Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110181 articles
Browse latest View live

VIONGOZI OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA WATEMBELEA MJI WA SERIKALI JIJINI DODOMA

$
0
0


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George Mkuchika (Mb) na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) wakionyeshwa ramani ya ofisi na Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro inayojengwa katika mji wa Serikali Ihumwa jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George Mkuchika (Mb) na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) wakionyeshwa mipaka ya kiwanja na Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro ya eneo linalojengwa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora katika mji wa Serikali Ihumwa jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George Mkuchika (Mb) na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakipewa maelezo kuhusu ujenzi wa ofisi na Msanifu Majengo wa TBA, Bw. Kileo Yusuph wakati viongozi hao walipotembelea mji wa Serikali Ihumwa jijini Dodoma kujionea maendeleo ya ujenzi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George Mkuchika (Mb) na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakiangalia msingi uliochimbwa kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora katika mji wa Serikali Ihumwa jijini Dodoma mara baada ya kutembelea eneo hilo ili kujionea maendeleo ya ujenzi wa ofisi.

Mkufunzi kutoka Japan kushuhudia ‘Ngorongoro National Athletics Open Championship’

$
0
0

MKUFUNZI wa Riadha kutoka Japan, Ayane Sato, anatarajiwa kushuhudia Mashindano ya Riadha ya Taifa ya Wazi ya Ngorongoro ‘Ngorongoro National Athletics Open Championship 2018’ yanayotarajiwa kurindima Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid Kaluta jijini Arusha, Ijumaa Desemba 14 mwaka huu.

Kwa mujibu wa Katibu Mkuu Msaidizi wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Ombeni Zavala, mkufunzi huyo ambaye yuko nchini kwa miaka miwili akijitolea, atashuhudia mashindano hayo ikiwa ni sehemu ya majukumu yake ya kikazi, ikiwamo kuwanoa wanariadha mbalimbali hapa nchini.Zavala, alisema itakuwa ni fursa pekee kwa Sato kujionea vipaji mbalimbali vya wanariadha kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania bara na Visiwani, jambo litakalomrahishia majukumu yake.

Ujio wa Sato ni kutokana na mahusiano mazuri kati ya Serikali ya Japan kupitia Shirika lake la Kimataifa la Maendeleo (JICA), na RT.Mashindano ya wazi ya Taifa ambayo yamewezeshwa na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA), yatashirikisha mbio za Mita 100, Relay 100×4, 200, 400, Relay 400×4, 800, 1,500, 5,000 na Mita 10,000, Kuruka Juu, Kuruka Chini, Miruko Mitatu, Kurusha Mkuki, Tufe na Kisahani kwa wanaume na wanawake.

Washindi watakaofanya vizuri watazawadiwa zawadi za fedha na medali, ambako mshindi wa kwanza atapata Medali ya Dhahabu na kitita cha Sh. 150,000 wa pili Medali ya Fedha na Sh. 100,000 huku wa tatu akiondoka na Medali ya Shaba na Sh. 50,000.Pia watapata fursa ya kushiriki mashindano mbalimbali ndani na nje ya nchi ikiwamo Japan, kusaka viwango vya kufuzu mashindano ya kimataifa ikiwamo World Championship na Olimpiki.

Sato katikati siku akitambulishwa kwa waandishi wa habari. Kulia kwake ni Katibu Msaidizi RT, Ombeni Zavala na Mjumbe RT, Tullo Chambo
 

NITAENDELEA KUFANYA ZIARA ZA KUSHTUKIZA KATIKA HOSPITALI NA VITUO VYA AFYA NYAKATI ZA USIKU MPAKA HUDUMA ZIIMARIKE - DC MURO

$
0
0
Na Imma Msumba Arumeru

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Jerry Muro amefanya ziara ya kustukiza usiku wa manane katika Hospitali mbili za Wilaya na kujionea hali ya utoaji wa huduma za Afya nyakati za Usiku , ziara ambayo alianza saa Saba na nusu Usiku mpaka saa kumi na moja alfajiri.

Hatua ya Mhe Muro kufanya ziara ya kushtukiza nyakati za Usiku katika hospitali imekuja Kutokana na kuwepo Kwa malalamiko kutoka kwa baadhi ya wananchi ambao wameonyeshwa kukerwa na huduma duni za Afya zinazotolewa nyakati za Usiku ikiwemo kutokuwepo Kwa wataalamu katika maeneo yao ya kazi kama inavyotakiwa Kwa mujibu wa sheria, Kanuni na taratibu.

Akiwa katika Hospitali ya Halmashauri ya wilaya (ARUSHA DC) Hospitali ya Oltrumet Mhe. Muro Alifika katika Eneo la mapokezi ambalo mbali na milango kuwa wazi pamoja na nyaraka na baadhi ya Madawa na vifaa tiba lakini hapakuwa na mtu yoyote katika eneo hilo na badala yake kazi ya mapokezi aliachiwa Askari mgambo anaelinda hospitali hiyo ambapo huwapokea wagonjwa na kisha kwenda KUWAAMSHA WAHUSIKA AMBAO MUDA MWINGI WANAKUWA Wamelala tukio ambalo limeshuhudiwa na Mhe Muro ambae alilazimika kwenda katika Hospitali hiyo akiwa na Usafiri Binafsi wa pikipiki na gari lingine la kawaida moja.

Pia Dc Muro alitembelea katika jengo la upasuaji na kukuta tukio la kukera ambapo wauguzi na wahusika wa chumba hicho walikuwa wamelala uku wamejifunika mablanketi hatua iliyomlazimu Mhe Muro kuwaamsha jambo ambalo liliwafanya wakimbie wakihisi wamevamiwa na Mzimu.

Pamoja na kuwepo Kwa changamoto hizo, Mhe Jerry Muro alioonyeshwa kufurahishwa na kitendo Cha muuguzi wa zamu katika jengo la kujifungulia kina mama ambae mbali na kuwa mwenyewe lakini alikuwa akitimiza wajibu wake wa kuendelea kuwahudumia kina mama ambao baadhi walikuwa katika hatua za kujifungua.
 Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe Jerry Muro Akizungumza na Waaguzi walikuwa zamu katika hospital ya Halmashauri ya Meru ( Tengeru) baada ya kufanya ziara yake ya kushtukiza usiku wa manane katika hospital hiyo.
 Dc Muro Akizungumza na moja ya wagonjwa walikuwa wamelazwa katika hospital ya Halmashauri ya Arusha Dc ( Oltrument) usiku wa kuamkia leo

 Dc Muro akipakua moja ya Nyaraka za Hospital ya Halmashauri ya Arusha Dc ( Oltrument ) alipozikuta katika chumba cha mapokezi kilichokuwa wazi na hapakuwa na mhudumu kwa muda huo.

Tutaendelea Kuunga Mkono Juhudi za Rais Magufuli Kulinda Utamaduni Wetu – Waziri Mwakyembe

$
0
0


Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bibi Susan Mlawi akimkabidhi Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe kwa niaba ya Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli zawadi ya Kamusi Kuu ya Kiswahili iliyotolewa na Baraza la Kiswahili Tanzania (Bakita) wakati wa Kilele cha Kampeni za Uzalendo na Utaifa mwaka 2018 leo jijini Dodoma. Kauli mbiu ya Kampeni hizo kwa mwaka huu ni ” Kiswali Utashi Wetu, Uhai Wetu”. Anayeshuhudia ni Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Juliana Shonza.
UZ3b
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa CD za makala ya uzalendo wakati wa hafla za Kilele cha Kampeni za Uzalendo na Utaifa mwaka 2018 leo jijini Dodoma. Kutoka kulia ni Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Juliana Shonza na Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bibi Susan Mlawi. Kauli mbiu ya Kampeni hizo kwa mwaka huu ni ” Kiswali Utashi Wetu, Uhai Wetu”.
UZ3c
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) akiwa pamoja na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Juliana Shonza (kulia) na Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bibi Susan Mlawi wakionyesha CD za makala ya uzalendo mara baada ya kuzinduliwa rasmi wakati wa hafla za Kilele cha Kampeni za Uzalendo na Utaifa mwaka 2018 leo jijini Dodoma. Kutoka kulia ni. Kauli mbiu ya Kampeni hizo kwa mwaka huu ni ” Kiswali Utashi Wetu, Uhai Wetu”.
UZ3d
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi Kitabu cha Uzalendo wakati wa hafla za Kilele cha Kampeni za Uzalendo na Utaifa mwaka 2018 leo jijini Dodoma. Kutoka kulia ni Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Juliana Shonza na Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bibi Susan Mlawi. Kauli mbiu ya Kampeni hizo kwa mwaka huu ni ” Kiswali Utashi Wetu, Uhai Wetu”.
 Waziri wa Nchi Ofis ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora. Kapteni Msaafu George Mkuchika akimkabidhi Tuzo, Bw.Vita Kawawa aliyeambatana na mwanafamilia mwenzake Bibi. Zamaradi Kawawa kwa niaba ya Waziri Mkuu wa zamani Hayati Rashid Mfaume Kawawa ikiwa ni kuthamini mchango wake katika kukuza lugha ya Kiswahili kupitia sanaa ya maonesha na michezo ya kuigiza wakati wa hafla ya kilele cha Kamapeni ya Uzalendo na Utaifa leo jijini Dodoma. Kutoka kushoto ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Juliana Shonza.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>

10 WAFANYIWA UPASUAJI WA KICHWA + MGONGO KWA MAFANIKIO BUGANDO

$
0
0


NA:- GSENGOtV

Wagonjwa 10 wenye tatizo katika ubongo na mishipa ya fahamu na mgongo wamefanyiwa upasuaji na kukamilika salama katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando jijini Mwanza.

Upasuaji huo unafanywa na daktari bingwa wa mifupa kutoka Marekani kwa kushirikiana na madaktari bingwa wa hospitali hiyo.

Akizungumza mwishoni mwa wiki wakati upasuaji huo ukiendelea hospitalini hapo, Daktari bingwa wa upasuaji Isidory Ngayomela, amesema hatua hiyo inalenga kutatua changamoto za upasuaji.

Ameongeza kuwa mpaka hapo walipofika wamefanikiwa kufanya upasuaji kwa watu 10 wale waliopata ajali na kuumia kichwani pamoja na mgongo kupinda kutokana na uzee.
Kwa upande wake daktari bingwa wa upasuaji kutoka Saint Francis Hospital and Medical Centre ya Hartford nchini Marekani, Dr. Christopher Comey (kulia katika picha juu akiwa na mwanahabari Albert G. Sengo wa Jembe Fm Mwanza) amesema tangu awasili Bugando ikiwa ni wiki moja sasa, wameshafanya upasuaji kwa wagonjwa 10 zikiwemo oparesheni mbili za ubongo.

"Mara kwa mara nimekuwa nakuja nchini Tanzania, kwaajili ya kutoa huduma ya kujitolea lakini safari hii nimeamua kutoa na mafunzo kupitia ujuzi niliona kwa madaktari wa hapa ili huduma ziendelee na hata kama sipo watu wasiendelee kutaabika"

Comey amewasifia madaktari wa Bugando akisema "Pamoja na changamoto ya uhaba wa vifaa na miundombinu mingine nafurahi kuona madaktari wa Bugando wakichapa kazi kwa bidii maarifa na weredi wa hali ya juu huku wakizingatia kile ninachowafundisha"

Waziri Kakunda Atoa Maagizo Mazito Mtwara

KAIMU MTENDAJI MKUU TEMESA AFANYA ZIARA MIKOA YA DODOMA, SHINYANGA NA SIMIYU

$
0
0

Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle kushoto akitoa maagizo kwa Meneja wa Temesa mkoa wa Shinyanga Mhandisi Margareth Mapela wakati wa ziara yake ya kukagua karakana ya wakala mkoani humo.
Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle kulia akikagua mojawapo ya mtambo wa kuchongea vipuri vya mashine mbalimbali katika karakana ya Temesa mkoa wa Shinyanga wakati wa ziara yake mkoani humo, watatu kulia ni Meneja wa TEMESA mkoani humo Mhandisi Margareth Mapela.
Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle kushoto akimpa maelekezo Kaimu Mkurugenzi wa Uzalishaji na Matengenezo wa wakala huo Mhandisi Sylvester Simfukwe wakati akikagua karakana ya Temesa mkoani Dodoma.
Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle kulia akikagua mojawapo ya kilainishi kinachotumika katika injini za magari wakati akikagua chumba cha kuhifadhia vipuri na mafuta ya vilainishi vya magari katika karakana ya wakala mkoani Dodoma. Kushoto ni Meneja wa Temesa mkoani Dodoma Mhandisi Liberatus Bikulamchi.
Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle kushoto akiwapa maagizo viongozi waandamizi wa wakala huo mkoani Shinyanga wakati akikagua baadhi ya mitambo katika karakana hiyo, kulia ni Meneja TEMESA wa mkoa Mhandisi Margareth Mapela.

MAGAZETI YA LEO JMATATU DESEMBA 10 ,2018


MNEC RATCO AKEMEA MAKUNDI,MIGOGORO KWA WANA CCM WILAYANI HANDENI

$
0
0
MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi Taifa Mkoani Tanga (MNEC) Mohamed Salim alimaarufu Ratco amewataka wanachama wa chama hicho wajiepushe na migogoro, makundi na majungu yasiyokuwa na tija kwa ustawi wa chama chao kwani yanaweza kusababisha mpasuko miongoni mwao.

Salim alitoa wito huo wakati wa ziara yake ya kujitambulisha na kuzungumza na wajumbe katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi wilaya ya Handeni ambapo alisema kwa sasa wanachama hao wanatakiwa kubadilika na kutokuipa nafasi kwani inaweza kurudisha nyuma maendeleo.

Alisema suala hilo limekuwa likimuumiza sana huku akiwataka wanachama kuhakikisha wanaachana nayo ili waweze kuunganisha nguvu za pamoja katika kukijenga chama chao ili kiendelee kuwa imara na kuendelea kuwatumikia watanzania.

“Ndugu zangu labda niwaambie kwamba mimi naumizwa sana na migogoro ambayo imekuwa ikijitokeza kwani haina tija kwa ustawi wa chama chetu na inaweza kutugawa sisi hivyo niwatake msiipe nafasi kwenye maeneo yenu tuungane kwa pamoja tushirikiana kwa lengo la kuhakikisha haipewi nafasi “Alisema Mnec huyo.
MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi Taifa Mkoani Tanga (MNEC) Mohamed Salim alimaarufu Ratco akizungumza na wajumbe cha Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi wilaya ya Handeni wakati wa ziara yake ya kujitambulisha ambapo alisisitiza umoja na mshikamano itakayofanyika mkoa mzima wa Tanga.
Mjumbe wa Halmashauri ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Mwalimu Mwantumu Zodo akizungumza wakati wa ziara hiyo kulia niMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi Taifa Mkoani Tanga (MNEC) Mohamed Salim alimaarufu Ratco kushoto ni Katibu wa UVCCM Mkoa wa Tanga Zawadi Nyambo 
MKUU wa wilaya ya Handeni Mkoani Tanga Godwin Gondwe akizungumza wakati wa ziara hiyo.
Sehemu ya wanachama wa CCM wilayani Handeni wakimsikiliza MNEC 
MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi Taifa Mkoani Tanga (MNEC) Mohamed Salim alimaarufu Ratco katiati akiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kikao hicho kushoto ni Mjumbe wa Halmashauri ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Mwalimu Mwantumu Zodo kulia ni Katibu wa CCM wilaya ya Handeni Salehe Kikweo.

RITA YAIBUKA MSHINDI WAKALA BORA WA SERIKALI KWA KUANDAA NA KUWASILISHA TAARIFA ZA FEDHA ZENYE KIWANGO

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii 

Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA) imekabidhiwa tuzo kwa kuwa Taasisi katika kundi la Wakala bora ya Serikali ulioandaa na kuwasilisha taarifa za kifedha zenye kiwango cha Kitaifa na Kimataifa kwa mwaka 2017.

Tuzo hizo zimekabidhiwa na Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe.Dkt Ashantu Kijaji  mwishoni mwa wiki Desemba 8, 2018 katika ukumbi wa APC Bunju Jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dk.Ashatu Kijaji akihutubia na kufunga mkutano wa mwaka wa Wahasibu na Wakaguzi wa Mahesabu NBAA, amezitaka taasisi nyingine za Serikali kuiga mifano hiyo kwani awamu hii ya tano chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli inahimiza matumizi sahihi ya fedha za umma ili zitumike katika utoaji wa huduma bora sambamba na kulifikisha Taifa katika uchumi wa Kati wa kilimo na viwanda. 

Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa RITA, Emmy Hudson amesema kuwa kwa tuzo waliopata inawapa moyo katika kuendelea kuchapa kazi kwa katika kuandaa vitabu vya mahesabu kwa viwango vya kitaifa na Kimataifa.

Amesema kuwa ushindi huo ni kutokana na kufanya kazi kwa ushirikiano na wahasibu na ndio matokeo yake taasisi inaibuka na ushindi ambao kila mtu anafurahi.Hudson amesema kuwa hata mwakani watafanya vizuri zaidi kutokana na ushindi huo ambao watu wengine wanakosa.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashatu Kijaji akikabidhi tuzo kwa Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa RITA Bi Emmy Hudson kwa Taasisi yake kuwa Wakala ya Serikali iliyoandaa taarifa bora ya kifedha yenye kiwango cha Kitaifa na Kimataifa kwa mwaka 2017, sherehe za makabidhiano ya tuzo hizo yaliyofanyika katika ukumbi wa APC Bunju Jijini Dar es Salaam. 
Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa RITA Bi Emmy Hudson akionesha tuzo ya kuwa uwa Wakala ya Serikali iliyoandaa taarifa bora ya kifedha yenye kiwango cha Kitaifa na Kimataifa kwa mwaka 2017, sherehe za makabidhiano ya tuzo hizo yaliyofanyika katika ukumbi wa APC Bunju Jijini Dar es Salaam. 
Picha ya pamoja ya wadau waliotunukiwa tuzo katika zinazotolewa na NBAA zilizofanyika katika katika ukumbi wa APC Bunju Jijini Dar es Salaam.

ASASI YA TANZANIA HORTICULTURAL ASSOCIATION(TAHA) YAWAKUTANISHA WAKULIMA NA TAASISI ZA FEDHA ARUSHA

$
0
0
 Afisa Masoko na Mahusiano wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo(TADB),Grace Ngailo(kulia) akimpa maelezo mgeni rasmi, Rais wa taasisi ya Southern African Confederation Agricultural Unions(Sacau),Dk Sinare Yusuf Sinare(kushoto)wakati wa maonesho ya taasisi za fedha kuwakutanisha na wakulima jijini Arusha.
 Rais wa taasisi ya Southern African Confederation Agricultural Unions(Sacau),Dk Sinare Yusuf Sinare(kulia) akisalimiana na maafisa wa Tanzania Horticultural Assocition(Taha) jijini Arusha.
 Wananchi wakiwa kwenye moja ya mabanda ya taasisi mbalimbali za fedha kwaajili ya kupata taarifa za mikopo kwaajili ya kilimo jijini Arusha.
 Wananchi wakiwa kwenye banda la taasisi ya serikali ya PASS inayojishughulisha na utoaji wa mikopo kwaajili ya kilimo nchini wakati wa maonesho ya yaliyoandaliwa na Taha jijini Arusha.
 Meneja Kiongozi wa Benki ya NMB anayeshughulikia Kilimo,Oscar Rwechungura(kushoto) akizungumza na wakulima katika maonesho ya taasisi za fedha yaliyoandaliwa na asasi ya kilimo cha mbogamboga na matunda(Taha) ya jijini Arusha.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA



Taasisi zinazojenga majengo katika mji wa Serikali Dodoma zatakiwa kulipia gharama ya umeme mapema

$
0
0
Taasisi zinazojenga majengo katika mji wa Serikali Dodoma zatakiwa kulipia gharama ya umeme mapema Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani ameziagiza Wizara na Taasisi zilizoanza ujenzi na zilizo katika maandalizi ya ujenzi wa majengo katika Mji wa Serikali jijini Dodoma kuhakikisha kuwa, wanalipia gharama ya kupeleka umeme katika maeneo yao ili kuharakisha shughuli za ujenzi.

Dkt Kalemani ameyasema hayo  wakati alipokuwa akikagua maandalizi ya ujenzi wa Jengo la Wizara ya Nishati katika Mji wa Serikali, Ihumwa jijini Dodoma ambapo aliambatana na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu, Raphael Nombo na Kamati ya Wizara inayosimamia ujenzi huo. Dkt Kalemani amesema kuwa tayari miundombinu ya umeme imeshafika katika eneo hilo kwani Tanesco wameshafunga transfoma inayosambaza umeme katika eneo husika.

Ameeleza kuwa endapo Taasisi hizo zitalipia gharama hizo mapema zitaweza kufanya shughuli za ujenzi, usiku na mchana na hivyo kukamilisha kazi hiyo ndani ya muda uliopangwa. Aidha ametoa agizo kwa Meneja wa TANESCO mkoa wa Dodoma kuhakikisha kuwa, anafahamu mahitaji ya umeme ya eneo hilo la Serikali ili nishati ya umeme isiwe kikwazo cha utekelezaji wa kazi za ujenzi katika eneo hilo.
 Waziri wa Nishati, Dkt Medard  Kalemani (mwenye shati ya bluu) akikagua shughuli za maandalizi ya ujenzi wa jengo la Wizara ya Nishati katika mji wa Serikali wa Ihumwa, jijini Dodoma. Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara ya Nishati, Raphael Nombo, wa Pili kushoto ni Mkurugenzi wa Uendelezaji Milki kutoka NHC, Haikamen Mlekio na wengine ni Kamati inayosimamia  ujenzi ya Wizara ya Nishati.
Waziri wa Nishati, Dkt Medard  Kalemani (wa pili kushoto) akikagua shughuli za maandalizi ya ujenzi wa jengo la Wizara ya Nishati katika mji wa Serikali uliopo Ihumwa, jijini Dodoma. Wengine katika picha ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara ya Nishati, Raphael Nombo, Mkurugenzi wa Uendelezaji Milki kutoka NHC, Haikamen Mlekio na Kamati inayosimamia ujenzi ya Wizara ya Nishati.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

BILIONI 83 ZIMEKWISHALIPWA KWA WAKULIMA 82,835 WA KOROSHO– HASUNGA

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo- Mtwara
Hadi kufikia jana tarehe 9 Disemba 2018 serikali imefanikiwa kuwalipa jumla ya wakulima 82,835 katika Mikoa ya Mtwara, Lindi na Ruvuma. Jumla ya fedha iliyolipwa kwa wakulima hao ambao tayari wamefanyiwa uhakiki ni Bilioni 83 ambapo katika mkoa wa Mtwara wakulima 50,835 wamelipwa mkoa wa Lindi wakulima 22,131 na Mkoa wa Ruvuma ni wakulima 9,445

Hayo yamesemwa na Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) tarehe 9 Disemba 2018 wakati akizungumza kwenye mkutano wa wabanguaji wadogo wa korosho kutoka katika mikoa mitano ya Mtwara, Lindi, Ruvuma, Pwani na Morogoro uliofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa mjini Mtwara.


Aidha, Mhe Hasunga alisema kuwa jumla ya vyama 328 vimefanyiwa uhakiki kati ya vyama 504 vilivyopo katika mikoa ya Mtwara, Lindi na Ruvuma ambapo jumla ya vyama 319 vimekwishalipwa. Vilevile amewatoa hofu wananchi wanaopotoshwa kuwa bado wakulima hawajalipwa kiasi chochote cha fedha huku akisisitiza kuwa wakulima wanalipwa kupitia njia ya benki hivyo wanapaswa kuwa na utamaduni wa kwenda benki.
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) akisisitiza jambo wakati akizungumza kwenye mkutano wa wabanguaji wadogo wa korosho kutoka katika mikoa mitano ya Mtwara, Lindi, Ruvuma, Pwani na Morogoro uliofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa mjini Mtwara tarehe 9 Disemba 2018. (Picha Zote Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo)
Kushoto ni Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe Joseph Kakunda (Mb) wakikagua korosho zikiwa kwenye kifungashio tayari kwa kuingia sokoni wakati akizungumza wa mkutano wa wabanguaji wadogo wa korosho uliofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa mjini Mtwara tarehe 9 Disemba 2018.
Mkutano ukiendelea
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe Joseph Kakunda (Mb) akisisitiza jambo wakati akizungumza kwenye mkutano wa wabanguaji wadogo wa korosho kutoka katika mikoa mitano ya Mtwara, Lindi, Ruvuma, Pwani na Morogoro uliofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa mjini Mtwara tarehe 9 Disemba 2018.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

TUMIENI CHUO CHA ARDHI TABORA KUPIMA MIJI NA VIJIJI VYENU-KABUNDUGURU

$
0
0
Na Tiganya Vincent
HALMASHAURI  za Wilayani Mkoani Tabora zimetakiwa kutumia wataalamu na wanachuo wa Chuo cha Ardhi Tabora ili kuhakikisha vijiji na miji yao inapimwa na kupagwa kwa ajili ya kuwa katika mpango wa matumizi bora ya ardhi. Hatua hiyo itasaidia kuepusha migogoro miongoni mwa wananchi na pia kuwawezesha kutumia maeneo yao kujiletea maendeleo ikiwemo kukopa fedha katika Taasisi mbalimbali zinazotoa mikopo kwa ajili ya shughuli za maendeleo.

Kauli hiyo hiyo imetolewa jana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi  Mathias Kabundunguru wakati wa sherehe za mahafali ya 36 ya Chuo cha Ardhi Tabora.
Alisema Serikali imenunua vifaa mbalimbali vya kisasa kwa ajili ya Chuo hicho ambavyo vinawawezesha wataalamu wachche kupima eneo kubwa kwa muda mfupi na kwa gharama nafuu ukilinganisha ambavyo wangetumia Kampuni binafsi.

Kabundunguru alisema hakuna sababu ya maeneo mbalimbali katika Halmashauri za Mkoa wa Tabora na mikoa jirani kuendelea kujengeka bila mpangilio wakati Chuo kipo karibu. Alisema upimaji wa maeneo ya mijini na vijiji Mkoani humo utasaidia kuwaondoa wananchi kuishi katika maisha magumu na hatarishi kutokana na maeneo yao kutokuwa katika mpangilio.
 Mkuu wa Chuo cha Ardhi Tabora (ARITA) Biseko Musiba(aliyesimama) akitambulisha wageni mbalimbali wakati wa mahafali ya 36 ya Chuo hicho yaliyofanyika jana mjini Tabora.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Ardhi Tabora(ARITA) Profesa Gabriel Kassenga akitoa salamu za Bodi wakati mahafali ya 36 ya  ARITA yaliyofanyika jana.
  Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi  Mathias Kabundunguru akiwahutubia wahitimu wa mahafali ya 36 ya Chuo cha Ardhi Tabora jana.
 Baadhi ya wahitimu wa Chuo cha Ardhi Tabora(ARITA) wakimsikiliza Mgeni rasmi wakati wa mahafali ya 36 ya Chuo hicho yalifanyika jana.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi  Mathias Kabundunguru (mwenye Joho la bluu waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali na wakufunzi wa Chuo cha Ardhi Tabora jana mara baada ya kumalizika kwa mahafali ya 36 Chuo cha Ardhi Tabora yaliyofanyika jana. Picha na Tiganya Vincent

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

BENKI YA AZANIA, WADAU WAKUTANA KUJADILI MAFANIKIO

$
0
0
 Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya Azania , Charles Itembe (kulia) akipongezana na  Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa benki hiyo ambae pia ni Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii ya Watumishi wa Umma (PSSSF) Bw Eliud Sanga wakati wa kikao kifupi  kilichofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dodoma ili kutathmini mwenendo wa benki hiyo  ikiwemo ufunguzi wa tawi lake jipya jijni humo. Mfuko wa PSSSF ni moja ya wanahisa wakubwa wa benki hiyo.
 Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya Azania , Charles Itembe (kulia) akimkabidhi zawadi kwa Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii ya Watumishi wa Umma (PSSSF) Bw Valerian Mablanketi wakati wa kikao kifupi  kilichofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dodoma ili kutathmini mwenendo wa benki hiyo  ikiwemo ufunguzi wa tawi lake jipya jijni humo. Mfuko wa PSSSF ni moja ya wanahisa wakubwa wa benki hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya Azania , Charles Itembe (wa tatu kulia) pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa benki hiyo ambae pia ni Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii ya Watumishi wa Umma (PSSSF) Bw Eliud Sanga (kulia kwake) wakiwa kwenye picha ya pamoja na wafanyakazi waandamizi wa Benki ya Azania pamoja na Mfuko wa PSSSF wakati wa kikao kifupi  mara baada ya kumaliza kikaohicho.

Waziri Kalemani aitaka Tanesco kuhakikisha umeme unapatikana Mji mpya wa Serikali

BoT YAWANOA WAANDISHI WA HABARI KUHUSU HABARI ZA UCHUMI NA FEDHA

$
0
0
*Naibu Gavana ahimiza uwajibikaji kwa waandishi wa habari nchini

Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

BENKI Kuu ya Tanzania(BoT) ,imesema imeamua kuanzisha utaratibu wa kuendesha semina kwa waandishi wa habari wa vyombo vya habari nchini kwa lengo la kukuza uandishi wa habari za uchumi na fedha.

Pia lengo la semina hiyo kwa waandishi wa habari nchini ni kuelimisha na kufafanua masuala yanayohusu majukumu na kazi za Benki Kuu , kujenga uwezo wa kutafsiri na kuchambua taarifa za uchumi na fedha, kuboresha na kudumisha uhusiano mzuri wa kikazoi kati ya vyombo vya habari na BoT.

Malengo mengine ya semina hiyo ni kupata mrejesho kutoka kwa waandishi wa habari kuhusu utendaji wao wa kazi na njia bora ya kudumisha mawasiliano baina ya taasisi zao.
 
Hotuba ya Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) upande wa Uchumi na Sera Dk. Yamungu Kayandabila ambayo imesomwa kwa niaba yake na Mkurugenzi wa Tawi la Benki Kuu Dodoma Richard Wambali amesema benki hiyo inatambua mchango wa vyombo vya habari nchini katika kuufahamisha umma wa Watazanzania na dunia
kwa ujumla.

"Mara kadhaa mmekuwa msaada mkubwa sana katika kutufikishia taarifa zetu kwa umma, na wakati mwingine baada ya kupokea mwito wa muda mfupi.Pia kupitia kazi zenu mnatuwezesha kujua ni nini wananchi wanasema au kutarajia kutoka katika taasisi zetu."Benki Kuu ya Tanzania imekuwa ikiendesha semina kama hii, tumeshuhudia kuimarika kwa uandishi wa habari za uchumi na fedha katika vyombo mbalimbali vya habari.Matokeo haya mema yametupa uthibitisho kwamba mafunzo tunayotoa kwa wadau wetu wakuu yana manufaa makubwa,"amesema.

Mkurugenzi wa Benki Kuu ya Tanzania tawi la Dodoma Bw. Richard Wambali aliyemwakilisha Dkt. Yamungu Kayandabila Naibu Gavana anayeshughulikia Uchumi na Fedha akifungua semina ya siku tano ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali kuhusu masuala ya uchumi na fedha inayofanyika kwenye ukumbi wa (BOT) jijini Dodoma. 

BALOZI WA NORWAY NCHINI AFANYA MAZUNGUMZO NA NAIBU WAZIRI WA NISHATI

$
0
0
Na Veronica Simba - Dodoma
Balozi wa Norway nchini Tanzania, Elisabeth Jacobsen leo Desemba 10, amemtembelea Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu, Makao Makuu ya Wizara jijini Dodoma na kufanya mazungumzo kuhusu fursa mbalimbali za uwekezaji katika sekta ya nishati nchini.

Balozi Jacobsen amemweleza Naibu Waziri kuwa kampuni mbalimbali nchini mwake zina nia ya kuwekeza katika sekta ya nishati nchini na baadhi yake ziko katika hatua nzuri kwani tayari zimewasilisha serikalini mchanganuo wake unaoainisha sifa walizonazo wakisubiri zoezi la kushindanishwa na kampuni nyingine ili kupata zabuni husika za uwekezaji.

“Mojawapo ya kampuni hizo ina nia ya kuwekeza katika uzalishaji wa umeme wa upepo eneo la Makambako, ambapo ni ubia baina yake (52%) na wazawa (48%),” amesema Balozi. Kwa upande wake, Naibu Waziri Mgalu amemshukuru Balozi Jacobsen ambaye ni mwakilishi wa Serikali ya Norway kutokana na ushirikiano ambao nchi hiyo imekuwa ikiuonesha kwa Tanzania ikiwemo uwekezaji nchini na pia kufadhili wanafunzi katika masomo ya fani za gesi na mafuta.

Aidha, amemweleza Balozi huyo kuwa bado zipo fursa nyingi za uwekezaji katika sekta ya nishati nchini na hivyo ametumia fursa hiyo kuendelea kukaribisha kampuni mbalimbali za Norway kuja kuwekeza.
 Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (kulia) akifafanua jambo kwa Balozi wa Norway nchini Tanzania, Elisabeth Jacobsen wakati Balozi huyo alipomtembelea mapema leo, Desemba 10, 2018 ofisini kwake Dodoma, kujadili fursa za uwekezaji katika sekta ya nishati.
 Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Norway nchini Tanzania, Elisabeth Jacobsen baada ya mazungumzo yao kujadili fursa za uwekezaji katika sekta ya nishati mapema leo, Desemba 10, 2018 Makao Makuu ya Wizara jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (kushoto) akiagana na Balozi wa Norway nchini Tanzania, Elisabeth Jacobsen, baada ya mazungumzo yao kujadili fursa za uwekezaji katika sekta ya nishati mapema leo, Desemba 10, 2018 Makao Makuu ya Wizara jijini Dodoma.

Una mpango wa kusafiri? Zingatia haya.

$
0
0

Una mpango wa kusafiri? Zingatia haya

Ni wakati mwingine tena wa msimu wa sikukuu za Krismasi na mapumziko ya mwisho wa mwaka. Katika kipindi hiki tunashuhudia pilikapilika za hapa na pale watu wakijiandaa namna watakavyosherehekea.

Kuna baadhi ya watu wanafikiria kusafiri nje ya mikoa waliyopo kwa ajili ya kusherehekea. Watu wengi wana kawaida ya kusafiri kurudi waliko zaliwa na kukulia ili kujumuika pamoja na ndugu na jamaa zao. Wengine hupanga kwenda kutembelea vivutio vya kutalii kwenye mikoa tofauti na walipo.

Kipindi cha nyuma kidogo usafiri wa umma ndio ulikuwa tegemezi ukilinganisha na sasa ambapo baadhi ya wasafiri wanamiliki usafiri wao binafsi. Kusafiri kwa usafiri binafsi kuna faida lukuki hususani kama mko wengi na wote mnakwenda sehemu moja. Hupunguza gharama lakini mnakuwa huru kuamua msafiri namna gani, muda wa kuondoka na kufika, kupumzika njiani nakadhalika.
Pamoja na faida lukuki za kusafiri kwa kutumia usafiri ubinafsi, yafuatayo ni masuala ya msingi kuyazingatia kabla ya kuanza safari yako.

Jipange mapema. Kabla ya kuanza safari yako hakikisha kuwa chombo chako cha usafiri kipo kwenye hali salama. Hali ya hewa inatofautiana kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine hivyo huna budi kuhakikisha gari lako linakuwa na uwezo wa kuhimili hali yoyote itakayokutana nayo safarini. Wasiliana na fundi wako ambaye huwa analihudumia gari lako mara kwa mara ili kukusaidia katika hili.

Pumzika vya kutosha. Miongoni mwa sababu iliyotajwa kusahaulika kuwa inachochea kutokea kwa ajali nyingi za barabarani ni madereva kutopumzika vya kutosha kabla ya safari. Hivyo basi kama dereva ambaye unatarajia kuendesha chombo cha usafiri kwa umbali mrefu hakikisha kuwa unapata muda wa kutosha kupumzika. Hii itakusaidia mwili kuwa katika hali nzuri na kupelekea umakini mkubwa barabarani.

Kuwa makini na mwendo kasi. Hakuna haja ya kushindana kwa mwendo kasi na madereva wengine barabarani. Zingatia umbali wa kutosha baina yako na chombo kingine cha usafiri ili kuweza kuepuka ajali pindi itakapotokea. Takwimu tofauti duniani zinaonesha kuendesha gari kwa mwendo kasi kunapelekea ajali nyingi, majeruhi wengi na hata vifo zaidi. Unashauriwa kuendesha kwa kuzingatia alama za barabarani.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>

LUGOLA AWAOMBA WANANCHI KUCHANGIA UJENZI VITUO VYA POLISI KUIMARISHA USALAMA NCHINI

$
0
0
Na Felix Mwagara, (MOHA) MARA.
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amewataka Watanzania wawe na utamaduni wa kuchangia ujenzi wa vituo vya polisi kama wanavyochanga katika michango mingine ya maendeleo nchini.

Lugola amesema ni mara chache sana kuona wananchi wanachangia ujenzi wa kituo cha polisi katika maeneo wanayoishi kutokana na baadhi ya Watanzania wanaamini vituo vya polisi ujengwa na serikali pekee jambo ambalo halina msingi la linakwamisha maendeleo ya nchi.

Akizungumza na mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Kibara B, Mwibara, Wilaya ya Bunda, Mkoani Mara, Lugola amesema ili usalama uzidi kuimarishwa katika maeneo mbalimbali nchini, wananchi wanapaswa kushirikiana na Serikali katika ujenzi wa vituo vya polisi.

Lugola alisema katika mikutano yake ya nchi nzima anayoendelea kuifanya, atazidi kuwahamasisha wananchi waweke utamaduni wa kuchangia kwa ajili wa ujenzi wa vituo hivyo ili ulinzi upatikane sehemu mbalimbali nchini na kupunguza au kuyaondoa kabisa matukio ya uhalifiu.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Kibara B, Mwibara, Wilaya ya Bunda, Mkoani Mara, leo.  Lugola aliwaomba wananchi wa kijiji hicho wachangie ujenzi wa kituo vya polisi katika eneo hilo ili kuimarisha ulinzi wa raia na mali zao. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kulia), akimsikiliza Mkazi wa Kijiji cha Sikiro, Kata ya Iramba, Mwibara Wilayani Bunda, Mkoa wa Mara, Elia Majinge alipokua anatoa kero yake katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji hicho, jimboni humo, leo. 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Kibara B, Mwibara, Wilaya ya Bunda, Mkoani Mara, leo.  Lugola aliwaomba wananchi kijijini hapo wachangie ujenzi wa kituo vya polisi ili kuimarisha ulinzi zaidi nchini. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Viewing all 110181 articles
Browse latest View live




Latest Images