Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110172 articles
Browse latest View live

WATAKA SHERIA YA WATIA MIMBA WANAFUNZI IONGEZWE MENO CALVIN GWABARA

$
0
0
Na: Amina Hezron, Morogoro

Wito umetolewa kwa serikali kuhakikisha wanawadhibiti na kuwachukulia hatua za kisheria wale wote watakaobainika wamebaka au kuwapa mimba wanafunzi wa shule za Msingi na Sekondari nchini.
Baadhi ya wadau wa Elimu Wilayani Mvomero Mkoani Morogoro wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya mkutano huo. 

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wadau wa elimu wilaya ya mvomero mkoani Morogoro wakati wa mkutano ulioandaliwa na mtandao wa elimu Tanzania TEN /MET ili kupeana mrejesho wa namna ya kukabiliana na changamoto za mimba za utotoni kwa wanafunzi wa shule ya msingi na sekondari.

Katika mkutano huo wa wadau wamebaini ushiriki wa karibu wa wazazi na watoto wao haupo kwa kiasi kikubwa jambo linaloelekea kuendelea kuwepo kwa changamoto hiyo.

Kwa upande wake afisa elimu wa wilaya hiyo Bi. Maajabu Nkamyemka amesema kwa wilaya ya mvomero takwimu zinaonesha hadi April 6 mwaka huu takribani mimba 90 zimebainika kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari ambapo miongoni mwa hizo mimba 13 ni kutoka shule za msingi.

Aidha Bi. Nkamyemka amesema kuwa ni jukumu la wazazi na walimu kwa kushirikiana na wanafunzi kuhakikisha wanawafichua wale wote ambao ni wahusika bila kuwafumbia macho ili sekta husika kupambana nao ili kutokomeza janga hilo.

"kwa kuwa binti akipewa ujauzito huwa tunahangaika tu na aliyempa ujauzito, na yule mwenye ujauzito tunamuacha sasa bhas sasa kwa kuwa wazazi hawataki kuleta ushirikiano tutamfungulia kesi mwanafunzi mwenye mimba pamoja na wazazi ili wazaz wawachunge watoto wao ipasavyo "Alisema Nkamyemka.
Wadau hao wa elimu wakiwa ndani ya mkutano huo 

Naye mratibu elimu wa kata za mhonda na Kweuma bwn, Heriamini Mariki amesema kuwa kumekuwa na changamoto ya mimba hasa kwa wanafunzi, wa sekondari jambo ambalo kwa kiasi kikubwa wazazi ndiyo chanzo cha tatizo hilo huku akitaja sababu zinazochangia kuwa ni pamoja na uelewa finyu wa wazazi na wakati mwingine umaskini kwa baadhi ya kaya nyingi wilayani humo.

“Sisi kama wadau wajibu wetu mkubwa ni kuwapatia elimu wazazi juu ya athari za kutokaa karibu na watoto wao na kuwa wawazi juu ya madhara ya kufanya ngono wakiwa na umri mdogo" alisema Mariki

Naye diwani wa kata ya mhonda Bw. Abdallah Hassani Khalifa ametoa rai kwa Serikali kujenga hosteli kwa shule za kata ili kuondokana na tatizo la mimba za utotoni linaloikumba nchi nzima kwa kiasi kikubwa, huku akiwataka wazazi na walimu wanawapa watoto wanafunzi ushirikiano wa kutosha na ulinzi kwani ndiyo haki pekee wanaotakiwa kuzipata ili kufanya vyema katika masomo yao.


WAANDISHI WA HABARI NI KUNDI MUHIMU KATIKA KUFIKISHA UJUMBE KWA JAMII.DC SONGEA

$
0
0
Vyombo vya habari,mitandao ya kijamii imeonekana kuwa na mchango mkubwa katika jamii kutokana na uwezo wa kufikisha ujumbe kwa haraka ukilinganisha makundi mengine.

Hayo yamesemwa na mkuu wa wilaya ya SONGEA POLOLET MGEMA wakati wa mafunzo kwa wataalamu watakaoenda kutoa chanzo kwa ajili ya kinga dhidi ya saratani ya mlango wa kizazi kwa wa watoto wa kike mwenye umri wa miaka 9 hadi 14 ambayo hufanyika leo mkoani Ruvuma na Tanzania kwa ujumla.

WANANCHI KIJIJI LUMWAGO MAFINGA MJINI WASHANGILIA KUWAKA UMEME

$
0
0
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani,mkuu wa wilaya ya Mufindi Jamhuri Wiliam,Mbunge wa jimbo la Mafinga Mjini Cosato Chumi pamoja na mwenyekiti wa chama cha mapinduzi wilaya ya Mufindi wakiwa nafungua na kuwasha umeme kwa mara ya kwanza katika kijiji cha Lumwago kata ya Upendo Halmashauri ya Mji wa Mafinga mkoani Iringa.NA FREDY MGUNDA,IRINGA. 

BENKI YA EXIM YATOA MSAADA HOSPTALI YA RUFAA YA MOROGORO KUPITIA KAMPENI YA “20 YA KUJALI JAMII”

$
0
0
 Hospitali na kliniki nyingi nchini zina tatizo la ukosefu wa dawa, vifaa na vitanda hasa katika hospitali za rufaa. Katika kukabiliana na uhaba huu unaosumbua taifa, benki ya Exim Tanzania, yenye uwepo wa kimataifa imeanzisha mradi unaolenga kusaidia upungufu wa vitanda katika wodi za wazazi kwenye hospitali nchini - hivyo benki ya Exim itatoa magodoro and vitanda 500 katika hospitali za serikali katika mikoa 13 nchini kama sehemu ya kampeni yake ya mwaka yenye lengo la kusherehekea miaka 20 ya kutumikia jamii.
Benki ya Exim Tanzania imekabidhi vitanda na magodoro 40 kwa Hospitali ya rufaa ya mkoa wa Morogoro, jijini Morogoro. Benki ya Exim Tanzania iliadhimisha miaka 20 ya huduma, mwezi wa Agosti mwaka jana, kwa kuzindua mradi wa mwaka mzima unaoitwa “miaka 20 ya kujali jamii” ambao Benki hiyo itawekeza katika sekta ya afya Tanzania hasa kwenye kuboresha huduma za afya zinazotolewa kwa wakina mama na wanawake. 
Hospitali ya rufaa ya mkoa wa Morogoro ni hospitali ya tisa kupokea mchango huu, baada ya hospitali ya rufaa ya Mwananyamala mwezi uliopita, hospitali  ya rufaa ya Bombo, mkoani Tanga mwezi Febuari, hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Mbeya mwezi Januari, hospitali ya Mount Meru, Arusha mwezi Desemba, Hospital ya rufaa Dodoma mwezi Novemba, hospitali ya rufaa Ligula, Mtwara mwezi Oktoba, Hospitali ya Mnazi Mmoja, Unguja, Zanzibar mwezi Septemba na Hospitali ya rufaa Temeke, Dar es Salaam mwezi wa nane mwaka jana.
Mkuu wa idara ya masoko wa benki ya Exim Tanzania, Stanley Kafu  akizungumza wakati wa makabidhiano ya vitanda na magodoro 40 katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Morogoro kupitia kampeni yao ya maadhimisho ya miaka 20 ya kujali jamii kwa benki hiyo.
Mwenyekiti wa bodi ya hospitali ya rufaa ya Morogoro, Dk Lucy Nkya akipokea Vitanda na magodoro 40 kutoka kwa Mkuu wa idara ya masoko wa benki ya Exim Tanzania, Stanley Kafu, yaliyotolewa na benki ya Exim kupitia kampeni yao ya maadhimisho ya miaka 20 ya benki hiyo yenye kauli mbiu ya "miaka 20 ya kujali jamii".
Mganga mkuu mkoa wa Morogoro, Dk Francis Jacob akizungumza katika hafla fupi ya kukabidhi vitanda na mahodoro 40 kutoka benki ya Exim Tanzania kupitia kampeni yao ya maadhimisho ya miaka 20 ya kujali jamii kwa benki hiyo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

RAIS WA TFF WALLACE KARIA AMWAGA PONGEZI KWA NGORONGORO HEROES NA SERENGETI BOYS

$
0
0
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania(TFF) Ndugu Wallace Karia ametoa salamu za pongezi kwa timu ya Taifa ya Vijana chini ya miaka 20 (Ngorongoro Heroes) na ile ya chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) kwa kufanikiwa kufuzu katika michezo yao iliyochezwa jana huko DR Congo na Burundi.

Ngorongoro Heroes wamefanikiwa kusonga kwenye raundi ya pili ya kufuzu fainali za Africa za Vijana chini ya miaka 20 zitakazochezwa Niger mwezi Novemba baada ya ushindi wake wa penati 5-6 dhidi ya DR Congo baada ya dakika 90 kumalizika kwa sare ya bila kufungana kama ilivyokuwa kwenye mchezo wa kwanza uliochezwa nchini Tanzania wakati Serengeti Boys wenyewe wamefuzu hatua ya nusu fainali ya mashindano ya Vijana ya Cecafa chini ya miaka 17 inayoendelea huko Burundi.

Rais wa TFF Ndugu Karia amesema kufanya vizuri kwa timu hizo za vijana ni faraja kubwa kwa Tanzania na inaonesha namna ambavyo TFF inaendelea kuwekeza kwenye soka la vijana.Amesema Vijana hao wa Ngorongoro Heroes na Serengeti Boys wameonesha jitihada kubwa na wanastahili pongezi kwa jitihada hizo pamoja na jitihada za mabenchi ya ufundi ya timu hizo.

“Tumepokea matokeo ya Vijana wetu wa Ngorongoro na Serengeti Boys kwa furaha kubwa kwasababu tumekuwa tukihakikisha timu hizi zinapata maandalizi mazuri ambayo yanaonekana uwanjani kwa kupata matokeo mazuri ambayo yanailetea sifa kubwa Tanzania kwa ujumla” alisema Karia.

Aidha Rais wa TFF Ndugu Karia amesema TFF itaendelea na jitihada kuzipatia maandalizi mazuri zaidi timu hizo ili ziweze kufanya vizuri katika mashindano mbalimbali yanayowakabili.

Amesema TFF inajivunia vijana hao ambao wanaonesha mwanga mkubwa na amewaomba watu mbalimbali,Taasisi,makampuni kuunga mkono jitihada za TFF na kuiga mfano wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro waliojitokeza na kuisaidia Ngorongoro Heroes katika safari yake ya kwenda DR Congo kwenye mchezo wa marudiano.

Amemalizia kwa kuwashukuru wote wanaounga mkono jitihada za TFF kuendeleza mpira wa Tanzania huku akiishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais John Pombe Magufuli kwa kuunga mkono na ushirikiano wao kwa TFF.

Airtel kuviwezesha vikundi vya kinamama kujiendesha kidigitali

$
0
0
· Zaidi ya vikundi vya wajasiriamali 100 kunufaika na huduma ya Timiza Vikoba na Mafunzo ya Tehama

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel imeviasa vikundi vya kina mama wajasiriamali kutumia fursa wanazozitoa kupitia bidhaa na huduma mbalimbali za kibunifu ikiwemo Timiza Vikoba ili kujiendesha kidigital na kukuza biashara zao. 
 

Hayo yalisemwa na meneja miradi wa Airtel Bi Jane Matinde wakati wa mkutano wa viongozi wa vikundi vya kina mama wajasiriamali jijini Dar uliondaliwa na Star Women group.

Akitoa ufafanuzi wa kina Matinde alisema “Timiza vikoba ni huduma inayowawezesha vikundi kuweka na kuchukua mikopo kupitia simu zao za mkononi kwa kupitia huduma ya Airtel Money, huduma inayotolewa na Airtel kwa kushirikiana na benki ya Maendeleo.

Timiza Vikoba inaviwezesha vikundi vya kuanzia watu 5 hadi 50 kujisaji na kufungua akaunti ili kufaidika na huduma ya kutuma michango yao ya kila wiki, kuomba mikopo na kufanya marejesho ya mikopo wakiwa nyumbani au mahali popote pale kwa usalama na urahisi zaidi masaa 24 siku saba za wiki kwa gharama nafuu”.

Matinde aliwashauri wanawake hao wajarisiamali kutumia njia za teknologia ya kisasa katika kufanya miamala ya kifedha kwa usalama, uhakika na urahisi zaidi kupitia huduma ya Timiza Vikoba “ huduma hii itawarahisishia sana kutuma pesa za michango na marejesho kupitia simu, itaokoa muda wa kukutana na kuweka uwazi kwani kila mwana kikundi anapoweka pesa fedha au kuomba mkopo kila moja anapata taarifa hapohapo nakuridhia, nawahimiza mchangamkie fursa hii.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

SEHEMU YA KWANZA YA HISTORIA YA VITA VYA MAJI MAJI.

$
0
0
Jina la vita vya Maji Maji lilitokana na imani ya matumizi ya “Dawa” iliyochanganywa na maji ,punje za mahindi na mtama zilizosadikika kuwa zitampa mpiganaji kinga ya kutodhurika kwa shambulio la risasi za Wajerumani .Kwa undani wa Historia hii ya Vita vya Maji Maji tizama sehemu ya Kwanza ya Historia ya Vita hivyo.

Benki ya Barclays Tanzania yasaidia kambi ya upasuaji watoto wenye tatizo la vichwa vikubwa na mgongo wazi,yakabidhi kadi za bima ya afya (NHIF) 200 kwa watoto hao.

$
0
0


Mkuu wa Kitengo cha Ukusanyaji Mikopo Isiyolipwa wa Benki ya Barclays Tanzania, Khatibu Mohammedy (wa tatu kushoto,) akikabidhi vifaa vya kusaidia upasuaji wa watoto wenye tatizo la vichwa vikubwa na mgongo wazi kwa Kaimu Mkurugenzi wa Tiba wa Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI), Dk.Nicephorus Rutabansibwa (wa pili kushoto), katika hafla ambayo Barclays pia ilitoa msaada wa kadi za Bima ya Afya (NHIF), kwa watoto 200 pamoja na kuwezesha kambi ya siku moja ya upasuaji wa watoto 30 wenye matatizo ya vichwa vikubwa na mgongo wazi. Hafa hiyo ilifanyika katika Taasisi ya MOI, Dar es Salaam jana. Wengine ni watumishi wa MOI na wa kutoka Barclays.

Mkuu wa Kitengo cha Ukusanyaji Mikopo Isiyolipwa wa Benki ya Barclays Tanzania, Khatibu Mohammedy(kulia), akikabidhi kadi ya bima ya afya (NHIF) kwa mmoja wa watoto wenye tatizo la vichwa vikubwa na mgongo wazi , Joy Jacob katika hafla ambayo Barclays pia ilitoa msaada wa kadi za Bima ya Afya (NHIF), kwa watoto 200 pamoja na kuwezesha kambi ya siku moja ya upasuaji wa watoto 30 wenye matatizo ya vichwa vikubwa na mgongo wazi. Hafa hiyo ilifanyika katika Taasisi ya MOI, Dar es Salaam jana. Wa pili kushoto (mstari wa nyuma) ni kwa Kaimu Mkurugenzi wa Tiba wa Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI), Dk.Nicephorus Rutabansibwa, watumishi wa MOI na wa kutoka Barclays. Madaktari wa upasuaji wa MOI wakifanya upasuaji mwa mmoja wa watoto wanaosumbuliwa na tatizo la kichwa kikubwa katika kambi ya upasuaji iliyodhaminiwa na Barclays katika hospitali hiyo jana. Baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo wakiongozwa na Mkuu wa Kitengo cha Ukusanyaji wa Mikopo Isiyolipwa wa Barclays Khatibu Mohammedy (nyuma katikati), wakishuhudia.

Baadhi ya watoto 200 waliopewa msaada wa kadi za bima ya afya (NHIF) na benki ya Barclays Tanzania wakionyesha kadi zao katika hafla hiyo katika hafla ambayo benki hiyo pia ilidhamini kambi ya siku moja ya upasuaji wa watoto 30 wenye matatizo ya vichwa vikubwa na mgongo wazi.


WADAU WA MAENDELEO WAIPONGEZA SERIKALI YA TANZANIA KWA MAFANIKIO YA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI UNAOTEKELEZWA NA TASAF.

$
0
0

NA. Estom Sanga-

Wadau wa Maendeleo wameipongeza Serikali ya Tanzania kwa kusimamia kwa ufanisi Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini unaotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF- Mpango ambao umeanza kuonyesha mafanikio makubwa katika mapambano dhidi ya umaskini kwa Walengwa wake.

Wadau hao wa Maendeleo ambao wamefanya ziara katika maeneo mbalimbali nchini kukutana na Walengwa na kushuhudia namna Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini unavyotekelezwa, wamejionea namna Walengwa wanavyoendelea kuboresha maisha yao kwa kutumia fursa ya kujumuishwa kwenye shughuli za Mpango zilizoanza takribani miaka mitano iliyopita.

Katika maeneo walikotembelea ikiwemo, Zanzibar, Korogwe,Shinyanga,Kagera, na Manyara,wadau hao wa Maendeleo walioambatana na Maafisa wa serikali na wale wa TASAF wameshuhudia mafanikio makubwa katika sekta za elimu, afya,ujenzi wa nyumba ,kilimo ,ufugaji na miradi ya uchimbaji wa malambo ya maji na jitihada mpya za kuunda vikundi vya kuweka akiba na kukopeshana miongoni mwa Walengwa ili kukuza zaidi uwezo wao kiuchumi.

Wadau hao wa Maendeleo pia wamevutiwa zaidi na namna Walengwa wa TASAF walivyoamua kwa hiari yao kutumia sehemu ya ruzuku wanayoipata kujiunga na Mfuko wa Bima ya Afya ya Jamii CHF-na kuwa na uhakika wa kupata matibabu wakati wote wa mwaka katika kaya husika, huku katika maeneo mengi mahudhurio ya watoto wanaotoka kwenye Kaya za Walengwa yamekuwa mazuri ikilinganishwa na kabla ya kuanza kwa shughuli za Mpango.

Kutokana na mabadiliko chanya kwa Walengwa, Kumekuwa na mahitaji makubwa ya Wataalamu hususani wa Ugani ambao wanahitajika kusaidia jitihada za Walengwa hao wa TASAF kutekeleza miradi ya kiuchumi wanayoianzisha ikiwemo ufugaji wa kuku wa kienyeji, mbuzi, ng’ombe,nguruwe,bata, na kilimo kulingana na maeneo yao.

Aidha imebainika kuwa idadi kubwa ya Wananchi ambao hawakupata fursa ya kuorodheshwa kwenye shughuli za Mpango ,wangelipenda kupata fursa hiyo ili waweze pia kunufaika na huduma zitolewazo kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini.Hata hivyo kwa nyakati tofauti Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF ,Bwana Ladislaus Mwamanga amezungumzia dhamira njema ya serikali ya kuhakikisha kuwa Wananchi wote wanaostahili kunufaika na shughuli za Mpango wanafanya hivyo nchini kote. Amesema serikali itafanya hivyo pindi fedha zitakapapatikana.

Hii leo Wadau hao wa maendeleo kutoka taasisi zinazochangia utekelezaji wa Mpango huo wa kunusuru Kaya Maskini unaohudumia takribani Kaya Milioni MOJA NA LAKI MOJA zilizoko katika vijiji zaidi ya ELFU TISA sawa na asilimia 70 ya vijiji vyote nchini, wanaendelea na Mkutano wao kwenye Ofisi za TASAF jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF ,Ladislaus Mwamanga (aliyesimama)akijadiliana jambo na Kiongozi wa Shughuli za TASAF Benki ya Dunia Mohammed Muderis kwenye Mkutano wa Wadau.

Baadhi ya Wadau wa Maendeleo wakiwa kwenye Mkutano wa kujadili shughuli za Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini unaotekelezwa na TASAF . 
Baadhi ya Wadau wa Maendeleo na Maafisa wa serikali na TASAF wakiwa kwenye Mkutano wa mapitio ya utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya maskini unaoendela kwenye ofisi za TASAF jijini Dar es salaam.

Mmoja wa Maafisa wa TASAF ,Peter Lwanda aliyeshika kipaza sauti, akiwasilisha taarifa ya ziara ya wadau waliotembelea mkoa wa Shinyanga kuona utekelezaji wa shughuli za Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini. 
Washiriki wa Mkutano wa Wadau wa Maendeleo wakifuatilia taarifa inayowasilishwa na mmoja wa Maafisa waliotemebelea maeneo ya utekelezwaji wa Shughuli za Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini (hayupo pichani). 

TUZO YA MO SALAH YALETA GUMZO

$
0
0
Na Zaynab Nyamka, Globu ya Jamii.

BAADA ya kuchukua tuzo ya mchezajo bora wa Shirikisho ijulikanayo kama PFA Player of the Year akiwa tayari ameshachukua tuzo ya kila mwezi mara tatu katika msimu mmoja na kujiweka rekodi hiyo ndani ya ligi ya EPL nchini Uingereza wadau mbalimbali wameonyesha kukataa kuchukua kwa tuzo hiyo na kumpa nafasi Kelvin De Bruyne.

Mohamed Salah mwenye miaka 25 usiku wa jana aliweza kutangazwa kama mchezaji bora wa shirikisho akiwa amepambanishwa na wachezaji wengine wa EPL na kuwa mchezaji wa saba kutoka Liverpool kuchukua tuzo hiyo.

Hizi ni  takwimu za Mo Salah 

Mohamed Salah - Msimu wa 2017-18 

Ameshiriki mechi: 33
Mikwaju iliyogusa wavu: 64
Magoli: 31
Dakika alizocheza: 2,657
Amechangia magoli: 9
Nafasi alizotoa: 57
Mikwaju: 132
Pasi alizokamilisha: 684

Kwa upande wa De Bruyne mwenye miaka 26 ameweza kutoa mchango mkubwa akichangia magoli 15 na kutoa nafasi za kufunga magoli 104 ikiwa ni zaidi ya mchezaji mwingine katika msimu na kufanikiwa kufunga magoli 8.

Takwimu za De Bruyne.

Kevin de Bruyne - Msimu wa 2017-18 
 Ameshiriki mechi: 34
Mikwaju iliyogusa wavu: 36
Magoli: 8
Dakika alizocheza: 2,836
Amechangia magoli: 15
Nafasi alizotoa: 104
Mikwaju: 84

WAZIRI MKUU MAJALIWA AKUTANA NA SPIKA WA BUNGE LA AFRIKA YA MASHARIKI MJINI DODOMA

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na Spika wa Bunge la Afrika ya Mashariki, Mhe. Martin Ngoga (watatu kushoto) baada ya mazungumzo, Bungeni mjini Dodoma, Aprili 23, 2018. Wengine pichani ni Wabunge wa Bunge la Afrika ya Mashariki, kutoka kushoto ni Dkt. Abdullah Hasnuu Makame, Fancy Nkuhi na Mariam Ussi Yahya. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Spika wa Bunge la Afrika ya Mashariki,Mhe. Martin Ngoga, Bungeni mjini Dodoma Aprili 23, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipeana mkono na Spika wa Bunge la Afrika ya Mashariki, Mhe.Martin Ngoga kabla ya mazungumzo yao, Bungeni mjini Dodoma, Aprili 23, 2018.

UPANDAJI MITI CHUO CHA MAFUNZO YA AMALI MKOKOTONI WAFANA

$
0
0
 Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Idirisa Musilimu Hija akizindua zoezi la upandaji Miti Chuo cha Mafunzo ya Amali Mkokotoni Mkoa wa Kaskazini Unguja.
 Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Idirisa Musilimu Hija akipanda mti baada ya kuzindua zoezi la la upandaji miti Chuo cha Mafunzo ya Amali Mkokotoni Mkoa wa Kaskazini Unguja.
 MKURUGENZI Mamlaka Mafunzo ya Amali, Bakari Silima akipanda mti katika zoezi la upandaji miti Chuo cha Mafunzo ya Amali Mkokotoni Mkoa wa Kaskazini Unguja (Picha na Abdalla Omar Maelezo – Zanzibar).
 Maafisa na Wanafunzi mbali mbali  waliojitokeza katika zoezi la upandaji miti lililofanyika Chuo cha Mafunzo ya Amali Mkokotoni Mkoa wa Kaskazini Unguja  (Picha na Abdalla Omar Maelezo – Zanzibar).

ALICHOKISEMA BALOZI WA SERIKALI YA JAMHURI YA WATU WA CHINA KUHUSU KUDHIBITI MAGONJWA KWA WANANCHI WA PEMBA

YALIYOJIRI LEO BUNGENI MJINI DODOMA

$
0
0
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mwenyekiti wa Bunge na Mbunge wa Ilala, Mussa Azzan Zungu Bungeni mjini Dodoma, Aprili 23, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani akijibu swali  bungeni mjini Dodoma, Aprili 23, 2018. (Picha na ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu,  Jenista Mhagama (kushoto) akizungumza na Naibu Waziri , Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira, Anthony Mavunde, Bungeni mjini Dodoma  Aprili 23, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama (kushoto) akiteta na Naibu Waziri ,Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza, Bungeni mjini Dodoma, Aprili23, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri M,uu)

MASAUNI AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA TAIFA LA USALAMA BARABARANI, MJINI DODOMA

$
0
0
 Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Mhandisi Hamad Masauni akizungumza na Wajumbe wa Kikao cha Baraza hilo kilichofanyika katika Ukumbi wa Wizara yake, mjini Dodoma leo. Kushoto ni Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi, ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Baraza hilo, Elius Kwandikwa. Kulia ni Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini ambaye pia ni Katibu wa Baraza hilo, Fortunatus Musilimu. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Mhandisi Hamad Masauni (katikati meza kuu) akimsikiliza Mjumbe wa Baraza hilo, ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chama cha Wamiliki wa Mabasi nchini (TABOA), Enea Mrutu alipokuwa masuala ya usalama barabarani katika kikao cha Baraza hilo kilichofanyika katika Ukumbi wa Wizara, mjini Dodoma leo. Kushoto meza kuu ni Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi, ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Baraza hilo, Elius Kwandikwa. Kulia ni Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini ambaye pia ni Katibu wa Baraza hilo, Fortunatus Musilimu. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini ambaye pia ni Katibu wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Fortunatus Musilimu, akimfafanulia jambo Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza hilo, Mhandisi Hamad Masauni (katikati meza kuu), wakati wa kikao cha Baraza hilo lililokua linajadili masuala mbalimbali ya usalama barabarani. Kikao hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Wizara yake, mjini Dodoma leo. Kushoto meza kuu ni Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi, ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Baraza hilo, Elius Kwandikwa. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Mhandisi Hamad Masauni (katikati meza kuu) akizungumza na Wajumbe wa Kikao cha Baraza hilo kilichofanyika katika Ukumbi wa Wizara yake, mjini Dodoma leo. Kushoto meza kuu ni Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi, ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Baraza hilo, Elius Kwandikwa. Kulia ni Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini ambaye pia ni Katibu wa Baraza hilo, Fortunatus Musilimu. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

PROFESA MTANZANIA CHUO KIKUU INDIANA APATA TUZO YA WALTON

$
0
0
Beatrice anayefundisha lugha ya Kiswali chuo kikuu cha Massachusetts akimwelezea Profesa Alwiya Omar kabala profesa hyuyo hajapewa tuzo hiyo. Picha na Vijimambo Blog na Kwanza Production chini ya udhamini wa Kilimanjaro Studio
Kulia ni Profesa Alwiya Omar ambaye ni Clinical Professor of Linguistics and Afrcan Languages wa chuo kikuu cha jimbo la Indiana akipokea tuzo ya Walton ya ufanisi wa utafiti na ufundishaji wa lugha za kigeni Marekani siku ya Jumamosi April 21, 2018 katika hotel ya Hyatts Regecy, Dulles Virginia.
 Profesa Alwiya Omar akipata picha ya pamoja na maprofesa wenzake wanaofundisha katika vyuo vya Marekani siku ya Jumamosi April 21, 2018 katika hotel ya Hyatts Regecy, Dulles Virginia, siku alipopokea tuzo ya Walton.
Profesa Alwiya Omar akiongea mara baada ya kupokea tuzo hiyo.
Profesa Alwiya Omar akipata picha na wadau
Profesa Alwiya Omar akipata picha na Rais wa Jumuiya ya waTanzania DMV.

VOA SWAHILI: Duniani Leo 23rd April 2018

HABARI ZA UMOJA WA MATAIFA LEO APRILI 23, 2018

TANZANIA NA ISRAEL KUANGALIA NAMNA YA KUSHIRIKIANA KATIKA MASUALA YA SHERIA

$
0
0
Na  Mwandishi Maalum
Tanzania na Israel zimekubaliana kwamba ,  mataifa hayo mawili yana mengi ya kujifunza baina  yao hususani katika eneo la utoaji wa haki na usimamiaji wa sheria.
Hayo yamejiri leo ( jumatatu) wakati Mwanasheria  Mkuu wa Serikali, Dk. Adelardus Kilangi, alipokutana na kufanya mazungumzo  na Waziri wa Sheria wa Israel Bi. Ayalet Shaked.
Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika katika Jengo la   Mikutano la Kimataifa la Mwalimu Julius Nyerere ( JNICC), viongozi hao walikubaliana kwamba kuna haja na umuhimu wa   Mwanasheria Mkuu wa Serikali wa Tanzania na Mwanasheria Mkuu wa Israel kukutana kwa lengo la kuainisha maeneo ambayo Ofisi hizo mbili  zinaweza kushirikiana.
“  Nadhani  tuna mengi ya  kujifunza kutoka kwenu na halikadhalika nanyi kuna maeneo ambayo   mnaweza kujifunza kutoka kwetu. Hivyo basi, ninaamini kwamba pale itakapowezekana,  kuna umuhimu wa mimi kukutana na mwenzangu ili tuweze kuangalia maeneo ya kipaumbele ambayo tunaweza kubadilishana uzoefu na kupanua wigo wa ushirikiano  baina ya nchi zetu”, akasema Dk. Kilangi.
Akayataja maeneo ambayo  anaamini Tanzania na Israel  zinaweza kushirikiana ni pamoja na  namna bora ya kuimarisha mifumo ya utoaji  haki na ushauri wa kisheria wenye tija, pamoja na eneo la uwezeshwji ( capacity  building).
Mwanasheria Mkuu , Dk. Kilangi  ambaye alifuatana na Naibu Mwanasheria Mkuu wa  Serikali Bw, Edson Athnas Makallo, aliyatumia mazungumzo  kati yake na Waziri Shaked kuelezea baadhi ya majukumu yake anayoyatekeleza  kama Mshauri Mkuu wa Serikali katika masuala yote yanayohusu sheria pamoja muundo mpya wa Ofisi  ya Mwanasheria Mkuu ambao umehusisha kuanzishwa kwa Wakili Mkuu wa Serikali.

Kwa upande wake,   Waziri wa Sheria wa Israel, ambaye  Tanzania inakuwa nchi yake ya kwanza kutembelea Barani Afrika, pamoja na kukubaliana na wazo la Dk. Kilangi la kuangalia uwezekano wa  Wanasheria Wakuu kukutana katika muda utakaopangwa. Amesema kwamba, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ni Ofisi nyeti na yenye hadhi ya  juu kabisa katika nchi yoyote ile ikiwamo Israel.
Akaongeza kwamba, majukumu anayoyatekeleza Mwanasheria Mkuu wa  Serikali, Dk. Adelardus Kilangi yanashabihiana na anayotekeleza  Mwanasheria Mkuu wa Israel yakiwamo ya kuisimamia serikali katika  masuala yote yanayohusu sheria, kuiwakilisha serikali katika mahakama za juu na mahakama za chini pamoja na kuendesha mashauri  ya jinai hivyo wawili hao wakipata fursa ya kukutana bila shaka watakuwa na mengi ya kujadiliana na kushirikiana.
Waziri wa Sheria wa Israel Ayalet Shaked anaongoza ujumbe wa  wafanyabiashara kutoka Israel ambao upo hapa nchini kukutana na  wafanyabiashara wa Tanzania.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dk. Adelardus Kilangi akiwa katika mazugumzo na  Waziri wa Sheria wa Israel Bi, Aylet Shaked.  Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika  katika  Ukumbi wa Mikutano wa Kimatifa wa Julius Nyerere ( JNICC) jijini Dar es Salaam,   viongozi hao walikubaliana kwamba Tanzania na Israel  zinayo maeneo ambayo  kila nchi inaweza kujifunza kutoka kwa mwenzie hususani katika  eneo la utoaji  haki na  usimamiaji wa sheria na kwamba kuna haja  kupitia kwa  Wanasheria  Wakuu wa Serikali wa nchi hizo mbili  kukutana ili  kujadiliana maeneo ya  kushirikiana.   Waziri wa Sheria wa Israel  yupo nchini akiongoza ujumbe wa wafanyabiashara.
Katika hatua nyingine, Mwanasheria Mkuu wa  Serikali  Dk. Adelardus Kilangi amekutana na kufanya mazugumzo na  Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Bw. Said Hassan Said. Katika mazungumzo  yao viongozi hao wamebadilishana mawazo  ya namna  ya kushirikiana  katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku  yanayosimamia   masuala ya sheria na utaoaji  haki. Pichani Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Bw. Said Hassan Said akimkabidhi Dk. Adelardus Kilangi  Katiba ya Zanzibar ( picha na Ofisi ya AG

BBC DIRA YA DUNIA JUMATANO 23.04.2018

Viewing all 110172 articles
Browse latest View live




Latest Images