Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109602 articles
Browse latest View live

RAIS DKT MAGUFULI AZINDUA JENGO LA PSPF PLAZA NA TAWI LA BENKI YA NMB MJINI DODOMA

0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipigiwa makofi na viongozi mbalimbali baada ya kufunua pazia kuashiria uzinduzi rasmi wa jengo la kitega uchumi la mfuko wa pensheni wa wafanyakazi wa umma la PSPF Plaza barabara ya Chimwaga mjini Dodoma leo April 23, 2018
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisaidiwa na viongozi mbalimbali akiakata utepe kuashiria  uzinduzi rasmi wa jengo la kitega uchumi la mfuko wa pensheni wa wafanyakazi wa umma la PSPF Plaza barabara ya Chimwaga mjini  Dodoma leo April 23, 2018 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisaidiwa na Naibu Waziri wa Fedha Dkt. Ashatu Kijaji na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB Bi. Ineke Bussemaker kuashiria uzinduzi rasmi wa Makao Makao Makuu ya Kanda ya Kati ya benki hiyo yaendayo kwa jina la Tawi la Kambarage mijini Dodoma leo April 23, 2018 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisaidiwa na Naibu Waziri wa Fedha Dkt. Ashatu Kijaji na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB Bi. Ineke Bussemaker pamoja na viongozi wengine kukata utepe  kuashiria uzinduzi rasmi wa Makao Makao Makuu ya Kanda ya Kati ya benki hiyo yaendayo kwa jina la Tawi la Kambarage barabara ya Chimwaga mijini Dodoma leo April 23, 2018  
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika kitengo cha huduma kwa wateja akiwa na Naibu Waziri wa Fedha Dkt. Ashatu Kijaji, Naibu Gavana Mkuu wa Benki ya Tanzania Dkt. Bernard Kibesse, Mkurugenzi wa Bodi ya NMB Bi. Margareth Ikongo  na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB Bi. Ineke Bussemaker baada ya kuzindua rasmi Makao Makao Makuu ya Kanda ya Kati ya benki hiyo yaendayo kwa jina la Tawi la Kambarage barabara ya Chimwaga mijini Dodoma leo April 23, 2018 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Waziri wa Fedha Dkt. Ashatu Kijaji, Naibu Gavana Mkuu wa Benki ya Tanzania Dkt. Bernard Kibesse, Mkurugenzi wa Bodi ya NMB Bi. Margareth Ikongo  na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB Bi. Ineke Bussemaker pamoja na wafanyakazi wa benki hiyo  na viongozi wengine baada ya kuzindua rasmi Jengo la PSPF Plaza na Makao Makao Makuu ya Kanda ya Kati ya benki hiyo yaendayo kwa jina la Tawi la Kambarage barabara ya Chimwaga mijini Dodoma leo April 23, 2018. Picha na IKULU

Awamu Ya Tano Uwanjani By Ngoma Africa Band based in Germany

SHILOLE : "Masogange Atafurahi Kuona nikipika Msibani"

ALICHOONGEA MAKONGORO NYERERE WAKATI WA UZINDUZI WA TAWI LA BENKI YA NMB DODOMA

TFDA,TBS WAINGIA MAKUBALIANO KUFANYA KAZI KWA PAMOJA KUELEKEA TANZANIA YA VIWANDA

0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

MAMLAKA ya Chakula na Dawa (TFDA),imeingia makubaliano ya miaka mitatu na Shirika la Viwango nchini (TBS) katika kufanya kazi kwa ushirikiano kuhakikisha wajasiriamali na wafanyabiashara wanahudumiwa katika kukuza kazi zao.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salam na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Agness Kejo wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa pamoja kati ya watendaji wa TFDA na TBS,ambapo amesema amesema kuwa changamoto za wafanyabishara na wajasiriamali ni vema zikapatiwa ufumbuzi wake ili watimize malego yao kwa maslahi ya Taifa.

Amefafanua kwenye ujenzi wa viwanda nchini kunategemea mashirika ya TBS na TFDA katika kuviwezesha viwanda nchini kuzalisha bidhaa bora na hatimaye kuwa na uhakika wa soko la ndani na nje ya nchi.

Amesisitiza hakuna sababu ya mjasiriamali au mfanyabishara kutumia muda mwingi kupata huduma kutoka TBS au TFDA , hivyo ni vema wakashirikiana katika kuondoa changamoto ambazo zipo na huenda zinakwaza wadau hao muhimu katika maendeleo ya nchi

Kejo ameongeza watendaji katika pande mbili hizo ni lazima waendane na azma ya Serikali ya kuwa Tanzania ya viwanda kuwasaidia afanyabiashara na wajasiriamali kupata elimu kuhusu bidhaa watazozalisha kwa kuzingatia ubora.Aidha amesema ushirikiano huo umefanyika na shirika la Viwango 
Zanzibar ikiwa ni kujenga Tanzania kwa pamoja katika kufikia uchumi wa kati watanzania.
 Kaimu Mkurugenzi Mkuu  wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Agness Kejo akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo kati watendaji wa TFDA na TBS katika vituo vya kanda na ipakani kufanya kazi kwa ushirikiano kutokana na makubaliano yaliyofikiwa na taasisi hizo,  jijini Dar es Salaam.
 aimu Mkurugenzi wa Usalama wa Chakula  (TFDA), Justin Makisi akizungumza kuhusiana na ufunguzi na mada zitakazojadiliwa katika kufanya kazi kama timu, jijini Dar es Salaam.
03. Kaimu Mkurugenzi Mkuu  wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Agness Kejo akiwa katika picha ya pamoja watendaji wa TFDA na TBS

Waziri Mhagama ampa Maagizo Msajili wa Vyama vya Siasa Utekelezaji Ripoti ya CAG

MICHUZI TV: MC PILI PILI AFUNGUKA HAYA KIFO CHA AGNESS MASOGANGE..

MICHUZI TV: ISRAEL KUSHIRIKI KATIKA MAPINDUZI YA UCHUMI WA VIWANDA NCHINI...


Rais Magufuli Aitaka Bodi ya NMB kuangalia Upya Gawiwo Linalotolewa kwa Serikali

0
0


Na: Lilian Lundo – MAELEZO, Dodoma.

Rais Dkt. John Pombe Magufuli ameiagiza Bodi ya National Microfinance Bank (NMB) pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo kuangali kiasi cha gawiwo kinachotolewa na benki hiyo, kutokana na kiasi hicho kutoongeza ndani ya miaka mitatu mfululizo.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo Mjini Dodoma wakati alipokuwa akifungua jengo jipya la Mfuko wa Pensheni wa Watumishi wa Umma (PSPF) pamoja na tawi jipya la NMB Kambarage lililoko katika jengo hilo.

“Kuna mambo mazuri mengi yaliyofanywa na NMB lakini tunahitaji uhakiki wa gawiwo linalotolewa kwa Serikali, kutokana na gawiwo hilo kutopanda kwa miaka mitatu mfululizo tangu mwaka 2014/2015 mpaka mwaka 2016/2017 ambapo benki hiyo imekuwa ikitoa shilingi Bilioni 16.525 kama gawiwo la hisa ya asilimia 32 iliyonayo katika Benki hiyo,” alisema Rais Magufuli.
Ameendelea kwa kusema, ni matumaini yake kuwa kiasi hicho cha fedha kitapanda kwa mwaka 2017/2018 kutokana na benki hiyo kutengeneza faida kila mwaka. 
Aidha, Rais Magufuli ameipongeza benki ya NMB kwa kuwa na matawi mpaka vijijini pamoja na kutoa ajira kwa zaidi ya Watanzania 3000 na kutoa misaada ya kijamii ikiwemo madawati 600, kompyuta 300 kwa shule za Sekondari na vitanda vya wagonjwa.
Vilevile Rais Magufuli ameupongeza mfuko wa PSPF kwa kuona fursa ya Serikali kuhamia Dodoma na kujenga jengo ambalo limeboresha na kupendezesha mandhari ya Dodoma ambapo pia ujenzi huo umetoa ajira kwa Watanzania takribani 250.Pia amesema, mfuko huo umekuwa ukitoa mikopo kwa wanachama wake pamoja na kuwekeza katika ujenzi wa viwanda mbalimbali ikiwa ni pamoja na kiwanda cha cha Sukari Kagera, kiwanda cha nguo na turubai vilivyopo mkoani Morogoro.
Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge amesema Rais Magufuli kupitia TAMISEMI ametoa shilingi bilioni 70 kwa ajili ya ujenzi mbalimbali wa miundombinu mkoani Dodoma.Dkt. Mahenge ametaja miundombinu hiyo kuwa ni pamoja na ujenzi wa stendi mpya ya kisasa yenye uwezo wa kuingia mabasi makubwa 250, magari madogo 600 pamoja na bajaji na bodaboda 300 kwa wakati mmoja.
Aidha, Dkt Mahenge ameitaja miundombinu mingine ambayo ni ujenzi wa soko la kisasa, sehemu ya kupaki malori, miundombinu ya majitaka, maeneo ya kupumzikia pamoja na kuboresha miundombinu ili kuondoa msongamano wa magari.kwa upande wake, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji ameutaja mfuko wa PSPF kuwa ndio mfuko wa kwanza kuwekeza katika vitega uchumi Makao Makuu ya Nchi ukiondoa mfuko wa LAPF ambao Makao Makuu yake yapo Mkoani Dodoma.
Jengo la PSPF ni moja ya majengo marefu yaliyoko mkoani Dodoma ambapo ina jumla ya ghorofa 11 pamoja na eneo la maegesho ya magari 161 ambapo mpaka sasa jengo hilo limeshapata wapangaji kwa asilimia 100.

BABA WA AGNESS MASOGANGE ASHANGAA KILICHOMUUA MWANAE...

Happy birthday Sensei Fundi Rumadha

0
0
I wish you will receive all best things in the world in the coming years, and fulfil all your dreams. Wish you a very happy birthday my Sensei!
- Ankal

MICHUZI TV: TUKIO ZIMA LA MAZISHI YA MASOGANGE, WIMBO WA BELLE 9 WAZUA GUMZO MSIBANI..

Water as an immediate energy solution for Tanzania

0
0
It is common knowledge that water sustains alllife on Earth and that nothing can be grown or survivewithout it. When used effectively, water can also provideclean electricityfor millions of people. In this review, we will discuss how it can be done without affecting the environment and why it is so important to us in Tanzania. 
Tanzania has abundant energy sources, most of which remain unexploited. Hydro has traditionally played a significant role, with an installed capacity of 562 MW, which accounts for roughly one-third of the total installed power capacity. With a hydro potential of 4.7 GW, the country plans to further development this source, but views weak transmission infrastructure as a significant short-term barrier.

Only 41% of the population currently has access to electricity. Low population density and expensive transmission costs have led to the government adopting targeted policies to develop off-grid schemes in order to increase the current levels of rural electricity access.


Power where it is needed

Minihydro power planttechnology available today may serve as an important alternative to traditional large scale hydro power generationinTanzania, because the resources of minor water streamsare practically omnipresent. Mini hydro power plantsare quick, cost effective and simple to installand maintain, and supplyecologically clean and affordableelectricity.Hungarian companyGANZ EEM, a subsidiary of state owned Russian nuclear corporation Rosatomrecently presented an innovative portable mini hydro power plant for the African market. The containerisedunits are easy to transport and are great forelectricity generation in remote areas.

Rosatom Central and Southern Africa regional vice-president Dmitry Shornikov notes that, “Rosatom offer numerous energy solutions for African countries and one of the most promising is our innovative containerized mini-hydropower plant, with a design capacity of up to 2 MW. A single facility is capable of providing electricity to between 250 and 400 houses for roughly 40 years”.

The mini hydro plants which have a life span of roughly 40 years and a warranty of 12 years can be monitored and operated remotely from anywhere in the world. The plantswhich operate at a 93% capacity factor requireminimalhead, and do not require dam construction and therefore cause no environmental harm to river and other reservoir ecology.

Mini Hydro plantsare able to meet electricity requirements for residential, retail and corporate consumers in remoteareas where central supplies are not available or where transmission lines aredifficultor costly to install.

Mini Hydro plants are also an excellent alternative to inefficient, costly and ecologically unfriendly diesel generators. The units can be installed inline of existing pipelines and are therefore also perfect for the mining and manufacturing sectors, particularly those that use a great deal of water. The plants dramatically reduce electricity costs and ultimately reduce production costs, making local products more cost effective on the global market.

MTOTO AMEPOTEA

Wakazi Dar, Mtwara kuanza kunufaika na Huduma ya Usambazaji Gesi yenye Punguzo ya bei ya Asilimia 40


Serikali kuanza kutoa hati za viwanja kwa njia ya kielektroniki

WANAWAKE WA GAIRO WAUNGA MKONO JUHUDI ZA RAIS MAGUFULI KATIKA KUANZISHA VIWANDA

0
0
Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Siriel Mchembe akipongezwa na mchungaji Canon Chamwenye wa kanisa Anglikana Msingisi mara baada ya kumaliza kuongea na akina mama juu ya kuanzisha kiwanda ili waweze kujikwamua katika maisha yao.
Mmoja ya akinamama akitoa shukrani ya kuku kwa mkuu wa wilaya ya Gairo, Siriel Mchembe. Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Siriel Shaidi Mchembe afanikisha ushawishi wa ujenzi wa viwanda kwa kuanzia na wanawake kanisa la Anglikana Dinari ya Rubeho Gairo. Ushawishi huo ulianza mwezi wa sita mwaka 2017 ambapo Mhe. Mchembe alihudhuria mkutano wa wanawake wa kanisa hilo akiwa Mgeni Rasmi. 

 Katika mkutano huo Mhe. Mchembe aliwashawishi akinamama hao kupitia umoja wao waanzishe kiwanda ili kiwainue kiuchumi. Aidha wapate mahali pa kuuza mbegu za alizeti ambazo kwa sasa alizeti ni kati ya mazao makuu ya biashara wilayani Gairo. 

 Hatimaye mpango umekamilika na Mhe. Mchembe amechangia pesa za Kitanzania shilingi laki tano kuhamasisha ujenzi wa kiwanda. Jumla ya gharama ya mradi ni shilingi milioni kumi na tisa. Majengo yanaendelea kufunguliwa na mradi unategemewa kuanza mwishoni mwa mwaka 2018. Mkuu wa Wilaya aliwashukuru wana Dinari hiyo iliyojumuisha Kata ya Rubeho na Msingisi. Wanawake ni nguzo ya Maendeleo na uchumi wa viwanda.

Mafundi mitambo wa redio jamii watakiwa kutumia nafasi zao kuleta mabadiliko

0
0
Na Mwandishi wetu
Washiriki wa mafunzo ya ufundi mitambo ya kurushia matangazo ya redio ambayo yameshirikisha mafundi kutoka redio jamii 25 zilizopo Tanzania Bara na Zanzibar wametakiwa kutumia vyema mafunzo ili yakalete mabadiliko katika maeneo yao ya kazi.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Idara ya Ufundi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Mwandisi Upendo Mbele wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo ya siku saba ambayo yameandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO).

Mbele alisema mafunzo hayo ni muhimu kwa kuwa yatawapa uwezo wa kujua vifaa ambavyo wanavitumia katika vituo vyao na hivyo ni vyema wakayatumia vizuri ili yalete mabadiliko katika maeneo ya kazi.

"Ukiwa fundi mafunzo ni lazima, tuwashukuru UNESCO kuandaa mafunzo haya na nyie mtumieni muda wenu vizuri mkiwa hapa. Lengo kuu la kuwa hapa ni kujenga na kuboresha kile kitu ambacho hakikuwepo, unavyokuwa na upana zaidi na wewe utakuja kuwa mwalimu kwa wengine," alisema Mbele na kuongeza.
 Mkurugenzi wa Idara ya Ufundi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Mwandisi Upendo Mbele wakati wa uzinduzi wa mafunzo ya ufundi mitambo ya kurushia matangazo ya redio kwa mafundi mitambo wa redio jamii 25 kutoka Tanzania Bara na Zanzibar ambayo yameandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO).
 Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya ufundi mitambo ya kurushia matangazo ya redio kwa mafundi mitambo wa redio jamii 25 kutoka Tanzania Bara na Zanzibar ambayo yameandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO).
 Washiriki wa mafunzo ya ufundi wa kurushia matangazo ya redio kwa mafundi mitambo wa redio jamii 25 kutoka Tanzania Bara na Zanzibar wakipewa maelezo kuhusu matumizi ya mitambo hiyo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

RAIS MAGUFULI AUFAGILIA MFUKO WA PENSHENI WA PSPF KWA UWEKEZAJI WENYE TIJA DODOMA

0
0




NA K-VIS BLOG/Khalfan Said, Dodoma


RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, amefurahishwa na uwekezaji uliofanywa na Mfuko wa Pensheni wa PSPF wa kujenga jingo la kitegauchumi mkoani Dodoma.

Kilichomfanya Rais Magufuli kufurahishwa na uwekezaji huo ni kuona jengo hilo lenye ghorofa 12 tayari limepangishwa kwa asilimia 100 hata kabla ya uzinduzi rasmi uliofanyika Aprili 23, 2018.

“Ninyi mmemaliza tu tayari asilimia 100, mliangalia kwamba Dodoma ni makao makuu na mahitaji ya nahitajika kwa ajili ya majengo, hongereni sana kwa kupanga mikakati yenu vizuri kisayansi.” Alisema Dkt. Magufuli na kutoa hakikisho, “Pamoja na kuunganishwa kwa Mifuko hii ya Hifadhi ya Jamii ninyi wafanyakazi wa PSPF mjihesabu kuwa hamtapoteza nafazi zenu, lakini pia jengo hili limeboresha na kupendezesha mandhari ya Dodoma ambako ni makao makuu ya nchi yetu.” 

Alisema Rais Magufuli wakati akihutubia kwenye uzinduzi wa jengo hilo uliokwenda sambamba na ufunguzi rasmi wa makao makuu ya NMB Bank (Kambarage) ambao ni miongoni mwa wapangaji wakubwa kwenye jingo hilo lililoko barabara ya kuelekea chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM). 

Rais pia alifurahishwa na ushiriki wa watanzania katika ujenzi wa jengo hilo.“Nimefurahi kusikia kuwa jingo hili limesanifiwa na ujenzi wake kusanifiwa na watanzania, ma contractors na consultants na kwamba takriban watanzania 250 walipata ajira wakati wa ujenzi.” Alipongeza. 
Rais wa Jamhuri ya Muunganio wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli mwenye mkasi), akiungana na baadhi ya mawaziri na viongozi wengine kukata utepe ikiwa ni ishara ya uzinduzi rasmi wa jingo la kitegauchumi la Mfuko wa Pensheni wa PSPF, (PSPF DODOMA PLAZA), mjini humo Aprili 23, 2018. Jengo hilo lenye urefu wa ghorofa 12, tayari limepangishwa kwa takriban asilimia 100.
Rais Magufuli, akimpongeza Mkurugenzi Mkuu wa PSPF, Bw. Adam Mayingu, mara baada ya kufunua kitambaa ikiwa ni ishara ya uzinduzi rasmi wa jingo la kitega uchumi la Mfuko huo mjini Dodoma.
Hili ndio jingo la PSPF DODOMA PLAZA lenye ghorofa 12 lililozinduliwa na Rais John Magufuli mjini Dodoma.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, akitoa hotuba yake.
Baadhi ya Mawaziri na Naibu Mawaziri, kutoka kushoto, Mhe. Luhaga Mpina (Waziri wa Mifugo na Uvuvi), Mhe.Juliana Shonza, (Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo), Mhe. Profesa Joyce Ndalichako, (Waziri wa Elimu) na Mhe.Jumaa Aweso, (Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji).
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama, (kulia), akimpongeza Mkurugenzi Mkuu wa PSPF, Bw. Adam Mayingu, mwishoni mwa hafla hiyo.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

WAZIRI MHAGAMA AMTAKA MSAJILI WA VYAMA KUCHUKUA HATUA KWA VYAMA VINAVYOKIUKA SHERIA NA MIONGOZO ILIYOPO

0
0
Waziri wa Nchi Ofisi anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama amemuagiza Msajili wa vyama vya Siasa kuchukua hatua kwa vyama vinavyokiuka sheria na miongozo ya vyama vya siasa.

Ametoa kauli hiyo Aprili 23, 2018 alipokuwa akitoa maelezo ya ufafanuzi juu ya hoja za ofisi yake, zilizoainishwa katika Ripoti ya Mthibiti na Ukaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Mwaka wa fedha unoishia Juni 30, 2018 alipokutana na  waandishi wa habari Bungeni Dodoma.

Waziri Mhagama ameelekeza kuhakikisha vyama vyenye mapungufu upande wa hesabu zao basi wawasilishe kwa Msajili wa vyama ndani ya wiki 3 hadi 4.

“Namtaka Msajili wa Vyama achukue hatua za Kisheria pasi kusita kwa chama chochote kinachokiuka sheria ya vyama vya siasa Na. 2 ya mwaka 1992”.alisema Waziri Mhagama

Aidha amemtaka Msajili wa Vyama vya siasa nchini kuhakikisha anaweka miongozo na mpango kazi ili vyama vilivyozoea kutowasilisha hesabu zao viache mara moja kwa mujibu wa sheria.

Waziri Mhagama aliongezea kuwa taarifa ya Mthibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ilibaini mapungufu kadhaa katika uendeshaji wa vyama vya siasa ikiwemo; Upungufu katika hesabu zilizowasilishwa chini ya viwango vya Kimataifa vya uandaaji wa hesabu katika sekta za umma na baadhi ya vyama kushindwa kuwasilisha hesabu zao kwa CAG kwa ukaguzi

Pamoja na hayo alibainisha kuwepo kwa vyama vya kisiasa visivyotumia rejista ya mali za kudumu ambapo vyama vinne ikiwemo;CHADEMA, NLD,ADC na Demokrasia Makini havina Daftari la kudumu la mali zao ikiwa ni kinyume na sheria zilizopo.
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama akizungumza na waandishi wa habari juu ya Ufafanuzi wa Hoja za ofisi yake zilizoainishwa katika Ripoti ya  Mthibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Mwaka wa fedha unoishia Juni 30, 2018 Bungeni Dodoma.
 Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia mkutano ulioandaliwa na Idara ya Habari Maelezo, Kwa Mawaziri walipokutana kutoa ufafanuzi kwa baadhi ya hoja zilizoainishwa katika Ripoti ya Mthibiti na Ukaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Mwaka wa fedha unoishia Juni 30, 2018.
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama akiteta jambo na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe.William Lukuvi wakati wa mkutano na waandishi wa habari Dodoma Aprili 23, 2018.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo, ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt.Hassan Abbas akizungumza na waandishi wa habari Bungeni Dodoma. (PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Viewing all 109602 articles
Browse latest View live




Latest Images