Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110175 articles
Browse latest View live

CHANNEL TEN: Habari za Kitaifa Novemba 20, 2018


HOSPITALI YA APOLLO YA INDIA YATOA OFA YA MATIBABU KWA WANAMUZIKI WA TANZANIA

$
0
0
Na Kulwa Mwaibale

Hospitali ya Kimataifa ya Apollo yenye makao makuu yake nchini India, imetoa ofa ya matibabu kwa wanamuziki wa Tanzania.

Akizungumza mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam, kwenye mkutano baina ya wawakilishili wa Hospitali ya Apollo nchini Tanzania pamoja na wanachama wa Umoja wa Wanamuziki Tanzania (TAMUFO), Parwez Audax alisema lengo la kutoa ofa hiyo ni kuhakikisha wanamuziki nchini wanakuwa na afya njema.

Audax alisema, baada ya kubaini watu wengi nchini wanasumbuliwa na maradhi hususan ya uvimbe kwenye kizazi kwa wanawake, tezi dume, saratani ya ini pamoja na magonjwa ya mgongo na uti wa mgongo wameamua kutoa ofa ya matibabu kwa gharama nafuu kwa wanamuziki.

"Kwa kuanzia tumeamua kutoa ofa ya gharama nafuu kwenu wanamuziki kwa watakaojiunga na bima ya afya ya Apollo," alisema mwakilishi huyo.

Naye Dr Sandip Jhala ambaye ni miongoni mwa madaktari bingwa wanaotibu bila kufanya upasuaji wa Hospitali ya Apollo, alisema baada ya kuona watu wengi kutoka nchi za Afrika wanasumbuliwa na uvimbe kwenye kizazi, tezi dume na magonjwa mengine aliamua kuja Afrika kutoa tiba.

"Nilipoona watu wengi kutoka Afrika hususan Tanzania wanakuja kwenye hospitali yetu ya Apollo India kutibiwa niliamua kuja kufanya utafiti kujua ukubwa wa tatizo na kutoa tiba," alisema Jhala.Dr. Jhala alisema matibabu ya kuondoa uvimbe katika kizazi kwa wanawake bila ya kufanya upasuaji hayahitaji nusu kaputi na mgonjwa hutumia siku mbili tu kukaa hospitali na anakuwa na asilimia 33 mpaka 53 ya kupata mtoto.
Daktari Bingwa wa kutibu bila ya kufanya upasuaji kutoka Hospitali ya Apollo, Dr Sandip Jhala akielezea namna wanavyofanya upasuaji wa kuondoa uvimbe kwenye kizazi, tezi dume na magonjwa mengine katika mkutano uliowakutanisha Wanaumoja wa Wanamuziki Tanzani (TAMUFO) pamoja na wawakilishi wa Hospitali ya Apollo hapa nchini mkutano uliofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Rais wa TAMUFO, Dkt. Donald Kisanga akizungumza kwenye mkutano huo.
Mwanamuziki Kasim Salehe Mafanya, akiwa na mwanamuziki wa nyimbo za injili katika mkutano huo.
Viongozi wa TAMUFO na wadau wa muziki wakiwa meza kuu. 
Lina Munisi aliyetolewa uvimbe na Dr.Jhala bila ya kupasuliwa katika Hospilati ya Apollo nchini India akitoa ushuhuda wake kwa wanamuziki.

NAIBU WAZIRI KANYASU AWATOA HOFU WATUMISHI JUU YA MASLAHI YAO BAADA YA UJIO WA JESHI USU

$
0
0
NA LUSUNGU HELELA
Naibu Waziri Wizara ya  Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu amewatoa hofu watumishi wa Taasisi zenye jukumu la kulinda na kuhifadhi Wanyamapori na Misitu nchini kuwa hakuna maslahi yao yatakayobadilika baada ya ujio wa Jeshi Usu

Naibu Waziri Kanyasu ameyasema hayo wakati akizungumza na watumishi wa Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro ikiwa ni mara yake ya kwanza  kukutana na watumishi hao tangu alipoteuliwa  kushika wadhifa wa Naibu Waziri katika Wizara hiyo  nyeti kwa uchumi wa nchi. Amesema ziara yake imelenga kuzifahamu Taasisi  anazoziongoza ili kujua namna zinavyotenda kazi na  changamoto zinazowakabili ili kuzipatia ufumbuzi.

Akizungumza kuhusu utendaji wa Jeshi USU, Naibu Waziri Kanyasu amesema kufuatia mabadiliko ya mfumo wa utendaji kutoka katika mfumo wa kiraia na kuwa Jeshi USU kutakuwa na mabadiliko kiutendaji yatakayoendana na taratibu za Jeshi USU lakini utakaoheshimu na kulinda maslahi ya watumishi.   Naibu Waziri huyo ameeleza kuwa, uanzishwaji wa Jeshi hilo haukusudii kubadili maslahi ya watumishi hao  na endapo maslahi hayo yatabadilika basi yatakuwa na mabadiliko chanya kwao.

Naibu Waziri Kanyasu ameongeza kuwa Jeshi USU litaongeza nidhamu uwajibikaji na maadili kwa watumishi wa sekta ya Maliasili na  Utalii ili waweze kusimamia ipasavyo uhifadhi endelevu wa maliasili na si vinginevyo. Katika hatua nyingine,  Naibu Waziri Kanyasu ameiagiza Menejimenti ya Mamlaka ya  Hifadhi ya eneo la Ngorongoro ibuni  vivutio  vipya vya  Utalii vitakavyosaidia  kuongeza  mapato kwa Serikali kwa kuzingatia majukumu makuu ya Taasisi.
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu (wa pili kushoto) akimsikiliza  Mhifadhi ,kuu  wa Mamlaka ya Hifadhi ya enoe la n Ngorongoro, Dkt.Freddy Manongi  wakati  alipowatembelea jana katika  Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kwa ajili ya kuzungumza na  kuwasikiliza watumishi wa Mamlaka hiyo juu ya changamoto mbalimbali zinazowakabili ili kuweza kuzitafutia ufumbuzi 
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu ( kushoto) akipewa maelezo na Dkt. Maurus Msuha (katikati) wakiwa kwenye sehemu ya kuonea wanyamapori (View point) ya Ngorongoro Kreta wakati alipotembelea jana  kwa ajili ya  kuzungumza na kuwasikiliza watumishi juu ya changamoto mbalimbali zinazowakabili ili kuweza kuzitafutia ufumbuzi
 Watumishi wa Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro wakimsikiliza Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu  wakati alipowatembelea jana.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu  akipewa maelezo na Juma Hamadi jinsi mfumo wa malipo unavyofanya kazi kwa watalii wanaoingia katika  Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro

                       (PICHA NA LUSUNGU HELELA-WMU) 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
  

KAMPUNI SABA KUTOKA NCHINI UTURUKI WAONESHA NIA KUWEKEZA NCHINI,TIC,BALOZI KIONDO WATOA NENO

$
0
0
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

KAMPUNI saba kutoka nchini Uturuki zimekuja nchini Tanzania na kuonesha nia ya kuwekeza katika ujenzi wa maduka makubwa ya nguo, uwekezaji katika sekta ya nishat ya umeme, hoteli zenye hadhi ya nyota tano katika Jiji la Dodoma na uuzaji wa bidhaa.

Ujio wa kampuni hizo ni muendelezo wa jitihada zinazofanywa na Kituo cha Uwekezaji Tanzania(TIC) kwa kushirikiana na wadau katika kuhakikisha wanaendelea kuhamasisha nchi mbalimbali kuja kuwekeza nchini.

Akizungumzia ujio wa Kampuni hizo kutoka nchini Uturuki,Balozi wa Tanzania nchini Uturuki Elizabert Kiondo amesema nchi yetu kwa sasa ipo kimkakati katika kuelekea uchumi wa viwanda na hivyo ujio wa kampuni hizo ambazo zitawekeza n chini zitasaidia kuongeza juhudi kwa vitendo.

Amesema nchi ya Uturuki inatambua hali tulivu ya n chini Tanzania katika masuala ya uwekezaji na hivyo moja ya jukumu ambalo amelifanya ni kuhamasisha kampuni mbalimbali za nchi hiyo zinakuja kuwekeza kwa maslahi ya Watanzania wote."Nchi yetu ipo kwenye mkakati madhubuti wa kuhakikisha tunaimarisha uchumi wetu kupitia viwanda na uwekezaji.Wenzetu wa Uturuki wameelewa tunakoelekea na hivyo sasa wamekubali kuja nchini kuwekeza.

" Hizi kampuni saba ambazo nimekuja nazo zimeonesha nia ya kuwekeza kwenye maduka makubwa ya nguo, kujenga hoteli zenye hadhi ya nyota tano,kushiriki kwenye sekta ya umeme na kuongeza thamani ya bidhaa zitokanazo na kilimo,"amesema Balozi Kiondo.

Amefafanua kuwa kampuni hizo zimeonesha kuamini Tanzania kuna soko la uhakika na kubwa zaidi baada ya kuanza shughuli zao hakutakuwa na sababu ya msingi kusafiri kwenda katika nchi hiyo kupata bidhaa kwani zitapatikana hapa hapa nchini Tanzania.Kwa upande wake Mkurugenzi wa Uhamasishaji Uwekezaji kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC)John Mnali amesisitiza kampuni hizo saba kuonesha nia ya kuwekeza nchini katika nyanja mbalimbali.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO NOVEMBA 21,2018

DC MURO AWAJIA JUU MADIWANI WA CHADEMA KUHUSU FEDHA ZA TASAF

Vikosi kazi vya Baraza la Taifa la Biashara (TNBC) vyazinduliwa rasmi

$
0
0
KATIBU Mkuu Kiongozi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati Tendaji ya Baraza la Taifa la Biashara(TNBC), Balozi John Kijazi amezindua vikundi kazi vya baraza hilo kwa lengo la kujenga na kuimarisha mahusiano kati ya sekta za umma na binafsi katika kuibua changamoto na
kuzijadili kwa mustakabali wa maendeleo ya Tanzania.

Akizungumza mara baada ya uzinduzi wa vikundi kazi hivyo jijini Dar es salaam juzi, Balozi Kijazi alisema madhumuni ya kuunda vikundi kazi hivyo vilivyowajumuisha wataalum katika sekta mbalimbali vitawezesha majadiliano juu ya changamoto zajadiliwe kwa kina zaidi kabla ya
kupelekwa katika ngazi ya Baraza.

“jumla ya vikundi kazi vinne nimevizindua leo (juzi) ikiwa ni pamoja na kikundi kazi cha Mazingira ya Biashara, Viwanda, Misitu na Kilimo vitavyokwenda kuibua changamoto na kuleta mapendekezo yatakayosaidia kuboresha sera na miongozo iliyopo,” alisema Balozi Kijazi. Alisema ushirikiano kati ya sekta binafsi na Sekta ya umma unahitajika sana ili kuweza kuibaini changamoto na kuzijadili na kuja na mapendekezo yatakayo leta tija katika mustakabali wa kujenga uchumi wa
Taifa.

“Serikali itapokea mapendekezo yote yatakayowakilishwa na timu za wataalum kutoka katika vikundi kazi hizi na tutayafanyia kazi mapendekezo yote, zaidi kwa mengine yanayoweza kuchukuliwa na maamuzi kwa ngazi yenu endeleeni lengo ni kupunga majadiliano katika ngazi ya
taifa,” alisema Balozi Kijazi Alisisitiza kuwa mijadala ya vikundi kazi hivi ifanyike kwa uhuru na usawa kwa kutoa hofia cheo cha mtu au mali wote wawekitu kimoja ili majadiliano yaweze kuleta tija na mapendekezo yatakayofanya mazingira ya biashara kuboresheka zaidi.
Katibu Mkuu Kiongozi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati Tendaji ya Baraza la Taifa la Biashara(TNBC) Balozi John Kijazi(kushoto) akisalimia na Kaimu Katibu Mkuu wa TNBC Bi.Oliver Vengula(kulia) mara baada ya kuwasili katika kikao cha uzinduzi wa vikundi kazi vinne vya Baraza hilo jijini Dar es salaam. Wapili kushoto ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania(TPSF) Salum Shamte na wapili kulia ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera na Uratibu, Prof.Faustine Kamuzora
Katibu Mkuu Kiongozi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati Tendaji ya Baraza la Taifa la Biashara(TNBC) Balozi John Kijazi akizungumza jambo na wajumbe wakamati tendaji wakati wa uzinduzi wa vikundi kazi vinne vya Baraza hilo jijini Dar es salaam zitakavyoleta mapendekezo ya kuboresha sera ,sheria na miongozi ili kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara nchini.

TAARIFA

$
0
0
The Economic Society of Tanzania (EST) and Tanzania Private Sector Foundation (TPSF) are organizing  Public Debt Dialogue on the 22nd November 2018 at Ramada Encore from 0730 to 1100. The dialogue aims to share understanding on basic elements of public debt management and debt sustainability.


WAZIRI LUKUVI KUANZA ZIARA NDEFU YA KUSHUGHULIKIA MIGOGORO YA ARDHI NCHINI

$
0
0
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi alhamisi tarehe 22 Novemba 2018 atafanya ziara ya kushughulikia migogoro ya ardhi nchini kwa kuanza kutembelea shamba la Singu na  Endasagu yaliyopo wilaya ya Babati mkoa wa Manyara kwa nia ya kutatua migogoro katika mashamba hayo baina ya wamiliki na wananchi.

Uamuzi wa Lukuvi kufanya ziara katika mashamba hayo ni moja ya jitihada zake za kushughulikia migogoro ya ardhi kutokana na uwepo kero na malalamiko mengi kutoka kwa wananchi kuhusiana na huduma za ardhi.

Akiwa wilayani Babati, Lukuvi atakagua mashamba ya Singu na Endasagu sambamba na kusikiliza malalamiko ya wananchi kuhusiana na mashamba hayo na baadaye kutafuta ufumbuzi.

Aidha, katika mfululizo  wa kushughulikia migogoro ya ardhi, Lukuvi mara baada ya kurejea kutoka mkoani Manyara atafanya ziara katika halmashauri zote za mkoa Dar es Salaam,Wilaya za Kinondoni, Ilala, Kigamboni, Ubungo na Temeke ambapo mbali na mambo mengine atakagua na kuhamasisha zoezi la urasimishaji ambalo limeonekana kuwa na changamoto katika baadhi ya maeneo.

Vile vile, katika kuhakikisha migogoro ya ardhi inapungua nchini Waziri Lukuvi mwanzoni mwa mwezi Desemba  atakuwa na ziara ndefu itakayohusisha mikoa ya Songwe, Mbeya, Njombe, Iringa na Pwani ambapo wananchi watapata fursa ya kuwasilisha kero za ardhi kupitia programu ya Funguka kwa waziri.

Ziara hiyo ya Waziri Lukuvi ni muendelezo wa ziara zake za kushughulikia migogoro ya ardhi na hivi karibuni alikuwa mkoani Kilimanjaro ambapo aliweza kutatua migogoro ya ardhi ikiwemo ya mashamba makubwa katika wilaya za Hai, Moshi na Same.

HESLB YAANZA KUPOKEA RUFAA ZA MIKOPO KWA 2018-2019

$
0
0

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) inawafahamisha wanafunzi wote wa taasisi za elimu ya juu kuwa leo, Jumatano, Novemba 21, 2018 imeanza kupokea rufaa za mikopo kwa mwaka wa masomo 2018/2019 kwa kwa njia ya mtandao.

Dirisha la kuwasilisha rufaa hizo litakuwa wazi kwa siku tano, kuanzia leo hadi Jumapili, Novemba 25, 2018 na linapatikana kupitia http.olas.heslb.go.tz. Wanafunzi watakaokua wametimiza masharti na sifa watapangiwa mikopo kabla ya mwisho wa mwezi huu wa Novemba, 2018.

HESLB imefungua dirisha hili ili kutoa fursa kwa wanafunzi wahitaji ambao hadi sasa hawajapata mkopo au hawajaridhika na kiwango cha mkopo walichopangiwa, kuwasilisha maelezo na nyaraka kuthibitisha uhitaji wao. Maelekezo ya kina kuhusu namna ya kuwasilisha na nyaraka zinazohitajika yanapatikana kwenye mtandao (http.olas.heslb.go.tz).

Ili kuwasilisha taarifa na nyaraka zake za rufaa, mwanafunzi anapaswa kufungua mtandao huo, kusoma maelekezo na kutumia namba yake ya mtihani wa kidato cha nne aliyoombea mkopo kwa mwaka huu (2018/2019) kuingia na kuwasilisha taarifa zake kwa njia ya mtandao tu.

Hadi leo (Jumatano, Novemba 21, 2018), jumla ya wanafunzi 37,969 wa mwaka wa kwanza wamepangiwa mikopo na wanaendelea na masomo katika taasisi mbalimbali za elimu ya juu nchini.

Katika mwaka huu wa masomo, Serikali imetenga TZS 427.5 bilioni kwa ajili ya mikopo ya elimu ya juu ambazo zitawanufaisha wanafunzi zaidi ya wanafunzi 120,000wakiwemo 83,000 wa mwaka wa pili, tatu na kuendelea waliopo vyuoni ambao wamefaulu mitihani yao ya mwaka.

Imetolewa na:
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu
DAR ES SALAAM
JUMATANO, NOVEMBA 21, 2018

Introducing "FAKE PROMISE" by Crevor Designer Ft Mr Blue Fake Promise

Public Debt Dialogue on public debt management and sustainability

$
0
0

The Economic Society of Tanzania (EST) and Tanzania Private Sector Foundation (TPSF) are organizing a Public Debt Dialogue on the 22nd November 2018 at Ramada Encore (5th Floor, Ghana Avenue, opposite Exim Towers near posta mpya) from 0730am to 1100am. The dialogue aims to share understanding on public debt management and sustainability.

IPP Automobile Ltd kuanzisha kiwanda cha kuunganisha magari ya Korea Kusini

$
0
0
KAMPUNI ya IPP Automobile Ltd imeingia ubia na Kampuni ya Youngsan ya Korea kusini kuwekeza katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi kwa kuwa na kiwanda cha kuunganisha magari nchini.
Gari la mwanzo kutoka katika uwekezaji huo wa zaidi bilioni 22, litaingia sokoni kati ya Septemba na Oktoba mwaka 2019.
Kiwanda hicho kinachotarajiwa kuunganisha magari 1000 kwa mwaka kitatoa ajira za moja kwa moja kwa wananchi 500, idadi inayotarajiwa kuongezeka kadri ya muda unavyokwenda.
Kiwanda hicho kitajengwa eneo la Kurasini, ujenzi utaanza mwanzoni mwa mwaka ujao.
Makubaliano ya uanzishwaji wa kiwanda hicho yalitiwa saini jijini Dar es Salaam jana kati ya Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Dk. Reginald Mengi na Bw Thomas Choi Mkurugenzi na Mwakilishi wa Kampuni ya Youngsan Glonet ya Korea ambao ndio wawakilishi wa kiufundi wa kampuni ya Zyle Daewoo Commercial Vehicle na Hyundai Motor Corporation ya Korea Kusini huku tukio hilo likishuhudiwa na Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini, Song Geum-young .
Katika mazungumzo wawakilishi hao na balozi walisema kuanzishwa kwa kiwanda hicho, kumelenga kuunga mkono juhudi za maendeleo nchini.
Akizungumzia hatua hiyo, Mwenyekiti Mtendaji  wa IPP,Dk. Reginald Mengi alisema kuanzishwa kwa kiwanda hicho, ilikuwa moja ya ndoto zake kama hatua ya kuitikia mwito wa Serikali ya Awamu ya Tano ya Rais John Magufuli, inayosisitiza kasi ya ujenzi wa viwanda nchini.
“Hakuna kinachoshindikana ukiwa na nia, hata Rais wetu anapambana katika mambo ambayo wengi waliona yanashindikana, amenunua ndege na  kufanya mengine mengi..hii ni hatua kubwa katika kukuza maendeleo yetu,” alisema Dk. Mengi.
 Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Dk. Reginald Mengi akizungumza katika hafla fupi ya kutiliana saini hati ya makubaliano ya kuanzishwa kwa mradi kuunganisha magari hapa nchini iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi za IPP jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi na Mwakilishi wa Kampuni ya Youngsan Glonet ya Korea, Bw. Thomas Choi na kushoto Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini, Mh. Song Geum-Young.
 Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini, Mh. Song Geum-Young (kushoto) akizungumzia furaha yake kushuhudia utiaji saini huo unaounga mkono jitihada za kuigeuza Tanzania kuwa ya viwanda katika hafla fupi iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi za IPP jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Dk. Reginald Mengi na kulia ni Mkurugenzi na Mwakilishi wa Kampuni ya Youngsan Glonet ya Korea, Bw. Thomas Choi.
 Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Dk. Reginald Mengi (kushoto) na Mkurugenzi na Mwakilishi wa Kampuni ya Youngsan Glonet ya Korea, Bw. Thomas Choi wakitiliana saini hati ya makubaliano ya kuanzishwa kwa mradi kuunganisha magari hapa nchini katika hafla fupi iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi za IPP jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia tukio hilo kutoka kushoto waliosimama kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa  IPP Touchmate, Bw. Victor Tesha, Msaidizi wa Dk. Mengi, Bw. Godfrey Bitesigirwe pamoja na Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini, Mh. Song Geum-Young.
 Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Dk. Reginald Mengi (kushoto) na Mkurugenzi na Mwakilishi wa Kampuni ya Youngsan Glonet ya Korea, Bw. Thomas Choi wakipeana mikono mara baada ya kutiliana saini hati ya makubaliano ya kuanzishwa kwa mradi kuunganisha magari hapa nchini katika hafla fupi iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi za IPP jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia tukio hilo kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa  IPP Touchmate, Bw. Victor Tesha, Msaidizi wa Dk. Mengi, Bw. Godfrey Bitesigirwe pamoja na Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini, Mh. Song Geum-Young.
Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Dk. Reginald Mengi (katikati), Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini, Mh. Song Geum-Young (wa pili kulia), Msaidizi wa Dk. Mengi, Bw. Godfrey Bitesigirwe (kulia), Mkurugenzi Mtendaji wa  IPP Touchmate, Bw. Victor Tesha (kushoto) pamoja na Mkurugenzi na Mwakilishi wa Kampuni ya Youngsan Glonet ya Korea, Bw. Thomas Choi (wa pili kushoto) wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya ya tukio la utilianaji saini hati ya makubaliano ya kuanzishwa kwa mradi kuunganisha magari hapa nchini katika hafla fupi iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi za IPP jijini Dar es Salaam.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

TAARIFA YA UTOAJI WA LESENI ZA MUDA MFUPI-MWISHO WA MWAKA.

Miradi mipya ya umeme ilenge maeneo yenye changamoto za upatikanaji umeme -Dkt Kalemani

$
0
0
Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani amewataka wataalam wanaopanga maeneo yanayopaswa kupelekewa umeme kupitia miradi mbalimbali kuhakikisha kuwa wanakuwa makini katika upangaji wa maeneo hayo ili kutorundika miradi mingi katika maeneo ambayo tayari yameshasambaziwa umeme.

Ameyasema hayo jijini Dar es Salaam wakati wa kikao chake na Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu pamoja na watendaji wa Wizara ya Nishati,  Shirika la Umeme Tanzania ( TANESCO), Wakala wa Nishati Vijijini ( REA) ambacho kililenga  kupata taarifa ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya umeme inayotekelezwa mijini na vijijini.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu katika Wizara ya Nishati, Raphael Nombo ( amemwakilisha Katibu Mkuu), Kaimu Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu, Eng. Innocent Luoga, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa REA, Eng. Amos Maganga, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Dkt. Tito Mwinuka na Kamishna Msaidizi wa Nishati Jadidifu, Edward Ishengoma.

“Kuna maeneo ambayo tayari yana umeme au kuna miradi kadhaa inayotekelezwa katika maeneo hayo hivyo kwa miradi tunayotaka kutekeleza sasa lazima tuweke msisitizo katika maeneo ambayo bado hayajafikiwa na nishati hiyo au hayajasambaziwa umeme kwa kiasi kikubwa,” alisema Dkt Kalemani.

Dkt. Kalemani alitoa kauli hiyo baada Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa REA, Eng. Amos Maganga  kueleza miradi mbalimbali ambayo ipo katika mchakato wa kutekelezwa ukiwemo wa kuongeza wigo wa miundombinu ya usambazaji umeme  (Densification) mzunguko wa pili  katika maeneo mbalimbali nchini na mradi wa usambazaji umeme wa awamu ya Tatu mzunguko wa pili.

Akielezea  kazi ya usambazaji umeme vijijini, Maganga alisema kuwa hadi kufikia Novemba 15, 2018, jumla ya vijiji  4,024  vimepatiwa umeme kupitia miradi ya REA ya Awamu ya Kwanza hadi Awamu ya Tatu mzunguko wa kwanza unaokamilika Juni 2019, mradi wa Makambako- Songea, Mradi wa umeme wa kV 400 wa Iringa hadi Shinyanga,  mradi wa Densification mzunguko wa kwanza na nishati jadidifu.
Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani (katikati) akiongoza kikao kati yake na Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (kulia kwa Waziri) pamoja na watendaji wa Wizara ya Nishati,  Shirika la Umeme Tanzania ( TANESCO), Wakala wa Nishati Vijijini ( REA) ambacho kililenga  kupata taarifa ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya umeme inayotekelezwa mijini na vijijini.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

PROFESA MBARAWA AWATAKA WANANCHI KULINDA VYANZO VYA MAJI

$
0
0
*Ashirikiana na Mkuu wa Wilaya ya Temeke,DAWASA kupanda miti pemebezoni mwa mto Kizinga.
*Mito zaidi ya 10,000 kupandwa Mto Mzinga, kampeni kuendelea hadi Mto Ruvu 
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii
WAZIRI wa Maji na Umwagiliaji Profesa Makame Mbarawa amewaomba wananchi kutunza vyanzo vya maji ili viwe endelevu  na kuacha kulima pembezoni mwa mito.

Ameyasema hayo leo wakati wa upandaji miti aina ya Mitomondo pembezoni mwa mto Kizinga akiwa ameambatana na Mkuu wa Wilaya ya Temeke Felix Lyaniva na Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na Majitaka (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja.

 Akizungumza na wananchi wa eneo la Mtoni Mashine ya maji, Profesa Mbarawa amesema wananchi wanatakiwa kulinda vyanzo vya maji ili wapate majisafi na salama kwa manufaa yaona vizazi vijavyo.

Amesema, amehakikisha wanaanza kampeni maalumu kwa ajili ya kulinda vyanzo vya maji, na wakivilinda vizazi vijavyo vitapata maji safi na salama na serikali watapoteza pesa nyingi iwapo wananchi wataharibu vyanzo hivyo.

Amesema Serikali inatumia pesa nyingi kujenva  miundo mbinu ya maji na iwapo vyanzo vikiharibikiwa na basi haitaweza kufanya kazi ya kusambaza maji safi na salama.

"Lazima tusimamie sheria, serikali inawekeza hela nyingi sana katika kujenga miundo mbinu na kampeni hii imeanzia  Mtwara, Ruvuma na Dar es salaam na hii itaendelea nchi nzima,"amesema Mbarawa.

Mkuu wa Wilaya ya Temeke Felix Lyaniva amesema mtambo huu wa maji wa Mtoni ulijengwa mwaka 1949 ukihudumia mkoa mzima wa Dar es Salaam.

Lyaniva amewasihi wananchi wanaoishi pembezoni mwa mto Mzinga kuacha kulima kwani kufanya hivyo wanasababisha maji kukauka na kusababisha ukosefu wa maji.

"Nilianza na nitaendelea kupanda miti pembezoni mwa vyanzo vya maji, suala hili nimeliwekea kipaumbele kwani maji ni muhimu na wananchi wanahitaji maji," amesema Lyaniva.

Naye Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA Cyprian Luhemeja amesema kuna changamoto kubwa ya uharibifu wa vyanzo vya maji kwa wananchi kulima pembezoni mwa mto na wameanza kampeni hii ya kupanda miti kwenye maeneo yote.
 Waziri wa Maji na Umwagiliaji Profesa Makame Mbarawa akipanda mti kwenye Chanzo cha Mto Kizinga ikiwa ni kampeni ya Upandaji miti pembenzoni mwa vyanzo vya maji.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke Felix Lyaniva akiwa anapamba mtikwenye Chanzo cha Mto Kizinga ikiwa ni kampeni ya Upandaji miti pembenzoni mwa vyanzo vya maji.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam ( DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja akipanda mti kwenye Chanzo cha Mto Kizinga ikiwa ni kampeni ya Upandaji miti pembenzoni mwa vyanzo vya maji.

KWA HABARI ZAIDI BOFYA HAPA 

MADARAJA YA KOROSHO YATAMBULIWE KUANZIA NGAZI AMCOS-MAJALIWA

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwaamewaagiza Warajisi Wasaidizi wa Ushirika katika Mikoa yote inayolima korosho nchini waandae semina kwa Maafisa Ushirika, viongozi wa vyama vya msingi (AMCOS), maafisa ugani na wakulima ili kuwawezesha kubaini na kupanga korosho katika madaraja kuanzia ngazi ya vyama vya msingi.
Amesema jambo hilo litasaidia mkulima aweze kujua korosho aliyoipeleka ina ubora gani akiwa huko kijijini na wanapoifikisha kwenye ghala kuu wafanye kazi ya kuthibitisha , kwa hatua hiyo itasaidia kuondoa malalamiko kuhusu madaraja . 
“Zoezi hili licha ya kuthibitisha ubora itasaidia kuboresha uzalishaji kwani wakulima wataelimishwa namna ya kuimarisha na kuboresha uzalishaji wa korosho nchini ikiwa ni pamoja na matumizi bora ya viatilifu ’’
Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumatano, Novemba 21, 2018) wakati alipotembelea kiwanda cha korosho cha BUKO kilichopo kwenye Manispaa ya Lindi, ambapo ameshuhudia korosho zikipimwa ubora kwenye ghala kuu lilipo kiwandani hapo.
Ameagiza semina ifanyike mwakani ili maafisa ushirika baada ya kupata mafunzo wawasaidie wakulima kwenye msimu ujao watambue korosho walizopeleka kuziuza zina ubora gani. 
Waziri Mkuu amesema katika semina hiyo wakutane maafisa kilimo na maafisa ushirika ili wapate taaluma hiyo itakayowawezesha kupima korosho na kuitenga katika madaraja na kuwaondolea shida wakati wa mauzo.
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua uwanja wa michezo wa Ilulu uliopo mjini Lindi, Novemba 21, 2018.  Kushoto kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi.  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua uwanja wa michezo wa Ilulu uliopo mjini Lindi, Novemba 21, 2018.  Kushoto kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi. 
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua kiwanda cha korosho BUKO  cha mjini Lindi ambacho kimesimamisha uzalishaji, Novemba 21, 2018.  Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi.  
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akikagua  magunia ya korosho yaliyohifadhiwa kwenye ghala la kiwanda cha korosho cha BUKO cha mjini Lindi wakati alipotembelea kiwanda hicho, Novemba 21, 2018.  Kushoto ni Mkurugenzi wa  Kampuni ya Namgongo Holding iliyopewa dhamana ya kutunza ghala hilo, Ramadhani Katau. 
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akishuhudia wakati ,   Afisa anayesimamia Ubora wa Korosho, Dastan Milazi alipokuwa akipima korosho zilizopokelewa kwenye ghala la kiwanda cha korosho cha BUKO cha mjini Lindi wakati alipotembelea kiwanda hicho kilichosimamisha uzalishaji, Novemba 21, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Fanyeni kazi Kwa Bidii Huku Mkimtanguliza Mungu Mbele kwani Huduma Wanayoitoa Inagusa Uhai wa Watu – Prof. Mohamed Janabi

$
0
0

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi amewataka wafanyakazi wa Taasisi hiyo kufanya kazi kwa bidii huku wakimtanguliza Mungu mbele kwani huduma wanayoitoa inagusa uhai wa watu.

Prof. Janabi ambaye pia ni daktari bingwa wa magonjwa ya moyo ameyasema hayo leo wakati wa hafla fupi ya kuwaaga maafisa uuguzi wawili ambao wamestaafu kwa mujibu wa sheria ya utumishi wa umma na kumpongeza mfanyakazi bora wa robo ya kwanza ya mwaka wa fedha wa Julai-Septemba 2018.

Alisema kazi ya kuwahudumia wagonjwa siyo kazi rahisi sana kuna wakati wagonjwa wanakuwa wakali wao na ndugu zao jambo la muhimu ni kuwa wavumilivu na kuwahudumia kwa moyo wa upendo.

“Leo hii tunawaaga wafanyakazi wenzetu ambao wanastaafu kwa mujibu wa sheria ya utumishi wa umma, kazi waliyoifanya ni ngumu wanastahili pongezi. Mmoja amefanya kazi miaka 40 na mwingine miaka 35 katika kipindi chao chote walichokuwa kazini hawakuwahi kushtakiwa kwa utovu wa nidhamu”.

“Jambo la muhimu kwetu sisi tunaobaki tuwaige mfano tujitahidi kuwahi kazini , tuwepo eneo la kazi na kufanya kazi muda wote wa kazi, tushirikiane na tuheshimiane kwa kufanya hivi tutaweza kutoa huduma bora kwa wagonjwa wetu wa moyo”, alisema Prof. Janabi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akimkabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni moja mfanyakazi bora wa robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2018/2019 Ramadhani Mpili wakati wa hafla fupi ya kuwaaga wastaafu na kumpongeza mfanyakazi bora iliyofanyika leo katika ukumbi wa Taasisi hiyo uliopo Jijini Dar es Salaam. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akimkabidhi cheti cha kutambua utendaji wake wa kazi kwa kipindi chote cha utumishi wa Umma Afisa Muuguzi Mkuu Msaidizi Mstaafu Agnes Mtaki wakati wa hafla fupi ya kuwaaga wastaafu na kumpongeza mfanyakazi bora iliyofanyika leo katika ukumbi wa Taasisi hiyo uliopo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Huduma ya Uuguzi wa Taasisi hiyo hiyo Robert Mallya. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akimkabidhi ngao ya kutambua utendaji wake wa kazi mhudumu wa Afya Mwandamizi Mstaafu Magdalena Masanno wakati wa hafla fupi ya kuwaaga wastaafu na kumpongeza mfanyakazi bora iliyofanyika leo katika ukumbi wa Taasisi hiyo uliopo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Huduma ya Uuguzi wa Taasisi hiyo hiyo Robert Mallya. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akiwa katika picha ya pamoja na wastaafu Magdalena Masanno na Agnes Mtaki na baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi hiyo mara baada ya kumalizika kwa hafla fupi ya kuwaaga wastaafu hao na kumpongeza mfanyakazi bora iliyofanyika leo katika ukumbi wa Taasisi hiyo uliopo jijini Dar es Salaam. 


WAJUMBE KAMATI YA MAREKEBISHO YA KATIBA, KAMATI YA WATAALAM CPA KANDA YA AFRIKA WAKUTANA KWA MAJADILIANO

$
0
0
 Mwenyekiti wa kamati ya marekebisho ya katiba kutoka Bunge la Ghana, Mhe. Osei  kyei Mensahu Bonsu (katikati) akizungumza na wajumbe wa kamati hiyo, kamati ya wataalam katika kikao cha kamati maalum ya utendaji ya Mabunge ya Jumuiya ya Madola kanda ya Afrika (CPA) kinachoendelea leo tarehe 21 Novemba 2018 Bahari Beach Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu wa Bunge la Tanzania na Katibu wa kanda wa Mabunge ya Jumuiya ya Madola kanda ya Afrika (CPA), Ndg. Stephen kagaigai, kulia ni Katibu wa Bunge la Zambia na Mwenyekiti wa kamati ya wataalum ya Mabunge ya Jumuiya ya Madola kanda ya Afrika (CPA), Ndg. Cecilia Mbewe.
 Wajumbe wa kamati ya marekebisho ya katiba kuanzia kushoto ni aliekuwa Spika mstaafu wa Bunge la Nigeria na Mweka hazina wa Mabunge ya Jumuiya ya Madola kanda ya Afrika (CPA), Mhe. Samuel Ikon, Mwakilishi wa Kanda kutoka Bunge la Namibia Mhe. Bernard Sibalatani na kulia ni Mhe. Vedasingam Baloomoody Mbunge kutoka Bunge la Mauritius wakiwa katika kikao cha kamati maalum ya utendaji ya Mabunge ya Jumuiya ya Madola kanda ya Afrika (CPA) kinachoendelea leo tarehe 21 Novemba 2018 Bahari Beach Jijini Dar es Salaam.
 Mjumbe wa kamati ya wataalam na Mshauri wa masuala ya kisheria kutoka Bunge la Ghana, Ndg. Ebenezer Djietror akizungumza na wajumbe wa kamati ya marekebisho ya katiba, kamati ya wataalam katika kikao cha kamati maalum ya utendaji ya Mabunge ya Jumuiya ya Madola kanda ya Afrika (CPA) kinachoendelea leo tarehe 21 Novemba 2018 Bahari Beach Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mjumbe wa kamati ya wataalam na mshauri wa masuala ya kisheria kutoka Bunge la Uganda, Ndg. Jacqueline Guma

 Wajumbe wa kamati ya marekebisho ya katiba, kamati ya wataalam wakiwa katika kikao cha kamati maalum ya utendaji ya Mabunge ya Jumuiya ya Madola kanda ya Afrika (CPA) kinachoendelea leo tarehe 21 Novemba 2018 Bahari Beach Jijini Dar es Salaam. (PICHA NA OFISI YA BUNGE)

TIMOTHEO MNZAVA KUFUATA NYAYO ZA RAIS MAGUFULI

$
0
0

MBUNGE wa Korogwe vijijini ndugu Timotheo Mnzava leo tarehe 21/11/2018 amekutana na kufanya mazungumzo na mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Korogwe Bw. Kwame Daftari pamoja na wakuu wa idara. 

Kikao hiko kifupi kilikuwa kimelenga zoezi la utambulisho baina ya mbunge na watumishi wa halmashauri ya wilaya ya Korogwe ikiwa ni katika kuunganisha nguvu ya pamoja katika kuleta maendeleo endelevu kwa jimbo la Korogwe vijijini na wilaya kwa ujumla. 

Kikao hiko pia kilihudhuriwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Korogwe vijijini ndugu Charles Mweta. 

“Nimekuja kukutana nanyi nikiwa na lengo kuu la mimi kuwafahamu ila nanyi mnifahamu, kwapamoja tuunganishe nguvu katika kuwatumikia wanakorogwe, tupunguze kuzungumza sana na tuongeze uwezo wa kiutendaji ili tuendane na kasi ya rais Mh. John Pombe Magufuli ya kufikia uchumi wa kati ifikapo 2025,” alisema Mh. Mnzava. 

Aidha Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Korogwe, Bw. Daftari kwa niaba ya wakuu wa idara ameahidi kutoa ushirikiano wa dhati kwa mbunge ili kufikia lengo la kuleta matokeo chanya ambayo yataleta maisha bora kwa wananchi wa Korogwe.
Mbunge wa Korogwe Vijijini,Ndugu  Timotheo Mnzava.
Viewing all 110175 articles
Browse latest View live




Latest Images