Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110181 articles
Browse latest View live

JE.! WAZIJUA FAIDA LUKUKI ZA FENESI.?

$
0
0
Imeandaliwa na ​ Geofrey Chambua ​kutoka vyanzo mbalimbali

Huenda umewahi kuliona na kulipita tu ama kutovutiwa na ladha yake ama kukereka na utomvu wake baada ya kula

Habari mbaya kwako ni kwamba umekosa kitu adimu na maridhawa sana......Hili ni moja ya matunda yanayochukuliwa kama MFALME WA MATUNDA (The King of Fruits) kwa kuwa na karibu vitamin vyote muhimu yaani A, B1, B2 na C..

Na sehemu zinazotumika ni majani, matunda, utomvu, mizizi na magamba. Na mfenesi unaweza kukua hadi kufikia kimo cha mita 20.........na nakusihi sana kuanzia leo ujitahidi kula walau punje tatu tu na ukiweza hata mbegu zake kwa kadri ya mada hii

Leo nimejikuta tu nafukunyua tunda hili baada ya kulikuta mahali fulani na jinsi watu walivyokuwa wanatua kilich cha thamani ndipo nilipoanza kugoogle nikakuta faida na hata hilo jina la lugha ya malkia huitwa Jackfruit

Fenesi ni miongoni mwa matunda ya msimu yenye umbo la kipekee huku likiwa na ladha tamu isiyomithilika. Licha ya sifa hii, tunda hili linatajwa kuwa na faida lukuki endapo litaliwa na mwanadamu.
Hakuna anayejua vizuri asili ya mafenesi lakini inaaminika asili yake ni katika misitu ya mvua nyingi ya Magharibi ya ghats (western ghats). Lakini kwa sasa inalimwa katika nchi za india, Burma, Sri lanka, China, Malaya, East in indies, Qeens land, Maturities, Hawaii, Suriname, Brazil, Kenya, Uganda na Tanzania, Na nchini Tanzania hulimwa Pemba, Unguja, Dar es Salaam, Pwani, Morogoro, Tanga na Mbeya(Kyela) nk.

Kwanza, linatajwa kuwa na virutubisho kadha wa kadha vyenye kazi mbalimbali mwilini. Baadhi ya virutubisho hivyo ni pamoja na vitamini za aina mbalimbali, madini, protini, mafuta, uwanga na nyuzinyuz (fiber) ambazo husaidia kwenye mfumo wa mmeng'enyo na kuchagiza tatizo la kupata haja (constipation) na linasaidia pia kuzuiwa kuvimbiwa.

Fenesi pia linatajwa kuwa chanzo kizuri cha nishati kisichokuwa na lehemu (cholesterol). Si hivyo tu, bali pia ni chakula chenye virutubisho vya kuondosha sumu mwilini vinavyoweza kuukinga mwili dhidi ya saratani na magonjwa mengine kadha wa kadha,

Sukari ya Fenesi ni dawa ya sukari sumu mwilini kwa kuwa linasharabiwa taratibu mwilini na kufyonza sukari sumu na hii husaidia pia katika kuhibiti shinikizo la damu mwilini ( Jackfruit is more slowly absorbed into the bloodstream, which prevents sugar crashes, sugar cravings, and mood swings, They are well known because of its high potassium content. This helps the blood vessels relax and maintains proper blood pressure.)


DKT.NDUGULILE ATAWAZWA KUWA CHIFU MWANYINGA WA KABILA LA WASAFWA MKOANI MBEYA

$
0
0

Na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile amesimikwa rasmi kuwa chifu wa kabila la Wasafwa linalopatikana katika mkoa wa Mbeya .

Dkt. Ndugulile amesimikwa uchifu huo wakati wa ziara yake mkoani Mbeya yenye lengo la kuamsha ari ya wananchi kushiriki katika shughuli za maendeleo katika maeneo yao.

Dkt. Ndugulile amesema kuwa Wizara yake imeamua kufuatilia utekelezaji wa Sera ya Maendeleo ya Jamii katika ngazi za Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa kushiriki kwa vitendo kwa kufanya kazi na jamii kwenye miradi ya ujenzi wa miundombinu ya elimu, afya, kilimo, barabara, viwanda na maji, nk.

Ameongeza kuwa lengo la ziara hiyo ni kufuatilia namna ya utekelezaji wa Sera ya Maendeleo ya Jamii ambayo inasisitiza ushirikishwaji wa jamii katika maamuzi, kupanga, kutekeleza, kufuatilia na kutathmini shughuli au miradi ya maendeleo ikiwemo upanuzi na uendelezaji wa miundo mbinu mijini na vijijini kama Shule, Barabara, Zahanati na Maghala kwa kutumia rasilimali zilizopo.

“Niwapongeze kwa kazi nzuri mliyofanya na hakikisheni mnafanya kazi kwa bidii inayotoa matokeo yenye mashiko na tija katika jamii. Tumieni stadi na mbinu shirikishi kuwezesha maendeleo jumuishi ambapo makundi yote katika jamii yanashiriki katika maendeleo yao” alisistiza Mhe. Dkt. Ndugulile.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile(Mb) akichanganya zege kwa ajili ya ujenzi wa boma la madarasa ya shule ya Kata ya Mwasanga iliyopo Jiji la Mbeya Mkoani Mbeya katika ziara yake ya kuamsha ari ya wananchi kujitolea kufanya shughuli za maendeleo katika maeneo yao.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile(Mb) akipiga plasta kwenye chumba cha madarasa katika ujenzi wa shule ya Kata ya Mwasanga iliyopo Halmashauri ya Jiji la Mbeya Mkoani Mbeya katika ziara yake ya kuamsha ari ya wananchi kujitolea kufanya shughuli za maendeleo katika maeneo yao.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile(Mb) akitunukiwa uchifu kutoka kwa Machifu wa Kabila la Wasafwa kama shukurani kwa jitihada za kuamsha ari ya wananchi kujitolea kuchangia shughuli za maendeleo katika ujenzi wa shule ya Kata ya Mwasanga iliyopo jiji la Mbeya Mkoani Mbeya wakati wa ziara ya yake ya kuamsha ari ya wananchi katika kujitolea kufanya kazi za maendeleo.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile(Mb) akiwa na vazi la kichifu la kabila la Wasafwa pamoja na machifu wengine wa Kabila la Wasafwa wakati alipotunukiwa uchifu wa kabila hilo katika ujenzi wa shule ya Kata ya Mwasanga iliyopo Jiji la Mbeya katika ziara yake ya kuamsha ari ya wananchi wakishiriki kutekeleza utoaji wa haki ya kumwendeleza Mtoto kwa kumpa elimu.

AGAPE YAKABIDHI BAISKELI KWA VIJANA 15 WALIOHITIMU MAFUNZO YA HISA SHINYANGA

$
0
0
Shirika lisilo la kiserikali la Agape AIDS Control Programme (AACP) limetoa mafunzo ya Hisa kwa vijana 15 kutoka katika kata za Mwamalili,Didia na Masekelo zilizopo katika wilaya ya Shinyanga. 


Pamoja na kuwapatia vyeti vya ushiriki wa mafunzo,shirika la AGAPE pia limekabidhi baiskeli 15 kwa vijana 15 walioshiriki mafunzo hayo ambazo zitawamsaidia kurahisisha kusafiri wanapotoa elimu ya hisa katika jamii. 



Mafunzo hayo ya uwezeshaji wa vikundi vya hisa ngazi ya jamii yalianza Januari 11,2018 na kufungwa leo Januari 17,2018 katika darasa la AGAPE AIDS Control Programme lililopo katika kata ya Lubaga katika manispaa ya Shinyanga. 



Mgeni rasmi wakati wa kufunga mafunzo hayo leo,yaliyohudhuriwa pia na maafisa maendeleo kutoka kata hizo tatu,alikuwa Afisa Maendeleo ya Vijana halmashauri ya manispaa ya Shinyanga Charles Luchagula aliyemwakilisha mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro. 

Meneja Miradi wa Shirika la AGAPE Mustapha Isabuda alisema mafunzo yametolewa ikiwa ni utekelezaji wa mradi wa kuzuia ndoa na mimba za utotoni unaofanywa na shirika hilo kwa kushirikiana na shirika la Firelight. 
Washiriki wa mafunzo hayo wakiwa katika picha ya pamoja
Mgeni rasmi ,Afisa Maendeleo ya Vijana halmashauri ya manispaa ya Shinyanga Charles Luchagula aliyemwakilisha mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza wakati wa kufunga mafunzo ya hisa kwa vijana 15 na kutoka kata za Mwamalili,Didia na Masekelo zilizopo katika wilaya ya Shinyanga.Aliwasisitiza vijana kufanya kazi kwa kujituma ili kuleta mabadiliko katika jamii.-Picha zote Kadama Malunde - Malunde1 blog
Meneja Miradi wa Shirika la AGAPE Mustapha Isabuda akielezea lengo la mafunzo hayo.Kushoto ni washiriki wa mafunzo hayo.
Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la AGAPE,John Myola akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo.Kushoto ni Kaimu Afisa Maendeleo ya jamii halmashauri ya manispaa ya Shinyanga,Aisha Mwinshali.Kushoto ni mgeni rasmi ,Afisa Maendeleo ya Vijana halmashauri ya manispaa ya Shinyanga Charles Luchagula aliyemwakilisha mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro. 

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

WAZIRI MKUU ASIMAMISHA UUZAJI WA MALI ZA KNCU

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Bibi Anna Mghwira asitishe uuzwaji wa mali za Chama cha Ushirika cha Kilimanjaro (KNCU).

Ametoa agizo hilo jana jioni (Jumatano, Januari 17, 2018) wakati akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Serengeti, wilayani Tarime.

Hatua hiyo imekuja baada ya KNCU kutangaza kuuza shamba lake kwa ajili ya kuiwezesha benki yake ya KCBL kutimiza sharti la mtaji la Benku Kuu ya Tanzania (BoT).Benki hiyo ya KCBL inatakiwa kutimiza sharti la kuwa na mtaji kamili unaotosha wa shilingi bilioni tano (5) katika kipindi cha miezi sita tangu kutolewa kwa tangazo hilo.

Waziri Mkuu alisema ni marufuku kuuza mali za Ushirika huo, hususan katika kipindi hiki ambacho Serikali inafanya uhakiki wa mali za vyama mbalimbali vya Ushirika nchini.

Alisema Serikali imedhamiria kuimarisha Ushirika nchini na sasa inafanya uhakiki wa mali za vyama vya Ushirika na watakaobainika kuhusika na ubadhilifu watachukuliwa hatua.Januari 4, 2018 BoT ilizipa miezi sita benki tatu ili ziweze kuongeza kiwango cha mtaji unaohitajika kutokana na matakwa ya kisheria ya kuwa na mtaji kamili wa kutosha.

Benki hizo ni Kilimanjaro Co-Operative Bank Limited, Tanzania Women Banki Plc na Tandahimba Community Bank Limited, zitakaposhindwa kutekeleza agizo zitachukuliwa hatua.

BoT ni itazifutia leseni na kusimamisha shughuli za kibenki chini ya ufilisi, iwapo benki hizo zitashindwa kutekeleza agizo hilo ihadi kufikia Juni 30, 2018.


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
ALHAMISI, JANUARI 18, 2018.

DKT. NDUGULILE AZINDUA SACOSS YA WANAWAKE MKOANI MBEYA

$
0
0

Kitengo cha Mawasiliano WAMJW

Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (Mb) amezidua Saccoss ya Wanawake katika Halmashauri ya Jiji la Mbeya kwa ajili ya wajasiriamali wadogowadogo ili kuweza kutatua changamoto zao na kuwawezesha kupa mbinu mbalimbali za kufanikisha matarajio yao na kupata maendeleo.

Ameizindua Saccoss hiyo Mkoani Mbeya wakati akiitambulisha Programu ya ‘Kikundi Mlezi’ katika Manispaa ya ya Jiji la Mbeya yenye lengo la kuwawezesha wanawake wajasirimali kuwezeshana kati yao wenyewe katika kuanzisha na kuendeleza miradi ya biashara.

Dkt. Ndugulile amesema kuwa katika zoezi la kuamsha ari ya wananchi kushiriki katika shughuli za maendeleo linaenda sambamba na uwezeshwaji wa wanawake katika kuwashirikisha wanawake wenyewe katika kuibua miradi na kuanzisha shughuli za uzalishaji kwa kuzingatia matumizi ya fursa na weledi wa wananchi wenyewe. 

Dkt.Ndugulile amesema kuwa ili kufanikisha kufikiwa kwa Tanzania ya viwanda Serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo itaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa wajasiriamali wadogo wadogo hasa wanawake kuwaweza kuanzisha vikundi vitakavyoanzisha viwanda vidogo vidogo na kuzalisha bidhaa zitakazo uzwa ndani na nje ya mkoa wa Mbeya na hivyo kuutangaza mkoa kupitia bidhaa zilizozalishwa kwa kutumia ubunifu na rasilimali zilizopo.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (Mb) akiangalia bidhaa ya Tea Masala wakati alipotembelea moja ya Kikundi cha wanawake wajasiriamali cha kilichopo Manispaa ya Jiji la Mbeya, mkoani Mbeya, katika ziara ya kuamsha ari ya wananchi kushiriki shughuli za maendeleo.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (Mb) akiangalia bidhaa ya Tomato Sauce wakati alipotembelea moja ya Kikundi cha wanawake wajasiriamali kilichopo Manispaa ya Jiji la Mbeya, mkoani Mbeya, katika ziara ya kuamsha ari ya wananchi kushiriki shughuli za maendeleo.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (Mb) akiwa aevaa koti lililotengenezwa na wajasiliamali wadogo wakati alipotembelea moja ya Kikundi cha wanawake wajasiriamali kilichopo Manispaa ya Jiji la Mbeya, mkoani Mbeya, katika ziara ya kuamsha ari ya wananchi kushiriki shughuli za maendeleo.

Rais Magufuli amteua Dkt Titus Mwinuka kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS JANUARI 18, 2018

shule ya Lupalilo Sekondari yakosa umeme zaidi ya mwezi mmoja sasa

$
0
0
Shule ya sekondari ya Lupalilo inakabiliwa na ukosefu wa nishati ya umeme kwa zaidi ya mwezi mmoja hivi sasa, baada ya Transfoma iliyokuwepo kuungua na kusababisha kukwama kwa shughuli mbalimbali shuleni hapo ikiwemo wanafunzi kushindwa kujisomea usiku pamoja na kuhatarisha usalama wa wanafunzi baada ya kukosekana kwa nishati hiyo hasa nyakati za usiku

Akizungumzia Hali hiyo makamu mkuu wa shule Mwalimu LUNANILO KILATU amesema ni zaidi ya mwezi mmoja sasa wamekosa nishati hiyo baada ya transfoma kuungua na kupelekea baadhi ya shughuli kukwama shuleni hapo ikiwemo wanafunzi kushindwa kujisomea nyakati za usiku hivyo shule kulazimika kutumia jenereta ambalo amedai linawaongezea gharama zaidi.

Amesema wamesharipoti suala hilo kwa shirika la umeme TANESCO wilaya ya Makete tangu lilipotokea lakini hadi sasa ufumbuzi haujapatikana ingawa anaimani kuwa wanashughulikia.Kwa upande wa baadhi ya wanafunzi shuleni hapo waliozungumza na mwandishi wetu wamesema wanakumbana na changamoto nyingi baada ya kukosekana nishati hiyo ikiwemo kushindwa kujisomea nyakati za usiku huku wakihofia juu ya usalama wao hususani wanafunzi wa kike

Hata hivyo Tumemtafuta Meneja wa Tanesco wilaya ya Makete Ndugu HENRIKO RENATUS kupata ufafanuzi ambapo amesema mpaka sasa wanasubiri Transfoma nyingine kwani wameshatuma maombi ya kuomba transfoma na pindi zitakapowasili wataipa kipaumbele shule hiyo kutokana na uhitaji

Ni zaidi ya mwezi sasa shule hiyo ikabiliwa na tatizo hilo la ukosefu wa umeme na kukwamisha mambo mengi pamoja na usalama wa wanafunzi kuwa mdogo na kupunguza uwezekano wa wanafunzi kujisomea nyakati za usiku kama ilivyokuwa awali.Habari/picha na Edwin Moshi.


Makamu Mkuu wa shule akizungumza na mwandishi wetu ofisini kwake

Mwanafunzi wa Lupalilo Sekondari akizungumza na mwandishi wetu
Muonekano wa shule ya Lupalilo Sekondari

Transfoma iliyopata tatizo
 

MICHUZI TV: HII NDIYO SABABU ILIYOMUWEKA PEMBENI KWA MUDA MSANII NURU THE LIGHT, ARUDI NA NGOMA MPYA YA UMENIACHA

$
0
0
*Asema suala la ndoa kwa sasa kwake bado analitafakari...

Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

UNAPOAMUA kuzungumzia au kutaja majina ya wasanii wa kike ambao wanajihusisha na muziki wa kizazi kipya a.k.a Bongo Fleva basi lazima utakutana na jina la Nuru The Light. Jina halisi la mwadada huyo ni Nuru Magram lakini kwenye muziki basi kama ambavyo wanafanya wasanii wengi tu wa ndani na nje ya Tanzania akaamua kuwa na a.k.a yake.

Nuru The Right ni moja kati ya wasanii ambao wanaheshima kutokana na kazi zao za muziki wa kizazi kipya.Moja ya wimbo alioutoa kwa mashabiki wake na kumfanya atambulike na kuwa maarufu zaidi ni wimbo wake wa Walimwengu, licha ya kwamba ni juzi tu ameipua wimbo mpya unaojulikana kwa jina la Nimeachwa.

Mbali ya muziki amekuwa akifanya mambo mengine mbalimbali na kwa sehemu kubwa anaishi nchini Swedeen, lakini kwa sasa amerejea nchini kusalimia ndugu, jamaa na marafiki.

Sifa kubwa ya Nuru The Right ni msanii wa kike ambaye anafahamu nini ambacho anakifanya katika muziki. Anajua wakati gani wa kutoa wimbo mpya na wakati gani wa kusoma soko la muziki linakwendaje.

Globu ya Jamii imepata nafasi ya kutembelewa na msanii huyo ambaye hana makuu, hana sifa za kijinga na siku zote amekuwa mnyenyekevu, mpole , mcheshi na mwenye kuheshimu kila mtu na kubwa zaidi ni msanii ambaye sauti yake inaweza kumtoa nyoka pangoni. Hakika ni msanii anayejali mashabiki wake.

Akiwa katika ofisi za Michuzi ameulizwa maswali mengi na kwa sehemu kubwa ameyajibu kadri ya uwezo wake.Hata hivyo moja ya swali ambalo ameulizwa lilikuwa linataka kufahamu kama ameolewa au la, Nuru The Light akatabasamu na kutoa sauti ya kicheko na kujibu kuwa kwa sasa hana mume, kwani wakati wa kuolewa na kuwa mke wa mtu bado hajafikiria kwa sasa.

Licha ya kwamba bado hajaolewa lakini anasema wakati ukifika kama mwanamke atahitaji kuwa na mume lakini si tu ilimradi mume, bali awe anasifa ambazo anahitaji kutoka kwa huyo ambaye atataka kumuoa.Kwanini hajafikiria kuolewa amejibu kuwa wakati haujafika bado kwani haipo kwenye mipango yake kwa sasa.
Nuru The Right hakusita kuelezea baadhi ya sifa ambazo anataka kuwa nazo mtu ambaye atataka kumuoa.Moja ya sifa ambazo anataka awe nazo mwanaume atakayetaka kumuoa ni mwanaume ambaye anajitambua, anajali na kubwa zaidi awe mwenye imani ya dini na kumjua Mungu.

"Zipo sifa nyingi za aina ya mume ambaye nataka awe nazo , lazima niwe na mwanaume ambaye anajitambua na anaelewa anachokifanya.Pia awe mwanaume mwenye imani ya dini,"amesema Nuru The Right huku akionesha kuwa zipo sifa nyingine nyingi ambazo anatamani mume atakeyemuoa awe nazo.

Alipoulizwa kama anazungumzia vipi aina ya maisha ya baadhi ya wasanii ambayo yanaonesha kutotulia kwenye mahusiano yao ya kimapenzi, amejibu kuwa binafsi hafurahishwi na tabia hiyo kwani anapofanya msanii mmoja inaonekana ndio tabia ya wasanii wote wakati si kweli.

"Binafsi najiheshimu na wakati mwingine ninaposikia habari za wasanii na mambo ambayo wanayafanya huwa inaniumiza sana moyo.Ni vema wasanii tukawa makini na aina ya staili ya maisha yetu.

"Hata hivyo kuna mambo ambayo wakati mwingine yanakera.Unaweza kukuta msanii fulani anafanya mambo ambayo yanavunja heshima yake lakini hakuna ambaye anamsema wala kumwambia

"Ila akitokea msanii mwingine akafanya hivyo hivyo watu wanakuja juu na kuanza kutoa maneno ya kila aina.Ni kama vile kuna wasanii wakifanya sawa na wengine wakifanya wanakosea,"amesema Nuru The Right.

Baada ya kukuleza sehemu ndogo tu kati ya mengi ambayo msanii huyo ameyazungumza kuhusu maisha yake ya muziki na nini ambacho amepanga kukifanya, usikose kufuatilia hatua moja baada ya nyingine ya maswali na majibu ya msanii huyo kwa kuangalia hiyo video hapo chini. 

SEKONDARI YA ST. JUDE yang'ara Mashindano ya Wanasayansi Chipukizi

$
0
0


 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Profesa Simon Msanjila akikabidhi zawadi kwa Prosper Gasper na Erick Simon kutoka Shule ya Sekondari St. Jude's jijini Arusha baada ya kuibuka washindi wa jumla wa Mashindano ya Wanasayansi Chipukizi (YST) yaliyofanyika leo yaliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

FURSA NYINGINE YA SCHOLARSHIP YAJA: SHULE ZA SEKONDARI ZATAKIWA KUTUMA MAOMBI SASA KUSHIRIKI MAONYESHO YA SAYANSI YA YST 2018!

WANAUME WA TARIME ACHENI UKATILI KWA WANAWAKE NA WATOTO-MAJALIWA

$
0
0


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewaasa wanaume wa wilaya ya Tarime kujiepusha na vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto pamoja na kuachana na kilimo cha bangi.

Alitoa kauli hiyo jana jioni (Jumatano, Januari 17, 2018) wakati akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Serengeti, wilayani Tarime.

Waziri Mkuu alisema vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto pamoja na kilimo cha bangi vinaitia doa wilaya hiyo, hivyo hawana budi wakaepukana navyo.

“Serikali inakemea vitendo vya ukatili, achaneni navyo. Mtu unamchapa mtoto makofi hadi anazimia, kitendo hicho hakiwezi kuvumilika na pia kinaitia doa wilaya yenu.”

Wakati Huo huo, Waziri Mkuu alimuagiza Mkuu wa wilaya hiyo, Bw. Glorious Luoga kuendelea na msako wa mashamba ya bangi na mirungi na kuchukua hatua kwa watakaobainika kuendesha kilimo hicho.

Alisema ardhi ya wilaya hiyo ni nzuri na inahimili kilimo cha mazao mbalimbali ya chakula na biashara kama mahindi, mihogo, ndizi, kahawa, pamba, ni marufuku kulima bangi.

Pia Waziri Mkuu aliagiza kuchukuliwa hatua kwa wakandarasi waliotekeleza ujenzi wa maji mkoani Mara kwa sababu miradi hiyo wameijenga chini ya kiwango.

Waziri Mkuu aliyasema hayo baada ya kupokea malalamiko ya wananchi kupitia mabango wakidai kutonufaika na miradi ya maji katika maeneo yao licha ya Serikali kutoa fedha.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
ALHAMISI, JANUARI 18, 2018.

WAZIRI WA KILIMO DKT.TIZEBA ATEMBELEA KIWANDA CHA MICRONIX-NEWALA.

$
0
0
Waziri wa Kilimo Dkt Charles Tizeba ametembelea kiwanda cha kubangua Korosho cha Micronix System Limited kilichopo Wilaya ya Newala Mkoani Mtwara na kuzungumza na Viongozi wa kiwanda hicho juu ya kupandisha malipo kwa Vibarua wanaofanya kazi Kiwandani hapo.

Kwa Sasa mfanyakazi analipwa Kati ya Shilingi elfu 7 mpaka elfu 8 kwa siku ambapo wanafanya kazi Kwa Siku 5 kwa Wiki.

Tayari uongozi wa kiwanda hicho kwa  kushirikiana na Mkuu wa Wilaya ya Newala Aziza Mangosongo wameahidi kulifanyia kazi Suala hilo.

 Waziri wa Kilimo Dr.Tizeba akiongea na Baadhi ya Wafanyakazi wa Kiwanda cha kubangua Korosho cha  Micronix System ltd kilichopo Wilaya ya Newala Mkoani Mtwara ambacho Kimeajiri wafanyakazi 350.
 Waziri wa Kilimo Dr.Tizeba akioneshwa aina za Korosho ambazo Tayari zimebanguliwa na kuwekwa kwenye vibakuli ili kupima Ubora Tayari kwa Kupakia, Kushoto kwake ni mkuu wa Wilaya ya Newala Aziza Mangosongo pamoja na Meneja Uzalishaji wa ETG Ltd Sunir Mizar.
 Waziri kilimo Dr.Charles Tizeba Akipanda Mche wa Mkorosho katika Kijiji cha Machombe,Kata Ya Marika kama Moja ya kuhamasisha upandaji wa Miche Mipya Wilaya ya Masasi mkoani Mtwara.

WILAYA YA CHEMBA YAANZA KUJIANDAA UZINDUZI WA SIKU YA MAADHIMISHO YA WANYAMA PORI DUNIANI.

$
0
0
Na Shani Amanzi,

Uzinduzi wa kuelekea siku ya Maadhimisho ya Wanyama Pori Duniani Kitaifa, utafanyika Marchi 03, 2018 katika Mkoa wa Dodoma ambapo Mgeni Rasmi atakuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa na Wilaya ya Chemba imechaguliwa kuwa sehemu ya Uzinduzi wa Maadhimisho hayo kwa shughuli ya upandaji miti iliyofanyika katika kijiji cha Kelema Kuu ,tarehe 15 Januari, 2018.

Katika uzinduzi huo Mgeni Rasmi alikuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Chemba Ndugu. Nyakia Ally kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Chemba Mhe.Simon Odunga.

Ndugu. Nyakia amesema, Jamii inatakiwa kuendelea kutunza mazingira kwa kupanda miti, sambamba na kutunza mazingira ya asili ya Wanyama Pori. Aliongeza kwa kusema zoezi la upandaji miti ni endelevu katika Wilaya ya Chemba na jumla ya miti elfu 2000 imepandwa katika kijiji cha Kelema Kuu kata ya Paranga, maeneo ya Taasisi na Makazi ya watu.

Wilaya ya Chemba imefanya shughuli ya upandaji miti katika Kijiji hicho kama sehemu ya kuunga mkono mkakati wa Serikali wa kuufanya Mkoa wa Dodoma kuwa wa kijani, sambamba na uhamasishaji wa utunzaji wa Wanyama pori kwa kuwa kijiji cha Kelema Kuu kinapakana na pori la akiba la Swagaswaga .

Pori la akiba Swaga swaga linatumika katika shughuli za Uwindaji wa Kitalii ambapo jamii inayozunguka pori hilo inanufaika kwa kupata mgao wa ruzuku unaotokana na shughuli za utalii.

Maadhimisho ya Uzinduzi wa siku ya Wanyama Pori Duniani umeshirikisha Katibu Tawala Wilaya ya Chemba Ndg. Nyakia Ally kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Chemba ,Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba Dkt. Semistatus H. Mashimba, Mkurugenzi wa Taasisi ya Rafiki Wild Life Foundation, Wakuu wa Idara/Vitengo Halmashauri ya Wilaya ya Chemba, Viongozi wa Ngazi ya Kata, Kijiji na Wananchi. 
 Katibu Tawala wa Wilaya ya Chemba Ndugu. Nyakia Ally kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Chemba Mhe.Simon Odunga akizungumza mbele ya Wananchi (hawapo pichani) kuhusiana na ujio wa Uzinduzi wa kuelekea siku ya Maadhimisho ya Wanyama Pori Duniani Kitaifa, ambao unatarajiwa kufanyika Marchi 03, 2018 katika Mkoa wa Dodoma,huku Mgeni Rasmi akitarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa,katika shughuli hiyo Wilaya ya Chemba imechaguliwa kuwa sehemu ya Uzinduzi wa Maadhimisho hayo kwa shughuli ya upandaji miti iliyofanyika katika kijiji cha Kelema Kuu ,tarehe 15 Januari, 2018.
 Katibu Tawala wa Wilaya ya Chemba Ndugu. Nyakia Ally kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Chemba Mhe.Simon Odunga akishiriki upandaji miti kuelekea Uzinduzi wa siku ya Maadhimisho ya Wanyama Pori Duniani Kitaifa, ambao unatarajiwa kufanyika Machi 03, 2018 katika Mkoa wa Dodoma,huku Mgeni Rasmi akitarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa.katika shughuli hiyo Wilaya ya Chemba imechaguliwa kuwa sehemu ya Uzinduzi wa Maadhimisho hayo kwa shughuli ya upandaji miti iliyofanyika katika kijiji cha Kelema Kuu ,tarehe 15 Januari, 2018.


DENMARK YAJADILI FURSA UWEKEZAJI NISHATI YA UPEPO NCHINI TANZANIA

$
0
0
Kampuni ya Vestas A/S ya Denmark kwa kushirikiana na Ubalozi wa Denmark nchini kwa mwongozo wa Wizara ya Nishati wameandaa mkutano wa kujadili fursa za uwekezaji katika nishati ya upepo (wind energy) nchini.

Mkutano huo ambao umewakutanisha wadau mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi ukiwa na lengo la kujadili na kuibua fursa muhimu za nishati ya upepo ili kuongeza upatikanaji wa umeme wa uhakika nchini, umefunguliwa na Kaimu Kamishna wa Nishati na Masula ya Petroli, Mhandisi Innocent Luoga kwa niaba ya Waziri wa Nishati Dkt Medard Kalemani.
Balozi wa Denmark Nchini Tanzania, Einar Hebogard Jensen akitoa maelezo juu ya mkutano wa wadau wa nishati ya upepo ulioandaliwa na kampuni ya nishati ya Vestas A/S kutoka Denmark kwa kushirikiana na Ubalozi wa Denmark nchini Tanzania.
Kaimu Kamishna wa Nishati na Masuala ya Petroli, Mhandisi Innocent Luoga akisoma risala na kufungua mkutano wa wadau wa nishati ya upepo kwa niaba ya Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani uliofanyika leo jijini Dar es Salaam. 
Mkurugenzi wa kampuni ya Vestas A/S kwa Afrika Kusini, akielezea mipango ya kampuni hiyo ya kuwekeza kwenye umeme wa upepo nchini Tanzania.
Meya wa Manispaa ya Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe akitoa maelezo kuhusiana na fursa za uwekezaji wa umeme wa upepo katika mkoa wa Dodoma wakati wa mkutano wa wadau wa nishati ya upepo uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Mradi wa Aldwych International, Mark Gammons akiwasilisha mada kuhusu miradi inayofanyika nchini Tanzania ikiwemo mradi wa umeme wa upepo  wa Singida wenye Megawati 100 na Ruhudji  wenye Megawati 358 wakati wa mkutano uliowakutanisha wadau mbalimbali wa masuala ya nishati wa ndani na nje ya Tanzania.
Baadhi ya wadau wakifuatilia mada kwenye mkutano huo wenye lengo la kujadili namna ya kuwekeza kwenye nishati ya Umeme wa Upepo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

POLISI SHINYANGA YAKAMATA BUNDUKI YA KIVITA AK -47 YENYE SKAFU YA CHADEMA

$
0
0
Na Kadama Malunde - Shinyanga.

Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga limefanikiwa kukamata silaha ya kivita aina ya AK-47 iliyotupwa na watu wanaodaiwa kuwa ni majambazi waliokuwa wanataka kuvamia kiwanda cha kutengeneza mafuta ya kupikia cha Jielong Holdings (Tanzania) Ltd kilichopo Nhelegani katika kata ya Kizumbi manispaa ya Shinyanga.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari leo Alhamis Januari 18,2018 Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule amesema walikamata silaha hiyo usiku wa kuamkia leo majira ya saa tano eneo la Tinde wakati majambazi hao wanafuatiliwa na polisi ndipo wakaamua kutupa bunduki hiyo.

“Silaha hii aina ya AK-47 yenye namba 18116428 ilikuwa imefungwa kwenye skafu yenye rangi ya nembo ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ikiwa na risasi 25 ndani ya magazine yake na risasi zingine 8,zikiwa kwenye mfuko mdogo wa nailoni”,alieleza Kamanda Haule.

“Majambazi wawili pia walitelekeza pikipiki aina ya SANLG yenye namba za usajili MC 856 BPF,mafuta ya cherehani ya kulainishia silaha,tochi mbili na koti zito”,aliongeza.

Alisema jeshi la polisi lilipata taarifa za majambazi hao kutaka kuvamia kiwanda hicho kinachomilikiwa na raia wa China tangu tarehe 6.01.2018 kisha kuanza kuwafuatilia na kubaini kuwa baadhi yao ni wakazi wa Kahama na Ushirombo ambapo amewataka kujisalimisha polisi.

Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule akionesha silaha aina ya AK-47 yenye namba 18116428 na mafuta ya kulainishia silaha yaliyotupwa na majambazi waliotaka kuvamia kiwanda cha Jielong 


Bunduki aina ya AK-47 yenye namba 18116428 iliyokuwa imefungwa kwenye skafu yenye rangi ya nembo ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) iliyotelekezwa na majambazi waliotaka kuvamia kiwanda cha Wachina mjini Shinyanga- Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog

Silaha na vifaa vilivyotelekezwa na majambazi Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule

Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule akionesha bunduki aina ya AK-47 yenye namba 18116428 iliyotupwa na majambazi waliotaka kuvamia kiwanda cha Jielong

MRADI MPYA WA VYOMBO VYA HABARI NA ASASI ZA KIRAIA KUINUA FURSA YA KUPATA HABARI NA KUIMARISHA UANDAAJI NA UPASHAJI HABARI

$
0
0

 Serikali ya Marekani kwa kupitia Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID), imezindua mradi wa kuimarisha asasi za kiraia na vyombo vya habari uitwao Boresha Habari Katika hafla fupi iliyofanyika jijini Dar es Salaam. 

Ukiendeshwa chini ya uratibu wa mashirika yasiyo ya Kiserikali ya Internews na FHI 360, mradi wa Boresha Habari utashirikiana na wabia wa Kitanzania, ikiwa ni pamoja na  Baraza la Habari Tanzania, Tanzania Bora Initiative, na Jamii Media,ili kuboresha weledi miongoni mwa waandishi wa habari na kusaidia kuweka mazingira yaliyo wazi kwa vyombo vya habari. Shabaha kuu ya jitihada hizi itakuwa ni kushirikisha na kujenga uwezo wa wanawake na vijana ili kuinua sauti, usemi na masuala yao katika nyanja mbalimbali za jamii wakiwa ni wazalishaji na watumiaji wa habari. 

“Serikali ya Marekani imedhamiria kwa dhati kusaidia kuinua ujuzi na weledi wa vyombo vya habari na asasi zisizo za kiserikali za Kitanzania – hususan katika kuwawezesha wanawake na vijana – kupaza sauti zao na kueleza dukuduku zao kwa ufanisi,” alisema Mkurugenzi Mkazi wa USAID Andy Karas Wakati wa hafla hii. 

Katika kipindi cha miaka mitano ijayo, mradi wa Boresha Habari unalenga kufanya kazi na wadau wa vyombo vya habari katika mikoa ya Dar es Salaam, Zanzibar, Iringa, Mbeya, Morogoro, Arusha, Manyara, Dodoma, Tanga, Mtwara, Mwanza na Kigoma. Aidha, mradi wa Boresha Habari utatoa mafunzo na msaada wa kitaalamu kwa vyombo vya habari vya humu nchini ukivisaidia kuanza kutumia teknolojia za kidijitali na kuimarisha uwezo wao wa kiusimamizi na kifedha. 

Hali kadhalika, mradi huu utatoa mafunzo kwa asasi za kiraia ili ziweze kushirikiana vyema na vyombo vya habari katika kusukuma mbele jitihada zao. Kwa kuzingatia umuhimu wa redio za jamii kama vyanzo maarufu vya habari za maeneo husika, mradi wa Boresha Habari utafanya kazi na vituo mbalimbali vya redio nchini kote ili kuboresha uwezo wao wa kitaalamu na uendelevu katika masuala ya kifedha. 

Executive Director of Tanzania Bora Initiative Abella Bateyunga (left) addressing participants during the launching of a civil society and media strengthening Boresha Habari project in Dar es Salaam yesterday. The 5 year USAID funded project will be coordinated by local organizations Internews and FHI 360 and implemented by a number of Tanzanian partners including Tanzania Bora Initiative, aims at enhancing professionalism amongst Tanzanian media and civil society with a particular focus of empowering women and youth – to raise their voices and concerns effectively as both producers and consumers of information. 
USAID Mission Director Andy Karas (right) congratulates Media and Communication Director of InterNews Wenceslaus Mushi after the launching of a civil society and media strengthening Boresha Habari project in Dar es Salaam yesterday. Looking on is the Executive Secretary of the Media Council of Tanzania Kajubi Mukajanga (center). The 5 year USAID funded project to be coordinated by local organizations Internews and FHI 360 and implemented by a number of Tanzanian partners including: the Media Council of Tanzania, Tanzania Bora Initiative, and Jamii Media aims at enhancing professionalism amongst Tanzanian media and civil society with a particular focus of empowering women and youth – to raise their voices and concerns effectively as both producers and consumers of information.

Article 3

MV MAGOGONI YASIMAMA KUTOA HUDUMA MAPEMA LEO ASUBUHI

JALADA KESI YA MHASIBU MKUU WA TAKUKURU NA WENZAKE LAPELEKWA TAKUKURU KWA UPELELEZI ZAIDI

$
0
0
Na Karama Kenyunko, Glogu ya jamii, 

Upande wa mashtaka katika kesi ya utakatishaji fedha na kumiliki mali zisizoendana na kipato chake  inayomkabili Mhasibu Mkuu wa Takukuru Godfrey Gugai na wenzake watatu umeiEleza mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa jalada la kesi hiyo limepelekwa Takukuru kwa ajili ya upelelezi zaidi.

Wakili wa Serikali Simon Wankyo akisaidiana na wakili Salim Msemo ameeleza leo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, wakati shauri hilo lilipofikishwa mahakamani hapo kwa ajili ya kutajwa upelelezi ikiwa haujakamilika

Wakili Wankyo amedai, jalada la kesi hiyo lilipelekwa kwa  Mkurugenzi wa Mashtaka nchini(DPP) kwa ajili ya kusomwa na sasa limerudishwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (Takukuru) kwa ajili ya upelelezi zaidi.Ameongeza, baada ya kukamilisha upelelezi, jalada hilo litarudishwa tena kwa DPP ili kujiridhisha kama maelekezo aliyoyatoa yamefanyiwa Kazi.

Hata hivyo, baada ya maelezo hayo, wakili wa Utetezi Alex Mshumbusi alidai kuwa hategemei upelelezi kuchukua muda mrefu kwa sababu mshtakiwa Gugai alikuwa mtumishi wa Takukuru na tayari alishashtakiwa kinidhamu na Takukuru yenyewe na kupoteza ajira yake.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Januari 31, mwaka huu itakapotajwa.
Mbali na Gugai, washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni George Makaranga, Leonard Aloys na Yasini Katera.Washitakiwa hao wanaokabiliwa na mashitaka 43 yakiwemo 20 ya utakatishaji fedha haramu, kumiliki mali zisizoendana na kipato na kughushi mikataba ya mauziano ya viwanja katika maeneo mbalimbali.

Katika shitaka la kwanza ambalo ni kumiliki mali ambazo hazina maelezo ambalo linamkabili Gugai, inadaiwa kati ya January 2005 na December 2015, jijini Dar es Salaam, akiwa ofisa wa umma ameajiriwa na TAKUKURU anamiliki mali zenye thamani  zaidi ya Sh 3.6bilioni  ambazo haziendani na kipato chake cha sasa wala cha nyuma.
Viewing all 110181 articles
Browse latest View live




Latest Images