Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110181 articles
Browse latest View live

UVCCM YAVUNA WANACHAMA 350 CHUO KIKUU DAR ES SALAAM

$
0
0

Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Kheri James amepokea jumla ya Wanachma wapya 350 katika Kongamano Maalum lililoandaliwa na Tawi la Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam.

Kheri amewataka Vijana wanaopata nafasi za uongozi kuitumia nafasi hiyo kwa ajili ya kuwakomboa wengine na kuacha kutumika na makundi ya watu.

“Vijana wengi ambao wameaminiwa wameacha kushughulika na matatizo ya Vijana na yenye tija kwa taifa, wamekuwa wakiendeshwa na watu ambao wanamaslahi yao binafsi” amesema Kheri

Amesema kuwa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi imeweza kuwaamini Vijana, hivyo kila kijana wa CCM  anabudi kuwaunga mkono viongozi wote Vijana ambao wana nia ya dhati ya kutaka kulifikisha taifa hili pale linapotakiwa liwe.

Alimaliza kwa kutoa wito kwa Vijana wote kujitokeza kwa wingi kushiriki katika Chaguzi ndogo zinazoendelea na kuifanya CCM ishinde kwa kishindo.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Chama Cha Mapinduzi(UVCCM),Kheri James akizungumza na Wanachama wa Umoja huo Tawi la Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam katika ukumbi wa Urafiki leo jijini Dar Es Salaam .
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Shaka Hamdu Shaka, akisalimiana na Mmoja ya Wanachama wapya waliojiunga na Chama hicho kupitia Tawi la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Sehemu ya wanachama wapya 350 waliojiunga na Chama cha Mapinduzi Tawi la Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam Wakila Kiapo cha Uaminifu.


INTRODUCING NEW SINGLE "KABAKA" BY SAIDA KAROLI

MICHUZI BEAT: "JINA LA MR. KESHO NILIPATA BAADA YA USUMBUFU WA MASHABIKI NA MAPRODUCER" - MR. KESHO

INTRODUCING Isha Mashauzi - Nibembeleze (Official Video)

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JANUARI 21, 2018

FAWOPA yapiga Msasa Wadau wa Elimu-Mtwara.

$
0
0

Shirika lisilokuwa la kiserikali la faidika wote pamoja FAWOPA limetoa Elimu kwa Wadau Mbalimbali wa sekta hiyo Juu ya uandaaji wa Bajeti na kuweza kuwasilisha kwa kamati za Shule, ili kuzifanyia kazi Kwa lengo la kuondokana na migongano inayojitokeza baina ya Wazazi na Walimu.

Mratibu wa shirika hilo Baltazar Komba amesema Bado viwango vya Bajeti mashuleni haijaainisha, matokeo yake Shule Nyingi wamekuwa wakitegemea wazazi kwa ajili ya michango kabla ya Mh. Rais John Pombe Magufuli kukataza Michango yoyote Mashuleni.

Aidha katika Ufuatiliaji uliofanywa na Kamati ya FAWOPA ndani ya Manispaa ya Mtwara Mikindani imebaini kuwa Halmashauri haina Bajeti maalum ya Elimu zaidi ya Bajeti kutoka Serikali Kuu.

Lengo la mkutano huo ni kuhakikisha manispaa hiyo inapiga hatua katika suala la elimu kutokana mkoa was Mtwara kuwa nyuma katika Ufaulu ukilinganisha na mikoa mwingine.
 Pichani ni mratibu wa shirika lisilokuwa la kiserikali la faidika wote pamoja FAWOPA iliyopo Mkoani  Mtwara  Baltazar Komba akizungumza na wadau mbali mbali wa elimu juu ya Uboreshwaji wa Elimu mkoani Humo.
Mshauri wa Mambo ya Kisheria FAWOPA Marythereza Namangi akitoa mafunzo kwa Wadau Mbalimbali wa Elimu Juu ya uandaaji wa Bajeti katika mashule kama Moja ya dhana ya Uwazi na Uwajibikaji.

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AMTEMBELEA MAMA MARIA NYERERE NA KUTOA HESHIMA KWENYE KABURI LA BABA WA TAIFA

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakizungumza na Mama Maria Nyerere wakati walipomtembelea nyumbani kwake Mwitongo, Butiama Januari 20, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakiongozana na Mama Maria Nyerere kuingia kwenye uwanja wa Mwenge katika mkutano wa hadhara uliohutubiwa na Waziri Mkuu katika kijiji cha Butiama Januari 20, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mama Maria Nyerere wakati alipomtembelea nyumbani kwake Mwitongo, Butiama Januari 20, 2018. Kulia ni mkewe Mary .
Mke wa Waziri Mkuu, Mama Mary Majaliwa akiwasha mshumaa kwenye kaburi la Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere eneo la Mwitongo, Butiama, Januari 2018. Wapili kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima na kushoto ni mkewe Naima .
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakiweka shada la maua kwenye kaburi la Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere eneo la Mwitongo, Butiama Januari 20, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa , Mkewe Mary na Mama Maria Nyerere wakiwapungia wananchi katika mkutano wa hadhara uliohutubiwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa katika uwanja wa Mwenge kijijini Butiama Januari 20, 2018.

MKUU WA MAJESHI YA ULINZI JENERALI MABEYO AKAGUA UHARIBIFU WA MIUNDOMBINU YA RELI KILOSA MKOANI MOROGORO

$
0
0
Na. Andrew Chimesela – Morogoro

Hali mbaya ya mafuriko yanayoendela kuathiri wananchi wa Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro yamemfanya Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Generali Venance Mabeyo kufika Kilosa na kutembelea baadhi ya maeneo yaliyoathirika ili kutafuta ufumbuzi wa pamoja wa kuokoa maisha ya wananchi wa maeneo hayo na mali zao.

Generali Mabeyo aliwasili Kilosa Januari.19, 2018 majira ya jioni na kuungana na mwenyeji wake Dkt. Kebwe Stephen Kebwe Mkuu wa Mkoa wa Morogoro aliyepiga kambi Wilayani humo kwa ajili ya mafuriko hayo kisha bila kujali mvua iliyokuwa inaendelea kunyesha muda wote wakatembelea baadhi ya maeneo yaliyoakuwa yamethiriwa ili kuona hali halisi ya mafuriko hayo.

Kwenye kikao cha majumuisho Mkuu huyo wa Majeshi nchini alishauri kuwa ili kutatua changamoto hiyo inatakiwa nguvu ya ziada na ya pamoja kwa taasisi zote kuungana, Ikiwa ni pamoja na taasisi mbali ili kuweza kuokoa maisha ya watu, mali zao pamoja na miundombinu iliyoathiriwa.

Hata hivyo alisema changamoto hiyo inatakiwa kuwe na mpango wa muda mfupi, muda wa kati na muda mrefu. Amesema suluhisho la mpango wa mda mfupi ni kuwa na kazi ya dharura, na kazi hiyo ya dharura inahitajika kuwepo na mpango wa dharura ambao ni kuokoa maisha ya watu waliozingirwa na maji ili wasiendelee kukosa huduma za kijamii na pia kuathiri afya zao kwa kunywa maji ambayo si salama.Pamoja na kuwepo kwa wazo la kurekebisha tuta la mto Mkondoa ikiwa ni mpango wa muda wa kati ili maji hayo yafuate mkondo wake lakini pia Generali Mabeyo ameshauri kuangalia namna ya kupunguza kasi ya maji hayo kuanzia yanakotoka kwa kujenga mabwawa ikiwa ni mpango wa muda mrefu.

“Maji haya yanakuja huku ni kama sisi ni waathirika zaidi lakini yanakoanzia hatujui hali iko namna gani, pengine katika mpango wa muda mrefu ingetazamwa namna ya kuyapunguza haya maji kasi yake.Sasa katika kuyapunguza, taasisi mablimbali zina wataalamu ambao wanaweza kusaidia kuweza kujenga mabwawa makubwa huko yanakoanzia ili haya maji kupunguza kasi yake kabla hayajafika huku” alisema Generali Mabeyo.

Akitoa maelezo ya awali Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Stephen Kebwe amesema tuta hilo la mto Mkondoa lilijengwa enzi za Mkoloni kama kinga kwa mji wa Kilosa na kwa mara ya kwanza lilipasuka mwaka 2010. Ujenzi wake kuanzia hapo haukukamilika vizuri kutokan na hali ya kifedha na sasa limepasuka baada ya Mvua nyingi kunyesha kuamkia Jan,11 mwaka huu.

Hata hivyo Dkt. Kebwe ametoa Ombi kwa Mkuu huyo wa Majeshi, kupata nguvu kazi ya wananjeshi, vifaa na utaalamu wao ili baada ya mvua hizi kupungua waendelee na kutafuta mbinu ya kuuongozo mto Mkondoa uweze kupita katika sehemu yake ya awali na hivyo kutoathiri wananchi, mali zao na miundombinu iliyopo eneo hilo .
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dk Steven Kebwe akimuongoza Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo kushoto na Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mh. Adam Mgoyi katikati wakati walipokagua athari za uharibifu wa madaraja, Mashamba na nyumba za wananchi kufuatia mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa zinazonyesha wilayani Kilosa mkoani Morogoro.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dk Steven Kebwe akitoa maelezo kwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo katikati na Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mh. Adam Mgoyi kushoto wakati walipokagua athari za uharibifu wa madaraja, Mashamba na nyumba za wananchi kufuatia mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa zinazonyesha wilayani Kilosa mkoani Morogoro
Maji yakiwa yametapakaa kandokando ya Reli ya kati na kusababisha uharibifu mkubwa wa reli, Mashamba pamoja na nyumba za wananchi.
Madaraja yakiwa katika hatari ya kusombwa kutokana na mvua hizo


SERIKALI YA JAPAN YAAHIDI KUENDELEA KUSAIDIA MIRADI YA UMWAGILIAJI NCHINI

$
0
0
Kaimu Mkuu wa Chuo cha Ufundi Arusha(ATC),Dk Masudi Senzia(kushoto) akimshukuru Balozi wa Japan nchini Tanzania,Mh. Masaharu Yoshida baada ya kuweka jiwe la msingi katika shamba la mafunzo ya Uandisi,Ujenzi na Umwagiliaji.
Miundombinu ya umwagiliaji kwenye shamba lenye ukubwa wa eka 150 litawezesha kupata wahitimu walioiva kivitendo 
Baadhi ya wanachuo wakitoka kwenye darasa la mafunzo kwa vitendo.
Balozi wa Japan nchini Tanzania,Mh. Masaharu Yoshida(katikati) akifatiwa nyuma na Kaimu Mkuu wa Chuo cha Ufundi Arusha(ATC),Dk Masudi Senzia kukagua bwawa linalotumika kwaajili ya kukinga maji ya mvua na kuyatawanya kwenye mashamba ya mafunzo.
Mkurungezi wa Elimu ya Ufundi nchini,Mhandisi Thomas Katebelirwe akizungumza katika halfa hiyo.
Makamu Mkuu wa Chuo cha ATC anayeshughulikia Utawala,Fedha na Mipango,Dk Erick Mgaya akizungumza umuhimu wa shamba hilo ambalo litasaidia kuwapata wataalamu waliobobea nchini katika fani ya umwagiliaji.

Waandishi wa Habari wa Dodoma Kupewa Kipaumbele Katika Mafunzo ya Kuwajengea Uwezo.

$
0
0
Na. Lilian Lundo – MAELEZO, Dodoma.

Serikali kupitia Idara ya Habari ya MAELEZO imesema itatoa kipaumbele kwa waandishi wa habari wa Dodoma kwa kuwapa mafunzo ya kuwajengea uwezo kutokana na mkoa huo kuwa na matukio mengi ya Kitaifa na Kimataifa pamoja na kutembelewa na wageni wa Kimataifa.

Hayo yameelezwa leo mjini Dodoma na Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi alipokuwa akiongea wakati wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Waandishi wa Habari Kanda ya Kati (The Central Press Club (CPC)).

“Nawathibitishia kuwa Serikali sasa iko Dodoma, Dunia sasa inategemea kusikia mambo mengi kutoka Dodoma. Shughuli za Kitaifa na Kimataifa zitakuwa zikifanyika hapa Dodoma ,” alisema Dkt. Abbasi.

Amesema mkoa huo utakuwa unapokea wageni mbalimbali wa Kimataifa hivyo ni lazima waandishi wa habari wa mkoa huo wawe na uelewa wa mambo ya Itifaki na diplomasia ili kuwasaidia katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku.“Lazima tubadilike hata katika uvaaji wetu, kwani sasa tunaenda kukutana na viongozi wakubwa wa nchi na wa Kimataifa,” aliongeza Dkt. Abbasi.

Aidha amesema, Idara ya Habari MAELEZO itaandaa mafunzo mafupi katika maeneo mbalimbali ya tasnia ya habari ikiwemo masuala ya itifaki na mambo ya diplomasia ili kuwajengea uelewa waandishi hao.Hata hivyo, Dkt. Abbas amesema Idara yake itatafuta ufadhili kwa mabalozi mbalimbali yaliyopo hapa nchini ili waandishi hao wakajifunze namna vyombo vya habari vya Kimataifa vinavyofanya kazi.

“Mwaka 2017 tulifanikiwa kupata ufadhili wa ubalozi wa China na waandishi Kumi walienda China, Bado hatujajua ni waandishi wangapi watafanikiwa kwenda mwaka huu, lakini tutao kipaumbele kwa waandishi wa habari walioko Dodoma,” alisisitiza Dkt. Abbasi.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge akifungua mkutano mkuu wa mwaka wa chama Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Dodoma uliofanyika mapema leo mjini Dodoma.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akizungumza na wanachama wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Dodoma wakati wa mkutano mkuu wa mwaka wa chama hicho uliofanyika mapema leo mjini Dodoma.
Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma Bw. Edwin Kunambi akizungumza wakati wa mkutano mkuu wa chama cha waandishi wa habari Mkoa wa Dodoma uliofanyika mapema leo mjini Dodoma.

FIGISU FIGISU KAMA HIZI KWENYE SOKA LETU,MPAKA LINI.!?

$
0
0
 Na Hafidh Kido, Moshi.

KWA nafasi yangu ya msemaji wa timu ya Coastal Union 'Wagosi wa Kaya' ninatakiwa kusafiri na timu popote iendapo lakini kutokana na majukumu mengine nashindwa kutenda haya.

Lakini nilijiapiza mechi baina ya Wagosi na Polisi Tanzania iliyochezwa mjini Moshi katika uwanja wa Chuo cha Ushirika lazima niende. Kwa bahati ikatokea dharura ya kifamilia nikapata ruhusa kibaruani nami nikahudhuria.

Kwa wiki kadhaa sasa kumekuwepo na maneno kuwa Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), anaikingia kifua Coastal Union kwa sababu ni mwenyeji wa Tanga lakini pia aliwahi kushika nyadhifa mbalimbali za kiuongozi kwenye klabu hiyo kongwe ya jijini Tanga iliyoanzishwa mwaka 1948.

Kama hiyo haitoshi ikaelezwa kuwa kikosi cha Coastal Union kinacheza soka kwa kubebwa waamuzi ambao wanapokea maagizo kutoka TFF.

Yamezungumzwa mengi, itoshe tu kusema baadhi ya klabu zinazoshiriki Ligi ya soka Daraja la kwanza wamekuwa na malalamiko ya mara kwa mara kudai Coastal Union inabebwa.

Nimeamua kuja kushuhudia 'kubebwa' kwa Coastal Union. Naomba nitangaze maslahi kabla sijaendelea na andiko hili nililoliandika saa nane usiku wa kuamkia Jumapili Januari 21, 2018 nikiwa chumba cha hoteli Mjini Moshi Mkoa wa Kilimanjaro.

Mimi ni shabiki wa Coastal Union lakini pia ni mwanahabari. Hivyo naandika kwa jicho la kihabari lakini naweza kuteleza nikaweka unazi katika andiko hili. Nipo tayari kukosolewa na hata kuzodolewa ikiwa nitaandika uongo au kuongeza chumvi.

Hadi naandika haya msimamo wa kundi B inayojumuisha timu nane yaani Coastal Union, Polisi Tanzania, JKT Mlale, Kinondoni Manicipal (KMC), Mbeya Kwanza, Mufindi United, Mawenzi Market na Polisi Dar es Salaam.

Coastal Union ilikuwa inaongoza kundi kwa jumla ya alama 22, ikifuatiwa na Polisi Tanzania (21), JKT Mlale (21), KMC (19), Mbeya Kwanza (16), Mufindi Utd (12), Mawenzi Market (7) na Polisi DSM (3).

Kwa namna yoyote ile Polisi Tanzania wameumizwa na suluhu tuliyowalazimisha katika uwanja wao. Hivyo walijiandaa kwa hali yoyote iwayo kuhakikisha tunawaachia alama tatu muhimu kwao ili kujihakikishia kupanda Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara.

SEKTA BINAFSI YARIDHISHWA NA UHUSIANO WAKE NA SERIKALI

$
0
0

Na Benny Mwaipaja-WFM, Dodoma

Sekta Binafsi nchini imekiri kuwa uhusiano kati yake na Serikali umezidi kuimarika kutokana na kuboreshwa kwa mazingira ya uwekezaji na ufanyajibiashara hapa nchini kuliko ilivyokuwa hapo awali na kwamba hatua hiyo itachochea ukuaji wa uchumi wa nchi.

Kauli hiyo imetolewa mjini Dodoma na Makamu Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF), Bw. Salum Shamte, wakati wa mkutano wa tatu kati ya Sekta Binafsi na Sekta ya Umma uliojadili namna ya kukuza ushiriki wa Sekta Binafsi katika kukuza uchumi wa viwanda nchini.

“Sekta binafsi imenituma kuleta pongezi kwa Serikali inayoongozwa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa kutekeleza kwa vitendo utambuzi wa kwamba Sekta Binafsi ni mbia muhimu wa maendeleo ya Taifa letu” alisema Bw. Shamte.

Aliyataja baadhi ya mafanikio yanayo onekana bayana kuwa ni pamoja na kuinusuru Bandari ya Dar es Salaam kwa mabadiliko ya sheria ya fedha ya mwaka 2017 hasa kuondoa VAT kwenye biashara ya mizigo ya kimataifa na kuondokana na umoja wa forodha ambao ulipunguza kwa kiasi kikubwa kiwango cha biashara kati ya Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Bw. Shamte alisema kuwa majadiliano hayo kati ya Serikali na Sekta Binafsi kumeikoa sekta ya utalii hasa kwa kuondokana na kodi ya ongezeko la thamani (VAT) kwenye leseni mbalimbali hatua ambayo imerejesha msisimko wa sekta hiyo.

“Serikali imepunguza pia mlolongo wa kodi kwa wakulima, japokuwa – kazi haijakamilika lakini mwanzo ni mzuri” aliongeza Bw. Shamte.Alieleza kuwa jitihada mpya na nzuri za kutatua changamoto za kodi kwa kampuni zinazojihusisha na biashara kati ya Tanzania Bara na Visiwani, na kuanza kufanya malipo kwa wakandarasi na watoa huduma wa ndani hatua ambayo wanaamini itakuza matumizi ya ndani na mzunguko wa fedha.
Makamu Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF), Bw. Salum Shamte, akizungumza wakati wa mkutano wa tatu kati ya Sekta Binafsi na Sekta ya Umma uliojadili namna ya kuboresha masuala ya biashara na uwekezaji nchini, mjini Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) akifungua mkutano wa tatu kati ya Sekta Binafsi na Serikali uliofanyika mjini Dodoma.
Baadhi ya Wawekezaji na wageni kutoka Taasisi za Kimataifa walioshiriki Mkutano wa tatu wa majadiliano kati ya wadau wa Sekta Binafsi na Sekta ya Umma uliofanyika mjini Dodoma.
Baadhi ya Wafanyabiashara na Wawekezaji walioshiriki Mkutano wa tatu wa majadiliano kati ya wadau wa Sekta Binafsi na Sekta ya Umma uliofanyika mjini Dodoma.
Baadhi ya Wafanyabiashara na Wawekezaji walioshiriki Mkutano wa tatu wa majadiliano kati ya wadau wa Sekta Binafsi na Sekta ya Umma uliofanyika mjini Dodoma.

MAAFISA WA BUNGE WATOA ELIMU KWA SHULE ZA SEKONDARI ZILIZOPO MUSOMA MJINI.

$
0
0
Mkurugenzi Msaidizi na Mratibu wa Dawati la Bunge la Afrika kutoka Ofisi ya Bunge, Ndg. Lawrence Makigi, akisisitiza jambo wakati akitoa Elimu kwa Shughuli Mbali mbali zinazofanywa na Bunge la Tanzania kwa Shule za Sekondari za Musoma Mjini, katika tukio lililofanyika leo katika Shule ya Musoma Sekondari iliyopo Musoma Mjini. Kulia ni Afisa Elimu wa Manispaa ya Musoma Mjini, Ndg. Exavery Ntambala na kushoto ni Makamu Mkuu wa Shule ya Sekondari Musoma, Mwl. Kilonda Salum
Katibu Msaidizi Uhusiano wa Kimataifa kutoka Ofisi ya Bunge Ndg. James Sapali, akizungumza wakati akitoa Elimu kwa Shughuli Mbali mbali zinazofanywa na Bunge la Tanzania kwa Shule ya Musoma Sekondari pamoja na Shule ya Sekondari ya Songe, katika tukio lililofanyika leo katika Shule ya Musoma Sekondari iliyopo Musoma Mjini.
Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari ya wasichana ya Songe iliyopo Musoma Mjini akiuliza swali kwa Maafisa kutoka Ofisi ya Bunge pale Maafisa hao walipotembelea Shule ya Sekondari ya Musoma kwa ajili ya utoaji wa Elimu kwa Shughuli Mbali mbali zinazofanywa na Bunge la Tanzania, katika tukio lililofanyika leo katika Shule ya Musoma Sekondari iliyopo Musoma Mjini.
Wanafunzi wa Shule za Sekondari za Musoma na Songe wakimsikiliza Mkurugenzi Msaidizi na Mratibu wa Dawati la Bunge la Afrika kutoka Ofisi ya Bunge, Ndg. Lawrence Makigi (katikati) akizungumza wakati wa utoaji wa Elimu kwa Shughuli Mbali mbali zinazofanywa na Bunge la Tanzania, katika tukio lililofanyika leo katika Shule ya Musoma Sekondari iliyopo Musoma Mjini.
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya wasichana ya Songe pamoja na Shule ya Sekondari ya Musoma wakifuatilia maada inayotolewa na maafisa kutoka Ofisi ya Bunge wakati wa utoaji wa Elimu kwa Shughuli Mbali mbali zinazofanywa na Bunge la Tanzania uliofanyika leo katika Shule ya Musoma Sekondari iliyopo Musoma Mjini.

DKT. MWAKYEMBE AOMBA WATANZANIA KUSAIDIA MATIBABU YA WASTARA

$
0
0
Na Anitha Jonas – WHUSM

Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe ametoa wito kwa watanzania kujitokeza kumchangia msanii wa Filamu Wastara Issa ili aweze kwenda kupatiwa matibabu India ya mguu wake unaomsumbua.

Mheshimiwa Mwakyembe ametoa wito huo alipokwenda kumtembelea msanii huyo wa filamu nyumbani kwake leo Tabata Sanene jijini Dar es Salaam kutokana na msanii huyo kuwa anasumbuliwa na mguu wake uliyokatwa mpaka kufikia kuhitajika kufanyiwa upasuaji mwingine.

“Ndugu zangu watanzania najua kutoa ni moyo na siyo utajiri ninawaomba mjitokeze kwa kumsaidia msanii huyo kwani mpaka sasa anahitaji kiasi cha milioni kumi na nane kwa ajili ya kufanikisha safari yake hiyo ya kwenda kupata matibabu na anatarajia kwenda kwenye matibabu hayo mwezi ujao,”Dkt.Mwakyembe.

Naye Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Tanzania Bibi.Joyce Fissoo alitoa wito kwa wasanii wote wa filamu nchi kujitokeza na kumsadia mwanatansia mwenzao wa filamu katika kufanikisha anapata matibabu ili aweze kurudi na kuendelea kufanya kazi zake kama kawaida .

“Bodi ya Filamu nchini kwa kushirikiana na Baraza la Sanaa laTaifa tumetoa kiasi cha shilingi Milioni moja kwa ajili ya kumchangia katika kufanikisha safari yake ya matibabu na serikali kwa ujumla inafanya jitihada mbalimbali katika kuhakikisha msanii huyu anapata kiasi hicho cha pesa kilichobakia,”Bibi Fissoo.

Pamoja na hayo Katibu Mtendaji BASATA Bw.Godfrey Mngereza alitoa wito kwa wasanii wote nchini kwa nao kijitokeza kumchangia msanii huyo kwani wasanii wote ni wamoja kwa maana wote ni wanafanya kazi ya sanaa hivyo ni vyema kuwa na mshikamano na kusaidiana.

Kwa upande wa msanii Wastara Issa aliishukuru serikali kwa kumtembelea na kumjulia hali pamoja na kumchangia na kusema imekuwa nifaraja kubwa kwake kuwaona na alitoa akaunti namba anayotumia kwa ajili ya kukusanyanyia michango ambayo ni EQUITY BENKI – 3007111415583 na namba za simu anazotumia kuchangisha ni 0768 – 666 113 na 0713 666 113 na alieleza amesajiliwa kwa jina la Wastara Issa katika namba hizo za simu pamoja na akaunti namba yake.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (wapili kushoto) akimsikiliza kwa makini Msanii Wastara Issa aliyeketi chini alipokuwa akimweleza namna mguu wake huo unavyomuuma na ni kwa muda gani amekuwa akisumbuliwa na tatizo hilo jana alipomtembelea nyumbani kwake Tabata Sanene jijini Dar es Salaam kumjulia hali na kufahamu ni kiasi gani cha pesa bado kinahitajika kumwezesha kwenda kwenye matibabu yake nchini India, wa kwanza kushoto ni Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Tanzania Bibi Joyce Fissoo.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (wapili kulia) akitoa wito kwa watanzania kujitokeza kumchangia msanii wa filamu Wastara Issa ili aweze kupata matibabu ya mguu wake huko nchini India alipomtembelea msanii huyo nyumbani kwake jana Tabata Sanene jijini Dar es Salaam, na wa kwanza kushoto ni Katibu Mtendaji Baraza la Sanaa la Taifa Bw.Godfrey Mngereza na anayefuata ni Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Tanzania Joyce Fissoo,na aliyeketi chini ni Msanii huyo wa Filamu Wastara Issa.
Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Tanzania Joyce Fissoo (kushoto) akimkabidhi mchango Msanii wa Filamu Wastara Issa aliyeketi chini kiasi cha shilingi milioni moja kilichotolewa na Bodi ya Filamu Tanzania kwa Kushirikiana na Baraza la Sanaa la Taifa kitakacho msaidia kwa matibabu ya mguu wake walipomtembelea jana nyumbani kwake Tabata Sanene jijini Dar es Salaam kumjulia hali ,katikati ni Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe akishuhudia tukio hilo.

MBUNGE KASULU VIJIJINI AAHIDI KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI

$
0
0
Na Rhoda Ezekiel Kigoma.

MBUNGE wa Jimbo la Kasulu Vijijini, Agaustine Vuma ameahidi kufanya ziara ya kutembelea vijijini vyote vya jimbo hilo kwa lengo la kuangalia changamoto na kero zinazo wakabili wananchi.

Amefafanua changamoto atakazokutanazo baada ya kuwasikiliza wananchi wake, hatua itakayofuata ni kuzifikisha Serikali zitatuliwe ili waendelee kufurahia uongozi wao uliopo madarakani.

Vuma amesema hayo jana wakati akikagua miradi inayotekelezwa katika jimbo hilo ikiwemo mradi wa Kituo cha Afya cha Nyakitonto kilichotengewa Sh. milioni 500." Ambapo mpaka sasa ujenzi huo umekamilika kwa asilimia 70 mpaka sasa na fedha Ilizo tumika ni Sh.milioni 290,"amefafanua Vuma.

Amesema Serikali ya Awamu ya Tano ipo kwa ajili ya kutatua changamoto za wananchi na ndio maana Rais,Dkt.John Magufuli ameanza kuboresha sekta za afya kwa kutoa fedha katika vituo vya afya.Ameongeza lengo la fedha hizo ni kuhakikisha wananchi huduma za afya vizuri pamoja na kuwawezesha wananchi kuwa na afya njema." Tunamshukuru sana Rais wetu kwa kuendelea kuwasaidia wananchi na sisi kama wawakilishi kazi yetu ni kuibua matatizo na kumpelekea aweze kuyatatua.

"Mpaka sasa tunaendelea kuboresha huduma za afya na nimeahidiwa kupewa fedha nyingine kwaajili ya kituo cha afya Rusesa na fedha hizo zitaendelea kutolewa kwa kuwa ni utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi(CCM)", amesema Vuma.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu Vijijini ambae pia ni Diwani wa kata ya Nyakitonto , Yohana Mshita amesema wananchi wa vijiji vilivyo karibu na kata hiyo walikuwa wakiteseka kupata huduma.Amesema wananchi wengine walikuwa wakilazimika kufuata huduma Kasulu Mjini na kusababisha kupoteza nguvu kazi lakini kwa sasa wataendelea kupata huduma karibu.

Ameongeza fedha zilizotolewa zimetumika kujenga chumba cha upasuaji, wodi za Wagonjwa, nyumba ya Mganga na chumba cha kuhifadhia maiti.Amesema mpaka sasa kuna fedha nyingi zimebaki, na wataendelea kuzihifadhi ili zitumike katika miradi mingine itakayo ibuliwa na wananchi

Nao baadhi ya wananchi, akiwamo Happynes Dastan amesema wamekuwa wakililia kupata kituo cha afya karibu kwani walikuwa wakilazimika kufuata huduma za upasuaji Wilaya ya Kasulu."Sasa tunauhakika wa kupata huduma za afya hapa hapa na kuendelea kufurahia huduma hiyo kwa karibu,"amesema. 

Amesema wanampongeza sana Rais wa Magufuli kwa kazi kubwa anayoifanya na shughuli ya kuwahudumia wananchi wanyonge kwa shida walizokuwa nazo.


 Mbunge wa Kasulu Vijijini Agaustine  Vuma akikagua miradi inayotekelezwa katika jimbo hilo ikiwemo mradi wa Kituo cha Afya cha Nyakitonto kilichotengewa Sh. milioni 500." Ambapo mpaka sasa ujenzi huo umekamilika kwa asilimia 70 
MBUNGE wa Jimbo la Kasulu Vijijini, Agaustine Vuma ameahidi kufanya ziara ya kutembelea vijijini vyote vya jimbo hilo kwa lengo la kuangalia changamoto na kero zinazo wakabili wananchi.

SIMANJIRO KUJENGA HOSPITALI YA WILAYA

$
0
0
Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, ambayo haina hospitali ya Wilaya imejipanga huhakikisha inaanza mchakato wa ujenzi wa hospitali hiyo. 

Wilaya ya Simanjiro iliyoanzishwa mwaka 1993 baada ya kugawanywa kutoka wilaya ya Kiteto, kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012 ina wananchi 178,693 lakini hadi hivi sasa haina hospitali ya wilaya. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Yefred Myenzi aliyasema hayo wakati akizungumza kwenye kikao cha Baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya hiyo. 

Myenzi alisema viongozi na wananchi wa wilaya hiyo kwa pamoja wanapaswa kushikamana ili kuhakikisha wanafanikisha ujenzi wa hospitali hiyo ya wilayani. 
Alisema ameshakutana na wataalamu wa idara ya afya waliotoka ofisi ya Rais Tamisemi, waliofika ofisini kwake na kupanga mipango ya kuanzisha hospitali ya wilaya hiyo. 

"Sikubaliani na pendekezo la kukipandisha hadhi kituo cha afya Orkesumet ili kiwe hospitali ya wilaya, hapana tunapaswa kujenga hospitali ya wilaya na kituo cha afya Orkesumet kitaendelea kufanya kazi yake kama kawaida," alisema Myenzi. 
Alisema tangu wilaya hiyo ya Simanjiro ianzishwe haijawahi kuwa na hospitali ya wilaya, hivyo huu ni wakati muafaka wa kuanza mchakato wa ujenzi wake. 

Diwani wa Kata ya Orkesumet, Sendeu Laizer alisema anaunga mkono hatua ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Yefred Myenzi kuanza ujenzi wa hospitali mpya ya Wilaya na kutopandisha hadhi kituo cha afya cha Orkesumet. 
Laizer alisema suala hilo ni maendeleo makubwa kwa wananchi wa kata ya Orkesumet na Wilaya ya Simanjiro kwa ujumla kwani wilaya hiyo haijawahi kuwa na hospitali ya wilaya tangu ianzishwe. 

Mkazi wa wilaya hiyo Meshack Tureto alisema ujenzi wa hospitali hiyo, itakuwa ni maendeleo mazuri kwa wananchi wa eneo hilo, ambao hawana hospitali ya wilaya. 
Tureto alisema uanzishwaji wa hospitali ya wilaya itakuwa ni muendelezo mzuri wa maendeleo kwenye eneo la afya, kwani mgonjwa ataweza kupata rufaa ya ugonjwa kwa ukaribu zaidi tofauti. 

Mkazi wa Orkesumet, Baraka John alipongeza jitihada za Myenzi kuanzisha mchakato wa ujenzi wa hospitali hiyo kwani anaamini mikakati hiyo itafanikiwa. 
"Tunaposema uongozi wa ubunifu na unaoacha alama ni huu alioufanya mashine ya kazi Myenzi kwani hospitali ya wilaya ni hitaji la muda mrefu kwa jamii ya eneo hili," alisema John.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara Yefred Myenzi akizungumza kwenye kikao cha Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Albert Msole na Katibu Tawala wa Wilaya hiyo Zuwena Omary. 
Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro Albert Msole akizungumza wakati akifungua kikao cha Baraza la madiwani wa Halmashauri hiyo, kulia ni Katibu Tawala wa Wilaya hiyo Zuwena Omary na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Yefred Myenzi.  

WALIMU WAWILI KIBAHA WASHUSHWA VYEO KWA KUKAIDI AGIZO LA ELIMU BURE

$
0
0

Na Mwamvua Mwinyi,Kibaha

MKUU wa wilaya ya Kibaha,Mkoani Pwani, Assumpter Mshama ameamuru walimu wawili wa shule za msingi washushwe vyeo kutoka nafasi ya mwalimu mkuu na kuwa walimu wa kawaida ,kutokana na kosa la kuchangisha michango wazazi.

Hatua hiyo ,ameichukua siku chache baada ya mkuu wa mkoa wa Pwani ,mhandisi Evarist Ndikilo ,kukemea tabia inayofanywa na baadhi ya walimu wakuu na bodi za shule kuchangisha wazazi na walezi michango ambayo serikali imeizuia.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Kibaha ,alisema walimu hao wamekiuka agizo la serikali na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk .John Magufuli .

Mshama aliwataja walimu hao kuwa ni mwalimu mkuu wa shule ya Msingi Miembesaba, Rashinde Kilakala ambaye alikuwa akipokea sh.1,000 kwa kila mwanafunzi kwa ajili ya mitihani jambo ambalo ni kinyume cha agizo la serikali.

Mwalimu mwingine ni wa shule ya msingi Jitegemee, Sapiensia Kilongozi ambae aliweka kikao na kuita wazazi na kuwataka wazazi wenye watoto watoe shilingi 2,000 kwa wiki kwa ajili ya masomo ya ziada na mitihani.

Mshama alisema,huo ni mwanzo kwani ataendelea kusimamia maagizo yanayotolewa na serikali ili iwe fundisho kwa walimu wanaokaidi mipango ya serikali hiyo.Alieleza atakaeendelea kufanya hivyo akibainika atachukuliwa hatua kali ikiwemo kufukuzwa kazi .
Mkuu wa wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani ,Assumpter Mshama ,aliyesimama akizungumza jambo kuhusiana na masuala ya Elimu bure .(picha na Mwamvua Mwinyi).

Maandalizi ya Ujio wa FIFA YAANZA

$
0
0
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Kimataifa wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA) (hawapo pichani) unaotarajia kufanyika nchini mwezi Februari 2018 kuhakikisha maandalizi yanakuwa mazuri ili ujio huo uwezekuletea manufaa kwa taifa katika kikao kilichofanyika jana jijini Dar es Salaam
Wajumbe wa Kamati ya Maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Kimataifa wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA) wakisililiza maagizo ya Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe aliyokuwa akitoa katika kikao hicho kwa lengo la kufanikisha ujio huo wa Kimataifa kuwa unaleta manufaa kwa taifa jana jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Kimataifa wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA) wakifuatilia maelekezo yaliyokuwa yanatolewa na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe katika kikao cha maandalizi ya ujio huo kilichofanyika jana jijini Dar es Salaam,wapili kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo kutoka Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Bw. Yusuph Singo.

ELIMU YA AFYA YA UZAZI YASISITIZWA KUOKOA VIJANA KISIWANI PEMBA

$
0
0
SHIRIKA la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia masuala ya Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) limetakiwa kutoa elimu ya afya ya uzazi kisiwani Pemba ili kuokoa kizazi kutokana na kukua kwa wimbi la kuingiliana kinyume cha maumbile.

Kauli hiyo imetolewa na washiriki wa mafunzo ya Elimu ya afya ya Uzazi na Elimu kwa mtoto wa kike yanayoendelea Micheweni, Kisiwani Pemba .

Wakichangia mada ya afya ya Uzazi, iliyotolewa na Mkuu wa Elimu ya Afya Wilayani Micheweni, Sulemani Faki Haji, mshiriki kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali anayeratibu masuala ya Jinsia, Hidaya Khamisi amesema kwamba takwimu za udhalilishaji za hivi karibuni zinaonesha Kisiwa cha Pemba hususan wilaya ya Wete inaongoza kwa asilimia 70 kwa vitendo vya ulawiti na ubakaji.Kikundi kazi cha wanafunzi na akina mama kikifanya zoezi la kuwapima uelewa wao kuhusu somo walilopewa na malengo ya mafunzo hayo katika shule ya Sekondari ya Chwaka Tumbe, Micheweni kisiwani Pemba.

Amesema vitendo hivyo vinasababisha fedheha katika jamii na kukatisha ndoto za mtoto kufikia malengo yake maishani.

Wakionyesha ukubwa wa tatizo washiriki wamesema kuwa kwa hivi sasa si shuleni, kwenye madrasa wala nyumbani ni mahali salama kwa watoto wa kiume na wa kike kwani kwa sababu si ajabu kumwona mtu anayeheshimika katika jamii hususan mzazi wa kiume akifanya mapenzi na watoto wake wa kuwazaa na kuwapa mimba huku walimu wa dini kuwadhalilisha watoto.

Hivi karibuni mkazi mmoja wa shehia ya Kiungoni Kimango, Hamad Omari Hamad mwenye miaka 56 alikamtwa na polisi kutokana na vitendo vya ubakaji alivyowafanyia watoto wake watatu akiwemo mtoto mdogo wa miaka minne na mmoja wao kupewa mimba na baba huyo.Kipindi cha mazoezi cha kuendesha mahojiano kwa ajili ya kupata habari kati ya Mtangazaji wa Redio Jamii Micheweni, Time Khamis na Mkuu wa Kitengo cha Elimu ya Afya ya Kujamiiana na Uzazi wa Mpango Wilaya ya Micheweni, Pemba Dk. Suleiman Faki Haji. Mahojiano hayo ni miongoni mwa vielelezo katika mafunzo ya Elimu ya Kujamiiana na Uzazi iliyofanyika Micheweni, Pemba yenye lengo la kuwapa ujuzi stadi wanafunzi wa shule nne za sekondari na kikundi cha akina mama Wilayani Micheweni Kutayarisha Vipindi vya redio vinavyohusu masuala yao.

Kwa mujibu wa Mratibu wa Masuala ya Jinsia, Hidaya Khamisi, kuna mtandao ujulikanao kama cheni ridhia unaendelea katika baadhi ya shule Kisiwani Pemba wa watoto kwenda kufanya vitendo viovu iwe kupiga punyeto, kufanya ngono au kulawitiana.

Utafiti uliofanyika wilaya ya Wete mwaka 2016 kuhusiana na masuala ya unyanyasaji wa watoto iligundulika kwamba darasa zima lenye watoto 60 walisema kwamba wanataka wawekewe mazingira ili wasidhalilishwe kwa sababu watoto wote darasa hilo wamefanyiwa vitendo vya udhalilishaji hususan kulawitiwa.
Picha ya pamoja ya washiriki wa mafunzo ya Afya ya Kujamiiana na Uzazi iliyofanyika Tarehe 18 hadi 23 Desemba 2017 katika shule ya Sekondari Chwaka Tumbe, Micheweni kisiwani Pemba. Mafunzo hayo yaliyoendeshwa na Shirika la Kimataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) yalifunguliwa na Mkuu wa Wilaya ya Micheweni, Salma Khatib Mbarouk (pichani mwenye gauni jeusi na kitambaa cheupe).

Aidha ripoti nyingine kutoka shule moja wilayani Micheweni kwa mujibu wa Meneja wa Kituo cha Redio Jamii Micheweni, Ali Kombo imeonyesha kwamba kati ya wanafunzi 60 ni wanafunzi 10 tu ambao walikuwa bado hawajafanyiwa udhalilishaji wa kingono.

Mafunzo ya Elimu ya afya ya Uzazi na Elimu kwa mtoto wa kike yanayoendeshwa na UNESCO yana lengo la kuunda Vikundi vya Vijana Shuleni na Akina Mama Watayarishaji Vipindi vya redio kwa kushirikiana na Redio Jamii Micheweni, ambavyo vitasambaza Elimu rika kwa Vijana na Akina Mama.

ZANA ZA UVUVI HARAMU ZA MAMILIONI ZATEKETEZWA GEITA

$
0
0
Na Joel Maduka,Geita.

Serikali Mkoani Geita Imeteketeza zana haramu zenye thamani ya shilingi milioni therathini na tatu zikiwemo Nyavu za makila zilizounganishwa 2,393,makokolo ya sangara 32,timba 142 makokoro ya dagaa 7 na dududu 11.

Hatua hiyo imetokana na oparesheni ya Kitaifa ya kupambana na uvuvi haramu ambayo inaendelea kwenye maeneo ya ziwa viktoria ikiwa na lengo la kuondoa uvuvi huo ndani ya ziwa hilo pamoja na kuondoa mitandao ya wafanyabiashara wa zana haramu za kuvulia ,biashara ya samaki wachanga na utoroshaji wa samaki na mazao ya yake,kwenda nje ya nchi kinyume cha sheria.

Zoezi hili la uteketezaji zana hizo limefanyika kwenye Kata ya Nkome ,ambapo kiongozi wa oparesheni hiyo Gabriel Mageni ,amemweleza mkuu wa mkoa huo kwamba kuna baadhi ya wafanyakazi wa hifadhi ya Rubondo wamekuwa wakihusika na uvuvi haramu kwa kuwaruhusu wavuvi kuingia kwenye hifadhi na wengine kuficha zana zao ndani ya hifadhi na kwamba wamekuwa wakilipwa fedha wafanyakazi hao maarufu kwa jina la "KIFUNDA"

Kufuatia malalamiko hayo mtandao huu umetafuta kwa njia ya simu afisa mahusiano wa TANAPA Pascal Shelutete alisema kuwa wao kama watu ambao wanamamlaka ya hifadhi za taifa na kwamba kwa mujibu wa kanuni na taratibu za sheria askari wao hawapaswi kushiriki kwenye vitendo vya ujangili na kwamba taratibu za kiuchunguzi zikifanyika na wakabaini kuna watumishi wanajihusisha na vitendo hivyo hatua za kisheria na za kinidhamu zitachukuliwa na hawawezi kuwakingia kifua.

Aidha Mageni aliongeza kuwa katika operesheni hiyo ambayo ina siku kumi na mbili baadhi ya mambo ambayo wameyabaini ni pamoja na baadhi ya viongozi wa vijiji na maofisa wanaosimamia maeneo ya uvuvi kuwapa hifadhi raia wa kigeni wanaojishughulisha na shughuli za uvuvi wakiwa hawana kibali na kusababisha serikali kukosa mapato.

Mkuu wa Mkoa huo,Mhandisi Robert Luhumbi,amewataadhalisha watendaji ambao wanashirikiana na wavuvi haramu na kwamba endapo kuna mtu hakibainika na kitendo hicho serikali itahakikisha inamchukulia hatua na kwamba kupitia oparesheni hiyo hatabakia hata mtu mmoja ambaye anajihusisha na shughuli hizo.

Nyawalwa Wange ni moja kati ya watu ambao wanajishughulisha na kazi ya uvuvi alisema agizo la Mkuu wa Mkoa ni la kuungwa mkono kutokana na kwamba uvuvi haramu umeendelea kuharibu kwa kiasi kikubwa samaki ambao wapo ndani ya ziwa viktoria na kwamba serikali iendelee kuwabaini wale wote ambao wanaendelea kufanya shughuli za uvuvi kinyume na sheria.

Katika oparesheni hiyo jumla ya fedha ambazo zimekusanywa ni zaidi ya milion, 111 fedha zinazotokana na faini ,malipo ya mrahaba pamoja na mauzo ya samaki.
Baadhi ya wananchi wakishuhudia zoezi la uteketezaji wa zana haramu za uvuvi kwenye Kijiji cha Nkome Wilayani Geita . 
Mkuu wa wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi akielezea mikakati ya wilaya ya kuhakikisha wanapamba zaidi na vitendo ambavyo vimeendelea kufanywa na wavuvi ambao awana mapenzi mema na samaki waliomo kwenye ziwa viktoria wakati wa zoezi la uteketezaji wa zana haramu. 
Wananchi wa Kata ya Nkome wakiwa kwenye mkutano ambao ulikuwa na lengo la kuelezea hali ya uvuvi haramu ilivyo kwenye kata ya Nkome na namna ambavyo oparesheni imeweza kufanyika kwenye maeneo hayo. 
Kiongozi wa kikosi maalumu kinachoendesha oparesheni ya kupambana na uvuvi haramu ziwa victoria Gabriel Mageni akielezea namna ambavyo wameweza kuendesha zoezi hilo ndani ya siku kumi na mbili. 
Mkuu wa Mkoa wa Geita,Mhandisi Robert Luhumbi akisisita kwa wale ambao ni watumishi na viongozi kuacha kuendelea na tabia ya kushirikiana na wavuvi haramu 
Viewing all 110181 articles
Browse latest View live




Latest Images