mkuu uliopita. Aidha aliwataka wananchi wa vijiji mbali mbali vilivyomo katika Jimbo hilo na Majimbo jirani walitumie vizuri Trekta hilo ili lidumu kwa muda mrefu na kulima mashamba mengi ya wakulima.
 BAADHI ya Wana CCM na wananchi waliohudhuria katika hafla ya kukabidhi Trekta moja lililonunuliwa na Mwakilishi wa Jimbo hilo Machano Othman Said kwa ajili ya wakulima wa kijiji cha Bumbwisudi kilichopo Wilaya Magharibi "A' Unguja.
 MBUNGE wa Jimbo la Mfenesini Col.mstaafu Masoud Khamis akizungumza na wana CCM pamoja na wananchi kwa ujumla hafla ya kukabidhi Trekta moja lililonunuliwa na Mwakilishi wa Jimbo hilo Machano Othman Said kwa ajili ya wakulima wa kijiji cha Bumbwisudi kilichopo Wilaya Magharibi "A' Unguja.
 MWAKILISHI wa Jimbo la Mfenesini Mhe.Machano Othman Said akizungumzia maendeleo yaliyopatikana katika Jimbo hilo hafla ya kukabidhi Trekta moja lililonunuliwa na Mwakilishi wa Jimbo hilo Machano Othman Said kwa ajili ya wakulima wa kijiji cha Bumbwisudi kilichopo Wilaya Magharibi "A' Unguja.
 MWENYEKITI wa Mkoa Mjini Magharibi Talib Ali Talib akizungumza katika hafla ya kukabidhi Trekta moja lililonunuliwa na Mwakilishi wa Jimbo hilo Machano Othman Said kwa ajili ya wakulima wa kijiji cha Bumbwisudi kilichopo Wilaya Magharibi "A' Unguja.
NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk. Abdulla Juma Mabodi akizungumza na wananchi mbali mbali waliohudhuria katika mkutano hafla ya kukabidhi Trekta moja lililonunuliwa na Mwakilishi wa Jimbo hilo Machano Othman Said kwa ajili ya wakulima wa kijiji cha Bumbwisudi kilichopo Wilaya Magharibi "A' Unguja.
 
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

MKULIMA WA MIHOGO ASHINDA MILIONI 10 KUTOKA CBA

$
0
0
Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii
BENKI ya Commercial Bank of Africa (CBA) kwa kushirikiana na kampuni ya simu ya Vodacom wamekamilisha rasmi leo kampeni yao  "Shinda na M pawa"  kwa kutangaza washindi watano waliojishindia bajaji na mshindi mkuu wa droo hiyo akijishindia pesa taslimu kiasi cha shilingi milioni 10.

Akimwakilisha Mkurugenzi mtendaji wa benki ya CBA Hakim Sheikh amesema kuwa benki hiyo inaendelea kutimiza ahadi kwa wateja wake kwa kuwazadia washiriki wote walioshiriki katika droo zote zilizofanyika.

Hakim amesema kuwa, "Kampeni hii imetupa fursa kubwa ya kuwahamasisha wateja wetu hasa kwa kujiwekea utamaduni wa kujiwekea akiba na tunawahimiza watanzania ambao bado hawajajiunga na benki ya CBA kujiunga na benki yetu ili waweze kufaidika na fursa mbalimbali zinazotolewa na benki ya CBA" ameeleza Hakim.

Hakim amesema kuwa benki yao itaendelea kutumia teknolojia katika katika kuhakikisha wanawafikia watanzania zaidi na kuongeza idadi ya wateja zaidi ya milioni 7 waliopo sasa.

Aidha amewapongeza washindi waliopatikana kwenye droo hiyo ya mwisho na kuahidi kudumisha  na kuboresha huduma yao na amewaomba watanzania waendelee kutumia huduma kutoka benki ya CBA.
 Mwakilishi wa Mkurugenzi wa benki ya CBA Hakim Sheikh akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kuchezesha droo ya mwisho ambapo tangu kuanza kwa kuchezeshwa kwa droo hiyo jumla ya washindi 200 kwa kila droo wamepatikana.
Meneja masoko wa Kampuni ya simu ya Vodacom, Noel Mazoya akizungumza  na waandishi wa habari mara baada ya kuchezeshwa kwa droo hiyo ambapo ameipongeza benki ya CBA kwa kuendesha  shindano hilo kwa uadilifu.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

‘Umuhimu Wako’ ya Monalisa na Rose Ndauka ni leo kwenye ST Swahili

$
0
0
 Wakati msimu wa Siku Kuu ukiwa unazidi kunoga, StarTimes kupitia chaneli yao ya ST Swahili wanazidi kuirudisha Bongo Movie kwenye ramani kwa kuonyesha filamu hizo kipindi hiki cha Siku kuu. 
Filamu hizi za kibongo zimeanza kuonyeshwa wiki iliyopita ikiwa ni katika jitihada za makusudi za kuiweka Bongo Movie katika chati nzuri na kutazamwa na watanzania wengi wanaopenda kufatilia maudhui ya nyumbani, pia kwa nchi za jirani.
Alhamisi hii saa 3:40 Usiku kupitia ST Swahili channel filamu ya ‘Umuhimu Wako’ inayowakutanisha Rose Ndauka, Yvonne Cherry (Monalisa) na Mama Natasha (Natashamamvi) itakuwa ikiruka kwa mara ya kwanza.Filamu hiyo inahusu binti mmoja na kijana wa kiume lakini kila mmoja wao ana safari na historia tofauti ambayo ameipitia maishani mwake. Kijana anapata misukosuko akijaribu kusimama tena baada ya mkewe kufariki na kumuachia watoto wawili. 


Upande mwingine; binti anakumbana na changamoto kwa baba yake mzazi ambaye anamuona binti huyo kama muhuni. Wawili hawa wanaingia katika mahusiano na huku wakikabiliana na changamoto zao. Baadaye wanatulia baada ya majirani zao kuwasaidia, wanaoana na kuishi maisha ya furaha.
Filamu nyingine zitakazoruka wikendi hii kupitia StarTimes Swahili ni ‘Mjerumani’ siku ya Ijumaa na ‘Milioni 10’ siku ya Jumamosi, filamu hizi za vichekesho zimesheheni mastaa wa Komedi kama vile Ringo na Mau Fundi.

Burudani hii ya kipekee inapatikana katika kifurushi cha NYOTA ambacho mteja atalipia Tsh 8000 tu kwa upande wa Antenaa ama Tsh 11,000 kwa upande wa Dish. Msimu huu wa Siku Kuu mteja atakapolipia kifurushi cha mwezi mzima atapata kifurushi cha juu zaidi na LIPA TUKUBUSTI.

Viewing all 110171 articles
Browse latest View live




Latest Images